Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

THE LOVE YOU HAD BEFORE (PENZI ULILOKUWA NALO KABLA) - 5

 







    Simulizi : The Love You Had Before (Penzi Ulilokuwa Nalo Kabla)

    Sehemu Ya Tano (5)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Laurence hakutaka kusikia, japokuwa aliambiwa kwamba hakutakiwa kwenda nyumbani kwa kina Evadia lakini kutokana na mapenzi mazito aliyokuwa nayo, kesho yake tu akajikuta akiwa huko.

    Mapenzi yalimsumbua, hakutaka kuona akimuacha msichana huyo kiwepesi kama ilivyotakiwa kuwa. Alipofika nyumbani hapo, hakuingia ndani, alibaki nje na kuanza kugonga.

    Katika kipindi hiki hali ilikuwa tofauti, kulikuwa na mlinzi getini ambaye aliambiwa wazi kwamba hakutakiwa kumruhusu mtu aliyeitwa Laurence kuingia ndani ya nyumba hiyo.

    Kitendo cha Laurence kugonga geti, likafunguliwa na mlinzi, kwanza alishtuka, hakutegemea kumuona mlinzi mahali hapo kwani kitu alichojua ni kwamba mama Evadia angekuja kufungua kama zamani.

    “Karibu kaka,” alimkaribisha mlinzi yule.

    “Asante. Nimewakuta wenyewe?”

    “Ndiyo! Unaitwa nani?”

    “Naitwa Laurence. Nimekuja kumsalimia Evadia,” alijibu Laurence.

    “Kumbe wewe ndiye Laurence?”

    “Ndiyo kaka!”

    “Hautakiwi kuingia humu.”

    “Kwa nini?”

    “Hayo ni maagizo, hautakiwi kuingia humu,” alisema mlinzi huku akimwangalia Laurence usoni.

    Alichokisikia, hakukiamini, alimwangalia mlinzi yule mara mbili mbili, alihisi kama hakusikia vizuri, akamwambia arudie, mlinzi akarudia kwamba hakutakiwa kuingia ndani ya nyumba ile, hilo halikuwa ombi bali agizo.

    Laurence hakuwa na jinsi, alichokifanya ni kuondoka mahali hapo huku akiwa na huzuni kubwa. Bilionea yeye, kisa tu kujiweka katika hali ya umasikini, leo hii aliambiwa kwamba hakutakiwa kuingia ndani ya nyumba hiyo.

    Hilo likamfanya kumpigia simu Matilda na kumwambia kila kitu kilichotokea huko. Alihuzunika sana, wakati mwingine alipokuwa akizungumza naye, alikuwa akitokwa na machozi.

    “Pole sana Laurence, ila naomba nikazungumze nao,” alisema Matilda.

    “Kuhusu nini?”

    “Wewe hapo!”

    “Hapana bwana, achana nao. Nimeamia sana lakini sina jinsi, ngoja nipumzike, nahisi mapenzi yataniumiza zaidi kama nitalazimisha penzi kwa Evadia,” alisema Laurence.

    “Basi sawa.”

    “Ok! Kesho naondoka kuelekea Marekani kupumzika, sidhani kama nitaonana tena na Evadia, nitatafuta msichana mwingine wa kumuoa,” alisema Laurence.

    “Kwa hiyo nikamwambie ukweli kuhusu wewe?”

    “Haina tatizo. Kwa kuwa sitomhitaji tena, hakuna tatizo,” alisema Laurence.

    Upande wa pili, Matilda hakuridhika, kitendo cha bosi wake kukataliwa kilimuumiza mno, alichokifanya mara baada ya kumaliza kuzungumza naye ni kuondoka na kuelekea Mabibo, alitaka kuzungumza na wote wawili, alitaka kujua sababu iliyomfanya Evadia kumkataa Laurence.

    Kutokana na kutokuwa na foleni barabarani, alitumia dakika chache mpaka kufika Mabibo. Alichokifanya ni kuingia katika mtaa aliokuwa akiishi Evadia, baada ya dakika kadhaa akafika nje ya geti la nyumba hiyo, akaanza kupiga honi.

    “Nikusaidie nini dada?” aliuliza mlinzi.

    “Nahitaji kuwaona wenyewe.”

    “Unaitwa nani?”

    “Matilda.”

    Mlinzi akalifungua geti na kuingia ndani. Moyo wa Matilda ulikuwa kwenye maumivu makali, kila alipofikiria jinsi Evadia alivyomkataa Laurence, moyo wake uliumia mno, hakuamini kile kilichokuwa kimetokea kwani huyo Laurence aliyekataliwa alikuwa miongoni mwa mabilionea wakubwa nchini Tanzania.

    Alipoliingiza gari ndani, Matilda akateremka na kisha kuelekea ndani ya nyumba hiyo, mlango wa sebuleni ukafunguliwa na mfanyakazi na kukaa katika makochi makubwa.

    Wala hazikupita sekunde nyingi, Evadia na mama yake wakatokea sebuleni hapo ambapo wakasalimiana kwa kukumbatiana kisha kukaa kochini.

    “Evadia, hebu nieleze tatizo nini,” alisema Matilda.

    “Tatizo kuhusu nini?”

    “Umefikia wapi na Laurence?”

    “Tumefikia sehemu nzuri tu.”

    “Ndoa ipo?”

    “Ndoa?”

    “Ndiyo!”

    “Bado tunalizungumzia hilo,” alisema Evadia.

    Matilda akamwangalia Evadia usoni, alitamani kumwambia ukweli kuhusu Laurence lakini kila alipotaka kufanya hivyo, akasita kabisa. Moyo wake ulijawa huruma mno, alimuona Evadia kuwa msichana mpumbavu ambaye bahati ilimjia mpaka mlangoni ila pasipo kujua, akaipiga teke.

    “Evadia….”

    “Abee dada.”

    “Hivi kweli umemkataa Laurence?” aliuliza Matilda, wote wakashtuka, wakajua kwamba Laurence alimwambia msichana huyo. Akabaki akiangaliana na mama yake.

    “Kweli umemkataa Laurence?” alilirudia swali lake.

    “Dada…”

    “Niambie ukweli!”

    “Sina cha kuongea.”

    “Au kwa sababu ya umasikini wake?”

    “Hapana!”

    “Kumbe kwa ajili gani? Haukumbuki kwamba alikusaidia figo yake ili mradi uweze kupona?”

    “Nakumbuka dada.”

    “Niambie tatizo nini?”

    “Hakuna kitu”

    “Ila umemkataa?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kimyaa.

    Matilda alionyesha chuki za waziwazi kiasi kwamba wote wawili wakaogopa. Matilda alionyesha kuchukizwa kwa kile kilichotokea, kitendo cha bosi wake kukataliwa kisa tu alionekana kuwa masikini ilimuumiza mno moyoni mwake, akabaki akimwangalia Evadia kwa hasira kubwa.

    “Evadia, wewe ni msichana mpumbavu,” alisema Matilda huku akionekana kuchukizwa.

    “Wewe ni mpumbavu kwa sababu humfahamu Laurence ni nani, amekuja kwako kwa lengo gani, yaani kisa masikini unamkataa Laurence, kweli una akili wewe? Hivi unamjua Laurence wewe?” aliuliza Matilda huku akimwangalia msichana huyo usoni.

    “Nisamehe dada…”

    “Evadia, kumsikiliza mama yako umekosa bahati, Laurence amekuja kwako, amejifanya masikini, amekusaidia kwa kutoa figo yake, mwisho wa siku unamwambia haumtaki. Evadia, hakuna mwanamke yeyote ambaye angekuwa na uwezo wa kumkataa Laurence,” alisema Matilda maneno ambayo yaliwafanya wote kubaki kimya.

    “Unatumia mtandao gani wa simu?”

    “Tritelcom.”

    “Unamjua mmiliki wa mtandao huo?”

    “Hapana.”

    “Evadia, sikutaka kukwambia hili, hata Laurence hakutaka ulifahamu hili ila kwa kuwa umemuacha na yeye ameamua kuondoka na kutorudi tena, ngoja nikwambie tu,” alisema Matilda.

    “Kuna nini dada.”

    “Huyu Laurence unayemsikia kwamba ni bilionea, mwenye fedha nyingi, kampuni za simu na mafuta, ndiye huyuhuyu aliyekufuata wewe na kujifanya masikini, fedha zote nilizokuwa nikiwapa, ni zake, zile milioni thelathini za hospitalini, ni zake, japokuwa aliniambia kwamba unamkataa, nikamwambia hata fedha asitoe kuwasaidia, ila yeye akasema fedha ziendelee kutoka kwani alikupenda sana, mwisho wa siku, kwa kutokujua kwako, kwa kupenda wanaume wenye pesa, umeamua kumuacha Laurence, ni aibu iliyoje,” alisema Matilda kwa uchungu mno.

    “Unasemaje?” aliuliza mama Evadia huku akionekana kutokuamini.

    “Mmechezea bahati. Laurence ameumia mno, amezungumza nami huku akilia, hivi anajiandaa kwenda Marekani kupumzika, umeuumiza mno moyo wake,” alisema Matilda, hapohapo akasimama.

    Wawili hao wakabaki wakimwangalia Matilda, hawakuamini kile walichokisikia, walitamani msichana huyo arudie tena kuwaambia juu ya Laurence kwani walihisi kwamba walisikia vibaya.

    Hapohapo Evadia akaanza kulia sana, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, hakuamini kilichokuwa kimetokea, hakuamini kama mwanaume aliyekuwa amemuacha ndiye yule ambaye kila siku alisikia kwamba alikuwa bilionea.

    Pamoja na biashara walizokuwa wakizifanya, lakini bado fedha walizopewa na Matilda ndizo zilezile ambazo ziliwasaidia kuyafanya maisha yao kuwa juu.

    Machozi yalimmwagika machoni mwake lakini hilo halikuweza kubadilisha matokeo, bado ukweli ukabaki palepale kwamba alichezea bahati ya kumkataa mwanaume bilionea, tena kwa dharau kubwa.

    “Dada…naomba ukaniombee msamaha kwa Laurence….” alisema Evadia huku akilia, hapohapo akapiga magoti mbele ya Matilda, si yeye tu aliyefanya hivyo, bali hata mama yake.



    Moyo wa Dickson ulikuwa kwenye maumivu makali, hakuamini kile alichokisikia kwamba mpenzi wake hakutaka aingie ndani ya nyumba hiyo kwa sababu tu alikuwa na mwanaume mwingine ndani ya nyumba hiyo.

    Dickson angeweza kujifanya kiburi, kuleta vurugu mahali hapo na kuingia kinguvu lakini kila alipomwangalia mlinzi yule, alikuwa na mwili uliojazia mno, tena mkononi alishika bunduki, hivyo akaogopa.

    Akanyong’onyea, kila alipomfikiria msichana huyo moyo wake ulimuuma sana, hakujua nyumbani angesema nini, hakujua ni kwa jinsi gani angewaambia wazazi wake juu ya kile kilichotokea nchini Rwanda.

    Hakuwa na jinsi, hakutaka kuendelea kukaa mahali hapo, alichokifanya ni kupiga hatua kurudi nyuma, kwa sababu dereva taksi hakuwa ameondoka mahali hapo, wakarudi garini na kurudi walipotoka.

    Akashindwa kuvumilia, kile kilichotokea kilikuwa aibu kubwa kwake, alishindwa kuyazuia machozi kububujika mashavuni mwake, japokuwa Buka alimbembeleza sana lakini Dickson hakutaka kunyamaza.

    “Nyamaza Dickson….”

    “Hivi kweli Luciana ananifanyia hivi!”

    “Pole sana, achana naye.”

    “Inaniuma sana, unajua tumeanza mbali sana na Luciana,” alisema Dickson.

    Machozi yake hayakubadilisha kitu chochote kile, alichokikuta nchini Rwanda ndicho kilichokuwa kimetokea, mpenzi wake alichukuliwa na mwanaume mwingine.

    Hakutaka kubaki nchini Rwanda, kwa kuwa alikata tiketi ya kuja na kuondoka, siku iliyofuatia alikuwa ndani ya ndege akirtudi nchini Tanzania. Bado maumivu ya mapenzi hayakupungua moyoni mwake, muda mwingi alibubujikwa na machozi tu.

    Alikosa tumaini, wakati anamfikiria Luciana hapo ndipo jina la Evadia likaanza kujirudia kichwani mwake. Akaanza kumkumbuka msichana huyo ambaye aliachana naye kipindi cha mwaka mzima uliopita kisa tu alimpata Luciana ambaye aliamua kuumiza moyo wake.

    Hakukuwa na kitu alichokifikiria kwa wakati huo kama kurudi kwa Evadia na kumuomba msamaha juu ya kile kilichokuwa kimetokea, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali mno, alikuwa tayari kwa kila kitu, kumfuata msichana huyo na hata kama lingekuwa suala la kumpigia magoti, kwake angekubaliana nalo.

    Baada ya saa kadhaa akafika nchini Tanzania na ndege ikaanza kutua katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere, akateremka na kisha kuchukua taksi na kurudi nyumbani.

    Mawazo hayakuisha, kila wakati aliendelea kumfikiria msichana Evadia, alijua fika kwamba alimuacha katika kipindi muhimu sana, ila katika kipindi hicho, alihitaji msamaha.

    “Nitahitaji anisamehe, dunia imenifunza, na mapenzi ya kukurupuka yamenifunza pia,” alisema Dickson wakati gari likiingia katika Barabara ya Kawawa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alipofika nyumbani, hakuwakuta wazazi wake, hivyo akaingia moja kwa moja chumbani na kujilaza. Moyo wake uliendelea kuwa kwenye maumivu makali mno, macho yake yalikuwa mekundu mno sababu ya kulia sana njiani.

    Ilipofika saa kumi na moja jioni, wazazi wake wakarudi nyumbani hapo na kumkuta. Walishangaa sana kwani ni jana yake ndiyo alikuwa ameondoka na kuelekea nchini Rwanda, sasa ilikuwaje mpaka arudi tena ikiwa ghafla mno? Kila walipojiuliza, wakakosa jibu.

    “Kuna nini?” aliuliza mama yake.

    “Mapenzi yamenishinda,” alisema Dickson huku akijaribu kuyafuta machozi yake.

    “Nini kimetokea?” aliuliza baba yake.

    Dickson hakutaka kuficha kitu chochote kile, alichokifanya ni kuwahadithia wazazi wake kile kilichotokea nchini Rwanda. Katika kipindi chote alichokuwa akisimulia, machozi yalimbubujika, alionekana kuumizwa na kile kilichokuwa kimetokea.

    “Pole sana, kwa hiyo umeamua nini?” aliuliza baba yake.

    “Kumuomba msamaha Evadia na nimrudie, tena nimuoe kabisa,” alisema Dickson.

    “Umrudie Evadia?”

    “Ndiyo! Haina jinsi baba. Kama kuumia nimeshaumia sana, sina jinsi, ni lazima nimrudie Evadia,” alijibu Dickson.

    “Atakubali kweli?”

    “Sijui! Ila ni lazima nimrudie.”

    Wote wawili walichanganyikiwa, maneno waliyoambiwa na Matilda yaliwachanganya mno, wakabaki wakiwa wamempigia magoti kana kwamba yeye ndiye alikuwa Laurence.

    Walijilaumu na kujuta kwa kile walichomfanyia mwanaume huyo ambaye kila siku walijua kwamba alikuwa kijana masikini. Evadia alilia huku mama yake akimbembeleza Matilda akawaombee msamaha lakini msichana huyo aliendelea kuwalaumu.

    Alimfahamu Laurence, alikuwa mwanaume mwenye msimamo, alipoamua kufanya jambo fulani, hakuwa akiangalia, alichokijua ni kufanya na kuendelea na mambo yake.

    Kitendo cha kukataliwa na msichana huyo kilimpa uhakika Matilda kwamba Laurence asingeweza kuwa naye, ila kwa sababu waliomba sana, hakuwa na jinsi, akawaambia wajiandae ili waweze kwenda nyumbani kwa Laurence, kwani kama wasingefanya hivyo siku hiyo, wasingeonana naye kutokana na safari ya kwenda nchini Marekani ambayo alikuwa nayo.

    “Fanyeni haraka,” aliwaambia.

    Hakukuwa na mtu aliyekwenda bafuni kuoga, kila mtu akabadilisha nguo na kuanza safari ya kuelekea Mbezi beach alipokuwa akiishi Laurence. Njiani, hawakuacha kumbembeleza Matilda awaombee msamaha kwa mwanaume huyo, yeye mwenyewe hakuwa na uhakika kama angekubali kuwasamehe kwani kama kulia kwa ajili ya mapenzi, alilia sana lakini mwisho wa siku hakuna aliyefahamu thamani ya kilio chake.

    Walichukua dakika kadhaa ndipo wakafika huko. Gari likasimama nje ya jumba moja kubwa na la kifahari, geti likajifungua na kisha Matilda kuanza kuliingiza gari.

    Hawakuamini kama jumba la namna hiyo lingekuwepo nchini Tanzania. Lilikuwa na eneo kubwa, bwa la kuogelea, mbuga ndogo ya wanyama, sehemu kubwa ya kufugia samaki huku kukiwa na sanamu kubwa ya Laurence ikiwa imesimamishwa, tena huku ikimuonyesha akiwa ameshika cheti mkononi.

    Evadia hakuamini kama jumba hilo la kifahari ndiylo alilokuwa akiishi mwanaume aliyemchukia, alishindwa kuyazuia machozi yake, yakaanza kumbubujika kwa uchungu.

    “Tumefika,” alisema Matilda na kuteremka.

    Katika sehemu ya kuegesha magari hakukuwa na gari lililokuwa chini ya shilingi milioni mia moja, yote yalikuwa juu mpaka Ferrari Spider ambalo dukani lilikuwa na gharama zaidi ya milioni mia tano.

    Evadia akahisi kuchanganyikiwa, alitamani kurudisha muda nyuma ili aweze kurekebisha mambo yake, awe na Laurence ili kila kitu alichokiona kiwe chake lakini hakuwa na uwezo huo tena, muda haukurudi nyuma.

    Kwa kuwa Matilda alikuwa mwenyeji, wakaanza kuelekea ulipokuwa mlango wa kuingilia sebuleni na kuingia ndani. Kila mmoja alikodoa macho, jumba lile lilikuwa na vitu vya thamani mno, kwa muonekano wake halikustahili kabisa kujengwa nchini Tanzania.

    “Hapa ndipo anapoishi Laurence?” aliuliza mama Evadia.

    “Ndiyo hapa. Subiri, atakuja tu,” alijibu Matilda.

    Mfanyakazi mmoja aliyevalia nadhifu akafika sebuleni hapo na kuwakaribisha kwa kuwaletea vinywaji. Hakukuwa na mtu aliyehisi radha yoyote ile kwani hali waliyokuwa nayo katika kipindi hicho ilikuwa tofauti kabisa.

    Hawakukaa muda mrefu, Laurence akatokea sebuleni hapo. Siku hiyo ndiyo walimuona jinsi alivyokuwa, mwanaume msafi aliyevalia mavazi mazuri na ya thamani, hata Evadia mwenyewe alivyomuona, alijuta moyoni kumpoteza mwanaume kama huyo.

    Hapohapo, kabla hawajazungumza naye neno lolote lile, wakampigia magoti na kuanza kumuomba msamaha.



    Laurence alibaki akiwaangalia, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, kila alipomwangalia Evadia na mama yake, alikumbuka saa chache zilizopita kwamba alitimuliwa kama mbwa na kuambiwa asirudi tena nyumbani kwao.

    Moyo wake uliumia sana kwa kuwa alikuwa na mapenzi ya dhati kwa msichana huyo. Alimwangalia sebuleni hapo, jinsi alivyopiga magoti na mama yake na kuanza kuomba msamaha, moyo wake ulimchukia, mapenzi yote aliyokuwa nayo kabla, yalipotea kabisa.

    “Naomba unisamehe Laurence,” alisema Evadia huku akilia kama mtoto.

    “Nikusamehe?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ndiyo! Naomba unisamehe kwa upumbavu nilioufanya,” alisema msichana huyo.

    “Upumbavu gani tena?”

    “Kukukataa na wakati ulikuwa ukinipenda kwa penzi la dhati,” alisema msichana huyo.

    “Evadia, kunikataa mimi si upumbavu, ni haki yako, kila mtu ana haki ya kumpenda mtu fulani na kumchukia mtu fulani, ulichokifanya si upumbavu bali ni uamuzi,” alisema Laurence kwa sauti ya upole kabisa.

    “Naomba utusamehe Laurence,” alisema mama Evadia.

    “Mama! Hakuna kosa mliolifanya.”

    “Tulikufukuza nyumbani.”

    “Pia hilo si kosa, ni uamuzi tu, unaweza kumkaribisha mtu fulani na kumfukuza mtu fulani, huwezi kufungwa kisa umemfukuza mtu fulani,” alisema Laurence huku akiwaangalia usoni.

    “Laurence, tunaomba utusamehe,”

    “Evadia, hamkunifanyia ubaya wowote, hakuna kosa mlilonifanyia, sasa niwasamehe kwa lipi? Kama kungekuwa na kitu kibaya mmenifanyia, sawa, ila hakuna lolote baya,” alisema Laurence huku akiwaangalia wa zamu.

    Walilia na kujuta, walitamani masaa yarudi tena ili wasifanye makosa tena lakini hilo halikuwezekana. Laurence aliumia kumuona msichana aliyekuwa akimpenda akipiga magoti mbele yake na kuomboleza lakini hakuwa na cha kufanya, alimpa nafasi ambayo aliichezea na kuona si kitu chochote katika maisha yake.

    Hakutaka kukaa sana nyumbani hapo, alichokifanya ni kuaga, siku hiyo hakutaka kulala nyumbani, alitaka kwenda kulala hotelini kwani kichwa chake hakikuwa sawa kwa wakati huo.

    “Matilda,” aliita.

    “Abee bosi.”

    “Utawasaidia kiasi fulani cha fedha. Nafikiri msaada wangu umeishia hapa,” alisema Laurence, hakutaka kuendelea kubaki hapo, alichokifanya ni kuondoka huku akiacha vilio vikali nyuma yake.

    Dickson na wazazi wake wakafika katika nyumba aliyokuwa akiishi Evadia na mama yake, walifika hapo kwa lengo moja la kumuomba msamaha ili waweze kuishi pamoja kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

    Hakujua kama angekubaliwa au kukataliwa, alifika hapo kwa ajili ya kuomba msamaha tu. Moyoni mwake alijisikia kuwa na huzuni tele, alihisi kwamba mapenzi yake kwa Evadia yalirudi kama zamani.

    Baada ya kufika karibu na eneo la nyumba ile, walichokishangaa ni kwamba nyumba hiyo haikuwepo bali kulikuwa na nyumba nyingine, tena iliyoonekana kuwa ya kifahari ikiwa kwenye ujenzi.

    Walishangaa, hawakuamini kile walichokiona, maswali mengi yakaanza kumiminika vichwani mwao kwamba watu waliokuwa wakiishi humo walikwenda wapi? Walikuwa masikini wa kutupwa, je nyumba ile walikuwa wameiuza kwa tajiri mmoja, kila walipojiuliza, walikosa jibu.

    Alichokifanya Dickson ni kusogea katika nyumba ile kwa lengo la kuwauliza mafundi juu ya wale waliokuwa wakiishi katika nyumba ile, walitaka kufahamu mahali walipokuwa.

    “Mbona walihama kitambo,” alisema fundi mmoja.

    “Walihamia wapi?”

    “Nasikia Mabibo.”

    “Kwani hii nyumba mnayoijenga ni ya nani?”

    “Ya hao waliohama hapa.”

    “Mmmh!”

    “Ndiyo! Mbona maswali mengi mwana, wewe polisi nini?” aliuliza fundi huyo, alionekana kuwa bize na hakutaka kusumbuliwa zaidi.

    “Hapana! Ila asante.”

    Alichokifanya Dickson ni kwenda kwa majirani waliokuwa karibu na nyumba hiyo kwa lengo la kuuliza juu ya mahali alipohamia Evadia na mama yake. Alipowauliza majirani hao, walimwambia kwamba walihamia Mabibo kipindi cha miezi miwili iliyopita.

    “Walipata wapi hela?”

    “Mmh! Hata sisi hatujui.”

    “Ila walipohamia mnapajua?”

    “Sana tu.”

    “Naomba mtupeleke.”

    “Hakuna tatizo. Ngoja niwaitieni kijana wangu awapeleke.”



    Aliyesimama mbele yake hakuwa mwingine bali Dickson, mwanaume ambaye kipindi cha nyuma alimwambia kwamba angemuoa lakini mwisho wa siku akamkataa kwa kuwa tu alimpata mwanamke mwingine ambaye alidai kwamba alikuwa akimpenda kwa mapenzi ya dhati.

    Kumuona Dickson mahali hapo kulimkumbusha mambo mengi, alizikumbuka vilivyo siku alizokuwa akijifungia chumbani na kulia kisa tu mapenzi, hakuwa na hamu naye lakini kwa sababu sehemu ya moyo wake ilikuwa kwa mwanaume huyo, hakuwa na jinsi, aliamua kumsamehe.

    “Nashukuru sana Evadia, naomba unipende kwa penzi ulilokuwa nalo kabla, naomba unipende namna hiyo, nakuahidi kwamba sitokuumiza tena,” alisema Dickson huku akilia kama mtoto.

    Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa safari yao nyingine ya mapenzi, pamoja na kuwa na mwanaume Dickson lakini haikuwa sababu ya kuisahau bahati ambayo aliichezea ya kutokumpenda Laurence kwa kuwa tu alikuwa masikini.

    Kitu hicho kilimuumiza sana, japokuwa Laurence alimwambia kwamba halikuwa kosa lakini kila siku alikuwa akilia na alikosa amani kabisa.

    “Ninataka nikuoe mpenzi, sina muda wa kupoteza,” alisema Dickson.

    “Kweli?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ndiyo! Sitaki kukupoteza tena,” alisema mwanaume huyo.

    “Sawa. Hakuna tatizo, ninafurahi kusikia hivyo,” alisema Evadia huku akiachia tabasamu pana, alichokihitaji kwa wakati huo ni kufunga ndoa na Dickson kwa kuamini kwamba angesahau kila kitu kilichotokea kati yake na Dickson.

    “Niambie vizuri bosi,” ilisikika sauti ya Matilda kwenye simu.

    “Nikwambie nini?”

    “Kwa hiyo unaishi na figo moja?”

    “Kwa nini?”

    “Si moja uliitoa kwa Evadia!”

    “Hahaha!”

    “Mbona unacheka sasa?”

    “Kiukweli sikutoa figo.”

    “Mmmh!”

    “Iliwezekana vipi na wakati kila mtu aliona kwamba ulitoa figo?” aliuliza Matilda.

    “Kawaida tu, ila amini kwamba sikutoa figo kwa kuwa nahisi hata yangu haikuwa na vinasaba vinavyoendana na vyake,” alisema Laurence.

    “Hebu niambie nini kilitokea,” alisema Matilda.

    “Nilitoa kiasi cha fedha kwa ajili ya Evadia kupatiwa matibabu lakini kitu cha kushangaza, hakukuwa na mtu aliyefika ambaye alikuwa na vinasaba vilivyofanana na vyake.

    “Nilichoamua ni kupotea, sikumwambia mtu yeyote, nilichukua ripoti ya majibu ya Evadia na kuondoka nayo kuelekea nchini Nigeria. Kule, niliwapa watu wa matangazo watangaze kama kulikuwa na mtu anayetaka kutoa figo yake kwa malipo makubwa, huwezi kuamini, walikuja wengi, na mwisho wa siku tukampata mtu ambaye vinasaba vyake viliendana na Evadia, nikaamua kumchukua na kumleta Tanzania huku nikiwa nimemlipa zaidi ya milioni hamsini,” alisema Laurence.

    “Mmmh!”

    “Ndiyo hivyo! Kilichofuata ni kufanya mchezo na madaktari mpaka kukamilisha kazi, ila kiukweli, sikutoa figo,” alimalizia Laurence na Matilda kushusha pumzi nzito.

    Kipindi hicho Laurence alikuwa nchini Marekani, kila siku ilikuwa ni lazima kuwasiliana na Matilda na kumwambia afuatilie kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika kampuni zake, alimwamini kwa kuwa kwa kipindi cha miaka mitano aliyofanya naye kazi, msichana huyo alimuonyeshea uaminifu mkubwa.

    Baada ya kukaa nchini Marekani kwa kipindi cha mwezi mzima ndipo akarudi nchini Tanzania. Haikuwa rahisi kumgundua Laurence, alijifanya mtu wa kawaida mno, alipanda ndege za kawaida na abiria wengine, alitaka kuishi huru, hakutaka kuzungukwa na watu au kuchukuliwa mtu wa tofauti.

    Hayo ndiyo maisha aliyoyazoea. Ndege ilipotua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Laurence akateremka na kuanza kutoka nje ya ndege hiyo kisha kuelekea katika jumba la uwanja huo ambapo baada ya kuchukua mizgo yake, akatoka nje.

    “Karibu sana bosi,” alisema Matilda ambaye alifika uwanjani hapo kumpokea.

    “Asante sana.”

    Wakaingia ndani ya gari na safari ya kuelekea nyumbani kuanza. Njiani, walikuwa wakizungumza mengi, kila mmoja alionekana kuwa mwenye furaha mno, hakukuwa na mtu aliyemkumbuka Evadia, kila kitu kilichopita waliamua kuachana nacho.

    “Nataka nikutoe mtoko wa usiku,” alisema Laurece.

    “Mimi?”

    “Kwani nazungumza na nani humu garini?”

    “Hahaha!”

    “Au kuna shemeji naye ana ratiba ya kutoka nawe?”

    “Shemeji? Kwa mapenzi haya ya kina Evadia?”

    “Ndiyo! Labda kuna mtu nyuma,” alisema Laurence.

    “Hakuna mtu bosi.”

    “Kwa hiyo itawezekana?”

    “Itawezekana, wala usijali.”

    Usiku Matilda alionekana kuwa na mawazo, moyo wake uliwaza mambo mengi ila kubwa zaidi ni kuhusu hicho alichotaka kuzungumza Laurence.

    Hakukuwa na alichojifikiria zaidi ya mapenzi, hakuamini masikio yake kwamba bosi wake ambaye kila siku alimfanyia kazi kwa kujitolea leo hii alitaka kuzungumza naye, tena katika sehemu ambayo wangekuwa wawili tu.

    Mara baada ya kujiandaa, Matilda akatoka chumbani kwake na kwenda katika sehemu ya maegesho ya magari na kuchukua gari lake kisha kuanza safari ya kuelekea huko alipopanga kuonana na Laurence kwani tayari muda ulitimia.

    Njiani, mawazo hayakumtoka, alijua fika kwamba kile ambacho kingekwenda kutokea huko kilikuwa ni mapenzi tu. Kama ingekuwa hivyo, kwake ilikuwa ni bahati kubwa, kuwa na mwanaume kama Laurence, mwanaume mwenye sura nzuri na fedha nyingi, kwake ilitosha kumkubalia.

    Mbali na hivyo, moyo wake kwa kipindi kirefu ulikuwa kwenye mapenzi juu ya mwanaume huyo ila kitu ambacho hakutaka kukiweka wazi ni juu ya jinsi alivyompenda.

    Kitendo cha Laurence kumng’ang’ania Evadia kipindi cha nyuma ilimuuma sana lakini hakuwa na jinsi, alikubali kuumia kwani hakutaka kumwambia ukweli bosi huyo kwa kisingizio cha kuogopa ila mwisho wa siku, leo hii aliambiwa kwamba walitakiwa kuonana sehemu wawili na kuzungumza.

    “Karibu sana mrembo,” alisema Laurence, alikuwa akimkaribisha Matilda mara baada ya kuwasili, hakuamini kama yeye ndiye aliyeitwa mrembo na Laurence.

    “Asante sana.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Laurence akabaki akimwangalia Matilda, siku hiyo, msichana huyo alipendeza mno, kila alipomwangalia, hakuisha hamu. Kichwa chake kikaanza kujifikiria juu ya msichana huyo kama ilikuwa sahihi kuwa naye au la, jibu pekee lililokuja kichwani mwake ni kwamba alistahili kuwa mke wake.

    Hakujua mapokeo ya maneno yake yangekuwa vipi, hakujua kama angekubaliwa na msichana huyo au angekataliwa. Hakutaka kuangalia fedha zake, hakutaka kuzipa nafasi, kwake, aliamini kwamba msichana angeweza kumkataa hata kama alikuwa na fedha.

    Kabla ya kuanza mazungumzo akamuita mhudumu na kuagiza vinywaji. Hakuwa mnywaji wa pombe, hivyo akaagiza juisi ambapo baada ya dakika chache mhudumu huyo akawaletea.

    “Matilda, kuna haja ya kuanza kukudanganyadanganya?” aliuliza Laurence huku akichia tabasamu pana.

    “Kunidanganyadanganya?”

    “Kuna haja hiyo?”

    “Kivipi?”

    “Najua unajua nimekuitia nini mahali hapa, sidhani kama nitatakiwa kuzungumza sana mpaka kutoka nje ya kile nilichopanga kukwambia usiku wa leo,” alisema Laurence, alionekana kutokuwa na wasiwasi kabisa. Kila alipoongea, alishushia na juisi.

    “Sijajua umeniitia nini?”

    “Matilda. Nimejikuta nikiwa kwenye hali ambayo sikuitarajia kabla, sikupanga kukwambia hili katika maisha yangu lakini nimejikuta sina jinsi ni lazima nikwambie ili niwe na amani,” alisema Laurence kwa sauti ya chini yenye kumaanisha alichokuwa akikisema.

    “Unataka kuniambia nini?”

    “Jinsi ninavyokupenda na jinsi ninavyotaka wewe uwe mke wangu wa ndoa,” alisema Laurence.

    “Niwe mke wako wa ndoa?” aliuliza Matilda huku akijifanya kushtuka.

    “Ndiyo!” alijibu Laurence kwa kujiamini.

    “Mimi?”

    “Ndiyo! Wewe!”

    “Hapana! Haiwezekani,” alisema Matilda.

    “Kwa nini?”

    “Sitaki tu.”

    “Kweli?”

    “Ndiyo! Sijisikii kuwa na mwanaume, na sidhani kama nitataka kuolewa, siwezi kuwa nawe bosi,” alisema Matilda, kwa kumwangalia usoni alionekana kumaanisha lakini ukweli kutoka moyoni mwake, alitingisha kiberiti.

    Kazi kubwa ikawa kwa Laurence, hakuamini kile alichokisikia kwamba msichana huyo aliyekuwa akimpenda hakuwa akitaka kuwa naye. Moyo wake ukaanza kupatwa na maumivu kama yale aliyoyapata kipindi alichokataliwa na Evadia.

    Alijiona akiwa na mkosi mkubwa. Alijaribu kumwangalia Matilda kwa macho ya kuonewa huruma lakini msimamo wa msichana yule ulikuwa huohuo kwamba hakutaka kuwa na Laurence, yaani hakutaka kuwa mkewe.

    Fedha hazikusaidia, Matilda alionekana kuwa msichana mwenye msimamo mkubwa, alijua fika kwamba mwanaume aliyekuwa mbele yake alikuwa na fedha lakini hiyo haikuwa sababu ya kujirahisisha namna hiyo.

    Alichokifanya ili kumuonyesha Laurence kwamba hakufurahishwa na kile alichoambiwa, hapohapo akasimama na kuanza kuondoka bila kuaga. Laurence hakukubali, alitokea kumpenda Matilda, alichokifanya ni kusimama na kuanza kumfuata, alipomkaribia akamshika mkono na kumwangalia usoni.

    “Matilda, pleaseee…nakupenda,” alisema Laurence huku akimwangalia msichana huyo usoni.

    “Laurence, naomba uniachie…”

    “Tatizo nini Matilda?”

    “Sikupendi!”

    “Umesema?”

    “Sikupendi…sikupendi….” alisema Matilda, hapohapo akaendelea na safari yake mpaka garini.

    Laurence alichanganyikiwa, hakuamini kile alichoambiwa, akamfuata Matilda mpaka lilipokuwa gari lake na kusimama mbele, hakutaka Matilda aondoke, pale mbele, akapiga magoti na kumuomba msichana huyo ateremke na kuzungumza naye lakini Matilda hakuteremka zaidi ya kupiga honi akitaka apishwe ili aondoke. Watu waliokuwa pembeni wakabaki wakiwaangalia tu.





    Laurence alikuwa tayari kwa kila kitu, kama kugongwa na gari hilo, alikuwa tayari lakini si kutaka kumuona Matilda akiondoka mahali hapo. Watu wengine waliokuwa katika mgahawa ule wakatoka nje na kumwangalia vizuri Laurence, -hawakumfahamu, wao walimuona mwanaume fulani ambaye alipiga magoti mbele ya gari ambalo ndani yake alikuwepo mwanamke kisha kumuomba kuteremka kutoka garini.

    Matilda hakuacha kupiga honi, aliendelea kumsisitizia Laurence atoke mahali pale ili aondoke lakini mwanaume huyo hakuweza kuondoka pale alipokuwa amepiga magoti.

    “Kuna nini dada?” aliuliza mwanaume mmoja, hakuwa akijua kinachoendelea.

    “Nataka huyo mwanaume aondoke hapo mbele,” alijibu Matilda.

    “Nani? Huyu?”

    “Ndiyo!”

    “Una mawe?”

    “Shilingi ngapi?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hata buku tano, naweza kumtoa peke yangu,” alisema jamaa huyo, hapohapo Matilda akachukua pochi yake na kutoa noti ya shilingi elfu kumi na kumkabidhi huku akitaka abaki na chenji.

    Jamaa huyo, ili kuonekana kwamba alikuwa na nguvu, akaelekea mbele ya gari na kusimama mbele ya Laurence, hakuwa akijua kwamba huyo ndiye alikuwa yule bilionea mkubwa nchini Tanzania, alichokifanya ni kumnyanyua mzobemzobe kumpeleka pembeni kabisa.

    “Tulia hapa wewe…” alisema jamaa yule, Matilda akawasha gari na kuondoka mahali hapo.

    Moyo wa Laurence uliumia mno, hakuamini kile kilichotokea, kipindi cha nyuma alifikiri kazi ingekuwa nyepesi sana lakini baada ya kuianza, akagundua kwamba ilikuwa ngumu mno.

    Hakuzungumza kitu chochote kile, alichokifanya ni kuondoka kulifuata gari lake huku kila mtu akimwangalia, wengi walimuonea huruma. Alipolifikia gari lake, kila mtu akashtuka, akashangaa ni kwa jinsi gani msichana yule alimkataa mwanaume huyo aliyekuwa na gari la kifahari ambalo lilionyesha ni jinsi gani alikuwa na fedha.

    Hakuliwasha gari hilo, alipandisha kioo, akaegemea usukani kisha kuanza kufikiria kwa kina, machozi yalimtoka, yaani kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo, wakati mwingine alihisi kwamba alikuwa ndotoni.

    “Matilda, why are you doing this to me?” (Matilda, kwa nini unanifanyia hivi?) aliuliza.

    “I want nobody than you,” (Simhitaji yeyote zaidi yako) alisema Laurence na kisha kuondoka mahali hapo.

    Njia nzima alikuwa mtu wa kulia tu, bado hakuamini kilichokuwa kikiendelea, aliendesha gari kwa umakini mkubwa kwani pasipo kufanya hivyo angeweza kupata ajali kutokana na kichwa chake kuwa na mawazo lukuki.

    Hakuchukua muda mrefu akafika nyumbani kwake, akateremka na kisha kuingia ndani. Safari yake ikaishia kitandani, alijilaza, usingizi haukumjia, alibaki macho huku akiendelea kuwa kwenye mawazo lukuki.

    Kwa kipindi kifupi, penzi la Matilda likaanza kumburuza, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea moyoni mwake, Matilda yuleyule, msichana aliyekuwa akimchukulia kawaida, leo hii ndiye huyohuyo ambaye alimfanya kuteseka moyoni mwake.

    Aliendelea kuwa macho mpaka ilipofika majira ya saa saba usiku, hakutaka kukubali, alichokifanya ni kumpigia simu msichana huyo, simu ikaanza kuita, iliita na kuita lakini haikupokelewa.

    Moyoni aliumia ila hakuwa na jinsi, aliendelea kupiga zaidi, matokeo yalikuwa yaleyale kwamba simu haikupokelewa. Moyo wake ukachoka, alichokifanya ni kujaribu kwa mara ya mwisho, hakutaka kujiuliza, akapiga tena, majibu yakawa tofauti na mwanzo, mara hii, simu haikupatikana kabisa, ilikuwa imezimwa. Maumivu aliyoyasikia moyoni hayakuelezeka.

    Hakutaka kujirahisisha, alichokuwa akitaka kumuonyeshea Laurence kipindi hicho ni kwa jinsi gani alikuwa msichana asiyebabaikia fedha, alimpenda sana mwanaume huyo lakini hiyo haikuwa sababu ya kumkubali kwa haraka sana.

    Alipoondoka kwenye ule mgahawa, alijifanya kuchukia lakini ukweli wa moyo wake ulikuwa na faraja tele, hakuamini kilichokuwa kikiendelea kwamba bilionea yule aliyekuwa akifanya kazi kwake, leo hii alikuwa akimpenda kwa moyo wa dhati.

    Alipofika nyumbani, Matilda akaelekea chumbani kwake na kukifuata kioo alichokibandika ukutani na kuanza kujitazama. Alijitazama kuanzia chini mpaka juu kisha akarudia kujitazama tena, alitaka kuona kama alibadilika na kuwa mzuri zaidi ya kipindi kilichopita, alipojiangalia na kujichunguza, akagundua kwamba alikuwa vilevile.

    “Sasa kanipendea nini?” alijiuliza.

    “Au hakuwa anamaanisha alichoniambia? Mmmh! Kweli Laurence anipende mimi? Au ananitega?” alijiuliza lakini akakosa jibu.

    Akaelekea kitandani na kutulia, mawazo yake juu ya Laurence hayakumtoka, aliendelea kumfikiria mwanaume huyo. Kila kilichoendelea katika maisha yake juu ya Laurence hakuwa akimaanisha, wakati mwingine alikuwa akijiuliza kama mwanaume huyo angechukulia kila kitu kuwa kweli, asingeamua kuachana naye?

    Hilo lilimuogopesha lakini hakuwa na jinsi, alichokifanya ni kupiga moyo konde, ilikuwa ni lazima kumuonyeshea Laurence kwamba alikuwa miongoni mwa wanawake wasiompenda mtu kwa kuwa tu alikuwa na fedha.

    Baada ya kupita saa mbili, Matilda akasikia simu yake ikianza kuita, alijua fika kwamba mtu aliyekuwa akipiga muda huo alikuwa Laurence kwani hakukuwa na mazoea ya kupigiwa simu katika usiku mkali kama ilivyokuwa.

    Alichokifanya ni kuichukua na kuangalia kioo cha simu yake, jina la ‘Boss’ lilionekana vilivyo kwenye simu ile. Akaanza kujifikiria kama alitakiwa kupokea au la, alikaa huku akiiangalia simu ile ilivyokuwa ikiita, hakupokea, akaamua kuachana naye kwa kuitupa pembeni.

    Hiyo haikuwa mwisho, mpigaji ambaye alikuwa Laurence akapiga tena lakini Matilda alifanya vilevile, hakuipokea simu ile. Simu ilipokata kwa mara ya pili, alichokifanya ni kuizima kabisa kisha kujilaza huku akiwa na mawazo tele juu ya mwanaume huyo. Alichojua ni kwamba ilikuwa ni lazima Laurence amtafute siku inayofuata.

    Dickson alimaanisha aliposema kwamba alihitaji ndoa tu kwa msichana Evadia. Hakutaka kumuona msichana huyo akiondoka mikononi mwake kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

    Alimrudia na kumuomba msamaha, kweli alisamehewa na hivyo mapenzi kurudi kama zamani. Muda mwingi msichana huyo alionekana kuwa na mawazo, hakuwa na furaha kama kipindi cha nyuma kitu kilichomfanya Dickson kuhisi kwamba bado Evadia alikuwa na wasiwasi naye.

    Huo haukuwa ukweli wenyewe, msichana huyo alikuwa na mawazo tele kwa kuwa tu bado alimfikiria Laurence na utajiri mkubwa aliokuwa nao ambao aliamini kwamba endapo angekuwa wake, basi ule utajiri wote naye angekuwa anahusika nao.

    Moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali lakini hicho hakikuwa kipindi cha kujuta tena, kama ni bahati aliichezea hivyo kuendelea mbele na maisha yake kama kawaida.

    Siku zikakatika, wazazi wa pande zote mbili wakakubaliana kwamba harusi ifanyike baada ya mwezi mmoja, maandalizi yakaanza kufanyika huku ndugu, jamaa na marafiki wakiambiwa wajiandae kusherehekea harusi hiyo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ukaribu wao ukaongezeka zaidi, mapenzi yao yakapamba moto zaidi. Maandalizi kabambe yaliendelea na michango kuanza kukusanywa kutoka kwa watu mbalimbali.

    “Nitamshukuru Mungu utakapoolewa binti yangu, ni faraja kwa mzazi kuona harusi ya mtoto wake,” alisema mama Evadia, alikuwa akimwambia binti yake.

    “Ninamshukuru Mungu kwa kila kitu.”

    “Ila mbona unaonekana hauna furaha, tatizo nini?” aliuliza mama Evadia.

    “Laurence mama!”

    “Binti yangu, kilichotokea achana nacho na usonge mbele na mambo mengine, kama ni bahati, si wewe tu bali hata mimi niliichezea, Mungu anapoamua kufunga mlango mmoja, jua kuna mwingine unafunguka. Huwezi jua, inawezekana Mungu hajataka uolewe na Laurence kwa kuwa kuna siku ungepanda ndege kwenda Marekani, ndege ingepata ajali na kufariki,” alisema mama Evadia.

    “Inawezekana mama?”

    “Ndiyo binti yangu! Mshukuru Mungu kwa kila kitu.”

    Walifarijiana usiku kucha, mioyo yao iliumia sana, kila waliposoma kwenye magazeti juu ya utajiri aliokuwa nao Laurence maumivu yakaongezeka mioyoni mwao.

    Baada ya siku tatu, Evadia akapokea bahasha iliyokuwa na karatasi ndani. Ililetwa na mwanaume mmoja aliyevalia nadhifu sana, alipofika nyumbani hapo akaomba kuonana na msichana huyo, akatoka nje.

    “Karibu,” alimkaribisha.

    “Asante sana. Mimi si mkaaji, nimekuletea mzigo wako huu,” alisema mwanaume huyo huku akimkabidhi bahasha ile.

    “Kutoka wapi?”

    “Imeandikwa hapo juu,” alijibu. Evadia alipoisoma, alikuta imeandikwa jina la Laurence.

    Moyo wake ukapiga paaa. Akataka kuifungua lakini yule mwanaume alimwambia kwamba alitakiwa kusaini karatasi maalum ili aondoke zake, Evadia akapewa karatasi ambayo alisaini na kisha kuingia ndani.

    Moyo wake ulikuwa kwenye presha kubwa, alitaka kuona mule ndani kulikuwa na kitu gani, wakati mwingine alifikiri kwamba ilikuwa barua ambayo ilimtaka kuweka mambo sawa ili warudiane na kuwa kama zamani.

    Breki ya kwanza ikawa chumbani kwake, alikuwa kwenye presha kubwa, akaifungua, alichokutana nacho humo ni cheki ya shilingi milioni hamsini iliyosainiwa huku ikiwa imeambatanishwa na maneno machache yaliyosomeka ‘Uwe na harusi njema, huo ni mchango wetu, mimi na mchumba wangu, Matilda. Tutakuwa nanyi bega kwa bega kwa kila kitu’

    Evadia akashindwa kuvumilia, machozi yakaanza kumbubujika machoni mwake, hakuamini kile alichokisoma, mwanaume yule aliyekuwa amemfanyia mambo mabaya, leo hii alitoa mchango wa kiasi kikubwa kwenye harusi yake.

    Hakuamini, pamoja na mchango huo, kitu kilichomshtua ni kwamba Laurence na Matilda walikuwa wachumba, yaani msichana yuleyule ambaye kila siku alitumiwa na Laurence ndiye hatimaye alibahatika kuwa mchumba wa Laurence.

    Moyo wake ukawaka moto mkali wa wivu, aliumia kupita kawaida. Akajilaza kitandani, majuto moyoni mwake kamwe hayakupungua, yaliendelea kuwa vilevile mpaka mama yake aliporudi na kumuhadithia kilichokuwa kimetokea.





    Asubuhi ilipofika, mtu wa kwanza kabisa kupiga simu yake alikuwa Laurence, kama kawaida yake akaipuuzia simu ile, iliita mpaka pale ilipokata. Moyo wake ulimuuma na kujuta alichokuwa akikifanya lakini hakuwa na jinsi, alitaka kuonyesha msimamo wake kwa Laurence kwamba hakuwa mtu wa kubabaikia fedha.

    Muda ulizidi kwenda mbele, kwa sababu ilikuwa ni katikati ya wiki, akainuka na kwenda bafuni kuoga kisha kujiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini. Kwa kumwangalia tu Evadia alionyesha kutokuwa na furaha kabisa, alionekana kuwa na mawazo tele mpaka baadhi ya wafanyakazi wenzake kumshangaa.

    Ilipofika saa sita, muda ambao wafanyakazi wote katika ofisi ya Laurence walikuwemo, tena wakiwa bize ile mbaya, Laurence akaagiza wafanyakazi wabaki ofisini humo kwani kulikuwa na kitu cha muhimu alichotaka kukifanya.

    Kila mmoja akatulia, minong’ono ikaanza kusikika kila kona, kila mmoja alianza kuhoji ni kitu gani ambacho bosi wao alitaka kukifanya siku hiyo. Wengi wakahisi kwamba kungekuwa na wafanyakazi ambao wangefukuzwa kazi lakini kila walipokumbuka namna ambavyo Laurence alivyokuwa mpole na kuwajali wafanyakazi wake, wazo hilo likaondoka vichwani mwao.

    Evadia alionekana kuwa na wasiwasi zaidi, alichoamini ni kwamba Laurence alikasirika na hivyo angeweka wazi uamuzi wa kumfukuza kazi au kumpumzisha kwa sababu tu alimkataa.

    Alipofikiria hivyo, Evadia akaanza kujuta, akatamani usiku wa jana urudi nyuma ili arekebishe kila kitu, amkubalie Laurence na mambo mengine kuendelea.

    Ilipofika saa sita mchana, saa moja kabla ya kupata chakula cha mchana, watu kutoka katika kampuni ya kuandaa vyakula ya Mama G Delicious Food wakafika ofisini hapo, wakapanga meza zao na kuwafanya wafanyakazi wote kushangaa kilichokuwa kikiendelea.

    “Vipi tena?” aliuliza jamaa mmoja, kila mtu humo ofisini alikuwa nadhifu, kuchomekea na kufunga tai ilionekana kama sheria.

    “Hata mimi nashangaa….kwani leo sikukuu?”

    “Hapana!”

    “Sasa mbona msosi? Au bosi ameshinda bingo?” aliuliza jamaa huyo.

    “Mmmh! Sijui.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya dakika chache, Laurence akatokea mahali hapo. Wafanyakazi wote wakaanza kupiga makofi kwa furaha, kila wakati bosi huyo alionekana mtu mwenye furaha ila kwa siku hiyo, alionekana kuwa na furaha zaidi ya siku zote.

    “Nimefurahi sana kuwa nanyi katika kampuni hii, mmekuwa watu wa tofauti ambao kila siku mmekuwa mkinisapoti katika kila hatua na ili kuonyesha malipo yangu kwenu, nimefanya vile ambavyo ilikuwa ni lazima niwafanyie kama kuwanunulia magari na hata kuanza ujenzi wa nyumba zenu,” alisema Laurence, kila mmoja alikuwa kimya. Akaendelea:

    Utajiri wangu umeongezeka, nimefungua kampuni nyingi, nina wafanyakazi wengi ila katika kila hatua, ninarudia kusema kwamba ninawashukuru sana kwa yote mlionifanyia na leo hii kuwa Laurence huyu mnayemuona,” alisema na kuendelea.

    “Ninataka kuoa….” alisema.

    Aliposema maneno hayo tu, minong’ono ikaanza kusikika ofisini humo, kila mmoja alishtuka kwani hilo lilikuwa jambo geni ambalo wala halikuwa na tetesi zozote zile hapo kabla kitu kilichowafanya wafanyakazi kushangaa, ilikuwaje tetesi za bosi wao kutaka kuoa zisijulikane kabla, maswali yakawajaa.

    Kwa Matilda, alionekana kuwa na presha kubwa, hakuamini kile alichokisikia kwamba Laurence alitaka kuoa. Alichohisi ni kwamba baada ya kumkatalia, mwanaume huyo aliamua kutafuta mwanamke mwingine kwa ajili ya kumuoa na kuachana naye, hivyo akajuta zaidi.

    “Ninayetaka kumuoa ni mmoja wa watu miongoni mwenu,” alisema Laurence, kilichofuata si minong’ono bali wanaume kuanza kuuliza alikuwa nani.

    “Au Magreth….Au Frida…..Au Amanda….” kila mmoja alisikika akilisema lake.

    Alichokifanya Laurence ni kurudi ofisini kwake, huku nyuma aliacha minong’ono mingi, aliporudi tena, mkononi alikuwa na maua kadhaa, alipiga hatua taratibu na kusogea kule alipokuwa Matilda, hakutaka kuzungumza lolote, watu wote ofisini walikuwa kimya wakimwangalia tu. Laurence alipomkaribia, akapiga magoti mbele ya Matilda na kuwafanya watu wote kushtuka.

    “Matilda, wewe ni msichana wa tofauti sana kwangu, nilijaribu kukwambia ukweli kwamba ninakupenda lakini haukunielewa. Leo, nipo tayari kusema hivyo mbele ya watu wengi, ili wawe mashahidi wa kile ninachokizungumza, wawe mashahidi wazuri wa moyo wangu, ninakupenda. Will you marry me?” alisema Laurence huku akimwangalia Matilda usoni, maua yaliwekwa chini, mkononi alikuwa na pete.

    Matilda akaanza kububujikwa na machozi, hakuamini alichokuwa akikiona.

    “Will you?” aliuliza.

    Watu wote wakataka kusikia jibu kutoka kwa Matilda, wote wakabaki kimya wakimwangalia msichana huyo aliyekuwa akibubujikwa na machozi. Hakujibu kitu zaidi ya kumsogelea Laurence, akamuinua na kumkumbatia, watu wote wakapiga makofi na vigelegele vya shangwe, hatimaye msichana Matilda akakubali kuolewa na Laurence.

    “Nitakupenda milele,” alisema Laurence.

    “Nitakupenda pia,” alisema Matilda, kilichofuata ni kumwagiana mabusu mfululizo.

    Watu walikusanyika ndani ya Kanisa la Ukombozi lililokuwa Mbezi jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushuhudia harusi kati ya kijana Dickson na Evadia ambao walitarajiwa kufunga ndoa dakika chache zijazo.

    Kila mtu aliyekuwa kanisa humo alikuwa na furaha mno, watu hao ambao walikuwa pamoja kwa kipindi kirefu, leo hii walikuwa wamefikia hatua ya kufunga ndoa na kuishi pamoja kama mke na mume.

    Miongoni mwa wahudhuriaji katika harusi hiyo alikuwepo Laurence na mchumba wake, Matilda. Muda wote nyuso zao zilikuwa na furaha tele, walimpenda Evadia, walikumbuka maisha aliyopitia na mama yake, yalikuwa na umasikini mkubwa na ndiyo maana waliamua kwa moyo mmoja kumsaidia yeyey na mama yake.

    Mara baada ya maharusi kuingia kanisani, hatimaye Dickson na Evadia wakawa mume na mke huku kukifuatiwa na sherehe kubwa usiku katika Ukumbi wa Hoteli ya Traveltine iliyokuwa Magomeni jijini Dar.

    “Hongereni sana,” alisema Matilda huku akimpa mkono Evadia na mumewe, Dickson.

    “Asanteni pia, asanteni kwa kuwa pamoja nasi,” alisema Evadia huku akiwakumbatia Laurence na mchumba wake.

    Hiyo ilikuwa harusi ya kwanza, baada ya miezi miwili, hatimaye Laurence na Matilda wakafunga ndoa katika Kanisa la Roman Catholic lililopo Mwenge jijini Dar.

    Watu wengi walihudhuria harusi hiyo, mabilionea wakubwa, waandishi wa habari, makamu rais na wengine wengi. Baada ya harusi hiyo kufungwa, sherehe kubwa ikafanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena na baada ya hapo fungate kwenda kufanyika nchini Marekani katika Visiwa vya Hawaii.

    “Hatimaye nimekuoa,” alisema Laurence.

    “Siamini kama miaka yote hiyo nilikuwa nafanya kazi kwa mume wangu!” alisema Matilda huku akimwangalia mume wake usoni.

    “Kumbe na mimi niliajiri mwanamke ambaye baadaye angekuja na kuwa mke wangu! Ni bahati iliytoje!” alisema Laurence.

    Walikaa nchini Marekani kwa muda wa mwezi mzima huku mchakato kamili wa kutafuta mtoto ukianzia nchini humo. Maisha yalibadilika, kila mtu akaonekana kuwa na furaha, hakukuwa na ugomvi, waliishi kwa amani, magazeti na vyombo mbalimbali vya habari vilimtangaza sana Laurence hasa mara baada ya kufanikiwa kuwa Bilionea Kijana ndani ya mwaka mmoja.

    Huo ukawa na muendelezo wa mafanikio yake. Katika kila hatua aliyokuwa akipiga, mkewe alikuwa pamoja naye.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    **MWISHO WA HADITHI**



    Toa Maoni yako Kuhusu Hadithi hii.



THE LOVE YOU HAD BEFORE (PENZI ULILOKUWA NALO KABLA) - 4

 







    Simulizi : The Love You Had Before (Penzi Ulilokuwa Nalo Kabla)

    Sehemu Ya Nne (4)



    Maisha yakaanza upya, kutokana na maagizo aliyoyatoa Laurence, Matilda hakutakiwa kuishia hapo, alichoambiwa ni kwamba aendelee kumhudumia msichana huyo mpaka pale ambapo angekuwa mzima kabisa.

    Kiasi cha fedha walichokuwa nacho ndicho kilichomfanya mama Evadia kuanza kufanya biashara ambazo kwa kiasi fulani ziliwafanya kuwa katika maisha nafuu. Maisha yao yakaanza kuona dira, mama Evadia hakutaka kuishia hapo, alichokifanya ni kupamba zaidi, majirani wakashangaa, mabadiliko ya maisha yao yalikwenda kwa kasi mno.

    Siku zikakatika, Evadia akapata nafuu na kuanza kutembea, hakujisikia kizunguzungu kama kipindi cha nyuma, kwa kifupi, afya yake ilirudi katika hali ya kawaida.

    Katika kipindi chote alichokuwa akiendelea kupata matibabu nyumbani huku maisha yao yakiendelea kuimarika kutokana na fedha walizosaidiwa, Laurence hakuweza kuonekana nyumbani hapo.

    Hilo halikumtia wasiwasi mtu yeyote yule kwani walihisi kwamba kutokana na ugonjwa aliokuwa akiumwa, aliendelea kupata matibabu nyumbani kwake. Mama Evadia alionekana kujisahau, alianza kumsahau Laurence ambaye ndiye aliyefanya maisha ya binti yake kutengemaa.

    Kitendo cha Laurence kutoonekana, hakutaka hata kumpigia simu na kumuuliza aliendeleaje, kila siku alikuwa mtu wa kuwa bize tu, alifikiria kuhusu biashara zaidi kwani maisha ya shida aliyokuwa ameyapitia yalionekana kumfundisha mambo mengi mno.

    “Niliwasiliana na Laurence, anawasalimia, hali yake si nzuri kwa sasa, anasema kidonda bado kinamuuma,” alisema Matilda, alikuwa akizungumza na Evadia aliyekuwa na mama yake.

    “Masikini weeee, mpe pole sana. Ningekwenda kumuona leo ila sina muda, kuna mzigo fulani nitakwenda kuchukua baadaye, ila nikiwahi kurudi, nitakwenda kumuona, nitakupigia simu uje kunichukua,” alisema mama Evadia maneno yaliyomfanya Matilda kushtuka.

    “Sawa mama! Unaonaje tukienda kumsalimia Evadia?” aliuliza Matilda.

    “Bado sijawa vizuri, nikipona, nakuahidi nitakwenda,” alijibu Evadia.

    Kilichowachanganya ni fedha walizokuwa wakizipata, ziliwachanganya mno, hawakuwahi kuwa na fedha kama kipindi hicho, walichokiangalia ni kuendelea kufanya biashara kwa kuamini kwamba kama wasingeweza kuzisimamia biashara hizo basi mwisho wa siku wangerudi kule walipokuwa.

    Hawakuwa wakiishi Mburahati, walihama na kuhamia katika nyumba nzuri iliyokuwa Mabibo, nyumba yenye umeme ambayo ilikuwa na kila kitu ndani yake. Kama maagizo ya Laurence yalivyokuwa, hakutaka kumuona Matilda akikata mguu kwenda huko, bado aliwatembelea na hata siku nyingine kuwapa fedha japokuwa walikuwa na fedha ambazo ziliwafanya maisha yao kuwa vizuri.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Dickson alichanganyikiwa na penzi la Luciana, hakutaka kusikia kitu chochote kile, kila wakati alikuwa na msichana huyo, alimpenda kwa moyo wa dhati, hakutaka kumuacha na kila alipomwangalia, mbele yake aliyaona maisha ya milele ambayo wangeishi kama mume na mke.

    Siku zikakatika mpaka msichana huyo alipoondoka nchini Tanzania kuelekea Rwanda, huko, kama kawaida mapenzi yaliendelea, waliwasiliana kwenye simu na hata mitandaoni, kwa Dickson hakuonekana kuwa na wasiwasi kwa msichana huyo, alimwamini kwa kila kitu na kuona kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima mwisho wa siku waishi pamoja kama mke na mume.

    “Unakumbuka nilichokwambia?” aliuliza Dickosn.

    “Kuhusu nini?”

    “Harusi!”

    “Nakumbuka, ulisema lini vile?”

    “Mwaka ujao, ninataka kuishi nawe milele, hakuna kingine,” alisema Dickson.

    “Kweli?”

    “Ndiyo!”

    “Nashukuru mpenzi, nakupenda pia, ninatamani niishi nawe milele,” alisema msichana huyo maneno yaliyomfanya Dickson kusikia furaha moyoni mwake pasipo kukumbuka kwamba tabia ni kama ngozi ya mwili ambayo huwezi kuibadili.



    Kila kitu kilibadilika, hawakutaka kusikia la mtu yeyote yule, masikini akapata, akasahau alipotoka, akasahau juu ya mtu aliyewafanya kufika mahali hapo. Hakukuwa na mtu aliyemkumbuka mwanaume aliyeonekana kuwa masikini kwao, Laurence, siku za mwisho kuonana naye zilikuwa kipindi kile kule hospitali alipoamua kubadilisha figo yake na kumpa Evadia, baada ya hapo, hakukuwa na mtu aliyemkumbuka.

    Evadia alipona, alisahau juu ya mtu aliyemfanya kuwa na afya njema, kila alipokaa, maneno yake yalikuwa ni Mungu ndiye aliyemfanya kuwa mzima wa afya na si Laurence kwani kama Mungu angeamua afe, angekufa tu hata kama angebadilishwa figo.

    Biashara zao ziliendelea vizuri, walikwenda walipotaka na fedha walizokuwa wakikabidhiwa na Matilda ziliendelea kuyabadilisha maisha yao huku biashara zao zikiendelea vizuri kwa kuwaingizia kiasi kikubwa cha fedha.

    Maneno ambayo kila siku walimwambia Matilda ni kwamba kama kwenda kumuona Laurence, wangekwenda lakini si katika kipindi hicho kwani walikuwa bize mno na biashara na msichana Evadia alihitaji mapumziko zaidi, hivyo kama kwenda kumuona Laurence ambaye ilisemekana kwamba alikuwa hoi, isingewezekana kufanyika siku hiyo, alitakiwa kusubiri mpaka siku nyingine.

    “Kwani wewe unazipata wapi taarifa za Laurence?” aliuliza mama Evadia huku akimwangalia Matilda usoni.

    “Aliwahi kunielekeza anapoishi, mbali na hilo, ana namba yangu ya simu,” alijibu Matilda kwa sauti ya upole.

    “Oooh! Kumbe! Sawa!”

    “Sasa inakuwaje?”

    “Kuhusu?”

    “Kwenda kumuona!”

    “Bado tupo bize kwa sasa, ila tutakwenda tu.”

    Huo ulikuwa mwezi wa pili lakini hakukuwa na aliyesumbuka kusimama na kwenda kumuona Laurence ambaye walisikia juujuu tu kwamba alikuwa hoi kitandani.

    Waliendelea na maisha yao kama kawaida huku mwanamke yuleyule ambaye kipindi cha nyuma alikuwa akikaa nje akisuka ukili, leo hii aliendesha gari, kwao, maisha yalikwenda kasi sana.

    Mwezi wa tatu ulipoingia, siku moja wakaanza kusikia mlango ukigongwa tena mgongaji akigonga kifujofujo sana hali iliyowafanya Evadia na mama yake kuwa na hasira kwani ugongaji ule haukuwa wa kistaarabu hata mara kidogo.

    Mama Evadia akasimama na kutoka nje, akalifuata geti. Kwa kipindi hicho, Jua lilikuwa kali mno, alipolifikia geti, akalifungua, macho yake yakatua usoni mwa Laurence.

    “Shikamoo mama,” alisalimia Laurence huku akitoa tabasamu pana.

    Kabla ya kuitikia salamu ile, akaanza kuyapeleka macho yake chini mpaka juu, mwanaume aliyesimama mbele yake ndiye aliyemsaidia binti yake kuwa na afya mpaka kipindi hicho. Hakumpenda kijana huyo, hakutamani kumuona maishani mwake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alionekana kupigwa na maisha, alichoka, mavazi yake yalikuwa mabovu, kichwani alikuwa na nywele timutimu huku miguuni akiwa na kandambili zilizochoka sana, muonekano wake tu ulitosha kuonyesha ni kwa jinsi gani alikuwa masikini.

    “Nani amekuelekeza hapa?” aliuliza mama Evadia hata kabla ya kuitikia salamu.

    “Kuna majirani zenu walinielekeza.”

    “Oooh! Sawa.”

    “Evadia yupo?”

    “Hayupo! Amesafiri.”

    “Amekwenda wapi?”

    “Moshi!”

    “Sawa mama! Nimechoka sana, naomba nipumzike ndani kwenye kivuli,” alisema Laurence huku akijionyesha kuchoka hasa.

    “Uingie ndani?”

    “Ndiyo!”

    “Utakaa na nani?”

    “Si na wewe mama.”

    “Hapana! Mimi natoka.”

    Mama Evadia alibadilika sana, fedha zikamtia jeuri hivyo hata Laurence kwake hakuonekana kuwa kitu, hakuwa na thamani hata mara moja. Hilo lilimuumiza sana Laurence, alijua fika kwamba mwanamke huyo hakuwa akitoka bali alisema hivyo kwa kuwa tu hakutaka aingie ndani.

    Moyo wake ulichoma kwa maumivu makali lakini hakuwa na jinsi, fedha zikambadilisha mwanamke huyo, alichokifanya ni kufunga geti na kurudi ndani huku akimwacha Laurence pale getini akiendelea kuchomwa na jua.

    Alipoingia ndani, akamfuata binti yake na kumwambia kuhusu Laurence, alifika mahali pale na kutaka kumuona lakini alikataa kwa kuwa hakuwa msafi, hakustahili kuingia ndani ya nyumba yao kwani angepachafua.

    “Hivi bado ananikumbuka?” aliuliza Evadia.

    “Anakukumbuka sana. Amechoka huyo, ungemuona, ungetema mate chini,” alisema mama Evadia.

    “Kweli?”

    “We acha tu. Mpaka anatisha.”

    Walikaa na kuanza kucheka, waligongesheana mikono kwa furaha tele. Mioyo yao ilibadilika, chuki kubwa ikajengeka kwa Laurence, alionekana si kitu tena, hata ule upendo aliokuwa nao uliompelekea kutolewa figo yake kwa ajili ya msichana huyo hakikuonekana kuwa kitu, hakikuonekana kuwa na thamani tena, fedha ziliwabadilisha wote wawili.

    Kwa upende wa Laurence, aliumia sana moyoni mwake, hakuamini kile kilichokuwa kimetokea, kitendo chake cha kutoa figo yake na kumpa msichana huyo hakikuonekana kuwa na thamani yoyote ile. Kilimuumiza moyo wake lakini hakuwa na jinsi.

    Huo ulikuwa mwanzo tu, hakutaka kukata tamaa, kila siku alifika nyumbani hapo lakini mama Evadia alipofungua geti na macho yake kugongana na ya Laurence, tayari alionekana kukasirika, hakukuwa na kitu kilichomuudhi kama kumuona mwanaume huyo nyumbani kwake.

    “Umefuata nini?” aliuliza huku akionekana kuwa na hasira.

    “Nimemfuata Evadia.”

    “Kwani umemuona?”

    “Hapana mama! Ninataka nimuone.”

    “Hayupo.”

    “Yupo wapi?”

    “Alikwishakufa kitambo sana,” alijibu mwanamke yule.

    “Naomba unionyeshee hata kaburi lake mama.”

    “Nenda Kinondoni, zunguka makaburi yote, utaliona tu,” alisema mama Evadia.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Laurence aliendelea kuumia lakini hakuwa na cha kufanya zaidi ya kuondoka mahali hapo huku moyo wake ukimuuma sana. Alipiga hatua huku machozi yakimdondoka, hakukuwa na kitu kilichomuuma kama hicho.

    Alimpenda sana Evadia, hakutaka kumpoteza maishani mwake, alikuwa na thamani kuliko kitu chochote katika maisha yake lakini siku hiyo hakuonekana kuwa kitu chochote kile.

    Kulikuwa na vitu ambavyo vilimuumiza sana lakini hicho kilikuwa ni zaidi ya vyote. Hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya, kuuficha ukweli kwamba alikuwa tajiri kulionekana kulififisha penzi lake kwa msichana Evadia.

    “Bosi! Imekuwaje tena?” aliuliza Matilda kwenye simu.

    “Wewe acha tu Matilda. Majanga.”

    “Kivipi?”

    “Nimefukuzwa, tena nimeambiwa kwamba Evadia amekufa.”

    “Kweli?”

    “Ndiyo! Yaani imeniuma sana. Kumbe fedha zinaweza kumbadilisha mtu namna hii?”

    “Ndiyo hivyo! Pole sana bosi. Kwa hiyo inakuwaje?”

    “Kuhusu nini?”

    “Kuwasaidia fedha, nisitishe?”

    “Hapana! Sipendi Evadia awe na maisha magumu. Ninampenda sana, ninapenda kumuona akiwa na furaha siku zote. Endelea kuwasaidia kwani hata biashara zao nahisi haziingizi kiasi kikubwa cha fedha,” alisema Laurence.

    “Basi sawa. Nitafanya hivyo bosi.”

    “Nitashukuru, ila kumbuka kwamba unatakiwa kuficha siri, kuanzia kwa wafanyakazi ofisini mpaka kwao wenyewe.”

    “Hakuna tatizo.”

    Alichokifanya Laurence ni kuchukua kalamu kisha kuanza kuandika barua ndefu. Hakupata nafasi ya kuzungumza na msichana huyo hivyo kitu pekee alichokiona ni kuzungumza naye kupitia maandishi tu.

    Alikaa chini na kufikiria ni jinsi gani alimpenda Evadia, alijaribu kukumbuka siku ya kwanza kumuona uwanja wa Taifa, alipoanza kuongea naye mpaka siku hiyo, hakika moyo wake ulimuuma mno, hivyo vitu vyote alitaka kuviandika katika barua hiyo kwa kuamini kwamba msichana huyo angeweza kukumbuka na kumuonea huruma.

    Akaanza kuandika huku moyo ukimuuma mno, utajiri wote aliokuwa nao ulionekana kuwa si kitu kwa kuwa tu msichana aliyekuwa akimpenda kwa mapenzi ya dhati hakuwa pamoja naye, alimkataa kwa kuwa alikuwa masikini, hakuwa na thamani maishani mwake.

    Alichukua muda wa saa moja kuandika barua hiyo yenye kurasa mbili, alipomaliza, akaifunga vilivyo kwenye bahasha kisha siku iliyofuata kuanza kuelekea huko Mabibo.

    Matilda alimpakiza ndani ya gari, walipokaribia, akateremka na kuanza kuelekea katika nyumba ile. Muonekano wake ulikuwa uleule kwamba kijana masikini asiyejiweza, mtu aliyepigwa sana na maisha, alipolifikia geti lile, kama kawaida akaanza kuligonga.

    “Jamani! Mbona unasumbua sana siku hizi?” aliuliza mama Evadia mara baada ya kufungua geti, alionekana kukasirika.

    “Mama! Ninampenda Evadia, kusumbuka kwangu hakukuanzia hapa, tangu kipindi kile cha nyuma,” alisema Laurence.

    “Aya nikusaidie nini?”

    “Najua kwamba Evadia yupo ndani, naomba umpe hii barua yake, sina mengi ya kuzungumza,” alisema Laurence huku akimgawia mwanamke huyo hiyo barua.

    “Sawa. Kuna kingine?”

    “Hakuna!”

    “Basi unaweza kwenda,” alisema mwanamke huyo na kulifunga geti.

    Mama Evadia akarudi ndani huku mkononi mwake akiwa na barua ile, alitaka kufahamu mwanaume huyo aliandika vitu gani, alipoingia ndani, akamfuata Evadia aliyekuwa chumbani akisikiliza muziki kisha kumgawia barua ile.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hii nini?”

    “Barua yako ameileta yule nguchiro wako,” alijibu mama yake.

    “Ila si ulimwambia nimekufa!”

    “Sasa yeye ameng’ang’ania kukufufua, nifanyeje!”

    “Sawa.”

    Alichokifanya Evadia ni kuanza kuifungua bahasha kisha kukutana na karatasi iliyokuwa imeandikwa kwa kirefu sana, japokuwa hakuwa msomaji wa maandishi mengi lakini alichokifanya ni kuanza kuisoma barua hiyo, kama mtu aliyejilazimisha, akaanza kulisoma neno moja baada ya jingine, mstari kwa mstari. Barua hiyo iliandikwa hivi....



    Kwako Evadia.

    Nakumbuka siku ya kwanza nilipokuona, hakika moyo wangu ulitokea kukupenda kuliko msichana yeyote yule. Ulikuwa msichana mrembo ambaye hakika sikujuta kukufuata mpaka ulipokuwa unaishi, sikuishia siku hiyo tu, ili kukuonyeshea kwamba nilikuwa nakupenda sana, niliendelea kukufuata mpaka pale ulipokubali kuwa wangu.

    Evadia, nini kimekukuta? Kwa nini unanifanyia hivi? Ninaumia, unajua ni jinsi gani ninakupenda, unajua ni kwa jinsi gani umekuwa msichana pekee katika maisha yangu. Niliamua kutoa figo yangu moja kwa ajili yako, sikutaka kukuona ukiteseka kitandani, sikutaka kukuona ukifa kitandani pale, kwa mapenzi yangu yote, nikaamua kutoa figo yangu kwa kuwa nilitaka kukuona ukiwa na afya njema, utabasamu kama zamani, na kwenye kucheka, ucheke pia.

    Kila kitu kimebadilika, upendo wangu mwingi umeonekana si kitu, matokeo yake, umeamua kuniacha kama nilivyo, tena mbaya zaidi nikiwa mgonjwa. Evadia, una figo mbili, kumbuka figo moja hiyo yenye nguvu ni yangu, kwa nini hutaki kunithamini? Kwa nini hutaki kunipenda tena?

    Gharama ya figo ilikuwa ni milioni ishirini, nilikudai chochote? Sikufanya hivyo, upendo wangu juu yako ulikuwa ni zaidi ya hiyo milioni ishirni, kwa nini umebadilika? Kwa nini umeamua kunifanyia hivi?

    Evadia, fedha si kitu, unaweza kuwa tajiri leo, ukabadilisha magari, ukawa na ndege yako lakini kesho ukawa mbeba mizigo katika soko fulani, ndiyo! Hayo ni maisha na wengi yamewatokea.

    Mama yako aliniambia kwamba umekufa, sikutaka kukubaliana naye kwa kuwa naamini upo hai ukitabasamu na kuringia figo yangu moja niliyokupa.

    Kama kweli upo hai, naomba ujue kwamba ninateseka kwa penzi lako, sijiwezi bila wewe, naomba uje kuniokoa masikini mimi kwani maisha yananipigika sana, nimekuwa sina kitu, sina pa kuomba msaada, ila kwa sababu kwa sasa maisha yako ni afadhali, naomba unikumbuke na mimi, kumbuka upendo wangu, kumbuka kwamba hakuna mwanamke ninayempenda maishani mwangu kama ninavyokupenda.

    Kama upo tayari, naomba urudi kwangu, naomba tutengeneze maisha pamoja. Siangalii fedha zenu, siangalii maisha yenu, ninachokiangalia ni upendo wa dhati nilionao juu yako.

    Nakupenda Evadia. Rudi kwangu.

    Mpweke, Laurence.



    Ilikuwa barua yenye kuhuzunisha sana, barua yenye kugusa moyo, barua ambayo kama angetumiwa mtu wa kawaida, angeamua kubadilisha maisha yake na kufanya kile kilichotakiwa kufanya lakini kwa Evadia, alipoisoma barua ile akabaki akitabasamu, maneno yaliyoandikwa hayakumchoma hata mara moja, alibaki akicheka, alipomaliza akaikunjakunja na kuichana, akazichukua hedifoni zake na kuziweka sikioni, kilichofuata ni kuendelea kusikiliza muziki.

    Moyo wake ulibadilika, mapenzi aliyokuwa nayo kabla yalipotea, hakumpenda tena Laurence, alimchukia kwa kuwa tu hakuwa na fedha, alisahau kwamba mwanaume huyohuyo aliamua kumpenda japokuwa nyumbani kwao maisha yao yalikuwa ya shida mno.

    Siku zikaendelea kukatika, mawazo ya Laurence akaanza kuyafuta kichwani mwake, hakutaka kumkumbuka, hakutaka kukumbuka lolote lile juu ya mwanaume huyo, kwa kifupi hakutaka hata kumuona.

    “Ameandikaje?” aliuliza mama yake.

    “Alikuwa analialia tu.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hebu niisome.”

    “Nishaichanachana, sina muda wa kuhifadhi uchafu,” alijibu Evadia.

    Kama kubadilika, alibadilika, hakutaka kusikia la mtu yeyote yule. Miezi miwili baadaye akapona kabisa na hivyo kumsaidia mama yake katika biashara zake alizokuwa akizifanya.

    Pamoja na mabaya yote hayo lakini ikawa kama Mungu amefungua milango ya baraka, waliingiza fedha, hawakuwa matajiri lakini waliweza kujikimu maisha yao na kiasi cha fedha kama milioni tano hakikuwapiga chenga kabisa.

    Alifanyiwa ubaya, alisahaulika lakini Laurence hakutaka kuacha kumsaidia msichana huyo, alimpenda kwa moyo wa dhati, alihakikisha kwamba maisha yake kila siku yanakuwa kama vile alivyotaka yawe.

    Hakutaka kutafuta msichana mwingine, kwake, Evadia alionekana kuwa kila kitu. Hakuacha kwenda nyumbani kwa msichana huyo, wakati mwingine alipofika huko na kugonga hodi, mama Evadia alipofungua mlango na macho yake kutua kwa Laurence, aliufunga mlango huo kwa dharau.

    Laurence hakuwa akiondoka, alichokifanya ni kubaki hapo nje, jua lilikuwa kali, alichokifanya ni kukaa hapohapo getini. Kwa jinsi alivyokuwa mchafu, watu waliokuwa wakipita nje walifikiri kwamba alikuwa ombaomba, hawakumjua kabisa kama alikuwa bilionea, kwao, mtu huyo alionekana kujaa umasikini mkubwa.

    Waliokuwa na fedha, walimsaidia hapohapo getini, hawakujua kama fedha hizo walikuwa wakimpa bilionea mkubwa. Laurence aliendelea kubaki getini, moyo wake ulijawa na hasira kali lakini hakutaka kuzionyesha, alitamani aingie ndani na kuwaambia kwamba yeye alikuwa bilionea na yule Laurence aliyekuwa akisikika mitaani na kuwa gumzo kutokana na utajiri wake alikuwa yeye lakini hakutaka kufanya hivyo, alitaka kuona mwisho wake ungekuwa upi.

    “Matilda, njoo huku kwa kina Evadia,” alimwambia Matilda kwenye simu.

    “Kuna nini bosi.”

    “Wewe njoo tu.”

    “Sawa bosi.”

    Laurence akakata simu na kuanza kumsubiri msichana huyo aweze kufika ili afanye kile alichotaka mafanyie. Ilipita nusu saa, gari aina ya Verrosa likafunga breki mbele ya nyumba hiyo na Matilda kuteremka, alipomuona Laurence pale chini alipokuwa, akabaki akishangaa, hakutegemea kumuona bosi wake mahali pale.

    “Nini kimetokea?” aliuliza Matilda huku akionekana kushangaa.

    “Yaani umesahau kama tunaigiza? Usihuzunike sana. Nimefungiwa mlango. Mama Evadia ametoka, aliponiona, akarudi ndani na kufunga mlango,” alisema Laurence.

    “Hapana! Haiwezekani.”

    “Ndiyo hivyo! Naomba upige hodi tena kwa honi ili aje kufungua tuingie ndani, tukifika humo, omba tuonane na Evadia,” alisema Laurence.

    “Sawa.”

    Hicho ndicho kilichotakiwa kufanywa, alichokifanya Matilda ni kurudi garini kisha kuanza kupiga hodi kwa kutumia honi ya gari. Wala hazikupita dakika nyingi, mama Evadia akatokea na kulifungua geti.

    Matilda akaingiza gari ndani ya nyumba hiyo, Laurence hakutaka kubaki nje, naye akatumia nafasi hiyohiyo kuingia ndani. Mama Evadia hakutaka kumwambia kitu chochote japokuwa alimwangalia kwa jicho kali lililoonyesha hasira kubwa kwani hakutaka kumuona hata kidogo.

    Matilda akateremka, uso wake ulijawa na tabasamu pana, akamsalimia Laurence kana kwamba hakuwahi kumuona kisha kumsogelea mama Evadia na kumsalimia pia.

    “Karibuni ndani,” alimkaribisha mama Evadia na wote kuanza kwenda ndani.

    Alichokifanya mama Evadia ni kuanza kuonyesha unafiki, akajifanya kumchangamkia Laurence ili Matilda asigundue kilichokuwa kikiendelea na wakati nyuma ya pazia, kila kitu kilichotokea kilijulikana na kila mtu.

    Wakaingia ndani, wakakaa kochini na kuanza kuzungumza mambo mengi. Muda wote huo mama Evadia aliendelea kulionyesha tabasamu pana usoni mwake. Alichokifanya Matilda ni kumuomba mwanamke huyo amuite Evadia, hilo halikuwa tatizo, hapohapo alipokaa, akamuita binti yake kwa sauti kubwa, akaitikia na kumwambia kwamba angekuja.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wala haikupita hata dakika moja, Evadia akatokea sebuleni hapo. Macho yake yalipotua kwa Laurence tu, akabaki akiwa na mshtuko mkubwa, hakuamini kumuona mahali hapo, ili kujifanya hajashtuka, akaanza kutoa tabasamu pana lakini mshtuko wake haukufichika usoni mwake.

    “Karibuni sana,” alisema Evadia huku akiwasogelea na kuwasalimia.

    Moyo wa Laurence ukapoa, hakuamini kama mpenzi wake alipona kabisa na kuwa mzima wa afya, akashindwa kuvumilia, hapohapo akasimama na kisha kumkumbatia kwa nguvu kama mtu ambaye hakutaka kumuacha aondoke zake.

    Mapenzi aliyokuwa nayo yalikuwa makubwa mno, alikuwa tayari kitu chochote kitokee lakini si kuona akimkosa msichana huyo ambaye hakuwa na habari naye kabisa.

    “Nimekukumbuka mpenzi,” alisema Laurence, tayari machozi ya hisia yakaanza kumtoka.

    “Nimekukumbuka pia,” alisema Evadia, lakini uso wake ulitofautiana na maneno aliyoyasema mahali hapo.

    Wakaanza kuzungumza, muda wote Laurence alikuwa akimwangalia Evadia, kila alipomtazama, alihisi mapenzi mazito moyoni mwake, alihisi kumpenda msichana huyo maradufu.

    Alichokifanya ni kuchukua simu yake, alitaka kurekodi sauti juu ya kila kitu ambacho kingesemwa mahali hapo, alitaka kubaki na kumbukumbu, ushahidi ambao hapo baadaye ungemfanya Evadia kulia sana, hivyo akaanza kurekodi.

    Matilda hakutaka kukaa sana, alichokifanya ni kuondoka kwani ndiyo meseji aliyoandikiwa kisiri na Laurence kwamba alitakiwa kuondoka, akaaga na kuondoka zake.

    Wakabaki watatu ndani ya nyumba, Evadia na mama yake wakaanza kumwangalia Laurence kwa macho ya chuki, hakukuwa na mtu aliyempenda kwa wakati huo kwa sababu tu alikuwa mtu masikini ambaye hakuwa na uwezo wowote ule.

    “Evadia...” aliita Laurence.

    “Nini?”

    “Mbona unanifanyia hivi mpenzi?” aliuliza.

    “Nani mpenzi wako?”

    “Wewe hapo.”

    “Tangu lini? Hivi mama hukumwambia kwamba ninataka kuolewa?” aliuliza Evadia.

    “Sikumwambia, nilisahau.”

    “Unataka kuolewa?”

    “Ndiyo! Tena ningetaka mchango wako,” alisema Evadia huku akimwangalia Laurence kwa macho ya chuki.

    “Evadia, mbona unaamua kunifanyia hivi?”

    “Hivi wewe mwanaume mbona unapenda kuishi kwa mazoea? Yaani unapenda kuishi kwa historia tu, hivi unafikiri kama zamani nilikuwa mpenzi wako basi mpaka sasa hivi ni mpenzi wako? Hebu acha maneno yako,” alisema Evadia na kumalizia na msonyo mmoja mkubwa.

    Maneno yalimuumiza moyo wake, maneno hayo yalimchoma, alihisi kitu chenye ncha kali, tena kikiwa cha moto kikiuchoma moyo wake, alisikia maumivu makubwa ya moyo, hakuamini kama kweli maneno yale aliyazungumza Evadia au mtu mwingine.

    “Unasemaje Evadia....”

    “Bwanaeeee...kwani hujanisikia,? Tangu lini umekuwa kiziwi.”

    “Evadia, kumbuka kwamba una figo yangu.”

    “Sasa nikishakumbuka?”

    “Nilifanya hivyo kwa kuwa ninakupenda.”

    “Kwani nilikulazimisha? Nilikulazimisha?”

    “Evadia mpenzi! Mbona umebadilika hivyo?”

    “Nimekuwaje? Mwekundu au wa njano? Halafu hilo neno la mpenzi unamwambia nani? Nani mpenzi wako? Nisikilize wewe masikini, sahau kila kitu kilichotokea kati yangu na wewe. Tena sahau kabisaaaa...” alisema Evadia huku akionekana kumaanisha alichokisema. Hapohapo Laurence akamgeukia mama Evadia.

    “Mama! Mbona Evadia kabadilika hivi?”

    “Nani mama yako?”

    “Jamani! Mbona mnakuwa hivi?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hakukuwa na mtu aliyejibu chochote, walichomwambia ni kwamba alitakiwa kuondoka nyumbani hapo mara moja. Laurence hakubisha alichokifanya ni kusimama na kutoka nje huku moyo wake ukiwa kwenye maumivu makali kwani kwa kile kilichokuwa kimetokea mahali pale, hakika hakuweza kukiamini huku wakati mwingine akihisi kama alikuwa ndotoni na baada ya dakika chache angeamka.



    Mapenzi yalikuwa motomoto, walipendana kwa mapenzi ya dhati hata pale msichana Luciana aliporudi nchini Rwanda, bado kila mmoja alijaribu kadiri ilivyowezekana kuwasiliana na mwenzake.

    Hakukuwa na kitu kilichowatenganisha, kila kilichokuwa kikiendelea katika maisha yao, walikikabidhi mikononi mwa Mungu ili mwisho wa siku wakutane tena na kufunga ndoa ambayo waliamini kwamba wasingeweza kutengana maisha yao yote.

    Luciana alikuwa na fedha, alijiona kuwa tajiri, hapohapo, alichokifanya ni kununua jumba kubwa katika mtaa mmoja wa kitajiri hukohuko Kigali, akanunua gari la thamani ambalo lilizua gumzo kubwa mitaani.

    Hilo hakutaka kuliangalia, alichokuwa akikitaka ni kuwaonyeshea watu kwamba alikuwa na fedha, alitoka nje ya nchi na kuvuna fedha nyingi, sasa katika kipindi hicho ndiyo ulikuwa muda wa kula matunda kwa kazi kubwa aliyokuwa akiifanya nchini Venezuela.

    Hakukatisha mawasiliano na Dickson, kila siku ilikuwa ni lazima kumpigia simu na kuzungumza naye. Uhusiano wao wa kimapenzi ulizidi kupanda juu, walizidi kupendana lakini baada ya miezi sita, hasa baada ya kukutana na mwanaume mwenye mchanganyiko wa mtu mweusi na uarabu, Luciana akajikuta akianza kupoteza dira katika penzi lake na Dickson.

    “Mmmh! Kumbe kuna wanaume wazuri namna hii, sijawahi kuona,” alisema Luciana huku akimwangalia mwanaume aliyesimama karibu na kaunta katika baa moja maarufu iitwayo Leopard ambayo ilikuwa katikati ya Jiji la Kigali.

    Kwa jina aliitwa Rahman Abdoulaziz, alikuwa kijana mtanashati ambaye baba yake, mzee Mohammed Abdoulaziz alikuwa Mwarabu kutoka nchini Oman huku mama yake akiwa Mtusi wa hapohapo Rwanda.

    Rahman alikuwa mzuri wa sura, wanawake wengi hapo Kigali walimpapatikia kwa kuwa ilisemekana yeye ndiye mwanaume mzuri kuliko wanaume wote waliokuwa katika jiji hilo.

    Rahman hakuwa mtu wa kupenda wanawake, alikuwa mtu wa kivyakevyake, wanawake waliokuwa wakimfuatilia, kila siku aliwatolea nje kwani alilelewa katika mazingira ya dini, hivyo hakutaka kufanya mambo ambayo yalionekana kama dhambi kubwa kwa Allah.

    Wanawake hawakuacha kumfuatilia huku na yeye hakuacha kuwakataa. Kila siku wanawake wapya waliibuka na kumtaka kimapenzi lakini msimamo wake ulikuwa uleule kwamba pepo ilikuwa muhimu kuliko mapenzi.

    Rahman alipoanza kuwa na marafiki wengi wa mitaani, hapo ndipo alipoanza kubadilika, wengi walimsifia kwamba alikuwa kijana mzuri hivyo kama alitaka kupata fedha kutoka kwa wanawake, basi uzuri wake ungekuwa chachu kubwa.

    Hilo likamfungua ubongo wake, hakutaka kuchelewa, alichokifanya ni kuanza kudili na wanawake waliokuwa wakimpapatikia ila fedha ndiyo kilikuwa kitu cha kwanza.

    Kulala kitanda kimoja na Rahman lilikuwa jambo zuri, kwa watoto wa matajiri hawakutaka kutulia, kila walipoambiwa kuhusu mwanaume huyo na kumuona, walikiri kwamba walikutana na mwanaume mzuri sana, hivyo wakataka kulala naye.

    Hakulala na mwanamke bila fedha, kama kulikuwa na machangudoa waliokuwa wakijiuza mitaani, basi naye kwa kipindi hicho akaamua kujiuza kwa wanawake hao ambao walimpa fedha nyingi kisha kulala naye.

    Kitendo cha Luciana kumuona Rahman hapo baa akachanganyikiwa, hakuamini kama nchini Rwanda kungekuwa na mwanaume aliyekuwa na sura nzuri kama alivyokuwa Rahman, akashindwa kuvumilia, alimwangalia sana na mwisho wa siku kuanza kumfuata.

    “Unakwenda wapi Luciana?” aliuliza mmoja wa rafiki yake aliyekuwa akinywa naye.

    “Nakwenda kuzungumza na yule mwanaume,” alijibu.

    “Yupi?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Yule pale,” alisema huku akimnyooshea kidole Rahman.

    “Kumbe Rahman!”

    “Anaitwa nani?”

    “Rahman,” alijibu rafiki yake, hapohapo akawarudia kwanza apate kusikia mengi kuhusu mwanaume huyo.

    “Kumbe mnamfahamu?”

    “Kuna mwanamke asiyemfahamu Rahman hapa Kigali? Hakuna asiyemfahamu. Ndiye mwanaume mzuri kuliko wote, wewe mwenyewe si unamuona!” alisema rafiki yake.

    “Ndiyo! Namuona. Ana mpenzi?”

    “Mpenzi? Rahman awe na mpenzi! Huyo mpenzi hajitaki!”

    “Kwa nini?”

    “Mmmh! Anavyopendwa na wanawake, nadhani huyo mpenzi atakufa kwa presha,” alisema rafiki huyo.

    “Hilo tu?”

    “Si hilo tu. Kuna jingine.”

    “Lipi?”

    “Kama hauna hela, huwezi kuwa na mwanaume mzuri kama Rahman,” alisema rafiki huyo.

    “Kivipi?”

    “Huyo jamaa kakaa kifedha zaidi, halali na mwanamke bila fedha, yaani kama anajiuza,” alisema.

    Moyo wake ulikufa na kuoza kwa mwanaume huyo, hakutaka kusikia chochote kile, alichokitaka kwa wakati huo ni kuwa na mwanaume huyo tu. Kuhusu fedha kwake halikuwa tatizo hata kidogo, alikuwa nazo nyingi hivyo kummiliki mwanaume kama Rahman wala halikuwa tatizo kabisa.

    Alichokifanya ni kuanza kupiga hatua kumfuata mwanaume huyo, alipomfikia, akasimama pembeni yake kisha kutoa tabasamu pana. Alipomwangalia vizuri kwa karibu ndipo akagundua kwamba mwanaume yule alikuwa na uzuri wa ajabu, damu yake ikaanza kuzunguka kwa kasi mwilini mwake, mapigo ya moyo yakawa yanadunda mno kiasi kwamba hata yeye mwenyewe akajishangaa.

    “Habari yako Rahman,” alisalimia Luciana.

    “Salama mrembo, karibu,” aliitikia Rahman huku akiachia tabasamu lililomfanya Luciana kuweweseka.

    “Asante. Naweza kuzungumza nawe?”

    “Kuzungumza nami?”

    “Ndiyo!”

    “Kuhusu nini?”

    “Mambo tu ya kawaida.”

    “Mmmh! Sawa. Nakupa dakika tano tu.”

    “Sawa. Tunaweza kwenda nje ya baa hii?”

    “Twende wapi sasa?”

    “Hata kwenye gari langu.”

    “Hakuna noma.”

    Rahman alikuwa mtu wa kupenda fedha, kwa jinsi alivyomuona Luciana, alijua kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima msichana huyo awe na fedha nyingi kwani kwa mtu aliyekuwa na fedha, hakika zisingeweza kujificha mwilini mwake.

    Alimtupia macho vizuri Luciana, alionekana kuwa msichana mrembo, mwenye fedha ambaye alivalia sketi fupi laini iliyoyafanya mapaja yake kuwa nje, juu alivalia blauzi laini huku ndani kukiwa kutupu kabisa kitu kilichofanya kifua chake kuonekana vizuri machoni mwa Rahman, mpaka kufika hapo, akachanganyikiwa.

    Wakatoka nje ya baa hiyo. Wakaelekea mpaka kwenye eneo la maegesho ya magari na kusimama nje ya gari moja la kifahari. Rahman alipoliona gari hilo, hakuamini macho yake, lilikuwa gari la kifahari lililoendeshwa na watu wenye fedha.

    Alizoea kuliona gari kama hilo kwenye video za wanamuziki nchini Marekani, hakuwahi kuliona laivu, kitendo cha kuliona gari hilo, akili yake ikamwambia kwamba mwanamke aliyesimama mbele yake hakuwa wa kawaida.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ingia tu,” alisema Luciana huku naye akizunguka mlango wa upande mwingine.

    Rahman akaufungua mlango na kuingia ndani. Harufu nzuri ndani ya gari lile likaifanya pua yake kuweweseka.

    Humo garini, Luciana hakutaka kuvumilia, alimwambia Rahman kile kilichokuwa kikiendelea moyoni mwake kwamba alikuwa akimpenda sana, alimhitaji na kutaka kuwa mpenzi wake wa milele.

    Rahman hakuzungumza kitu, alibaki kimya. Kila alipomwangalia Luciana, kweli alikuwa msichana mrembo, alikuwa na fedha lakini tabia yake ya kukaa kimaslahi ilionekana kama kumharibia, hivyo alichokifikiria kwa haraka sana ni kumtalia Luciana.

    “Haiwezekani,” alisema Rahman.

    “Kwa nini?”

    “Siwezi kuwa na msichana wa kudumu, muda wa kuoa bado kabisa,” alisema Rahman kwa kujiamini.

    “Rahman, najua unachokifikiria, nimesikia mengi kuhusu wewe, jua kwamba ninajua mengi, nimeamua kukufuata wewe kwa sababu ninakupenda, u mwanaume mzuri mno, naomba uwe nami, naomba uwe mmiliki halali wa moyo wangu,” alisema Luciana huku akimwangalia mwanaume huyo usoni.

    “Kuwa na mimi?”

    “Ndiyo!”

    “Ni kitu kisichowezekana. Wewe unakuja kimapenzi na mambo ya kuishi milele na wakati mwenzako nipo kimaslahi, siwezi kuwa nawe,” alisema Rahman, alionekana kumaanisha, hapohapo akaufungua mlango kwa lengo la kutoka nje, kabla hajafanya hivyo, akashtukia akishikwa mkono na Luciana, alipogeuka, msichana huyo akamsogelea na kuanza kubadilishana naye mate ghafla.



    Dickson alichanganyikiwa, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea maishani mwake, alijaribu kumtafuta msichana wake, Luciana simuni lakini hakuwa akipatikana na hata hizo mara chache ambazo alipatikana, majibu yake yalikuwa tofauti na vile alivyokuwa akitegemea.

    Alimpenda sana, hakutaka kuwa na msichana mwingine katika maisha yake zaidi ya Luciana ambaye alimfanya kumuacha Evadia na kuwa naye. Kwake, maisha bila Luciana yalikuwa mateso makubwa, hivyo kitendo cha msichana huyo kutokueleweka simuni kulimchanganya mno.

    Hakuridhika, hakuishia hapo, aliendelea kumpigia simu msichana huyo na mara ya mwisho kabisa kuwasiliana naye, akafungiwa simu yake kitu kilichomuweka katika wakati mgumu mno.

    Alihangaika na kuhangaika, alijaribu kubadilisha simu yake lakini kitu kilichomuumiza zaidi hapo baadaye ni kwamba msichana huyo aliamua kubadilisha simu kitu kilichomsababishia maumivu makali ya mapenzi ambayo hayakuelezeka hata mara moja.

    Hakutaka wazazi wake wafahamu kitu chochote kile, yale maumivu makali, yalikuwa moyoni mwake, hakutaka kumwambia mtu yeyote. Kile kilichokuwa kikitokea kwa msichana Evadia ndicho kilichoanza kumtokea kipindi hicho.

    Hakutaka kurudi tena chuoni, hakuona kama angeweza kusoma na wakati alikuwa kwenye hali mbaya, mapenzi yalimtesa, yalimuonea na kumnyima fura ambayo alitarajia kuipata katika kipindi kifupi kijacho.

    Hakutaka kubaki nchini Tanzania, kitu alichokifanya ni kupanga safari ya kuelekea nchini rwanda, alichotaka kufahamu ni juu ya kilichokuwa kikiendelea kwa msichana Luciana kwani kuna kipindi alihisi kwamba msichana huyo alipobadilisha namba hiyo alisahau kuisevu namba yake.

    “Mbona upo hivyo?” aliuliza mama yake.

    “Nipo vipi?”

    “Unaonekana una mawazo. Halafu si leo tu, tangu juzi,” alisema mama yake.

    “Hakuna kitu mama.”

    “Sawa. Chuo vipi?”

    “Nitakwenda, ila si leo wala kesho.”

    “Kwa nini?”

    “Mama! Kuna safari nataka kwenda.”

    “Wapi?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Rwanda, nataka niende kumsalimia Luciana,” alijibu Dickson.

    Huo ndiyo uamuzi aliouamua, tayari taratibu zote za safari alikwishazifanya na kitu pekee alichokuwa akikisubiria ni kuwaaga wazazi wake kisha kuondoka nyumbani hapo.

    Usiku, mama yake akamwambia baba yake juu ya kilichokuwa kimetokea kwamba kijana wao, Dickson aliamua kufunga safari kuelekea nchini Rwanda kuonana na mpenzi wake, mzee huyo alichokishangaa ni kwamba safari ilikuwa ghafla sana.

    “Kuna nini Dickson?” aliuliza baba yake.

    “Hakuna kitu.”

    “Mbona ghafla hivyo?”

    “Hakuna tatizo baba. Ninataka kumuona Luciana.”

    “Kuna amani lakini?”

    “Ipo, tena nyingi tu.”

    “Na chuo?”

    “Nitakwenda tu.”

    Hakukuwa na wa kumzuia, aliamua kuondoka nchini Tanzania na kuelekea Rwanda kwa kuwa alitaka kuonana na mpenzi wake. Japokuwa wazazi walijitahidi kumwambia maneno mengi ya kumzuia lakini Dickson hakuzuilika, hakutaka kusikia lolote lile, alichokuwa akikitaka ni kuelekea nchini Rwanda tu.

    Siku iliyofuata, mchana, akaanza safari ya kueleke uwanja wa ndege ambapo akapanda ndege na kuanza kuelekea nchini humo huku akiwa na mawazo lukuki.

    Hakuzungumza na mtu yeyote yule, abiria ambaye alikaa naye alijaribu kumuongelesha lakini majibu yake yalikuwa mafupi yaliyoonyesha kwamba alitakiwa kuachwa apumzike.

    Alichukua saa kumi mpaka kufika nchini Rwanda. Ndege ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kigali, iliposimama, hapohapo abiria wakaanza kuteremka.

    Hakuwa mwenyeji sana hapo Kigali lakini siku ya kwanza aliyofika mahali hapo ilimfanya kukumbuka vilivyo kule alipoelekea na msichana Luciana, alichokifanya ni kuzifuata taksi kadhaa zilizokuwa pembeni na kuanza kuzungumza na dereva mmoja.

    “Naomba unipeleke Mwongozo,” alimwambia dereva huyo.

    “Hakuna tatizo, ingia.”

    “Ila kwanza nipeleke kwenye duka la kubadilisha fedha kisha twende huko.”

    “Hakuna tatizo.”

    Hapo ndipo safari ya kuelekea katika duka la kubadilishia fedha ilipoanza. Njiani, Dickson alikuwa na mawazo tele, alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa, kile kilichokuwa kikitokea katika maisha yake kilimchanganya mno.

    Mpaka taksi inasimama, hakuwa akijua, alikuwa kwenye lindi kubwa la mawazo. Dereva ndiye ambaye alimshtua kwamba tayari walikwishafika katika duka hilo hivyo angeendelea kufanya kile alichotaka kufanya.

    Kwa harakaharaka Dickson akateremka kutoka garini na kuanza kuelekea ndani ya duka lile ambapo akachukua fedha zake za Kitanzania na kisha kubadilisha kwa fedha za Rwanda kisha kurudi garini na kuanza safari ya kuelekea katika Mtaa wa Mwongozo.

    “Mbona una mawazo hivyo?” aliuliza dereva, wakati huo teksi ilisimama kwenye foleni.

    “Mapenzi yanauma sana.”

    “Kivipi tena? Kuna mtu kakutenda?”

    “Kuna mchumba wangu simuelewielewi kabisa, yaani yupoyupo tu,” alijibu Dickson.

    “Pole sana,” alisema dereva yule.

    Safari iliendelea mpaka walipofika katika mtaa huo ambapo kwa maelekezo ya Dickson, gari likasimama nje ya nyumba moja ambapo nje kulikuwa na mafundi waliokuwa wakirekebisha baadhi ya vitu katika nyumba hiyo.

    Dickson akateremka na kuelekea ndani. Alipofika huko, akakaribishwa na kutulia kitini. Alijulikana hapo nyumbani hivyo haikuwa kazi kubwa kuambiwa kwamba mchumba wake, Luciana hakuwa nyumbani muda huo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Amekwenda wapi?”

    “Alihama.”

    “Alihama? Amehamia wapi?”

    “Kivikile…”

    “Ndiyo wapi?”

    “Si mbali kutoka hapa. Kwani hakukwambia?” aliuliza mama Luciana.

    “Hapana! Nilipoteza simu na namba yake sikuwa nimeikariri,” alidanganya.

    “Basi hapa alihama, amenunua nyumba huko Kivikile, subiri nimwambie mtu akupeleke,” alisema mama Luciana.

    Dickson hakutaka kubaki mahali hapo, alipoletewa kijana ambaye alitakiwa kumpeleka alipokuwa akiishi Luciana, wakatoka nje na kuanza kuelekea huko.

    Moyo wake ulikuwa na presha kubwa ya kutaka kumuona Luciana, alimkumbuka mno, alimpenda, mapenzi aliyokuwa nayo moyoni juu ya msichana huyo yalikuwa hayaelezeki hata mara moja, kama ni baharini, tayari yalikuwa maji ya shingo.

    “Hivi kuna kitu gani kinaendelea?” aliuliza Dickson.

    “Wapi?”

    “Kwa Luciana, yaani simuelewielewi.”

    “Hakuna kitu kinachoendelea.”

    “Buka! Mimi ni mwanaume mwenzako, inakuwaje unanificha bwana, au unaona raha kuona nikiumia hivi?” aliuliza Dickson.

    “Kweli hakuna kitu.”

    “Buka, macho yako tu yanaonyesha jinsi unavyonidanganya, hebu shika hii kwanza,” alisema Dickson, hapohapo akatoa fedha ya Rwanda, Franc elfu moja na kumpa Buka.

    Hicho kilikuwa ni kiasi kikubwa cha fedha, hapohapo Buka akakichukua na kujiweka sawa kitini, hakutaka kuficha siri, fedha ilimpagawisha, akaamua kutoa siri.

    “Luciana ana mwanaume mwingine,” alisema Buka.

    “Ana mwanaume mwingine?”

    “Ndiyo! Mwarabu fulani hivi, tena huku tunapokwenda unaweza kukutana naye,” alisema Buka.

    “Kweli?”

    “Kwa nini nikudanganye na wakati umenipa hela? Kweli tena,” alisema Buka.

    Dickson akashusha pumzi nzito, hakuamini kile alichokisikia kutoka kwa Buka, akahisi presha ikipanda na kushuka, kijasho chembamba kikaanza kumtoka, hakuamini kile alichokisikia kwamba mpenzi wake alikuwa kwenye uhusiano na mwanaume mwingine.

    Wakati akiwa ameshikwa na hasira, wivu ukiwa umemkaba kooni, hapohapo wakafika katika jumba la kifahari ambalo aliambiwa kwamba msichana wake, Luciana alikuwa akiishi, dereva akasimamisha na wao kuteremka, wakaanza kupiga hatua kuelekea getini.

    “Karibuni,” aliwakaribisha mlinzi aliyeshika bunduki.

    “Asante. Dada yupo?”

    “Yupo ndani kapumzika na shemeji.”

    “Naomba tukamuone.”

    “Subiri kwanza Buka, huyu nani?”

    “Mshikaji wangu!”

    “Mgeni wa nani?”

    “Dada!”

    “Hapana! Hatakiwi kuingia!”

    “Kwa nini sasa?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mama alimpigia simu Luciana na kumwambia ulikuwa unakuja na mgeni, hivyo aliniambia nisiwaruhusu kuingia, kama kuingia, ingia peke yako, ila huyu abaki,” alisema mlinzi.

    “Unasemaje?”

    “Ndiyo hivyo kaka! Hautakiwi kuingia, kama vipi rudini mlipotoka,” alisema Buka maneno yaliyomfanya Dickson kuumia kupita kawaida. Akahisi miguu ikikosa nguvu na mwili kumtetemeka. Akajiona kama muda wowote ule angekufa.



    ITAENDELEA

Blog