Search This Blog

Friday, October 28, 2022

NENDA NA MOYO WANGU - 2

 

     





    Simulizi : Nenda Na Moyo Wangu

    Sehemu Ya Pili (2)





    Aliponyanyuka Jafary Hiza, ndipo na yule mwanamke aliifikia meza tuliyokaa

    na nikauona mshangao wa Jafary Hiza aliomtazama mwanamke yule kuanzia chini

    mpaka juu naamini pia alivutiwa naye. Mwanamke yule akatabasamu hapo

    akazidi kuvutia kutokana na lile tabasamu lake muruwa. Akasalimiana na

    Jafary Hiza kisha akajitambulisha kwake.

    "Naitwa Vanessa Noel" Huku tabasamu likiwa pana usoni mwake.

    "Naitwa Jafary Hiza"

    Kisha Jafary Hiza akamruhusu akae na yeye akaondoka. Vanessa alinitazama

    kwa makini kwa sekubnde zisipongua dakika 10 kisha akaivua miwani yake

    akazungumza nami.

    "Siamini kama unaweza kumuuwa mpenzi wako" akatoa karatasi kadhaa na

    kuziweka mezani kisha akatoa tepurekoda akaiweka pia mezani na kuongea tena

    "kwanza kwanini umuuwe mwanamke uliyempenda? Pia ulikuwa hufahamu ukimuuwa

    utaingia katika matatizo makubwa na mheshimiwa Oscer Valerian?" Hilo

    lilikuwa ni jina la baba yake Beatrice ambaye alikuwa naibu katibu mkuu wa

    umoja wa mataifa.

    "Dada yangu hata nikikueleza vipi huweza kuamini ninachozungumza lakini

    sina ukweli mwingine ninaoweza kukuambia zaidi ya kwamba sijamuuwa

    Beatrice"

    Akafanya kitu cha dharau sana na sijapenda na pia nilichukia ila kwa kuwa

    nilikuwa mtuhumiwa, basi sikutaka kufanya fujo yeyote. Kisha akaniambia



    "Naitwa Vanessa Noel nakufahamu unaitwa Ramon Lameck, mimi ni mpelelezi wa

    kesi hii kwa upande wa mlalamikaji na ni mpelelezi binafsi. Mlalamikaji

    ambaye ni mteja wangu amenilipa pesa nyingi sana za kung'amua kitendawili

    hiki. Hataki tu kukufunga pia anataka kujua sababu ya wewe kumuua mtoto

    wake. Hivyo mbali ya kuwa mpelelezi wa kesi nimesimama hapa kama

    mwanasheria wako ambaye nitakutetea kutokana na vifungu vya sheria

    vitakavyoniruhusu kufanya hivyo na ukweli utakaonieleza"
    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikahisi ni mtego. Mpelelezi wa kesi ya mauaji aliyemtuma ni Mlalamikaji na

    hapo hapo ananieleza kuwa yeye ameletwa na mlalamikaji ili anitetee!!

    Nikamuuliza Mungu, Ulinikutanisha na Beatrice ili maisha yangu yaishie

    hapa? Kwanini kile nilichokiota na kutamani kukifanya katika maisha yangu

    kinayeyuka kama mshumaa? Chozi likanidondoka kisha nikameza donge zito la

    mate. Nikiwa katika kulia, Vanessa Noel akaipiga meza ile ya bati na

    kuniambia.

    "Huna sababu ya kulia sasa nitakuuliza mambo kadhaa na ninaomba unieleze

    kile nitakachokuuliza"

    Nikatingisha kichwa kwa kukubali, akaiwasha tepurekoda yake akaanza kuongea

    huku akiwa amebonyeza kitufe cha kuruhusu sauti zetu kuingia katika kifaa

    kile kwa ajili ya kumbukumbu.

    Vanessa Noel akaniuliza swali la msingi ambalo sikutarajia kuulizwa katika

    mazingira kama hayo. Akaniuliza kama nimeshakula tangu nikamatwe? nikamjibu

    kuwa si tangu nikamatwe tu majira ya saa sita, yaani tangu asubuhi mpaka

    sasa saa 9:38 alasiri(kulingana na saa iuliyopachikwa juu ya ukuta mbele

    yangu ilivyokuwa ikisema) sijapata muda wa japo kunywa maji.

    Vanessa alisikitika sana nilipomueleza hivyo, kisha akazima ile tepurekoda

    na kubonyeza kitufe kile chekunde kwenye meza na kuzungumza na mtu wa

    upande wa pili.

    "Nahitaji chakula kwa ajili ya mteja wangu"

    "Dakika chache" sauti ile nzito ikajibu.

    Dakika chache baadaye, kweli lango lile likafunguliwa na toroli

    lililosheheni hotpot tatu za vyakula na jagi kubwa la kuvunjika lililobeba

    maji ya matunda, lilikuwa likisukumwa na askari wa kike mrembo .

    Hotpot zikafunguliwa, Vanessa akaitwaa sahani yake na glass ya kujimiminia

    maji yale ya matunda ya embe na pansion, kisha akachota tambi akachanganya

    na nyama roast pamoja na zile za kukaangwa wa kuku. Nikapata nafasi ya

    kumuuliza Vanessa baada ya kila mmoja akiwa anashughulika katika kung'ata

    minofu ile.

    "Hapa ni wapi? Na kwanini nimeletwa hapa na si mahabusu kama

    nilivyotarajia?"

    "Hapa panaitwa Safe house watu kama wewe huletwa sehemu kama hii kutokana

    na makosa yenu mliyoyatenda. Kama unamkumbuka yule kijana aliyemuua Mtoto

    wa Raisi Baraka katika ule mkasa ulioibua hadithi iliyouza nakala nyingi ya

    kitabu kilichoitwa NISAMEHE MWANANGU, aliletwa hapa kabla hajapelekwa

    Mwanza kwa ajili ya hukumu. Hata yule aliyemuua Waziri mkuu Peter Chongola,

    katika mkasa uliandikwa na mwandishi mashuhuri mwenye njaa stallone na

    kuita TAKSI YA KIJIVU(MUUWAJI ANAYETAFUTWA), yeye pia aliletwa hapa. Hivyo

    na wewe uliyemuua mtoto wa kigogo wa Un umelazimika kuletwa hapa kwa ajili

    ya mahojiano kabla ya kesi yako kunguruma"

    Hapo nikawa nimemuelewa sana Vanessa kisha tulipomaliza kula alikuja askari

    yule yule akatoa vyombo tulivyolia mazungumza yakaendelea.

    "Anafanana na Beatrice kwa mbali?" Vanessa akanitoa katika mawazo ya

    kumtazama askari yule akaniuliza kiuchokozi. Mimi sikumjibu, bali nilicheka

    kiasi na kumtazama Vanessa.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Vanessa ni mwanamke mrembo sana niliyewahi kukutana naye katika maisha

    yangu. kwa ufupi si rahisi kumuelezea Vanessa nikamaliza. Vanessa akawa

    anaweka kifaa kile cha kurekodia sawa na akaniuliza swali.

    "Nataka nianze kufahamu mlikutana wapi na Beatrice"



    Nikaanza kusimulia tangu siku ya kwanza nilipopelekwa na baba chuoni pale-:



    CHUONI UDOM



    kilikuwa ni kipindi cha kipupwe na baridi kali ilivuma kiasi cha kila

    mwanafunzi pale chuoni alikuwa amevaa sweta la kumkinga na baridi. Mimi

    nikiwa mtoto wa pekee katika famili yetu, baba yangu mzee Lameck alikuwa na

    furaha sana kwa kuwa sikumuangusha tangu nilipomaliza kidato cha nne,

    nikapata alama nzuri za kuniwezesha kuchaguliwa na serikali kwenda shule ya

    Tambaza kisha baada ya hapo ndipo nikachaguliwa kwenda Udom.

    Naweza kusema kuwa baba yangu ni rafiki yangu wa karibu sana katika maisha

    yangu. Alifurahia mafanikio yangu na kuhuzunika kwa shida zangu hakika

    najivunia sana kuwa na baba kama yeye. Siku hiyo ya kwanza akaniacha niende

    kuripoti ofisini na kupewa chumba changu akaniambia kuwa

    "Soma kwa bidii sana mwanangu, wewe ni mtoto wa kiume wa kike ataolewa wewe

    utaowa hakikisha unaposoma ukitazama daftari unamuona mke na watoto wako

    pale" akawasha gari na kuondoka.

    Mimi nilienda kwa Den of student kisha akanikabidhi kwa warden ambaye

    atanipa ufunguo wa chumba changu pale hostel za chuo. Nikakaa katika hostel

    za watu wa social huku mimi nikiwa nasomea Public administration. Huko

    nikakutana na vijana wawili Steven Ngonyani pamoja na Michael Stambuli.

    Hapo ndipo nilianza kumfahamu Beatrice.

    Tukiwa tumetoka dinner na wale vijana wenzangu yaani steve na michael,

    tulienda katika Carteen ambayo Michael alituelekeza kwa kuwa yeye alikuwa

    ni mwenyeji pale chuoni kabla yetu. Huyu Michael alikuwa mwaka wa pili huku

    mimi na Steve tukiwa mwaka wa kwanza steve akiwa amenitangulia wiki moja

    kabla mimi sijawasili pale chuoni.

    "Huku kuna watoto balaa" Michael akaendelee kutudokeza kama alivyoanza

    kutushawishi mpaka tukaja katika mgahawa huu. "Nyinyi rukeni kote ila kuna

    mtoto anaitwa Beatrice huyo niachieni, chombo changu hicho"

    Nikapatwa na hamu sana ya kumuona huyo Beatrice ambaye Michael alikuwa

    haachi kumtaja. Niliagiza wali samaki huku wenzangu wakila ugali na samaki

    mkavu. Ghafla Michael akatushitua wote tutazame kule alipokuwa akitazama

    yeye.

    Alipokuwa akitazama Michael, kulikuwa na wasichana watatu waliokuwa

    wakiingia pale katika ule mgahawa tulipo sisi. Kutokana na mgahawa ule kuwa

    mrefu sana, japo walikuwa mbali niliweza kuuona urembo wao sawia.

    Mmoja alikuwa chotara bila shaka, kutokana na nywele zake za singa zilizo

    ndefu kiasi zilifika mgongoni zilipeperuka peperuka; alikuwa akicheka na

    mmoja aliye kuwa upande wake wa kushoto huyu alikuwa mweusi wa kawaida

    mwenye shepu ya kibantu kwa mbali nilifanikiwa kuuona mwanya wake yeye

    alivaa sketi fupi hivyo miguu yake minene niliweza kuiona kwa ukaribu

    zaidi. Msichana huyo mwingine ndiye ambaye Michael alitaka tumuone bila

    shaka. Maana alipoona tu tumegeuka, akaropoka kama aliyewehuka.

    "Huyo anakuja, huyo hapo anayeongea na simu"

    Kwa mara ya kwanza nikawa nimemuona Beatrice, ilikuwa ni siku ya kwanza ya

    mimi kuingia hapo chuoni na ndiyo siku ya kwanza kukutana na Beatrice.

    Itachukua kitabu kizima endapo nikitaka kuelezea uzuri wa msichana huyu.

    Niliacha kula nikimtazama. Alikuwa ni mrembo kweli, mrembo haswa. Sasa

    nikagundua kilichokua kikimchanganya Michael.

    Kwa ufupi tu ni kwamba Beatrice alivaa sketi kama yule mbantu, yeye hakuwa

    mweusi wala mweupe rangi yake wala haikuwa maji ya kunde, ila alikuwa

    anaukaribia weupe. Siwezi kuelezea kwa ufasaha rangi hiyo ukanielewa. Sura

    yake ilikuwa ya mviringo lakini alikuwa ana asili ya nywele kwa sababu

    alijaa vinyweleo juu ya ngozi yake kiasi cha kunivutia zaidi kwa kuwa mimi

    ni mmoja kati ya wanaopenda aina ile ya ngozi. Vinyweleo laini vilivyolala

    juu ya ngozi. Kifuani alikuwa amebeba embe sindano ambazo ziliendelea

    kusimama wala hazikutaka kulala hivi karibuni. Kiuno kilikatika kikike huku

    hipsi zikijichora sambamba na makalio yaliyovimba na kuinua sketi ile na

    kuifanya iwe ndogo zaidi. Alikuwa akiongea na simu mpaka alipovuta kiti

    akakaa na mara nikashituka nikishikwa.

    "Hoya brother, ndio ushachanganyikiwa?" Alikuwa ni Michael huku Steven

    akinicheka "Haya ulikuwa ukimtazama nani? Yule Alisia, Prisca ama Beatrice?"

    "Duh! Kaka! Mtoto Beatrice namba nyingine" nikaishia hapo nikachota kijiko

    cha wali nikakitupia mdomoni, nikavuta mrija wa juisi nikautia mdomoni

    nikawa nanyonya juisi taratibu nikimtazama Michael.

    Chuki!! Nikaiona hasira katika uso wa Michael iliyozaa chuki. Ndita

    zikaharibu paji lake la uso kisha akasonya na kufinya kidogo macho yake

    kama atiaye mkazo kwa jambo alilotaka kuzungumza, hakuongea bali midomo

    iliishia hewani akatupa kidole chake cha shahada kama akinionya jambo.

    Steve akawa anatazama hali hiyo kwa mshangao sanjari na ilivyokuwa kwangu.

    Sikuwa na shaka kwa kuwa moyoni mwangu sikumaanisha kumpenda Beatrice kwa

    wakati ule ila kama ujuavyoa wavulana tumuonapo mwanamke mzuri lazima nafsi

    zetu ziwake tamaa. Wao waliumbwa kwa ajili yetu.

    Tuliendelea kula huku mimi nikiibia ibia kutupa jicho katika meza ya sita

    aliyokaa Beatrice na wenzake. Mara ya kwanza, ya pili na ile ya tatu

    niligongana macho kwa maho na Beatrice halafu kama waliyekuwa wakiniteta na

    yule chotara ambaye baadaye nilikuja kufahamu kuwa ndiye Alisia. Sikujua

    walichozungumza lakini walikuwa wakitazama meza yetu. Nikazuga kumtazama

    Michael nikamkuta yeye akiachia tabasamu pana huku akiwapungia mkono

    akiwasalimia. Nilitamani kucheka ila nilijizuia kwa kujifanya nakunywa

    juisi.

    Nikanyanyuka kwenda kunawa mikono kwenye ndoo itiririshayo maji kama

    bombani, ghafla nikagongana na mtu, mtu yule hakuwa mwingine bali ni

    Beatrice. Akanimwagia juisi iliyobaki kidogo kwenye glass yake na kuchafua

    shati langu nililovaa.



    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MAHOJIANO NA VANESSA SAFE HOUSE

    Kabla sijamaliza kueleza kila kilichokuwa kikiendelea, Vanessa

    akanikatisha.



    "Sasa ni saa 11 jioni naomba tuishie hapa kwa leo kesho tena nitakuja

    kukutembelea ili niweze kujua kilichoendelea. Naomba usiache hata moja

    unalolijua niweze kujua jinsi ya kukusaidia"

    "Sawa" nikamkubalia, kisha tukaagana na Vanessa.

    Vanessa alipoondoka askari wawili waliingia katika kile chumba na mnyororo

    fulani uliunganisha pingu za miguu na mikono ambao nilifungwa mimi kisha

    nikavalishwa kitambaa cheusi mfano wa kofia ya mzula kisha nikatemnbezwa

    taratibu kutoka katika chumba kile.

    Nilipokuja kuvuliwa kile kitambaa, nilikuwa ndani ya selo ya peke yangu

    lakini ni chumba chenye hadhi ya kulaliwa na mtu mzito. Chumba hicho

    kilikuwa na hewa ya pekee na utofauti wa chumba hiki hakikuwa na dirisha

    wala mlango.

    Hapana! Sasa mimi nilipita wapi? Sikushuka ngazi wala kupanda ila kuna

    mlango ulifunguliwa, uko wapi sasa? Mauzauza!!!

    Nilijaribu kugusa kuta za pande zote nne za chumba kile baada ya kufanikiwa

    kufunguliwa kile kitambaa cheusi, sikufanikiwa kuona chochote kinachofanana

    na mlango. Hapo nikakumbuka kile chumba nilichowahi kukiona katika

    tamthilia moja pendwa inayoitwa 'The legend of the seeker' sasa nikajiona

    mimi nikiwa ni muhanga mmoja wapo kama wale wasichana wawili ndani ya

    tamthilia ile.

    Nilijaribu kupiga kelele lakini chumba kile kikameza sauti yangu hata

    mwangwi haukurudi kama nilivyotaraji. Niligusa hapa na pale sikufanikiwa

    kupata chochote ninachokitafuta. Nikaamua kukaa pembeni mwa kitanda kipana

    chenye godoro zito pana kutoka chini kwenda juu na kulia kwenda kushoto

    lenye mashuka meupe pee! Kisha usingizi ukanipitia. Nikiwa hapo hapo bila

    kujitambua.

    Niliamka mara baada ya kuamshwa na askari wa kike ambaye alibeba sahani ya

    chakula pamoja na glass ya juisi. akaniambia

    "Kesho kuna ndugu zako watakuja kukuona"

    Nikamshika mkono, nikamuuliza mara alipotaka kuondoka.

    "Mlango wa hiki chumba uko wapi? Kwanini nipo hapa na si mahabusu yeyote

    chafu kama wafanyiwavyo wavunjaji wa sheria kama mimi?"

    Msichana yule alitabasamu kisha akauputa mkono wangu na kunieleza.

    "Hapa ni Safe house, wewe ni mtu katili sana na inabidi ulindwe kwa

    uangalifu sana kabla hatujajua chanzo cha wewe kufanya mauaji yale.

    Unalindwa kwa kuwa inaaminika kama umeweza kumuuwa mwanamke ambaye usiku

    uliopita uliweza kudanganya wazazi wake kwa kumvisha pete ya uchumba na

    mbele za watu wengi ukakiri unampenda yeye tu huku ukitabasamu kinafki, je

    tutajuaje kama umetumwa kumuangamiza mheshimiwa Oscer? Nimekusaidia

    kukueleza siri nyingi ila sijilaumu kwa kuwa huoneshi kuwa katili kama

    inavyotangazwa huko nje" akatoa gazeti na kunitupia katika mapaja yangu

    "Nilipoitazama sura yako katika gazeti hili, sikukubaliana na kichwa hicho

    cha habari"

    Mara, mara!! Nini hiki? Nasinzia jamani, mara nikalala wala sikumuona yule

    askari wa kike wakati anatoka.

    Nilipokuja kuamka nililikuta gazeti lile pale pale mapajani mwangu pembeni

    kukiwa na sinia la chakula. Nilitazama huku na kule sikumuona yule mwanamke

    wala sikuona chochote kilichobadilika katika kuta zile. Nilipotazama katika

    sinia lile la chakula, sikukitamani chakula kwanza kabla sijasoma

    kilichoandikwa katika gazeti hilo.



    "MUUWAJI WA MTOTO WA KIGOGO WA UMOJA WA MATAIFA AKAMATWA NDANI YA NYUMBA YA

    MAREHEMU"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kisha picha kubwa ikinionesha nikiwa ndani ya nyumba ya mpenzi wangu

    Beatrice. Picha hiyo alinipiga yule askari ambaye hakuvaa sare za kipolisi

    kisha akanicheka mara nilipokuwa nimejikojolea. Niliitazama picha ile kwa

    uchungu na kuisoma habari ile kwa hasira kisha nikameza donge zito la mate

    lililonikaba kwa uchungu. Nikakunja kunja lile gazeti na kulitupa kisha

    nikapiga kelele za maumivu kutokea ndani ya moyo wangu kutokana na kesi

    hiyo mbaya ya kusingiziwa.

    Nikalipiga teke sinia lile la chakula nikapiga magoti kwenye kitanda changu

    cha kulalia kisha nikalia kwa uchungu. Hakika hakuna kipindi kigumu

    nilichokuwa nikipitia zaidi ya hiki katika maisha yangu. Wakati nikiwa

    nimejiinamia pale, askari watatu wakaingia.

    "Wewe muuwaji! Una nini?"

    Ilikuwa ni sauti ya askari mmoja mnene mrefu kiasi, kidevu chake kilikuwa

    chakavu kutokana na ndevu na mapele yake yaliyokomaa. Nilipoinuka na

    kumtazama ila sikumjibu kitu.

    "Mtoeni humu labda hapendi Ac mpelekeni mahabusu za kawaida kule napo kuna

    ulinzi mkali"

    Wale askari wawili ambao walisimama pembeni yangu wakanibeba msobemsobe kwa

    kunishika makwapani kwangu huku mimi nisisimame, hivyo walikuwa

    wakiniburuza. Hapo nikawa nimeuona mlango ulivyokuwa wazi na jinsi ya

    kuufungua na kuufunga ilinishangaza teknolojia ya namna hii. Sikutegemea

    kama hapa hapa Tanzania nilipoishi zaidi ya miaka 26 kungekuwa na sehemu ya

    namna hii.

    Nikaburuzwa mpaka katika sehemu yenye selo nyingi ambazo zilikuwa tupu na

    kutupwa katika moja ya mahabusu hizo bila huruma, kisha wakaniacha hapo

    bila kusema lolote. Baada ya dakika chache baadaye, alikuja yule askari wa

    kike aliyeniletea chakula mwanzo akaniambia.

    "Nimekuletea chakula ule ukikimwaga na hiki shauri yako sintakuonea huruma

    tena"

    Uso wake haukuwa na mzaha, akakisukumiza kile kibakuli kilichojaa wali,

    paja la kuku na ndizi mbivu kwa mguu wake kisha yeye akaondoka.

    Nilikula kile chakula mpaka nilipomaliza kisha nikaenda kujitupa katika

    kitanda kidogo kipatacho futi 4 kwa 6 cha chuma, nikasinzia.

    Ilikuwa asubuhi, alikuja yule askari wa kike na kuniamsha kwa kirungu.

    "Wewe, wewe!!"

    Nikaamka.

    "Embu njoo! Una mgeni wako"

    Niliamka haraka haraka kwenda kukutana na mgeni huyo. Sikujua ni nani,

    lakini nilitamani sana kukutana na ninayemfahamu ili niweze kupata faraja

    ya moyo japo kujua ni vipi watu wanachukulia kesi yangu. Yule askari

    akanifunga pingu mikono yangu kwa nyuma kisha akaniongoza mpaka ilipo

    sebule ya nyumba ile.

    Hapo mwanzo sikuweza kufahamu kabisa kama nilikuwa ndani ya nyumba ya

    kifahari namna hii. Samani za gharama zilisheni katika sebule ile. Kila

    kona kulikuwa na vitu vya thamani sana. Sikuvalishwa tena kile kitambaa

    cheusi ila ulinzi wa kuvalishwa pingu mfano wa minyororo haukukoma.

    Nilipotokeza nikiwa katika mshangao wa nyumba ile, niliweza kuwaona walinzi

    lukuki wakitembea tembea huko nje na nilipoyatupa macho yangu kwenye

    makochi ya pale ukumbini, mgeni aliyekuwa akinisubiri ni Michael rafiki

    yangu. Yule askari akazungumza

    "Dakika mlizopewa ni 30 tu za kuzungumza"

    Nikatazama ukutani kulipokuwa na saa ilikuwa ni saa 3:14 asubuhi siku ya

    pili tangu Beatrice auwawe. Nasema auwawe kwa kuwa si mimi muhusika wa

    mauaji hayo licha ya kuwa kila mtu anaamini ni mimi ndiye niliyeua.

    Nikamtazama Michael nikiwa na furaha lakini Michael alionesha wasiwasi mara

    aliponiona. Wasi wasi ule wa Michael ukanitisha sana. Hakuzungumza wala

    mimi sikuzungumza kama kwa sekunde kumi hivi, kisha akaniuliza.

    "Ramon" kama aliyekuwa akiniita lakini hakumaanisha kuniita, akaendelea

    "Umekuaje rafiki yangu?"

    Sikujibu haraka, nilimtazama Michael moja kwa moja katika macho yake kama

    niliyekuwa nikimsoma jambo kisha nikamuuliza "Michael wewe una amini

    nimeua?"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Unadhani mimi nitaamini vipi Ramon?" Alinijibu huku akiitupa mikono yake

    miwili hewani na uso wake ukiwa katika hali ya msisitizo.

    Hapana! Kuna kitu nakiona katika macho ya Michael si kizuri. Kwanini

    Michael anayenifahamu mimi kwa miaka 4 zaidi leo anaamini mimi nimeua? Mimi

    nina sura ya kuua? Michael anaigiza na kuna kitu anafahamu. Nikapatwa na

    wasiwasi na Michael juu ya kifo cha Beatrice.

    "Kiukweli habari hizi zimenishangaza sana Ramon. Sikutegemea mtu kama wewe

    unaweza kufanya jambo la kikatili namna ile"

    Sikumjibu kitu ila kuna kitu kikawa kimenikaba ndani ya koo yangu na

    machozi yakinilenga kwa uchungu.

    "Sina cha kukusaidia au kukushauri katika hili kwa kuwa unafahamu fika mzee

    Oscer(baba yake Beatrice) ana nyadhifa gani hapa Tanzania. Cha ajabu na

    kinachonishangaza wakati umeua na bado ukaendelea kubaki eneo la tukio.

    Ramon pombe ulizokunywa, pombe mbaya rafiki yangu nilikuwa nikikuambia kila

    siku"

    "Unasema nini wewe Michael? Kwanini unanituhumu moja kwa moja bila kuwa na

    uhakika Michael? Mimi wa kuuwa?" Uvumilivu ukanishinda sasa nikawa naropoka

    kwa hasira huku sauti yangu ikipaa juu hata niipoinyanyuka ikaongezeka

    zaidi "nakuuliza, mimi naonekana muuwaji kwako leo? Au kwa kuwa msichana

    yule ulikuwa unampenda? Ina maana nilidhani huna chuki tena nami kumbe

    ulikuwa mnafki? Michael.." Nikamuinamia mpaka ulipo uso wake na kunyoosha

    kidole katika kifua changu nikamwambiwa kwa dhati na hisia kali kwa sauti

    ya chini "Mimi sijamuuwa Beatrice lakini muuwaji atapatikana"

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walinzi waliovalia sare nyeusi ambazo si za askari niliowazoea wa hapa

    Tanzania, walikuja na silaha nzito na mmoja wao alituuliza

    "Kuna nini? Ustaarabu umewashinda?"

    Michael alinyanyuka huku akinitazama, akacheka kwa dharau na kutingisha

    kichwa. Akaniambia

    "Pole rafiki yangu nitakuja kukuona siku nyingine"

    Michael akaondoka.

    Nilibaki pale sebuleni wale walinzi nao wakaondoka. Machozi sasa

    yakadondoka kwa uchungu. Rafiki yangu amenisaliti. Vipi kuhusu wazazi

    wangu? Mama yangu ataniamini?Sina shaka na baba kwa kuwa yeye hunijua vyema

    mimi. Nikatupa jicho pembeni nikakutana na gazeti la udaku.







    ITAENDELEA 

0 comments:

Post a Comment

Blog