Search This Blog

Friday, October 28, 2022

NENDA NA MOYO WANGU - 5

 

     





    Simulizi : Nenda Na Moyo Wangu

    Sehemu Ya Tano (5)





    MAMBO HAYO YALIKUWA HIVI

    Nikiwa chumbani kwangu siku ambayo Michael

    alikuja na mimi ndio kwanza nilikuwa nimetoka kumsindikiza, babaaliingia akiwa na hasira.

    "Ni mara ngapi nikuambie sitaki kumuona yule kijana hapa nyumbani?"Nilimtazama baba kwa hasira kila nilipomtazama na kumuona ni mzeeanayezeeka vibaya. Kwanza Michael alipokuwa akija nyumbani,

    akimsalimia baba alikuwa haitiki. Sikupenda kumuuliza kwanini alikuwahaitiki salamu ya rafiki yangu huyo na hata hivyo sikumjibu palealipouliza mpaka aliporudia tena

    "Nakuuliza, kwanini unamleta yule muhuni nyumbani kwangu?"

    "Baba yule sio muhuni na sioni ubaya wowote aliokufanyia naomba umuheshimu"

    Baba alicheka kicheko ambacho hakikuwa na ladha ya kuwa kicheko balikaraha, kisha akanizaba kibao kikali na kunieleza"Yule si rafiki mwema kwako na hafai kuwa rafiki yako mshenzi wewe"

    Akatoka huku akiniacha nimelishika shavu langu kwa maumivu. sikuwaza

    kwanini aliniambia vile, au kwanini alimchukia kiasi kile mpaka siku

    ambayo nikiwa nimekaa nje ya nyumba yetu nikijisomea kitabu ndipobaba

    aliponijia tena.

    "Hujambo!?"
    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nilimtazama na kuitika sijambo kisha nikamsalimia.

    "Marahaba, nataka kuzungumza na wewe Ramon"nikakitua kitabu kile kwenye mapaja yangu nikamtazama baba"Mwanangu, wewe ni mwanangu wa pekee na unajua ni kiasi ganinakupenda. Sio kwamba ninapokukataza kuwa na urafiki na Michael ninania mbaya na urafiki wenu. Michael ni rafiki mliyekutana chuo wotemkiwa mmeshakuwa wakubwa na kila mtu ana tabia zake, Michael unazijuazake?" akaniuliza, mimi nikatingisha kichwa"Hapana" nikajibu

    "Basi ni hivi, Michael anawatumia wanawake waliomzidi umri kwa

    kuwachuna na kuyaendesha maisha yake, miongoni mwa wanawake hao ni

    mama yako"

    Nilikumbwa na mshituko nikayatoa macho pima nisiamini nilichokisikia

    nilibaki kinywa wazi huku nikiendelea kumtazama baba, wala yeye hakuongea

    chochote alipoona nimehamanika, akaondoka.Mawazo hayo yalikatishwa na sauti ya Bella yule askari wa kike.

    "Chakula tayari"nikala pale na kisha nikarudi pale ukumbini kutazama runinga.

    Kesho yake alikuja Vanessa kama alivyoahidi akiwa na ujumbe mzitoulionishitua na kunifanya nijue mengi. Hapo mwanzo sikujua kama Bella alihusika katika

    kumuuwa Beatrice, basi ndivyo ilivyo kwenye ripoti ya Vanessa

    aliyoshika mkononi mwake.

    Mimi na Vanessa tulisalimiana akiwa amebebabahasha pekee ya kaki mkononi mwake. Hakuwa na chochote, hata ulemkoba wa kuhifadhia tepurekoda yake.

    "Pole sana kwa matatizo"ghafla kabla sijaitikia salamu ile, nilimsikia yule askari wa kike,

    Bella akipiga kelele"Niacheni, niacheni nasema. Mnaniumiza!!"

    Nikamgeukia Vanessa kwa macho ya mshangao na kumuuliza

    "Vipi, kuna nini?"Vanessa alibitua midomo huku tabasamu laini likimpitia akiwa ameinua

    mabega yake kwa dharau. Akanitupia ile bahasha

    "Tulipopima ile simu ya mpenzi wako(Beatrice) alama za vidole

    vilivyoshika na kutuma ujumbe ule kwako, ni alama za vidole vya huyu

    askari"

    Wakati nikiyasikiliza hayo, nilikuwa nikimtazama Bella aliyekuwa

    akitolewa nje ya jumba lile kinguvu. Alikuwa akilalamika kwa huruma na

    majonzi

    "Mimi sihusiki jamani, mimi sijauwa"Ndio neno la mwisho kulisikia kutoka kwa Bella na mara nikamgeukia

    Vanessa, aliendelea kunieleza"Unajua si rahisi kupata matokeo ya alama za vidole vya mtu ambaye

    rekodi yake haipo katika rekodi ya jeshi la polisi lazima mtu huyu awe

    ni mtu ambaye amewahi kutenda makosa ya jinai na kukamatwa ama kwa mtu

    ambaye ni mwajiriwa wa serikalini ambaye alitia sahihi ya dole gumba

    kwa wino katika karatasi zake za mkataba. Hivyo ilikuwa rahisi kupata

    taswira ya huyu koplo Bella Daniel Zagamba na uzoefu wake kazini

    pamoja na mwaka alioajiriwa"Nikashusha pumzi ndefu kwa uzito wa taarifa ile iliyozidi

    kunikanganya, ikabidi nimuulize Vanessa huku nikimrudishia zile

    karatasi

    "Huyu askari amekua karibu na mimi kwa kipindi chote tangu nimeletwa

    humu ndani na alionesha kuyajua mengi kuhusu kesi hii lakini

    inawezekanaje yeye awe ndiye muuaji? Vile vile haitwi Bella Daniel Zagamba yeye ni Bella Matondane inakuaje hii?"Vanessa alicheka kwa kebehi na kunieleza kwa umakini"Hili jambo ni zito Ramon si rahisi kuamini ukitajiwa muuwaji lakiniinabidi uvumilie na uyashinde. Wivu wa mapenzi ndio uliosababisha kifocha mwenzi wako na aliyemuua ni mtu wako wa karibu"

    Nikamkatisha "nilijua tu, nilijua ni Michael. Michael ndiye alimuuwa

    Beatrice kwa kuwa Beatrice alinipenda mimi"

    "Usipende kuongozwa na hasira katika jambo kama hili nimekwisha

    kueleza Michael hausiki na mauaji haya"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Una maana huyu askari alikuwa anamuonea wivu Beatrice? huyu askarialikuwa ananitaka? mbona mimi nilikuwa simjuhi?"

    Vanessa alicheka kwatuo na kunyanyuka kisha alitembea taratibu mpaka

    mlangoni akafungua mlango na alipokuwa akirudi ndani, alikuwa

    ameushika mkono wa baba yangu. Sikuweza kutambua chochote lakini

    nilibaki na mshangao nilipomuona baba yangu ni mzima na mwenye afya

    ukiacha kiasi cha siku mbili nyuma alipokuwa akitembelea magongo.

    Vanesa alimkaribisha baba katika ile meza yetu maongezi yakaanza mara

    nilipomsalimia baba

    "Ramon baba yako ana mengi ya kukueleza ndio maana

    sikuwa na sababu ya kukueleza yote kuhusu nilichogundua ila huyuatakueleza kila kitu"

    Vanessa aliongea yake na baba alikohoa kama anayeitafuta sauti yake,

    mimi nikabaki njia panda nikimtazama baba na kisha Vanessa alikuakitabasamu.

    "Kuna nini?" Niliuliza"Mwanangu" Baba akazungumza "Nilikueleza nitakapopata nguvu ya

    kuzungumza nitakueleza muuwaji wa msichana wako(Beatrice)"

    Baba akaanza kunihadithia kila kilichokuwa kikiendelea hapo nyuma

    mambo mengi ambayo nilikuwa mimi siyafahamu.

    HAPA NAKUHADITHIA KILE AMBACHO BABA ALIKUWA AKINIELEZA.

    Ilikuwa ni baada ya miezi miwili tangu niingie pale chuoni nikiwa

    tayari nimeshazoeana na Michael, Beatrice akawa mpenzi wangu. Katika

    muda ndipo kipindi ambacho hatukuwa na mahusiano ya karibu na Michael,

    tuligombana kwa sababu ya Beatrice. Mama aliwahi kuja chuoni na

    kuniulizia kwa watu. Sehemu ya watu aliowauliza, wakamuonesha Michael

    aliyekuwa akipita kwa mbali na wakimwambia mama kuwa yule ndiye rafiki

    yangu na labda amuulize yeye wapi nilipo. Mama alimuita Michael na

    kuniulizia, Michael akamuelekeza wapi angenipata kwa muda huo. Ni siku

    hiyo ambayo Mama alinikuta tukiwanaBeatrice darasani tunataniana huku

    tukifurahi pamoja. Nilimtambulisha Beatrice kwa mama na mama alifurahi

    sana kumuona Beatrice. Maisha yakaenda na mara niliporudi nyumbani

    baba akaniuliza swali"Mama yako ameshakuja chuoni kwenu mara ngapi?"

    "Mara moja"Nilimjibu hivyo na kwenda zangu nje chini ya mti fulani wa mwembe

    uliokuwa ukitoa kivuli safi. Hapo chini ya mti nilimkuta mama amekaa

    mkekani akifuma vitamba vyake vya makochi kwa sindano ya mkono

    "Oh Ramon! njoo ukae"Nikakaa, mama akaniuliza"Hivi yule kijana Michael anakaa wapi?"

    "Hapana mama sifahamu" Nilimjibu mama bila kutilia manani maswali yake

    "Anaonekana ni kijana mzuri aliyetulia kwanini humkaribishi mwenzio

    apajue kwenu?"nilizisikia hatua za mtu ajaye pale tulipo na mara nikafahamu kuwa ni

    baba mara alipozungumza"Kwanini Michael?" Baba hakukaa aliendelea kusimama, sasa akiwa mbele

    yetu "mbona hukuwahi kuwaulizia rafiki zake wengine na sasa iwe

    Michael?"

    Nilimuona mama akisonya na kujinyanyua pale mkekani na kishaaliondoka. Ni hapo nilipoanza kuona tofauti kati ya mama na baba. Mama

    alionesha kumpenda Michael lakini baba alimpinga sikujua yote hayo

    sikujua chochote kwa kuwa nilikuwa nikiwekwa mbali na ukweli. Siku za

    kukaa nyumbani zilipokwisha nikarudi chuo.. Ndipo siku moja baba

    alikuja chuoni na kunieleza kuwa haupendi ukaribu wangu na Michael, Mimi baba alinishangaza kwa kuwa ukaribu huo hatukuwa nao.

    "Baba mbona mimi sipatani na Michael kwa sababu ya Beatrice!"

    Nadhani hakuniamini baba akaniambia kuwa mara nyingi mama alipokuwa

    akitoka kunitembelea alipokuwa akimuaga baba, alikuwa akimzungumzia

    sana Michael kuliko mimi. Niliingiwa na wasiwasi nikamuuliza

    "Kwani mama amekuja mara ngapi chuoni kwetu?"

    "Ni zaidi ya mara tatu, kwanini wakati ni wewe ndiye alikuja kukutembelea?"

    "Mnh hapana baba, mama nimemuona chuoni mara moja tu"

    Nilieleza ukweli kwa kuwa nilianza kuwa na mashaka ili nisijiingize

    mahali pabaya. Basi baba akanieleza kuwa ni zaidi ya mara tatu alikuwa

    akiaga nyumbani kuwa anakuja kunitembelea chuoni. Mimi nilishituka

    sana kwa kuwa sikuelewa sababu ya mama kumdanganya baba kuwa anakuja

    kunisalimia na alikuwa haji.

    "Alikuwa anakuja kukutana na Michael"

    Baba alizungumza kwa uchungu na nilielewa uchungu alio nao, nikataka

    kumjaribu baba"Lakini baba kuna umuhimu gani wa kunieleza haya yote kuhusu Michael

    na mama leo wakati huu ikiwa nina kesi ya kumuua Beatrice?"

    nikamgeukia Vanessa na kumuuliza kwa hasira "Na wewe unakaa kaa hapa

    ukitabasamu bila kumueleza baba kuwa ninachohitaji ni kujua ukweli wa

    mauaji ya Beatrice, nani kamuua Beatrice ndicho ninachohitaji kusikia

    nahitaji kukijua kwa sasa na si hadithi ya Michael na mama"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Ndipo naelekea"Nilimgeukia baba baada ya kuzungumza hayo na kumsikiliza alikuwa

    anamaanisha nini. Baba akaendelea

    "Japo unasema mlikuwa hampatani baadae nadhani mlikuja kuwa marafiki

    kwa kuwa alikuwa anakuja nyumbani nawe"

    "Ndiyo kwa hiyo"

    "Mama yako na Michael walikuwa wapenzi"

    "Wapenzi?" nilihamanika. Vanessa alitingisha kichwa huku tabasamu

    liking'ang'ana katika papi zake. Niliumizwa na taarifa hizo lakini

    bado sikuwa nimeelewa chochote. Baba akaendelea

    "Mama yako alimpenda Michael japo Michael alionekana hampendi mama

    yako. nilikuwa nikimsikia mama yako mara nyingi akimlalamikia Michael

    kwanini anapoteza pesa nyingi kwake na yeye akawa hampendi. Mara

    kadhaa pia nilikuwa nikimsikia akilalamika kuwa atamkomesha huyo

    Beatrice anayemfanya Michael asimpende yalikuwa ni mabishano

    yaliyotokea wiki moja kabla ya mauaji ya Beatrice hayajatokea, siku

    chache baadaye aliweka kikao na watu ambao kwa mimi sikuwahi kuwaona

    watu wale pale nyumbani hapo mwanzo, mmoja wa watu hao alikuwa ni huyu

    askari wa kike. Nilifuatilia kwa umakini bila wao kujua chochote kama

    nilikuwa nikiwafuatilia maongezi yao yalikuwa yakinishangaza maana mara nyingi walikuwa wakimtaja Beatrice sikuweza kukueleza mapema kwa kuwa nilidhani kuwa ningeidhibiti hali ile mwenyewe lakini nathikitika kuwa nimeshindwa mpaka Beatrice amefikwa na mauti”

    Nilihisi ni kama utani ama ndoto ambayo nilikuwa nikiota na labda ninakaribia kuamka. ‘Ina maana baba anamaanisha mama ndiye muhusika wa mauaji ya Beatrice?’ nikajiuliza kwa uchungu huku machozi yakinitoka. Nikauinua uso wangu na kumtazama baba, baba pia alikuwa akinitazama mimi kwa uso wa upole. Nikamuuliza “una maana mama ndiye muhusika wa mauaji ya Beatrice?” baba akatingisha kichwa kwa kukukubali kile ambacho nimemuuliza. Nikahisi nachanganyikiwa kiukweli ni hali ngumu niliyokuwa nayo kwa wakati ule na hata sikuwa na uwezo wa kuendelea wa kuwasikiliza tena na hivyo mahojiano yalikatishwa huku Vanessa akiniahidi kuwa atakuja siku ya kesho ili aweze kunieleza mengi ambayo bado nilikuwa sijayafahamu mpaka kwa wakati huo.







    Haikuwa rahisi kuelewa ni vipi Bella amehusika na mauaji ya Beatrice. Sawa Bella alionekana kuyajua mengi kuhusu kesi hii sasa ni vipi alihusika? Sijawahi kumuona hapo kabla japo baba anadai kuwa aliwahi kumuona akija pale nyumbani lakini ilikuwaje achukue uamuzi wa kumuua Beatrice akiwa yeye ni askari? Nilihisi nazidi kuchanganyikiwa kwa kuwa sikujua pia mama yangu alihusika vipi na kwanini amuuwe Beatrice.

    Kila nilichokitazama katika nyumba hiyo mara baada ya vanessa na baba yangu kuondoka, niliona kama namuona askari yule wa kike, Bella. Nilijiuliza mengi kiasi kwamba nilianza kuelewa kiasi au sehemu ya mambo yalivyokuwa yakienda. Nilianza kuelewa kuwa kulikuwa na uhusiano fulani kati ya mama yangu na yule askari. Niliikumbuka ile siku ambayo mama alikuja na yule askari alimuita pembeni na hivyo walizungumza jambo ambalo mama alisita kunieleza kile ambacho alitaka kunieleza, labda huenda kilihusiana na Michael. Nakumbuka siku ile ndiyo ilizidi kuniongezea hisia kuwa huenda ni Michael alihusika katika mauaji ya Beatrice.

    Nilirudi katika chumba changu nikakuta sahani iliyojaa vipande vya mikate vilivyopakwa siagi ya karanga na kikombe cha maziwa. Bila shaka ni Bella aliyeniandalia. Nilikunywa chai ile pale huku nikiwa na mawazo lukuki kichwani mwangu. Machozi yaligoma kutoka kwa kuwa ilikuwa ni kama nimekumbwa na taharuki ama ugonjwa ambao si rahisi kuuelezea. Nikakumbuka mara kwa mara jinsi ambavyo mama alikuwa akimuulizia Michael na kushindwa kuelewa sababu ya msingi yeye kufanya uchafu wa namna ile na mtu tuliyelingana umri tena akiwa sawa na mtoto wake yaani mimi. Kipande cha kwanza niliweza kukimaliza lakini sio cha pili nilichohisi kikinikaba koo kwa uchungu ulionikumba. Niliiacha chai ile na hapo machozi yakaanza kunibubujika kwa uchungu. Siku hiyo sikuoga nilishinda nikilia siku nzima mpaka nilipohisi nikishikwa begani na mikono iliyo laini sana. Nilipoinua uso wangu kumtazama yule aliyekuwa akinitazama, alikuwa ni Vanessa akiwa amejawa na hudhuni na uso wake ukionesha utulivu wa hali ya juu. Alikuwa amerudi mara baada ya ujio ule wa asubuhi akiwa na baba

    “Pole sana Ramon” akanyamaza huku akiwa ameinama na kunipatia kitambaa cha kujifuta machozi, akaniambia “kesho utatoka na kuwa huru kwa dhamana baada ya Oscer kuondoa vipingamizi vya dhamana yako lakini hii inatokana na asilimia themanini ya ushahidi kukamilika na sehemu ya wahusika wa mambo haya kukamatwa na kusekwa mahabusu. Hutaruhsuiwa kuzungumza chochote kwa mtu yeyote ili usiharibu taratibu za upelelezi. Yangu ni hayo na kesho nitakuja na baba yako kukuchukua mpaka nyumbani kwenu”

    “hapana sitaweza kukubali uondoke siku ya leo mpaka unieleze”nilizungumza kwa uchungu “unieleze ni vipi yule askari anahusika na mauaji haya huku mama yangu akihusika pia na mauaji haya. Kwa kuwa sielewi chochote sielewi yaani nazidi kuchanganyikiwa ni heri ningejua ni Michael aliyehusika lakini si mama yangu. Imekuwaje Vanessa?”

    Akanieleza jinsi ilivyokuwa mwanzo mpaka mwisho kwa jinsi na yeye alivyohadithiwa na kuelewa.

    YALIYOTOKEA KATIKA KIFO CHA BEATRICEhttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilikuwa ni wiki mbili zilizopita mama yake na Ramon akiwa amerudi mapema na rafiki zake akiamini kuwa mzee Lameck bado hajarudi kutoka kazini. Alikuwa ni yeye pamoja na washirika wake watatu mwanamke akiwa mmoja kati ya wale aliokuja nao ambaye ndiye Bella, askari aliyekuwa akiishi na Ramon katika nyumba ya Safe house kumlinda ili asitoe yote yale ambayo huenda alikuwa akiyafahamu. Hiyo ilikuwa ni kazi yake baada ya mambo kuharibika au kwenda tofauti na mipango ya kambi yao ya mauaji ya Beatrice. Wanaume wengine wawili waliobakia alikuwamo Moses aliyetoroka jela kipindi kifupi tu akiwa na kesi ya mauaji ya watu wengi wasio na hatia huku aliyebakia akiwa James mattaba kijana aliyetumwa kuipeleleza nyumba anayoishi Beatrice akijifanya kama muuza mchicha na magazeti kwa siku nyingine bila kushitukiwa na mlinzi wa Beatrice, Baraka. Kikao chao kilikuwa kina ajenda ya kumuangamiza Beatrice siku ambayo anavishwa pete na Ramon.

    “lakini mama kwanini unataka kufanya jambo hili ikiwa mtoto wako anampenda sana huyu binti?” Bella ndiye alihoji

    “kha! We vipi?” Moses aliropoka “acha ujinga, ni mara ngapi madam akueleze kuwa Michael ndiye sababu?”

    “kivipi?” Bella akahoji kiushabiki. Ubishani huo ukamshitua Lameck kule alipokuwa na kunyata taratibu kuelekea pale mlangoni karibu na ukumbini walipokutania kusikiliza maongezi yale. Mara akaisikia sauti ya mkewe

    “Sikia wewe mwanamke nafahamu kuwa Beatrice ni mpenzi wa mtoto wangu lakini Beatrice amekuwa akininyima usingizi kutokana na kulikosa penzi la Michael kwa muda mrefu sasa. Michael amekuwa na ugomvi na ramon tangu wakiwa chuo kwa sababu ya Beatrice na hata nikiwa nimeshamkanya mara nyingi sana kuwa aache mahusiano hayo na Beatrice akawa hanisikii kwa kuwa niliwahi kumkuta akibusiana na Beatrice nyumbani anapoishi Michael” Bella alishituka kusikia hayo na hakuongea chochote akabaki kuwa msikilizaji wa kila kilichopangwa. Moses ndiye alikuwa mratibu wa mchezo mzima baada ya kumsikiliza James jinsi ramani ya nyumba ile na muda ambao mbwa wa nyumbani kwa Beatrice wanafunguliwa. Mpango ulisukwa vyema na hivyo mauaji yale yalipangwa kutekelezwa na james akishirikiana na Moses pamoja na Bella.

    Dakika chache mara baada ya Ramon kumuacha Beatrice pale pale getini, hakutambua kuwa kulikuwa na watu watatu waliokuwa wakitambua ujio wao huku wamejibanza katika giza zito nyumba nne kutoka pale walipo wao. Watu hao walikuwa ni Moses, Bella pamoja na James waliokuwa wakiwasiliana muda wote na mama yake Ramon ili kutambua muda gani Beatrice atatoka katika sherehe ile.

    Katika mifuko ya Moses, kulikuwako na chupa yenye kilevi kilichotiwa sumu kali ya kukausha maini huku akiwa ameviweka visu vinne vyenye makali kote kuwili kwa ajili ya mauaji. Kiunoni mwake akiwa amepachika bisu kubwa la kimasai aina ya sime. Bella alikuwa ameshikilia nyama kilo tatu alizozikata kwa vipande vipande huku akiwa amepakaza sumu pia kwa ajili ya kuwatupia mbwa wale. James hakushika chochote James alikuwepo pale kwa kazi maalumu.

    “Dogo ndiyo anasepa sisi tunaingia” Moses akatuma ujumbe kwa mama yake Ramon akajibiwa “kuweni waangalifu”

    Jambo la kwanza kufanywa kabla ya kuingia ndani, ni kuzima umeme wa zile kamera ambazo ni James pekee alijua kamera nne zilizopachikwa kwa ajili ya ulinzi wa nje tu na jinsi ya kuzikata nyaya zake. Baada ya kufanya hivyo kwa kitendo kisichozidi dakika kumi. James mwenyewe tena, ndiye aligonga getini. Baraka mlinzi aliyevalia sare za ulinzi kutoka Jinja Security, aliuliza kwa lafudhi ya watu wa shinyanga(sukuma)http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nani?”

    “James yule muuza magazeti kaka”

    Hakuwa na wasi juu ya kuulizwa amefuata nini usiku wote huo kwa kuwa asubuhi ya siku hiyo alimpitishia magazeti na akawa ameisahau chenchi yake kwa makusudi kwa ajili ya faida ya baadaye. Hakuzisahau ndevu zilizokuwa zikimdanganya Baraka mara tatu alizokuja hapo akijifanya kama muuza magazeti na mara muuza mchicha. Wakiwa wamesimama pale nje, walimsikia Baraka akilalamika juu ya zile kamera ambazo haziwaki

    “haya ngoja nakuja ndugu yangu”

    Ujinga alioufanya mlinzi yule mweusi na mfupi wa kimo, ni kufungua geti dogo lililomruhusu Moses kummwagia pombe ile yenye kilevi kidogo sehemu ya usoni Baraka na hivyo alipovuta tu kimiminika kile cha baridi hakuweza kupiga kelele wala hatua alizojaribu kutaka kupiga kwa hofu aliyokumbana nayo kwa kushuhudia watu watatu asiowafahamu usiku wa saa nane kama ule. Akiwa bado anaipigania roho yake pale chini alipoanguka, Bella akawa amekwishawarushia mbwa wale yale mapande ya nyama huku mbwa hao wakali wakiyafakamia kwa uroho bila kujua kuwa ndani yake kuna sumu iliyowafanya wanyong’onyee mithili ya mlenda na kunguka chini mmoja mmoja kama kuku mwenye kideri. Ukimya uliokuwepo nje ukamtisha Beatrice kwa kuwa bado hakuwa hajapitiwa na usingizi. Na kwakuwa alikuwa na shida ya kumuuliza jambo Fulani Baraka, akaipiga ile simu ya mezani ambayo iliita tu na haikupokelewa, akahisi hali ya hatari, ndipo kwa wakati huo alimpigia Ramon. Ramon naye hakupokea simu kwa wakati ule kutokana na usingizi uliokolezwa na wingi wa pombe alizokunywa akatika sherehe.

    Beatrice akafanya kosa la kufungua mlango na kukutana na mtu mrefu tofauti na Baraka anayemjua yeye, akaita kizembe “Baraka” hakuitikiwa kwa kuwa hakuwa yeye bali kimiminika kile chenye kilevi lakini chenye sumu kali ya kukausha maini akarushiwa na kuivuta sumu ile iliyomo ndani yake. Kilevi kile kilikuwa ni pombe ya kawaida tu lakini iliyochangwa na sumu kali ili kuupoteza ushahidi, ilitengenezwa na Moses. Beatrice alianguka chini na kuishiwa nguvu mara baada ya kuvuta kimiminika kile cha hatari.

    James akiwa amekishika kiwiliwili cha Baraka kilichotenganishwa na kichwa chake huku damu nyingi zikiwa zimemtapakaa mikononi mwake, ndipo alishika pale ukutani na alama ya kiganja chake kutokea karibu na mlango wa kuingilia ndani kwa Beatrice. James akishirikiana na Bella walimburuza Baraka mpaka kilipo chumba kilichofanyika kama stoo ndani ya nyumba ya Beatrice na kumuweka huko.

    Moses alikuwa akiendelea kung’ang’ana na mwili wa Beatrice kuuingiza ndani ya chumba chake huku akiwa ameshamkata sehemu ya koromeo lililokuwa likivuja damu nyingi, ndipo Bella alipomsaidia kwa kumbeba miguuni huku Moses kwa mikono aliyovaa gloves akiwa amemshika sehemu ya kichwani. Moses alikuwa makini sana katika kazi hizo labda huenda kwa kuwa alikuwa ni muuaji mzoefu lakini si kwa James na Bella walioacha acha ovyo alama zao za vidole kutambulikana hapo baadaye. Mara walipomlaza Beatrice sakafuni kwake katika chumba chake, akaumalizia uhai wa Beatrice kwa kulichomeka sime kubwa alilolipachika kiunoni mwake katika tumbo la Beatrice bila kutumia vile visu vine katika moja ya mifuko ya koti lake. Ilikuwa ni picha mbaya kuitazama na ndiyo aliyoikuta Ramon saa aliyokuja. Bella akaiona simu ya Beatrice pembeni ya kitanda, akawaza jambo kiaskari Zaidi. Mara baada ya Moses kutoka huku akimuamrisha waondoke haraka eneo hilo kwa kuwa ilikuwa ni usiku mno yeye akabaki nyuma kuichunguza simu ile ya Beatrice. Alifungua sehemu ya meseji hakukuta meseji yoyote ya kumgusa ila alipofungua sehemu ya simu zilizpoigwa simu ya juu iliyopigwa muda mchache uliopita ilikuwa ikipigwa kwenda kwa Ramon. Katika akili yake akaamini kuwa mambo yamekwishaharibika. Yeye pia akaona ni bora aharibu Zaidi tofauti na mpangilio wa jinsi walivyopanga. Akapanga kuirudisha kesi hiyo kwa mtoto wa bosi wake ambaye yeye ni kama rafiki yake. Akamtumia meseji ile Ramon mwenyewe iliyoandikwa kuwa “kwanini unaniuwa Ramon?’ akiamini huo ni ushahidi wa kutosha kumuingiza Ramon katika matatizo. Na ndivyo ilivyokuwa hapo baadaye mpaka alipodanganya wenzake kwa kuwatumia meseji akijifanya kuwa ni msamari mwema anayetoa taarifa za tukio la mauaji yaliyotokea huko mikocheni. Baada ya wao kutokomea alirudi nyumbani kwake akiwa anajiandaa kuitwa ofisini kwa ajili ya kwenda kumkamata mtuhumiwa wa mauaji ambaye ni Ramon.

    Mama yake na Ramon alikuja kuelewa kuwa lameck mumewe, amekuwa akimfuatilia kwa mambo mengi aliyokuwa akiyafanya. Alifahamu hata kuwa kifo cha Beatrice anakifahamu na hivyo aliwatumia watu wake kumuonya ili afunge mdomo wake asije kuitoa siri ile. Ni siku ile ambayo alivnjwa mguu na watu wa mama yake Ramon wakishirikiana na Moses.



    SAFE HOUSEhttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya kusikia hayo yote, nilizidi kulia huku nikiona dunia ni chungu na sistahili kuishi ikiwa mama yangu mwenyewe aliyenizaa ndiye aliyesababisha haya yote kutokea. Nilimuomba Vanessa aniache peke yangu kwa muda nipate nafasi ya kutafakari mambo mengi yaliyotokea huku nikiamini kuwa sina muda mrefu wa kuendelea kuishi. Vanessa akaniaga huku akinieleza kuwa

    “Michael pia amekamatwa huku ukitakiwa kwenda kutoa ushahidi kati ya mama na rafiki yako ni nani aliyemuuwa mpenzi wako”

    “vipi kuhusu mama yangu, amekamatwa pia?”

    “ndiyo”

    “sawa nakusubiri kesho acha sasa nikalale”

    Sikwenda kulala kama nilivyomuomba Beatrice aniache nikalale bali niliutumia muda wote wa usiku kuandika sehemu ya hadithi ya maisha yangu yaliyoniumiza kuliko yote. Nitawezaje kumtazama Michael ikiwa nimeshamshutumu kuwa ndiye muuaji ikiwa mama yangu ndiye aliyehusika na mauaji haya? Nitawezaje kumnyooshea bwana hakimu kuwa muuaji ni yule pale huku nikitazamana na uso wa mama yangu aliyenizaa baada ya kuniweka tumboni kwake miezi tisa tena kwa uchungu na kisu cha operesheni kikipanua njia yake baada ya mimi kushindwa kupita kwa hali ya kawaida? Hapana yanipasa moyo wangu uende na yule nimpendaye. Ninachoamini kuna maisha baada ya kufa kama ilivyoandikwa na mwandishi mashuhuri mwenye ujuzi wa pekee stallone joyfully katika kitabu chake cha msitu wa wafu. Kwanini nisiende kukutana na mpenzi wangu kuliko kuishi katika dunia ya dhuruma na manyanyaso kama hii ya kifedhuli? Namkumbuka Christian aliweza kukutana na Munira tena katika msitu ule, acha na mimi nife nikiwaachia kitendawili kiziro walimwengu ni vipi utathibitisha kuwa mama yako ndiye muuaji wa mpenzi wako Betarice eti kwa kuwa alikuwa anampenda rafiki yako? Mimi siwezi kusimama kizimbani ndio sababu ya kuchukua uamuzi huu. Siku ya leo jumapili ya saa 11 alfajiri ya mwezi wa saba tarehe nne ndio siku ya mwisho ya uhai wangu duniani. Mnisahamehe kwa wote niliowakwaza kwa uamuzi niliouchukua ila naiombe sharia ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ichukue mkondo kwa kila dhulumu ya haki iwe ya kuishi na yeyote iwayo ifuatwe kwa mujibu wa katiba ya nchi hii yenye Amani na upendo inavyosema.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MWISHO



    “Ramon alikufa kwa kujinyonga na shuka kukiwa na walinzi wachache waliopunguzwa kutokana na ushahidi kukamilika. Michael alichiwa huru mara baada ya kuthibitika kuwa mama yake Ramon ndiye aliyehusika na mauaji yale huku Bella na mama yake Ramon wakihukumiwa kifungo cha maisha jela ikiambatana na mateso makali. Moses na James hawakukamatwa.









     

NENDA NA MOYO WANGU - 4

 

     





    Simulizi : Nenda Na Moyo Wangu

    Sehemu Ya Nne (4)





    Nikaanza kulia kwa uchungu kwa kuwa nilihisi mambo yanazidi kuwa mazito katika kichwa changu. Unadhani ingekuwa rahisi kumsikiliza baba kuwa nisimuamini mama kwa atakachonieleza? Yaani mwanamke aliyeniweka tumboni kwake miezi tisa kisha akanizaa kwa uchungu? Hakika nilijihisi naukaribia uchizi. Yule askari wa kike akanieleza. "Michael ahusiki na mauaji nakusaidia kidogo ili usichanganyikiwe zaidi"



    Kisha akanipapasa kwa mikono yake laini akaondoka.

    "Huyu naye!?" Nikajiuliza, ina maana anamtetea Michael kwa kuwa anamjua muuwaji? Ina maana yeye ananifahamu basi kabla mimi sijakamatwa na kukutwa na kesi hii?



    "Ni nani mwanamke huyu?" Nikaanza kuingia katika uchunguzi wangu. Nikahisi kuwaza sana kichwa kitaniuma, wazo la mwisho ndio nililiona nafuu. Kumchunguza huyu askari wa kike.



    Nilikuwa na nia ya kumchunguza kwanza katika uhusiano wake yeye na mama yangu mzazi, kwa kuwa nakumbuka mara ya mwisho mama kuja alimvuta pembeni na kuna mambo walizungumza kwa siri, ni nini hicho walikuwa wakizungumza? Ndio nilitaka nianze hapo. Kwa kuwa mara baada ya mama kutoka pale aliondoka akiwa na haraka huku akiwa ameacha lile alilotaka kuanza kuniambia hewani na mwisho akilikana.



    Kisha nitataka kujua amenijuaje mimi na kujua mambo mengi yanayonihusu, si rahisi kwa askari wa kawaida ambaye si mpelelezi wa kesi yangu kugundua watu wanaonihusu. Ningeweza kumuhusisha na mauaji haya lakini kwa kuwa alikuwa na ukaribu na mama nilijua fika huenda mama alimueleza mengi nikataka kuyajua. Pia nikachanganya ile hali ya aksari kuja pale nyumbani kwa Beatrice nikazidi kusisimkwa na vinyweleo vyangu huku akili ikizidi kuwa makini na yote yaliyokuwa yakiendelea.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kisha alionekana kuvutiwa hivyo nilifahamu fika isingekuwa shida kutumia hila zangu katika udhaifu wake kumpata na kumteka kimapenzi na kisha atanieleza mengi. Nikaingia katika njama za kumpeleleza askari yule wa kike. Nikarudi zangu mahabusu nikimsubiri aniletee chakula cha usiku. Saa 2:14 haikuwa mbali na wakati niliusubiri akawa anaingia amebeba sinia lenye sahani ya chakula. "Leo kuna ugali, kisamvu na samaki"



    Akaniambia huku akiweka sinia lile chini mbele ya meza yangu. "Ahsante nitakula"

    Nikamshika mkono kwa minajiri ya kumpapasa nikiwa nimeanza rasmi kuingia kazini kujua ni kitu gani anafahamu.Mpapaso muruwa wa mikono yangu laini hakika ukamchanganya yule askari wa kike. Niliona akilegea na kunitazama kwa jicho la huba. Zilidumu sekunde kadhaa kisha akauputa mkono wangu akaropoka.



    "Niache, usithubutu tena kufanya hivyo nitakushitaki" Akaondoka huku akiwa ametazama uso wake juu sehemu zilipo kamera za ulinzi wa eneo hilo. Nikaelewa kwanini hata uso wake haukonesha ile hasira aliyoiigiza. Nikajipa moyo siku bado zipo

    Siku iliyofuata aliniletea gazeti lenye kipande cha karatasi ndani yake. Sikuweza kujua mwanzo sababu ya kunitupia gazeti lile, aliponikonyeza nikakionana kikaratasi kilichoanguka.

    Kiliandikwa hivi

    "Hii si sehemu sahihi ya mimi na wewe kuwa kama unavyotaka iwe. Jitahidi kucontrol hisia zako ili wasishitukie chochote wakubwa"

    Nilipomaliza nikatabasamu na kukikunja kunja kipande kile cha karatasi nikakitupia mdomoni. Yule askari wa kike aliona nilichokifanya akatabasamu kule alipo na mimi nilimuona pale nilipo. Tabasamu langu lilikuwa la kikebehi kwa kuwa huenda hakutambua kua mimi sikufanya vile kwa lengo la kimapenzi bali kumchimba nipate kile alichokuwa akikificha.

    Majira ya saa saba mchana alinijia tena yule askari wa kike akiwa ameongozana na Michael, walinikuta nikiwa nimekaa kwenye makochi ya sebule ya nyumba ile nikitazama kipindi cha Tusker project fame. Nilitabasamu nilipomuona Michael lakini yeye uso wake ulikuwa wenye huzuni na hasira iliyoambatana nayo.

    "Karibu"

    "Siamini kama umeona unisingizie upumbavu wako"

    "Una maanisha nini?" Nikamuuliza Michael kwa kuhamanika kiasi.

    "Ina maana si wewe uliyemuelekeza yule malaya(akimaanisha Vanessa) nyumbani kwangu? Amekuja kuniuliza na kunishitumu kuwa mimi ndiye muhusika wa mauaji ya Beatrice, ina maana Ramon umedhamiria kuniangamiza? Kweli?"

    Nikacheka kwa kebehi na wala sikuona kama Michael alikuwa hana hatia, macho na uso wake huku sauti yake ikimtetemeka ilionesha dhahiri ni kiasi gani alikuwa akificha jambo alilojitahidi kulificha lakini alishindwa kutokana na uoga.



    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Sina cha kukuambia lakini sheria itafuata mkondo wake na ukweli hautajificha"

    Akaniambia jambo lililonishangaza "Laiti kama ungemjua muuaji, usingethubutu kunipakazia ujinga wa namna hii ninachopenda kukuambia kuwa usitamani kumjua muuaji wa mpenzi wako maana hutatamani kumuhukumu na wala hutatamani kuishi"

    Akanyanyuka na kuondoka huku maneno yake yakaja kufanya kazi baada ya siku ishirini na moja. Siku ya leo nikiwa naandika barua hii huku nikiwa nimemjua muuaji wa Beatrice na kweli dakika chache baadaye na dhamiria kuitoa roho yangu nikapumzike na Beatrice. Inauma! Inauma sana...

    "Basi tuendelee wewe ukisoma barua hii yenye kisa cha kweli kwa mtiririko sahihi ili hadithi ya mambo mabaya kuliko yote niliyowahi kuyapitia yasikuchanganye" Ikabidi niwe mpole mara baada ya Michael kuondoka. Yule askari wa kike akanijia akiwa amepishana na Michael pale mlangoni alipokuwa anaingia na Michael akitoka.



    "Huyu rafiki yako vipi? Mbona ana hasira hivi?" Alikuwa amesimama wala hakutaka kukaa karibu yangu. Nikaona uso wake kama wenye kunipa ujumbe fulani lakini sikuutambua. Ikabidi nimuulize swali.

    "Unaitwa nani?"

    "Jina langu wewe la nini?"

    "Unadhani najisikia vizuri kuishi na mtu nisiyemfahamu? Kwanza huna kwenu?" nikamtazama kisha nikaendelea "maana haiwezekani wewe ushinde na mimi tu kila siku na sikuoni ukienda kwako ina maana wewe hujaolewa" Yule askari akacheka kisha akanijibu huku nusu akicheka nusu akijitahidi kutaka kuongea

    "Naitwa Bella"

    "Bella!? Yule msichana aliyezungumza na shetani?" Yeye akacheka zaidi na mimi nikatabasamu tu, akanijibu "kile ni kitabu tu cha kubuni hakina uhalisia wowote. Unadhani ni rahisi kuzungumza na lucifa? Utazungumza na pepo wake lakini sio yeye mwenyewe bwana" Nikaona uelekeo wa kuelewana na huyu askari sasa ulikuwa mzuri, nikafurahi kumfahamu kuwa anaitwa Bella.

    "Ni jambo zuri kukufahamu, acha nikalale"

    "Haya usiku mwema" Nikamuacha mimi nikaelekea zangu kulala.

    Asubuhi iliyofuata niliamshwa na moshi wa sigara uliokera pua yangu, ile kuamka tu nikakutana uso kwa uso na yule mpelelezi Jafari Hiza.

    "Za siku nyingi?" Kwa mang'amung'amu huku usingizi bado ukiendelea kung'ang'ana katika macho yangu nikaitika huku nikipikicha macho kutoa tongotongo.

    "Salama habari yako"

    "Nimekuja kuzungumza na wewe muda wa kuchezeana akili na kuulizana kuhusu habari umepitwa na wakati jiandae kisha kuna chumba utaletwa mimi nitakuwepo huko nakusubiri"

    Akatoka akiwa ameizima sigara yake pale mlangoni aliposimamiahuku akiwa aaisaga kwa kisigino cha mguu wake. Wakaja askari wawili kutoka nyuma ya mgongo wake na kunifunga pingu, Bella akaingia.

    "Naomba kuzungumza naye" Wale askari wawili hawakuzungumza chochote wakaniacha kisha walitoka wakiniacha mimi na Bella katika chumba kile cha mahabusu.

    "Unajua unapoenda?" Bella akaniuliza uso wake ukionesha wasiwasi.

    "Sio katika chumba cha mahojiano?"

    "Ni cha mahojiano lakini si kile ulichokizoea huko kuna hatari zaidi ya uijuavyo hatari yenyewe. Jitahidi kila neno ulilokwishazungumza usilibadilishe zaidi ya kuliongea lile lile ulijualo"

    Hofu ikanikumbatia na kunipa joto kiasi cha kunitoa jasho. Bella akatoka na kuwaita wale askari wawili waliondoka mwanzo na kunifunga ile pingu ya myororo, wakanipeleka katika chumba fulani hivi. Huko wakanivua shati nikabaki kifua wazi na kukalishwa katika kiti ambacho sikufahamu hapo mwanzo sababu ya kuletwa hapo licha ya kujuwa kwa kuambiwa kuwa ni chumba cha mateso.

    "Leo utaeleza ukweli" Jafary Hiza akazungumza huku wale askari walionileta ndani ya chumba hiki nilichokuwa nikikiogopa, wakinifunga kwa kukaza kamba zao miguu yangu na mikono kwa kuniunganisha na kiti kile.

    "Mfungeni vizuri asilete shida baadaye" Niliisikia sauti kutoka nyuma ya mgongo wangu huku mlango ukiwa unafungwa. Jafary hiza akawa anatabasamu kwa kebehi akimtazama mgeni huyo aliyeingia kwa sasa. Nilipogeuka kumtazama alikuwa ni Oscer Valerian, baba yake Beatrice. Yeye akanitazama kwa dharau zaidi.

    "Kwanini mnanifanya hivi?"

    "Kwa kuwa wewe ni muuwaji na unastahili kuuwawa" Mapigo yangu ya moyo yalikuwa yakienda kasi kuliko kawaida ya mapigo yake. Nilitamani kulia lakini sikuona sababu ya kulia mbele za watu wasio na huruma.

    Mbele yangu askari wale wakaleta vifaa ambavyo sikuvifahamu kazi yake, Jafary hiza akainua kifaa kimoja kinachofanana na bisibisi na kukifunua na kubana sehemu ya chuchu zangu.

    "Nitakuuliza na utajibu niliochokuuliza" Nikiwa naugulia maumivu, niliuma meno huku nikiitikia kwa kichwa kwa kumaanisha kukubali.

    "Yule msichana alikukosea nini?" Hapo alipunguza ukali wa kukibana kile kifaa huku Oscer akiwa pembeni ya Jafary hiza akitazama kila kinachoendelea.

    "Hatukuwahi kugombana hata siku moja" nikasema na alipobana tena nikapiga kelele "ayyyy!!!"

    "Sasa inawezekanaje ukamuua kinyama kiasi kile? Ulirukwa na akili?"

    "Mimi.. Mimi sifahamuuuuu yalaaaaaaa!!"

    "Kwanini umeuwa pumbavu!" Oscer alizungumza kwa hasira na kuninasa kibao. Jafary hiza akahama kutoka kwenye chuchu zangu na kuhamia kinywani.

    "Nitakung'oa meno usipowataja washirika wenzako wengine mlioshirikiana kumuuwa Beatrice na kusema sababu ya kumtoa roho yake"

    "Kwanini mnamchelewesha? Hana anachoeleza yeye na mpuuzi mwenzake Michael lazima damu ya mwanangu ilipwe" Oscer alifoka kwa hasira.

    "Nipo tayari kufa kama mmekosa imani nishamkabidhi Beatrice moyo wangu muda mrefu na kufa kwake kunanishangaza hata iweje moyo wangu bado unafanya kazi nifanyeni mtakacho kama mnadhani mnatenda haki"

    Kisha kilichofuata sikukitambua kutokana na lile lililofanyika ghafla bila kutarajia. Niliona giza zito likitanda mbele yangu na kila kiungo changu cha mwili kikikosa nguvu. Kumbe kile kiti nilichokalia kina umeme na swichi yake iliwashwa na Oscer mwenyewe, nilimuona nilipokuwa nikifunga macho taratibu huku nikijaribu kupambana na hali ile. "Nakufa!? Hapana siamini sio sasa, bado sijamaliza kuandika bado sijamjua muuwaji kwanini nalala? Sitaki kufa sasa hivi" nilijisemea hivyo na kisha nikapokelewa na usingizi.

    Nilipofumbua macho yangu kwa mara ya kwanza kitu cha kwanza kukiona mbele yangu anha! Hapana ulikuwa ni uso ulionitazama kwa chini ulipo uso wangu mimi nikimtazama juu ulipo wake.

    "Baba"

    nikaita kwa sauti ya utulivu na kavu bila shaka.

    "Pole sana mwanangu utapona" Kitendo cha kupewa pole kutokana na kukumbuka kuwa nilipigwa na yule askari Jafary Hiza akishirikiana na Oscer Valerian kuniadhibu, roho yangu iliniuma na kuanza kubwabwaja "Acha waniue baba acha nife kwa ajili ya Beatrice najisikia fahari kufa kwa ajili ya Beatrice. Nimemkabidhi yeye moyo wangu hawezi kuondoka mpaka na mimi nife acha baba"

    Niliongea maneno ya uchungu kiasi kwamba mimi na baba tulilia kama watoto pale wodini. Pia nikaona kitu ambacho kabla sijaendelea sana na mtiririko wa kisa hiki nisije nikasahau kukueleza, nilishangaa kumuona baba akitembelea gongo huku hali yake ikionesha kuwa ni dhaifu sana, nikahisi anaumwa au amepata ajali. Nikamuulizahttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Baba unaumwa?"

    "Hapana mwanangu" Sauti yake ikakaa mbali na ukweli mara nikahisi kitu kikubwa kimejificha ndani ya nafsi yake. Sikuking'amua wakati huo ambao na mimi nilikuwa katika matatizo ni mpaka hapo baadaye alipokuja kunieleza mkasa mzima ambao sikuwa nikiujua hapo mwanzo. Lakini kabla sijafika huko ambako ndiko mwisho wa story hii nikueleze tu kuwa baba alipigwa na watu waliohusika kumuua Beatrice wangu, kwa kipindi hicho ambacho nipo hospitalini, sikuweza kujua kwa kuwa hakunieleza chochote.



    "Baba kuna kitu unanificha" nikamdodosa nikijaribu kumkazia macho kwa ukali kidogo.

    "Kila kitu kina wakati wake utakuja kuelewa baadaye mwanangu pole kwa mateso yote unayoyapata"

    "Ahsante baba lakini mbona unafahamu mengi ambayo hutaki kunieleza?"

    "Nikikueleza yote sasa nitakufa! Subiri nipate nguvu ya kupambana"

    Nilishituka na kushangazwa sana sikutaka baba afe kabla hajanieleza ukweli nikanyamaza kimya nikimtazama kwa kustaajabu. "Unataka nikueleze sasa? Nipo radhi kufa kwa ajili yako?"

    "Hapana baba, bado nakuhitaji" "

    "Basi subiri muda utakapofika" Baba akaniambia, kisha aliingia Vanessa pamoja na daktari aliyevalia joho jeupe la kiuuguzi. "Du ana bahati sana. kuzimia siku mbili kutokana na shoti ya umeme?nilidhani angekufa. Ana maisha marefu sana huyu kijana" alisema yule muuguzi na kunichanganya zaidi.

    'Ina maana mimi nililala hapa kitandani siku mbili mnh!!' Nikajiuliza kwa wasiwasi nikimtazama baba kisha Vanessa aliyekuwa akitabasamu nikamgeukia yule muuguzi akiwa anafunga dripu mpya ya maji.

    "Umepona wewe ni jasiri mwenye nguvu" muuguzi yule alinieleza maneno ya kunitia nguvu kiasi nikafarijika. Baba akaniaga "Nitarudi tena siku nikipata nguvu zaidi"

    "Njoo mapema kabla hawajaniua baba"

    "Hauwezi kufa mpaka uijue haki yako" baba akaondoka mimi nikamtazama mpaka alipoishia. Yule muuguzi akamfuata nyuma baba yangu nikabaki mimi na Vanessa.

    "Hapa ni hospitali ama wapi?"

    "Safe house" Vanessa akanijibu kiuwepesi.

    "Ina maana hii nyumba ni kubwa hivi? Nilidhani ni hospitali"

    Vanessa akacheka hakunijibu jambo. Akakaa pembeni yangu akinipa pole kwanza na mimi nilipoitikia mahojiano mafupi yakaanza tena hapo hapo nikiwa kitandani mara tu baada ya kutoa ile tepurekoda yake.

    "Nilikutana na Michael" aliniambia huku akiitengeneza tepurekoda yake.

    "Alinieleza na kunijia juu sana kwamba kwanini nimemchoma kwa mpelelezi kuwa yeye ndiye anahusika na mauaji"

    "Inawezekana akawa ama asiwe bado kuna utata"

    Nikamtazama Vanessa kwa mshangao mkubwa macho yakinitoka pima na kuanza kunichanganya upya. 'Iweje Vanessa naye abadilike sasa na kuwa upande wa Michael'

    "Sipo upande wa Michael" ni kama kwamba aliweza kuyasoma mawazo yangu, akaendelea "Nilipomuhoji Michael sikuona hatia katika maelezo yake lakini sitaki kuthibitisha ni hakika kuwa hajahusika ila uchunguzi bado unaendelea lakini nilipochukua alama za vidole vya Michael havikurandana na vile vilivyokutwa katika mwili wa Beatrice. Sifahamu nini sababu au nini kimetokea lakini Michael hakuna kidhibiti cha kumuhusisha na mauaji yale hivyo bado uchunguzi unaendelea huku utata mwingi ukiendelea kugubika mauaji haya"

    "Kivipi"

    "Kuna alama nyingine ya vidole tulipozipima na vyako vimeshabihiana kwa asilimia tisini hivyo unaendelea kuwa muuaji namba moja uliyeshirikiana na wenzako katika kutekeleza jambo lile. Hutapelekwa mahakamani mpaka uchunguzi utakapokamilika. Jopo la wapelelezi nikishirikiana nao pia tumepewa siku kumi na nne tu kukamilisha zoezi hili kuanzia leo nasubiri ukipata nafuu niweze kuendelea kukusikiliza maisha yako kwa ujumla na Beatrice ili niweze kuangalia ni nani mwingine ambaye anaweza akawa amehusika na mauaji yale"

    Nikashusha pumzi nzito kwa kuwa niliyaona maji shingoni mwangu. Sikuwa na jinsi sasa maana hata tumbo nilihisi likinguruma kwa uoga huku nikitoa hewa chafu kwa mbali. Vanessa akanyanyuka na kuniaga huku akinieleza "Sasa ni saa 4 na dakika ishirini asubuhi nitakuja saa 12 jioni kuzungumza na wewe kwa kuwa hatuna tena muda mrefu wa kukaa na kuzungumza"Wakati Vanessa ametoka hazikupita dakika nyingi na Bella akawa ameingia. Aliingia akiwa amebeba chupa ya maji makubwa ya kilimanjaro na hotpot la kuhifadhia chakula. Alipolifunua, kulikuwako na vipande vya nyama ya kukaangwa na wali hotpot la pili kulikuwa na mchuzi wa maharage.

    "Umeamini sasa nilichokuwa nikikueleza?"

    "Nini?"

    "Kuhusu Michael!"

    "Anha! Mi nachanganyikiwa tu hata sielewi"

    "Unaonaje ukisikia muhusika ni baba yako?"

    "Unasemaje?" Kiukweli nikahamanika kwa jambo hilo aliloniuliza. sidhani kama kipo ambacho kingetokea na kunifanya niamini kuwa baba au mama yangu anaweza akahusika na mauaji.

    "Haiwezekani" nikasema huku nikikaa vizuri "baba yangu hawezi kumuua Beatrice"

    Bella akacheka kwa kebehi na kunieleza. "Ngoja nikupe kama hadithi tu ya kubuni halafu upime maelezo yangu na uchambue utakavyoweza. Lakini huu ni msaada mdogo tu ninaokupa usinihusishe kama shahidi katika kesi yako" aliniambia hivyo huku mimi nikiwa nimelala nikabaki kimya kumsikiliza.



    "Mama na baba yako wamekuwa na ugomvi wa mara kwa mara"

    "Ndiyo ni kweli" nikamjibu.

    "Baba yako amekuwa akiuchukia ujio wa Michael nyumbani kwenu na mara kwa mara amekuwa akikuambia usimuamini mama yako kwa lolote atakalokueleza"

    "Ndiyo" nikaendelea kumjibu.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kwanini baba yako amekuwa akificha mambo kwa visingizio kuwa atauwawa"

    "Nini?" Nikaanza kuingiwa na wasiwasi. Huyu Bella amejua mambo mengi sana yanayonihusu mimi na familia yangu amejuaje yote hayo? "Wewe ni nani? Na umejuaje mambo haya yote?"



    Bella akacheka na kuniambia "Mimi ni Bella Matondane ni askari wa jeshi la polisi la jamhuri ya muungano wa Tanzania umenisahau? Kufahamu hayo ni sehemu ya jukumu langu kufanya uchanguzi katika kutaka kukusaidia juu ya tatizo hili linalokukabili. Ninachoamini mimi na wachache kati yetu ni kuwa wewe hujauwa ila hapa kuna mkono wa mtu na mkono huo ni mtu wako wa karibu sana na anayekuhusu ndiye amehusika amka Ramon usipende kuamini vitu nusu nusu chunguza kwa umakini utambue nani mbaya wako"



    "Huna unachoniambia nikakuelewa" nilihisi naanza kuchanganyikiwa. Sikutaka kuamini kuwa huyu askari sasa anamuhusisha baba yangu na mauaji ya Beatrice, nikabaki nikiwa nimeikunja midomo yangu na macho pia





    "Ni kweli unachanganyikiwa haswa ukisikia kuwa anayehusika ni ndugu yako sina shaka ukija kumjua utaumia zaidi na kuchanganyikiwa kuliko hata hivyo hivi karibuni mambo yatatimia"



    Akawa anatoka na mara mlango ukafunguliwa. Alikuwa ni baba akiwa ameongozana na Oscer baba yake na Beatrice. Bella alipowaona wakiingia watu wale alishituka sana, nilishangazwa kushituka kwake kwa kuwa kama Oscer wameshakutana mara kadhaa hapo katika nyumba salama iweje ashituke wakati yule ni baba yangu aliyekuwepo katika chumba hiki dakika arobaini na tano zilizopita. Baba pia alishituka vivyo hivyo huku akijitahidi kumtazama kwa makini Bella bila kupata jawabu la msingi ambalo lilimfanya aulize kwa sauti

    "Bibi, nadhani tuliwahi kukutana sehemu?" Akawa anamtazama juu mpaka chini na kuendelea "Sikujua kama wewe ni askari"

    Oscer alikuwa akiwatazama baba na Bella kama nilivyokuwa nikifanya mimi kwa mshangao.

    "Nini kinaendelea!?"

    Bella akajibu kwa sauti ya kitetemeshi “Hapana mzee, umenifananisha”

    Nikajiuliza huku nikisubiri ujio wa Oscer na Baba chumbani kwangu una ujumbe gani kwa mara nyingine niliyodhani baba amekwishaondoka.

    Bella alipojibu hivyo, alifanya haraka akatoka nje huku baba akibaki akimtazama kwa nyuma akiwa ameshikilia magongo yake. Kisha alipogeuka akawa kama ananong'ona na mzee Oscer



    "Huyu binti namfahamu na niliwahi kumuona sehemu ambayo si nzuri sasa sikumbuki ni wapi kabisa yaani"



    Oscer akamshika bega baba kiurafiki kitu ambacho kikanifaraji huenda kuna mapatano kiasi ambayo sikuyafahamu.



    "Habari yako ndugu" Oscer akanisalimia

    "Salama shikamoo"

    "Marahaba, pole kwa yote”

    "Ahsante" nikajiulliza ina maana si yeye aliyenifanyia? Mbona hana dalili za kuomba radhi?

    "Ona unavyotesa wazazi wako? Wanabaki kugombana huko nje kwa sababu yako? Naomba uniambie tu mwanangu kwa urafiki sasa achana na yale yaliyopita siku chache zilizopita, kwanini umemuua mwanangu, mwanangu mpendwa na wa pekee ambaye alibaki badala ya mama yake kwanini umemuuwa!"



    Akaanza kushika shati yangu huku akinitingisha tingisha kwa hasira machozi yakimtoka yaliyoongozana na kamasi jepesi. Baba alijitahidi kumzuia lakini alionekana kuelemewa na ulemavu wake.



    "Naumia sana Lameck mtoto wangu wa pekee? Shenzi nitamuuwa Ramon. Hatonyongwa nitahakikisha namuuwa kwa mkono wangu"

    "Niue sasa hivi usichelewe ukamuumiza baba yangu"

    "Pumbavu nyamaza!" Ikawa patashika ndani ya chumba hicho. Baada ya Oscer kuninyamazisha, baba akanizaba kibao. Ikabidi ninyamaze kutazama kinachoendelea.

    "Niambie kwanini umemuuwa mwanangu" Oscer akazungumza kwa tuo aliouwekea msisitizo.

    "Mzee wangu mimi sijamuuwa nakuhakikishia mimi sijamuuwa"

    "Na alama za vidole vilivyokutwa shingoni na mikononi mwake vilikuwa ni vya nani?"

    "Sifahamu mzee wangu mimi sijauuwa" nikaanza kulia kwa uchungu huku baba akinitazama akiwa analia. Oscer akanitazama kwa hasira akiwa amekunja ngumi akanieleza "Mimi hutaniona tena, siku utakayoniona jua kuwa ndio siku ya kifo chako kwa heri" Akatoka baba akimfuata kwa nyuma.

    walipokuwa wakitoka, nikawa katika hali ya hudhuni huku hali hiyo ikinikosesha rah asana. Nikajaribu kukumbuka kila hatua zangu na vipi niambiwe ni mimi nahusika hata alama za vidole vyangu vikutwe katika shingo na mikono ya Beatrice. Akilini mwangu kukagonga kengele, ndioyo ni kengele ya kunikumbusha jambo. Nilikumbuka siku niliyopata taarifa kutokana na ujumbe uliotoka kwa Beatric akiniuliza kuwa kwanini namuuwa na hali ya uoga iliyonikumba siku hiyo. Nimekumbuka jambo, nimekumbuka, nimekumbuka jamani. Nikapata picha ya siku ile ya mwisho naukuta mwili wa mpenzi wangu ukiwa chini unaelea juu ya dimbwi la damu. Nimekumbuka sababu ya mimi kuhusishwa na mauaji. Nikatamani kunyanyuka nimuite baba yake Beatrice na baba yangu pamoja na Vanessa awepo niwaeleze jambo hili mara nikagundua kuwa mkono wangu umefungwa kwa pingu kwenye kitanda kile, harakati zangu zikapoa nikaendelea kuwaza tukio lile kwa nikiwaza uzembe nilioufanya.Niliwaza kuwa, siku ambayo nilifika nyumbani kwa Beatrice, mara nilipomkuta amelala kwenye dimbwi la damu na bila shaka roho ilikuwa imekwishamtoka; niliogopa sana na hivyo nilichanganyikiwa na kila nilichokifanya nilifanya kwa kuongozwa na uoga nilio nao. Vidole vile vilivyokutwa katika mwili wa mpenzi wangu, ni kweli zilikuwa ni alama za vidole vyangu lakini si kweli mimi nilihusika kumuuwa Beatrice. Nilimshika mara nilipoingia katika chumba kile ili kuhakikisha kama amekufa kweli, hapo ndipo nilipoacha alama za vidole vyangu. Lakini ninani atakayeamini? Ni nani atakayenisikiliza kama kila mtu ananiona

    mimi ni muuaji? Nikakumbuka jambo lingine. Beatrice alinitumia ujumbe usiku ule kuwa mimi nimemuua na kwanini namuua, si kweli kama Beatrice atakuwa alituma ujumbe ule kwa mkono wake mwenyewe, na kama siye yupo aliyehusika. Hapo ndipo nilipokuwa nikipataka kwa hamu, nikalivua

    shuka nililofunikwa kisha nikakaa kitako nikaitazama ile dripu iliyokuwa ikitiririsha maji katika mishipa yangu, kasha na mkono ule mwingine niliofungwa pingu katika kitanda kile cha chuma, nikaendelea

    kuliwazia jambo lile kwa undani zaidi nikiona kuwa lilikuwa lina mantiki kubwa ya kumshirikisha pia na Vanesa. Basi nikaona endapo kamasi ujumbe ule ulioandikwa kwa kutumiwa simu ya Beatrice uliandikwa na mtu mwingine, kuna uwezekano mtu huyo aliacha alama za vidole katika simu ya mpenzi wangu. Lazima apatikane na ajulikane ni nani na hiyo ndiyo njia ya kuvua kitanzi cha lawama na fedhea iliyonikumba kuwa nimemuua Beatrice.

    Bado wasiwasi wangu ukaganda kwa Michael huku nikitabasamu kwa ushindi na mara mlango katika wodi ile ukafunguliwa.Alikuwa ni dokta ambaye alikuja kuniambia kuwa nimekwishapata nafuu, hivyo baada ya dripu hiyo ningeruhusiwa kutoka katika chumba hicho. Daktari mwenyewe hakuwa mbali na uaskari kutokana na ukakamavu wa sura yake na ujamali wa misuli ya mikono yake. Hiyo ikawa habari njema kwangu kutoka katika chumba hicho kinachonuka madawa lakini pia nilitaka kumuomba Vannesa aipeleke kesi mahakamani haraka ili nipate kujua hatima ya maisha yangu. Nimechoka kuishi kwamawazo, hisia na wasiwasi. Hali hiyo ikasukumwa na hamu iliyojaa huku shahuku ikimwagika nilipotaka kumuona Michael akiadhibiwa kwa kosa la kumuua Beatrice. Niliamini upelelezi ukikamilika utaangukia kwa

    Michael. Pia jambo nililowaza la kupima alama za vidole kutoka kwenye simu ya Beatrice lilikuwa wazo zuri, nilitaka kumshirikisha Vanesa pia.

    Masaa matatu baadae niliruhusiwa kutoka hapo nikiwa katika ulinzi mkali wa polisi. Baada ya kula chakula cha usiku nikiwa nimejipumzisha katika mahabusu yangu, Bella akanijia na mimi wazo

    fulani likaniingia. Nikamwambia "Hivi ninaweza kuwasiliana na Vanesa?"

    "Unataka kumwambia nini?" Aliniuliza kwa mshituko uliojitengeneza

    katika uso wake kisha alizuga nisiweze kumuona, nikaonesha kutojali

    nikamwambia "Kuna kitu nimeanza kugundua nahitaji kuzungumza nae"

    nilizungumza hivyo kumpima kama ataamua kunisaidia au lah! Lakini

    alinisaidia kwa kunipa usiku huo huo tena kwa usiri mkubwa. Alioondoka

    kisha alirudi dakika chache baadaye na mto mweupe msafi na akaniambia

    jambo ambalo nilimuelewa kwa haraka "Utumie mto huu" akiushika kwa

    msisitizo "Usiku wa manane sana kwa kuwa huu ni msafi tofauti na

    uliolalia hiyo ni baada ya kwenda kuoga" nikatingisha kichwa kwa maana

    ya kuonesha kuwa nimeelewa kisha yeye akaondoka. Nikauweka mto

    ule wenye simu chini yake

    kwenye kitanda changu nikisubiri muda wa

    kuwasiliana na vanesa.

    Nilipoegesha kichwa changu kwenye tendegu ya kitanda, nikapitiwa nausingizi mwepesi ule wa mang'amung'amu. Muda mchache baadaye niliamshwa na kelele za mbwa waliokuwa wakibweka ovyo nje ya nyumba hiyo. ilikuwa yapata saa saba na dakika zake kwa mujibu wa saa ya kwenye simu niliyokabidhiwa na Bella. Ilipowaka nikairudisha ile simu chini ya mto na mimi nikanyanyuka kwa

    hatua za kunyata mpaka katika geti la mahabusu il. nilijitahidi kutazama kushoto, kisha kulia

    nikauona moshi ukitoka upande ule kilipo chumba kilichotumika kama jiko. Nikarudi pale kitandani

    na kuitoa ile simu; kitu cha kwanza nilichofanya ni kutazama salio, ilikuwemo ya kutosha. Nikajaribu

    kuzikumbuka namba za Vanesa alizonipatia siku za nyuma endapo nitahitaji kuzungumza naye kwa

    wakati ambao hatakuwepo. Nikaijaribu ya kwanza sauti ya kike ikanijibu kuwa

    "namba unayopiga haipo, ..."Sikutaka kumalizia kusikiliza nikasonya kwa hasira huku nikinakili namba nyingine, hiyo ikaita. Sekunde chache sauti ya kike ikakoromachomboni huku ikiwa katika utulivu wa uchovu wa usingizi.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Halo"

    Nikajikohoza kidogo kuirekebisha sauti yangu ilianisikie kwa ufasaha nitakapozungumza kwa sauti

    ya chini kabisa. kisha nikasema "Ramon hapa tafadhali naomba tuzungumze kwa

    meseji" nilimsikia akishituka mara aliposikia jina langu, bila shaka alikuwa na maswali mengi ya kuniuliza

    lakini sikumpa nafasi hiyo nikakata simu. Punde ukaingia ujumbe kutoka kwake

    "umepata wapi simu ya mkononi?"

    "huku huku ndani ya nyumba salama, kuna jambo nimegundua nadhani litasaidia" nikamjibu

    huku nikiwa makini kuuficha mwanga wa simu ile usije ukawashitua walinzi, nilikuwa nikituma na kusoma jumbe zile chini ya mto

    "kesho nitakuja huna sababu ya kumuamini yeyote kuanzia sasa kwa kuwa kuna mengi nimegundua ya kukushitua lakini wewe ni mwanaume yapasa ujipe moyo na kuukubali ukweli. usiku mwema"

    Nikatamani kumuuliza mambo mengi lakini ikawa ni kama kwamba hakuitaji kuendelea kuchati na

    mimi, hivyo nikaizima simu nikalala.

    kesho asubuhi niliamshwa na sauti ya Bella "Nipatie mto na foronya yake nitakuja jioni tena"

    Nilipoelewa alichomaanisha, mimi nilimwambia "Hapana huu wangu unatosha usiniletee tena"

    akatingisha kichwa na kuondoka, mara nikashituka. Nikakumbuka kuwa zile jumbe

    nilizokuwa nikichati na Vanesa sikuzifuta hali ya wasiwasi na uoga ukanivaa kwa kuwa bado sikuwa

    nikimuamini askari yule moja kwa moja. "potelea mbali" nikaitupa mikono hewani na

    kuelekea zangu sehemu ya kunawia uso na kusafisha meno. Nilipomaliza na kuoga, ndipo

    niliambiwa kuwa kuna mgeni wangu ananisubiri ukumbini. Nilifanya haraka haraka nikijua kuwa ni

    Vanesa.

    Nilipofika pale ukumbini, nilimkuta Vanesa amesimama eneo la dirishani huku akitazama nje. Alikuwa ameikunja mikono yake kifuani nakama aliyekuwa ameikalia meza ya vitabu iliyopo pale. Mchakacho wa

    hatua zangu huenda zikamfanya ageuke kule nilipokuwa natokea mimi, kisha nikafunguliwa zile pingu za mikono zilizounganisha mpaka miguu yangu kisha wale askari wakaondoka. waliniacha mimi na Vanesa pekee,

    Vanesa akanisalimu. "Nimeshapoa dada yangu ila nahitaji unisaidie jambo hili kabla ya

    yote" Baada ya salamu nikamwambia Vanesa. Yeye alivuta kiti kilichopo pale karibu yake na kuutua mkoba begani mwake huku nami nikikaa mkabala naye. Vanesa alionekana kuwa mtulivu zaidi na kuniambia

    "Nieleze unahitaji msaada upi na kisha usinifiche jambo" Akayakaza macho yake na vituta vya mistari juu ya uso wake vikajichimba,akaendelea "Ni nani aliyekupa simu ama wapi ulipata"

    Nikacheka niliposikia hivyo na sikuwa na sababu ya kumficha jambo, ilakule kuwa na sura siriazi kukanifanya nimuone kama kituko. Nikamueleza ukweli "Kwanza nashukuru kwa kuamua kunitetea au kuisimamia kesi hii japo ni upande wa mlalamikaji uliokutuma kusikiliza utetezi wangu. Hivyo

    sijajua nia na sababu ya mzee Oscer lakini naamini hana nia mbaya

    kabisa na mimi. Vanesa kuna alama za vidole katika faili la kesi hii

    vilivyopatikana katika mwili wa marehemu Beatrice, basi naamini

    nikikueleza hili hutaweza kuamini"

    "Nieleze kila kitu" vanesa alinikatisha huku akiwa amekwishawasha tepurekoda yake. Nikaendelea kumueleza jinsi ilivyotokea mpaka nilipomshika Beatrice aliyekufa na alama za vidole vyangu vikabaki katika mwili wake

    "Hiyo ni kesi mbaya na ngumu sana"

    "Sasa nitafanyaje Vanesa na imeshatokea?" Nikauliza kwa kukata tamaa

    na nikaamua kuitupa kete yangu ya mwisho, nikamueleza "Kuna jambo nimelifikiria nadhani litanisaidia"

    "Lipi?" akauliza huku akinitazama kwa makini.

    "Kama unakumbuka inasemekana Beatrice alinitumia ujumbe kwenye simu yangu kuwa kwanini namuuwa je unadhani kulikuwa kuna uwiano wa yeye kuituma meseji ile kama ni mimi kweli nilimuua?"

    nilimuona Vanesa akiwa amebung'aa na huenda alikuwa akisisimukwa na kile

    nilichokuwa nikimueleza, nilimuona akivutiwa na mkondo wa maongezi

    lakini alishindwa kuzungumza neno, nikaendelea

    "Basi kama kulikuwa hakuna ulazima kuna aliyefanya jambo lile na mtu

    huyo ndiye amehusika na mauaji haya kwa asilimia kubwa lakini je

    unadhani tutampataje?"

    "Wewe umefikiria nini kwanza? maana umenipa mwanga mpya" alisema nusu akifurahi kwa raha huku akiwa amejawa na shahuku

    "Aliyetuma ujumbe ule aliiacha simu eneo la tukio?"

    "Ndiyo" Vanesa akanijibu

    "Simu ile ipimwe alama za vidole kisha itakuwa rahisi kumjua muhusika

    wa tukio hili kwa kuwa naamini atakuwa ni muhusika ambaye askari

    wanayo rekodi ya mambo yake ya kijambazi hapo nyuma. muuaji mgeni

    hawezi kufanya tukio la kijasusi kama hili na baada ya hapo tutajua pa

    kuanzia"

    Vanesa alisimama na mimi nikasimama, akawa anaizima tepurekoda ile kisha akanipa mkono wa pongezi.

    "Nafurahi kumtetea mtuhumiwa mwenye kunuka upelelezi naomba nikafanye

    jambo hilo sasa hivi na jioni ama kesho nirudi na majibu kamili"

    "Je yale uliyogundua wewe ni yapi?" Nikauliza nilipomuona akifungasha

    "Nishamjua muuaji lakini si sahihi kukwambia sasa ila nilizungumza na

    Michael pia hausiki na mauaji haya acha niukamilishe ushahidi ili

    keshokutwa upande mahakamani"

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilikaa na mawazo mengi mara baada yaVanessa kuondoka. Nilijiuliza kwanini Vanessa aone Michael tenaahusiki katika mauaji haya? sasa kama si yeye, ni nani basi anahusika?amesema anamjua, atakuwa ni nani huyo ambaye mimi sijamjua katikamaelezo yangu yote niliyoyatoa? Nilipokuwa nimekaa peke yangu, nikawanimezama katika tafakuri iliyonikumbusha mambo kadhaa nyuma

    yaliyopita.









    ITAENDELEA  

NENDA NA MOYO WANGU - 3

 

     





    Simulizi : Nenda Na Moyo Wangu

    Sehemu Ya Tatu (3)





    "RIPOTI YA KIfO CHA BEATRICE MTOTO WA KiGOGO WA UN YASIKiTISHA"

    Nikavutika na maandishi hayo, kisha nikachukua gazeti lile na kusoma

    kilichoandikwa ndani. Habari ile ilinishangaza na kunishitua sana,

    mwandishi aliandika kilichotolewa na daktari baada ya uchunguzi.

    "Katika damu ya binti huyo wa Bw Oscer, kumekutwa na sumu kali aliyoinywa

    katika bia" sehemu ya habari hiyo ambayo ilinishitua. Ni saa ngapi Beatice

    alikunywa pombe? nilirudi naye mpaka nyumbani kwake kisha mimi nikaondoka,

    hakuna sehemu ambayo Beatrice alikunywa pombe.

    "Haiwezekani" nikasema kwa nguvu kisha mapigo yangu ya moyo yakaenda mbio

    sana "kuna mchezo"

    Nikarudishwa mahabusu na yule askari wa kike na kukuta nimekwisha andaliwa

    chai ya maziwa pamoja na mkate uliopakwa Blueband na jam. Nikiwa mwenye

    mawazo mengi juu ya ujio wa Michael na habari ile ya kifo cha Beatrice,

    ilinibidi nile haraka haraka kabla sijapoteza hamu ya kula kisha nikashinda

    njaa. Nilipomaliza kula, nikapanda kitandani kwangu miguu nikaikunja na

    kuikumbatia katika kifua changu. Hapo nikawa nawaza.



    SIKU YA TUKIO LA MAUAJI YA BEATRICE.

    "Usiku ule wakati tunatoka pale katika sherehe, Beatrice hakuwa na kilevi

    chochote kichwani mwake wala kinywa chake hakikutoa harufu ya pombe. pombe

    aliinywa saa ngapi kwa kuwa hata nilipokuwa nikimbusu, sikusikia harufu ya

    kilevi"



    INAENDELEA HAPA Nikakunjua miguu yangu na kuifunga mnikono yangu kifuani

    kisha nikasimama nikawa nazunguka zunguka katika kile chumba.

    "Vipi Michael? Kwanini haoneshi kuumia kwa mimi kupata kesi kubwa namna

    hii? Kwanini yeye ni kama anashiriki kunihukumu kuwa mimi nimeuwa?

    Inawezekana Michael akawa anahusika ama anamjua muuwaji? Muuwaji ni nani na

    Michael afurahie kufungwa kwangu? Ama Michael ameamua kufanya kitendo cha

    heri tukose wote?"

    Hapo nikakaa tena kitandani nikashika kichwa changu kwa mkono niliopegemea

    katika paja langu.

    "Tukose wote? Yaani Michael anaweza kumuua Beatrice ili tukose wote? Ina

    maana hana roho ya huruma kiasi cha kutazama hisia zake? Na kama si Michael

    ni nani basi? Nani awezaye kuwaza kuwa Beatrice ana uhusiano na mimi?"

    Niliwaza mengi na kukiri kwa sauti ya juu mara baada ya kushusha pumzi

    ndefu nikajisemea "Nimekamatika"

    Sauti ya yule askari wa kike ikanizindua aliposema "Muda wa kuoga na

    kubadilisha nguo zako za kiraia"
    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilijitazama nikakumbuka kuwa tangu nilipokamatwa jana, sikuwa

    nimebadilisha nguo wala kuoga. Nikavua ile shati niliyovaa kisha suruali

    nikajifunga taulo lililopo pembezoni mwa mto katika kitanda changu. Yule

    askari alirudi tena akiwa na nguo yaani suruali na shati nyeupe

    zilizokuinjwa vizuri na kunipatia pamoja na sabuni na mswaki kisha mimi

    nikaziweka zile nguo pale kitandani na kutoka naye nikiwa na sabuni na

    mswaki mkononi. Akanipeleka katika vyoo vya mahabusu huko nikaoga kwa muda

    wa nusu saa. Nilioga kwa muda mrefu kutokana na mawazo yaliyoandama kichwa

    changu kwa muda mrefu.

    Nilipotoka na mara baada ya kuvaa, alikuja Jafary Hiza aliyeongozana na

    Vanessa Noel.

    "Habari yako Ramon"

    Vanessa alinisalimu huku Jafary Hiza akinitazama kwa jicho baya ambalo

    sijapata kuliona kamwe.

    "Nzuri tu sister za tangu jana?"

    Vanessa akatabasamu kisha akanijibu "Nzuri pia, naona leo umechangamka

    tofauti na jana?"

    Sikumjibu. Wakaingia askari wawili wakataka kunifunga ile pingu yenye

    mnyororo Vanessa akawasihi.

    "Msimfunge tafadhali kuna ulinzi wa kutosha kuliko kumfanya hivyo" Vanessa

    akamtazama Jafary Hiza kisha akasema "Unajua unapomtuhumu mtu haina ulazima

    wa kufanya hivi tunavyomfanya kwa kuwa kama ni kesi ya kusingiziwa

    itamuondolea kujiamini na kujihisi kuwa yeye ni mhukumiwa tayari. Tumpe

    uhuru kiasi"

    Jafary Hiza hakujibu kitu na uso wake ulionesha kukereka na jambo hilo

    akaondoka na kutuacha mimi na Vanessa. Vanessa alinichukua mimi mpaka

    katika chumba kile cha mahojiano tulichokaa siku ya kwanza mimi naye.

    Nilikaa na yeye akakaa, akaniambia huku akiwa na uso wenye tabasamu.

    "Ramon, nilipokuwa nyumbani nilitamani sana muda huu. Naomba uendelee na

    ile hadithi ya wewe Beatrice na Michael"





    AKAWASHA ILE TEPUREKODA YAKE NA MIMI NIKAANZA KUZUNGUMZA-:



    "Unakumbuka nilipoishia?"

    Nilimuuliza Vanessa. Kisha akaniambia

    "Mlikuwa carteen mkila mara Beatrice akakumwagia juisi mlipogongana"



    SASA NIKAWA NIMEKUMBUKA, NIKAENDELEA.



    Beatrice aliniomba msamaha kwa kunichafua na ile juisi kisha akatoa kitambaa chake cheupe chenye maandishi yaliyoandikwa kwa wino mwekundu ambayo sikuweza kuyasoma, akawa ananifuta pale juisi iliponimwagikia. Wakati huo Michael na Steven walikuwa wakinitazama, Lakini Michael alinitazama kwa jicho baya sana tofauti na Steven aliyekuwa akitabasamu na kunioneshea dole gumba la poa. Sikujali kuhusu Michael.

    Nilimshika Beatrice mkono ambao alikuwa akinifuta futa pale nilipochafuka, kisha akauinua uso wake na kunitazama. Nikamwambia kwa sauti ya upole

    "Usijali nitaenda kuifua"

    "Naomba unisamehe sana ilikuwa ni bahati mbaya" akanisihi kwa sauti laini ya kubembeleza na mimi ikaniteka sauti yake nikabaki nikimtazama. Kisha kwa sekunde kadhaa akautoa mkono wake kutoka kwangu na kuniambia "Naitwa Beatrice" akanipatia mkono wake kama ananisalimia na mimi nikaupokea nikajibu.

    "Ramon"

    Niliona macho yake yaking'aa kama aliyesikia nikiwa nimezungumza jambo la ajabu sana, nikatoa lile tabasamu ambalo huwa ni nadra sana kulitoa kwa kila msichana kwa kuwa si wote walistahili zawadi hiyo adhimu kutoka kwangu. Lakini Beatrice alistahili.

    Nilipomuona Beatrice kwa mbali sikuwa na chochote nilichohisi kutokana na ukweli kwamba nilishagundua kuwa Michael anampenda msichana huyu lakini nilipokuwa karibu yake tukitazamana, moyo wangu ulibadilisha mapigo yake ya kawaida na kwenda kasi sana. Jasho lilikuwa likinitoka huku mikono yetu ikiwa hewani imeshikana.

    "Nimefurahi kukufahamu Ramon" akatoa tabasamu laini na kubahatika kuliona jino la rangi ya madini ambayo kwa kipindi kile sikuweza kuyajua ni madini ya aina gani kisha akanieleza "Mimi nipo Ba wewe uko wapi?"

    "Social leo ndio nimewasili chuo"

    Akatabasamu tena kisha akautoa mkono wake kwangu na kuniambia "sawa Ramon tutaendelea kuonana na si vibaya siku moja ukaja kunisalimia katika hostel zetu"

    "Poa"

    Kisha kila mmoja akarudi katika meza yake. Kwa Beatrice ile kusimama na mimi ikawa kama sherehe kwa kuwa niliona wenzake wakifurahia jambo ambalo mimi sikulijua huku kwangu ikiwa kasheshe kwa Michael.

    "Umefurahi sasa we boya?" Michael akaniuliza akiwa amekunja ndita kwa hasira. Kabla sijamjibu chochote akanyanyuka na kuondoka zake. Mimi nikabaki nikimtazama Steve kwa mshangao huku nikipandisha mabega yangu juu kisha nikayashusha chini steve akautupa mkono wake hewani na kunieleza.

    "Mpotezee boya tu"

    Baada ya kumaliza kula tukanyanyuka na Steven kisha tukaondoka.



    BAADA YA KUAMALIZA HADITHI HIYO YA CHUONI NIKAKUMBUKA JAMBO LINGINE MUHIMU:-"Halafu nisisahau jambo Vanessa!" Vanessa akanitazama na kuacha kile alichokuwa akikiandika "Michael alikuja leo asubuhi"

    "Alikuja? Enhe ilikuaje?"

    Nikamuelezea Vanessa kila kitu kilichotokea asubuhi juu yangu mimi na Michael lakini hakuzungumza chochote bali aliguna tu na kuniambia niendelee kuhusu Beatrice.

    Nikaendelea kumueleza maisha yangu ya siku ya kwanza pale chuoni. Siku hiyo yote Michael hakuniongelesha licha ya kuwa ndio siku ya kwanza kukutana na Michael katika maisha yangu. Nikaifahamu tabia ya Michael vyema. Niimuona kuwa ni mtu asiye na busara mwenye wivu kupindukia na pia ni mtu asiye na ustahimilivu. Nikajichekea nilipomuona kajinunisha akitazama movie ya mwanadada Angelina Jolie "salt" moyoni nikajisemea 'unatazama kwa macho lakini huna unachoelewa wala kufurahia kwa kuwa una hasira na mimi' nikatoa mguno wangu wa kebehi ambao bila shaka ulimkera Michael, nikamsikia akisonya wakati nikipanda juu ya kitanda changu.

    Siku ya kwanza ikawa imeisha nikiwa ndio mgeni katika chuo kikuu cha dodoma.

    Ikawa ni siku ya kwanza kukutana na Beatrice mwanamke aliyebadilisha maisha yangu kutoka katika hali ya kutamani kila mwanamke na kufanya naye ngono na kuwa naye yeye peke yake. Mwanamke ambaye leo ameniweka katika kitanzi ambacho sielewi nini hatima yangu hapo baadaye mwanamke niliyempenda kuliko kitu chochote katika maisha yangu. kwasababu unajua kuna kipindi niliwahi kukorofishana na Michael hadi kutaka kukatana visu kwa sababu ya Beatrice.

    Hapo kukamshitua Vanessa akainua uso wake akanitazama na kuniuliza

    "Ilikuwaje?"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Nitakuhadithia kila kitu kama unataka kujua kila kitu

    SIKU HIYO IlIIKUWA HIV ISiku moja tukiwa chumbani, nilikuwa nikichart na Beatrice baada ya wiki moja tangu ile siku ya kwanza tuliyoonana. Najua unajiuliza ni vipi nilichart naye na siku hiyo hatukupeana namba za simu, lakini ukweli ni kwamba nilimfuatilia Beatrice binafsi kwa kuwa sikutaka kuanzisha ugomvi na Michael. Sikutaka kuanzisha ugomvi kwa kuwa nilimjua anampenda na penzi lake lingeweza kuzua tatizo kama akigundua na mimi ninampenda Beatrice. Katika kumfuatilia, niliingia mpaka chumbani kwao siku iliyofuata mara baada ya siku ile. Alifuarahi sana kuniona nikiwa naranda randa chini ya ghorofa kilipo chumba chao.

    "Romy"

    Aliniita kwa kifupi na wala hakuendelea kuniita Ramon hivyo hilo likawa kama jina langu jipya kwake. Nilipogeuka na kuinua uso wangu kwa juu, nilimuona Beatrice akiwa ana khanga aliyoifungia kuanzia kifuani na bila shaka ikaishia magotini. Nilimpungia mkono na kuvunga kuwa nilikuwa kama simfuatilii yeye ila ukweli wa jambo hilo nilikuwa nao moyoni mwangu. Akaniita.

    "Njoo upaone chumbani kwangu basi"

    Akaniambia akiwa na furaha, hivyo sikutaka kupoteza nafasi hiyo hadhimu nikapanda ngazi na kwenda mpaka kilipo chumba chao. Huko nikakutana na Alicia pamoja na Prisca wakiwa wanasukana. Tukasalimiana huku wao wakiniachia tabasamu zao nzuri. Nilikaa katika kiti ambacho alikikalia Prisca alipokuwa akimsuka Alicia, kisha yeye akakaa kwenye kitanda.

    "Karibu Romy"

    "Ahsante sana Beatrice" Akanitambulisha kwa Alicia kisha kwa Prisca, nikajichekelesha na kusema

    "Nafurahi kuwafahamu sana"

    "Na sisi pia" kisha wakagongana wakaachia kicheko cha haya. Sikupenda kukaa kwa kuwa nilihisi kama walikuwa wakinichora. Nilihisi walikuwa wakinichora kwa kuwa niliona wakiwa na kitu ambacho walikuwa wakinizungumzia kabla ya mimi kuja tena. Ina maana tangu jana bila shaka walikuwa wakinizungumzia kwa muda mrefu na imekuwa kama bahati ya mimi kuja kwao.

    "Oh! Unakunywa nini Romy?"

    "Hapana sinywi chochote nilikuwa napita tu kuelekea kimwaga"

    Nikamuona Alicia akimsuka Beatrice mimi nikajifanya kama sijaona jambo lile, Beatrice akaniambia.

    "Romny upo whatsapp?"

    Nilishituka lakini nikajua janja hiyo, nikaitika kwa kichwa nikimtazama akiachia tabasamu laini la furaha.

    "Niandikie namba yako"

    'Mtoto wa kishua' Simu yake ilitangaza ufahari na hapo nikamtazama Beatrice kwa jicho la tofauti zaidi. Simu aliyokuwa akiitumia kwa kipindi hicho ni Iphone sijuhi Iphone ipi hivyo ikanionesha ufahari wa Beatrice. Nikaandika namba yangu kisha akaniambia jibipu na wewe uipate na yangu, hiyo ndiyo ikawa sababu ya mimi na yeye kuanza kuwasiliana. Wiki moja ilitosha mimi na yeye kuwa na mawasiliano ya karibu kiasi kwamba hakuna ambaye angekataa kuwa tulianza kuwasiliana zaidi ya mwaka mmoja uliopita, lakini haikuwa hivyo. Kisha baada ya kubadilishana namba ya simu hizo, nikaaga kuondoka. Nilichokuwa nikikitamani ndio hicho, nikae kupoteza muda zaidi nini? Prisca na Alicia wakanitania,

    "He ina maana zetu huchukui" Nikahisi aibu sana nikataka nibaki nichukue na zao wao wakajua wamenipata wakaniambia nisijali tu niende walikuwa wakinitania.

    Sasa siku hiyo wakati tukiendelea kuchati mimi nikicheka kwa kila meseji iliyokuwa ikiingia, Nilikuwa nikimsikia Michael akisonya sonya kwa hasira. Mimi sikuzungumza nikaendelea kufurahi kuchati na Beatrice. Mara nikatoka kwenda chooni nikaiacha simu kitandani kwangu huku akiwa amebaki Michael peke yake. Sikujuwa kama alikuwa amesoma meseji zangu, niliporudi nikawa naendelea bila kuwa na shaka yeyote. Katika sehemu ya meseji hizo, tulikuwa tumepanga kukutana maeneo ya Kwa mama wajasiriamali. Kumbe yote Michael alikuwa ameshasoma na alipanga kunifuatilia ahakikishe. Jambo hilo ndio likazua utata wa kutaka kunikata visu.

    Muda ambao tulipanga mimi na Beatrice ulipofika, nilitoka nikiwa nimehakikisha kuwa nimependeza sana sanajari na kunukia manukato yangu safi. Kwa kuwa nilifahamu fika ilikuwa ni sehemu ya gizani basi manukato yangu yangu kuwa silaha tosha ya kuniona "smart" nikatoka wakati ambao Michael naye alikuwa ametoka. Kwa mama wajasiriamali ilikuwa ni mita chache tu kutoka katika hostel zetu.

    "Habari yako Beatrice?"

    "Salama tu Romy nilitegemea ungechelewa sana" alisema Beatrice akiwa amesimama kunikaribisha.

    "Mimi sikutegemeakama ungewahi kuja kabla yangu nashukuru kwa kuwahi"

    Kisha tulikumbatiana, nikakaa pembeni yake akiwa ametandika khanga chini pembeni ya mti fulani. Tukawa tunapiga hadithi mbalimbali na kufahamiana kwa ufupi.

    "Mimi ni mtoto wa pekee katika familia yetu. Baba yangu anaitwa Oscer kama unamfahamu"

    Sikujuwa sababu ya yeye kuniambia kuwa kama namfahamu, nikakataa lakini Beatrice hakupenda makuu ya kuzidi kunifahamisha ni Oscer yupi alikuwa akimzungumzia, japo nilikuwa namfahamu Oscer kabla hajawa naibu katibu mkuu wa umoja wa mataifa.

    "Mimi ni mtoto wa pili lakini kwa sasa nipo peke yangu kwa kuwa kaka yangu alifariki kwa ajali ya gari iliyowahi kutokea chato katika lile gari lilokuwa likienda Rwanda"

    Beatrice akawa amenyamaza na mimi ni kama hadithi zikawa zimeniishia, ukimya wetu uliotupitia tukasikia mchakato wa kitu chenye uhai katika nyasi zilizopo karibu yetu.

    "Nini hicho?"

    Beatrice alitoa macho pima sanjari na pumzi zake kupishana kwa hofu. Mimi nikasimama kutazama kile kilichokuwa kikifanya zile nyasi kutingishika, alikuwako mtu. Mtu huyo alivaa shati nililolifahamu na nilimfahamu mtu huyo fika, nikamtoa hofu Beatrice.

    "Hapana mtu usiogope"

    "Haya" aliongea lakini sauti yake haikuwa na dalili zozote za kuwa kama aliamini nilichozungumza. Mimi na Beatrice tukasimama na kushikana mikono kwa sekunde kadhaa.

    "Nimefurahi sana kukuona Romy"

    "Nimefurahi pia Beatrice"

    Tulikumbatiana tena kisha Beatrice akanitupia busu zito la kuzivamia papi zangu. Tukaondoka moyoni nikiwa nimehakikisha kumkomesha Michael kwa kuwa ndiye aliyekuwa akitutazama kule alipojificha kwenye nyasi.

    "Kwanini unatabasamu"

    Beatrice alifahamu kuwa nilikuwa nikitabasamu lakini si tabasamu la kile alichonifanyia kwakuwa halikuwa tabasamu halisi.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Una lips za moto" nikamdanganya yeye akacheka, tukaondoka. Nilipofika hostel nikiwa ndio kwanza nimekaa natafakari kuhusu tukio la Michael kuja kututazama kule tulipo mimi na Beatrice, Michael aliingia. Alikuwa akihema kwa fujo macho yamemtoka pima.

    "Ramon, Ramon" Akawa ananiita kwa hasira. "Wewe sio wa kunifanyia mambo ya(akatukana tusi zito la kunidhalilisha)nasema huwezi kunifanyia hivi" Akapanda kitandani kwangu na kuanza kuniangushia makonde. Mimi niliziba uso wangu kwa kuwa sikutaka kupigana na Michael. Michael aliendelea kunipiga mpaka tukaanguka kutoka juu ya doubledeker mpaka chini mkono wangu ukateguka lakini aliendelea kunipiga. Mezani kukawa na kisu kidogo kilichotumika kukatia embe, nikiwa nimesimama huku michael naye amesimama akihema kwa nguvu mimi nikiugulia maumivu, akawa anapanga kunichoma na kisu kile. Nilishuhudia hilo na niligundua kwa kuwa machale yalinicheza mapema, nikamkwepa kisha nikakimbilia nje ya chumba chetu. Michael hakuwa mtu kabisa, michael alikuwa tayari kuuwa kwa ajili ya Beatrice. Michael alimpenda sana Beatrice.

    Mara mpaka hapo, Vanessa akanikatisha "Dah kuna mambo mazito sana katika kesi yako, nilipopewa kuhusu habari za kifo cha mtoto wa mteja wangu nilidhani ingekuwa ni kazi nyepesi lakini kuna mazito"

    Hofu ikanivaa kwa kuwa sikufahamu kwanini aseme hivyo, kwanini aanze kuingia na uoga wa kuifuatilia kesi yangu? Sikuwa na nafasi hata ya kumuuliza hayo yote kwa kuwa muda ulikuwa umekwisha kwa wakati ule.

    "Acha niende Ramon, lakini kuna umuhimu wa mimi na wewe kukutana kila siku kwa ajili ya uzito wa kesi yako. Kuna jambo moja nimelipata kutoka katika maelezo yako lakini inabidi nisikie zaidi huenda fikra zangu zikanidanganya kutokana na kusikia upande mmoja wa shilingi" Akaniaga na kuondoka zake. Siku hiyo nilibaki mwenye mawazo sana. Nikasema yawezekana nilichowaza ni sahihi ndio maana hata Vanessa alisema vile. Sikuwa nimekosea kuelezea kila kitu kweli nilichofahamu kuhusu Michael.



     Hisia zangu zikanifanya kumshinikiza Vanessa aamini kama nilichoamini mimi ili Vanessa apate muda wa kumchunguza Michael na kugundua kila kitu. Nilipotazama saa sikujua kama ilikuwa imeshafika saa 10:48 jioni, yule askari wa kike akaniletea chakula ugali na maharage kwa samaki wa kukaanga na mchuzi wa maharage. Nilipokula nikashiba, nikalala mpaka majira ya saa 2 usiku. Niliamshwa na kirungu cha askari aliyekuwa akiniita kwa kebehi. "We jambazi" Nilipoinuka na kumtazama alikuwa ni yule askari ambaye alinikamata nyumbani kwa Beatrice. Akaniambia "Una mgeni" Nilitoka nikiwa najiuliza ni vipi mgeni aruhusiwe kuniona kwa wakati huo ambao sidhani kama ilikuwa ni sahihi. Nikatoka na kwenda kumuona. Sebuleni pale alikuwako mtu ninayemfahamu. Mtu huyo ni mtu mzito sana. Mtu huyo nilimzoea kumuona katika mikutano mingi mikubwa ya kitaifa mtu huyo hakuwa mwingine bali ni baba yake Beatrice, mzee Oscer.Kwa kueleza tu kiufupi unaweza ukahisi ni kiasi gani nilikuwa na hofu juu ya kutazamana ana kwa ana na Oscer. Sikumbuki fika kama niliweza kumsalimia au kuzungumza chochote mara nilipokutana naye macho kwa macho tena mara baada ya sherehe ya juzi usiku wa kifo cha Beatrice. Zilipita dakika mbili kwa kadirio chini mpaka alipoanza kuzungumza tena nami.

    "Umeshindwa kunisalimia?" Kwa sauti ya kigugumizi bila kuelewa fika kile nilichokuwa nikikizungumza, nikamsalimu "shikamoo mzee!" "Nashindwa kuelewa kitu gani kimekupata kijana. Kwanini umeukatisha uhai wa binti yangu mpendwa siku niliyokukabidhi mbele ya wazazi wako. Ni hivi walivyokufundisha ama nini alikukosea Beatrice, mwanangu? Kwanini umeamua kumuhukumu hata kama lipo alilokukosea?" Nikayaona machozi yakilowesha mashavu yake huku akivuta kamasi jepesi na kunitia simanzi hata mimi. "Sina sababu ya kukueleza ni nini nitafanya mara baada ya kuthibitika wewe unahusika na mauaji ya binti yangu lakini naomba ujieleze vizuri ili yule mwanasheria akuelewe usije ukaenda nje na ukweli utakaokutia kitanzini. Nimempangia adhabu nzuri yeyote aliyehusika na mauaji ya binti yangu" Akanyanyuka mara baada ya kumaliza aliloongea na mimi nikanyanyuka na kumtazama alipotaka kuongea na maneno aliyotaka kuzungumza kuishia mdomoni kwake. Mimi nikazungumza mara aliponipa mgongo na kutaka kuondoka. "Mheshimiwa, ukweli ni kwamba mimi sihusiki na mauaji ya Beatrice kwa kuwa pia ninampenda na nilimpenda sana Beatrice kuliko kitu chochote. Nitajitahidi kueleza kila kitu kinachohusu kazia hii lakini iwapo itathibitika n'nastahili adhabu hii sina sababu ya kukubali nipatiwe adhabu yeyote ili moyo wangu uende na yule nimpendaye" Sauti yangu ikakumbwa na kitetemeshi cha kuzungumza kwa hasira iliyokaba koo yangu na kutengeneza donge fulani la hasira. Oscer hakugeuka kunitazama lakini alinijibu huku akianza kupiga hatua za kuondoka. "Auwaye kwa upanga... " Hakumalizia kile alichotaka kuongea akawa ameshafunguliwa mlango na kutoka nje. Mimi nikajibu kwa sauti ambayo haikusikika na mtu "Atakufa kwa upanga. Atakufa kwa upanga au nitakufa kwa upanga!!" Kisha nikarudi katika mahabusu yangu baada ya kuletewa chakula kule kule na askari yule yule wa kike.

    "Nadhani juisi ya rozela niliyotengeneza utaipenda" Kisha akaondoka. Nilikila niliposhiba nikaenda kuoga kwa ajili ya kwenda kulala. Siku iliyofuata asubuhi na mapema mara baada ya kunywa chai, nilielezwa leo siku ya nne ni siku maalumu ya kukutana na wazazi wangu. Nilifarijika sana kwa kuwa nilitamani sana kukutana nao nisikie wao pia wanamaono gani juu ya kesi yangu na vipi wameichukulia kesi hii iliyonikuta mtoto wao. Alipokuja yule askari wa kike akanieleza kuwa hawakuja wazazi wangu wote wawili bali mama yangu peke yake. Ilinishangaza kwa kuwa sikutegemea kama baba angeweza kukaa nyumbani ikiwa mimi nina kesi nzito inayonikabili ya mauaji. Sikuwa na la kufanya nikatoka katika mahabusu ile nikaelekea kule alipo mama. Askari yule wa kike akaninong'oneza jambo

    "Mama yako anaonekana kijana! Anayajua mambo mengi ya mjini" Nikampuuza kwa kuwa aliongea kwa kunikejeli na kama ningejua maana ya maneno yake tangu mwanzo leo nisingeweza kuandika haya ninayoandika saa chache kabla ya kifo changu. Saa chache kabla sijaamua uamuzi mgumu wa kuitoa roho yangu na kumkabidhi Beatrice moyo aende nao kule popote aendako yeye.

    Nikafika pale alipo mama yangu tukasalimiana na alionesha kuwa na furaha sana kuniona. Mama alinitazama baada ya mimi na yeye kukaa kwenye kochi, kisha akazitazama kwa kuzigusa gusa nguo nilizovaa akatoa tabasamu fulani dhaifu. "Habari yako mwanangu?" Akanisalimu kwa sauti ya upole "Salama mama, shikamoo!"

    "Marahaba" kisha akawa kama anataka kuongea tena, akaendelea "Imekuaje ukafikwa na jambo kama hili mwanangu?"

    "Mama ina maana na wewe unaamini kuwa nimeua?" Nilimuuliza "Hapana sitaki kukuuliza kama umeuwa au hujauwa kwa sababu sitaki kuamini kama unaweza kumuuwa Beatrice na siwezi kuamini kamwe lakini ilikuwaje wewe ukakamatwa kama muuwaji wa Beatrice na baba yake akithibitisha kuwa umekamatwa na vithibitisho vyote kuwa wewe ndiye muuwaji! Hicho ndicho n'nachotaka kufahamu ilikuwaje ukakamatwa kwa kesi hii?" Nikashusha pumzi kwanza kwa kushukuru kuwa mama yupo upande wangu na anaamini kuwa mimi siwezi kumuuwa Beatrice pili nilihisi kuwa nina mzigo mpya wa kumuelezea upya juu ya kila kilichotokea lakini sikuwa na sababu ya kuacha kumuhadithi kwa ufupi kila kilichotokea bila ya kuacha la maana hata moja. Nikamueleza kwa ufupi tangu nilipopata ujumbe mfupi kutoka kwa beatrice kuwa ninamuuwa kisha nikaja kuupata asubuhi ya siku ya pili nikiwa n'na hangover ya pombe nyingi kichwani mwangu kisha nikachukua uamuzi wa kwenda nyumbani kwa Beatrice huko ndipo nilipokutana na madhira haya yaliyonifanya niwe mbali na kitanda changu, nyumbani kwangu kule mtoni kijichi. Hadithi hiyo haikuonesha kumshitua sana mama yangu, akaropoka jambo ambalo sikulielewa.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Yule mtoto mshenzi sana" kisha akanitazama kwa chati kana kwamba alikuwa akisubiri nimuulize swali, akaendelea kuongea "Ngoja kwanza nikuulize, hivi Michael ameshakuja kukuona?"

    "Ndiyo mama alikuja juzi lakini yeye alinishitumu kuwa mimi nimemuuwa na sikutegemea kabisa kama rafiki yangu wa siku nyingi kiasi hiki asinijue hata kuniamini kuwa mimi ni muuwaji, mimi ninaweza kuwa muuwaji kweli?" Nikaanza kulia mbele ya mama.

    "Usilie mwanangu, wewe ni mtoto wa kiume. Inabidi ujikaze na upambane kutafuta haki yako, yule Michael ni mtoto mshenzi sana na usije kumuamini kabisa ndio maana siku zote nilikuwa nikikueleza kuwa Michael asimzoee kabisa mpenzio sasa nadhani utakuwa umenielewa"

    Wakati mama akizungumza hayo yule askari wa kike alikuwa ametujia na kumtoa pembeni mama na kumueleza mama jambo, sikuweza kujua nini alizungumza naye. Nikakaa kitambo kidogo nikimtazama mama na askari yule walivyokuwa wakizungumza huku wakinitazama kwa kuniibia kama vile walikuwa wakinizungumzia mimi. Mimi pia sikuelewa maana ya mama kumsema Michael ni motto mshenzi na vipi ilihusiana na kesi yangu juu yay eye kunikataza Michael kuwa na mahusiano ya karibu na Beatrice.



    ...

    Mama aliporudi pale nilipo mara baada ya kumaliza kuzungumza na yule polisi wa kike, aliniaga kuwa anaondoka. Alionesha kuwa mwenye haraka na kusahau kabisa kuna kitu ambacho aliniambia kabla hajaenda kwa yule askari wa kike.

    "Mama" nikamuita kisha akageuka aliponipa mgongo na kutaka kuondoka "kuna jambo la kushangaza umenieleza naomba uniambie ukweli"

    Mama akageuka na kukaa tena kochini kisha na mimi nikakaa baada ya yule askari wa kike kuondoka akiwa ametuacha wawili mimi na mama.

    "Kitu gani hicho? Muda wa kukuona umeisha"

    "Kuhusu Michael" nikamtazama kwa makini mama kupitia machoni kwake "umejuaje kuhusu mauaji ya Beatrice naina maana unataka kusema kuwa Michael ndiye muhusika?"

    Nilimuona mama akiyatoa macho pima na akaunda tabasamu la uongo. Ndiyo tabasamu la uongo, tabasamu ambalo halikuwa na ladha yeyote ya raha niliona hivyo. Akanieleza "Mwanangu, zile ni hisia tu naomba uachane nazo hazina maana yeyote katika kesi hii ila ukweli ni kwamba nishakukataza mara nyingi kuhusu urafiki wako na Michael tuongeze maombi tu ili hii kesi ipate ufumbuzi lakini ni mbaya sana na imekukalia vibaya " akasimama kisha akaniambia "acha niende namuwahi baba yako, huenda akaja wiki ijayo"

    Sikuwa na sababu ya kumng'ang'ania mama anieleze chochote kwa kuwa mama alipoamua kufanya jambo lake, basi hakuna ambaye angeweza kumbadili mawazo yake, mama akaondoka.

    ....



    Zilipita siku kadhaa nikiwa mahabusu. Nikiwaza kila aina ya jambo linalonipitia kwa umakini zaidi. Nilitumia muda mwingi kuwaza mengi kipindi ambacho Vanessa aliukata mguu kuja kuzungumza nami. Ni hapo nilipofuatwa na yule askari wa kike na kunieleza jambo la kushangaza

    "Ramon wewe ni kijana mdogo sana uliyeingia katika matatizo ambayo si yako lakini anayepigana vita hii anajuta sasa kukuingiza wewe katika matatizo ya namna hii" kisha akanitazama kwa tuo kana kwamba alisubiri nimuulize jambo, akaniuliza yeye "je! Ukimfahamu utamsamehe?"

    "Siwezi kumsamehe abadani, amemuuwa mwanamke ninayempenda amenifanya nikose imani kwa watu wangu wote wa karibu siwezi kumsamehe zaidi ya mimi kumuua na yeye ili astahili linalomfaa"

    Nikamjibu kwa hasira kutokana na hali ambayo imenikuta na inayoendelea kunitafuna kutokana na kutokujua ukweli ambao umeniweka katika giza hili zito la kutofahamu kinachoendelea.

    Askari yule akabetua mabega yake kwa kebehi mimi nikaendelea na ratiba yangu ya siku hiyo.

    Siku hiyo nikiwa nimejipumzisha katika chumba changu baada ya chakula cha jioni, alikuja Vanessa. Niliingizwa katika chumba kile kile cha kila siku nikiwa najihisi huru zaidi. Tukasalimiana na Vanessa kisha akanitaka radhi kutoonana takribani siku nne.

    "Kulitokea nini hata usije?" Nikamuuliza

    "Nilikuwa katika uchunguzi wa awali juu ya ripoti ya kifo cha beatrice. Kwanza nikuulize, Beatrice alikuwa akinywa pombe?" Akanitazama akisubiri jibu langu. "Hapana si mnywaji kabisa"

    "Lakini siku ile alikunywa kutokana na furaha ya siku yenyewe? Na alikunywa akiwa na wewe au nani mwingine?"

    "Unajua Vanessa, nashindwa kuwa na jibu kamili juu ya swala hilo kwa kuwa hiyo habari ya kukutwa na pombe ndani ya mwili wake Beatrice na kuwa kama chanzo cha awali ya kifo chake nilisoma katika gazeti. Lakini ukweli wenyewe ni kwamba siku hiyo baada ya kutoka katika sherehe mimi na Beatrice nikamsindikiza mpaka pale kwao. Nilishuka katika gari nikamfungulia mlango na tukasimama pale getini kwao kama dakika ishirini au zisizopungua hizo. Kisha nikamuaga baada ya kuongea naye mengi juu ya mapenzi yetu. Hakuwa amekunywa pombe wala nini na nilihakikisha anaingia ndani ingawa ni mimi nilikuwa nimelewa siku hiyo"

    Vanessa akashusha pumzi ndefu kisha akatoa kalabrasha lenye karatasi kadhaa akalitupa mbele yake akafunua funua pale huku akijaribu kuzisoma karatasi kadha wa kadha akagota katika moja wapo. Akauinua uso wake na kunitazama, kisha akaanza kuongea

    "Ndani ya damu yake, kumekutwa pombe hiyo yenye sumu ya nyoka kwenye kilevi hicho iliyompelekea kumuozesha maini yake ghafla na kusimamisha mapigo ya moyo yaliyopelekea Beatrice kupoteza fahamu na kufa taratibu kabla hawajatenda unyama walioutenda wa kumtoboa tumbo kisu kile kikubwa kilichokutwa eneo la tukio huku alama ya vidole ikionekana ni ya mwanaume kisha wakamkata sehemu ya shingoni" kisha akanitazama kwa hali ya huzuni akaniambia "Beatrice ameuwawa kinyama sana, kwa yeyote aliyeyafanya yale, hastahili kuishi"

    Akaniangalia nilivyokuwa nikisisimuka kutokana na taarifa zile ikawa zamu yangu kuvuta pumzi nyingi kisha nikazitoa kama zilivyo, nilihamanika. "Sijuhi walimkosea nini mpenzi wangu" Nilisema kwa huzuni nikitazama karatasi ile mbele ya Venessa ambayo bila shaka ndiyo iliandikwa ripoti aliyonisomea.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Alama ya vidole katika nyumba na maeneo yote ya mauaji ni za mkono wa kiume kutokana na vina saba vilivyotoa ripoti yake ya awali" Vanessa akanitazama kisha akaniambia "kuna kila sababu ya kesi hii kuendelea kuwa ngumu kwako kwa kuwa unayehusishwa na mauaji haya wewe ni mwanaume"

    Hofu ikazidi kunipanda tumaini likapotea. Nikamuuliza Vanessa kwa unyonge “Na wamejuaje kama alama za vidole vile ni vya mwanaume?”

    “Ramon, hayo ni mambo ya kisayansi na ni ngumu kujibu kiurahisi lakini inawezekana kupimwa alama na kugundulika ni mkono wa mtu gani”

    Vanessa akanieleza huku akifunga kalabrasha lile lenye karatasi ya ripoti "Sasa tuachane na hayo tuendelee na maelezo yako. Kuhusu maisha yako chuoni mahusiano yako na Beatrice pamoja na Michael"



    Nikavuta pumzi kwa kile tulichotoka kuzungumza punde. Kiukweli mawazo ya kesi hii, yaliniumiza nafsi na kunifanya ninyong'onyee kila dakika jinsi majibu kadhaa yanayokuja juu ya upelelezi wa mauaji ya Beatrice. Nikatazama juu nikijaribu kukumbuka kila kilichotokea hapo zamani. "Kiukweli uhusiano wangu mimi na Michael ulipungua kama si kupotea kabisa. Alikuwa akinifanyia visa sana pale chumbani mpaka nikapaona pachungu"





    Vanessa akiwa anaitazama tepurekoda aliyoiwasha wakati naanza kuzungumza akanikatisha kwa swali "Visa gani alikuwa akikufanyia"

    "Kuna wakati nilikuwa nikikuta godoro langu lina maji, wakati mwingine nguo zangu nilizoziandaa kabisa nataka kuzivaa nazikuta kwenye beseni la kufulia, ni mengi ambayo si rahisi kuelezeka na kuisha ila ikafikia hatua mimi kuhama baada ya kukubaliana na Steven kuhama kuelekea kule jirani na ghorofa alilokuwa akiishi Beatrice. Maisha yangu mimi na Beatrice ndiyo yakazidi kuwa matamu haswa tulipokuwa na hakika ya kila siku kuonana na kila dakika tunayotamani kukutana hiyo ikazidi kumuumiza Michael"

    Vanessa akanihoji “Na je Beatrice alikuwa akifahamu ugomvi wenu?”

    “Ndiyo kwa kuwa ilikuwa ni ngumu kwa Michael kuficha chuki zake kwangu”

    Nikiwa nataka kuendelea kumuelezea mengine Vanessa, kwa kuwa hatukuendelea na uhasama ule mpaka tunamaliza chuo, nilimuona akitazama saa yake mkononi ilipobidi ninyamaze yeye akauinua uso wake kunitazama

    "Sasa muda umekwenda lakini jambo hili nitalifanya kesho. Unayo ramani ya nyumbani kwa Michael" Sikuwa nimemuelewa nikamjibu "Mimi sijuhi kuchora ramani za nyumba ya uswahilini kiasi kile" Vanessa akacheka na kujisahihisha pale alipohisi amekosea mpaka akanikanganya mimi. "Nina maana unapafahamu anapoishi Michael" Nikakenua meno nikitabasamu mara baada ya kumuelewa vizuri, nikamuelekeza.

    "He msewe? Kwani alikuja kusoma chuo cha Ud(University of Dar es salaam)?"

    aliniuliza kwa kuchanganyikiwa. "Hapana hakuwa na pesa na hapo nilimlipia mimi pesa ya pango kwa kuwa chumba hicho kilikuwa chumba cha rafiki yangu Nambode Issack Njinjo, yeye alipokuwa akihama alinieleza na mimi nikamchukulia Michael"

    "Ina maana Michael hakuwa na wazazi? Na ilikuwaje wewe umlipie wakati mlikuwa mna ugomvi?"



    Nilipotaka kumjibu, akanizuia. Akanyanyuka na kuanza kupiga hatua za kuondoka mara aliponiaga.

    "Kesho sitakuja ila nitakuja baada ya kesho kukueleza wapi nilipofikia na nitakusikiliza zaidi maana una zaidi ya kunieleza"

    Nilikaa siku hiyo bila kuwa na mawazo yoyote. Nahisi nilikwishazoea maisha ya humu ndani. Kwanza sikuona utofauti wa maisha haya na maisha wanayoishi watoto wanaoishi maisha ya kifahari ambayo hakuna uhuru lakini kila nilichokitaka nilikipata. Nikaenda kwenye meza iliyojaa vitabu huku nikitazama wingi wa askari walioletwa kunilinda. Wengi wao wakiwa wamebeba silaha nzito za moto.



    "Psiii"

    Nikamuita mmoja wapo aliyesimama mita chache namimi nilipokuwa nimekaa mimi.

    "Una fegi?" Hakuzungumza bali alitoa kasha la sigara aina ya embassy na kunipatia kiberiti cha gesi nikaiwasha kisha nikaanza kuuvuta moshi wake. Mimi sikuwahi kupenda kuvuta sigara lakini si kwamba sikuwahi kuivuta katika maisha yangu. Niliwahi kuvuta katika wakati ambao nilikuwa nimelewa ama nikiwa katikati ya marafiki zangu ambao sikupenda wanione kama mtoto wa mama sana.

    "Naomba kukuuliza jambo" hilo ndio likawa lengo langu la kuomba sigara "kwanini mnanilinda wengi tofauti na idadi ya askari wa mwanzo?"

    Yule askari akanitazama na wala hakuwa na dalili yeyote ya utu wema. Alionesha sura ya ukatili na mbaya kuliko nilizowahi kukutana nazo kisha akanijibu kwa mkato na sauti iliyojaa hasira

    "Wewe ufahamu fika kuwa wewe ni mtu hatari? Unataka kutoroka?"

    Nikajichekesha na wala sikujibu chochote. Nikaigeukia meza ile kisha nikakitwaa kitabu kimojawapo mezani pale hicho kiliitwa SIRI kitabu hiki sikuwahi kukutana nacho mtaani lakini kilinishangaza uhodari wa Vanessa jinsi alivyoweza kupambana na nguvu za giza katika kuwaumbua wauaji waliosababisha uchonganishi kati ya Khatib na Ubwa katamba.

    "Hapana inawezekana Vanessa ninayemsoma humu si huyu ninayekutana naye"

    "Ndiye" ile sauti ya askari wa kike ikanijibu nikageuka kumtazama. Alikuwa ameshika mkonga wa simu na kunipatia "Baba yako mzee Lameck yupo hewani"

    Niliipokea simu ile haraka haraka na kuiweka sikioni kwangu.

    "Halow, halow baba!" Nikaisikia sauti ya baba katika hali ya utulivu ikiniuliza naendeleaje "Naendelea vizuri baba mbona hujaja kuniona?"

    "Nitakuja mwanangu ila siendelei vizuri kiafya. Mama yako ameshakuja kukuona? Kuna chochote amekueleza kuhusu kesi yako?"

    "Hapana baba hajanieleza chochote kuna nini kwani? Maana nahisi kuna kitu anafahamu"

    "Usimwamini..."

    Simu ikawa imekatika na kuniacha njia panda. Niliita, baba baba kuhakikisha kama simu ilikuwa hewani, nilikuwa naongea na chombo kitupu.

    Nikiwa naitazama ile simu iliyokatikia sikioni mwangu kana kwamba ilikuwa na uwezo wa kuzungumza nikashikwa na bumbuwazi hata nisizungumze chochote kwa nusu dakika. Yule askari wa kike akanishika bega na kuniambia

    "Huna sababu ya kushangaa kwa kuwa ni mengi utasikia na mengi utaelezwa cha msingi ni kuvumilia kama mwanaume na kujua kuwa hayo ni majukumu yako na inabidi ujitetee kuondoa kitanzi ulichoandaliwa kwa ajili ya hukumu ya kunyongwa"

    Akanipokonya ile simu na alianza kupiga hatua za kuondoka. Nikamuuliza swali akasimama

    "Kitanzi? Ina maana hukumu yangu ni hiyo?"

    "Unadhani hukumu ipi inakufaa muuwaji wa mtoto wa kigogo?"Nikamuacha aende kwa kuwa nilihisi anazidi kunichanganya. Kasha nilijiuliza mengi ni vipi huyu askari ambaye aliondoka mara baada ya kunikabidhi simu na arudi akiwa anajua nini nimeambiwa? Japo hakunieleza kuwa amesikia lakini kwa jinsi alivyoongea nilielewa kuwa alifahamu kitu ambacho baba alinieleza na vipi aje mara baada ya simu kukatika? Nililala juu ya mikono yangu niliyoilaza juu ya meza nikaingia katika tafakuri fupi.



    'Mama anamjua muuwaji na anamuhisi ni Michael, mimi na Vanessa tumekuwa tukimuhisi Michael pia lakini baba anasema nisimuamini mama kama ameniambia kuwa anamfahamu muuwaji! Haya yote yanatoka wapi? Kwanini inakuwa hivi?'

    "Ahaaa"

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikapiga kelele mpaka wale waliokuwa wakinilinda wakashituka. Walikuja mbio kwa kuwa walikuwa hawakai ndani mara kwa mara, nyakati za usiku. Nyakati hizi huwa wanaongeza nguvu ya ulinzi huko nje. Niiwasikia wakizungumza

    "Ana nini huyo mwehu?"

    Nilipogeuka nikamkuta yule askari wa kike akicheka kisha akawajibu kwa kebehi huku akinitazama "Na amekuwa mwehu kweli, kwa kuwa ameanza kuongea mwenyewe" Sikujua kabisa kama yule askari alikuwa nyuma ya mgongo wangu sikujua kama nilikuwa nawaza kwa kuzungumza sikujua jamani! Sikujua mimi ah!! Nini sasa kilichokuwa kinataka kunitokea? Jasho jingi lilikuwa likinitoka na wala sikutambua nini kilikuwa kinaendelea katika kichwa changu. Ilikuwa ni hali mbaya kuliko kuumwa hata malaria.







    ITAENDELEA  

Blog