Search This Blog

Thursday, November 24, 2022

NILIVUNJA NDOA ZANGU 3 KULIPIZA KISASI - 1

 

     

     

     

    IMEANDIKWA NA : IRENE MBOWE



    *********************************************************************************

    Simulizi : Nilivunja Ndoa Zangu 3 Kulipiza Kisasi

    Sehemu Ya Kwanza (1)

     

     KISA CHA KWELI ,,,,



    Charlote, mwanamke aliyeishi kwenye ndoa yake kwa miaka 5. lakini baada ya kukutana na changamoto za ndoa ambazo alishindwa kuzivumilia na kujikuta kuwa na kisasi rohoni,  Sasa aliamua kulipiza kisasi hicho na kupelekea kuvunja ndoa tatu.



    Hembu msikilize Charlote anachokisimulia. Hii inaweza kukusaidia sana  katika maisha yako kutokuwa na kisasi moyoni.



    ONYO.. HURUHUSIWI KUNAKILI.. HAKI ZOTE ZIMEHIFADHIWA.



    SEHEMU YA KWANZA.



    Nimelelewa kwenye mazingira ya maisha ya utulivu na amani. Wazazi wangu walipendana na kuheshimiana sana. Na kutufanya sisi watoto wote kuwa na heshima na kupendana . lakini pia kujali jamii iliyotuzunguka na kuishi kwa adabu sana.

    Nilipata bahati ya kupata elimu nzuri na ya viwango. Wazazi wetu walitusomesha, tena shule zenye hadhi na gharama kubwa mno.

    Nikiwa kidato cha pili , Mtoto wa mzee ambaye ni family friend na sisi aliingia kidato cha tano katika shule niliyosoma. Hivyo kijana huyu Jones tuliheshimiana sana. Alinipenda na nilimpenda wote tulipendana na kuhurumiana na kuheshimiana.

    Wengi shuleni walijua sisi ni family friends, na hivyo kila mmoja ni kama alikuwa akimchunga mwenzake. Jones aliogopa kufanya upuuzi akiamini ni lazima ningemsemea nyumbani, lakini na mimi pia niliogopa kufanya upuuzi nikiamini kabisa jones angenisema Nyumbani.

    Hivyo Jones na mimi tukajulikana kama wana ndugu haswa haswa, na heshima ikawepo. Sikuwa na utani wala mizaha na watoto wa kiume.. hii ni kwa Vile Jones alikuwa akinifuatilia sana. Lakini na mimi nilimfuatilia sana kuhusu kuwa na mazoea na mabinti na hivyo aliogopa pia nay eye.

    Wengi walisema Jones na Charlote ni ndugu. Wengi wa vijana walimtania Jones na kumwambia mwenye dada hakosi shemeji. Na Jones alichukia sana.

    Tuliendelea kupendana sana.

    Baada ya kumaliza masomo ya Secondary Jones alienda kujiunga na chuo wakati mimi nikiendelea na masomo ya Secondary. Lakini tuliendelea kuwasiliana sana. Na hatukutupana hata kidogo.

    Alinipenda na kunikumbuka kila mara.

    Nilipomaliza kidato cha sita, yeye tayari alikuwa ameshaanza kazi ya kuajiriwa.

    Na sasa nilikuwa najiandaa na mimi kuanza chuo.

    Nakumbuka siku moja alinipigia simu na kunitaka tukutane tuzungumze. Wana familia walijua urafiki wangu na Jones. Hakuna aliyekuwa na mashaka juu ya urafiki wetu. Kila mmoja alitupenda na kutufurahia kwa urafiki wetu.

    Nilimpa ahadi Jones ya kukutana na mimi. Kwanza nilishangaa sana kwa namna ambavyo alikuwa kabadilika. Alikuwa kanawiri sana, kawa na hali ya utu uzima zaidi na pia alionekana ni kijana ambaye alikuwa na pesa.

    Tulikutana na kukaa mahali kwa ajili ya kuzungumza.

    Kitu cha kwanza aliniuliza …

    Charlote,,, je una rafiki ama mpenzi?

    Nilitabasamu sana kwani moja kwa moja nilianza kuona akili yake ikiwa inanihitaji kuwa mpenzi wake. Ni kweli sikuwa bado nina mahusiano. Na hii ni kwa vile nilikuwa sitaki kuwakere wazazi wangu na nilitamani mahusiano nitakayokuwa nayo yaishie kwenye ndoa ni we mke wa mpenzi nitakaye kuwa naye. Badala ya kubadilisha mara huyu ama huyu kama nilivyokuwa nikiona wengi. Hivyo niliamini nitakapofikisha umri mkubwa ndipo nianze mahusiano. Wakati huo nilikuwa na miaka 20 wakati Jones akiwa na miaka 26.

    Aliniuliza kwa kusisitiza tena, je una mpenzi?

    Nilimjibu hapana sina mpenzi na si hitaji. Ni kama hakamini.

    Ila akaamua kufunguka na kuniambia kwamba,, hata yeye hana mpenzi na hana mahusiano, ila amekwua na marafiki kama marafiki lakini amegundua kwamba marafiki hao hawana viwango avitakavyo. Na aliogopa kunieleza kwani alifikiri tuna mahusiano ambayo yasingeweza kuruhusu sisi kuoana.Ila baada ya kuongea na wazazi wake walimruhusu na kumueleza kama Charlote atakubali kuwa mchumba wako haina neno. Hivyo akaamu akusitisha urafiki wowote na hivyo kuja kuniuliza kama niko tayari.

    Nilishindwa kutoa jibu la haraka kwani sikuwa tayari ninamhitaji. Alionekana ni kijana nadhifu, msomi na mwenye upendo. Lakini bado sikuwa na hitaji mpenzi, hivyo nilimueleza sina mpenzi na sihitaji mpenzi. Na nilimueleza kwa nini sihitaji mpenzi, na sababu mojawapo ikiwa ni kwamba natamani mpenzi nitakayekuwa na mahusiano naye awe mume na sio kuwa na wapenzi wengi wa kila mara.

    Jones alinitazama na kuonyesha anamaanisha anachotaka kukisema.

    Aliniambia,, Sharlote wewe ni msichana mrembo sana, na ukweli ni kwamba nakupenda sana, na kwa vile sasa hatuna uhusiano wa kindugu kama nilivyofikiri natamani kama ungekuwa mpenzi wangu kisha uwe mke wangu.

    Nilimtazama na nilifahamu kabisa kwamba Jones anamaanisha mimi kuwa mpenzi wake. Sikuwa na historia mbaya ya Jones hata kidogo. Lakini bado sikuwa na sababu ya kumkubali. Bado jibu langu lilikuwa ni mapema sana, nahitaji kusoma na kuwa na kazi ndipo maswala ya mapenzi niyaanze.

    Aliniambia anaweza kunisubiri na kunihakikishia kwamba nikimkubali nitasoma, nimalize nipate kazi ndipo anioe. Kama hilo ndilo ningelihitaji.

    Nilitabasamu na kumwambia ni mapema mno sina jibu la kumpatia ila asubiri.

    Aliniambia Charlote tafadhali najua mapema utaenda chuo. Hivyo endapo utakuwa na maamuzi ya kuwa na mahusiano usinisahau, ninakuahidi sitakuwa na mahusiano mpaka utakaponieleza msimamo wako .

    Tulimaliza maongezi yetu na kila mmoja akaondoka.

    Siku hiyo ilikuwa ngumu sana kwangu, kwani sasa nilianza kuwa na shauku ya kuwa na mpenzi. Niliyatafakari maneno ya Jones usiku kucha. Nikiamini kabisa alikuwa anamaanisha anachokisema.

    Nilipokuwa naendelea kutafakari aliniandikia msg na kuniambia,,, CHARLOTE TAFADHALI KABLA HUJAAMUA KUMPA MTU NAFASI NAOMBA UNIFIKIRIE MIMI, NAKUPENDA SANA, NAKUFAHAMU NA NINGETAMANI UWE MKE WANGU . WEWE NI MZURI SANA NA MREMBO MNO, BADO SIJAONA MWANAMKE MZURI NA MREMBO KAMA WEWE.

    Nilipomaliza kusoma msg ile niliisave ili iwe kumbukumbu yangu, ni msg ya kwanza ya kimapenzi kuipokea yenye nguvu na heshima. Si kama nilizozoea kusipokea za kishenzi na kipuuzi puuuzi.

    Hivyo niliisave.



    SEHEMU YA PILI.

    Muda wa kwenda chuo ulifika. Wazazi wangu walinipenda sana, hivyo walinitafutia chuo kizuri na nilichokipenda Nchi jirani. Nilianza masomo yangu ya Usekretari. Lengo langu ni niwe na kiwango kikubwa cha taaluma hii. Wengi waliniambia Charlote wewe ni mrembo sana, unapendeza sana ukifanya kazi kwenye maofisi makubwa. Urembo wako na kazi ya usecretari vitakufaa sana. Kila mtu aliniambia hivyo, na hata nilipokuwa shule ya sekondari kila mmoja aliambia hilo, hivyo nikajikuta natamani sana Taaluma hii. Hivyo nikiwa nchini Nairobi niliisoma vyema na kuhakikisha nafaulu vyema.

    Niliipenda sana Taaluma hii, na nilifanya vizuri sana.

    Tuliendelea kuwasiliana na Jones, nilimueleza ninachokifanya. Na bado nikiwa mwaka wa kwanza chuoni bado sikuwa nimemueleza kuhusu suala la mimi kumkubali yeye kuwa mpenzi wangu.

    Lakini nikiwa Nairobi nilikuwa na kijana rafiki tu ambaye ni Mtanzania, isipokuwa naye alikuwa ni rafiki na si mpenzi. Na sikumpenda kama mpenzi ila rafiki ili niwe na mtu wa karibu mtanzania mwenzangu. Hivyo niliamua kuwa na urafiki naye wa karibu nikiamini kuwa na mwanaume rafiki nitakuwa salama.

    Nilipendeka sana chuoni, wanaume wengi walinipenda na kunitamani, lakiini bado msimamo wangu ulikuwa pale pale sihitaji mpenzi wa kuniacha, ila mpenzi ambaye atakuwa mume.

    Muda ulipita nikiwa chuoni , na nilisifika kwa tabia njema na kujiheshimu, wengi walinifurahia na hawakuweza kuwa kama mimi kwani walikwua na tama sana.

    Nakumbuka siku moja nikiwa hostel. Nimejilaza. Rafiki yangu Penina, msichana wa Kinyarwanda ambaye tulipenda sana, na wengi walisema tumechaguana warembo,, alikuja kuniamsha na kuniambia .. Charlote,,, uko na mgeni, kijana handsome sijui katoka wapi ila ana sound kama mtzedi… he is outside anakusubiri kwa nyumba ya wageni ukaonane naye…

    Mh… haraka nilijua huenda ni kaka zangu na si mtu mwingine, wazo halikuwa kwa Jones kabisa.

    Dah.. sikuamini kwa kadiri nilivyokuwa nikisogeza hatua zangu.. nilimuona kabisa ni Jones,, nilianzakupata furaha sana moyoni. Nilimsogelea na kumkumbatia kwa furaha kama mtu na kaka na dada yake. Nilifurahi sana kumuona.

    Tulizungumza na akaniambia kama naweza kupata ruhusa ya kutoka chuoni na kwenda mjini basi nifanye hivyo na siku inayofuata atanirudisha kwani ilikuwa ni week end. Nilizungumza na rafiki yangu Mnywaradwa Biera na alikubali kwamba tutoke. Hivyo tukaomba ruhusa na kkwetu ilikuwa rahisi sana kuruhusiwa kutokana na tabia zetu. Tuliondoka na Jones na Biera mpaka mjini.

    Jones alituvutisha raha za kila namna, tulikunywa, tulikula na kufanya shorping. Kisha jioni wakati wa dinner kabla hatujaenda kulala kwenye hotel nzuri ya kifahari aliyobook kwa ajili yetu nay eye, aliniomba sana nimpatie jibu.

    Alinieleza nia yake na lengo lake kwamba bado anahitaji niwe mpenzi wake.

    Sikuona sababu ya kukataa sasa. Moja kwa moja kwa moyo wa hiyari kabisa, nilimwambia Jones nampenda na niko tayari kuwa na mahusiano naye ya mapenzi , awe mpenzi wangu na kisha mume wangu. Na nilimueleza kwamba natamani sana tuheshimiane, tupendane na kuwa mke na mume kama Mungu akitupa maisha.

    Jones alifurahi na kwa mara ya kwanza kuona machozi ya Jones. Ilikuwa ni furaha kubwa sana kwake mimi kumkubali.

    Tulilala usiku huo. Mimi na biera kwenye room yetu. Usiku kucha tulipiga mastory na kumueleza juu ya Jones. Biera alinishauri vyema na kuniambia nimepata kijana mwenye anaonekana ni smart, muaminifu na anayemaanisha mahusiano. Aliniambia sio kijanahohe hahe ni kijana ambaye yuko smart na very handsome and educated.

    Tulifurahi na kulala.

    Asbh tuliamka na kuelekea kwenye chai. Kisha tukazunguka tena mjini na ndipo sasa Jones akaturudisha chuoni. Huku akinisisitiza kwamba mimi nay eye sasa tuko kwa stage ingine kabisa na sio ya urafiki tu, ni urafiki wa uchumba kwani tunafahamiana miaka mingi, hivyo ni vyema sasa tukaheshimu mahusiano hayo.

    Nilimuhakikishia kwamba mimi niko salama sana na asijali, nay eye pia awe salama.

    Aliondoka na kuniacha. Nilianza kumuwaza sana, nilianza kumuona alivyo mzuri,na kijana wa thamani sana kwangu.

    Nilimfurahia sana Jones. Lakini Biera naye aliniambia sio kijana ambaye ni chokoraa ama mang’aa. Akaniambia kwa namna vile anaonekana kama angekuwa mang’aa angetafuta tu msichana wa kuspendi naye na asingehangaika kuja naibori kwa ajili yangu. Nilimuelewa Biera.

    Sasa Jones alianza kunifuatilia kwa simu. Alipiga simu kila mara, alijua natoka darasani saa ngapi na aliongea na mimi zaidi ya lisaa kila siku mara agunduapo niko na nafasi. Wakati mwingine nilichelewa hata kuoga ama kula. Hii ni kwa sababu alishikilia simu muda mrefu. Na kama ingekuwa naongea na simu basi ni lazma nimueleza naongea na nani.

    Jones aliingia wazimu juu yangu. Na mimi sikushawishika kutompenda, ila nilimpenda zaidi na zaidi.

    Muda ulipita. Sasa ni mwaka wa pili niko chuoni.

    Jones ameshajulikana kila mahali, si chuoni wala nyumbani kwamba ni mpenzi wangu na mchumba wangu.

    Wasichana wengni walinionea wivu, hali kazalika vijana wa kiume nao. Walinitamani sana na walitamani mahusiano yetu yangekuwa kamayao. Kwani mara nyingi walikorofishana.

    Biera naye alikuwa akikorofishana na mpenzi wake kila mara.

    Jones alifika Nairobi kila mara alipohitaji, hasa siku za jumamosi na jumapili, hivyo ijumaa jioni nilitoka chuoni na kurudi jumatatu asbh.

    Tulipendana sana. Na tulpofunga chuo Jones alikuja na kunichukua na gari yake.

    Marafiki wa Tanzania walinitamani na waliomba lift ila Jones aliniambia hakuja kuchukua chuo ila kunifuata mimi hivyo hawezi mpatia mtu yeyote lift, isipokuwa mimi ambaye ni mpenzi wake.

    Mapenzi yalipamba moto. Tulipendana sana.

    Niliporudi kutoka chuo, nilifikia kwa Jones ambaye alikuwa na nyumba yake aliyopangisha, nilikaa kwake siku tatu kisha ndipo nilienda nyumbani, na muda wowote alinifuata nyumbani na kutoka na mimi. Wazazi wangu walimpenda kijana ambaye alijiheshimu sana.

    Wakati narudi chuoni kwa ajili ya kumaliza elimu Yangu, Jones aliniomba kunivisha pete. Nilimuomba anivishe pete mara baada ya mimi kumaliza chuo. Aliniambiahapana naomba kabisa nikuvishe pete ya uchumba, nilimuomba sana asubiri. Na akakubali.

    Nilienda chuoni nikiwa msichana mwenye furaha na kujiona ni mwenye bahati sana.

    Maisha yaliendelea kwa furaha mno. Na nilibahatika kufanya mitihani yangu vyema.

    Kabla sijamaliza chuo, Jones aliniambia kaka yake anaoa, na angependa nihudhurie harusi hiyo. Nilimueleza situation ya masomo, aliniomba sana kwamba nichukue ndege nifike jijini kwa harusi na baada ya siku mbili nitarudi.

    Nilimtii wkani nilimpenda. Alinilipia tiketi ya ndege na kwa mara ya kwanza nilipanda ndege. Nilienda kwa ajili ya harusi ya kaka yake. Alinipeleka shorping kwa ajili ya nguo za harusi. Kisha Jumamosi siku ya harusi tukawa tuko pamoja kwa ajili ya harusi ya kaka yake

    Kila mtu alimhurumia na kumwambia huyo Charlote kakukamata haswa, na alifurahi kusikia hivyo. Alikuwa muaminifu sana kwangu, na hakuwa na mahusiano na msichana yeyote Yule. Mara nyingi aliambiwa ukimuamini sana Charlote iko siku atakutenda, na mimi sikutaka kukamilisha ndoto hizo na misemo hiyo mibaya. Hiyvo nilijitahidi kumpenda na kumuonyesha yuko mahali salama na kwenye penzi salama . na sikushawishika na kutamani mwanaume yeyote.

    Harusi ilikuwa kubwa sana na ilifana sana.

    Maharusi waliingia ukumbini kwa nderemo na vijijo.

    Kisha wageni waalikwa nasi tukaingia ukumbini.

    Baada ya utambulisho, Maharusi walifungua champagne kisha tukagongeza kuwatakia mafanikio mema.

    Baada ya Hapo Jones naye alipewa nafasi ya kuongea, sikuwa na wasi wasi kwani nilijua anataka kusema jambo kama mwanafamilia.

    Kisha Jones alisema kwa sauti ya juu kwa kutumia kipaza sauti… CHARLOTE MY LOVE WHERE ARE YOU?

    Ukumbi mzima ulitulia kutaka kujua nini kinaendelea. Nilitoka nilipokuwa, hofu na kutetemeka kwa aaibu kutokana na umati wa watu, na sikuwa na ujasiri wa kusimama mbele za watu wengi. Ila kwa vile nilimpenda sana Jones sikutaka kumuangusha, nilijikaza sana huku natetemeka.

    Kisha nikafika, na akanibusu. Baada ya sekunde kazaa alitoa kitu mfukoni mwake,, na kusema..

    Huyu hapa ni mpenzi wangu, rafiki yangu na mchumba wangu, mke wangu mtarajiwa, naomba kusema kwamba baada ya harusi hii ya kaka inayofuata ni yangu…

    Charlote will you marry me?

    Dah…. Ilikuwa mtihani,, nilijikuta naogopa,machozi yanatoka,,, na Jones naye hali kazalika… Alipiga magoti na nikamwambia yes,,, will marry you….

    Watu walishangilia sana, na kufungua champagne. Kisha nikaenda kukaa na wazazi wangu walikuwa harusini kwani ni family friend wakaambiwa Jumamosi ijayo wajiandae na ugeni wa kupelekewa mahari.

    Ilipendeza sana japo nilishtukizwa kabisa.

    Harusi iliishia vyema na nikarudi chuoni.



    SEHEMU YA TATU.

    Nilimaliza masomo yangu salama. Na tayari nilikuwa na ujauzito wa miezi 2. Kwanza Jones alifurahia sana kusikia nina ujauzito. Haraka mipango ya harusi ilifanywa na tulioana, na sasa ikawa ni mke na mume rasmi. Harusi yetu ilifana sana, ilipenda mno. Na wengi walitupenda, na baada tu ya mimi kujifungua tulisimamia harusi kama mbili hivi, hii ni kwa vile waliotuomba tuwasimamie walivutiwa na maisha yetu ya ndoa na kupendana kwetu.

    Jones alinipenda sana.

    Nilipata kazi nzuri nay a mshahara mzuri kutokana na elimu yangu ilivyokuwa ya juu. Nilifanya kazi kwenye ofc kubwa mjini na ambao wanalipa vizuri.

    Haraka sana Mume wangu alininunulia gari nzuri ya kutembelea na kuniambia hataki nipate shida.

    Nilimpenda Jones nay eye alinipenda sana.

    Sikuwahi kumuwazia mambo mabaya hata kidogo. Na pia hatukupenda kugombana wala kulumbana kwani wazazi wetu walipendana sana na hatukutaka kujiaibisha. Mara tulipokoseana pole pole tuliambiana na kurekebishana kabla mambo hayajawa magumu na mabaya zaidi.

    Hivyo matatizo ya ndoa yetu hakuna aliyeyajua zaidi yetu wawili.

    Nakumbuka ni mara moja tu Jones aligomba kwa tabia yangu ya kunywa pombe, na nilimuahidi kuacha, kwani nilikuwa natumia pombe hasa balantine, na alipokuwa akisafiri ndipo nilikunywa sana. Japo sikuwa natoka ila nilinyewa nyumbani tu. Na alinikataza tabia hiyo. Na siku moja aliniaga anasafiri na kwa vile nilimwambia nimeacha alitaka kuhakiki je nimeacha ama la? Na hivyo alisafiri safari feki na kurusi na kunikuta niko bwii. Alikasirika sana na kuniitia mama yangu anionye. Huu ndio ugomvi ambao naweza kusema kwa mara ya kwanza niliuona mkubwa na kumuona Jones alivyobadilika. Na kuanzia siku hiyo nilimuahidi sitakunywa tena pombe. Japo sikuweza kwa mara moja ila nilimuahidi sitakunywa tena pombe.

    Ndoa yetu na maisha yetu yalkuwa gumzo mtaani , kwenye familia , kwa ndugu na marafiki, hata wafanyakazi wa jones na wafanyakazi ninaofanya nao kazi walikwua wakitushangaa sana.

    WENGI WALISEMA IVUMAYO HAIDUMU….. NA WALITUBEZA MNO.

    WENGINE WALITUFURAHIA, WENGINE WALITUTAMANI.

    Ndani ya ndoa ya miaka mine nikabahatika kupata mtoto mwinngine. Mungu akatujalia watoto 2. Tuliwapenda sana. Walikuwa wavulana wote, walifanana na sisi sana.

    Maisha ya ndoa yalikuwa matamu haswa.

    Sikuwahi kumuwazia Jones kuwa na mwanamke hata kidogo.

    Nakumbuka siku moja nikiwa natoka kazini, niliamua kumfuata ofcn kwake ili tupitie mahali nimuonyeshe friji ili tununue. Ilikuwa ni saa kumi na moja.

    Wakati natoka napanda ngazi za ofcn kwake nilikutana na mfanyakazi mwenzake, aliponiona alirudi kwa speed ya ajabu, nilishikwa na butwaa nini kinamrudisha? Lakini nikasema ni ofc za watu.

    Sikujali sana, nikaendelea kupanda ngazi. Kisha ghafla nikapishana kwenye ngazi na msichana ambaye ninamfahamu. Lakini hakunisalimia, ila alinipita kwa kasi ya ajabu, niligeuka nyuma kumtazama na aliendelea kuziruka ngazi kwa speed ya ajabu mpaka akamalizikia sikumuona tena, Nilipogeuzauso wangu nilikutana macho kwa macho na Jones, alinikumbatia na kunibussu, kisha akanishika mkono na kunipelake ofcn kwake. Akanipatia juice. , na nikamueleza kilichonipeleka kwake na tukaondoka kuelekea madukani na kununua friji hiyo kisha kwenda nyumbani.

    Siku hiyo mume wangu alionekana kuwa busy sana na simu sana, na si kawaida yake. Na tuliwekeana sheria hakuna kuweka simu pw, na kila mmoja ana ruhusa na simu ya mwenzake. Na hii ilitufanya tukaaminiana sana na kutokuwa na wasi wasi kwenye ndoa yetu.

    Kwa vile ilikuwa ni sheria sikuona shida nilijua tu acha awe busy kuna saa nitaishika simu yake na kuikagua.

    Na kweli usiku kabla ya kulala nilimuomba simu yake na nilifanikiwa kuikagua.

    Nilikuta ametuma msg na kasahau kuifuta na kasema ,, Samahani Husna naomba tuongee kesho nimeshafika nyumbani sihitaji kukuudhi, tutaongea kesho mpenzi.

    Dah,, nilipaniki kimoyo moyo,, lakini sikumuonyesha kama nimejua, ila Husna ni binti ambaye alinipita kwenye ngazi na speed za ajabu, Namfahamu mama yake, namfahamu baba yake, na ninawajua ndugu zake. Dah. Kiliniuma. Kisha nikafuta ile msg wala sikumuonyesha mume wangu kwamba nimejua kitu.

    Usiku sana muda wa saa saba nilimuamsha, nikamwambia Jones, naomba usinifiche, niambie ukweli wote kuhusu jambo nitakalo kuuliza.

    Je husna ni nani? Kwanza alisema alienda kuomba kazi, mara mpenzi wa mfanyakazi mwenzake nk. Nilikasirika nikamwambia kwa nini unanidanganya? Akaniambia mke wangu sio kweli sina mahusiano naye.

     

     

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog