Search This Blog

Thursday, November 24, 2022

FACEBOOK IMEHARIBU MAISHA YANGU - 2

 

     

     



     Simulizi : Facebook Imeharibu Maisha Yangu

    Sehemu Ya Pili (2)

     

     



    Resh alipiga kelele ghafla gari ikayumba huku na huko,dereva akajaribu kwa uwezo wake wote kuirudisha barabarani "Paaaa!!" mlio mkubwa ukasikika.





    *******************?



    Adam alipokea ujumbe kutoka kwa Reshmail akiwa maeneo ya kijiweni barabara ya lami kuelekea chuo kikuu cha mtakatifu Augustino,kupitia shule ya wasichana ya Ngaza.Adam alikuwa pamoja na rafiki yake (Huha) katika pikipiki ya rafiki yao aliyekuwa amewaazimisha wazungukiezungukie maeneo.



    "Huha hebu endesha twende hapo Nyegezi kona kuna mtu nataka kuonana naye mara moja"



    Adam alimwomba Huha.



    "Tayari Halima ametuma meseji mwambie hatuna mafuta atufate na gari yake bwana"



    Alitania Huha huku akianza kuiondoa pikipiki taratibu



    "Ungejua hata usingesema wewe twende ukajionee maajabu ya mwaka" alijibu Adamu huku pikipiki ikizidi kushika kasi.



    Ndani ya dakika tano tayari walikuwa Nyegezi kona ambapo Huha alipaki pembezoni kidogo na barabara iendayo stendi kuu ya Nyegezi jijini Mwanza,Adam alielekea dukani kununua vocha,na Huha akasogea pembeni kidogo aweze kuvuta sigara yake.



    ***



    Dereva akiwa mwingi wa mawazo yake binafsi yasiyomuhusu Reshmail wala Eve na hata kama yangekuwa yanawahusu ule haukuwa muda muafaka wa kuwaambia.



    Macho ya Reshmail yalikuwa yamekutana na bango kubwa lililoandikwa "KARIBU CHUO KIKUU CHA MTAKATIFU AUGUSTINO" kwa hamu kubwa aliyokuwa nayo ya kumwona Adam ambaye alikuwa pia mwanafunzi ndani ya chuo hicho ndio sababu kuu ya kujikuta akipiga kelele kwa nguvu hali iliyomshtua dereva kutoka katika mawazo mazito na kujikuta akiyumbisha gari huku na huko hadi ilipokutana na pikipiki iliyokuwa imepakiwa pembezoni mwa barabara na kuirusha umbali ambao si wa kutisha sana,



    Iligeuka vurumai madereva wa teksi na bodaboda za pikipiki walikuwa wakali sana hawakutaka kusikia la mtu,wengine hasira za kukosa abiria tangu waingie kijiweni asubuhi walizihamishia katika tukio hilo.



    Usingekuwa upole wa yule dereva basi mawe waliyobeba wananchi yangeigeuza ile gari kuwa mkweche. Eveline alitelemka garini kwenda kumsaidia dereva kujitetea lakini Reshmail uoga ulimtawala akawa amejibana kwenye viti vya nyuma vya ile gari huku akitetemeka.



    "Mh! Adam hawezi kukosa mwenyeji maeneo haya ngoja nijaribu kumpigia,ah! hii safari imetawaliwa na mikosi dah!" aliwaza Resh huku akichukua simu yake kutoka katika kipochi chake.



    Lakini kelele zilizokuwa pale aliamini hawezi kusikilizana vizuri na upande wa pili,taratibu huku akitetemeka alifungua mlango akashuka na kuanza kutembea kuelekea pahali ambapo kidogo pametulia. Zaidi ya asilimia 50 ya wananchi wenye hasira eneo lile wakageuza vichwa vyao kuangalia kazi ya Mungu ilivyotendeka vyema katika mwili wa Reshmail,



    Badala ya kumpigia kelele dereva,miluzi mikali ikiongozwa na dereva mkongwe wa teksi eneo lile ndugu Sanya Bonda ikahamia kwa Reshmail,



    Resh akajifanya kama hasikii vile "Ilikuwa haki ya dereva kupotea njia jamani" Bonda alisema kwa sauti ya juu na kugeuza hasira za watu kuwa vicheko. Resh taratibu akaufikia mti mdogo mbali na eneo la tukio akabonyeza namba za Adam.



    Simu iliita muda mrefu bila kupokelewa. Alipopiga mara ya pili simu ilipokelewa.



    "Helow Resh subiri nisogee pembeni nakupigia kuna tatizo limenipata" alijibiwa na Adam katika simu.



    "Hata mi....." kabla hajamalizia kauli yake Reshmail simu ilikatwa akiwa bado anaduwaa kama dakika mbili pembeni yake alizengea kijana mmoja ambaye Resh hakutaka hata kumwangalia machoni,alijua ni walewale waliokuwa wakipiga miluzi na kumwita majina waliyotaka.



    Resh taratibu akajisogeza pemben.



    "Vipi dada mbona wanikimbia au mi nanuka halafu we mrembo haya basi umebarikiwa sana najua unataka kusifiwa" aliongea yule kijana lakini Resh hakujibu.



    Simu yake ya mkononi iliyokuwa katika mfumo wa kimya(Silence mode) ilikuwa inatoa mwanga kuashiria aidha kuna ujumbe umeingia au kuna simu inaingia,lakini kwa jinsi alivyoandamwa na yule kaka kwa maneno hata hakuweza kugundua.



    Baada ya dakika kadhaa akaondoka yule kaka ndipo kuangalia simu akagundua ilikuwa imeita mpaka imekata na hakuwa mwingine bali ni Adam alikuwa amepiga,harakaharaka akapiga tena.



    Ulikuwa mshangao wa hali ya juu sana Reshmail hakuamini alipomwona yule kijana aliyekuwa ametokea pale dakika chache zilizopita kuelekea kwenye zile vurugu ndio anapokea simu.



    "Resh mbona nimekupigia hupokei mamaa" alimshuhudia yule kaka akiongea kwenye simu huku akirejea lile eneo kukwepa kelele,kama ilivyo kwa mtu aliyenaswa na umeme Reshmail alikuwa ametulia tuli na simu sikioni huku yule kaka akizidi kulikaribia eneo lile



    ?Reshmail mbona huongei!!? aliendelea kuuliza bila kupata majibu.



    "Adam"



    Alijitutumua Resh na kutamka akiwa jirani naye kabisa,bila kujua yule kijana akaangusha simu yake hakuamini msichana aliyetoka kuongea nae dakika kadhaa ndio Reshmail wa Arusha.





    Vurumai lilisawazishwa haraka sana Adam na Huha ndio waliokuwa wamiliki wa ile pikipiki iliyogongwa na gari waliyokuwemo akina Reshmail.



    "Jamani huyu hapa ni dada yangu,ndio alikuwa amenipigia simu tuonane hapa naomba haya mtuachie sisi"



    Adam aliuambia umati ule ambao hasira zao zilikuwa zimeanza kupoa na haraka walimwelewa wakaacha kumzonga dereva.



    Reshmail bila kupoteza muda akamwongoza Adam wakaingia garini akampa pesa taslimu shilingi laki tatu kwa ajiri ya matengenezo ya ile pikipiki naye Adam akamkabidhi Huha kisha akajumuika na Eve pamoja na Reshmail katika gari,huku Reshmail akiwaacha watu hoi kwa uzuri wake wa asilia ambao hata Adam alikuwa amechachawa nao na kukubaliana na ukweli kwamba picha zilizotumwa zilikuwa za Resh kweli.



    ***



    Bi Gaudensia alifika Dar-es-salaam majira ya saa tatu usiku,bado alikuwa hajaridhika kumaliza siku yake bila kuongea na mwanae,hivyo punde tu baada ya kuingia chumbani mwake aliamua kujaribu kupiga namba za simu za Reshmail ambazo zilikuwa hazipatikani siku nzima.



    Furaha aliyoipata ilikuwa haisimuliki,pale simu ilipoita upande wa pili"Mh! kalala nini huyu?" alijiuliza simu ilivyoita kwa muda mrefu bila kupokelewa,lakini mara ikapokelewa



    "Helow! samahani Reshmail amelala"



    sauti ya kiume ilijibu baada ya kupokea kisha simu ikakatwa na kuzimwa.



    Mama Resh hakuamini kuwa amesikia sauti ya kiume katika simu ya mwanae alidhani amekosea namba lakini alipohakikisha zilikuwa zenyewe,wivu mkali ukamshika,akajaribu kupiga mara nyingi lakini bado hali ilikuwa ileile simu ilikuwa imezimwa usingizi ulipaa,alitokwa na jasho,hisia mbaya zikamvuruga na kufanya kichwa chake kiume sana,mama huyu alikuwa amejisahau kabisa kuwa Reshmail ni mwanae wa kumzaa, alizurura kama mtu anayetafuta kitu ambacho amesahau alipokiweka pale chumbani,alitamani kupiga kelele lakini aliamini hazitasaidia kitu.



    ***



    Reshmail akiwa usingizini Adam pembeni yake,yeye(Resh) alikuwa hoi kwa uchovu wa safari na misukosuko yote waliyopitia,na alipomaliza kuoga tu na kupata chakula alisinzia,hata simu yake ilipoita hakuisikia hata kidogo na hata angeisikia asingeweza kunyanyuka kupokea



    "Resh ni kipetito anapiga" Adam alimuuliza Resh aliyekuwa hoi kitandani.



    "Ah! ni rafiki yangu mwambie nimelala" alijibu kwa taabu akiwa hata hajui anachokiongea.



    Naye Adam bila kugundua kwamba Resh hajui anachokisema na ile namba ni ya mama yake Resh alipokea na kuzungumza





    Kitendo cha Adam kumkuta Reshmail akiwa bado ni bikra kilimzuzua sana,mapenzi yake kwa Halima yalipungua sana na kuisha kabisa hatimaye.



    Siku tatu mfululizo walizotumia pale Millenium Hotel zilitosha kuvunjilia mbali penzi la Adam na Halima na kujenga penzi imara kati ya Adam na Reshmail.



    "Mwezi wa pili uje ujitambulishe nyumbani Adam yaani siwezi kusubiri kwa kweli nakupenda Adam wewe ni mwanaume wangu wa kwanza na ninakuahidi nitajitunza kwa ajili yako"



    Reshmail alikuwa anamsisitiza Adam siku alipokuwa amewasindikiza uwanja wa ndege tayari kwa wawili hawa kurejea Arusha shuleni.



    "Mama anapiga! Eve" Resh alimwambia Eve pale simu yake ilivyoita.



    "He! usiniambie huyo ndio mama,sasa mbona ulikubali niongee nae usiku ule? aliduwaa Adam.



    "Eti! uliongea nae? Yesu wangu!"



    alishtuka Resh lakini Eve akamshauri azime simu kwanza mengineyo watajua mbele kwa mbele naye Resh akatii amri hiyo haraka akaizima simu bila kupokea Resh kwa kiasi kukuwa alikuwa amemzoea na kumwamini Eve.



    Adam,Resh,na Eve waliagana kama watu waliofahamia na kukaa pamoja siku nyingi sana,Resh alimkumbatia Resh alimkumbatia Adam kwa muda mrefu hadi Eve alipowatenganisha na kuambiana Kwaheri.



    ***?



    Ilikuwa imebaki miezi minne wafanye mtihani wa kumaliza kidato cha tano,Resh akiwa amekolea katika penzi la Adam na kusahau kuhusu Mama yake ambaye alikuwa amezuiwa na mwanaye huyo kwenda pale shuleni kumsalimia kwa madai kwamba yeye(Reshmail) anataka ajikite zaidi katika masomo.



    Reshmail kwa maksudi akabadilisha namba yake ya simu ili mama yake asiweze kumpata mara kwa mara badala yake muda mwingi akawa anawasiliana na Adam.



    Mwezi wa pili ilikuwa ni likizo ya mwezi mzima kwa wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita na pia wakati huohuo wanafunzi wa chuo kikuu cha mtakatifu Augustino huwa katika mapumziko mafupi baada ya kumaliza muhula(Semister) ya kwanza.



    **********************?



    Kwa Reshmail ulikuwa wakati muafaka wa kumtambulisha Adam kwa wazazi wake jambo ambalo aliamini lingesaidia kupunguza makali ya mama yake. Tangu akiwa mtoto kamwe hakuwahi kuwakwaza wazazi wake kwa sababu ya wanaume hata siku moja hivyo alitegemea hawatampinga.



    Ilikuwa siku ya furaha kubwa sana kwa Bi. Gaudencia na familia yote kwa ujumla kumwona tena Reshmail nyumbani baada ya miezi mingi tena akiwa mwingi wa furaha. Lakini tofauti na mama yake alivyofikiria kwamba mwanae huyo anafurahia kurudi katika ulimwengu wao wa mapenzi haramu yeye(Reshmail) alikuwa anafuraha ya kumtambulisha Adam ndani ya siku chache.



    Kwa kujua wazi kabisa mama yake atachukizwa na maamuzi yake hayo,Reshmail aliamua kulifikisha hilo mbele ya Mzee. Manyama ambaye ni baba yake.



    "Kwa sababu ni uchumba tu na hakupeleki popote hamna tatizo hata kidogo,mlete tu mwanangu mlete una maamuzi mazuri sana sio kama wasichana wengine wanafanya upuuzi kimyakimya mambo yanapokuwa mabaya ndio wanasema" alijibu mzee.Manyama huku akimshika mwanae huyo shavuni,



    Resh akatabasamu na kumkumbatia baba yake



    "I love you dad(Nakupenda baba)" Resh akamwambia kwa furaha tele mzazi wake huyo,huku moyoni akijiaminisha kwamba hapatakuwa na kikwazo tena kwa mama yake kwani baba ndiye kichwa cha familia.



    Baada ya siku tano Adam aliwasili ndani ya kasri la mbunge huyu.Alikuwa anaogopa na hakuamini kama angepokelewa na kama angepokelewa alijua yatakuwa mapokezi mabaya sana kwani katika simulizi mbalimbali anazozisikia kwa watu zilimwonyesha kwamba ni vigumu sana kwa wazazi kumwelewa mtoto wa kike linapokuja suala la kumtambulisha mwanaume kama mchumba wake.



    "Da Rosemary nina hofu mie" Adam alimwambia dada yake kipenzi waliyekuwa wameongozana naye



    "Acha uoga bro mbona hata sisi babu yetu alikuwa chifu? kwani chifu na mbunge nani zaidi" alitania Rosemary kumwondoa hofu kaka yake.



    Mapokezi waliyoyapata kutokea kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo yaliwashangaza mno waliwakuta watu wa kuwapokea na kwenda nao kwenye gari mbili walizokuja nazo,waliwafikisha hadi getini ambapo kina dada wawili kwa heshima kabisa waliwaongoza hadi sehemu maalum iliyoandaliwa kwa ajili yao,japo usoni waliuficha mshangao wao lakini moyoni uliwajaa tele.



    Adam akiwa ndani ya suti nyeusi wanazotumia wanasheria katika shughuli zao na Rosemary aliyevaa suti pia walielekezwa wapi walipo wazazi wa Reshmail wakaenda kutoa salamu zao,ilikuwa ni hafla kubwa sana ndugu,jamaa na marafiki wapatao miamoja walikuwa wamealikwa na mheshimiwa huyu. Ilikuwa kama harusi kwa asiyejua lakini ulikuwa utambulisho tu.



    Bwana na bibi Manyama walipendeza kwelikweli na walikuwa na kila haki ya kuitwa wakwe na Adam. Furaha ya Bi. Gaudencia ilificha chuki aliyokuwa nayo moyoni dhidi ya Adam kwa kumchukua mwanae ambaye ndio alikuwa anampa raha zote za dunia.



