Search This Blog

Thursday, November 24, 2022

NILIVUNJA NDOA ZANGU 3 KULIPIZA KISASI - 2

 

     

     

     

    Simulizi : Nilivunja Ndoa Zangu 3 Kulipiza Kisasi

    Sehemu Ya Pili (2)

     

     

    Nikamwambia poa haina neno.

    Tulilala, asbh nikakasirika sana, nikampigia Husna simu kumuuliza ana nini na mume wangu, alipokea simu na kusema hana mahusiano yoyote ila ni kama shemeji yake. Nilinyamaza na nikamuuliza anatoka na nani akaniambia anatoka na Damson. Nikamkumbuka Damson. Nikampigia simu, nikamuuliza shem samahani, Husna unamfahamu? Akasema ndio namfahamu, nikamuuliza ni nani? Akasema kwa nini shem unaniuliza hivyo? Nikamwambia mbona kasema ni demu wako? Kwani wewe umemuacha prisca? Maana alijua namfahamu prisca, akasema aa shem vunga. Kisha akakata simu, na mara simu yake ikawa busy sana, nikajua anaongea aiza na Husna ama Mume wangu. Haraka nikampigigia mume wangu, simu ikawa busy sana. Nikanyamaza.

    Jioni mume aliporudi home akawa kaweka simu pw. Tena kwenye kila kitu, nikamuuliza kulikoni? Akasema naona tu tutakosana kisa simu, naona niweke pw. Na mimi nikamwambia so na mimi niweke sio? Na mimi nikaweka. Kisha nikaanza kugombana naye, kwanza nikampigia Prisca nikamuuliza kuhusu Husna, akaniambia Charlote naomba tu nikuambie kweli, Husna anatoka na mumeo, ila wanatabia ya kusame ni demu wa Damsosn ili usijue. Lakini Husna anatoka na mumeo, ila wewe tulia nitakukamatisha naye. Wewe nyamaza.

    Prisca akanihakikishia kuwakamata. Na kweli akachonga njia mpaka akanipigia simu siku moja na kuniambia niende ofcn.Nilifika ofcn na kweli hamadi, Husna na mume wangu hawa hapa . Sikuamini, kwanza aligoma kufungua ofcn lakini nilisukuma mlango wa alminium ambao niliwaona kwa ndani .

    Jones hakuamini, aliogo pa sana, niliomba tu wafungue, mwisho akafungua. Kiliniuma sana, nikamwambia Husna ni nini hiki? Hakunijibu, nikataka kumshika nimpige akaniponyoka.

    Nikamwambia mume wangu ni nini unanifanyia? Akaanza kuomba msamaha, mwisho nikaona sina sababu ya kuendelea kulumbana naye, nikaondoka na kwenda nyumbani, kufika nyumbani nikalia sana, kikaniuma sana.

    Akaja na kuniomba msamaha, nikamuuliza kulikoni nini anakosa? Hakuwa na jibu. Nikamuuliza mimi nikifanya hivi utajisikiaje? Hakujibu pia.

    Alikuwa mpole sana. Akaniambia nisamehe mke wangu sitarudia tena naomba yaishe.

    Nikamwambia poa haina neno, ila asante sana.

    Kuanzia hapo nikaanza kujiuliza inakuwaje mume anabadilka hivyo. Mume niliyemjali kiasi hicho na kumuamini.

    Niliogopa kuwapa watu faida, nikasema sitaondoka wala kufanya lolote, ila nitaenda kumshtaki Husna kwa mama yake.

    SEHEMU YA NNE:

    Nilijua mama yake Husna alipofanyia kazi. Nilimfuata asbh sana, kabla hajaingia ofcn kwake.

    Nilimsalimia na kumwambia mama samahani nataka kuzungumza na wewe.

    Namna alivyonitazama ni kama aliyenibeza na mwenye kujua jambo, niligundua hilo mapema sana.

    Nilimwambia shikamoo mama, alinitazama chini juu, hakuniitikia. Ni mwanamke mweusi mnene na mfupi. Hivyo hata aliponitazama ilikuwa ni rahisi mimi kujua ananitazama yani kunishusha kwani ilibidi anyanyue sana shingo kunikuta nilipo.

    Sikkujali, alisema enhe unasemaje?

    Nilimwambia mama samahani,, nimegundua mwanao ana mahusiano na mume wangu.

    Akaguna, na kusema ninao watoto wengi ni nani?

    Moja kwa moja nilisema ni Husna…. Alicheka kwa kejeli,, akaniambia,,,

    Uliwashika ama ni umbea umekusanya mtaani?

    Nikamwambia niliwashika.

    Akaniambia uliwashika wapi? Nikamwambia niliwashika ofcn kwa mume wangu.

    Akaniambia kwa hivyo huyo mumeo haruhusiwi kufanya kazi na wanawake? Kwani uliwakuta wako uchi ama?

    Mh.. hii ilinishangaza,, nilijiuliza huyu ni mama ama ni Jini? Mbona hana huruma kama hajaolewa?

    Nilimwambia mama nina uhakika ndo maana nimekuja ili umuonye mwanao.

    Akaniambia naona huna jipya mama,,, sikia,, naomba sisikilizi umbea, Nenda kamtosheleze mumeo sawa.

    Alivuta hatua na kuniacha nikiwa nimeshangaa nisijue la kufanya, kiliniuma sana.

    Nilienda kazini kwangu huku nina mawazo debe zima.

    Nililia sana, ila kwa vile sikutaka ofcn wajue kisa changu nilijikaza sana na kunyamaza tu.

    Sikuongea lolote.

    Baada ya muda kidogo Husna akaniandikia msg na kuniambia,,, Umeongea na mama yangu ili nini? Itakusaidia nini? Mchunge mumeo usinifuatilie.

    Niliisoma ile msg bado nikajikaza, nikasema sina sababu ya kushindana kwa maneno, nahitaji matendo zaidi.

    Nikanyamaza kimya sikuijibu.

    Nikamaliza kazi nikaenda home kama hakuna kilichowahi kutokea.

    Nikaanza kujidunga balantine moja. Kila siku lazima soda moja ya ginger lemon na glass ya balantine.

    Kila jioni, ili kupoteza mawazo. Na jones alishindwa Kunizuia kwani sasa alikuwa na kosa na hakutaka kukubali kosa. Kuomba msamaha anashindwa, kuniambia nisinywe pombe anashidwa,

    Akaniambia mke wangu naomba tufungue simu zetu.

    Nikamwambia sio tu kufungua yani yangu hata chini sitakaa niiache. Nitaenda nayo mpaka chooni. Nikaweka pw kila kona, japo sikuwa wala na baya la kufanya.

    Nikawa nawaza nifanye nini ili roho yangu isikie raha?

    Miezi mitatu nilikuwa nikinywa tu pombe huku nawaza nifanye nini.

    Je nimpige ama kumfanyizia Husna? Je nimfanyeje? Nikaona haya yote hayamfai.

    Nikajikausha kama sio mimi, nikaanza kumpotezea, na kuanza kuishi maisha yangu mimi kama mimi.

    Mume wangu akaanza kuwa na wasi wasi akasema anaomba nisifunge simu yangu, nikamwmabia poa.

    Nikafungua pw zote na nikamwambia simu hii hapa.

    Maisha yakaenda.

    Baada ya miezi mitatu kuuisha nikafuatilia nikagundua mume wangu na Husna wameachana. Hawana mahusiano kabisa, na Husna kapata mpenzi wake.

    Nilianza kumfuatilia Husna kujua mpenzi wake ni wa wapi, na nilijua na kujua ofcn anayofanyia kazi.

    Na baada ya muda nikasikia husna kavishwa pete ya uchumba. Kwangu ilikuwa ni shangwe siku hiyo. Nilifurahia sana, nilijisikia rah asana, Nilikunywa sana usiku huo. Husna alikuwa na miaka 25 hivi. Na mpenzi wake kama miaka 28. Na mimi nilikuwa na miaka 28 na mume wangu miaka 34.

    Baada ya kuhakiki kweli husna ana mchumba nilitulia kidogo huku napanga mbinu zangu za kulipiza kisasi.



    Siku moja nilikuwa nimekaa ofcn,, nikakumbuka Babayake Husna mzee Zuberi Muarabu anapofanyia kazi, niliinua simu yangu na kutaka kuongea na Huyo mzee nimsikie ni wazee wa aina gani?

    Nilimpigia simu na kuongea naye, alikuwa ni boss wa kampuni Fulani mahali Fulani. Nikamwambia samahani Baba mimi naitwa Charlote, naomba nije na cv’s zangu ili kama unaweza unisaidie kazi.

    Aliniambia sasa hivi hawana nafasi za kazi. Nilitumia akili ya kike ya kumshawishi aniruhusu tu nizipeleke ili likitokea la kutokea basi anisaidie. Alikataa sana, lakini badae alikubali.

    Na ndipo nilisema sasa njama zangu za kulipiza kisasi zimekamilika.

    Siku ya jumatano asbh saa nne nilitoka nyumbani nikiwa nimevalia vizuri sana kwa heshima, tena kwa kujitanda. Nilienda moja kwa moja ofcn kwa mzee Zuberi, nilifika nikaomba kuingia ofcn kwake.

    Secretary aliniambia naweza kuingia. Nilingia, ni mtu mzima, nilimsalimia, nilijitambulisha, Na akanisifia sana na kusema dah, umevalia vyema sana, sikuwaza kama wewe ni Charlote, pengine ungesema unaitwa Hidaya… nilicheka na kumueleleza nina shida na kazi. Alishangaa inakuwaje kwa elimu ile sina kazi? Nilimwambia ninafanya kazi ila sipati mshahara mzuri. Nilimdanganya. Aliniambia kwa saa hana nafasi za kazi, ila akaniomba nimpe wakati kisha atanitafutia kazi yeye mwenyewe kwa elimu yangu.

    Nilifurahi sana na kuondoka.

    Wakti naondoka alinitazama na kuniiita, Charlote,,, niligeuka na kusema abee baba.. Aliniuliza umeolewa? Nilimwambia ndio baba.

    Akaniambia, dah,, mumeo ana mke mrembo sana, Nilicheka kwa kujishebedua kisha nikamfinyia jicho na nikatoka. Lengo langu lilishakuwa la kishetani, sikuwa na mswalie Mtume tena, nilishajivika uibilisi, sikwua na huruma hata kidogo.

    Nilipokuwa natoka nilipofika reception, Yule dada aliniambia Umeambiwa urudi.

    Ni mara ya kwanza tu nimeonana na mzee Zuberi, aliniambia Charlote, naomba kesho ninaenda kwenye mkutano mkoani, tafadhali kama hutajali naomba uongozane na mimi ukafanye kazi zangu. Ukanisaidie kazi. Nilimueleza kwamba atanilipaje maana nina shida na pesa nadaiwa kodi ya nyumba, nilidanganya.

    Aliniambia unadaiwa shilingi ngapi? Nilimwambia nadaiwa laki saba na nusu, kodi ya miezi mitatu.

    Mzee zuberi alinitazama kisha akaniambia subiri hapa. Alipiga simu accounts na kuitisha pesa hiyo. Mh, sikuamini, nilipatiwa Laki Saba na nusu na kuniambia basi kalipe hizi ili uwe na uhakika usije haribu kazi.

    Niliondoka hapo nikiwa na kicheko cha hali ya juu, na kuanza kuona mission zangu zikitiki.

    Nilifika nyumbani nikiwa na rah asana, nikachukua balantine yangu na kujidnga kama kawaida.

    Mume waangu alirudi na kunikuta niko njwii. Alianza kuongea na mimi, nilimwambia wala usijali mpenzi, ulilianzisha wacha nilimalize, mimi sitafanya umalaya ila nitafanya umalaya na balantine, sitaacha kunywa pombe, ukitaka niache.

    Mume wangu alikuwa akiwaza sana na kujuta kunikosea, ila azma yangu ilikuwa kulipiza kisasi.

    Asbh nilimuaga nasafiri . Aliniuliza naenda wapi sikumjibu.

    Niliondoka nimejiandaa vyema, na kupitia hoteli niliyoambiwa nitafuatwa pale na gari la mr Zuberi. Kweli muda ule nilikuwa nimeshafika pale, na mr zuberi na dereva wake waliwasili.

    Tulianza safari nje kidogo ya mji, haikuwa mbali sana ni kama km 60. Na kufikia kwenye hotel ya kifahari, nilifika hapo na Mr Zuberi aliniambia Charlote wewe ni msichana wa kwanza mimi kukutamani tangu nimeoa, na sijui kwa nini umenivutia, ila nakupenda sana tafadhali naomba uwe mpenzi wangu.

    Kwangu hii haikuwa na shida kwani ndicho haswa nilitaka.

    Sikujali hata kidogo, nilijivunga na kulalamika shida ya maisha, na aliniambia atanisaidia kwa chochote nitakacho. Na akanihakikishia uhakika wa maisha.

    Tulilala hotelini hapo siku tatu, kisha siku ya nne tukarudi.

    Mume wangu niliporudi aliniuliza nilikuwa wapi, nilimwambia aniache, alishikwa na hasira na kunipiga, nikamwambia umeharibu sana kunipiga, nikaanza kufungasha niondoke.

    Alipogusa pochi yangu alikuta pesa taslimu milioni moja na laki mbili, akaniambia pesa hizo nimetoa wapi? Nilimwambia ni zangu na asinibabaishe, alizichukua pesa zile,na kisha kunifungia chumbani kisha kumuita mdhamini wa ndoa yetu na mkewe.

    Walikuja na tukakaa kikao. Tuliongea sana na nikasema nilikuwa nimeenda kupumzika kwa hasira, hivyo aniache kwani alikwua na mahusiano na husna. Mume aliomba msamaha sana na kusema anaomba yaishe, na akaomba nifungue simu yangu.

    Nilifungua na akanirudishia pesa na kuniambia yaishe , nikamwambia poa. Ila bado nilikuwa na kisasi.

    Tuliishi maisha ya mimi kumficha sana mume wangu tabia zangu na hakuwezi kunikamata kabisa.

    Mwezi mmoja kabla ya harusi ya Husna, nilihama kwa mzee Zuberi, na sas nilitaka kuwasiliana na Majidi, mpenzi na mchumba wa Husna, hii ilikuwa ngumu kidogo. Kwani Majidi alikuwa ni mfanya biashara na alikuwa na duka kubwa la kuuza tv, simu na vifaa vya umeme, hivyo ningeenda pale ningeonekana. Na pengine Husna angepewa taarifa.

    Nilijiuliza nitawezaje kumpata Majidi? Ohoooni rahisi sana. Ni rahisi sana, Niliangalia bango la tangazo la biashara yake, na namba za simu niliziona.

    Nilichukua namba za simu na nikasema nitampigia, ila nitamwabia nini? Hiyo ilikuwa juu yangu.

    Wakati huu mzee Zuberi alishanieleza kamba binti yake anaolewa siku za usoni. Na nilikuwa namsifia sana na kumwambia una bahati kuozesha binti kwani sio kila mtu anaozesha bintiye.

    Na yeye alifurahia sana na kunipenda sana, sikuwa mapepe na alinisifia namna ambavyo namheshimu yeye na mkewe kwani huwa sipigi simu wala kumsumbua kabisa akiwa nyumbani.

    Mzee wa watu maskini asijue nini lengo langu.



    Charlote, baada ya  mume wake kujihusisha na mapenzi na msichana aitwaye Husna, Charlote anaamua kumtafuta mama wa Husna ili kumueleza juu ya swala hili akiamini kwamba  ni mama mwenye busara ambaye anaweza kumuonya bintiye kuacha mahusiano na Jones, mumewe Charlote. Lakini kwa bahati mbaya anakutana na mama ama mke ambaye hana busara wala  hekima na kumjibu  Charlote majibu ambayo kwayo sasa anaamua kulipiza kisasi.



    Tayari  Charlote ameshaanza mahusiano ya mapenzi na mume wa mwanamke huyo yaani baba wa Husna, na mapenzi yao yamepamba moto , isipokuwa Charlote anafanya kwa siri sana ili isijulikane, sijui nini azma yake.



    Je kisasi chake kitafanikiwa ama la?Endelea kujisomea katika sehemu hii ya Tano.



    SEHEMU YA TANO;

    Kwa Majidi nilipata mtihani kidogo mkubwa, sikujua nimuingilieje, na lengo langu ilikuwa kuvuruga na kuharibu haswa, niliamua kulipiza kisasi ambacho si mama yake Husna wala Husna ambao wataumia maishani mwao mwote,

    Kitendo cha Mume wangu Joe kuwa na mahusiano na Husna kiliniuma sana, niliumia kwani nilikuwa msichana ambaye nilikuwa najitunza, nampenda na kumheshimu sana, lakini niliamini pendo lake la dhati kwangu.

    Hiyo haitoshi , kiliniuma zaidi pale ambapoo nilipomuuliza alikataa na kunifanya mimi ni kama mtoto mdogo na asiyetambua jambo.

    Hizi fikara ndizo ambazo zilikuwa zikizidisha chachu katika kisasi change, na hata pale akili zinaponirudia na kuona nakosea ninapokumbuka hayo, hasa maneno ya mama yake Husna eti, KAMTOSHELEZE MUMEO… haya yalinifanya nishikwe na hasira kama swira aliyepigwa jiwe likamkosa.

    Kumtosheleza ndio nini? Alikuwa na uhakika gani kwamba simtoshelezi? Ohooo,, hivi kumbe mwanaume akitoshelezwa hatoki eeee.. sasa Jones kilichomtoa ndani ni nini na kumfuata Husna msichana ambaye kila nilipojaribu kuangalia na kufananisha namna tunavyoonekana mimi nay eye wala hakunifikia kwa lolote, si umbo, sura , elimu wala Tabia, nilijiuliza na kukosa jibu.

    Kisha nikapata jibu kwamba kuna wakati wanaume wanapenda wanawake wabaya. Hili ndilo jibu nilipata.

    Kwa uzuri niliokuwa nao, kwa heshima na utii kwa mume na urembo kamwe usingenifananisha na Husna.

    Sura umbo wala tabia ya husna havikuwa vizuri, na wala hakuwa msichana mrembo. Nilipata jibu kwamba wanaume hupenda pia wasichana wa SURA MBAYA.

    Nilishikwa na hasira kila mara nilipokuwa nikitafakari haya.

    Lakini msaidizi wangu Balantine alikuwa pembeni akiniliwaza kila nilipokuwa ninapata mawazo.

    Mapenzi ama mahusiano yangu na Mzee zuberi hayakuwa ya furaha wala sikuyafurahia hata kidogo, ni kwa vile nilikuwa nalipiza kisasi tu.

    Jones kilimuuma sana kwa namna nilivyobadilika , alikuwa akijuta kwa nini nakunywa pombe kiasi kile, nilipenda pombe sana, niliifurahia, nilikunywa nililala na kuridhika kabisa.

    Jones alianza kukonda na kuwa na mawazo mengi sana, sijui kwa nin…

    Kuna wakati nilimueleza bila kumficha, Husna si yupo, go, nenda she is available.

    Kila nilipomueleza hivyo alichukia sana na mimi kilinichekesha sana.

    Muda ulipita,

    Nikiwa nimekaa sebuleni nilipata wazo jipya, ilikuwa ni siku ya Jumatatu asbh nikiwa namalizia kunywa juice ili nielekee ofcn.

    Nilifika ofcn, baada ya kufungua ofc na kuangalia kazi zangu za siku hiyo nilijiona nina nafasi.

    Mara moja nilichukua simu ya ofcn na kupiga kwa Majidi.

    Halooo.. upande wa pili ulipokea.

    Haloo… nilijibu.

    Kisha nikajitambulisha…. Kwamba mimi ni mteja nahitaji flat screen za sumsang kama pc 10 hivi kwa bei nzuri.

    Majid alionekana kwenye simu kufurahi sana, alitaka kujua napatikana wapi,,

    Nilimueleza kwamba anipatie kwanza bei , nilimpa aina ya screen na ukubwa.

    Aliniambia zinauzwa milioni 1.2.

    Nilimuambia nikichukua pc 10 atanifanyia punguzo la bei? Alikubali akasema ndio atafanya punguzo la bei.

    Aliniomba sana tuonane ili tuweze kuzungumza kwani hana dukani kwa sasa ila ameziagiza na mzigo wake utafika Zanzibar bandarini muda si mrefu.

    Nilimueleza niko na shunguli nyingi, isipokuwa nitamjulisha nitakapokuwa na nafasi

    Alinihoji ni za matumizi gani,, nilimueleza ni mepata oder kwa mwenye hotel , anataka pc zaidi ya 30. Ila kwa kuanzia anahitaji pc 10 kwanza.

    Majid ni kama aliingia uchizi, kwani nilimchizisha pia kwa kumwambia nitahitaji simu za mezani extentions, friji za vyumbani na mazulia.

    Aliniambia hivi vyote ana uwezo wa kuvipata.

    Nilikubaliana naye nionane naye siku inayofuata jioni. Na kumuomba sana hii deal asijaribu kuongea na mtu kwani sitaki kuipoteza, hivyo asishirikishe mtu ili tusije kosa pesa.

    Aliniambia nisijali.

    Nilikata simu na kuachia tabasamu kwani tayari nilishajua ndege kanasa kwenye mtego wangu, sina haja ya kikimbia pole pole namkuta kwenye mtego. Maskini Majid bwana harusi mtarajiwa.

    Tulikubaliana kukutana kwenye hotel Fulani na baadae nilikata simu huku nikiwa na furaha sana.



    Siku iliyofuata nilijua fika ninatakiwa kukutana na Majid, ninamfahamu kwa sura na muonekano wako. Ni kijana mdogo ambaye anaonekana kujiheshimu, kujipenda na kusaka pesa. Ni kijana mwenye asili ya Kiarabu, ni mwenyeji wa Tabora, hupendelea kumuita Majidi Muarabu wa Nzega… hivi ndivyo ilikuwa ukitaka kufika dukani kwake lazma utumie jina hili. Ni kijana ambaye anapenda maendeleo sana, anajishughulisha mno, mpenda dini yake sana . Na hata baada ya kuanza kuwa na mahusiano na Husna , husna naye alianza kuvalia vyema, kwa kujitanda na kujifunika sana, sio husna Yule niliyemuona amevaa leggings na dress top siku ile niliyopishana naye kwenye ngazi, lakini pia siku nilimkuta ofcn kwa mume wangu alikuwa kavalia kigauni kifupi sana kilichoacha paja zake wazi. Nilipokumbuka hili nilianza kupata tena hasira.

    Ohooo, sasa nitafanya hivi, najua umbo langu ni zuri, linavutia, nitavalia vyema kama Salha, nilimkumbuka Salha, mwanachuo mwenzangu miaka hiyo iliyopita, alinifundisha kuvalia kama yeye mara kwa mara. Aliniambia nina umbo zuri sana sipaswi kuliachia ila kulihifadhi kwa ajili ya mume wangu. Mara zote aliponiambia hivyo tulicheka. Hivyo nilisema sasa nitavalia hivyo.

    Nilikumbuka kwamba nina sketi nzuri ndani, nilikumbuka nina mtandio, nilipoamka ashb nilijiandaa.

    Nilivalia vyema sketi ndefu, sendoz zilizoacha vidole vyangu vya miguu wazi, na blauzi ya mikono mirefu, kisha nikafunga kitambaa kichwani na kutupia ushungi, Manshalah,, ungeniona katu usingeniita Charlote, ungeniita pengine Hidaya jina alilonibatiza Mzee Zuberi.

    Pole pole nilitoka ndani. Jones mume wangu alinitazama, akaniambia wewe… niligeuka akaniuliza umevaaje hivyo? Nilimtazama na kumwambia kwani nimevaaje?

    Akasema unaenda wapi? Nikamwambia naenda ofcn.

    Akaguna,,, kisha akasema subiri tuongozane. Sikukataa, nilimsubiri,

    Geti lilifunguliwa kisha tukaondoka kuongozana.

    Nilitangulia mbele akafuata nyuma.

    Nilifika ofcn nikashuka, akaniaga na kuniambia siku njema, nilimwambia asante.

    Niliona namna ambavyo Jones anaumia kwa kunikosea.

    Lakini hata nilipojaribu kumhurumia nilikumbuka neno la mama yake Husna,, KAMTOSHELEZE MUMEO… nilijiuliza tena, hivi wanaume wote ambao wanamahusiano nje ya ndoa huwa hawatoshelezwi? Nikajichekea tu nikasema ohooo,, kumbe mama husna hamtoshelezi mzee Zuberi ndo maana akanipenda eee…. Nikacheka na kuingia ofcn na kuanza kazi zangu.

    Nikiwa kati kati ya kazi, nilishtuliwa na binti ambaye hutuhudumia chai , akiniambia dada Charlote chai tayari nikuletee..

    Niliinua uso wangu kwani nilikuwa busy na kazi, nilimtazama na kumuachia tabasamu kisha nikamwambia asante, nipatie chai, kisha vitumbua viwili.

    Aliniambia haya dada. Ni binti mzuri anajipenda ana heshima na hutuhudumia kwa heshima sana, na huwa hunipenda mno. Na mara zote huanza kuniuliza kama nitahitaji chai. Na wengi humtania na kumwambia Ni miss kampuni yetu.

    Aliniletea chai, nikiwa nakunywa chai, simu yangu ya mezani iliita, nilipokea.

    Mume wangu, alinipigia…. Charlote mke wangu habari….

    Mh… niliguna kwanza,, kisha nikamwambia salama.

    Akaniambia,, tafadhali naomba tutoke wote kwa lunch leo nina maongezi na wewe.

    Nilimwambia sawa haina tatizo.

    Kisha nikakata simu.

    Baada ya nusu saa alinipigia tena simu akaniambia nichague nataka kula nini.

    Nilimjibu na kumwambia, unajua choice zangu naomba nichagulie.

    Alicheka kwenye simu kicheko cha furaha, nikajua kapata faraja.



    ****************************************************************************

     

     

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog