Search This Blog

Friday, November 18, 2022

MUHANGA WA MAPENZI - 1

 






IMEANDIKWA NA : ALLY MBETU



*********************************************************************************



Simulizi : Muhanga Wa Mapenzi 
Sehemu Ya Kwanza (1)


 Athumani alijikuta akiwa njia panda asijue aelekee upande gani, ilikuwa ni baada ya kumsindikiza rafiki yake aliyekuwa amekuja kunitembelea. Hii yote ilitokana na kuwa mgeni maeneo yale , akiwa amekuja kwa kaka yake ambaye alikuwa amekwenda masomoni nje ya nchi na muda huo alikuwa bado hajaoa.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Hivyo kumuita kumlindia nyumba yake, japokuwa alikuwa mgeni maeneo yale lakini hakupenda aonekane si mwenyeji wa maeneo lile. Kwa kuwa vile alipitia njia ndefu wakati wa kusindikiza aliamua apitie njia ya mkato ili niwahi nyumbani.

Cha ajabu baada ya kuingia uchochoro mmoja alijikuta nimetokea mbele ya jumba moja la kifahari. Ilimchanganya kidogo asijue nielekee upande gani . Alijiuliza nirudi au atafute kichochoro apenye. Wakati akiwa katika kujishauri mara gari la kifahari Toyota VX V8 NEW Model lilisimama mbele yake baada ya muda kidogo mlango ulifunguliwa.

Ulitangulia mguu mmoja ambao olionesha raba aina ya NIKE kisha supu ya mguu ilionesha kinachotemka si kitu cha kawaida. Naam kitu kilichoteremka si cha kawaida. Alikuwa binti mmoja mweupe akiwa katulia katika vazi la shule siketi yake iliyombana na kuonesha makalio yalivyotulia si masihara. Binti alikuwa amepewa upendelea na muumba. Baada ya kuteremka alifunga mlango wa gari na gari kuondoka.

Baada ya gari kuondoka binti yule alielekea ndani ya jumba lile la kifahari, Ahumani alionelea ni vizuri amuulize njia ya kutokea barabarani. Kabla ya kuingia getini alimwita lakini hakumjali alichepua mwendo kuingia ndani. Alifikiria labda hajamsikia. Alichapulisha mwendo na kumwahi kabla hajagusa kengele ya getini. Alipomgusa tu yule msichana alimkalipia.

“We kaka umerogwa … Usinishike wewe una hadhi ya kunishika mtu kama mimi,” alimjibu huku alijifuta sehemu aliyomshika kwa kitambaa cha mkononi.

“ Samahani sister nilikuwa nataka kukuliza,“ Athumani alisema kwa upole.

“ Uniulize uliniona na nafanya kazi mapokezi?” alimjibu kwa nyodo.

“ Samahani,” Athumani alimuomba msamaha msichana aliyeonekana ana dharau sana.

“Ninyi ndio vibaka achana na mimi.”

Mabishanoyao yalisababisha askari wa getini afungue mlango na kuhoji.

“Rachel vipi ?“ Aliuliza askari.

“ Si hili libaba eti linataka kuliuliza kama sio likibaka linataka kuniibia.”

Ilibidi mlinzi aingilie kati na kumwambia Rachel aingie ndani na kuniuliza shida yangu. Alimweleza hali halisi mlinzi alimuelewa na kumuonyesha njia ya mkato.

Baada ya kuachana na yule msichana alirudi nyumbani kuendelea na shughuli zake, maneno ya yule binti hakuyatilia maanani hasa akizingatia watoto wa kubwa. Wengi wametawaliwa na dharau

RACHELhttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Rachel msichana aliyeubwa akaumbika mtoto wa tajiri mmoja jijini anayetambuliwa kwa jina la John Mulisa. Pamoja na uzuri wake alikuwa ni binti anayejiona sana si nyumbani hata shuleni alichagua rafiki wa kuzungumza naye wengi walipenda kumwita mama mashauzi.

Siku moja Rachel chumbani kwake baada ya kutoka shule jicho lake lilikuwa barabarani sehemu kulikokuwepo dirisha lake. Jicho lake lilitua kwa mvulana mmoja aliyekuwa akipita katika vazi la kuvutia pia mwili wake ulijengeka kiume hasa.

Mvulana yule alikuwa mgeni machoni kwake, alijikuta akimpenda ghafla ya kutamani siku moja awe wake. Rachel alimsindikiza kwa macho hadi alipopotea machoni kwake. Alijikuta akijiuliza kijana mzuri kama yule anakaa wapi na atawezaje kumpata mtoto wa kike. Alijukuta akiuvaa ugonjwa usio na dawa ya kumeza wala kupaka.

Alijikuta akiwa katika ugonjwa wa kupenda bila ampendaye kujua. Akiwa shule alijikuta yupo katika kipindi kigumu darasani masomo yalikuwa kero kwake baada ya muda mwingi kuutumia kumuwaza mtu asiyemjua.

************

Rachel baada ya kutoka shule alikuwa chumbani kwake alibadili nguo akiwa mbele ya dressing table iliyokuwa karibu na dirisha ambalo lipo upande wa barabarani alivutiwa na kijana mmoja aliyekuwa anapiti sawa na dirisha lake ambaye alikuwa akimuona kwa mara ya pili mfururizo .

Bila kujielewa alijikuta akipenda kila kitu alichokuwa nacho yule mvulana . kuanzia mavazi yake mwendo wake, umbo lake na sura yake . Aliacha shughuli ya kubadili nguo alinyanyuka dirisha ili aliweze kumuona vyema yule kijana wa kiume.

“Ama kweli kuna vijana wa kiume walioumbwa wakaumbika hata ukipita mbele ya watu wanakuonea wivu “ alijikuta akijisemea mwenyewe.

Baada ya yule kijana kupita alimwacha Rachel katika lindi la mawazo juu ya kijana yule na kujiuliza sijui kama atamtia tena machoni . Rachal baadaya kubadili nguo na kuvaa nguo za kupendeza alisimama mbele ya kioo na kujisifia jinsi alivyo mzuri na jinsi alivyopendeza . Alijikumbatia mwenyewe huku akisema:

“ Jinsi alivyopendeza halafu nipate kijana mzuri kama niliyemwona muda ule mbona dunia nitaisanifu.“

Rachal alizivua zile nguo na kubakia na nguo ya ndani na kujitupa katika kitanda cha sita kwa sita na kujipindua kitanda kizima huku akimuwaza yule kijana ambaye ameuteka moyo wake kwa ghafla.





Rachel alijikuta kwenye wakati mgumu wa kuugua homa ya mapenzi huku akimuogopa kumweleza muhusika kutokana na dharau alizomfanyia alijuuuta kumdharau asiyemjua. Hali ile ilimfanya awe mwingi wa mawazo muda wote kila alipokuwa akimuona yule kijana akipita moyo wake ulimlipuka na kujikuta kwenye wakati mgumu.

Muda mwingi alikuwa mtu wa mawazo kipindi kitu kilichopelekea kumshtua kila mmoja kuanzia wazazi wake , walimu hata rafiki yake mkubwa Joyce .

“Rachel vipi mbona siku hizi mbili unaonekana una mawazo mengi,“ Joyce alimuuliza.

“Joyce ni kweli kuna kitu kimenisibu lakini si leo, ila ipo siku nitakuelezea ili unisaidie, “ alimjibu rafiki yake kwa sauti ya unyonge.

“Hapana Rachel wewe ni rafiki yangu na siri zetu hatufichani naomba uniambie huenda nikakusaidia hata kimawazo.”

Rachel ilibidi amueleze ukweli Joy jinsi anavyompenda mtu asiyejua mapenzi yake kwake.

“ Kwanini uutese moyo wako wakati mtu mwenyewe hayupo mbali mueleze ukweli ujue moja siku zote kwenye maumivu ya moyo unatakiwa kujitoa muhanga kwa kujiweka wazi mbele ya yule umpendaye.”

Rachel aliahidi kuyafanyia kazi yale aliyoelezwa na shogae Joyce .

***

Kutokana na gari linalomfuata kumchukua shule kuchelewa Rachel aliomba lift kwenye gari la kina Joyce ambalo lilimshushia karibia na kwao. Baada ya kuteremka katika gari aliagana na Joyce wakati anageuka ili aondoke nusra aanguke kwa mshtuko pale alipokutana uso kwa uso na mtu ambaye alimuona hana hadhi ya kuzungumza naye lakini akatokea kuwa ugonjwa wa mahaba yake.

Kutokana na tabia yake ya nyodo hata kumueleza alishindwa alibakia kumsindikiza kwa macho tu na kuingia ndani mwao huku moyo wake ukizidi kutaabika juu ya mapenzi.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Siku iliyofuata baada ya kutoka shule na kuingia chumbani kwake alielekea dirishani ili afungue pazia atazame nje wapita njia. Hakuamini macho yake pale alipomwona tena yule kijana akipita. Safari hii alifurahi zaidi kwani alikuwa amesimama akizungumza na mtu na alipomwangalia vizuri alimtambua kuwa ni yule kijana aliyemzodoa siku moja akiwa katika mavazi ya kawaida.

“ Dah! Kumbe bonge la hand some boy, ni kijana mzuri sana tena sana …. Mmh, maskini sijui kama atanielewa nikimweleza nampenda wakati niliisha mtoa nishai,” Rachel aliwaza peke yake bila kupata jibu kitu kilicho mnyima raha.

****



Athuman akiwa anatoka katika shughuli zake, alijirudisha nyumbani kwa mwendo wa taratibu mara alishtushwa na sauti ya mtoto mdogo wa kiume ikimwita kwa nyuma.

“Kaka ……kaka.”

Athuman aligeuka na kumtazama yule mtoto na kumuuliza.

“Unasemaje?”

“Kuna barua yako, “ alisema yule mtoto huku akinyoosha mkono kumpa barua.

“Inatoka kwa nani?” aliuliza huku akiipokea.

“Yule.”

Alimuonesha binti Rachel aliye juu katika jumba la kifahari ambalo anakaa tajiri mmoja John Mulisa. Alimuangalia yule binti ambaye alikuwa amesimama mbele ya kibaraza. Alipomwangalia vizuri ili amtambue alijificha kwa aibu, lakini Athuman alimkumbuka ndiye aliyenitoa nishai siku moja.

Aliifungua ile barua na kuisoma palepale maneno niliyoyakuta yalimshtua kidogo nakumchanganya. Eti anamtesa moyo wake, yeye ndiye mwokozi wake na anasubiri jibu kama wokovu barua yenye maneno machache ilimalizia kwa manane: deep love Rachel.

Athuman alicheka kidogo kisha alinyanyua tena macho na kumwangalia kama mwanzo alijificha tena . Alijiuliza ni yeye au kuna mtu mwingine aliyempelekea ile barua mwenye hadhi ya kuzungumza naye . Athuman aliamini ile barua si yake mtumwaji atakuwa amekosea.

Aliachana na ile barua na kutupa vipande vyake vilivyo peperushwa na upepo kisha alipiga hatua kuondoka eneo lile. Rachel alimfaidi Athuman kwa kumuona vizuri tena kwa ukaribu zaidi.

Wakati Athuman anasoma ile barua Rachel alikuwa amefumba macho huku amejikumbatia kwa mikono yake miwili. Lakini moyo ulipasuka baada ya kushuhudia barua yake ikichanwa na kalatasi kutupwa barabarani. Kitendo cha Athuman kuichana barua yake kilikuwa kama kuuchana moyo wake.

Alijikuta akilia kwa uchungu huku akikimbilia kitandani na kuukumbatia mto huku akiendelea kulia na kulitaja jina la yule mvulana baada ya kulitambua jina lake kutokana na kusikia akikitwa na mtu.

“Athuman mpenzi kwa nini umeuchana moyo wangu, kwa nini huna huruma na mateso yangu ya moyo? Athuman nisamehe sikujua nitendalo lilikuwa sawa na kuupasua moyo wangu kwa kisu kisicho na makali bila ganzi. Hebu fikiria ni maumivu gani moyoni mwangu?”

Rachel alijizungumza huku akilia kwa sauti ya chini, mama Rachel alikuwa akiingia chumbani kwa mwanaye ili kumwita kwa ajili ya chakula cha mchana. Sauti ya kilio cha kulalamika kilimshtua na kuingia ndani taratibu ili ajue kuna nini. Alishangaa kumkuta akiwa amekumbatia mtu kitandani peke yake huku akizungumza kama anazungumza na mtu. Alipomwita aligundua mwanaye yupo usingizini.

Alitoka huku akijiuliza Athuman ni nani anayemsumbua mwanaye na kumuingiza kwenye dunia mbaya ya mateso ya nafsi ya mapenzi. Moyoni aliapa kumsikisha adabu huyu kijana anayeitwa Athuman.



.

****

Siku ya pili Rachel akiwa ndani ya gari akirudishwa shuleni alimuona Athuman akipita karibu na kwao kama ilivyokuwa kawaida yake. Alijikuta mapigo ya moyo yakimwenda kasi. Alijikuta akikosa uvumilivu na kujikuta akimwambia dereva wao.

“Peter naomba uniteremshe hapa.”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Kwa nini?’

“Nimekueleza niteremshe hapa,” Rachel alisema kwa sauti ya ukali.

Dereva hakubisha alisimamisha gari, Rachel aliteremka haraka na kumkimbilia Athuman aliyekuwa ameanza kulipita jengo la jumba lao.

“Kaka..kaka,” alimwita huku akimkimbilia.

Athuman aligeuka baada ya kujiona eneo lile yupo peke yake, alishika kifuniani na kuuliza.

“Mimi?”

“Ndiyo.”

Alisimama kumsubiri Rachel, baada ya kufika alimuomba samahani.

“Samahani kaka,” Rachel alisema huku akihema kutokana na kuja mbio.

“Bila samahani.”

“Naomba kwanza uniache kidogo nipumue, unajua nimekuja nakimbia.”

“Hakuna tatizo.”

Wakati Rachel akivuta pumzi na kujenga ujasiri ya kuzungumza na Athuman, baba yake mzee John Mulisa alikuwa akirudi na kumuona binti yake akizungumza na mwanaume. Alisimamisha gari na kuteremka na kwenda kwa kasi alipokuwa amesimama binti yake na Athuman.

Alipofika bila kuuliza alianza kuangusha kipigo kwa Athuman ambaye alipigwa butwaa. Athuman alijikuta njia panda na kushindwa kuelewa kinachoendelea. Mama mmoja mwenye mwili mkubwa alimshika yule mzee ili asiendelee kumsuburu Athuman aliyekuwa amepigwa butwaa.

“Baba Rachel hebu mwache mtoto wa watu utamuumiza bure.”

Yule mzee alimwachilia Athuman na kumfanya aondoke na wakati huo watu walianza kukusanyika na kuanza kumuuliza maswali.

“Vipi mshikaji, mbona dingi anakupa maumivu bila kumpa dispirin,” kijana mmoja alimuuliza.

“Achana naye si unajua watu wengine wanatafuta sababu.”

Athuman alijibu huku akiondoka eneo la tukio na kuelekea nyumbani. Alifikiria mengi juu ya binti yule hakujua nia yake, alijiuliza kweli anampenda au ana sababu zake.

***

Athuman akiwa sebuleni amejipumzisha kwenye kochi baada ya chakula huku akitazama tivii, alishtushwa na sauti ya kengere mlangoni. Iliyomuashiria kuna mtu mlangoni, alikwenda hadi mlangoni na kufungua mlango.

Hakuhamini macho yake, aliyekuwa mbele yake hakuwa mwingine ila Rachel mtoto wa tajiri John Mulisa.

“Athuman mbona unanishangaa? Nikalibishe ndani basi,” Rachael alisema huku akiachia tabasamu pana.

“Sishangai ila siamini kama wewe, pia umenitia wasiwasi juu ya mzazi wako pale tu kunikuta barabarani nusra anitoe roho. Kama akikukuta huku si atanitoa roho kabisa?” Athuman alisema huku akimkaribisha Rachel ndani.

“Athuman ukufikiria hivyo basi wazazi wasinge jifungua kwa uchungu.”

Alimkaribisha Rachel ndani baada ya kukaa kwenye kochi alimuuliza.

“Mrembo unatumia kinywaji gani?”

“Nipatie maji ya matunda” Rachel alijibu huku akitabasamu.

“Mbona sina, kuna soda tu.”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Yoyote upendayo mpenzi,” kauli ile ilimshtua Athuman na kujifikiria alichokisikia ni kweli au masikio yake.

“Mmh! Nimeisha kuwa mpenzi wake? Wacha tuone mwisho wake,” Athuman aliwaza moyoni.

Wakati Athuman akijiandaa kumfungulia Rachel soda kengele ya mlango ililia na kumfanya Athuman aache kufungua soda. Aliiweka juu ya meza na kwenda kuufungua mlango.

He! Baada ya kufungua mlango Nusra Athuman azimie na kutamani ardhi ipasuke na kummeza. Aliyekuwa mbele yake amesimama hakuwa mwingine ila mzee John Mulisa, baba yake Rachel. Kama umeme alimvamia na kuanza kunishushia kipigo kingine akisaidiana na askari alikwendanao, mkongoto aliopata ulisababishia apoteze fahamu.

Alipozinduka alijikuta akiwa amelazwa hospitari huku akiwa nimefungwa kitu kama chuma mkononi. Baaada ya kupata uelewa aligundua mkononi alikuwa amefungwa pingu mkono mmoja. Pembeni kulikuwa na askari akinilinda kama vile ameua.







Ilikuwa nivigumu kutathimini nini kilichomkuta hadi kufikia hatua kujeruhiwa hivyo bila sababu ya yeye kuhukumiwa vile. Athuman hakujua binti yule alikuwa na ajenda gani yeye na baba yake.

Mara ya kwanza amepigwa bila kosa mara ya pili amepigwa mpaka akapoteza fahamu na kujeruhiwa hata bila kuulizwa. Alishangaa kuvishwa pingu bila kosa. Alijikuta akiwaza au ndiyo ule useme mwenye pesa hana kosa ila mlala hoi hawana haki hata kama umeonewa?

Akiwa bado yupo katika windi la mawazo alishutushwa na kundi la watu wasiopungua watano mmoja alimtambua alikuwa mkuu wa polisi wa mkoa RPC pamoja na daktari, walisogea hadi kitandani kwake.

“Mkuu kijana mwenyewe ndio huyu,” daktari alimsonta kidole Athuman aliyekuwa amelala kitandani. Mkuu wa polisi alikwenda hadi pale kitandani na kumsemesha.

“ Kijana unajisikiaje hali yako?” alimuuliza Athuman kwa upole.

“Sijambo kidogo mzee, Shikamoo.”

“Marahaba,” Mkuu wa polisi aliitikia kisha alitaka maelezo ya Athuman kuwa pale.

Athuman alimpa kisa kizima bila kuacha hata neno moja, mkuu wa polisi baada ya kumsikiliza alimpa pole.

“Pole sana kijana kama ni hivyo, lakini bado tunaendelea na uchunguzi. Hivyo utakuwa chini ya polisi mpaka tupate ushahidi wa kutosha wa pande zote.”

Baada ya mazungumzo yasiyo na msaada kwa Athuman, mkuu wa polisi aliondoka. Baadaye Athuman alichukuliwa na kupelekwa mahabusu . Akiwa mahabusu aliona bado anaonewa kama ukweli amesema bado anawekwa rumande. Aliamini pesa na ubabe ndivyo vilivyotawala haki za wanyonge siku zote.

***

Rachel alijawa na simanzi mkubwa moyoni mwake baada ya kufumaniwa ndani kwa Athuman pia alijilaumu kuchelewa kumwelezea ukweli kuwa anampenda hata kama akifungwa angejua amefungwa kwa kosa gani. Yote yale ilikuwa sababu za mapenzi yake ya dhati kwa yule kijana .

Kukosa raha kulimfanya mama yake kuyaona mabadiliko ya mwanaye, alimfuata na kumtuliza kwa kumwambia:

“Mwanangu wewe huna kosa ila tunataka kumfunza adabu huyo mwana haramu anayetaka kukuharibia masomo.”

“Mama yule kijana hana kosa mwenye makosa ni mimi,” Rachel alimtetea Athuman.

“Hata ukimtetea vipi lazima atujue sisi ni kina nani na lazima aozee gerezani gerezani hata kwa kesi ya kichwa tutampa.”

“Mamaaa!” Rachel alishtuka.

“Unashtuka nini? Tena ondoka hapa usichefue nitakugeuzia kibao sasa hivi,” mama Rachel alimchumba mkwala mwanaye.

Rachel alikuwa mpole, lakini alimdadisi mama yake kuhusu hali ya Athuman huko mahabusu, mama alisema hajui kitu labda amsubiri baba yake atakaporudi. Mara aliingia Mzee John Mulisa, mkewe alimpokea mkoba. Baada ya kutulia alitaka kujua juu ya yule kijana aliyefumwa na binti yao.

“Mume wangu vipi kuhusu yule kijana?”

“Mama Rachel yule kijana lazima nimwonyeshe mimi ni nani, lazima itakuwa fundisho kwa yeyote atakayetaka kuchezea anga zangu,” Mzee John Mulisa alijigamba mbele ya mkewe.

Rachel aliyekuwa amejificha nyuma ya mlango aliyasikia yote yaliyosemwa na baba yake, alitulia tuli ili asikie mwisho wake.

” Lazima tuonyeshe sisi ni wazazi wenye uchungu na mtoto wetu, hawezi kutaka kumuharibia masomo yake hivihivi halafu tumchekee,” mama Rachel aliunga mkono.

“ Ile kazi hiyo nimempa mkuu wa polisi aishughulikie nasuburi taarifa yake.”

‘Mume wangu lazima uhakikishe anafungwa mwana Hizaya yule tena ikiwezekana maisha.”

Kauli ile ilizidi kumuumiza roho Rachel ambaye alizidi kumuonea huruma Athuman kwa vile yeye ndiye aliye muingiza kwenye matatizo.

“Mke wangu nina imani unanijua vizuri, yule nani kwangu, wacha kufungwa maisha hata nikitaka kuyongwa haitashindikana kwangu,” mzee John Mulisa alizidi kujitapa mbele ya mkewe.

“ Aah! Baba afungwe kwa kosa gani? Mbona mna roho mbaya, mnataka kumwonea mtoto wa watu. Nakuhakikishieni hafungwi kwa hali na mali, acheni roho mbaya,” Rachel alitoka nyuma ya mlango na kuwakata kauli wazazi wake baada ya maneno yao kumchoma moyo.

Maneno yale yaliwafanya wazazi wake washikwe na bumbuazi, hawakutegemea kusikia maneno makali kama yale toka kwa mtoto wao. Mzee John Mulisa, alicheka kicheko cha kivivu na kusema:

“Mama Rachel, maneno ya mtoto ni ya kitoto achana naye tuendelee na maongezi yatu...” Rachel alimkata kauli baba yake.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Mnafanya mzaha eeh! Nasema msipomwachia mtanijua mimi ni nani? Kwa nini hamuachi kumfuatafuta mtoto wa watu amewalia nini? Japokuwa ninyi ni wazazi wangu msije mkajilaumu baadaye,” Rachel alizidi kuwapandishia wazazi wake.

Kitendo kile cha Rachel kukosa adabu mbele ya wazazi wake, baba yake mzee John Mulisa alinyanyuka na kwenda kumzaba vibao. Rachel alikimbilia chumbani kwake na kujitupa kitandani na kuanza kulia kwa sauti. Mama yake huruma ilimwingia na kumfuata kumbembeleza bila mafanikio.







ITAENDELEA  

0 comments:

Post a Comment

Blog