    Hadi hafla inafikia tamati majira ya saa mbili usiku kila mtu alikuwa amepata furaha kubwa sana,wabunge na madiwani ambao ni marafiki wa karibu wa Manyama walitoa zawadi nyingi kwa wawili hawa huku babu yake Reshmail akitoa mawaidha yenye maana kubwa sana katika maisha waliyotarajia kuyaishi Reshmail na Adam siku za usoni.



    Mzee Manyama kwa ombi la mwanae aliwasiliana na wazazi wa Adam kuwa muda wa mapumziko ya siku tano alizobakiza Adam amalizie katika familia yake,hapakuwa na kinyongo wala kipingamizi chochote walikubali kwa moyo mmoja na Adam akaendelea kuishi pale huku dada yake akirejea Mwanza kwa usafiri wa ndege ambao gharama zote zilikuwa juu ya mheshimiwa Manyama.



    Kila alipowasiliana na wazazi wake Adam hakusita kuelezea upendo wa kipekee anaoupata kutoka familia ya Reshmail hata wao walifarijika sana.



    ***********************

    Ilikuwa jumapili moja tulivu sana baada ya kutoka kanisani familia yote akiwemo pia Adam,baba yake Reshmail aliongozana na mwanae kwenda mjini kwa lengo kuu la kuonana na walimu mbalimbali wa masomo ya ziada(Tution) watakaompendeza Reshmail basi waweze kumfundishia nyumbani.



    Huku nyuma alibaki Adam pamoja na mkwewe (Mama Reshmail) baada ya kupata kifungua kinywa Adam alimwaga mkwewe kuwa anaenda kuzungukazunguka bustanini



    "Tena nilitaka nikwambie leo unataka uondoke hata bustanini hujawahi kufika,afadhali nenda mwanangu" alijibu mama Reshmail.



    Ulikuwa mpango kabambe uliosukwa na Bi. Gaudencia,kwa dhumuni kuu la kumwondolea mamlaka Adam ya kuwa na Reshmail. Kwa kuwatumia vijana kutoka katika ngome ya vigogo,ngome maalum iliyokuwa inatumiwa na watu wenye pesa zao kwa ajili ya kuwatenda vibaya watu wanaoonekana kuingilia mambo yao aidha kimapenzi au kibiashara.



    Alipoaga anaenda bustanini Gaudencia alitumia fursa hiyo kupiga simu kwa wanaume hao wa shoka ambao tayari alikiwa ameelewana nao bei.



    "Ndani ya dakika tano tutakuwa hapo" ndio jibu lililotolewa upande wa pili

    Bila kuongezea lolote Bi.Gaudencia alikata simu yake na kutoka nje.



    "Babu kwa mama Veneranda si unapajua?" alitoa swali hlo Bi. Gaudencia kwenda kwa mlinzi wao wa getini.



    "Ndio si yule mama anayesuka pale mbele"



    "Hapo hapo haya haraka nenda kaniangalizie kama kuna foleni kubwa" aliamrisha Bi. Gaude na mlinzi akatii amri hiyo haraka haraka akaondoka katika lindo lake akaenda kutimiza amri ya bosi wake.

    Baada ya dakika takribani kumi alirejea mlinzi yule



    "Yupo mmoja tu anamaliziwa" alileta taarifa hiyo kwa furaha.



    "Haya mi ninatoka nimemwacha Adam ndani amelala akiamka mwambie nimetoka kidogo" alisema mama Reshmail huku akiondoka.



    "sawa bosi nitamwambia"



    Masaa mawili badae alirejea akiwa amesukwa tayari nywele zake,ni muda huohuo Reshmail na baba yake walikuwa wametoka mizungukoni, walimkuta Gaudencia anatokea ndani.



    "Babu Adam alivyoamka ameenda wapi? au bustanini?"Aliuliza Gaudencia na kuongezea



    "Maana nimegonga chumbani kwake kimya, hebu Reshmail ingia ukamwangalie ndani mwake humo huenda amelala bado" kwa mwendo wa maringo lakini harakaharaka Reshmail alijongea ndani.



    "Babu unasema Adam hajatoka?" Resh aliuliza baada ya kurejea akiwa na hofu kidogo usoni.



    "Hajatoka na mimi hapa sijatoka tangu mama alipoenda kusuka na kumwacha Adam amelala" alijieleza mlinzi yule jibu lililopokelewa kwa furaha na Bi.Gaudencia.



    Jambo gumu zaidi kwa ambao hawakujua janja ya mama huyu ni kwamba simu ya Adam ilikuwa haipatikani hali hiyo ilileta wasiwasi sana, walisubiri huenda atarudi hadi jioni hali ilikuwa tete ndipo mzee Manyama alipoamua kupiga simu kituo cha polisi maeneo ya jirani kwa sababu alikuwa mbunge msako ulianza usiku huohuo.



    Siku tatu zilipita bila taarifa yoyote kutoka katika kituo cha polisi,Reshmail alikuwa amepooza sana kupita maelezo mara kwa mara alimpigia baba yake simu na kuuliza kulikoni lakini jibu bado lilikuwa lilelile kuwa hajapatikana.



    "Mama niache tafadhali,tena niache nasema upuuzi wako siutaki tena niache!" alifoka Reshmail pale mama yake alivyomkuta amekaa sebuleni na kujaribu kumpapasa huku akimpa pole ya kupotelewa na Adam wake ghafla.



    "Mwanangu usiwe na hasira kiasi hicho polisi watafanikisha upelelezi na watamrejesha Adam akiwa mzima wa afya" alibembeleza Bi. Gaudencia lakini Reshmail hakujibu kitu akajiondokea akiwa ameuvuta mdomo wake sana.





    Siku ya tano polisi waliopewa jukumu la kufanya upelelezi huo walirejea na taarifa yao huku wakiambatana na ushahidi. Zilikuwa nguo aliyokuwa amevaa Adam kwenda kanisani ikiwa na matundu sita ya risasi na ikiwa imetapakaa damu pote, suruali ilikuwa na matundu matatu ya risasi.



    "Hapana hawezi kuwa Adam hata kidogo nasema hawezi kuwa yeye" alifoka Manyama huku akiwa wimawima mbele ya mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai jiji la Dar-es-salaam Chacha Boniphace au maarufu kama Chacha B.



    "Mheshimiwa lakini huu ni upelelezi wa awali tunaendelea zaidi na zaidi tutazidi kutoa taarifa kadri tunavyopata majibu mapya" alijieleza kwa utulivu bila wasiwasi kabisa jambo ambalo kidogo lilirejesha amani ya Manyama japo hofu tayari ilishaukumba moyo wake kwamba huenda Adam ameuwawa tena kikatili.



    Ilikuwa ni shughuli pevu kwa Reshmail kuamini kile ambacho alikuwa anaelezwa na baba yake kwamba Adam anadhaniwa kuuwawa kwa risasi nane kisha mwili wake hauonekani. Bi. Gaudencia tayari alikuwa anaangua kilio kikubwa hata kabla maelezo hayajaisha ikawa kazi kwa mumewe kumbembeleza.



    "Mke wangu Adam hajafa ila inadhaniwa pia upelelezi bado unaendelea jamani,ukilia hivyo unakuaribisha msiba mama watoto sawa" alibembeleza mzee Manyama huku amemkumbatia mkewe.



    "Baba haiwezekani baba haiwezekani nguo za Adam zipatikane katika hali hiyo halafu mnasema hajafa,jamani Adam wangu wamemuua"



    alipiga mayowe Reshmail ikamlazimu mzee Manyama kufanya kazi mara mbili jambo ambalo lilimtoa jasho mzee huyu.



    "Reshmail mwanangu,tulia hiyo siyo taarifa rasmi jamani ni majibu ya awali mbona mnanifanyia hivyo au mnataka nipate presha nife?" alijieleza Manyama huku akijifuta jasho kwa kutumia shati lake.



    Reshmail mbio mbio akaondoka pale sebuleni akaanza kuzipanda ngazi kuelekea chumbani kwake huku akilia,mzee Manyama nae huyo nyuma yake.



    "Reshmail mwanangu,njoo malkia wangu,njoo mwanangu"



    aliyazungumza hayo huku akimkimbiza kwa nyuma. Wakati huo Bi. Gaudencia tayari alikuwa amenyamaza kimya kabisa,akijaribu kupikicha macho yake.



    Reshmail hakusimama hadi chumbani kwake akajifungia,baba yake alibembeleza mpaka akachoka hakupata jibu zaidi ya kilio cha kwikwi kutoka ndani.



    "Baba Resh twende chumbani mume wangu,twende utakaa hapa hadi saa ngapi cha msingi tumwombe Mungu asije akajidhuru mwanetu"



    Gaudencia alimnyanyua mumewe wakajikongoja kuelekea chumbani kwao,Manyama akiwa amelegea kabisa.

    Asubuhi ya siku iliyofuata naibu waziri wa ulinzi na usalama,alifika na msafara wake wa magari matano kwa mbunge Manyama kuja kutoa pole ya kutokewa tukio hilo lenye utata kwa mwenzao.



    Shughuli ngumu iliyokuwa mbele yao ni jinsi gani watawaeleza wazazi wake Adam ambao hadi dakika hiyo waliamini Adam yupo salama na mwenye furaha kwa mchumba wake Reshmail,Manyama alimuomba waziri ashughulikie hilo suala na bila kupoteza muda alinyanyua simu yake ya mkononi na kutoa taarifa hiyo kwa mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Mwanza pamoja na mawasiliano anayoweza kumpata baba yake Adam.



    Ilikuwa vigumu sana kwa baba Adam kuelewa anachoelezwa lakini kwa kadri ya uwezo wake na taaluma yake mkuu huyo alifanikiwa kumwelewesha ambapo baba yake Adam aliondoka akiwa na matumaini kwamba ipo siku Adam atapatikana.



    Nyumba nzima ya kina Adam ilipooza sana dada yake Adam (Rosemary) alikuwa analia muda wote kwa uchungu hakuamini kwamba siku ile pale uwanja wa ndege alivyosindikizwa na familia nzima ya mhe.Manyama ndio ilikuwa mara ya mwisho kumwona kaka yake kipenzi(Adam).



    Uongozi wa polisi uliifikisha taarifa hiyo pale chuoni ambao pia walipokea kwa simanzi kubwa.



    "MAUAJI YA KUTISHA",



    ndivyo mandishi meusi kabisa kwenye magazeti mbalimbali yalisomeka,hali hiyo ilithibitisha kabisa kuwa Adam hayuko hai tena.



    Picha yake iliyoambatanishwa na habari hizo akiwa na mtoto wa mbunge iliteka na kuumiza mioyo ya watu wengi hasahasa vijana.



    "Tumempoteza mwanasheria"



    ndilo neno la pamoja walilosema wasomi wa chuo kikuu cha mtakatifu Augustino Mwanza katika misa ya pamoja kumwombea mema Adam kama yupo hai au kumtakia pumziko jema la milele kama tayari Mungu ameichukua roho yake,kila uso ulikuwa na simanzi kubwa ilikuwa kama tamthilia.



    Reshmail alikuwa kama zezeta,hamwelewi mtu yeyote,roho yake ilimwambia kwamba mama yake mzazi anahusika kwa namna moja au nyingine katika tukio hili lililojaa utata.



    Lakini ataanzia wapi kumweleza baba yake,atajisikiaje mzee Manyama akigundua kwamba mke na mtoto wake walikuwa katika ndoa haramu ya siri ndani ya nyumba yake.



    "Hapana sitaki kuongeza tatizo juu ya tatizo nitasubiri liwalo na liwe,kama Mungu alimpanga Adam awe wangu naapa sitaolewa na mwingine kamwe,lakini kama hakuwa halali yangu basi ataletwa mwanaume duniani kwa ajili yangu tena"



    Alijipa ujasiri wa hali ya juu Reshmail huku akijipigapiga kifuani.



    "Nitarejea shule na nitasoma tena kwa bidii sana,sitamwaza mwanaume yeyote tena alikuwa Adam na atabaki kuwa Adam hadi Mungu aamue tena"



    aliendelea kujipa matumaini.

     

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog