Search This Blog

Thursday, November 24, 2022

NILIVUNJA NDOA ZANGU 3 KULIPIZA KISASI - 5

 

     

     

    Simulizi : Nilivunja Ndoa Zangu 3 Kulipiza Kisasi

    Sehemu Ya Tano (5)

     

     

    Nimeamua kukupatia kiwanja hichi , Na ninakuahidi mambo yangu yakiwa mazuri nitakujengea nyumba mpenzi, sawa mama?

    Alinibusu tena. Wakati huo huo alipomaliza kunibusu,, mlango wa ofcn kwake ulisukumwa.

    Hamadi… nilitamani ardhi ipasuke, niliogopa sitakaa nisahau katika maisha yangu yooote, mapozi yaliniisha,, uwiiii,,, niliogopa.. Nilikuwa natetemeka vibaya mno.

    Aliyefungua mlango naye alishangaa kwani alitukuta tumekumbatiana na mzee Zuberi, Mkumbato wa nguvu na kumaanisha kwa kila mmoja. Mzee zuberi akushukuru mimi kumpatia penzi tamu, na mimi nikimshukuru kunipatia kiwacha cha nusu heka. Nilikuwa namaanisha kumkumbatia kwa dhati, nay eye alikuwa anamaanisha kunikumbatia kwa dhati. Wote tukiwa tumekumbatiana haswaaaaa. Hivyo hata aliyeingia alishuhudia tukio hilo na lilimshangaza kama tulivyoshangaa na sisi.

    Baada ya sekunde kadhaa baada ya kugundua kuna mtu kaingia ofcn tuliachiana, huku mzee Zuberi akiniambia sogea pale. Na aliyeingia akionekana kushikwa na jazba huku akihema kwanguvu sana,na akitetemeka asijue la kufanya.

    Mungu wangu, shit, Mungu wangu, shit, ni maneno ambayo alikuwa akiyatoa mama yake Husna baada ya kuniona ni mimi Charlote nimemkumbatia mumewe,,, shit,, huku akinisogelea, shit…. Mzee Zuberi aliniambia Charlote tupishe,, huku nikiwa najificha mgongoni mwa mzee Zuberi. Niliondoka lakini sikusahau Bahasha ile, niliikwapua na kuondoka nayo. Nilishakuwa mang’aaa, yani ndani ya zali kama hilo lakini sikusahau Bahasha ile. Niliondoka kwa speed ya ajabu na kuelekea Ofcn.

    Nilifika ofcn na kumuomba rafiki yangu anihifadhie bahasha ile. Alinihifadhia kisha nikaingia ofcn na kumpigia mume wangu simu kumuomba aje kunipitia akitoka kazini ili tuelekee nyumbani wote. Jones alifurahia sana, alifurahia mno.

    Jioni kweli alikuja kunichukua na nilijichangamsha sana kwake ili asijue kama kuna jambo limetokea, na hangeweza kujua kwa namna nilivyokuwa mchangamfu.

    Na niliamini hata kama Yule mama angekuja kunishtakia ningemruka futi mia na kumrudishia kesi yeye kwamba bado ananifuata fuata.

    Baada ya kama lisaa limoja baada ya kula mimi na mume wangu, simu yangu ya mkononi iliita.. niliitazama sikujua ni nani. Niliamua kuipokea baada ya kuita mda mrefu.

    Nilipokea… … Asante sana mwanangu asante sana.. ni sauti ya mwanamke ilikuwa ikiongea,,, niligundua ni sauti ya mama Husna. Nilisjisahau kama mume wangu yuko karibu,, nilishikwa na hasira na kujikuta nimemjibu na kumwambia,, MTOSHELEZE MUMEO…. Na nikakata simu.

    Neno hili mume wangu alilifahamu kwani nilipomuelezea kuwa nilizungumza na mama yake husna na akanijibu hivi aliona nilivyokuwa nimelishikilia na lilivyokuwa linaniummiza. Hivyo aliniambia tu Charlote mke wangu , charlotte mke wangu,,, hembu achilia basi mama.

    Nilimwambia kuna mtu kanikera, akaniambia sitaki kuongelea issue yako mamiii, tulia mke wangu. Nilijjidekeza na kuamua kutulia kama alivyosema. Ila usiku kucha ile hali ya kufumaniwa nilikuwa naikumbuka, nikasema natamani kuzungumza na mzee Zuberi nisikie ataniambia nini. Nilitamani pakuche haraka sana ili nimpigie simu nimuulize kulikoni.

    Ni siku kadhaa tu baada ya harusi ni kama siku tano ama nne sasa harusi ifungwe, na shamra shamra zimepamba moto, kwa vyovyote vile hawezi kususa na kuondoka, kwanza mtu mzima ataenda wapi? Atachekwa,, niliwazz peke yangu kisha nikatabasamu.



    ***************************************************************************************************



    Nilichokuwa natamani ni kuongea tu na Mzee Zuberi, sikuwa natamani kuongea na mtu mwingine yeyote.

    Nilifika ofcn mapema sna, nafikiri ni saa kumi na mbili na robo. Nilikuwa sina la kufanya, ila tu ni kutamani kuongea na mzee Zuberi anieleze kulikoni? Sikuwa najali kabisa mkewe kuniona, ila nilikuwa natamani kujua ili nijue je nitafanyeje kuhusu Husna na Majid, kwani bado natamani Husna naye kimuume bara bara,,, na sasa nilikuwa najipongeza kwa nilichokifanya kwa mke wa Mzee Zuberi, japo ilikuwa mapema sana, lakini bado nilijipongeza yeye kuniona, kwani lengo langu ilikuwa ni siku moja nimshawishi mzee Zuberi tukutane hoteli moja mjini na nitafuta mtu atakayemueleza mkewe yaaani mama Husna kwamba niko na mumewe na aje kushuhudia, ni kama nilikuwa nimepanga kutafuta mmbea atakayemueleza Mama huyo taarifa zamahusiano yangu na mumewe. Lakini kama nilivyopanga ilitokea hivyo hivyo, isipokuwa kuja kwa mama Husna ofcn kwa mumewe haikuwa kuja kufumania ila kuja kuongea na mumewe kwa habari ya harusi ya mwanao na kupeana taarifa kama sio kuja kuchukua michango aliyoitiwa .

    Saa mbili kamili, nilichukua simu yangu ya ofcn na kumpigia mzee Zuberi…. Iliita kwa dakika kadhaaa.

    Kisha ikapokelewa… alipokea mzee Zuberi, mara zote nilimsalimia.

    Shikamoo … marahana bi mdogo,, hujambo?

    Aliiitikia kwa furaha sana,, nikajua hakukuwa na tatizo kubwa, wala hakuonekana kujali.

    Pole sana dadiii.. pole sana. Nilimwambia hivyo… aliniambia mamii pole wewew tena pole sana, ni mimi nilifanya makosa, nilisahau kwamba mama Husna tuliongea aje kuchukua pesa za sherehe ofcn, nilisahau mamii,,, lakini hakuna lililoharibika. Mimi mwanaume,,, kwani wewe vipi?

    Hapana nilikuhurumia tu dadii… aaa haina shaka…

    Mimi naogopa sana dadii, hembu niambie imekuwaje? Nilimhoji…

    Aaaa, mimi nwanaume bwana,, usiogope. Alilalamika sana, alilia sana, na kunishtakia kwa dada zake wawili………… ambao ni wakubwa, na wakamuonya asiharibu sherehe ya mtoto, wala wasimshirikishe mtoto jambo lolote kuhusiana na matatizo yetu kwani hayamhusu. lakini pia mimi sikushirikishwa kwa kikao hicho, ila watakusumbua kidogo hao wanawake . lakini usijali, wewe usijibizane nao, sawa mama.

    Mzee Zuberi alinipa mkanda mzima, na kunionya na kunitaarifu kwamba ni wanawake wa Kiswahili ambao wana maneno sana hivyo nisijaribu kushindana nao. Nilimhakikishia nitatulia, na kumuomba kwa sasa tujaribu kutuliza kwanza mahusiano mpaka tuone mambo yametulia.

    Aliniambia una akili sana shalote mpenzi wangu,, ndio maana nakupenda na kufurahia mapenzi yako.

    Nilimueleza pia namshukuru kwa kiwanja. Aliniambia usijali, usijali kabisa, nitakusaidia kujenga usijali .

    Nilijiuliza ni kitu gani cha mno ambacho nimemfanyia mzee huyu wala sikupata jibu. Tulimaliza kuzungumza kisha nikakata simu na kuendelea na siku yangu kama kawaida.

    Nilikuwa nimejipanga vyema, sikuwa najali hata kidogo, nilisema endapo hao wanawake watanijia na maneno basi ningeajibu na mimi bara bara wala singejali na ningewaeleza mkuki kwa nguruwe mtamu kwa binadamu mchungu. Nilikuwa na wasubiri kwa hamu wanijie.

    Na kwa bahati nzuri sana, hakuna aliyenifuata, nafikiri ni wanawake ambao wana hekima Fulani, kwani hata kumshauri mke wa mzee zuberi kutogombana ni moja ya hekima tu ilitumika. Na pia nafikiri mama Husna alikuwa akirewind mkanda na kuona ni kama nilikuwa najaribu kulipiza kisasi, japo najua hakuamini lakini baada ya kunipigia simu ndo nilijua kimemuuma.

    Haikuishi hapo tu, baada ya dakika chache kabla sijatoka kwenda nyumbani, mke wa mzee Zuberi alinipigia tena simu,, lakini sikutaka kuipokea wala kujibizana naye, kwani nilihisi yuko na jopo la wanawake wale na sikutaka kuharibu jioni yangu.

    Aliniandikia msg na kuniambia, Nitakuliza…. Sikujibu msg ile. Nilikaa na kutafakari sana nifanyeje.

    Kisha nikampigia simu, na alivyo wa ajabu akapokea, nikwambia mama sikiliza, mkuki kwa nguruwe mtamu kwa binadam mchungu,,, mimi nilishalia, ila najua sasa hivi ndo zamu yako kulia na unalilia machozi yanadondokea tumboni , nab ado utalia sana. Nilimaliza kumueleza hivyo huku akitukana lakini sikujali nilikata simu na kuizima kabisa . kisha niliiwasha na nikamblock. Sikutana usumbufu naye.

    Kilipita kiya cha siku kadhaa, na Harusi ikafanyika, kweli ilikuwa harusi nzuri sana na iliyopendeza mno, kwani mzee Zuberi alikuwa na pesa za kutosha, lakini pia Majdi na familia yao nao walikuwa na pesa ya kutosha, na baada ya harusi Majid na Husna walisafiri kwenda Dubei kwa ajili ya honeymoon. Majid ni mfanya biashara anayechipukia, hivyo alisafiri na kuelekea Dubei na mkewe kwa ajili ya fungate.

    Na mimi nilikuwa nawasubiri kwa hamu.

    Baada ya wao kusafiri, mimi akili yangu ikiwa imetulia kiasi huku nasubiri warudi na waendelea na maisha yao ya wana ndoa.

    Niliamua kubadilika kabisa, mawasiliano yangu na mzee Zuberi yalikuwa ya nadra sana na kwa siri sana, hatukutaka kufumaniwa tena na tulionana mara chache chache sana na kwa vile nilikuwa nataka tu pesa ya kujenga nyumba nilikuwa nikiwasiliana naye ili asisahau ahadi yangu, na siku zote aliniambia anakumbuka, na saa nilimpatia bank accaount number yangu na ilikuwa ni rahisi yeye kuniwekea pesa mara anapoenda bank, na aliniambia kwamba niwe naangalia salio kujua kwamba ananipenda na hatonisahau.

    Lakini kwangu na mume wangu, nilirudisha mapenzi, na tukawa tunaishia kwa upendo wa hali ya juu kama hakuna kitu kilichowahi kutokea. Jones alifurahia sana namna nilivyokuwa namjali na kumpenda na kumtunza, alijifunia mimi.

    Niliendelea kunawiri na kupendeza sana. Na siku moja nilipoelekea bank nilishangaa sana kukuta account yangu imeingiziwa milioni 11, hii ilikuwa ni maajabu kwangu, Haraka sana nilijua tu ni Mzee Zuberi, nilifurahi sana na kweli alikuwa ni yeye, nilifurahi sana na nisingeweza kuacha kumshukuru, niliamua kumpigia simu. Nilimpigia simu na iliiita sana haikupokelewa, iliiita mda mrefu sana, na haikupokelewa kabisa. Badae niliacha. Kwani sikupenda kuandika msg.

    Na sikuandika kabisa msg. Badae sana mzee Zuberi alinipigia simu kwa namba ingine na kuniambia mkewe ameshkilia simu, hivyo nisipige wal akuandika msg, nilimwambia samahani nilitaka kukushukuru tu kuhusu pesa niliyokuta kwenye account yangu,, aliniambia haina neno mwanangu usijali.. mhh, nilishangaa kaniita mwanawe… nilishangaa sana.

    Nilimuaga na kkubaliana sasa tuwe tunawasiliana kwa simu za ofcn tu na sio za mikononi. Nilimuelewa, na alinipenda kwani kila alichoniagiza nilikifanya sawa sawa na alivyosema.

    Shaloo naomba uwe makini ili niweze kukusaidia, sitaki kukutafutia matatizo, ndoa yako bado changa. sawa mama,,, ndio nilijibu.. na alinipenda sana kwa utii wangu.

    Nilirudi nyumbani nikiwa na furaha ya milioni kumi na moja. Na kiwanja hiki sikutaka k umshirikia mume wangu hata kidogo, sikutaka kabisa.

    Ni kiwanja kizuri, kikubwa na kilichopo maeneo ambayo ni hot cake, ni kiwanja ambacho nikikigawa mara mbili na kuamua kuuza pc moja ni zaidi ya mamilioni ya pesa, pc moja tu ya mita 35 x 20 ni kama milioni 40 hivyo ni pesa nzuri sana. Na nilishaanza kuwazakuuza pc moja ili moja nijenge.

    Na wateja walikuwa kila mara wakiulizia hicho kiwanja ni cha nani na je anauza? Hizi ni taarifa nilizokwua nazipata kutoka kwa majirani ambao wanaishi kwenye eneo hilo, na majirani wote wamejenga mijumba ya haja, ni mtaa ambao husifika kwamba ni mtaa wa wenye nazo. Kwani majuumbo yote ya mtaani hapo ni ya kifahari. Na mimi nilikuwa nataka niweke kitu chenye adabu pia.



    ********************************************************************************************



    Maisha yalisonga sana, Majid na Husna walirudi kutoka Dubei, waliishi maisha yao mazuri sana, walikuwa wamepangisha nyumba nzuri tu ya kifahari, Husna alikuwa na gari yake nzuri ya kutembelea, na mara nyingi alikuwa akipendelea kukaa tu nyumbani, hakuwa ni msichana wa kupenda kujishughulisha, zaidi ya kukaa nyumbani. Na alikuwa ni mke wa kwanza kwa Majidi, na majidi naye alikuwa ni mume mkewe wa kwanza.

    Walikuwa na ndoa nzuri. Miezi sita ilikuwa imeshapita, Husna alipendeza sana, alikuwa ni mke ambaye bila shaka aliipenda na kuimudu ndoa yake, alikuwa ni mke wa kujitanda sana na kuvalia vyema, hakuwa mke mang’aa, alimpenda sana mumewe.

    Muda wote Majid aliponitafuta nilimueleza tafadhali naomba kaa na mkeo kwanza, afurahie ndoa yako. Mimi nipo tu wala kisikusumbue. Mimi wakati huo nilikuwa ni mtu wa kupanga taratibu zangu, sikutak Husna asiumie, nilitaka aumie kama nilivyoumia, Na nilipogundua Husna ana mimba nilifurahia sana, nilifurahia sana, nikasema sasa huyu ndiye mke haswa, na kama nikilipiza kisasi kipindi hiki ndipo kitanoga.

    Bado sikuwa na haraka. Deal la flat screen nilishalikancell kwa Majid na nilimueleza tumepata ambaye atatupatia flat screen hizo. Hivyo bado aliamini ninaweza kumpatia biashara.

    Na nilimueleza tu kwamba na mimi nahitaji kufanya biashara za kutoka na kwenda china, na je ni shilingi ngapi kama nikitaka kufanya biashara? Aliniuliza ni biashara gani nataka kufanya? Nilimueleza yoyote ambayo ingelipa, na aliniambia atanisaidia ila niandae kama milioni 50 hivi atanisaidia na kuniambia nifanye biashara gani.

    Haraka nilikumbuka kiwanja, na nilikiweka sokoni. Na baada ya hapo nilikumbuka nina cach yangu kama milioni 15 hivi.

    Kiwanja niliuza pc moja tu na nikapata milini 48, nilifurahia sana, na kisha nilimueleza Majid nina pesa ya kutosha kabisa.

    Alinishangaa nawezaje kuwa na pesa nyingi hivyo? Nilimueleza huwa napokea tenda za watu wengi na wakinituma vitu huwa Napata na faida. Hivyo hizo pia ni kazi zangu.

    Aliamini, kwani aliijua tabia yangu vyema, na sikuwa mwanamke was kendo mtaani, ila asijue ndo natengeneza skendo nay eye.

    Aliniambia akitaka kusafiri atanijulisha, na atashughulikia kila kitu change, kuanzia ticket na visa na kil a kitu, na safari ya kwanza ilikuwa ni tunaenda Hongkong. Nilikuwa nimeshajipanga.

    Niliongea na mume wangu na kumueleza nataka kufanya biashara hivyo anitafutie mtaji. Jones alinipenda sana, na hakuwa akiniwazia mabaya, aliniambia ni biashara gani nataka kufanya? Nilimwambia nataka kufanya biashara ya nguo na chochote ambacho nitaona kinafaa, ila taget yangu ni nguo.

    Alifurahi kwa namna ambavyo nachanganya akili, na aliniambia yeye hana pesa ila kuna mikopo hutokea kazini, anaweza kunikopea kama milioni 20 ila nijue kwamba atakuwa hana pesa kwa yeye kukatwa marejesho ya kila mwezi.

    Nilimhakikishia kwamba mimi ninapokea mshahara mzuri tu, na nitampatia card yangu ya bank ili awe nayo yeye kila mshahara ukiingia basi tusaidiane kubajet, tulimaliza makubaliano yetu vyema.

    Sasa ikawa imebaki muda ufike ili nisafiri.

    Ni kama miezi mitatu mpaka kusafiri, Na tayari nikawa natafuta frem.

    Na jones naye akinisaidia kutafuta frem.

    Husna ujauzito uliendelea kukua, nafikiri sasa ni mimba ya miezi 7 ama 8.

    Safari ya China iliwadia. Nilikuwa nimekamilisha kila kitu change, kuanzia pesa, passport na visa. Hakuna ambacho sikuwa nacho.

    Kazini niliomba ruhusa yangu ya mwaka mzma. Siku 28. Na pia sikujali sana kazi wkani sasa nilikuwa nataka kuwa mfanya biashara na kujikita kwenye biashara, niliona inavyolipa na mtu pia kupata muda wa kupumzika na kujipangia mambo mwenyewe. Niliamini ili uwe tajiri ama matajiri wengi ni wale ambao wametoka kwenye kuajiriwa, kujiajiri kisha Kuajiri, hawa ndio niliamini ni matajiri. Nilitamani kujiajiri kisha niajiri na mimi watu siku moja.

    Nilishaanza kuona ukubwa wa duka langu la nguo, pochi na viatu, nilitaka kuwa famours in town ndizo ndoto zangu.

    Saa kumi na mbili jioni tayari safari ya kuelekea airport ilianza. Mume wangu alinisindikiza mpaka airport.

    Nilifika na tukawa tumekaa kwenye restaurant huku tukiwa tunapata kahawa tukisubiri muda usogee kidogo kwani tuliwahi sana kuogopa jam za mji.

    Baada ya nusu saa nilimuona Husna na mumewe, niliweza kumgundua Husna baada ya kumuona Majdi, Nilitaka Husna anione na ajue ninasafiri. Hivyo nilimwambia mume wangu kwamba sasa nataka kucheck in kabla foleni haijawa kubwa.

    Mume wangu alinikumbatia na tukaagana na akaondoka.

    Kisha nilienda kukaa kwenye vitu nikisubiri kucheki in.

    Baada ya kuhakiki Jones kashaondoka, nikiwa nimevalia Skin tight nyeuzi ambayo imeshika umbo langu sawia nd dress top nzuri ambayo ilinikaa vyema,, nilichukua cheni zangu mbili za miguuni kwenye pochi na nikazivaa, zilikaa vyema mguuni kwani Mungu kanijali mguu wa chupa ya bia,, na sendoz nilizovaa zilikamilisha umaridadi wa muonekano wangu wa miguuni. Kila mwanaume alinitazama kwa kunitamani.

    Baada ya sekunde kadhaa nilitazama huku na huku, kisha nikaona Majdi na Husna wakiwa wanaagana… Nilipata kicheko moyoni,, huku nikishangilia sana .

    Majid alikuwa na uhakika kabisa kwamba mke wake hanifahamu, hivyo hakuwa na wasi wasi.

    Nilipita mbele yao,, Husna nilimuona kama ameshangaa Fulani hivi… Kisha nikapiga simu kumuaga rafiki yangu na kumueleza naenda china na nitarudi baada ya siku kadhaa.

    Nilimuaga na Husna akasikia, lengo langu ilikuwa ni Husna atambue kwamba ninasafiri na mumewe.

    Kisha nilisogea na kurudi kukaa kwenye kiti nikisubiri muda wa kucheki in ufike.

    Muda ulifika na nailicheki in. Nilijua tu Husna ana mawazo, kwani kila nilipogeuka nilikuta akinitizama. Asiweze kuniambia lolote, na mumewe alipocheki in nilimsogelea na kumsalimia kwa mmkono, huku tukiwa tunaongea mawili matatu, Na husna alituona tukiongea,, maskini tayari nilishamuwekea alama ya ulizo. Na ndilo lilikuwa lengo langu, ajue maumivu ya mume na utamu wa mume. Hili ndilo nilikusudia miaka miwili iliyopita ya seke seke zima, na kuhakikisha KISASI CHANGU KINAFANIKIWA.

    Tulisafiri, na Majid alizima simu yake.

    Nilishangaa kupigiwa simu na mtu ambaye nina takribani miezi kama tisa hatuwasiliani,, akili ikaniambia huyu lazima ametumwa na Husna, kwani ni mtu ambaye pia alimfahamu husana na kisanga kizima.

    Nilisema sasa ni muda wa kumueleza kila kitu kuhusu safari yangu. Nilimueleza nasafiri kwenda china, hongkong nitakaa huko siku kama 14 hivi, nimeenda kuvuta raha tu na kutuliza akili.

    Aliniambie niko na nani? Nilimjibu si juu yako kufahamu, ila take care, nikirudi nitakuletea zawadi. Akaniambia basi usiache kunitumia mapicha yaw hats app, nikamwambia poa hizo umezipata,, na kwa kuanza tu nilimtumia picha kama mbili hivi ambazo mimi niko mbele form y amble na Majdi yuko form ya nyuma yangu tukisubiri ku board, nilifanya makusudi nikijua na kuhisi katumwa.

    Husna roho yake ilikuwa ikidunda sana, bila shaka. Kwani huyu aliyekuwa akiwasiliana na mimi ni kama aliyekuwa akisukumwa kufanya hivyo na nilijua tu ametumwa. Baada ya dakika chache nilimuaga na kumueleza ninazima simu tutaongea nikifika, nikakata simu, na hao tulikuwa tunaelekea kwenye ndege.

    Safari yetu ilikuwa nzuri sana nay a utulivu wa hali ya juu.

    Tulifika na kupokelewa na mwenyeji wa Majid, Majid aliniambia huwa hapendelei kufikia hotelini na huwa anafikia kwa mwenyeji wake huyo, na tulienda pamoja .

    Kweli nilikuwa nashangaa sana kwani ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kutoka nje ya nchi na kwenda kwenye nchi kama hiyo, nilikuwa nashangaa kila kitu, majengo bara bara na kila kitu.

    Wiki ya kwanza ilikuwa ni wiki ya kutembea na kuujua mji, kisha nikaingiwa uchizi, nikaona kuliko kufanya biashara ya nguo ni bora nifanye biashara ya stationery,, niliona inavyolipa, basi nilkaa na kupiga mahesabu na kuona endapo nitamua kufanya biashara ya stationery nitapata pesa nyingi sana na kufanikiwa sana kuliko biashara ya nguo, na tayari niliamua kuwasilian na Jones na kumueleza. Hivyo akaniambia ni sawa tu, kikubwa nihakikishe kwamba nakwua makini kweye biashara na sio mchezo mchezo.

    Mara zote Husna alipokuwa akizungumza na Majid ni kama walikuwa wangombana, Nilimuuliza Majid ni nini tatizo?

    Aliniambia yani mke wangu sijui kaambiwa umbea gani, kaambiwa nimesafiri na mwanamke ila hataki kumtaja,, na ninajua hakuna mtu anajua issue yangu mimi na wewe. Nilimwambia ni kweli, ila wanawake tuna wivu tu, wewe ongea naye vizuri na muulize anataka ufanye nini ili asikie raha?

    Majid alicheka na kusema dah kuoa kazi kweli kweli. Tulicheka wote, kisha tukaenda kupumzika na kukubaliana siku inayofuata ni kukusana mizigo baada ya kutembea maduka mengi kujua tunataka vitu gani.

    Kweli siku iliyofuata ilikuwa ni siku ambayo tuko busy sana, tulitiembea sana na kuchoka sana, kisha tukapata mizigo yote na kuikusanya, Na majidi akaniambia kwamba ataaweka mzigo wangu kwenye contena lake hivyo nisijali kwani haoni sababu ya kuniombea mizigo yangu kwa baadhi ya watu anaowafahamu, hii ni ili kulinda usalama wa mahusiano yetu.

    Nilifurahia sana na kweli siku mbili zilizofuata ikawa ni kufunga mizigo kwenye contena kisha kuanza hatua za kukabidhi mzigo ili usafirishwe. TUlimaliza process zote hizo salama na sasa kujipongeza, na siku sita zilizobaki kabla ya kurudi Tanzania, tuliazimia kujirusha na kutembea baadhi ya miji ya jirani kuvuta raha tu.

    Tulivuta raka kama tulivyokubaliana. Na baada ya kupongezana tulijiandaa kurudi Tanzania. Kiusalama zaidi, Nilitangulia mimi na siku iliyofuata Alikuja Majid.

    Jones alifurahia kuwa na mwanamke kichwa ambaye anawezakubuni biashara nzuri kwa haraka. Nilifika na kumueleza kila kitu kuhusu safari yangu, na miji ya china ilivyo, alitamani sana kusafiri nay eye. Nilimwambia tuombe Mungu biashara iwe nzuri kisha tutasafiri tu.

    Aliniambia ameshapata frem, na tulianza kuifuatilia na kuiandaa kwa ajili ya kuweka biashara yetu.

    Baada ya muda kidogo tu, mizigo iliwasili na kufngua stationery. Ilikuwa kubwa, nzuri ,nilikwua na mashine za photocoyy. Scarner na kila kitu, kila mteja aliyekuja pale alipata huduma zote alizohitji pamoja na kuuza bidhaa zote za muhimu ambazo zinahitajika kwenye stationery. Nilianza kuktafuta wateja kila mahali, Na mzee Zuberi alinisifia sana kwa kazi nzuri niifanyayo na alinitafutia wateja kwa hali na mali. Sasa nilikuwa naingiza pesa bara bara.

    Maisha yalianza kuwa matamu, na niliandika barua ya kuacha kazi. Na niliacha kazi. Wala sikujuta, stationery yetu tuliiweka karibu na maeneo ambayo watu walihitji huduma hiyo.

    Siku moja nikiwa ofcn, Majid aliamua kunitembelea, Alikuja na hakuamini kunikuta kwenye stationery ambayo imejaa, imependeza sana, na kwa vile kazi hiyo niliisomea nilitafuta pia wasichana wawili wambao ni liwakagua vyema na kujua wanaijua kazi hiyo vyema na kuwaajiri. Biashara ilikuwa nzuri sana, Majid alinisifia sana na alinipenda sana.

    Sasa kupatikana kwangu kukawa shida, kwanza kumbuka Sikumpenda Majidi kimapenzi ila kulipiza kisasi.

    Kisha sasa nina biashara yangu naifanya na sitaki kuharibu biashara yangu, hivyo kunipata kwangu ikawa taabu sana, na hakuweza kuvumilia, ikawa anapiga simu kila mara hajali tena, na mkewe akawa yuko kwa mama yake akila uzazi, alijaliwa mtoto wa kike.

    Maisha yangu yalikuwa mazuri mno, ni kama nilikuwa natamani sasa nisilipize kisasi, lakini hapana nitaachejee kulipiza kisasi ili hali Husna hajaonja joto ya jiwe?

    Hili ndilo lilikuwa likinikera, ni lazima kimuume kama kilivyoniuma mimi.

    *************************************************************************



    Sehemu ya Mwisho ya kisa cha Charlote. Alivyoamua kulipiza kisasi baada ya kugundua mahusiano yamapenzi ya mumewe, na kuvunja ndoa Tatu



    SEHEMU  YA KUMI



    Majid alinisumbua sana. Hakunipa kabisa nafasi ya kupumzika. Muda mwingi alinitaka. Na mimi nilikuwa busy. Lakink pia sikutaka jones ajue lolote. Majidi alinisumbua kila mara kwa simu. Alishindwa kabisa kujizuia. Nilijaribu kuongea naye kwamba ajaribu walau kuwa na kiasi asijisahah sana. Aliniambia wazi kwamba hawezi. Penzi langu limekuwa zito sana moyoni mwake.

    Alinieleza namna ambavyo kinamuuma kunikosa.

    Sasa alipiga simu mpaka usiku. Na aliniambia mamii ni bora upokee simu kwani ukiacha nashindwa kukuelewa. Nilijaribu kupokea kwa kificho hivyo hivyo. Sasa alianza kunikera. Na nikaona ni bora walau nimridhishe kidogo.

    Niliendelea kupanga miadi na yeyw ya kukutana. Ili mradi tu mume wangu asijue.



    Mimi na Jones tukishakubaliana kwamba kila mtu simu yake iwe huru. Na hivyo hatupaswi kuweka pw. Hivyo niliacha simu yangu wazi. Na kila mmoja alikiwa huru na simu ya mwenzake.

    Sasa majid kawa kichomi. Ni lazima niweke simu yangu pw. No mata what.

    Niliweka. Jones alikasirika sana. Lakini sikujali. Bora akasirike kwa asilolijua kuliko ajue.

    Ugomvi ulikuwa mkubwa sana. Ila nilimwambia sina tatizo isipokuwa nimeweka kwa ajili ya mambo yangu biñfsi. Na baafae nilimwambia nimesahau pw. Ilikuwa ugomvi. Simu ya kwanza tuligombana sana. Alitaka kujua nani kapiga simu saa nne usiku tukiwa tunawatch movie. Na kwa nini nimepimelea jikoni. Nilimueleza nilienda kufuata maji. Akasea kwa nini niliongea pole pole?

    Sikuwa na jibu. Tukikurupushana. Akaichukua simu na kuibamiza

    ukutani.

    Jones alichukia sana. Bado niliona bora kaona hiyo ya kuvunja simu kuliko kujua niko na majid.



    Maisha yakaanza kuwa mabaya. Sasa jones alinifuatilia sana.

    Nikiwa na majid nilimueleza ajaribu kuwa makini.

    Sikia shaloo… nakupenda sana. Siwezi kujikaza. Siwezi. Kumbuka na mimi nina mke. Na mke wangu karudi. Ila kuna saa natoka nje kuongea na wewe. Hembu ona hili mamiii. Nakupenda. Sana mnoo. Jaribu kulitambua hili mama. Nakupenda sana.

    Alinieleza hivyo nguvu zikaniishia.

    Majid alishindwa kweli kujizuia.

    Husna alishaaanza kuwa na mashaka na mumewe. Tena mashaka yake aliyaweka wazj juu yangu. Japo hakutaka kuliweka wazi kwa mumewe aliogopa kuhisi.

    Na ninafikiri alitaka kuwa na uhakika.

    Ni miezi imepita sasa. Husna mwanaye ana miezi sita. Ni siku ya birtday ya mwanae.

    Jambo hili nililifahamu mapema. Na siku hii nilimueleza majid ni birrhday yangu pia. Ila nilimanganya.

    Nilitaka kumsumbua tu katika kuhakiki nakamilisha kisasi changu.

    Akili hizi za kishetani na kifirauni sijui nilizitoa wapi. Sikuwa na woga hata kidogo.

    Nilimuomba Majid niwe naye usiku huo.

    Sikujali sana kwangu. Ila nilitaka kuwa na majid.

    Majid alihangaika huku na huko kutafuta zawafi zangu. Na alishakamilisha.

    Kisha akanipigia simu kuniambia tukutane wapi.

    Niliendelea kumsumbua sana siku huo kwa ajili ya birthday yangu feki.

    Mkewe alihisi jambo. Na akamuuliza mumewe hiyo ni namba ya shalote?mum alikana. Hivyo kukawa na ugomvi fulani hivi nyumbani.

    Majid akaamua kuondoka. Na birthday ikaanza kuharibika. Maana husna aliijua namba yangu. Hakuwa anabahatisha.



    Baada ya kukutana na majid alinieleza kama mkewe ananifahamu. Nilimueleza sijui labda ila sina mazoea naye.

    Aliniambia kaona simu inaita akaweza kugundua namba yako. Mh… nilishangaaa ila moyoni nilikuwa na raha sana.

    Nilifurahia kuona sasa Husna anaanza kukosa usingizi kama mama yake.

    Nikifurahi mno.

    Usiku wote huo nilikuwa na Majid. Sijui aliahaje kwake. Na mimi niliaga nilivyojua. Wote tukawa hotelini.

    Jones alishanichoka sasa. Alishajua nimekuwa mke sugu nisiyesikia. Na alishajipanga kwa lolote. Alichoka kunibembeleza.

    Haikuwa kawaida kwa Majid kulala nje.

    Majid aliingia kuoga na kuacha simu yake. Niliichukua na kutoka nayo nje. Kwani ilikuwa inaita sana.

    Nilipoangalia niliona jina la my wife ikiita.

    Nilipokea na kucheka kwanza

    Ha ha ha.. Husna.. usijali. Anakuja muda si mrefu. Tulikuwa wote na yeye hotelini. Pole mamiii. Jifunze kumtosheleza mumeo. Bye.

    Na nilizima simu. Sikumpa nafasi ya kujibu wala kupiga. Ni kama aliyekosa nguvu. Akilalamika sana na kukosa muelekeo nilimgundua kwenye simu.



    Majid alitoka kuoga. Kisha tukanywa chai na kuondoka.

    Nilipitia stationary kwangu. Nilikaa kwa muda kisha nikaenda nyumbani. Sikumkuta mr. Hakuwepo.

    Nilijibwaga kitandani nikishangilia seke seke la majid na mkewe .

    Baada ya kama nusu saa simu ya majid iliita. Nikiwa kitandani nimekaa niliongea na majid kwa uhuru sana. Huku akinielezea kuhusu mkewe kulalamika mimi kumpigia simu.

    Nilimueleza kwamba ni kweli. Akaniambia kwa nini umefanya hivyo shalote?alionekana kugomba ssna. Mimi nikiwa nacheka tu.

    Huku akiniambia mkewe anahasira na anaweza kuvunja ndoa.

    Nilimwambia tafadhali naomba tukutane mahali tuongee nimueleweshe jambo.

    Alikubali. Asijue kama mkewe anamsikiliza kwa maongezi hayo.

    Na kujua tunapoenda kukutana.

    Haraka aliwasha gari. Na mimi nilikurupuka nilipokuwa. Kisha nikamfuata majid. Tulikutana kwenye hotel yetu kama kawaida.

    Sikutaka tuzungumze nje. Nilimwambia tuzungumze ndani. Alikubali.

    Tuliingia ndani.

    Nilimueleza majid kila kitu kuhusu mkewe na jones. Nilimueleza mwanzo mwisho.

    Alisikitika sana na kuniambia Shaloo kwa nini umenipa penzi feki? Na kuniharibia ndoa yangu na kutembea na baba mkwe wangu?kwa nini?

    Majid alilia sana na kujilaumu mno.

    Nilimueleza hii ndiyo njia pekee ya kuganga moyo wangu na ninaomba tu unisamehe.

    Tukiwa tunaendelea kulumbana na Majid. Mara tukishangaa mlango unagongwa. Na niliona askari wawili. Wa kike na wa kiume.

    Kisha wakatuambia mko chini ya ulinzi.

    Dakika chache tukisikia kishindo cha watu wakitembea.

    Alikuwa ni husna.jones. wadhamini wangu wa ndoa na mama yake husna.

    Walikuja pamoja wote. Na husna akidai talaka.

    Ilikuwa aibu fulani ila mimi nilikuwa nashangilia fulani kujiona mshindi.

    Tulifikishwa polisi. Na kuandika maelezo. Jones alikuwa akilia ssna. Na husna pia.

    Baada ya maelezo tuliachiwa kwq dhamana. Na kutoka. Majid alielekea kwake na akatoa talaka.

    Na mimi nikagoma kwenda nyumbani. Nikaenda kwa mdhamini. NikamueleA kwamba sasa naweza samehe jones kama atanisamehe. Jones alikuwa akilia tu. Na akisema hawezi kunisamehe kamwe.

    Niliwaambia wadhamini hili ndilo nililitaka. Waone je msamaha ni jambo jepesi tu?

    Jones alijilaumu sana kunikosea.

    Nilikaa kwa wadhamini wiki nzima na ndipo nikawaeleza kwamba sasa nahitji kuwa na maisha yangu.

    Wakasema hapana mpaka wazazi wajulishwe.



    Sikutaka kukaa kikao cha aibu na wazazi wangu. Singekuwa na la kuongea. Kila walipouliza kuna shida gani niliwaambia jones anajua. Na walipomuuliza jones aliwajibu shaloo anajua.

    Maisha yakabadilika. Nikaanza kuishi mwenyewe. Ila mwenye furaha sana. Husna alirudi kwao kwa talaka kabisa na kuiacha ndoa. Majid alisikitika sana.

    Mzee zuberi nilimheshimu. Hakutaka kuongea na mimi mapema.

    Na alitambua jambo hilo. Alisikitika sana. Maana sasa alijua yeye na mkwe wake wameshea msichana mmoja.

    Na bahati mbaya sana mama husna alimueleza Husna juu yangu na dadiye. Kiliwauma sana. Waliumia sana.

    Husna alikonda na kuanza kuparama. Hii ni kwa sababu ya maumivu ya ndoa yake. Lakino shaloo kuwa na baba yake pia kikimuuma.

    Jones aliendelea kuwa na hasira. Sasa alilewa. Hakupenda kula. Maisha yakamuwia magumu hasa.



    Story zilianza kichini chini. Watu wasiamini kwa kilichotokea. Maana walijua shaloo mimi mpole sana. Nikapiga mahesabu nitafanyaje.

    Nikaanza kuhangaikia sasa future yangu. Sina jipya kwenye mapenzi na mahusiano. Nimeshachefukwa. Nimelipiza kisasi nafsi yangu kwatuuu. Nilichofanya ni kuuza ile stationary. Nikapata chance ya kwenda Denmark. Nikakaa huko miaka miwili kwa rafiki yangu huku natafuta kazi. Kisha nikamaliza miaka miwili. Nikapata rafiki wa kizungu m denmark ambaye alitaka nichukue wanangu. Nikarudi tz nikakuta Jones amechoka na pombe nikamaa naye miezi miwili huku namuomba watoto ambao walikuwa kwa mama yake. Mama yake akakubali na nikachukua wanangu

    Husna mpaka leo hajaolewa.

    Jones ameshajaribu mahusiano zaidi ya mara tatu. Na msichana mmoja alishi naye na kuzaa naye ila wakashindwana. Ndiye ambaye alinipokea nilipotoka denmark.



    Sasa Naishi na wanangu Denmark. Jones yupo tu. Husna yupo tu.

    Maisha yamekuwa Mazuri kwangu. Nimeathirika sana saikolojikali. Maana najiuliza mwanaume mzuri ni yupi?jones hakufaa. Majid hakufaa. Mzee zuberi hakufaa. Wote sio waaminifu.

    Hili limenifanya nachukia sana mahusiano na kuchukia mwanaume.

       

0 comments:

Post a Comment

Blog