Search This Blog

Friday, October 28, 2022

WABEBA NDOTO (THE DREAM HOLDERS) - 2

 









    Simulizi : Wabeba Ndoto (Dream Holders)

    Sehemu Ya Pili (2)





    Sauti Kali ya filimbi ilisikika ikipulizwa kutoka kwa kocha wao "okay boys njooni tusikilizane,nachotaka leo ni ufundi zaidi nataka kuona uwezo defence wa pamoja na offence,mpira uzunguke kiufundi zaidi.Wanaoanza wanajulikana Gerald kaa nje kwanza" aliongea kocha kwa sauti ya juu sana.Zoezi lilianza kwa kasi sana huku Paul akionekana kupata mipira mingi lakini hakufika nayo mbali maana Daniel alimpiga kikumbo kizito kilichomrusha mbali na kumdondosha "yeah!safi sana Daniel Paul bado sijaona ufundi kabisa" aliongea kocha.Paul alinyanyuka na kuelekea kwenye nafasi yake huku akimtazama Daniel.Upande wake ulimpa mipira mingi lakini kila Mara alikuwa akipigwa vikumbo vizuri na Daniel na kumdondosha chini kumfanya ashindwe kufunga magoli.Paul alikunja uso wake kwa hasira kila mara alipopigwa vikumbo hivyo.Paul alidaka mpira vizuri kutoka kwa mchezaji mwenzake na kukimbia nao kwa kasi sana alikwepa kila mtu aliyejaribu kumzuia,kasi yake na chenga zake za mwili ziliwachanganya sana wapinzani wake ambao walidondoka chini kila mara Paul alipokuwa akiwapita.Kipaji kikubwa alichokuwa nacho Paul kilimshangaza Gerald hakuamini kama Paul alikuwa ana kipaji kikubwa vile kiasi cha kufaa hata kuchezea timu ya taifa.Alizidi kukimbia kwa kasi,alimkaribia Daniel ambaye alijiandaa kumkabili,alipeleka mwili wake upande wa kulia na kugeuka kwa kasi upande wa kushoto chenga ambayo ilimpeleka Daniel upande wa kulia na kuacha uwazi upande wa kushoto wa Paul kupita.Chenga hiyo ilikuwa ni Kali sana kwa Daniel na kujikuta akidondoka chini huku akinyoosha mguu wake na kumkwatua Paul aliyedondoka chini kwa kishindo kikubwa.Watu Wote walishangaa tukio hilo ambalo lilikuwa siyo la kimichezo "faulo" aliita kocha wao.Paul alinyanyuka kwa hasira na kumsogelea Daniel kwa nguvu na kumsukuma kwa nguvu "una matatizo na mimi mse** wewe!" Daniel naye alinyoosha mikono yake kumsukuma Gerald "wewe ndiye mwenye matatizo na mimi,Mimi nafanya defence tu" alijibu Daniel kwa hasira "mmh wote mtapata adhabu siyo mahali pa kupigana hapa wala kuoneshana ubabe,nimeita faulo" "kocha mimi sikuelewi maana kila mara Daniel akicheza faulo unaishia kuita tu wala humpi adhabu yeyote au mpaka avunje mtu siku au unasubiri mimi nimvunje!" aliongea Paul kwa hasira na kumgeukia Daniel kabla hajamgeukia kocha wake tena "unaharibu timu kocha" alifoka Paul na kukndoka kwa hasira "usiondoke mbele yangu umesahau unaongea na nani!,rudi hapa" aliamuru kocha wake lakin iilikuwa bure Paul aliendelea kuondoka zake mpaka kwenye benchi alilokaa Gerald "uko sawa?" "hujaona kilichotokea uwanjani au! ipo Siku nitavunja ile miguu ya Daniels " aliongea Paul kwa hasira.Walisikia sauti ya Kylie kwa mbali ikilalamika wote kwa pamoja waligeuza Shingo zao na kumuona kijana mmoja akijaribu kumtomasa Kylie kwenye makalio.Tukio hilo lilizidi kuwasha hasira ndani ya moyo wa Paul ambapo alinyanyuka haraka "hey! Paul subiri unaenda wapi,tulia" aliongea Gerald huku akimfuata kwa nyuma.Maneno hayo hayakusaidia lolote maana alikwishamkaribia kijana yule na kumpiga ngumi nzito iliyompeleka chini "nyanyuka mse*** wewe " "Paul huna haja ya kupigana tunaweza kuongea tu" alibembeleza Kylie.Hakuna ambacho kilipenya kwenye masikio ya Paul,hasira zilimtawala alimnyanyua kijana Yule na kumpiga ngumi nyingi za uso zilizomjeruhi vibaya.Tukio hilo lilijaza wanafunzi wengi kwenye eneo hilo kiasi cha kukatisha mazoezi ya timu huku baadhi ya wanafunzi wakishangilia kana kwamba wanaangalia pambano Kali la ndondi.Mwalimu wa nidhamu aliingilia katikati na kuamulia "wote wawili ofisini kwangu haraka" alifoka mwalinu huyo wa nidhamu.Wanafunzi wote walimshangaa Paul aliyekuwa akihema kwa hasira huku macho yake yakiwa mekundu sana.Gerald alimsogelea Kylie aliyekuwa pembeni kidogo "uko sawa?" "sijawahi kumuona Paul akiwa na hasira vile!" "kawaida,walimkorofisha tokea uwanjani" "no siyo kawaida umeona macho yake! anatisha sana,naanza kuogopa anaweza kunidhuru Siku moja" "usijali hakuna atakayekudhuru mimi niko hapa" aliongea Gerald na kumsogeza Kylie karibu yake.

    "Tafadhali usifanye hivyo,tafadhali nakuomba" kilio hicho hakikumzuia yeye kufungua mkanda wa suruali yake na kuishusha tayari kwa kumbaka.

    "Kwa nini nimetokea tena hapa?"aliuliza Gerald akiwa ukingoni mwa barabara usiku huo huku magari machache yakikitembea na watu wachache sana wakionekan kuzurura "ni kwa sababu mara ya mwisho ulitokea hapa kwa hiyo kila mara utakapokuja Grotto utatokea hapa mpaka ujue kujidhibiti mwenyewe" alijibu Sebastian "okay tunaenda wapi sasa hivi?" "tunaenda nyumbani kwangu" "una nyumba huku!" alishangaa Gerald "yah nina nyumba huku niliiumba mwenyewe ili nikiwa huku niwe nina sehemu ya Kuala" "aisee!" "usijali utaweza tu na wewe ni jambo la kujifunza wewe utaweza kuumb vitu vingi hata ambavyo hatuwezi kudhania ila unahitaji mda tu na hiyo ndiyo sababu kuu ya Kronos kutaka kukuua anataka kuwa wewe anataka kuwa supreme" aliongea Sebastian na kusimamisha taksi iliyokuja mbele yake "tupeleke mtaa wa Stian" aliongea Sebastian kumpa maelekezo dereva taksi.Gerald hakuamini kama mambo yote hayo yalikuwa yanatendeka ndani ya ndoto za watu zilizoungana kutengeneza dunia moja ndiyo iliyoitwa Grotto.Haikuchukua mda mrefu gari ilifika na kupaki mbele ya jumba kubwa la kifhari liliokuwa kwenye mtaa huo,Sebastian alitoa pesa kadhaa na kumkabidhi dereva yule na wote walishuka.Ukubwa wa jumba la Sebastian ulimshangaza Gerald ambaye alipata wakati mgumu kuamini kuwa jumba lote lile liliumbwa na Sebastian.Walianza kutembea taratibu kukaribia mlango ambao ulifungiliwa huku binti mzuri alitokea mbele yao kuwalaki alikuwa mzuri na mwenyewe ngozi nyeupe iliyong'aa vizuri "mbona umewahi leo?" aliuliza binti yule ambaye alianza kumuangalia Gerald "inabidi nimfundishe huyu dogo mambo fulani,Gerald huyu ni mdogo wangu anaitwa Kate..Kate huyu ni Gerald ni mmoja wetu sema yeye ndiye supreme,namfundisha baadhi ya vitu" "supreme! Kwa hiyo ni supreme! alishangaa Kate "anyway nice to meet you Gerald,your highness" aliongea Kate na kumpa mkono huku akitoa tabasamu zuri lililojaa aibu usoni mwa Gerald "twende Gerald" aliongea Sebastian na kuondoka huku Gerald akimfuata kwa nyuma.Walielekea moja kwa moja hadi nyuma ya nyumba ambapo ilikuwa na uwanja mkubwa uliopandwa ukoka mzuri uliong'aa.Gerald alishangaa sanamu kubwa za chuma zilipangwa vizuri na kutengeneza mstari mrefu "nini hizi?"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/ "ndio hatua yako ya kwanza ya mazoezi,hizi ni sanamu za chuma inabidi uzivunje kwa mkono yako" "nini! Kwa mkono yangu!" "usijali Gerald wewe una nguvu sana unachotakiwa ni kuhisi nguvu kutoka ndani mwako.Mwanzo mgumu lakini kadri ya siku zinavyokwenda utazoea tu" aliongea Sebastian.Kate aliwasili na kuketi vizuri pembeni alikaa kushuhudia mazoezi makali ya supreme ambaye alisimuliwa tokea zamani kwamba supreme ana nguvu sana na ndiye kiongozi mkuu wa dream holders wengine lakini kwa mtu aliyekuwa mbele yake alishindwa juamini kama alikuwa kweli supreme au la."Aaaa...h" alilia Gerald kwa maumivu baada ya kupigana ngumi nzito juu ya sanamu mojawapo.Kicheko kikubwa kilisikika kutoka kwa Kate "usicheke Kate siyo utani huu" aliongea Sebastian " siyo kama nacheka ila supreme gani huyu hawezi hata kurusha ngumi!" aliongea Kate.Maneno hayo yalimfadhahisha Gerald ambaye aliendelea kupiga ngumi nyingi bila mafanikio.Sebastian alitazama saa yake "Gerald kwa leo inatosha inakaribia kufika asubuhi inabidi urudi nyumbani sasa".

    Saa yake ndogo iliyokuwa pembeni ya kitanda chake ilikuwa kwa nguvu kwa lengo la kumuamsha kutoka usingizini,aliamka na kujiandaa vizuri kuelekea shuleni,alielekea sebuleni na kumkuta mama yake akifunga mlango huku akimuaga mtu"shikamoo" "marahaba" "ulikuwa unamuaga nani?" aliuliza Gerald huku akibugia mkate uliokuwa mezani "huyo ni mama yake Beatrice yule mnayesoma naye shule moja" " tangu lini wewe na mama yake Beatrice ni marafiki!" " tuko naye kwenye chama kimoja cha wanawake alikuwa akiniambia kuhusu mwanaye livyoharibikiwa" "ameharibikiwa! kivipi!" "siku hizi anajihusisha na ngono bado mdogo kabisa" aliongea mama yake "ngono! hapana haiwezekani Beatrice ni mwanakwaya mzuri sana mama!" "haiwezekni nini sasa halafu cha ajabu anasingizia amebakwa anaulizwa alibakwa wapi hawezi kujua kapasahau,kweli! watoto siku hizi mna mambo ya kikubwa" aliongea mama yake na kuelekea chumbani kwake.Gerald alibaki akishangaa ilikuwaje Beatrice msichana aliyekuwa kwenye mazingira ya dini ajihusishe na ngono katika umri huo.Aliendelea kuwaza bila majibu na kuamua kuondoka kuelekea shuleni.

    Kwenye korido mrefu kuelekea darasani Gerald na Kylie walitembea huku wakizungumza "Paul kapatwa na nini?" aliuliza Gerald "amesimamishwa shule kwa wiki tatu,alikuwa akijaribu kunitetea najisikia vibaya sikuweza kumsaidia" "usijali usingeweza kuamua chochote,na yule jamaa aliyepigwa na Paul vipi?" yule yupo hajapewa adhabu yoyote" "kwa nini! yule naye alistahili adhabu kwa alichokufanyia" "nasikia wazazi wake ni watu wakubwa halafu walikuja hapa nafikiri walimu waliogopa" alijibu Kylie "huyo jamaa anasoma darasa gani?" unataka kufanya nini Gerald?" aliuliza Kylie kwa mashaka "anaitwa nani?" "anaitwa Joseph form six tafadhali Gerald usifanye upumbavu wowote "tangulia darasani nakuja" aliongea Gerald na kushika njia kwenye korido ndefu iliyokuwa kulia kwake.Kylie alivuta pumzi kwa nguvu na kushindwa kumzuia Gerald.Gerald alielekea mpaka darasa moja la kidato cha sita na kuingia ndani alimkuta Joseph aliyekuwa amezungukwa na wasichana waliokuwa wakijiweka karibu naye kwa sababu y a utajiri wa wazazi wake.Gerald alielekea moja kwa moja na kumnyanyua kwa nguvu na kumsogeza karibu yake kwa hasira "sikiliza wewe msenge sijui na sijali wazazi wako ni kina nani mpaka hujapewa adhabu ila nakuonya usifuatilie tena rafiki zangu wala usijaribu kurudia kile kitendo alichokufanyia maana nitakupiga kipigo kikali zaidi ya alichokupa Paul" aliongea Gerald kwa hasira na kumsukuma kwa nguvu mpaka alipodondoka,tukio hilo lilifanya wasichana waliokuwa mahali hapo kupiga Kelele,Gerald aliondoka kwa hasira na kurudi darasani.Alimkuta Kylie akiwa anamsubiri "umemfanya nini?" "tumeongea tu kama wanaume na nikamuonya basi..unasoma nini leo?" aliongea Gerald huku akifunga begi lake kutoa madaftari,ghafla kitambaa kikubwa kilionekana ndani ya begi lake "hilo shuka au! umekuja na shuka!" "nililiweka Jana nikasahau kulitoa,tuna mitihani karibu tunasoma nini?" aliuliza Gerald.Baada ya masaa kadhaa mwalimu Ngeze aliingia kufundisha somo lake la kemia kama kawaida,Gerald alisimama na begi lake na kuondoka taratibu "Gerald unaenda wapi,kaa chini" "sijisikii vizuri mwalimu naomba niende zahanati" "Gerald nishakuonya juu ya haya mambo una mitihani karibu" "naelewa mwalimu aliongea Gerald akijaribu kikunja uso wake kana kwamba aliugulia maumivu "haya nenda"alimruhusu na Gerald kuondoka haraka huku Kylie akimshangaa kwa mashaka.Gerald hakuenda zahanati alizunguka nyuma ya majengo ya shule na kuelekea mahali yalipopaki mabasi makubwa ya shule ya kubebea wanafunzi.Aliingia ndani ya moja ya mabasi hayo na kuelekea siti za nyuma,aliangalia huku na huko kuona kama kulikuwa na mtu yeyote karibu.Aliporidhika kuwa hakukuwa na mtu alifungua begi lake na kutoa shuka lake.

    Kengele ililia mlango kuashiria kuna mtu mlangoni wakati ule,Kate alishuka ngazi taratibu na kuelekea kufungua mlango "oh Gerald!" "hey Kate mambo.Sijui Sebastian nimemkuta?" "hayupo ametoka yuko duniani nafikiri" "nini! lakini aliniambia nije leo saa hizi" alijibu Gerald "ndiyo hayupo sasa,karibu ndani unaweza kuendelea na mazoezi wakati unamsubiri".Gerald aliingia ndani na kuketi juu ya Kochi refu "hukuenda shule leo?" aliuliza Kate huku akiwa anaelekea jikoni "yaani hapa nimeacha vipindi,huwezi kuamini muda huu niko ndani ya 'schoolbus' nimelala halafu nakuja hapa Sebastian hayupo" "nini! ndani ya basi! ulikuwa unafikiria nini!" alijibu Kate aliyekuwa jikoni "nilikuwa sina njia nyingine" alijibu Gerald huku akiangalia saa yake.Kate aliingea na bilauri kubwa la juisi na kumkabidhi "inabidi ujifunze kuingia humu Grotto bila Kulala ili kuepuka hayo matatizo ndo creators wote hufanya hivyo ukizingatia wewe ni supreme" "ndiyo bado najifunza" alijibu Gerald huku akimtazama Kate aliyekaa mbele yake akiwa amevalia kaptula fupi iliyombana sana na kuonyeaha sehemu kubwa ya mapaja yake.Umbo lake zuri na maziwa yake yaliyojaa yalionekana vizuri ndani ya shati lake jepesi "mnafikiri mtamshinda Kronos?" aliuliza Kate "hayo sijui lakini kaka yako aliniambia kuwa kuna uwezekano mkubwa tukamshinda" "kama wewe ni supreme kama mnavyodai basi haitakua shida maana una nguvu sana.Kronos siyo mtu rahisi kama anavyoonekana ni dream holder mbaya sana na anazidi kupata nguvu kila siku"aliongea Kate huku akijaribu kujigeuza kwa mapozi yaliyomchanganya Gerald "unajua nini kuhusu Kronos?" aliuliza Gerald "sijui vingi,Kronos akijaribu kutuua mimi na kaka zangu wote wawili alipogundua kuna uwezekano wa sisi wote tungekuwa creators alitaka ajiongezee nguvu.Unajua ukimuua creator kama na wewe ni creator unakuwa na nguvu zisizoelezeka unakuwa zaidi ya supreme.Kwa bahati nzuri baba yako creator Donald alitokea na kumfunga Kronos ndani ya jela kubwa aliyompeleka huku huku Grotto "umesema ulikuwa na kaka wawili! mmoja yupo wapi?" "Kwa bahati mbaya Kronos alimuua pamoja na wazazi wetu" "kwa huyo na wewe ni creator?" alizidi kuuliza Gerald "hapana kwa bahati mbaya alikuwa creator Sebastian tu ndiyo alibahatika mimi nikaishia kuwa dream holder wa kawaida tu" Gerald alitikisa kichwa kuonyesha kutafakari kuwa kumbe alikuwa anapambana na mtu mbaya sana "unafikiri naweza kumuua Kronos?" Kate alisimama na kumsogelea karibu "wewe unaonaje mmh utaweza kumuua umuokoe baba yako!" "Kate inabidi niondoke nisije nikakutwa ndani ya basi" Kate alizidi kujisogeza na kukaa juu ya Gerald huku akishika mdomo "no kaa na mimi zaidi" alijibu Kate kwa sauti laini huku akipeleka mdomo wake juu ya mdomo wa Gerald.Kate alipeleka mkono wake mpaka katikati ya suruali eneo la zipu na kupapasa taratibu "ooh utaondoka supreme wangu" aliongea Kate huku akisogeza uso wa Gerald karibu na uso wake kwa mkono wake wa kushoto huku mkono wake wa kulia ukiendelea kupapasa eneo lile."Kate hapana" aliongea Gerald kwa sauti ya chini kama mtu aliyekabwa.Kate alifungua zipu ya Gerald na kuingiza mkono wake mpaka alipozikamata nyeti za Gerald na kuzikusanya kwa pamoja huku akiziachia taratibu "oh Kate hapana" ushawishi wa Kate ulikuwa mkubwa sana,Gerald alilegea na kusogeza mdomo wake juu ya Shingo ya Kate na kuibusu taratibu.Alishuka na mabusu taratibu mpaka kwenye kifua kikubwa cha Kate na alikusanya maziwa yake kwa pamoja huku akiyapa mabusu polepole.Mikono yahttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/ Gerald ilishuka taratibu na kushika mapaja ya Kate ambapo alimnyanyua na kumlaza juu ya Kochi huku akiendelea kumbusu.Alichana shati la Kate na kumtembezea mabusu kuanzia kifuani kushuka tumboni huku akishika maziwa ya Kate.Kate alitetemeka kwa baridi Kali huku akitoa milio ya ajabu kuashiria kuzama kwenye tendo alilolianzisha mwenyewe.Mikono ya Gerald ilisogea mpaka juu ya nyeti za Kate na kumshusha nguo yake ya ndani taratibu na kumpapasa taratibu,hisia kali zilisababisha Kate ajiinue na kushuka taratibu.Gerald alifika kwenye hatua ambayo asingeweza kurudi nyuma alisafisha njia vizuri kabla ya kuingia.Mtanange ulikuwa mrefu na kila mmoja alionyesha ufindi wa hali ya juu.Baada ya masaa mawili ya tendo hilo Gerald alikurupuka kwa haraka kutoka chini alipolala "inabidi niondoke Kate,tusingetakiwa kufanya hivi namuheshimu sana Sebastian" "acha utoto bwana Gerald kwani Sebastian ndio nani! hii ni mimi na wewe" alijibu Kate,Gerald alitoka nje haraka na kubamiza mlango "Gerald! Gerald!" aliita Kate bila mafanikio ya kumuua Gerald asiondoke.

    Gerald alishuka ndani ya basi hilo na kucheki saa yake na kuona muda wa mapumziko ulikaribia,shuka lilikuwa limelowa eneo dogo, alilikusanya vizuri na kusimamisha.Suruali ilituna kwa mbele,alikunja uso wake kwa hasira na kuamua kushuka nje ya basi.Ghafla alikutana na Kylie nje kabisa hilo karibu na mlangoni alipomtazama kwa mshangao "Gerald! una tatizo gani!".



    Alimpiga Kofi zito sana lililomdondosha chini.Lisa alilia sana lakini hapakuwa na msaada wowote,alikabwa koo na kuanza kubakwa.Lisa aliingiliwa kimwili kwa mara ya kwanza tena kwa kubakwa.

    "Kylie! Kylie!" aliita Gerald kwa nguvu lakini Kylie alitembea haraka bila ya kumsikiliza,alimkimbilia na kumshika bega lakini aligeuka kwa hasira "usinishike Gerald!" "Kylie nisikilize basi,Kylie leo ni siku ya pili hutaki kuniongelesha eeh! usifanye hivyo Kylie "unategemea niongee na wewe nini Gerald baada ya kukukuta katika hali ile,unajua sikuelewi Gerald,unafanya mambo ambayo siyaelewi,mara uje na mashuka darasani,unaota ndoto za ajabu siku nyingine unapotea tu siku nzima hatukuoni.Kuna kitu unanificha Gerald kama hauko tayari kuniambia usitegemee nitakuongelesha tena" aliongea Kylie kwa hasira na kuondoka zake.

    Filimbi ya kocha ilipulizwa kwa nguvu sana kuita wachezaji wote uwanjani.Gerald alitembea kwa unyonge na kuelekea uwanjani huku hasira zikiwa zimemjaa "Gerald leo utafanya majukumu ya Paul nafikiri unajua peleka mipira mbele ukashinde" aliongea kocha.Alipata mpira na kukimbia nao kwa kasi,alimpiga kikumbo cha nguvu mchezaji mwenzake na kumrusha mbali sana kiasi cha kumtegua mkono.Kitendo hicho kilishangaza wengi kwa kuwa hawakutegemea jambo hilo kutoka kwa Gerald mchezaji aliyeonekana ni mzembe sana,walimzunguka mchezaji aliyejuruhiwa na Gerald kumjulia hali.Gerald aliondoka mahali pale bila hata ya kugawa pole wala kuomba samahani.Daniel alimtazama Gerald aliyekuwa akiondoka na kukaza macho yake.

    Kengele iligongwa kuita wanafunzi wote katika uwanja mkubwa wa shule huyo ambao walikusanyika kwa haraka na kwa wingi huku minong'ono yao ikileta kelele uwanjani hapo.Mwalimu mkuu alisimama mbele juu ya kijukwaa kidogo kilichokuwa mbele ya mkusanyiko wa wanafunzi wake.Uwepo wake mbele ulinyamazisha kabisa kelele za wanafunzi "habari zenu" alisalimia mwalimu mkuu "basi tusikilizane mara moja,kuna tatizo shuleni kwetu tena tatizo kubwa tu hasa kwa nyie wasichana,nafikiri mtakuwa mnalijua au mmelisikia na wengine kushuhudia.Kuna tatizo la wasichana kubakwa hapa shuleni kwetu" kauli hiyo iliamsha minong'ono tena kwa wanafunzi "tusikilizane tusikilizane siyo utani wala jambo la kufanyia mzaha.Kuna kesi kama sita hivi za wasichana kubakwa ofisini kwangu nafikiri baadhi mtakuwa unajua.Tumeshatoa taarifa polisi wanatusaidia cha msingi watoto wa kike muepuke mazingira hatarishi ili..." Kylie aligeuza na kumuona Gerald kwa mbali aliyekuwa akisikiliza kwa umakini,Gerald alitoka eneo lile taratibu huku akisukuma watu kuomba njia.Kylie aliona tukio lile na kuamua kumfuatilia kwa nyuma.Gerald alitembea haraka mpaka nyuma ya shule huku Kylie akiendelea kumfuatilia kwa Siri.Gerald alifika mahali na kusimama Kylie akajibanza vizuri pembeni ya ukuta kujificha "uko tayari tuondoke?" aliuliza Sebastian"tuondoke hatuna vipindi saa hizi" alijibu Gerald.Kylie aliona kila kitu hakuweza kumfahamu kijana aliyekuwa akiongea na Gerald "una uhakika hakuna aliyekuona?" aliuliza Sebastian kwa mashaka,Gerald aligeuka nyuma kana kwamba alihisi mtu,kwa haraka Kylie alijibanza vizuri kwenye ukuta huku akihema kwa nguvu.Baada ya sekunde chache Kylie alitoa kichwa chake kuangalia lakini hakuona mtu,Gerald na Sebastian hawakuonekana tena! Kylie alisogea taratibu huku akishangaa imekuwaje Gerald na yule kijana wapotee kwa muda mfupi vile "Gerald!" aliita Kylie bila majibu.Aliguswa bega na kushituka kwa nguvu"oh!" aligeuka nyuma na kukutana na Joseph "umenishitua!" "samahani sana" alijibu Joseph "soo.. what's up?" "aah Kylie nimekufuata kukuomba samahani kwa kile nilichokifanya Siku ile,nakiri kitendo kile kilikuwa ni cha udhalilishaji mpaka kumsababishia Paul asimamishwe shule.Samahani sana nachohitaji sisi kuwa marafiki kusiwe na chuki Kati yetu" "usijali nimeshakusamehe potezea tu" "kweli!" "yah,potezea" "asante sana Kylie.Mmh ulikuwa unafanya nini huku?" aliuliza Joseph "huku! hakuna cha maana nazurura tu,assemble inaboa watu wanabakwa tu.Tuondoke" aliongea Kylie na kuondoka.Joseph alitazama huku na huko huku akikaza macho yake na kuamua kuondoka.

    Katikati ya msitu mnene usiku huo watu wawili walionekana kuzungumza "Kronos Gerald anaanza kupata nguvu taratibu" "una uhakika na unachokisema?" "ndiyo nimeona kwa macho yangu mwenyewe itakuwa vigumu kumuua kama akipata nguvu" "ndio maana nilikuweka pale sikukuweka umshangae anavyopata nguvu,inabidi umuue fanya chochote ili afe nitakusidi ukihitaji msaada wangu" aliongea Kronos.

    Kesho yake Gerald alielekea shule kama kawaida,muda wote hakuzungumza chochote na Kylie.Kylie aliendelea kumnunia Gerald wakati wote.Muda wa mapumziko Gerald alitoka darasani,alishika njia taratibu kwenye korido ndefu huku akivuka madarasa,ghafla alirudi kwenye darasa Kati ya yale aliyoyapita,alimuona msichana aliyekuwa peke yake akijiinamia juu ya dawati lake,Gerald aliingia taratibu huku akimshangaa kwa mashaka "Beatrice! Beatrice!" aliita Gerald.Beatrice alinyanyua uso wake pole pole uliokuwa mwekundu sana kuonyesha alikuwa akilia."Beatrice mbona uko peke yako! ni mapumziko sasa hivi!" "najua" "kwa hiyo huendi nje?" aliuliza Gerald na kuketi karibu yake "hapana sijisikii tu" "Beatrice wewe ni msichana nzuri,mrembo na bado una thamani bila kujali chochote kile,hutakiwi kukosa raha kwa yaliyokukuta chukulia kama mapito tu na uendelee na maisha yako" "maneno hayo yalibubujisha machozi machoni mwa Beatrice "unajua!" "ndiyo,mama yako alimuambia mama yangu,umebakwa si ndio?" aliuliza Gerald kupata uhakika zaidi "kwa bahati mbaya mama yangu hataki kuniamini" aliendelea kulia "usijali ataelewa,ila siku nyingine usiwe peke yako kwenye mazingira hatarishi kuepuka jambo hili lisitokee tena" "unataka kuniambia inabidi niwe nalala na mtu chumbani,maana niliingiliwa chumbani nikiwa nimelala,hakuna anayeamini" aliongea Beatrice huku akifuta machozi Gerald alikaza macho yake na kumgeukia Beatrice "usijali,kuwa na amani,twende nje ukafurahie maisha" Beatrice alitikisa kichwa chake kukubali na kusimama.Gerald na Beatrice walitembea pamoja mpaka nje huku http://deusdeditmahunda.blogspot.com/Gerald akijaribu kumchekesha Beatrice ili asahau matatizo yake.Kwa mbali Gerald alimuona Sebastian akiwa amesimama karibu na jengo kubwa la utawala "Beatrice nisubiri hapa nakuja" aliongea Gerald na kuelekea kwa Sebastian"unafanya nini hapa Sebastian! Nipo shule saa hivi siwezi kwenda popote" "oooh! Yule msichana pale mzuri ni nani!" aliuliza Sebastian huku akimshangaa Beatrice "Beatrice,Kwa nini?" "Ndio girlfriend wako?" "Hapana,mama yake na mama yangu ni marafiki kwa hiyo namfariji tu maana na yeye alikumbwa na janga la kubakwa wiki iliyopita" "polisi hawajamkamata tu huyo mtu!" aliuliza Sebastian kwa mshangao "hapana hawajampata na wala hakuna dalili zozote za yeye kupatikana,inaonekana jamaa anabaka kwa uanglifu sana" "mmh! inaonekana kuna dream holder hapa shuleni kwenu "nini! Una maana gani!" "Inawezekanaje mtu akabaka wasichana wa shule yenu tu kama hawajui! ni obvious huyo mtu atakuwa anawajua hao wasichana wa shule yenu ina maana huenda na yeye ni mwanafunzi wa hapa au anahusika na hapa kwa namna moja au nyingine.Haiwezeka wote waliobakwa wasimjue na wengi wabekw kiajabu si ndio? uyo jamaa atakuwa tu ana uwezo fulani wa ajabu.Nafikiri hivyo" aliongea Sebastian.Kwa mbali Kylie alimuona Gerald akiongea na mtu ambaye alishindwa kumfahamu kwa kuwa hakuwa mwanafunzi na ilikuwa mara ya pili anamuona pamoja na Gerald.Alishangaa na kukaza macho yake "kwa kuwa umesema una vipindi basi nitakuacha leo kumbuka mazoezi makali muhimu una mda mchache sana" aliongea Sebastian na kurudi nyuma taratibu kuingia ndani zaidi ya jengo hilo na kupotea ghafla.Gerald aligeuka na kushuka ngazi zilizokuwa mbele yake,alishituka baada ya kumuona Kylie kwa mbali,alimpungia mkono huku akitabasamu "hey Kylie!" alisalimia Joseph kwa kushitukiza baada ya kutokea mbele ya Kylie.Tukio hilo lilimsononesha Gerald na kuamua kusogea kwa Beatrice aliyekuwa akimsubiri "samahani kwa kumchekesha" "ah usijali,yule mkaka uliyekuwa unaongea naye ni nani?" "Sebastian,ni ndugu yangu,mtoto wa shangazi yangu" " aah na Kylie?" "Oh! Kylie ni rafiki tu" "huoni wivu ukaribu wake na Joseph siku hizi?" "Wivu! Kwa nini nione wivu ni rafiki yangu tu.Ukizingatia wote tunajua kuwa anatoka na Paul.Subiri kwanza! Joseph! Unamjua Joseph!" alijibu Gerald kwa mshangao."Yah namjua niliwahi kutoka naye kabla sijaachana naye" alijibu Beatrice .Wakati huohuo Gerald na Beatrice walipishana na Kylie na Joseph "mambo Kylie" alisalimia Gerald bila kupata majibu " "mambo Beatrice" alisalimia Kylie na kila kundi likishika njia yake.Ghafla kitabu kikubwa kilidondoka kutoka kwenye begi la Joseph,Gerald aligeuka na kutazama "hey Joseph umedondosha kitabu chake" Joseph alishituka na kuokota kitabu kile kwa haraka "halafu sikiliza hutakiwi kuwa na hicho kitabu,hakuna mwanafunzi ambaye anacho umekipata wapi!" Joseph hakujibu kitu alifunga vizuri zipu ya begi lake na kuondoka pamoja na Kylie.Gerald aligeuka mbele kuendelea na safari yake " kitabu gani kile?" aliuliza Beatrice "ni jarida la shule limechapishwa na shule hakuna mwanafunzi ambaye analo kwa sababu shule bado haijaviuza ndo nashangaa yeye amekitoa wapi!" "au ameiba!" "nafikiri hivyo" alijibu Gerald huku akitembea na Beatrice.

    Gerald alimuacha Beatrice darasani alitembea taratibu kurudi darasani kwake,kabla ya kufika njiani alimuona Joseph akikatiza kuelekea ofisini kwa mwalimu Ngeze,aliweka begi nje na kuingia ofisini.Gerald alipoona kuwa Joseph alikuwa tayari amekwishaingia ofisini alikimbilia begi lile na kulifungua kwa haraka ambapo alitoa jarida alilomuona nalo Joseph.Alifunga begi vizuri na kuondoka.Alitembea kwa haraka mpaka darasani kwake na kushangaa kutomkuta Kylie darasani.Alielekea moja kwa moja mpaka kwenye meza yake na kuketi vizuri,alifungua vizuri jarida lile na kuanza kulisoma picha nzuri za shule yao pamoja na matukio mengi ya shule yao yalionekana vizuri kwa picha.Alizidi kufunua kurasa hadi kurasa mpaka alipoganda kwenye ukurasa mmoja ulioandikwa 'cooks club' aliona picha nyingi za wasichana aliokuwa anawajua ila cha ajabu walizungushiwa maduara makubwa vichwani mwao kwa peni.Gerald aliweza kusoma majina yaliyokuwa chini ya picha zile"Lilian,Mary,Agness,Aisha,Kelly, Beatrice... Kylie Kylie!" alishangaa Gerald na kuwaza sana juu ya picha zile.

    Wasichana wengi walitembea kwenye korido za shule huku wakizungumza na kucheka "nakwambia Beatrice yaani nilivyojitutumua kupika kile chakula halafu mwalimu akaniambia hakina chumvi aisee nilitamani hata kummeza" aliongea Kylie huku wasichana wenzake wakicheka.Ghafla Joseph alitokea mbele yao "Beatrice tunaweza kuongea" aliongea Joseph.Beatrice alimsogelea Joseph taratibu "huyo jamaa ni nani?" aliuliza msichana mmoja aliyeitwa Aisha " ni Joseph anasoma biashara" alijibu mwingine aliyeitwa Jenifer "ana uhusiano gani na Beatrice?" aliuliza Kylie "mwenzangu,wanatoka wote hao ila huyo jamaa ni kiwembe balaa yaani playboy tu.Anachezea wasichana kisa kwao ni matajiri" alijibu Aisha.Lisa alishangaa na kumuangalia Joseph aliyekuwa akimshika Beatrice kiuno chake.Lisa alitembea haraka kuwasogelea "Lisa unakwenda wapi!" aliongea Kylie kujaribu kumzuia "sikia wewe Joseph kama umezoea kutongoza na kuchezea visichana vyako huko tunakuomba usimsumbue rafiki yetu" Joseph alishangaa "kwani wewe tatizo lako nini au unamuonea wivu mwenzako!" "hahaha! eti nione wivu sikia kaka eeh tunajua tabia zako sijui unafikiri sifa kubadili wasichana na kuwachezea wewe usituharibie mwenzetu na ukiendelea na huo ujinga tutakufanya kitu mbaya" aliongea Lisa na kumsukuma kwa masingi huku wakimcheka.Beatrice alitikisa kichwa chake na kuondoka lakini Joseph aliwahi mkono wake "niache!" alifoka Beatrice na kumpiga Kofi zito huku akimsukuma mpaka alipodondoka chini " malaya wewe kumbe ndio tabia zako!" aliongea Beatrice kwa jazba na kuondoka huku rafiki zake wakimfuata nyuma.Joseph alibaki chini huku akihema kwa hasira,machozi ya hasira yalimtoka,alinyanyua mkono wake na kuyafuta taratibu kwa hasira.

    Kylie aliingia darasani,Gerald alinyanyua uso wake na alipomuona alifunga jarida lile haraka na kuliweka chini ya meza.Kylie alifika n kuketi taratibu huku akifungua begi lake na kutoa vitabu vyake bila kusema chochote kwa Gerald "Kylie utaendelea hivi mpaka lini..mmh..! unataka kumaliza urafiki wetu hivi!" aliongea Gerald lakini Kylie hakujibu neno lolote " huwezi kujibu siyo! anyway unanisikia tafadhali kaa mbali na Joseph urafiki wenu muuvunje" aliongea Gerald.Kylie aligeuka kwa dhihaka "kwa sababu mimi na wewe hatuongei basi unafikiri sitakiwi kuongea na kila mtu" "nisikilize Kylie nakuambia hivi kwa faida yako,Joseph siyo mtu mzuri" "najua kwamba anatongoza wasichana ovyo lakini hilo halimfanyi yeye kuwa mbaya na wewe kujiona Safi.Halafu tangu lini unanichagulia marafiki! hujui mipaka yako!" "Kylie inabidi unisikilize,Joseph ndiye mbakaji ndiye anayebaka wasichana wote hapa shuleni na ndiye aliyembaka Lisa,Kelly,Aisha,Beatrice na atakubaka na wewe Pia" aliongea Gerald kwa msisitizo "Gerald wivu wako usikufanye umsingizie mtoto wa watu kisa tu humpendi na hata kama yeye ndio mbakaji hawezi kunibaka mimi" "Kylie huwezi kujua atakavyokubaka,haji kama unavyofikiri" "hivi Gerald huna la maana la kuongea kama huna kaa kimya maana utaniboa" alijibu Kylie "okay basi nisikilize kwa mara ya mwisho sitaongea tena,leo usiku wakati unalala usifunge dirisha lako" "sina haja ya kutofunga dirisha langu" alijibu Kylie.Gerald aligeuka na kuendelea kusoma huku akiwa kimya,Kylie alimuangalia na kuendelea kusoma.

    Saa sita usiku siku hiyo nje ya nyumba ya Kylie Gerald alionekana kuzunguka huku na huko,ghafla Sebastian alitokea na kumsogelea kwa haraka "mbona umeniita usiku huu kuna nini!" " nahitaji msaada wako Sebastian.Kylie yupo kwenye hatari kubwa saa hivi ya kubakwa" " kubakwa!" "Yah na..na..ulikuwa sahihi mbakaji huenda ni dream holder anabaka wasichana kupitia ndoto.Hapa ni nyumbani kwa rafiki yangu nahisi anabakwa usiku huu " aliongea Gerald kwa hofu " Gerald! hebu tulia relax,unataka nikusaidie nini?" " msaada wowote ule nataka niingie kwenye ndoto ya huyo msichana nikamuokoe.Uliniambia mimi ni supreme nafanya lolote naingia kwenye ndoto za yeyote nahitaji msaada wako" "sawa Gerald naelewa wewe ni supreme ila hujajifunza kuingia kwenye ndoto za watu ni vigumu" alijibu Sebastian kwa sauti ya chini " no! Sebastian huyu msichana ni rafiki yangu inabidi nimuokoe.Nenda wewe umuokoe wewe unaweza si ndio!" " Gerald natamani sana niingie nimsaidie ila naweza nikasababisha akafa kwa sababu rafiki yako siyo dream holder" " usiniambie tunamuacha abakwe!" aliongea Gerald kwa hasira "ngoja nifikirie" aliongea Sebastian.Baada ya sekunde chache alimgeukia Gerald "sasa utaingiaje kwao utavunja mlango au" "nilimuambia aache dirisha wazi asilifunge.Tuombe Mungu awe amenisikiliza" aliongea Gerald "sasa chukua hiki kidonge cha usingizi ingia ndani ukalale karibu yake" Gerald alichukua kidonge kile haraka na kupanda dirishani,alifungua dirisha taratibu na kuhema kwa nguvu baada ya kulikuta wazi.Aliingia ndani taratibu na kumtazama Kylie aliyekuwa amelala kitandani na kuanza kutikisa kichwa chake.Gerald alitafuna kidonge kile haraka na kuingia uvunguni mwa kitanda.

    "Nini! yaani tumekuja Grotto! nilikwambia nataka kwenda ndani ya ndoto za rafiki yangu Kylie na siyo huku" " Gerald wewe huwezi kwenda moja kwa moja kwa sababu hujajifunza ndio maana ulipolala umekuja huku.Utaenda ukitokea huku kuwa mpole kama unataka kumuokoa rafiki yako.Walitembea mpaka walipofika nyumbani kwa Sebastian na kuingia ndani " lala juu ya Kochi hapo" aliongea Sebastian.Mda huo Kate aliwasili kwa haraka baada ya kusikia sauti zao "Sebastian kuna nini!" "kuna tatizo.Sikiliza Gerald unalala tena hivyo utakuwa katika dimension tatu za ndoto hii inaweza kuondoa maisha yako" " Sebastian hatuna muda suala la kufa sitaki kulisikia tumuokoe Kylie ndo la msingi" alijibu Gerald kwa ujasili." Sawa kunywa tena hiki kidonge.Halafu Kate mshikilie Gerald kwa nguvu maana atatikisika huku hakikisha hajiumizi" Gerald alikunywa kidonge kile na Kulala mara moja "kaka Sebastian una uhakika na mnachokifanya!" aliuliza Kate kwa mashaka " sijui,ambacho nna uhakika nacho ni kwamba Gerald anaweza kufa.Lakini anaonekana anataka sana kumuokoa rafiki yake" aliongea Sebastian na kupotea ghafla.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Gerald na Sebastian walitembea na kupanda juu ya kilele cha mlima mrefu sana "tunafanya nini hapa?" aliuliza Gerald,Sebastian alimshangaa Gerald aliyeanza kuvuja damu puani "unataka damu puani" Gerald alinyanyua mkono wake na kufuta damu iliyokuwa ikitoka puani mwake "asante,tunafanya nini hapa?" aliuliza Gerald "Gerald una uhakika unataka kufanya hivi maana Kylie hata akibakwa hawezi kufa lakini wewe unahatarisha maisha yako" "Sebastian tunafanya nini hapa nimechoka kukuuliza!" Sebastian aligeuka mbele na kunyoosha mikono yake " mimi ni creator kumbuka natengeneza daraja tulia" upepo mkubwa ulivuma huku tetemeko dogo lilitokea.Mbele yao lilitokea tufe kubwa liling'ara kama jua huku likiwa na rangi nyeusi katikati "tembea ukaingie pale kwenye rangi nyeusi,fanya haraka ukamuokoe Kylie" aliongea Sebastian kwa sauti ya juu ili Gerald aweze kumsikia kwa sababu upepo mkubwa ulivuma.Gerald alitembea taratibu huku akiziba macho yake kwa sababu ya mwanga mkali aliingia taratibu kama alivyoelekezwa.

    Alifungua macho yake na kumuona Joseph juu ya kitanda cha Kylie akimkaba huku akijaribu kumvua nguo " Joseph!" aliita na kumkimbilia kumpiga kikumbo kizito kilichomuangusha Joseph chini Joseph alinyanyuka na kumtazama "Gerald!" alishangaa " ndiyo ni mimi,unakumbuka nilikuambia usiguse tena rafiki zangu nafikiri hukunielewa" aliongea Gerald kwa hasira.Joseph alirusha ngumi nzito iliyomrusha Gerald hadi kitandani mwa Kylie.Kylie alijaribu kuwatazama lakini hakuweza kuona sura zao.Joseph alimkaba koo Gerald na kumshushia ngumi mbili za uso lakini y tatu Gerald aliitoa vizuri na kumpiga kichwa kilichomrusha Joseph chini.Gerald alimsogelea Joseph na kumpiga ngumi nyingi za uso pamoja na tumboni.Joseph alisimama na kumpiga teke zito lililomrusha Gerald ukutani na kupasua picha kubwa ya Kylie.Gerald alinyanyua uso wake ambao alianza kubadilika rangi na kuwa wa bluu Joseph alishangaa "Supreme!" alishangaa Joseph na kukimbia huku Gerald akimkimbiza.

    Kylie alishituka kutoka usingizini huku jasho likimtoka na kuhema kwa nguvu,alishangaa kuona watu wawili wakitoka kwa kasi sana kupitia dirishani kwake.Alipiga kelele kwa uwoga na kuwashitua wazazi wake waliomkimbilia kwa haraka "Kylie! Kylie! uko sawa!" aliongea mama yake huku akiufuta uso wake kwa kitambaa "itakuwa ameota ndoto mbaya tu" aliongea baba yake.Walimtuliza mtoto wao kwa muda mpaka alipopoa na kuamua kuondoka "funga dirisha lako" aliongea baba yake wakati wakiondoka na kufunga mlango wa Kylie.Kylie alisimama na kuelekea kufunga dirisha lake,alirudi kitandani.Aligeuza Shingo yake na kuokota picha yake iliyopasuka fremu na kioo.Alikumbuka mmoja wa mtu aliyemuona kwenye ndoto alidondokea picha yake na kuipasua.Aliogopa sana ilikuwaje ndoto ile.

    Usiku huo Gerald alirudi nyumbani akiwa mchovu sana,uso wake ulijaa makovu huku damu nyingi zilivuja puani kwake,alitembea kwa kupepesuka maana hakuweza kuona sawasawa,uwezo wake wa kuona ulianza kufifia.Jambo zuri ni kwamba alikaribia mlango wa nyumba yao na kuufungua taratibu,mama yake aliyeketi sebuleni usiku huo wa saa tisa akiwa ana hofu na mwanaye kutorejea nyumbani alinyanyuka kwa haraka baada ya kuona mlango ukifunguliwa.Alipatwa na mshituko baada ya Gerald kudondoka mlangoni kabisa akiwa anajaribu kuingia ndani "Gerald!" alishituka mama yake na kumkimbilia "Gerald! " aliendelea kuita mama yake na kunyanyua simu yake kutoka kwenye Kochi.

    Ndani ya hospitali kubwa ya Broodville katika chumba kimoja Gerald alionekana akiwa amelala juu ya kitanda cha mgonjwa mahututi huku akisaidiwa kupumua na machine.Mama yake aliangalia sura ya mwanaye iliyokuwa imejeruhiwa sana na kumwaga machozi,alisali kuomba mwanaye aamke tena kutoka kwenye usingizi wa nusu umauti.Mda huohuo Kylie aliingia ndani kwa haraka " shikamoo" alisalimia Kylie na kumkumbatia mama yake Gerald "anaendeleaje?" "hamna chochote hajaamka tokea Jana nilivyomleta hapa" aliongea mama Gerald kwa sauti ya unyonge "my God! nani kafanya hivi!" aliongea Kylie baada ya kushangazwa na majeraha makubwa aliyokuwa nayo Gerald usoni " hata sijui naogopa sana,masikini mwanangu" alijibu mama Gerald huku akilia.Kylie alimsogelea na kumkumbatia "usijali mama atapona".Muda huohuo daktari aliwasili na kumfanya mama Gerald anyanyuke kwa haraka "dokta mwanangu anaendeleaje,je atapona? hali yake ikoje?" "usijali mama yangu,unajua tabia za mwanao?" "tabia za mwanangu! una maana gani dokta? mwanangu ni kijana mzuri tu na hana tabia yeyote mbaya inayoweza kumfanya awe katika hali hiyo" "hapana mama sina nia mbaya ila kwa hayo makovu usoni anaonekana alikuwa akipigana na mtu" aliongea daktari.Kauli hiyo ilimshitua Kylie na kugeuka kuangalia makovu usoni mwa Gerald huku akikumbuka watu aliokuwa akiona wakipigana kwenye ndoto yake "lakini kinachomweka hapo siyo hayo majeraha maana siyo makubwa sana ila kinachomweka hapo hata sisi wenyewe tumeshangaa na hatujawahi kukutana na kesi kama yake" una maana gani dokta?" aliuliza mama Gerald kwa mashaka "kwa inavyoonekana ni kwamba ubongo wake umefanya kazi kubwa sana kuliko kawaida mpaka seli zake zilianza kutengana.Ni kama aligawanywa au sijui nisemeje kama ubongo wake uligawiwa kwa watu watatu tofauti!.Hivyo seli zake za ubongo zimeachana.Na tumegundua alitumia dawa Kali za usingizi,kwani ana tatizo la Kulala?" "hapana dokta hana tatizo hilo!" alijibu mama Gerald "tumekuta dawa hiyo kwenye damu yake,nafikiri kama kila kitu kikiwa sawa ataamka baada ya siku tatu baada ya seli zake kurudiana" aliongea daktari uyo na kuondoka kumuacha mama Gerald akigusa kichwa cha mwanaye.Kylie alikaza macho yake baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwa daktari aliingiwa na wasiwasi huenda Gerald alihusika na ndoto yake.

    Kylie alikaa mwenyewe darasani akiwaza juu ya afya ya Gerald na ndoto aliyoota,mawazo yalijaa kichwani mwake je Gerald alijuaje kuwa Joseph angejaribu kumbaka usiku ule? na alijuaje mbakaji kuwa alikuwa ni Joseph? ndoto aliyoota na kuona watu asiowatambua usiku ule walikuwa ni kina nani?. Kylie aliwaza sana bila majibu kila wakati alikumbuka ndoto ile na kuongeza mawazo kichwani mwake.

    Baada ya vipindi darasani Kylie alishika njia kuelekea dukani kujipatia chakula huku mawazo yakimsonga aliomba Mungu sana Gerald apone ili asije akafa akiwa ana chuki naye.Ghafla aligongana kikumbo na mwanaume mmoja na kuangushwa chini,mwanaume huyo alivaa koti lenye kofia iliyofunika uso wake "samahani sana" "aah usijali..subiri,Joseph!" alishangaa Kylie huku akisimama,Joseph alianza kuondoka lakini Kylie alimkimbilia na kusimama mbele yake "oooh my God! Joseph uso wako umepatwa na nini!" alishangaa Kylie baada ya kuona uso wa Joseph ukiwa umevimba na kujeruhiwa vibaya "hamna kitu Kylie" "usiniambie hamna kitu wakati uso wako umevimba,una majeraha na hata Gerald ana tatizo hilo hilo sema lake kidogo kubwa.Najua ulichojaribu kufanya jana usiku" Joseph alishituka na kumgeukia Kylie "unajua..sikia Kylie,naomba unisamehe" "kukusamehe wala sio tatizo,niko radhi kukusamehe kama ukiniambia ukweli wote.Gerald alijuaje kama wewe ndiye unayebaka wasichana hapa shuleni na kwamba ungenibaka jana usiku.Pili niliona kwenye ndoto watu wanapigana na leo wewe na Gerald wote sura zenu zina majeraha.Ukiniambia ukweli niko tayari kukusamehe kabisa" alisema Kylie.Joseph alihema kwa nguvu "sikia Kylie,Gerald sijui alijuaje kuhusu mimi labda alihisi na alikuwa sahihi,na kuhusu ndoto yako sijui chochote binadamu huwa tunaota na wewe ni binadamu kwa hiyo umeota kawaida" "na hayo majeraha yenu usoni?" "Kylie mbona..." "mmmh kama huwezi kunijibu maswali yangu naomba urafiki wetu uishie hapa hapa,sawa.Shika zako nishike zangu" aliongea Kylie kwa hasira na kuondoka Joseph alijaribu kumsimamisha bila mafanikio.Alivaa kofia yake na kuondoka kwa hasira.Maisha yalimbadilikia Joseph hakuwa na rafiki shuleni hapo kwa sababu ya tabia yake mbaya ya kutongoza wasichana ovyo na kitendo cha yeye kusababisha Paul kipenzi cha shule asimamishwe shule kiliongeza Joseph kuchukiwa zaidi.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya siku tatu shule iliandaa sherehe kubwa ya kutimiza miaka hamsini tokea kuanzishwa kwake.Siku hiyo ilikuwa ni ya kitofauti maana hakukuwa na vipindi vilivyokuwa vikiendelea.Mziki mkubwa ulisikika kuburudisha nyoyo za wanafunzi,michezo mbalimbali iliendelea kufanyika kufanya siku hiyo iwe ya kipekee "tusikilizane wote,naomba tusikilizane" sauti ya mwalimu mkuu ilisikika kutoka kwenye kipaza sauti "najua wote mna furaha na furaha yenu si kwamba tu shule yetu inatimiza miaka hamsini ila wengi wenu mna furaha kwa sababu hakuna vipindi leo" wanafunzi wote walicheka na kupiga kelele "tuachane na hayo,bado leo ni siku muhimu sana kwa shule yetu,tunatimiza miaka hamsini ya kutoa elimu bora nchini.Nisiongee mengi nimkaribishe mgeni mualikwaa bwana Harrison.Kwa wale msiomjua bwana Harrison ni mtoto wa mwenye shule zetu hizi.Alitakiwa aje mwenyewe sema ubize kidogo, akashindwa ila hakijaharibika kitu.Bwana Harrison karibu".Makofi yalipigwa kumkaribisha Mr Harrison jukwaani,alionekana mdogo ki umri kama tu mmoja wa wanafunzi shuleni hapo "habari zenu wote,mna bahati sana ya kuwa wanafunzi wa Broodville high school,sio shule nyingi zina sifa kama za kwetu nadhani nyie wenyewe mnajua hilo.Ubora wa elimu na mambo mengine bora kabisa tunayotoa mahali hapa hakuna pengine popote panatoa haya.Mtu asiwadanganye kwamba ana ubora kuliko sisi nyie wenyewe ni mashahidi mnajua tumekuwa wangapi kitaifa mwaka huu na kila mwaka,sasa mtu awadanganye nini!.." aliongea maneno mengi mazuri yaliyohamasisha wanafunzi kuipenda zaidi shule yao na kujivunia kusoma pale "ana raha huyu" "kwa nini?" aliuliza Paul "yaani mtoto mdogo lakini maisha yake mazuri sana,pesa kwao ipo sisi tunasoma tu hapa" alijibu Kylie.Paul alitabasamu na kuweka mkono wake juu ya bega la Kylie,alifurahi kurudi shule na kikubwa zaidi alifurahi kumuona Kylie kwa mara nyingine "sijamuona Gerald tokea nimekuja!" "alikuwa anaumwa hakuja shule kama kwa siku mbili hivi nafikiri hajapona bado" alijibu Kylie.Mgeni rasmi aliongea kwa muda mrefu lakini hatimaye alimaliza na wanafunzi wote walimpigia makofi kumshukuru kwa maneno yake ya faraja.

    Kocha wa shule na timu ya http://deusdeditmahunda.blogspot.com/THE THUNDERS hakuwa nyuma kuandaa mechi ya kirafiki dhidi ya timu jirani ya THE BEASTS.Wanafunzi wengi walijaa uwanjani kutaka kushuhudia mechi hiyo,kikubwa zaidi walitamani kumuona Paul akicheza tena kwa kuwa nyota wao alirudi.Kylie alikaa kwenye moja ya jukwaa kuungana na mashabiki wengine kushangilia.Uwanja mzima waliimba jina la Paul kwa nguvu.Baada ya dakika chache timu ziliingia uwanjani na kupokelewa na makofi mazito,timu ya thunders walipendeza na jezi zao nyeusi zilizokuwa na mistari ya rangi nyekundu huku Beasts wakipendeza na jezi zao za rangi nyeusi "okay,tisikilizane hii mechi tuitumie vizuri kama mazoezi kujiandaa na michuano ya kitaifa ambayo ipo mbele yetu,Paul vizuri umerudi utaongoza mashambulizi Daniel wewe utaongoza defense.lets go!" aliongea kocha wao kwa nguvu.Mwamuzi alipuliza kipenga kuita timu zote katikati.Mgeni rasmi aliketi karibu kabisa ili kushuhudia mechi hiyo muhimu ya kusheherekea miaka hamsini ya shule yao.





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog