Search This Blog

Friday, November 18, 2022

FUNDO LA UMIVU - 5

 





    Simulizi : Fundo La Umivu
    Sehemu Ya Tano (5)






    Kwa siku hiyo hakufanikiwa. Alifanikiwa siku iliyofuata, alipata ruhusa, kwa kisingizio cha ugonjwa uliokuwa unamsumbua kipindi cha nyuma, ugonjwa wa ini! Kuanza kumsumbua. Hivyo aliomba ruhusa kuwa anakwenda hospitali kuhudhuria kliniki ya ugonjwa huo. Ambayo alikuwa nayo kipindi cha nyuma. Alipewa ruhusa ya siku tatu. Alifurahi, tena alifurahi haswa, na kuuona mwanga wa mafanikio wa kile kilichopo mbele yake. Maandalizi yalivyokamilika aliondoka na kwenda kulala nje ya kambi kwa Madam Cecy, ambaye alikwishafahamu mipango yote iendeleayo. Siku ya safari ilivyowadia, mapema sana, akiambatana na Mzee Matatizo waliwasili kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoni, kilichopo Ubungo. Waliiendea moja ya basi inayoelekea kule wanakohitaji na kukata tiketi. Walivyokamilishiwa, hawakuwa na haja ya kuzubaa zubaa, waliingia ndani ya basi na kuketi siti husika zilizoandikwa kwenye tiketi walizokabidhiwa.



    Safari ilianza saa 12:00 asubuhi. Ndani ya basi la Dar Lux ielekeayo jijini Mwanza. Walikuwa tulivu, huku wakikesha kuangaza angaza mazingira ya maeneo mbalimbali wapitayo. Na muda mwingine kuangalia burudani iliyokuwa inatolewa kwenye skrini zilizofungwa ndani ya basi hilo. Lenye mahadhi ya kifahari. Baada ya mwendo wa muda mrefu, hatimaye basi liliwasili kituo cha mabasi mjini Dodoma, kilichopo maeneo ya Nanenane. Mzee Matatizo na Upendo waliteremka, kisha, kuita bajaji na kumuamuru dereva awapeleke mjini wawezako kupata sehemu yenye huduma ya malazi kwa siku hiyo. Dereva alifanya hivyo, aliwasha bajaji yake na kuianza safari. Ambayo moja kwa moja iliishia maeneo ya Jamatini. Huko walichukua vyumba katika moja ya loji waliyopendezwa nayo, na kupumzika kutokana na uchovu wa safari uliowachukua zaidi ya saa kumi. Kesho yake walianza rasmi shughuli iliyowapeleka punde walivyomaliza kupata stafutahi. Na kukabidhi funguo za vyumba walivyolala jana yake, ikiwa na maana hawatoendelea kulala hapo.

    “Itakuwa vipi kuhusu kulala kwa baadaye? Ilhali mwanao anaishi chumba kimoja na ana huyo mwanamke?” aliuliza Upendo, pindi wakimaliza kuutembea faja wa loji waliyofikia.

    “Tutabanana humohumo chumbani. Ama nitawaacha kisha mimi nitaenda kulala sehemu yoyote ile.”

    “Huogopi kuitwa mwizi?”

    “Hayo ni matokeo ya mafikirio. Yaweza tokea ama yasitokee.”

    “Mmmmmh! Una moyo.”

    “Yeah! Lazima niwenayo. Kwani sipaswi kuonesha uoga. Siku zote ushindi ndicho kipaumbele kwangu,” alisema Mzee Matatizo wakizidi kuchanja mbuga kuelekea sehemu ambayo hawaifahamu.

    “Sasa tutaanzia wapi kumpata?”

    “Hamna sehemu nyingine, zaidi ya kwenda kituo cha polisi kumuulizia.”

    “Ooooh! Hapo umenena mkwe wangu, ndiyo maana huwa nakukubali sana.”

    “Upo na mzee mjanja, kwa huko kijijini kwetu. Ila ni mshamba kwa miji mingine. Ndiyo maana huwa nashangaa sana,” alisema Mzee Matatizo, kauli iliyoambatana na kicheko mwishoni toka kwa wote.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Mbele, waliita bajaji na kumuomba dereva awapeleke katika kituo chochote cha polisi, ambacho ndicho kingelianza wapatia msaada wa kumpata yule wamtakaye. Vumilia! Safari haikuwa ndefu sana, ilikuwa fupi tu, na baada ya dakika nane, dereva bajaji alipaki mbele ya kituo kikuu cha polisi kilichopo jirani na kambi ya askari. Walilipa kisha kuteremka. Na kuongoza moja kwa moja kaunta, wakapokelewa na askari wawili, mmoja akiwa na tepe ya sajini mwingine tepe ya koplo na kwa mbali alisimama askari mwingine asiye na tepe yeyote begani. Alikuwa konstebo, aliyeonekana kushughulika kuandika maelezo ya raia mmoja aliyosimama mbele yake. Walijitambulisha, ila Upendo hakujitambulisha kuwa ni askari jeshi, wa jeshi la wananchi, kwa kuhofia kuulizwa mwasali kemkem kuhusu nyaraka zake zinazomruhusu kusafiri toka kambini kwao. Mzee Matatizo, ndiye alikuwa mzungumzaji. Aliongea huku akionesha picha ya mwanaye, Vumilia, aliyovaa sare za kazi kukazia kile waulizacho kuonyesha kuwa hawajakosea. Bali humaanisha.



    Yule sajini na koplo ndiyo walikuwa wanafuatilia maongezi hayo, wakati huo wakiichunguza ile picha kwa makini, na kuvuta kumbukumbu kama wanamfahamu ama lah! Walitumia takribani sekunde hamsini, lakini baina yao hakuna aliyeonekana kumfahamu Vumilia. Baadaye ilibidi wamuite yule konstebo, walimuonesha ile picha na kumaptia maelezo machache yahusuyo.

    “Aaah! Huyu si Vumilia,” alisikika yule konstebo. Alimtambua kwa haraka tu. Kwani alikuwa wa depo yake.

    “Anaishi hapa kikosini?”

    “Hapana! Yupo kule Kisesa.”

    “Una mawasiliano naye umpigie awafuate wageni wake hawa.”

    “Haaa! Sawa,” alisema konstebo huyo, na kutoa simu yake ya mkononi mfukoni.



    Aliitatufa, kwa kupangusa kikoo cha simu yake ya kisasa, aina ya Oppo F3, alivyoipata, hakusita, kufikiria kama ana salio, au hana, alipiga. Simu iliita kwa muda mchache, kisha kuingia kwenye mazungumzo.

    “Mbabaishaji!” aliita yule konstebo, aliyefahamika kwa jina la Manjambwa.

    “Niambie kijana,” alisikika Vumilia.

    “Wahi chap, Kituoni hapa, kuna ugeni wako,” alisema yule konstebo na kukata simu.



    Waliombwa kufanya subira, kwa muda mfupi, wakimsubiri mlengwa wao. Ambaye katu, hakukawia. Dakika tisa tu, toka simu ile ilivyokatwa, aliwasili kituoni. La haula! Vumilia alishtuka. Kwani, hata kabla hajaonana na yule aliyempigia amuonyeshe wageni wake, alikumbana, ana kwa ana na na Mzee Matatizo, baba yake, akiwa ameketi chini ya muembe pamoja na Upendo. Alinyong’onyea, moyo ulibadili hali, ulijaa mashaka, hasira na mfadhaiko ghafla kwa kutotaraji kuona akionacho. Pia isitoshe, alifahamu dhamira ya ujio wao ni nini. Hakuwa na budi, ni mzazi. Hivyo alipiga miguu kuwafuata pale walipoketi. Pindi anawasabahi, yule konstebo aliyempigia simu alijumuika nao pamoja. Kutoa maelezo kadhaa kuhusu simu aliyopiga, kisha naye alitambulishwa ugeni huo unamhusu vipi Vumilia. Baada ya zoezi hilo kuhitimika waliondoka. Kuelekea kituo cha daladala, ambapo walifanya subira, kusubiria hiace za kuwapeleka Kisesa anakoishi. Umbali mdogo toka mjini. Walibahatika, punde tu walivyowasili, kosta moja ifanyayo safari zake Vyeyula kwenda Nanenane, iliwasili kituoni hapo. Haraka sana walipanda na kufanikiwa kupata siti, wakaketi. Muda wote Vumilia alikesha akiwaza. Mambo yatakuwaje afikapo nyumbani, na ugeni huo, ambao kwa namna yoyote ni sumu kwa Zamzam. Alitamani kuwapeleka hata kwa rafiki yake yeyote, ili awafiche wasipate kumuona Zamzam, kwa kuhofia varangati litalozaliwa. Ama hofu ya kumkimbiza Zamzam moja kwa moja.



    Sauti ya kondakta, iliyonadi kuulizia abiria wa kuteremka Kisesa, ndiyo ilimshtua toka kwenye tafakuri iliyomchukua muda mrefu. Na kumuamuru kondakta awashushe eneo hilo. Gari ilisogezwa pembezoni mwa barabara, waliteremka, na kuanza kutembea kwa mguu kuelekea sehemu husika anakoishi. Haikuwa safari ndefu sana. Ya muda mchache tu, waliwasili, na kupokelewa kwa ukarimu na Zamzam, huku moyoni akiwa mwingi wa chuki, kisa, kumuona Upendo. Ila hakutaka kuionyesha waziwazi, baada ya kutaarifiwa kisiri kuwa yule aliyeongozana naye ni mkwewe. Hivyo alikuwa na mawili, kuondoka, kuachana na Vumilia, ama kuonesha mvuto kwa mkwewe ambadili imani iliyotawala akilini mwake.

    “Mke wangu, usijisikie vibaya juu ya ujio wa hawa watu. Mimi ndiye muamuzi, japo umenibadilikia, ila bado nina mapendo nawe. Hivyo, kama nawe bado moyo wako upo kwangu, unaweza baki, kama haupo ruksa kufanya utachodhamiria,” alisema Vumilia kwa unyonge sana. Sauti iliyojaa tamanio la kutoa machozi, pindi akiteta jambo na mkewe Zamzam kumfahamisha ujio wa ugeni uliowatembelea.



    Zamzam hakutoa mrejesho wowote zaidi ya kutumbua macho yake kumuangalia Vumilia, namna alivyonyongeka. Ishara ya kutokubaliana na kitokeacho. Walivyomaliza alirudi sehemu aliyowaacha wageni, huku akijivika furaha usoni, ili asionekane kachukizwa. Shida ilikuja kiza kilivyoingia, sehemu ya kulala. Watalala vipi? Ilhali kuna chumba kimoja na sebule. Vumilia alijitahidi kuwazua, lakini akili haikuwazuka namna ya kutatua suala hilo. Ilifikia mahali, alitamani hata kuondoka kwenda kwa rafiki yake yeyote aliyeingia kazini usiku huo wakalale na mkewe, ili pale kwake awaache wageni. Ila wazo hilo nalo, halikuafikiwa, baada ya kutafakari umbali uliopo toka anakoishi na kwa huyo mtu aliyemfikiria. Hakuwa na budi, ilimpasa akubali matokeo, vyovyote itavyokuwa ili siku ipite, halafu kesho aandae mazingira mazuri.



    Usiku wa siku hiyo ulipita, kwa wale wageni kuwaacha walale ndani, Mzee Matatizo chumbani, Upendo sebuleni, wenyewe uani. Walitandika mkeka, wakalala. Ila baadaye yalifanyika mabadiliko, baina ya Mzee Matatizo na Upendo. Upendo alielekea chumbani, Mzee Matatizo sebuleni pasipo wenye nyumba kutaarifiwa.

    “Kama una vyovyote vya kufanya, fanya ili mambo yako yakae sawa,” alisema Mzee Matatizo pindi wakipishana. Akimtaka kama ana mchezo wa kuchezesha, utaoharibu mahusiano ya Vumilia na Zamzam huo ndiyo wakati wake.

    “Aaaah! Baba, nawe una mambo,” Upendo alichangia, kauli iliyoambatana na kicheko.



    Asubuhi kulivyopambazuka, punde walivyofanya usafi wa mwili na kusabahiana maongezi yalianza. Kuhusu lengo lililowapeleka wageni mahali hapo. Wakati huo, Zamzam alikuwa anasikilizia dirishani. Akiwa nje anakosha vyombo. Hasira ikiwa imetapakaa tele moyoni, iliyojidhihirisha kwa namna sura yake ilivyofura. Na yote ni kwa sababu ya kukosa maelewano baina yake na ugeni uliowatembelea. Kwani, walikosa kuzungumza, na kila alivyojitahidi kuonesha wema mbele ya mkwe aweze kumshawishi, mkwe alimtolea maneno ya kejeli, yaliyokosa kuvumilika.

    “Mwanangu hawezi oa mwanamke kama wewe. Hebu nitolee hapa sura yako,” aliwaza Zamzam, akikumbuka kauli aliyotamkiwa asubuhi na Mzee Matatizo alivyoketi mbele yake kumsabahi.



    Hakika! Furaha ya ndoa aliisikia kwa jirani. Kwake haikuwepo kwa muda huo. Kutokana na wingi wa mawazo yaliyokesha kunyanyasa moyo wake, kufikiria hatma itakuwaje. Si kama hampendi mumewe, Vumilia, hapana! Anampenda. Tena sana, ila kikwazo kipo kwa mzazi. Aliyetawaliwa na imani za kikale, huku akisahau dunia kila leo inabadilika.

    “Mwanangu, huyo mwanamke uliyonayo sasa hakufai. Huyu ndiyo mwanamke sahihi kwako. Mzuri, tabia zake ni njema, kushinda hata huyo kinyaragosi unayemng’ang’ania. Kakuwekea nini huyo? Mbona unashindwa kuambiwa kila unaloshauriwa?” alisema Mzee Matatizo kwa sauti ya ukali, iliyosikika vyema kwa Zamzam na wapangaji wengine wa jirani.

    “Huyo kakuroga wewe ndiyo maana huambiliki. Na nasemaje, ukiendelea nayo mimi usinitambue kama mzazi wako. Lolote litalokupata, ni lako. Usituhusishe watu wa nyumbani,” aliendelae kuongea Mzee Matatizo pasipo mpatia nafasi Vumilia ya kujitetea.

    Muda wote Vumilia alikuwa kimya, kila alivyojaribu kutaka kuzungumza alishindwa, kutokana na Mzee Matatizo kutotoa mwanya wa yeye kufanya hivyo. Upendo naye alikuwa kaketi mbele yake kapiga goti akibembeleza hitajio lake likubaliwe.

    “Haina haja ya kuongea kwa nguvu na kuwafaidisha majirani. Hata ukizungumza kwa utaratibu nitasikia pia. Maoni yako nimeyasikia, ila mimi nitabaki kuwa vilevile nilivyokuwa mwanzo. Siwezi badilika, na katu, sitomuacha Zamzam kwa ajili ya Upendo. Namfahamu Zamzam, hizo sabab...” alisema Vumilia punde alivyofanikiwa kupata mwaya wa kuchangia. Ila hakuweza malizia kauli yake, alikatishwa na Mzee Matatizo.

    “Ona sasa, onaaaa, unavyoenda kuharibika. Kakuwekea nini huyu mtu? Sio bure, hapa inabidi tumlete mganga akutoe hicho ulichowekewa,” alisema Mzee Matatizo. Kauli iliyochangia kupandisha hasira moyoni mwa Zamzam pale nje, kiasi kwamba hata vyombo alivyokuwa anaviosha alivitupa chini na kutoka mbio.







    Kishindo cha vyombo kuvunjika kilimwinua Vumilia pale alipoketi. Hima alipiga hatua kuelekea nje kushuhudia kulikoni. Alivyofunua pazia na kuangaza, akaona vyombo vingi vilivyotengenezwa kwa udongo vimetapakaa chini, vikiwa vipande vipande, vimevunjika vibaya mno, na alivyoangaza mbele, akamuona Zamzam akikimbia mithili ya mtu aliyeanza kurukwa kichaaa. Hakuvumilia, naye ikambidi aunge kumfukuzia ili aweze kutambua kilichomsibu. Lakini muda mwingine, alipatwa na wazo kuwa maongezi waliyokuwa wanaendelea nayo ndani, ndiyo yaliyomfanya awe hivyo.

    ****



    Mzee Matatizo na Upendo hawakufahamu kiendeleacho. Ila walijipongeza kwa mwanzo mzuri, ambao waliamini kwa namna yoyote unaweza mwondoa Zamzam.

    “Naamini kwa kauli tulizozungumza yule mwanamke hawezi vumilia. Ni lazima aondoke tu ndani ya nyumba hii. Na akishaondoka mama unatia mguu,” alisema Mzee Matatizo.

    “Mmmmmmh! Yanifaa kuendelea kukukubali mkwe wangu. Maana, ulivyo na ukitendacho havifanani.”

    “Siasa hii mama, ndiyo imenitengeneza na kuwa hivi.”

    “Hongera yako,” alisema Upendo, huku akinyanyuka na kuelekea nje. Mazingira aliyokutana nayo yalimshangaza. Namna vyombo vilivyovunjika na baadhi ya watu waliokusanyika jirani kabisa, walioonekana kufuatilia maongezi yaliyokuwa yanaendelea. Hakukaanalo, alimuita Mzee Matatizo naye aje ashuhudie.



    Mzee Matatizo alivyotokeza, picha ya haraka ikamvaa, kuwa Zamzam kakimbia. Jambo lililochanua faraji moyoni mwake. Baadaye akamvuta Upendo pembeni akamnong’oneza.

    “Ashakimbia, nafasi sasa ni yako.”



    Tena kwa kutaka uhakika zaidi, walimuuliza mmoja, miongoni mwa majirani wapi wameelekea na kujibiwa kile kilichohisiwa. Baadaye walirejea ndani kuwasubiri. Vumilia akisubiriwa haswa, maana ndiye mlengwa. Walifanya subira, wakiwa wanabadilishana mawazo kuhusu hili na lile, hadi usingizi ulianza wanyemelea na kuwapitia kabisa. Walivyokuja zinduka saa zilishayoyoma, na hakukuwa hata dalili ya wale walioondoka kurudi. Sasa ilibidi wajadiliane namna ya kufanya baada ya kuonekana dalili zote za wenye nyumba kutorudi. Ila kuna muda walijipa moyo, kwa kuamini watarejea, hasa Vumilia, kwa sababu atalazimika kwenda kazini, na akihitaji kwenda yampasa kurudi nyumbani aweze kujiandaa. Hadi kiza kilivyoingia, hakuna hata mmoja aliyerejea. Si Zamzam, si Vumilia, hali iliyowapa wakati mgumu kuwazua mambo ambayo katu hawakutaraji.

    “Huyu mtoto anatafuta laana sio bure,” alisema Mzee Matatizo, pindi wakitayarika kwa ajili ya kulala.



    Hawakuwa na budi, walienda kulala. Huku wakiwa na mafikirio makubwa waliyotamani kutokea siku za karibuni. Siku iliyofuata, waliamshwa na sauti ya hodi, iliyobishwa na Vumilia. Aliyeonekana kuchafuka mno masizi na tope jeusi mwilini. Pasi na sahau, mikwaruzo iliyozaa michubuko tele baadhi ya sehemu ya maungo ya mwili wake. Alionekana kufura. Ishara tosha, kuna jambo lilikuwa linamtatiza, kwani hata alivyojaribu kusemeshwa, alitoa majibu kwa mkato. Kwa namna yoyote alikuwa radhi kutofautiana na Baba yake, ili tu, mahusiano yake kwa yule aliyemuamulia yasiingiliwe. Kwa hitajio la kuyavunja.

    “Nishawaambia, kama dhamira ya ujio wenu ni hicho mzungumzacho, ni heri muondoke kwangu. Sihitaji, na wala siwezi kubadilisha msimamo,” alisema Vumilia, kuwataarifu, baada ya walivyomvaa—vaa kutaka kufahamu alipotelea wapi kwa muda asiokuwepo.

    “Lakini baba, wanawake wa kanda ya huku hawakufai. Tabia zao si nzuri, acha ung’ang’anizi.”

    “Daima tabia haziendani. Kila mtu ana tabia yake, hata huo ukanda wa kwetu wapo wenye tabia hizo unazozisema. Ama huyu uliyenaye sasa na kunishauri niwenayo, aidha ni mmoja miongoni mwa hao wenye hizo tabia.”

    “Huyu hana kabisa...hana, hizo tabia. Ndiyo maana nikashawishika muwe pamoja. Ama lah! Uwe nao wote wawili.”

    “Unasemaje?”

    “Ina maana hujanielewa au?”

    “Na siwezi kukuelewa juu ya hiyo kauli uliyoitamka sasa. Uwezo wangu ni wa mwanamke mmoja, na ndiye huyu niliyenaye.”



    Mambo hayakuwa mepesi. Kwani, hata chembe ya mabadiliko ya ushawishi, akubaliane na kile aambiwacho, hayakuwepo kwa Vumilia. Hakuwa radhi wake msimamo kuyumbishwa. Na alikuwa tayari kwa lolote ilimradi abaki katika msitari. Baadaye aliondoka tena, pasipo maagano mazuri. Maana alivyoulizwa wapi anaelekea, alitoa jibu la juujuu lisilo na uelewa kwa yule mwambiwa. Alivyoondoka. Nyuma, waliketi kikao. Cha muda mfupi, kihusucho namna ya kujitwalia ubingwa katika sakata hilo. Kuchezewa, alikochezewa awali, sasa Upendo hakuwa ridhaa kumkabidhi mwanaume yeyote mwili wake tofauti na Vumilia. Mwanaume waliyeshinda kwenye urafiki kwa muda wa miaka miwili ndipo, likafuatia suala la utongozaji. Ambalo Upendo alilikana kutokana na utashi wake. Kikao kilivyohitimishwa, Upendo alipiga simu kwa rafikiye, kuwataarifu kiwango cha mafanikio alichojitwalia. Aliwaeleza kila kitu, nao walipopata pa kuchangia, hawakukosa kuchangia, katika kuboresha, mwenzao atimize alichodhamiria.

    “Huu si wakati wa kuendekeza huo udini wako. Yakupasa kuweka pembeni ili utangulize unyama mambo yaweze kukunyookea,” anasema Mzee Matatizo.

    “Una maanisha nini baba?”

    “Kama nimeamua kukusaidia. Nawe inabidi ujisaidie,...ukiwa ridhaa, twende kwa mtaalamu, ili tumalize haya mambo mapema. Hayo mambo ya dini, sijui nani, weka pembeni kwa muda,” aliendelea kunena, akimsaili Upendo namna apokeavyo ujumbe huo.



    Upendo, alivuta fikra, kufikiri. Macho pima kwa Mzee Matatizo, wakawa wanatazamana, mithili ya wanadeni. Wanaodaiana kwa muda mrefu.

    “Nakupatia muda wa kufikiri zaidi. Ifikapo kesho, hakika yangu, utakuwa na cha kujibu juu ya hiki nilichoteta,” anasema Mzee Matatizo na kuinuka pale alipoketi akatokomea nje.



    Siku iliyofuata, kabla hawajafikiri namna ya kula itakuwa vipi? Na vipi kuhusu wenyeji wao, jambo la kwenda kwa mtaalamu ndilo walianza nalo. Kwa kusailiana mazingira yanavyokuwa, baada ya hapo waliendelea na mengineyo. Maongezi waliyoteta kuhusu mada ya jana iliyovumbuliwa na Mzee Matatizo, Upendo aliiridhia. Tena pasipo kuonyesha chembe ya kusitasita pindi atoapo maelezo yake ya uridhiaji. Hivyo wakakubaliana. Asubuhi hiyohiyo wawahi kwa huyo mtu. Wafanye uuliziaji kwa majirani wakishafanikiwa kufahamishwa waongoze njia moja kuelekea. Ndivyo walifanya. Punde tu walivyostafutahi, walifunga mlango na kuzuru chumba jirani kimoja wapo. Walibisha hodi. Ilivyoitikiwa, mhusika hakuchelea, alitokeza mlangoni. Walisabahiana, kisha walielekea kwenye maongezi husika.



    Bahati iliyoje, yule waliyekuwa wanamsaili kuhusu mtaalamu wanayemhitaji alikuwa muislam. Nao walikuwa wanamhtaji mtaalamu ahusikaye na mambo ya kimajini majini, hivyo, waliamini wataelezwa sehemu nzuri, apatikanayo fundi, hodari na shupavu wa kisomo katika kufanikisha mambo hayo haramu. Ila katika uliza yao hakwenda moja kwa moja kwenye lengo lao. Walimuongopea, kwa kumwambia wanahitaji kwenda kuchukua dawa kwa ajili ya mgonjwa aliyoko nyumbani kwao, watokako. Na kuwafanya wasitiliwe shaka. Jirani, hakuwaficha. Aliwajibu ipasavyo anavyofahamu kuhusu mambo hayo, waliporidhika maelezo yake waliaga na hatimaye kuondoka.



    Waliinza safari, kwa usafiri wa bajaji hadi sehemu husika. Ambayo haikuwa mbali sana toka watokako. Waliteremka, walifanya malipo kisha walianza tembea kwa mguu huku wakihesabu nyumba wapitazo. Walivyoifikia ya sita toka kule walikoteremka walisimama, na kuanza angaza kuitathmini nyumba iliyopo mbele yao, huku wakikumbuka maelezo waliyoambiwa na yule jirani.

    “Mkishateremka hapo stendi, mvukie upande wa pili wa barabara, kisha muongoze hadi kwenye mti mmoja hivi wa mwembe. Mkishafika, mutauona uchochoro fulani, ingieni kwenye huo uchochoro halafu muanze kuhesabu nyumba muzipitazo kuanzia hiyo ya kwanza inayoanza na huo uchochoro. Mkishafika ya sita ndiyo yenyewe. Ambapo mbele yake kuna msikiti mkubwa wa Sunni,” kila mmoja alikumbuka maneno ya jirani. Kwa uthibitisho, waligeuka nyuma kuutazama msikiti walioambiwa.

    “Ndiyo penyewe,” waliropoka pamoja.



    Hawakusita! Waliusogelea mlango, wakaanza kubisha hodi. Iliitikiwa dakika nne baadaye. Baada ya kuita sana na kugonga mlango. Hodi yao ilipokelewa na mtoto mdogo apataye umri wa miaka sita. Hawakumdharau, walimtakia hali, wakafuatia kueleza shida yao. Yule mtoto akawapatia muda wa kufanya subira, awasiliane kwanza na baba yake ndipo awafahamishe Kama wana ruksa ya kuingia ama lah! Kwani, alikuwepo kwa muda huo. Ila alikuwa na ugeni, akiuhudumia. Ilichukua takribani sekunde hamsini na tisa, mtoto kurejea pale alipowaacha kisha kuwapatia mrejesho ulioamuliwa na baba yake. Maelezo waliyopatiwa na yule mtoto kwa niaba ya baba yake yaliwapa faraja. Na kuwapa moyo wa matumaini kwamba kile walichodhamiria kinaenda kutimia. Waliruhusiwa kuingia, na kuwa katika foleni ya kumuona mtaalamu. Afahamikaye kwa jina la Maliatabu. Al– maarufu Mzee Kijana, ndivyo alivyozoeleka mtaani kwao. Walipita na kulifikia sebule, wakakaribishwa kwa ukarimu kwa kuonyeshwa sehemu ya kuketi pindi wanasubiri. Walionyeshwa sofa, wakaketi.



    Ndani mlitawaliwa na harufu kali iliyofukiza sehemu kubwa ya nyumba. Japo harufu hiyo ilitoka chumba kimoja. Hata kwa mgonjwa wa mafua kiasi gani, namna harufu hiyo ilivyokuwa inafuka ni lazima aisikie. Kwa mtu asiyewahi sikia, hakukosa kughafirika, lakini kutokana na shida alilazimika kuvumilia, atokapo ndipo hutoa manung’uniko yake kwa kujisemeza mwenyewe moyoni. Ilikuwa hivyo kwa Upendo. Ila hakusubiri kutoka alianza malalamiko ya kuumizwa na harufu angali papohapo, kiasi kwamba kuna muda alifutika kichwa katikati ya mapaja yake apumzishe pua kuvuta harufu hiyo. Dakika nane baadaye tangu waketi pale sebuleni mlango wa chumba waliokuwa wanautazama mbele yao ulifunguliwa na kuonyeshwa kidole kilichoashiria kuitwa. Waliinuka pale sofani na kuingia chumba husika. Harufu ya udi na ubani uliofukizwa chumba kizima huku mwingine ukiwekwa akiba iliwapokea na kuwapa ukaribisho mkubwa uliowafanya nao wafukizwe vyema. Namna harufu ilivyojijenga humo chumbani, katu, kitu chochote hata kichomwe kwa wingi kiasi gani harufu yake haiwezi izidi iliyopo. Hakika ilijitwalia!



    Punde, pasi na kuchelea. Mzee Matatizo alifanya utambulisho wa wote kwa niaba. Alivyohitimisha, alielekea kwenye dhamira iliyowapeleka. Ambapo sasa wasaa huo, aliachiwa Upendo aelezee atakavyo mambo yawe. Aliondoa tahayari, moyo alijaza matendo ya kidunia, yaliyomsahaulisha matendo mema aliyokesha kuyaabudu. Penzi lilimbadili. Binti huyo wa Kifipa, hivyo kwa lolote aliloshauriwa kwake lilikuwa poa. Kwa minajili ya kutimiza atakacho. Alimwaga hisia zake, aliposahau jambo, Mzee Matatizo alikumbushia yalivyojaa uridhisho, wakamtupia mpira mtaalamu amalize kazi. Mtaalamu alivuta kitabu kimoja wapo, miongoni mwa vilivyopo karibu katika kono lake la kushoto. Kisha alisogeza kalamu ya wino mwekundu na daftari ndogo ambayo alifunua kurasa kadhaa akachana karatasi na kulirejesha alipotoa. Aliandika maneno machache ya kuran katika kile kikaratasi alichochana kwa kutumia kalamu ile nyekundu akampatia Upendo akamatie, baadaye alianza kisomo kwa kutumia kile kitabu.



    Kisomo kikakubali. Kwani aya zilipanda na kushuka, toa hii weka ile hitimisho lilivyofikiwa, mtaalamu alitoka na hitajio.

    “Leteni nguo za ndani za hao wahusika,” anasema mtaalamu akiwa anafunika kitabu, kusubiri tekelezo la hilo hitaji amalizie kazi.



    Kutokana na shauku kubwa iliyotamalaki moyoni mwake ya kuona mafanikio yanapatikana kwa uharaka, Upendo alirudi nyumbani kufuata vitu alivyoombwa ili kazi ikakamilike kwa asilimia zote, na si nusunusu. Alitumia muda wa robo saa kuwasili nyumbani. Lakini isivyo bahati mazingira aliyokutana nayo, yalikuwa tofauti na walivyoacha pindi wanaondoka. Wao walivyoondoka hawakufunga mlango. Waliegesha tu, ila sasa alikuta umefungwa na kufuli. Tena kubwa ambalo hana kumbukumbu kama ashawahi liona sehemu. Tukio hilo lilimfanya apate unyong’onyo. Na hisia za mara kwa mara za kufeli takwa lake. Hakukaa nalo moyoni, alimpigia simu Mzee Matatizo kumtaarifu alichokutana nacho ili ikiwezekana apate ushauri toka kwa mtaalamu nini afanye. Mzee Matatizo alivyomtaarifu mtaalamu, alipewa kauli moja tu, na kuirejesha kwa Upendo kama ilivyo.

    “Ili kazi ipate kuwa ya uhakika lazima hizo nguo zipatikane. Zaidi ya hapo itakuwa sawa na kazi bure. Utafanikiwa kwa siku chache, nyingi utaingia majutoni,” anasema Mzee Matatizo kwa msisitizo.

    “Kwa hiyo unashaurije?”

    “Fanya subira. Na endapo hatofika mapema huyo aliyefunga na kuondoka na funguo, tafuta mafundi wavunje kufuli, hamna njia nyingine ya msaada zaidi ya hiyo.”

    “Sawa,” anasema Upendo na kukata simu.





    Akatafuta eneo akaketi, kumsubiri aliyefunga mlango, ambaye baadaye alitaarifiwa kuwa ni Vumilia alivyojaribu kuchombeza chombeza kwa majirani. Aliketi sehemu hiyo kiasi kwamba al–manusra usingizi umchukue kwa sababu ya upepo mwanana uliopepea kutoka upande mmoja kutawanyikia pande zilizosalia. Muda wa subira ulikuwa dakika sita na sekunde takribani arobaini na nne, Vumilia akarejea, baadhi ya sehemu ya mwili, hasa paji la uso likitiririsha damu iliyoenea sehemu nyingine ya maungo ya mwili. Juu ya tofauti walizonazo, kwa hali hiyo Vumilia akamruhusu Upendo amhudumie. Maumivu yapate kupungua. Msisimko alioupata Upendo haukuwa wa kawaida. Mwili ulijaa shauku ya kusisimka kila sekunde kwa sababu tu karuhusiwa kugusa sehemu ya mwili wa mwanaume ampendaye. Alimhudumia, pia kutumia nafasi hiyo kuingia chumbani kutafuta vile alivyovifuata. Hakuangaika sana. Punde tu, alivyoingia moja kwa moja aliongoza lilipo boksi litumikalo kuhifadhi nguo chafu. Alipekua mara mbili tu, akakutana na lundo kubwa la vyupi vya Zamzam na boksa za Vumilia. Hakuchambua, alibeba atakazo kisha kuzihifadhi katika mfuko mweusi aliousundika ndani ya dila alilovaa.



    Alivyofika nje alimuongopea Vumilia anaenda dukani, lililopo mtaa wa pili, mita mia nne sabini toka aishipo. Hakutiliwa chembe ya shaka, kwani maumivu aliyokuwa anaugulia si ya kuruhusu kumchunguza mtu anafanya nini? Maumivu yalikuwa makali mno. Yaliyomfanya ajifikirie mwenyewe kwa asilimia zote. Upendo alivyowasili umbali wa mita kadhaa, aliutoa ule mfuko aliousundika akaukamatia mkononi kisha kuzidi kupiga hatua awahi kwa mtaalamu. Mbele aliita bajaji, usafiri wa haraka utumikao ndani ya mji huo. Alimuamuru dereva wapi anahitaji kufika. Baada ya kuuliza bei na kuona anaimudu kulipa. Alivyowasili alimlipa dereva na kuongoza ndani ambako aliwakuta wote wawili wamepoa kumsubiri. Kabla ya muendelezo wa tukio waliloanza nalo, aliwahabarisha kilichomkuta Vumilia na mengineyo yaliyomkawiza.



    Zoezi liliendelea baada ya majadiliano ya muda mfupi yamhusuyo Vumilia. Kisomo kilivyoanza ni mtaalamu pekee ndiye alisikika, wengine kimya kusubiri matokeo yapatikanayo. Vile vyupi vilifukizwa majimaji fulani, yenye rangi ya udhurungi, kisha kufukizwa kwenye moshi wa ubani na udi uliokuwa unafuka. Halikuchukua muda mrefu kuhitimishwa, kisha kuambiwa Upendo kwa mara nyingine anene maneno kadhaa, kunuia akiwa kakumbatia vile vyupi karibu kabisa na sehemu yake ya kidevu. Halikuwa zoezi refu, alivyomaliza alirudisha vyupi kwa mtaalamu, akaviloweka kwenye maji yenye rangi nyekundu, rangi iliyotengenezwa kupitia maneno ya kuran yaliyoandikwa kwenye kitambaa fulani cheupe.

    “Hivyo vyupi mukafiche chini ya uvungu wa kitanda chao. Kwa muda wa siku moja tu, kisha viondoeni. Halafu viosheni, pasipo kutumia sabuni. Muosho mmoja tu. Maji yapatikanayo baada ya kukamua hizo nguo, changanyeni kwenye kinywaji chochote watumiacho,” anasema mtaalamu na kuwakabidhi vile vyupi.

    “Ina maana pasi na kufanya hivyo lengo halifanikiwi?” aliuliza Upendo.

    “Hapana. Lishafanikiwa, ila hiyo mbinu ya mwisho niliyowaeleza ni kujidhatitia kusiwe na chembechembe ya kufeli,” anasema mtaalamu akiinuka pale alipoketi kuwasindikiza wakiwa washanyanyuka muda.



    Walifunga safari ya kurudi hadi nyumbani, na kumkuta Vumilia ameketi barazani akiendelea kuugulia maumivu. Ambayo walivyomdadisi wafahamu chanzo, hawakuambiwa. Hivyo wakaishia kujawa na mengi matamanio ya ufahamu. Ingawa kuna muda walihisi, tatizo hilo limempata katika mihangaiko yake ya kumpambania Zamzam arejee nyumbani. Walitumia muda mrefu kumbembeleza, ila Vumilia hakushawishika. Aliwachunia, mwishowe, wakaendelea na mipango yao. Kama walivyoambiwa na mtaalamu. Wakatumia wasaa huo kufanya mambo namna yalivyopangwa, baada ya kukamilisha waliendelea na taratibu zingine. Uwepo wa nguvu ya mtaalamu, na uondokaji wa Zamzam, waliamini Vumilia anaenda kulainika. Ule msimamo aliokesha nao muda wote, utaenda toweka, ukizingatia mtoto wa kiume, daima hatii neno kwa mtoto wa kike aamuapo kufanya vitimbi vya ulainishi.

    “Nataka nianze kumfanyia mitego yote ya kumjaza mate ya uchu mdomoni. Kila anionapo atamani kuketi karibu nami, anioneone, na mwisho auvunje mwiko wake,” anasema Upendo, pindi akizungumza na Mwanjaa kwa njia ya simu.

    “Hee! Shoga, hukomi tu?”

    “Naanzaje kukoma wakati Mama mwenye nyumba kakimbia?”

    “Acha utani,”

    “Ndiyo hivyo rafiki, sasa wakati ni wangu. Ni muda wa kuweka mitego yote, hadi amsahau mkewe.”

    “Lakini si unafahamu kuwa muda wa mapumziko mwisho kesho? Kesho kutwa unahitajika kazini.”

    “Lisikupe shida hilo. Kama mahabusu nitakaa tu. Ilimradi niuone mwanzo wangu mzuri katika hili.”

    “Haya ila kuwa makini.”

    “Ondoa shaka.”



    Hakutaka kulaza damu. Haraka sana alibadili mienendo, yote Vumilia ashawishike kuingia ndani ya ngome yake. Lilikuwa jambo la kawaida, kuvaa khanga moja ndani chupi pekee, ili makalio yake yaonyeshe ulegevu atembeapo, kitendo kitachomsukuma, Vumilia kwa namna yoyote aanze kumfikiria. Nyakati zingine alitembea akiwa kavaa khanga ama kitenge pekee, ndani pakijitawala kwa kufukizwa na ka-upepo kadogo. Hasa alivyokuwa anaenda au kutoka kuoga ama wakati wa kufua.

    “Hapa huwezi chomoka, utavumilia, mwisho utashindwa. Zigo lazima ulihitaji,” anasema Upendo akiwa kaketi mbele ya Vumilia anajikagua kagua sehemu iliyofungwa bandeji iliyozuia kidonda. Huku mapaja ya Upendo yakiwa njenje, kwani nguo aliyovaa ilikuwa fupi iliyoruhusu sehemu kubwa ya mwili wake kukata kiunoni, hususani mapajani kuonekana. Ndani akiwa kapiga kufuli la wavuwavu. Lilionekana kupitia mwanya mdogo alioutengeneza makusudi, baina ya paja na paja.



    Aliendeleza matendo hayo hadi siku waliyoondoka, na Mzee Matatizo kurejea jijini Dar es salaam. Akiwa kazidisha siku takribani nne achilia zile za awali alizopewa. Moja kwa moja akili yake ikamtuma, kwamba mahabusu hatoikwepa. Hivyo anapasa atengengeneze mazingira mazuri yatayomwezesha kuikwepa, na kama atakaa, akae kwa muda mfupi. Ndivyo ilivyotokea. Punde tu, alivyowasili kambini kwao, alifikia mahabusu, huku Mzee Matatizo akiliunga kuelekea Mangaka. Siku hiyohiyo alilala mahabusu, ya pili yake, alifunguliwa mashtaka ya utoro. Kesi iliyofunguliwa katika mahakama ya kijeshi papohapo kikosini kwao. Alisomewa mashtaka kisha kuhukumiwa siku hiyohiyo, kwa kifungo cha mwezi mmoja mahabusu na adhabu kali ya ung’oaji visiki. Aliitumikia adhabu yake, kwa asubuhi hadi jioni kung’oa visiki sehemu tofauti tofauti vipatikanavyo kambini kwao, usiku mahabusu. Akiwa chini ya uangalizi wa MP (Military Police).



    Muda wa adhabu ulikuwa mrefu. Na ulikuwa unaua takwa lake. Ukizingatia hakuruhusiwa kutumia simu kwa muda wote hadi atavyomaliza adhabu. Jambo lililomfanya akose mawasiliano na watu wake muhimu, Vumilia akiwemo. Kukosa mawasiliano baina yao alifahamu fika, ndoto aliyonayo inaenda kupeperuka. Alihisi hilo toka siku ya kwanza alivyoondoka mjini Dodoma, kwa kigezo cha wapenzi walio mbali, ngumu sana kudumisha mahusiano. Si wapenzi tu, hata marafiki pia. Hivyo naye aliliona hilo, na hakuhitaji litokee. Kwa gharama yoyote, japo kuna muda kile kilichofanywa na mtaalamu kilimpa matumaini katu Vumilia hachomoki kwa unono alionao. Muda wote wa adhabu alikesha kumfikiria. Sambamba na matendo yake maovu yenye lengo la kumvuta. U–hali gani kule aliko? Alimwazia sana.

    “Kwa vile nilivyofanya, naamini akili yake imejenga hitajio la kukutana na mtoto wa kike. Tena si mwingine, bali ni mimi mwenyewe. Maana kwa yale niliyofanya lazima awe na matamanio ya kunigusa gusa. Hivyo nikiremba, akili yake inaweza badilika na kumfikiria mwanamke mwingine. Kabla hicho hakijatokea, yanipasa kuwa ndani ya mji wa Dodoma siku ya kesho,” anasema Upendo kimoyomoyo, akiwa kaketi mahabusu, kiza totoro kimemzunguka.



    Mapambazuko aliyatambua kupitia mwanga hafifu uliokita kiambazani, ulioruhusiwa kupita kwenye dirisha dogo lililojengwa kwa juu karibu na mwanzo wa paa. Uliofukuza kiwango kidogo cha kiza na kuruhusu mwanga uliomwezesha kuona kwa ufinyu eneo la chumba alichopo. Kila siku aonavyo hivyo, aliamka na kuketi, kisha baadaye kupunguza uchafu mwilini na kuuweka mwili tayari kwa ajili ya shughuli atazopangiwa, katika muendelezo wa adhabu yake. Ila siku hiyo mambo yalienda tofauti. Kama ilivyo ada, aliamka mapema sana, na kufanya subira ya kuja kuchukuliwa akaendelee kutumikia adhabu. Mawazo ya uhitaji wa kutoka na kufika ndani ya mji wa Dodoma nayo yakitamalaki kwa kasi akilini, kiasi kwamba hakuacha kutoa malalamiko kimoyomoyo kwanini hafwatwi. Kuna wakati alihisi, kama washatambua dhamira aliyonayo, ndiyo maana hawajaja. Alikesha kujilaani, na kwanini hakuwanalo mapema hilo wazo, pia kuomba wale askari jeshi aliokabidhiwa kumsimamia wamfuate.



    Saa zilizidi katika, bado akiendelea kusota ndani ya chumba cha mahabusu, muda wa kupata chakula alipitishiwa kwenye tundu fulani mlangoni, mahitaji mengine pia, alipitishiwa hapohapo. Alivyojaribu kuhoji kwanini hatolewi, alipatiwa majibu yaliyompandisha hasira na kujenga chuki kali moyoni mwake, dhidi ya wote ambao aliamini wanaenda poteza bahati yake. Ya kuwa himayani mwa Vumilia.

    “Wakuu washakataa wewe kutoka. Hivyo muda wote utabaki humo hadi muda wako wa adhabu utapomalizika,” anasema mmoja wa askari jeshi wamuhudumiao pale ahitajapo kitu fulani, pindi akimpatia maji.

    “Nani kaamua hilo jambo?”

    “CO (commanding officer) tena kang’aka mbaya juu ya siku ulizotolewa. Al-manusra watu wapewe siku.”

    “Duh! Wapi kayaongelea hayo?” alisema Upendo akirejea mahali alipoketi.

    “Kwenye bataliani.”



    Walizungumza mengi, yamhusuyo Upendo juu ya hatma ya adhabu yake. Yaliyojaa machungu, huzuni na manyanyaso lukuki moyoni mwake. Tamanio na hitajio la kuwa ndani ya mji wa Dodoma, sasa aliliona kutofanikiwa. Na ikiwa hivyo, ni sawa na kuruhusu katazo la mawasiliano baina yake na yule ampendaye. Afanyaje lisitokee, alikesha kufikiria mengi ya kuyatumia, lakini hakuna aliloona linaweza mfaa katika yote.

    “Niwaombe wanitoe kwa kisingizio cha kwenda haja kubwa, humu ndani hakuna sehemu ya kuhifadhia haja hiyo,” anawaza Upendo. Moyo ukiwa na chuki zito juu ya mtu aliyeambiwa. CO! Kamanda wa kambi yao.

    “Huyu mzee, ananitafuta nini? Haoni yale aliyonifanyia kipindi cha nyuma kama yanatosha hadi aendelee kunibana bana? Kunichezea, anichezee. Halafu anaendelea kuniwekea vikwazo vya kujipatia japo furaha? Hapana! Kama awali nilimsamehe sababu ya wokovu uliokithiri moyoni mwangu, sasa niko kivingine. Akizidi, ama endapo nitampata mtu wa kuniongezea machungu, nitakula naye sahani moja,” anaendelea kuwaza, akifuta futa sakafu kwa ajili ya kulala.



    Imani ya kutoka ilikatika kabisa. Kwamba hatotoka, na hatoweza kufanikisha dhamira aliyojiwekea. Akiwa kwenye tafakuri hiyo, alishtushwa na mwanga mkali uliotoa nuru ya kutosha mule chumbani na kumpa ufahamu kuwa mlango umefunguliwa. Kuthibitisha hilo, aliinua kichwa kuangaza kule mlango ulipo. Kweli! Mlango ulifunguliwa, katikati akiwa kasimama mzee mmoja aliye na tepe ya MP mkono wa kushoto na cheo cha sajini.

    “Unanenepa nenepa tu hapa. Twende kalipie chakula ulichopewa,” anasema mzee huyo kwa sauti ya kumdhihaki. Kwamba anapata raha mule ndani.



    Upendo hakutilia maanani dhihaka aliyopatiwa. Aliinuka, akapiga alama ya msalaba kumshukuru muumba wake kisha akapiga hatua kuelekea nje.

    “Hawana bahati. Lazima niitumie hii nafasi kukamilisha takwa langu,” alinena kimoyomoyo, wakati huo akichukua vifaa vya kwenda kufanyia kazi, alivyowekewa pembezoni mwa mlango. Ambavyo ni sururu, jembe na chepeo.



    Akavibeba. Viwili begani, kingine kakamatia mkononi kisha taratibu akajiondoa kuelekea sehemu husika, ambayo aliitambua kuwa ni kulekule alikofanyia kazi jana. Akatangulia, MP akifuatia nyuma, umbali mita arobaini, huku sababu kubwa ya kutengeneza umbali huo, alipitia dukani kufanya manunuzi ya sigara, ambayo angeenda vuta uwanja wa kazi ulioko umbali wa mita mia tatu toka majengo ya kambi yalipo. Hiyo ilikuwa nafasi pekee kwa Upendo, na alidhihirisha hilo, punde alivyoanza ingia kwenye kichaka kilichojaa miti mchanganyiko, mikubwa kwa midogo pasi na sahau nyasi zilizokauka na makambakamba yaliyojifunga mitini. Lengo la safari yao ni kufika lilipo shamba dogo la kikosi, lililo na miti mingi ya matunda, kwenda kuchimbua visiki vizuiavyo usafiri kupita kutokanana na kuwepo katikati ya barabara. Alivyoanza ingia humo alizidisha mwendo. Ili amuache yule mzee umbali mrefu utaomwezesha akifanya jambo asionekane, na endapo ataonekana, aonekane sehemu ndogo ya mwili wake, si mwili mzima.



    Alivyojihakikishia kaufikia huo umbali, alianza tumia mbinu mbalimbali za mafunzo kutekeleza. Kama vile kuroll, kutambaa na aina nyingine ya mitembeo iliyomwezesha kutooneka. Katika kufanikisha mpango huo kwa ufanisi, akatupa zile zana, sehemu ambayo yule mzee hatotumia kupita pindi anaelekea shamba. Nje ya njia. Akakatiza sehemu tofauti tofauti, alivyokutana na wadudu, awaogopao, hasa nyoka, alijivika ushujaa kwa kubadili njia, kupita sehemu nyingine hadi akafanikiwa kutokeza barabarani.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Habari ya kubainika kuwa katoroka, ilitambulika baadaye sana. Pindi mzee alivyofika eneo la shamba na kutofanikiwa kumkuta. Kila alivyojaribu kuita, na kufanya jitihada zingine za utafutaji, pasi na kuona mafanikio ndipo alitambua, kuwa Upendo katoroka. Hakukanalo moyoni. Haraka sana alitumia silaha yake ya msaada, filimbi. Alipuliza ili wanajeshi wengine waliopo karibu yake wasikiapo, wawahi eneo alilopo wakamsikilize tatizo alilonalo. Alitoa mipulizo mitatu, iliyosikika eneo jirani na alilopo, na kuwafanya waliosikia kuwahi kutambua kulikoni baada ya ufahamu, kuwa aina ya muito wa filimbi iliyopulizwa ni ya mtu kuomba msaada. Wale waliowahi, aliwaambia kiendeleacho, taarifa iliyowashinikiza kuungana na kuendelea kumtafuta Upendo, lakini hakukuwa na matokeo tofauti na yale ya awali aliyoyapata yule mzee. Baadaye ilibidi waghairishe, kisha kurudi kikosini na kuutaarifu uongozi tukio lililojiri.



    Wakati huo, Upendo alishakuwa ndani ya gari. Gari kubwa zifanyazo safari za kimataifa Long Vehicle, alipata lifti baada ya kupiga mkono, akiwa katika muonekano wa siku zote. Ndani ya gari mlikuwa na watu watatu, dereva, kondakta pamoja naye. Na kuifanya safari kuwa tamu kutokana na soga za hapa na pale walizokuwa wanaendelea nazo. Ilivyo bahati, gari ile ilikuwa inaelekea Dodoma, hukohuko alikopanga kuelekea.

    ****



    Juu ya maumivu makali ya kuugulia kidonda. Matamanio hayakukosa, kwa kile alichokuwa anafanyiwa na Upendo. Kitendo cha kuona namna makalio yalivyoshindana kutikisa, na kuonesha utepetepe, ulimfanya mwili wake kusisimka. Achilia mbali, mapaja yaliyoonyesha unofu. Jogoo hakustahimili, alikesha kuonyesha urijali wake kila aonapo kwa kusimama, ishara ya kutoa ukumbusho kwamba kionekanacho ni halali kwake pia kukipata. Hapa alimsahau Zamzam kwa muda. Akatamani kumsaliti, apate unofu uliokithiri kwa Upendo kisha kushuhudia maufundi ya kifipa, kabila ambalo hakuwa na habari zake kwa kina, zaidi ya kusikia kuwa ni wataalamu wa uchawi. Uchu ukamvaa, uliomshinikiza afanye, huku upande wa pili ukimwambia subiri kidonda kipone, ndipo ufanye utakalo.

    “Dah! Kananitamanisha,” aliwaza Vumilia, jioni moja alivyoketi nje kupunga upepo, mbele yake kasimama Upendo, akijitahidi kusugua mguu kwenye jiwe mara baada ya kutoka kuoga. Huku khanga aliyovaa ikishikana vyema na mwili wake.



    Mwishowe uvumilivu ulimshinda. Haifahamiki kama ni kazi ya mtaalamu, ama mwenyewe tu aliamua. Akadiriki kuweka apizo la kutoka na msichana yeyote, lengo kupooza shauku aliyojengewa na Upendo kabla hajaondoka. Kwani kwa wakati huo mkewe, Zamzam, hakuwa vizuri kutokana na maradhi ya hapa na pale ambayo hakufahamu chanzo. Alikuwa radhi kumsaliti mkewe, kwa sababu hakukuwa na uwezekano tena wa wawili hao kuingiliana hadi Zamzam atapokaa sawa kiafya. Waanze kusuluhishana, wakipatana ndipo waendelee na mengine waliyoyaachia kati. Wakishindwana watalikiane.



    Ilikuwa ni usiku, wa kiza kinene, fikra tele zilimtawala. Ikitoka hii, inaibuka hii, zilizo na mchanganyiko, wa furaha na huzuni ndani yake. Zote kuhusu mwenendo wa maisha. Akiwa hivyo, ndipo ikaibuka hisia iliyomsukuma kuvunja mwiko baada ya kukaa muda mrefu pasipo kutana na mwanamke kimwili. Hisia hiyo ilimsumbua, kwa jogoo wake kusimama kila muda na alivyojaribu kumtuliza, hakutulizika, zaidi ya kusimama kidete. Ilimpatia wakati mgumu. Kiasi kwamba alitamani arejee kwenye zama zake za awali, kujichua. Kwani kwa usiku huo ilikuwa ngumu kumuita mwanamke. Pia alitamani, aondoke aelekee maeneo wajiuzao wanawake, ila lilimkwamisha suala la usafiri. Atautolea wapi? Ikamlazimu atulie, kusubiri kupambazuke ndipo atekeleze takwa alilonalo. Na jinsi alivyokuwa na ugwadu, alijiapiza kufanya shughuli hiyo asubuhi asubuhi. Tena mtu aliyehitaji kufanya naye ni mwanamke anayejiuza, maana ndiye wa haraka haraka asiyehitaji kutumiwa maneno mengi. Ni pesa tu huzungumza. Alivuta hisia, kufikiri kama ana namba za mwanamke yeyote afananaye na hao anaowahitaji. Alivuta kilongalonga chake, akaanza tafuta namba moja baada ya nyingine katika orodha iliyopo. Alifanya hivyo karibia mara mbili, lakini katika orodha ya namba hiyo hakupata ya mlengwa. Na kumfanya afikirie mara mbilimbili kama alishawahi kuhifadhi namba za simu aina ya hao watu anaowahitaji. Alivyojihakikishia kutowepo, alipanga safari ya kwenda sehemu moja wapo atayofanikiwa kupata mmoja wapo. Hasa wale wajiuzao nyakati za usiku, baada ya kuona baamedi atatumia mzunguko mkubwa pia hatopata raha aitakayo kwa uhuru. Kutokana na hofu ya muda kwa baamedi.



    Aliamka, na kutandika vyema kitanda chake, alivyomaliza, alijiandaa kwa ajili ya kufanya usafi wa mwili ndipo baadaye aianze safari ya kwenda eneo husika. Akiwa katikati ya maandalizi yake, alishtushwa na sauti ya hodi iliyoambatana na kugongwa kwa mlango. Kabla hajaiitikia, aliisaili, ni nani aliyemvamia asubuhi asubuhi namna hiyo, kwani alivyoangaza muda kwenye simu ilisomeka 12:03. Alijifikiria kwa sekunde kadhaa, alivyoona yule apigaye hodi anaendelea akaamua kwenda kumfungulia. Alipiga hatua, akakamata kitasa akakizungusha, mlango ulivyojiachia, sura ya Upendo ilijitanabaisha mbonini akiwa kwenye vazi la kazini kwake, lililomshtua Vumilia.

    “Usishangae sana, naomba niingie, nitakueleza ukweli,” anasema Upendo akimsukumiza Vumilia waingie.



    Alianza kwa mgomo. Ila baadaye akakata shauri, akamruhusu Upendo kuingia ndani. Alimtanguliza, kisha yeye kufuatia nyuma yake. Kabla hawajafanya jambo lolote walianza sabahiana, ilivyohitimishwa salamu na maongezi machache yaliyofuatia, Upendo aliomba kwenda kuoga, alivyomaliza hilo, akafuatia kuomba chakula. Vyote Vumilia hakupingana navyo, aliruhusu avifanye huku akimfikiria kapatwa na nini. Alivyomaliza kuoga hakuvaa kitu kingine, zaidi ya kitenge cha Zamzam alichoomba tangu awali, alivyoenda kuoga. Na kumfanya Upendo wake abarizi na kaji kaupepo kadogo kilichokuwa kinaingia ndani kupitia mianya michache iliyopo dirishani. Kiasi kwamba atembeapo aliamsha na kuongeza zaidi hisia za Vumilia alizonazo toka jana.

    “Haina haja ya kwenda kule nilikopanga, namalizana na huyuhuyu,” anasema Vumilia huku akimeza fundo la mate akiyatathmini makalio ya Upendo yalivyonona.



    Baadaye alianza mdadisi, kipi kimemleta na mambo mengineyo. Pasi na bakisha akiba. Upendo alimhadithia kila kitu, tangu alivyoondoka hapo hadi muda huo aliorejea. Penye kuchangia, kwa kutoa pole, Vumilia hakuacha kufanya hivyo. Na alipohitaji maelezo ya kina zaidi napo aliomba kueleweshwa. Simulizi ilivyokuja hitimishwa, walikwisha karibiana. Hatua ambayo mtu akipumua moja kwa moja hewa itokayo hugonga mwili wa mtu mwingine. Kutokana na sogea sogea aliyokuwa anaifanya Upendo katika kujiweka sawa. Sehemu kubwa ya paja ikiwa wazi iliyozidi kuongeza mshawasha kwa Vumilia.



    Haifahamiki ni muda gani, viganja vya mkono wa kuume vya Vumilia vilizuru kwenye paja la Upendo. Haijulikani kama alikuwa anamuweka sawa kurudisha kitenge kilivyo na hatimaye Upendo kung’ang’aniza vibakie, ama Vumilia mwenyewe alinogewa kuvipeleka. Baadaye vilianza ambaa ambaa, toka sehemu hii, kwenda sehemu nyingine ya maungo, hasa sehemu iliyobeba jinsia yake. Upendo aliishia kutoa macho pima kumsaili, msisimko ukianza chipua taratibu, ulipochanganya naye alitoa mrejesho wa kutumia viganja vya mikono yake kupapasa maungo ya Vumilia. Wakati huo kila mmoja alikuwa na lake alilokuwa anafikiria kichwani mwake. Vumilia, amalize haja zake aachane naye, huku Upendo akijihakikishia hatua hiyo itampeleka kule anakohitaji. Japo kuna muda alikuwa na nia ya kumuomba Vumilia wasifanye chochote hadi wawekeane mikakati ya mahusiano yao yatakuwa ya aina gani, wazo lililopeperuka haraka mno alivyopatwa na wazo lingine juu yake.

    “Dunia ya sasa hamna mwanaume aliyeradhi kuoa mwanamke ambaye hajaonja utamu wake,” alikumbuka kauli hiyo. Aliyoisikia jioni moja akiwa na rafiki zake wakiteta jambo kambini kwao.

    “Mmmmh! Sasa nikimuuliza juu ya hatma ya mahusiano yetu yatakuwa vipi si ndiyo utakuwa mwanzo wa kunifukuza hapa nyumbani kwake? Nampenda sana, japo yeye hana dalili hizo kwa sasa. Vyema kupalilia wakati huuhuu ambao mkewe hayupo. Ili nimdatishe aweze kumsahau kabisa. Tena yakichanganyia na yale mambo ya mtaalamu, hachomoki,” aliendelea kunena kimoyomoyo, akiwa kamkumbatia Vumilia mithili ya ruba, huku sehemu ya mbele ya kitenge kishaachia na kuruhusu maungo yote yaliyopo upande huo yaonekane bayana pasi na kizuizi.

    “Namgeuza mtumwa wa ngono kwa hizi siku kadhaa, wakati huo nikiendelea kufanya usuluhishi na mke wangu, baada ya hapo namfukuzia mbali, kama kaharibu huko kikosini kwao atajua mwenyewe,” aliwaza Vumilia.







    Kwa hulka na pupa, walianza kutafuta ulimwengu wa huba. Kwa kuonyeshana maufundi ya hapa na pale waliyonayo kila mmoja. Vumilia aliutumia vyema ujuzi alionao katika hiyo tasnia, ili asifanye uzembe utaomfanya kuonekana mshamba mbele ya kimwana hicho kisicho na ujuzi wa kutosha kutokana na udini uliomtawala kipindi cha nyuma. Ndimi na vidole ndivyo vilitumika sana kwa wote. Kutembeza sehemu mbalimbali za maungo ziongezazo nyege na uhitaji wa kuingiliana. Vumilia hakuwa nyuma, katika kuongeza kumchachawisha Upendo, aliipeleka ndimi yake ukeni. Ambako tayari kulishaanza tepeta na kutoa kila ishara ya kuhitaji jogoo wa shamba aingie ndani ya himaya ashughulike. Alitumia ndimi kugusa huku na kule, kwenye ukuta wa uke na baadaye kinenani. Kitendo hicho kilibadili mwenendo kwa Upendo, ulegevu ulianza mtawala na nyonga alikesha kuinyonga nyonga kutokana na utamu uliotokana na namna alivyokuwa ananyonywa. Alijibaragua kona hii, mara ile, ilimradi Vumilia aachie kunyonya, lakini ilishindikana. Kila kona aliyojisogeza, aliambatana na Vumilia, ambaye sasa mdomo wake ulishaenea ukeni kusaidia ulimi, uliokesha kuzunguka kila pande.



    Nguvu ya uongeaji ikapotea kwa Upendo. Kila alivyojaribu kuzungumza, maneno yaliishia kati, kisha kufuatia na miguno iliyomwashiria ananogewa na kile afanywacho. Miguno ilikuwa ya kimahaba pekee. Kauli chache za kuomba aachiwe huru na muda mwingine ya kutaarifu wahusika waburudishao zaidi watokapo washaianza safari. Vilevile kuomba jogoo liingie ndani. Kuna muda alikuwa analivuta kabisa kulazimisha bwana wa majeshi akamalizie shughuli.

    “Vumi!...ingia, ingia nataka nikojoe...pindi imo ndani,” anasema Upendo, wakati huo yupo hoi akikazana kukata nyonga.

    “Mmmh!...mmmh! Subiri kidogo.”

    “Aaaaah! Vumi,...hizo! Hizo! Hizo zinatoka, zinatokaaaa, ongeza kasi kidogo ya kuninyonya kwa juu hapo, nikojoeee,” aliendelea kusikika, sauti ya chini, baadhi ya maungo yakionekana kupoteza ushirikiano kwa sababu ya uchovu.

    Vumilia hakumwachia hadi alivyojihakikishia kakojoa, ndipo akaacha kunyonya. Akamwacha apumzike kwa sekunde chache, takribani nne, kisha akalisogeza goma karibu, pasi na chelea, taratibu akamuingiza jogoo aianze upya shughuli.

    “Vumi! Hutaki hata nipumzike kidogo,” alisema Upendo huku akisikilizia namna jogoo linavyokata kutafuta sehemu ya kukita.



    Alipoona lishatosheleza kwa ajili ya kushughulika, mtanange ulianza upya. Wa kukatana shoka, kwani kila mmoja alihitaji atangulie kuliona lango, kabla ya mwenziye. Hadi wanaifikia kupumzika, tayari wote walishaliona lango kwa pamoja, Upendo akitangulia kwa bao mbili, Vumilia akifuatia kwa bao moja. Nyoyo zao zilitakasika, kwa furaha iliyokosa kifani, namna burudisho lilivyojitosheleza. Siku hii ilikata kwa wawili hawa kuufaidi uhondo wazuiao kwa mavazi yao, pia kwa kufichwa ndani ya viungo husika. Ili kuupata lazima vishughulike. Na ndivyo walifanya, walikesha kuvishughulisha. Hata siku iliyofuata, walikesha kwenye burudiko la miili yao. Mmoja wao alivyotosheka kwa siku hiyo, kwa sababu ya uchovu ndiyo ulikuwa mwisho wao.



    Vumilia alipokamilisha takwa la moyo wake, hakuwa na mwendelezo wa hitajio kwa Upendo. Alimuona wa nini? Na kutokuwa na thamani yoyote tena. Kwa sababu ana mke ampendaye, hivyo hawezi kuwa na mwanamke mwingine. Upendo hakuwa na bahati kwake, na ule ufundi wa mtaalamu haukuonekana kufanya kazi. Si, hakika kama walitapeliwa ama walikosea masharti. Kwani juu ya yote waliyofanya hayakuonekana kumvaa Vumilia. Sio Vumilia tu, hata Zamzam pia aliyekuwa kwa dada yake kwa kipindi hicho. Vumilia alijivika tabasamu bandia muda wote, huku akifikiria mbinu za kumuondoa Upendo, ambaye alishaanza sahau kuwa Vumilia ana mke, na kutaka kujihalalisha umiliki.

    “Haina haja ya kuchelea, isije wanafiki wa mtaani wakatumia nafasi hii kumfikishia ujumbe mke wangu. Liwalo na liwe. Huu si wakati wa yeye kuendelea kuwepo nyumbani,” anawaza Vumilia, akiwa hima kupiga hatua kuelekea nyumbani kwake.



    Siku hii ilikuwa ya kipee, Vumilia aliitumia kwa mara ya mwisho kufahidi urembo, na unono wa Upendo, siku iliyofuata mapema tu, punde walivyoamka, waliketi kitako Vumilia kumtaka Upendo aondoke. Aliiondoa sura ya tabasamu aliyokesha kumuonesha siku zote, akaivaa ya simba ili asimuonee huruma amwamuliapo. Kauli alizitamka pasipo mung’unya na kufanya zisikike vyema kwa Upendo, na kuumpa umizo aliloshindwa livumilia, mwishowe akatumia sauti ya kilio kuwa sehemu ya kuonewa huruma. Alianza kulia, tena kilio cha nguvu kilichovuta majirani wasogee karibu wajionee kiendeleacho, ila kwa sababu walikuwa wameketi ndani, hawakuambulia chochote. Kuonyesha, Vumilia hatanii kile alichozungumza, alilitoa begi dogo la mgongoni la Upendo, lililo na nguo chache za kiraia ambazo alianza nunua, akalitupia nje kisha kumvuta mvuta Upendo naye aende nje. Hakika, hakutania. Japo Upendo aliweka vizuizi vya hapa na pale asitoke, ila havikusaidia. Kwani alizidiwa nguvu iliyomfanya avutwe vutwe kama mtoto mdogo.



    Nje! Vumilia hakukaa. Alivyofanikiwa kumtoa alifunga mlango akaondoka zake, huku akimwachia kiasi kidogo cha pesa kama shukrani kwa kile alichotendewa, chenye uwezo wa kumsaidia kwa siku kadhaa. Uchungu ulijikusanya, ukatengeneza fundo kubwa la malipizo. Kwa Vumilia, na wote waliochezea hisia zake na kumwacha soremba. Alivuta kumbukumbu, kuwakumbuka wabaya wake wote, akianza na Kamanda wa Kikosi chao, Kanali (Knl) Sospeter Kembo, alifuatia Mchungaji wa kanisa, alilokuwa anasali. Mch. Jumanne Somola, wa kanisa la waadventista sabato lililopo maeneo ya Magomeni. Mwanaume ambaye amemfanyia zaidi ya unyama. Kitu ambacho katu hakufikri kama ipo siku sehemu hiyo itaingiliwa na mwanaume. Alifanywa tendo kinyume na maumbile. Aliliwa jicho. Pia fikra zake zilienda mbali zaidi, na kumkumbuka mtaalamu, namna walivyolianza zoezi ile siku, alivyoambiwa maneno mengi yaliyojaa ushindi lakini mwishowe mambo yameenda kinyume, tena kwa muda mfupi sana. Naye alimjumuisha. Wa mwisho aliyeibuka katika kumbukuzi hiyo ni Vumilia. Mwanaume ampendaye, ambaye hakuwa hata na chembe ya shaka naye, kwamba ipo siku atakuja fukuzwa ama dhalilishwa mithili ya mbwa kama alivyofanywa.

    “Hakika! Sitowasamehe,” aliropoka, kisha kuvuta begi lake na kuondoka.



    Macho ya majirani yalimsindikiza. Wenye kumuonea huruma hawakukosekana, na wenye kumdhihaki, kwa kutaka kujimilikisha mwanaume wa mwanamke wenziye nao hawakukosekana, wakiwa na lengo la kumpatia msaada baada ya kumhisi katawaliwa na tahayari. Alifunga safari, pasi na kufahamu wapi aendako na nini hitimisho la maisha yake baada ya tukio hilo. Safari yake iliishia nje ya mji kidogo. Eneo la tambarare lililotawaliwa na kichaka kifupi. Alilitumia eneo hilo, kwa kupumzisha mwili na akili kwa muda baadaye akajiwekea mikakati nini afanye moyo upate kutakasika. Jioni ilivyowadia. Saa kumi, akarejea tena mjini, katika maduka ya hardware akanunua vifaa kadhaa, bisibisi, praiz, na nyundo ndogo. Ambavyo alinunua kwa kiasi kidogo cha pesa, zile alizopewa na Vumilia. Kiasi kilichosalia alihifadhi kwa matumizi mengine siku zijazo yenye manufaa kwake. Muda wote, alikuwa mwingi wa hasira, chuki, uchungu na wehu kana kwamba kashikwa na wendawazimu.



    Pia alifanya manunuzi ya kalamu ya wino, sambamba na daftari la kumbukumbu, ambalo aliandika jumbe mbalimbali katika kila kurasa kisha akazichana na kukunja. Juu yake, aliandika majina ya watu kadhaa, alipokamilisha alizihifadhi begini. Siku iliyofuata, alianza kutekeleza kile kilichotamalaki moyoni mwake. Nafsi ya kisasi. Kwa wanaume wote waliomhadaa. Ila alinza na mmoja mmoja akifanikiwa ahamie kwa mwingine mpaka wote watavyomalizika. Mtaalamu, ndiye alimchagua kuanza naye.

    “Hata kama sitokufikia moja kwa moja, ila nitafanya tendo ambalo katu huwezi lisahau maishani mwako. Litalokupatia fundo la umivu kila leo, kama mlivyonipatia,” alisema Upendo, akiwa wanguwangu, mwendo usio na papara akiongoza kuelekea nyumbani kwa mtaalamu, Mzee Kijana.



    Moyo wa huruma, uliotawala udini, wenye kusamehe kila baya, kama ilivyo awali, sasa haukuwepo kwa Upendo. Udunia ulimtawala, na kuamini kila kitu lazima kifanikiwe katika hilo kwa uwezo pekee wa binadamu na si Mwenyezi Mungu tena. Mafundisho yote yaliyojaa kichwani mwake aliyasahau, kama si kupuuzia. Sasa alikuwa na roho zaidi ya simba, kwa binadamu wenziye waendao kinyume naye. Neno msamaha alilisahau, kama asisitizavyo Mwenyezi Mungu kwenye vitabu vyake takatifu vya kidini. Alitanguliza kisasi, atendewapo baya, kutokana na imani aliyonayo kwa wakati huo. Kwamba hiyo ndiyo njia sahihi ya maamuzi. Aliwasili nyumbani kwa Mzee Kijana akiwa katika muonekano wa kazi yake, aliyokuwa anaihudumu kipindi cha nyuma kabla hajatoroka. Alivaa kombati. Alibisha hodi, ikaitikiwa na sauti ambayo bado ilikuwepo kwenye kumbukumbu zake. Sauti ya mtoto wa Mzee Kijana. Sekunde chache baadaye alifunguliwa mlango, akaangaza huku na kule kisha akaingia.

    “Sijaja kihuruma, kama nionekanavyo katika wajihi wangu. Ndani nina machungu sana, ambayo katu siwezi yaelezea. Hivyo yeyote ni halali yangu, ili-mradi mlengwa afikiwe na taarifa,” alisema Upendo kimoyomoyo, wakati huo akijifuta kijasho chembamba kilichokuwa kinamtiririka kwa leso yake ndogo ilioyoonekana kuwa na ubora upungufu.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walisabahiana, baada ya hapo walienda moja kwa moja kwenye hoja husika. Ambayo ni ya ufahamu wapi Mzee Kijana anapatikana kwa wakati huo. Mwana pasi na chembe ya shaka, kuwa mtu aliyoko mbele yake kaja kishari shari, alifunguka ukweli, wapi baba yake anapatikana. Ambapo kwa wakati huo alikuwa kaenda mjini kufanya manunuzi ya mahitaji fulani.

    “Unaweza fanya mpango nikawasiliana naye, hata kwa njia ya simu?” aliuliza Upendo.

    “Kuhusu hilo ondoa shaka. Fanya subira nikuletee,” alisema yule binti wa Mzee Kijana, kauli iliyoambatana na kitendo cha kuinuka pale alipoketi kisha kuanza kupiga hatua kuifuata simu alikoiacha.



    Dakika moja ilikuwa kubwa, haikukamilika, alirejea pale sebuleni akiwa kakamatia simu mkononi, ikiwa katika masubirio ya kupokelewa maana alishapiga toka alikoichukua. Alimkabidhi Upendo, kisha kurejea atokako hali iliyompatia wasaa mzuri wa kujimwaya mwaya aongeapo. Tena kwa sauti ya upole, iliyokosa uashirio wa nia mbaya.

    “Mzee Kijana!”

    “Naam! Binti yangu,” alisikika Mzee Kijana, kwa sauti ya bashasha.

    “Mzee Kijana, sauti uisikiayo si sauti ya mwanao. Naamini, ni moja ya sauti uikumbukayo katika kumbukumbu zako...” alisema Upendo, ila hakuweza malizia kauli yake, alikatishwa na tamko la Mzee Kijana.

    “Hapana! Bado sijakufahamu. Naomba uniambie ni nani.”

    “Haina haja ya kunitambua kwa jina. Sauti tu yatosha kukufahamisha. Acha nikuambie kitu mzee wangu. Daima, hamnaga marefu yasiyo na ncha. Hata uhangaike vipi hiyo hatua lazima ifikiwe. Nakuhabarisha, malipo ya utapeli ulionitendea, unaendwa kulipwa leo,” alisema Upendo na kukata simu.



    Mzee Kijana akabaki kwenye sintofahamu, kufikiria huyo mtu ni nani na wapi alishawahi isikia sauti yake. Pindi anaendelea na fikra hizo, pasipo kufikiri nini anachoenda kufanyiwa, tayari Upendo alishakifikia chumba alichopo mwanaye. Aliyekuwa anafanya mihangaiko ya mapishi. Mwendo wake ulikuwa wa mnyato, asisikike, ili kile atachofanya kiwe sehemu ya mshangazo kwa mtendewa. Tena kwa udhihirishaji kwamba hasamei, awe mtoto, ama mhusika lazima atende alichopanga, alivaa mavazi mengine makubwa makubwa juu ya kombati ili ifahamike afanyaye ni mtu mwingine. Mkononi alikuwa kakamatia kisu kidogo, chenye ufanano na vile vitumikavyo kufanyia oparesheni mahospitalini. Usoni alifunga nikabu, mkono mwingine, ambao ni wa kushoto alifunga kamba iliyoning’iniza chupa ya mnyunyizio iliyotengenezwa kwa kemikali zenye athari kubwa sana zigusapo mwili wa binadamu ama kiumbe chochote hai na vile visivyo hai.

    “Nitatubu baadaye,” alisema kimoyomoyo, pindi akiuongoza ule mkono ulioning’iniza chupa ya mnyunyizio kwa yule binti.







    Alivyomfikia, aliutumia huo mkono kumgusa, katika moja ya bega lake. Yule mtoto alivyogeuka kuangalia ni nini, hakuwa na bahati. Alikutana na majimaji kiasi kidogo yaliyotua usoni. Alivyojaribu kujitetea kwa kukinga na kiganja cha mkono, alishutukia amepigwa kofi, katika moja ya shavu, lililochangia kumtoa kilio, na ombi la kuomba msaada asaidiwe. Kabla hajarudia kwa mara ya pili, ile anaanza tu, kutaka kutamka, kitu chenye ncha kali kilipita na kipande cha ulimi. Wakati huo hakuwa na uwezo wa kujitetea kikamilifu, kila alivyojitetea alifanya kwa kubashiri, kwani, hakuwa na uwezo tena wa kuona. Yale majimaji ya awali yalimwathiri. Upendo alivyoridhishwa na matokeo, aliyaondoa yale mavazi yake ya utendaji wa unyama, kisha kusalia katika muonekano wake wa kawaida. Alifungua lile begi, akatoa kikaratasi kimoja wapo kati ya vile alivyoviandika akutupia juu ya mwili wa binti huyo, ambaye alikuwa agaagaa huku na kule kujinusuru. Kisha akaondoka.



    Mzee Kijana alirejea nyumbani baadaye sana, takribani baada ya saa tatu, tangu alivyoondoka Upendo. Huku akiwa kapiga simu za kutosha kwa mwanaye pasipo kupokelewa zenye lengo la kutoa maagizo fulani. Laiti angelifahamu kilichompata mwanaye, angelirudi mapema, ama angelikuwa na mshawashwa wa kufahamu kwanini simu apigazo hazipokelewi. Angelifanya bidii pia, ya ufahamu. Ila yeye hakujali hilo, aliendelea na mipango yake. Aliivyoingia ndani alifikia kuita jina la mwanaye, karibia mara mbili, alivyoona hakuna muitikio, alihisi labda katoka, kaenda kwenye mizunguko ya kukutana na wenziye. Katika kuthibitisha hilo, aliamua kumpigia simu, ila alivyosikia muito unatoka mulemule ndani. Ikabidi aelekee alikousikia. Ambapo ni jikoni. Ghalfa, alishtuka. Na kufanya hima ya kupiga goti chini ili awe naye usawa wa karibu. Alijaribu kumuita. Lakini hakuitikiwa, kwani alishapoteza fahamu muda, kutokana na damu nyingi iliyokuwa imemtoka. Pasi na kutaraji, alijikuta anamwaga chozi palepale, huku akijitahidi kuusoma ujumbe ulioandikwa kwenye kikaratasi kilichoachwa.

    “Hisia za kweli hazichezewi,” yalisomeka maandishi hayo.



    Sauti ya kilio aliyokuwa anaitoa, iliwafanya majirani kuzuru wapate kufahamu tatizo. Kwa kujiuma uma, huku maneno yakiwa hayakamiliki aliwahadithia kwa uchache baadaye walimsaidia kuongezana naye kuelekea kituo cha polisi, ambako walipatiwa PF3 kwa ajili ya matibabu. Walivyoondoka hapo walielekea hospitali, tena kwa msaada wa gari ya polisi, ambao baadaye walienda nyumbani kwa Mzee Kijana punde walivyotoka hospitalini, kwenda kuchunguza na kuchora ramani ya tukio.



    Muda wote wa matibabu Mzee Kijana aliketi nje ya chumba cha daktari kilichokuwa kinatumika mwanaye kutibiwa. Chozi likiwa linamdondoka kama mtoto mdogo, huku akivuta picha kukumbuka sauti na uhalisia wa mtu aliyefanya tukio alivyo. Hilo lilienda sambamba na dua, kumuomba Mwenyezi Mungu amnusuru, kwani ni binti wa pekee anayejivunia. Hana mtoto mwingine zaidi yake. Jitihada za madaktari zilitoa matunda saa nne baadaye. Baada ya kukamilisha kila kitu kilichopaswa kufanyika kwenye matibabu waliyokuwa wanaendelea nayo. Jitihada zao zilirejesha fahamu na kupunguza uzito wa tatizo.

    “Tushakamilisha jukumu letu. Ila hatuna hakika kama binti yako atakuwa na utimilifu katika uonaji na uzungumzaji,” alisema daktari aliyeongoza jopo la matibabu.

    “Ina maana mwanangu hatoweza ongea tena?”

    “Muombe Mungu mzee wetu. Anaweza akamtendea miujiza.”



    Hakuwa na budi, ilimlazimu kukubaliana na yote, pindi akisubiri miujiza ya uponyaji na kumbainishia mhusika wa tukio toka kwa Mwenyezi Mungu. Alivyoanza pata nafuu, siku kadhaa baadaye polisi walimtembelea, awaeleze uhalisia wa mtu aliyefanya tukio. Kwa sababu hakuwa na uwezo wa kuzungumza, alisogezewa kalamu ya wino na daftari aandike mazingira ya tukio yalivyofanyika.

    ****



    Wakati wote makazi ya Zamzam yalihamia nyumbani kwa dada yake, aishiye mtaa jirani na ule waliokuwa wanaishi, mara baada ya kutoka mbio pale kwao. Huku akiwa mwingi wa kudondosha kilio, kilichoambatana na machozi ya kutosha, kutoa hisia namna aumizwavyo na hali iendeleayo. Haikumfurahisha, kiasi kwamba mawazo yalizidi ongezeka kichwani, yote yaliyomuondolea morali ya uwepo wake duniani, kutokana na kumbukumbu ya ufanyaji wa mambo mengi mema kwa baadhi ya ndugu wa Vumilia halafu leo hii si chochote, si lolote kwao. Hakika! Mambo yalimfika kooni, kuitafuta furaha ya moyo wake ilimlazimu, aachane na Vumilia amtafute mwanaume mwingine atayepooza yote yaliyomuumiza, japo hakudiriki kuruhusu ipate tokea siku kuona hilo linatimia. Kwa kipindi cha awali, ila kutokana na hali iendeleavyo alipaswa kuruhusu utengano. Kila akumbukapo sehemu ya kiapo chake, punde walivyofungishwa ndoa ya mkeka ule mchana hakusita, kudondosha kilio hata kama alikwishanyamaza. Kwani maumivu aliyokuwa anayasikia si ya kuelezeka. Hali hiyo ilimsukuma, kutohitaji kuonana na watu wengi, hasa waishio maeneo ya mbali na pale aishipo sasa. Alikuwa anahitaji kuonana na dada yake pekee, na baadhi ya majirani. Wengine hakuhitaji kuonana nao. Vumilia akiwemo, sababu ndiye chanzo cha maumivu ayapatayo.



    Hata baadhi ya ndugu, dada wengine, wajomba, Shangazi na wazazi, nao hakuruhusu wajitolee kuingilia tatizo hilo. Aliomba aachiwe mwenyewe, ili afanyapo maamuzi yawe maamuzi ya kujiamulia na si nguvu ya mtu imetumika kumshawishi kuamua. Hakuhitaji kabisa watu wengine waingilie mahusiano yao kuyajadili, kama majadiliano ya usuluhishi watafanya wahusika wenyewe, ataporidhia. Upendo alionao Vumilia juu yake, hakuruhusu kirahisi akubaliane na uamuzi wa mkewe. Akawa anamfuata kila muda, tena kwa msaada zaidi wa kufanikisha familia yake irejewe na amani, kazini walimpatia ruhusa kwa muda usiofahamika, hadi pale mambo yatapokaa sawa. Alifanya jitihada za kutosha kumbembeleza, ila hakusikilizwa kwa lolote atamkalo. Kwa udhihirisho, mara ya mwisho kwenda, pindi anafanya harakati za kung’ang’aniza aingie ndani, alishtushwa na ubaridi wa ghafla uliotawala kwenye paji lake la uso mara baada ya kitu cha ncha kali kupita. Alivyofanya tafakuri ni nini, matone ya damu yaliyokuwa yanadondoka chini yalimjibu kwamba kuna sehemu kakatwa.



    Toka afanyiwe hivyo, hakugusa tena ardhi ya mahala hapo. Ila hakufa moyo, aliamini ipo siku yataisha, ukawaida wa awali utarejea. Kwa kuwa bado alikuwa na mapendo naye, hakudiriki, kuonyesha uchovu mapema wa ushindwa, kisa tu, awamu zote aendazo kakataliwa. Aliithamini yake afya. Kwa kutaka kuendelea na Zamzam pekee mpaka pale walipopangiwa na Mwenyezi Mungu kuwa mwisho wao. Utofauti uliojitokeza hakutaka kabisa upoteze mahusiano yao, kwamba sababu hawaelewani basi atafute mwanamke mwingine, kwa kigezo cha kuamini ndiyo suluhisho pekee. Hapana! Dawa ya tatizo, ni kulitatua. Vumilia alijiapiza kutumia kanuni hii. Baada ya kumfukuza Upendo na kidonda kilivyopona kabisa akawa anazuru kwa mara nyingine, aidha kwa wakati huo alihisi yawezekana akili yake ishabadilika.



    Kila siku. Asubuhi, mchana, jioni na siku nyingine usiku akawa anashinda huku, akiwa na Zamzam mwenyewe ama dada yake. Pasipo na ufahamu wowote, miongoni mwa siku alizokuwa anatembelea, Upendo alikuwa nyuma yake. Kwa usiri mkubwa, kwani muda wote alikuwa mtu wa kujitanda baibui na nikabu usoni. Pasi na sahau dila, mithili ya wamama wa kipwani. Hivyo aliweza kushuhudia mengi, na kumpa utambuzi, nani anayefuatwa na Vumilia mahala hapo.

    “Nakupenda sana Vumilia, ila sababu umecheza na hisia zangu. Naweka kwanza upendo pembeni, kisha nafanya kile nilichojipangia. Hakika, katu sitokusamehe. Lazima upate funzo,” alijisemea Upendo. Akiwa kaketi jirani na soko akipanga panga vitu fulani kwenye begi. Alivyomaliza, taratibu alipiga hatua kuondoka eneo hilo.



    Mbele aliita bajaji, akapanda na kumuamuru dereva ampeleke ule mtaa aliokuwa anamfuatiliaga Vumilia. Sababu kulikuwa na umbali mrefu toka sokoni, dereva aliendesha mwendo mkali mno, uliowafanya wachukue dakika chache kufika. Hakuhitaji ashukuie moja kwa moja kwenye usawa wa nyumba aliyokuwa anaenda Vumilia, aliteremkia nyuma kidogo, baada ya hapo alianza kuelekea punde alivyomlipa dereva nauli yake. Alipiga hatua kadhaa, akaanza kusikika ananadisha biashara ya vipodozi vya kike, tena akiwa kakamatia vichache mkononi. Hayo aliyafanyia barabarani, muda mwingine alipiga hodi nyumba za watu, walivyotokeza wenye nyumba aliwatangazia, waliopendezwa walimchangia, na wale wasiopendezwa waliishia kutoa shukrani kisha akaendelea na safari.

    “Dada samahani,” alisikika Upendo, akimsaili dada mmoja aliyemkuta kaketi barazani, kwenye ile nyumba aliyokuwa anatembeleaga Vumilia. Kwa dada yake na Zamzam. Ambaye ni Zamzam, akiwa anajisomea jarida la Tanuru la simulizi.

    “Bila samahani,” alijibu Zamzam.

    “Nina biashara ya vipodozi, bei poa karibu na bure.”

    “Mmmh! Dada yangu, uchumi wenyewe huu tunatolea wapi hela za kununulia vitu kama hivi? Zote tuzipatazo tunakimbizia kwenye chakula,” alisema Zamzam. Huku akipokea vipodozi kadhaa vya mfano. Mafuta ya mgando, losheni, na pafyumu. Pia alitoa chupa refu kiasi aliyomtambulisha kuwa ni dawa ya kuuwa wadudu mbalimbali watambaao.



    Pindi Zamzam anahangaika kusaili yale manukato aliyokabidhiwa, Upendo aliingiza tena moja ya mkono wake kwenye begi, akatoka na chupa nyingine, ifananayo na ile aliyomtambulisha ni ya kuuwa wadudu. Akaikamatia vyema mkononi, kidole gumba juu ya kibonyezo kinachoruhusu kile kilichopo ndani kutoka.

    “Wakati ni sasa, nikichelea naweza fumaniwa halafu azma yangu mwishowe isitimie,” alijisemeza. Na kuanza kuongeza nguvu taratibu kwenye kile kibonyezeo. Wakati huo, Zamzam anainua uso wake amtazame aeleweshwe kuhusu maneno yaliyomtatiza yaelezayo namna ya utumiaji katika moja ya chupa alizoshikilia.



    Kitendo cha uso kukaa sawa, kuweza kumtazama aliyoko mbele yake akakumbana na majimaji, ambayo tone moja lilivyodondokea ulimini, alishindwa kung’amua yana ladha gani. Hata kabla hajatoa neno kuzungumza kwanini anafanyiwa hivyo, kisu kilekile kilichotumika kulenga ulimi wa mtoto wa Mzee Kijana, kilitumika kwa mara nyingine hapa. Kilitua katika ulimi wa Zamzam na kumfanya ashindwe kutoa neno alilohitaji kuzungumza na hatimaye kuanza kuugulia maumivu. Upendo hakujali madhara gani yatayojitokeza, alichojali ni burudisho la moyo na uhitaji wake kwa wakati huo ukoje. Alivyojihakikishia kile alichofanya kishaanza kuchanganya, alitoa kikaratasi kimoja wapo akamdondoshea karibu yake kisha akaondoka. Huku nyuma Zamzam alibaki kugugumia maumivu, ya ulimini na yale ya usoni, ambayo yalitokana na macho. Kwani yale maji aliyomwagiwa yalifanikiwa kuingia machoni. Watu wachache wapitao jirani na hapo, walioshuhudia namna alivyokuwa anahangaika kwa kujiviringisha toka upande mmoja kwenda mwingine, kwa sababu ya muwasho uliozalishwa na yale majimaji, ndiyo waliokuwa wakwanza kumpatia msaada. Walimpatia huduma ya kwanza, kisha walimkimbiza hospitalini, pindi wengine wakifuatilia suala la PF3. Dada yake na Vumilia walifikiwa na taarifa baadaye sana. Kwa muda tofautitofauti waliofika nyumbani. Kupitia kwa majirani ambao walishuhudia harakati za kumsafirisha hospitalini. Kila mmoja alivyofikiwa na taarifa, chap, aliwasili hospitalini, kuhakikisha aambiwacho. Kufahamu maendeleo na mengineyo yanayopaswa.



    Maumivu waliyojisikia dada yake Zamzam na Vumilia, kana kwamba wao ndiyo wametendewa. Waliumia mno, walilidhihirisha hilo kwa kilio cha sauti ya chini kilichokesha kuwatoka pindi wakiwa wameketi nje ya chumba cha wagonjwa wahitajio uangalizi, wakisubiri taarifa toka kwa daktari anayeshughulika ipasavyo kurejesha ubora wa afya ya mwenzao ambao ulionekana kupotea kwa kasi. Kila mlango wa chumba ulivyofunguliwa, hawakuacha kuinua macho yao kuangaza nani atokaye, ila walivyomuona kuwa sio mhusika wanayemhitaji waliendelea na kawaida ya awali. Mlango ulivyofunguliwa na kutokeza mhusika. Ambaye ni daktari aliyekabidhiwa jukumu la kuratibu matibabu ya Zamzam, walimvaa na kumporomoshea maswali lukuki aliyoshindwa aanze lipi kulijibu. Mithili ya watoto wadogo, wamuonapo mtu wampendaye halafu zimepita siku nyingi pasipo mtia machoni.

    “Musiwe na haraka, vuteni subira, tuwapa taarifa kamili ila si kwa leo,” alisikika yule daktari, huku akijitahidi kuwasukuma taratibu apate nafasi ya kupita.



    Ndani ya chumba cha wagonjwa wahitajio uangalizi, hali ya Zamzam ilikuwa mbaya. Tena mbaya mno, iliyokosa kuonyesha hata chembe ya dalili ya unafuu. Madaktari na wauguzi waliokizunguka kitanda alicholazwa, walifanya kila jitihada, lakini jitihada zote hazikuonyesha matumaini ya uponyaji. Yaani ndiyo kwanza walizidisha hali kuwa mbaya zaidi. Hasa usoni. Aliharibika, kwani, kulitengeneza vijishimo vidogovidogo vilivyojizidisha kila sekunde kadhaa zilivyopiga hatua. Urembo alionao, wote ulipotea, sasa alikuwa mbioni kuitwa mlemavu, maana achilia mbali vishimo, macho yalipoteza nguvu ya kuona. Aligeuka kuwa kipofu hata kabla matibabu hayajakamilika. Kilichowapa shida madaktari, ni kukosa ufahamu, hali hiyo imesababishwa na nini. Laiti wangelifahamu, hakika! Mapema sana wangelitatua tatizo. Hivyo walifanya mambo kwa kubashiri, kwani hata walivyojaribu wapate ufumbuzi wa tatizo toka kwenye mashine mbalimbali, mashine hazikuonyesha ugonjwa.



    Kuna muda walijaribu. Kupiga simu hospitali zingine kubwakubwa zilizopo nchini, na zile za nje ya nchi kuulizia hali kama hiyo inakuaje kuaje, ila hamna mrejesho wa maana walioupata. Zaidi ya kupoteza muda. Mwishowe ilibidi wamshukuru Mwenyezi Mungu, lolote litalotokea walazimike kulipokea, na ndiyo ule muda daktari muongozaji alitoka chumbani. Ila hakuchukua muda mrefu kurejea, tena alirejea akiwa mwingi wa furaha katika wajihi wake uliowashangaza wenziye.

    “Vipi? Kulikoni?” aliulizwa na mmoja wa wenziye kwa sauti isiyotoka vizuri kwa kuwa alijifunga kizuia bakteria mdomoni.

    “Nimepata wazo jipya. Nikaamua nije niwashirikishe tulijaribu, likishindikana ndipo nielekee.”

    “Lipi tena?”





    “Tumchome sindano ya fangasi,” alisema na kutulia. Kusikilizia litapokewaje na wenziye.

    Alimtazama, mmoja baada ya mwingine, na kuwaona wako tuli wametulia. Hali iliyomfanya ahisi wazo lake halijaleta ushawishi kwao. Lakini baadaye alishtuka kuwaona wakitingisha vichwa vilivyoashiria kukubaliana na kitu alichozungumza. Haraka sana, wazo likatekelezwa. Lilisogezwa bomba la sindano, kisha dawa ya fangasi iliyotengenezwa katika muundo wa kimiminika, ifahamikayo kwa jina la Sporanox. Mmoja wao alinyonya dawa, ilivyofikia ujazo unaotakiwa aliikita taratibu mwilini kupitia kwenye moja ya mishipa ya mkono.

    “Tusubiri matokeo,” walisikika kwa pamoja.



    Walijipa muda. Kusubiri matokeo tarajiwa, kisha wakaondoka. Muda walioupanga ulivyowadia, ambao ni dakika kumi na tano. Walirejea, wakafanya uchunguzi wa hapa na pale, wakabaini imesaidia. Hivyo baadaye. Usiku wa saa nne, walimpeleka wodi ya kawaida, iliyowapa nafasi ndugu, rafiki, majirani na wengineo wenye uchungu naye kumuona.

    “Naamini, afya ya ndugu yenu itaendelea kuimarika kila sekunde zinavyozidi kupiga hatua. Ila cha kusikitika, hatoona wala kuongoea kwa ufasaha katika maisha yake yote,” alisema daktari aliyeongoza matibabu ya Zamzam, alipokutana na Dada yake Zamzam na Vumilia.

    “Dokta! Ina maana mumeshindwa kabisa kutatua moja ya tatizo kati ya hayo uliyotuambia?” aliuliza Vumilia.

    “Hatuna jinsi kaka yetu. Uwezo wetu umeishia hapa. Labda hospitali za mataifa yaliyoendelea, kama muna uwezo munaweza kumpeleka mukajaribu bahati yenu.”

    “Dah! Zamzam wangu. Ama kweli, hujafa hujaumbika,” alijisemeza Vumilia.



    Inavyoonekana Upendo alitumia kemikali nyingine kwa Zamzam. Tena komesha, tofauti na ile aliyoitumia kwa mtoto wa Mzee Kijana. Kwani lengo lake likiwa ni moja tu. Kuleta maumivu makali kwa wale waliomtenda. Ambayo katu hawatoyasahau katika maisha hadi mwisho wa uhai wao. Siku za baadaye uchunguzi ulianza, kumtafuta nani aliyefanya matukio hayo. Tena kupitia ule ujumbe ulioachwa, walibaini kuwa mhusika ni mmoja yuleyule aliyefanya tukio la kwanza, ndiye aliyehusika na tukio la pili. Kwa sababu jumbe iliwiana. Ileile ya hisia za kweli hazichezewi. Kwa kuwa watendewa afya zao hazikuruhusu, ndugu wa watendewa, Mzee Kijana, Dada yake Zamzam na Vumilia kila kukicha wakapewa jukumu zito la kuripoti kituo cha polisi kuorodhesha watu wanaowahisi kuhusika na tukio.



    Kuna muda, Vumilia alimhisi Upendo. Hisia iliyokatishwa na kumbukumbu kwamba Upendo kaondoka ndani ya mji huo siku nyingi zilizopita kabla ya tukio, pia, kuhusu ufahamu baina ya Mzee Kijana na Upendo, wanafahamiana vipi? Ilichangia kumtoa kwenye uhusika. Kwa kuamini sababu hamfahamu Mzee Kijana basi hatokuwa na ufahamu na mtu aliyefanya tukio.

    “Hapana! Wawili hawa hawafahamiani. Itakuwa mtu wa huyu mzee wanafahamiana na Zamzam, wamegombana katika mambo yao, akaamua kumfanyia jambo hili la ajabu,” aliwaza Vumilia.



    Waliishia kubashiri. Pasipo kumpata mhusika sahihi wamdhaniaye. Kwani kila walivyofikirisha akili zao, mzunguko uliishia palepale walipoanzia. Yaani kama walianza na mtu mmoja hadi mwisho wa mzunguko waliishia na mtu huyohuyo. Hali hiyo ilipelekea wakati mgumu kwa jeshi la polisi. Wataanzia wapi kumfuatilia mtendaji mkuu wa tukio. Mwishowe faili liliwekwa kapuni, huku wakijinadi kuendelea na uchunguzi, pale mhalifu kamili atapopatikana, awekwe hatiani. Pia walitoa kazi hiyo kwa ndugu watendewa. Endapo watafanikiwa wasisite kutoa taarifa kituoni, hatua za haraka zichukuliwe.



    Mwezi mmoja baadaye Zamzam aliruhusiwa kuondoa hospitalini. Kwani tayari afya yake ilikwisha tengemaa, ila alibaki na kovu la ulemavu. Wa kutoona na uzungumzaji wa kukatakata pia. Alirejeshwa palepale kwa dada yake, Vumilia akawa na jukumu la kumtembelea siku zote kumtakia hali pamoja na kuendeleza maombi yake ya awali, waendelee kuishi pamoja. Kwa sababu bado alikuwa na mapendo naye. Hakutaka ulemavu uliomkumba uharibu dhamira, kisa tu kabadilika muonekano. Siku za baadaye, Zamzam aliridhia. Kwa ishara, maana ndiyo lugha pekee aliyokuwa anatumia kwa wakati huo kwa sana. Walianza maisha mapya. Wakiwa na mfanyakazi anayeshughulika na kazi mbalimbali za nyumbani. Kupika, kuosha vyombo na kufua pia kwa baadhi ya nguo. Zingine zilikuwa zinafuliwa na Vumilia hasa nguo za ndani. Siku mojamoja, aliyojisikia kuchangamsha mwili wake, ndipo Zamzam alifanya shughuli. Kwa ushirikiano na wenziye asipate kufanya ovyo.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Maisha ya wawili hawa yaliendelea hivyo. Vumilia akijihangaisha huku na kule, kujitafutia riziki, achilia mbali ajira aliyopata kuwa nayo mkononi ambayo siku za baadaye alidiriki kuiacha, kwa sababu ya ufinyu wa muda alioupata wa kumfanya mwenziye afarijike. Tena kipindi alichoacha, ni wakati walioondokewa na mfanyakazi aliyekuwa tegemezi kwao katika majukumu ya nyumbani. Hivyo majukumu yote yakahamia kwa Vumilia, na yalimpasa kuyafanya mwenyewe mpaka walipofanikiwa kupata mfanyakazi mwingine. Haikuishia kuacha kazi pekee. Hata mji nao walihama. Walihamia mjini Ifakara, moja ya wilaya iliyoko mkoani Morogoro. Walivyofika huko, walipanga chumba, chumba kimoja na sebule, kama ilivyokuwa Dodoma. Pia walikodi shamba, hekari mbili wakalima nyanya zilizowasadia kwa kiwango kikubwa kujikwamua kimaisha. Kwani mauzo ya mavuno yao, yaliwafanya wanunue kiwanja cha makazi, chenye ukubwa wa nusu hekari, kisha kujenga banda lenye umbo la saba pamoja na banda lingine dogo pembeni, ambalo waliliandaa kwa ajili ya biashara siku zijazo.



    Hakika! Machungu na maumivu waliyokesha nayo kipindi cha nyuma walianza yasahau. Furaha iliwatawala, na walifanikiwa kumpata mfanyakazi mwingine toka hapohapo mjini aliyewasaidia majukumu mbalimbali. Furaha yao ilizidi ongezeka zaidi, Zamzam alivyokamata ujauzito. Walifurahi, tena walifurahi haswa. Kwani kiwango chao cha furaha si cha kuelezeka. Muda wa kujifungua ulivyowadia, Zamzam alijifungua na kabahatika kupata mtoto wa kike ambaye walimpatia jina la Rahma. Hawakutaka kumpatia jina la urithi, kwa kuhofia anaweza kuiga matendo ya huyo mtu.

    ****



    Baada ya kukamilisha matakwa yake kwa wahusika. Upendo alirejea jijini Dar es salaam. Ila si kambini tena, mtaani. Aliamua rasmi kuwa raia wa kawaida. Tena alivyoona hajabainika katika uhusika wa yale matukio alifurahi mno. Na kumuomba Mwenyezi Mungu, amjalie pia kufanikisha kwa watu waliosalia hata kama akifanyacho ni tendo ovu. Makazi yake ndani ya jiji hili yalikuwa ya kutanga tanga. Leo huku kesho kule, na muda mwingi alidumu mikahawani, ili apate kudowea chakula. Alikuwa anasaidia kazi kadhaa mwenye mkahawa aridhikapo ndipo humpatia. Hiyo shughuli ilikuwa kuanzia asubuhi hadi kiza kiingiapo, akishapata chakula cha usiku hutafuta uelekeo mwingine. Mara chachechache sana, alipita maeneo jirani na makazi ya wale watu awatakao kuangalia mazingira yalivyo, yatayompatia mwanya wa kufanikisha azma. Usiku wa kiza kikali akawa anakesha kwenye madanguro, yajiuzayo wanawake. Lengo naye apate senti kadhaa zitazosukuma maisha yake endapo wamama wauza mikahawa watamchoka.



    Usabato uliokithiri kipindi cha nyuma sasa ulishaisha. Sasa alikuwa mjuvi wa matendo yote ya kihuni, na alifanya hivyo, baada ya ile sehemu aliyoamini atapewa mapenzi ya dhati na upendo timilifu kaachwa soremba. Hakuona haja ya kuendelea kujiumiza, kwa watu ambao hawako makini naye, hivyo ni heri ajichanganye tu. Pia kitendo cha kujichanganya katika madanguro, si kwa lengo la kupata pesa za kuendeshea maisha yake pekee, hapana! Ilikuwa sehemu ya rada pia, kumpata mmoja miongoni mwa wale awatafutao. Mchungaji Jumanne Somola.



    Wakati huo hakuwa na urafiki na mtu. Si ndugu, jamaa, rafiki ama wazazi wake. Alikuwa jeshi la mtu mmoja, hadi pale atapokamilisha azma yake ndipo ajaribu kuwaangalia. Hata aendapo maeneo ya kujiuza, alisimama sehemu ya kipekee, asogelewapo na mwenziye, hakuacha kuwafukuza na kuwakata kauli kabisa kwamba hapendi mazoea. Hayo ndiyo yalikuwa maisha mapya ya Upendo. Maisha ambayo katu, hakuyafikiria kama atakuja ishi siku moja. Maisha ya uchangudoa na uzururaji. Yaliyochangia kwa kiasi kikubwa mabadiliko ya afya yake. Kwani kuna baadhi ya siku alikuwa mwingi wa uchovu, mtapikaji na mambo mengi yaliyomfanya asiwe mwenye furaha. Kwenda hospitali, kuangalia nini kimsumbuacho kwake ikawa ngumu, aliishia kujinunulia vidonge vipunguzavyo maumivu maduka ya dawa kisha akaendelea na kawaida.



    Ulikuwa usiku kiza kinene. Usiku wa saa nane, Upendo akiranda randa huku na kule pembezoni mwa barabara, akijaribu kutafuta bahati yake kwa kuparamia waume wapitao na magari pia, aliyediriki kusimama ama kupita taratibu kuthaminisha warembo waliopo kama wanafaa. Pindi akiwa na mkazano huo, uliochangiwa kwa kukosa mteja tangu alivyofika mahali hapo, alishtushwa ghafla na sauti yenye ngurumo nzito ikimuita toka ndani ya gari iliyosimamishwa umbali wa mita kadhaa toka aliposimama. Alivyoitwa kwa mara ya kwanza hakusikia, ila mara ya pili alivyosikia muito, alipiga hatua chap kulisogelea gari husika. Ambayo ni Toyota Land Cruiser GX V8.

    “Ingia ndani ya gari,” alisikia sauti ikimuamuru, hata kabla hajafika upande husika ambayo mtu aliketi. Upande wa dereva.



    Naye pasi na kuleta ukaidi wa kuhoji hoji, alifungua mlango, nyuma ya dereva akapanda kisha gari ikaanza ondolewa taratibu. Alivyoketi kuna fikra fulani ikampata. Alirudisha kumbukumbu nyuma, na kukumbuka, kwamba kuna siku ashawahi pita maeneo hayo akitokea kwenye sherehe ya harusi ya rafiki yake usiku wa saa saba, akafanikiwa kuliona gari litumiwalo na mchungaji wa kanisa lake. Likiwa na mfanano wa lile alilopanda. Haraka sana, akahisi, wenda aliyoko mbele yake ni Mchungaji Somola, amtafutaye. Hivyo afanye vipi athibitishe ahisicho na asibainike? Alijiuliza, takribani dakika nne, anavyokuja kuzinduka, gari ilishapakiwa sehemu ya maegesho, mbele ya nyumba kubwa ya kifahari.

    “Tushafika, unaweza kuteremka,” aliisikia sauti ya yule mtu kwa mara nyingine ikimuamuru. Kwani toka walivyotoka ile sehemu ya kujiuzia hadi mwisho wao wa safari, hawakupata kuzungumza chochote.







    Hata kabla hajateremka, alivyoyachunguza tu, yale mazingira, aliyatambua na kufahamu yupo mazingira gani. Mwishowe alionekana kutikisa kichwa, kilichoashiria kukubaliana na jambo fulani. Alivyoteremka alitoa moja ya khanga kwenye begi lake akajitanda kichwani, ili uso wake usipatwe onwa vizuri. Baadaye alifuatia mhusika. Ambaye ndiye Mchungaji Somola. Mtu aliyejivika udini kuficha matendo ovu anayojihusisha nayo. Waliongozana hadi chumbani, huko ndipo Upendo alitumia wasaa vizuri wa kujionyesha ni nani, ili mwenyeji wake apate kumfahamu.

    “Hee! Ni wewe?” Mchungaji Somola alishangaa.

    “Haina haja ya kuonyesha mshangao. Haya ndiyo maisha yangu kwa sasa. Sema unachohitaji niwajibike, kisha nipate kuondoka.”

    “Ye...” alisema Mchungaji Somola, ila kabla hajamaliza kauli yake, alikatishwa na Upendo.

    “Acha unafiki. Wa kumshirikisha huyo mtu katika akili zetu sasa. Zilizotawaliwa na ushetani, kwani hatotusaidia.”



    Kimya kidogo kikapita. Kila mmoja akifikiria lake. Mchungaji Somola afanye mapenzi na Upendo, ilhali ashawahi kutokanaye miaka ya nyuma? na Upendo naye alikuwa anafikiri namna ya kupeleka umivu la milele.

    “Kama ashaanza haya mambo, basi ndiye atakuwa mwanamke wangu wa siku zote. Na nadhani sasa atakuwa ridhaa kwa ile michezo ya nyuma,” aliwaza Mchungaji Somola, akiwa kaketi kitandani.



    Baada ya fikra za muda mrefu, baadaye walianza yaondoa mavazi waliyovaa, tayari kuingia mchezoni, ambako sasa Upendo alikuwa zaidi ya mjuvi kwa ajili ya kukutana na kila aina ya muhogo. Walivyomaliza walienda bafuni kuoga, ili wafanye mambo kwa uzuri zaidi, utaowapatia burudisho muruwa litalokonga nyoyo zao. Walivyotoka bafuni, moja kwa moja walifikia uwanjani. Huku wakisindikizwa kwa manukato fulani yaliyofukizwa dakika chache zilizopita. Walianza kwa mitomaso, kuvipa viungo na akili pia ufahamu wa kutosha kipi kinachoenda kujiri punde. Huyu alishika huku, mwingine kule, huyu alitumia hiki, mwingine kile, yote katika kutoa taarifa mwili usisimke na ujawe na uhitaji wa tendo kufanyika kwa uharaka. Walitumia zaidi ya dakika kumi, na kumfanya Upendo kuwa mtepeta aliyeshinikiza aingiliwe baada ya Upendo mwenyewe kuonyesha dalili zote za uhitaji wa kushughulikiwa mwili upate kuwa mwepesi. Kwani uteute wa kutosha ulishatapakaa, na kuufanya mwingine utiririke na kuchafua sehemu ndogo ya shuka lililotandikwa. Lakini Mchungaji Somola, hakuafiki mapema hivyo. Aliendelea kung’ang’aniza aendelee kufanya kilekile afanyacho, akili itaporidhia kuingiza muhogo sehemu husika ndipo atekeleze.



    Upendo hakuwa na budi, ikambidi aridhie, japo si kwa mapendo yake. Bali kwa nguvu zilizotumiwa na Mchungaji Somola, kwani kuna kipindi alijaribu kubana miguu yake asiendelee kuchezewa, ila hakufanikiwa, baada ya kulazimishwa kupanuliwa na kushikwa shikwa sehemu zilizomtia nyege zaidi. Lengo la Mchungaji Somola lilikuwa moja tu, kufanya tendo lake sehemu iliyokoswa uhalali wa kutumiwa. Wakati huo alikuwa tepetepe, jicho liko legevu na uteute umekithiri vya kutosha. Huku kukiwa na kila dalili za Upendo kufika kileleni. Taratibu akaanza kuingiza. Upendo akiwa makini kuupokea na kuupa ukaribisho adhimu uliomfanya aanze kuukatikia nyonga upate jinafasi humo ndani. Alianza na sehemu iliyohalalishwa, tena pasi na kutumia kinga, alivyoridhika napo alimwinamisha hali iliyomfanya viwanja vyote viwili vijitanabaishe upande alioko. Hakukawiza, ili upepo usipate kukausha ule uteute ulioenea mhogoni.



    Awamu hii aliipeleka kule kusikohalalishwa. Kulikochangia kwa kiasi kikubwa kipindi cha nyuma atengane na Upendo. Ila kwa sasa, sababu alishajiingiza kwenye ufuska hakuwa na budi kuiruhusu sehemu hiyo kutumiwa.



    Pindi wao wanaendelea kupata unono katika ulimwengu wa huba. Vijana watatu walioambatana na wazee watatu pia, walizuru nyumbani kwa Mchungaji Somola usiku huo. Hawa walionekana kumfuatilia mchungaji, toka alikoianza safari yake wakiwa na nia fulani. Wao walikuwa ndani ya gari dogo aina ya Toyota Vanguard, nyenye rangi ya kijivu iliyo na vioo vya tinted. Ambavyo haviruhusu mtu wa ndani kuonekana. Hivyo mchungaji alivyopitia sehemu ya machangudoa na kumchukua mmoja wapo, wao walisimamisha gari yao umbali mdogo ili wasibainike kama wanamfuatilia. Juu ya hayo, pia walikuwa wanapiga picha katika mazingira fulani, ambayo ni tatanishi kwa mtumishi wa Mungu kama yeye haruhusiwi kuonekana. Alivyoondoka walizidi mfuatilia hadi alivyowasili nyumbani kwake. Tena ilivyo bahati, wigo uliozunguka jengo unaruhusu mazingira yazungukayo jengo kuonekana. Sehemu kubwa ilikuwa wazi. Hivyo pindi wanateremka waliwaona na walipiga picha pia.



    Baada ya sekunde kadhaa walionekana kuongea na simu. Ambazo hata hazikuchukua dakika moja walimaliza maongezi kisha wote waliteremka na kuongoza jengo lilipo. Walipofika langoni, walijitambulisha ni kina nani kwa mlinzi waliyemkuta, naye pasi na hiyana aliwaruhusu waendelee na safari. Miongoni mwao kulikuwa na askari wawili, wengine ni watumishi kanisani. Lengo la ujio wao ni kumkamata Mchungaji kutokana na matendo yake anayojihusisha nayo, waliyoyahisi toka muda, ila kipindi cha nyuma walishindwa kuthibitisha sababu hawakuwa na ushahidi. Maana walikuwa wanasikia sikia tu pembezoni kuwa mchungaji wao ni muovu. Hivyo baadaye walimuundia tume ya kumfuatilia na ndiyo hiyo iliyozuru nyumbani kwake muda huo. Walipiga hatua hadi usawa wa dirisha lake, ambalo mara nyingi huliacha wazi. Wakatega sikio vizuri wanyake umbeya juu ya kile kiendeleacho ndani. Walitulia tuli. Wasisikike wala kuhisiwa na wapate uhondo vizuri zaidi. Sauti ya mtoto wa kike akiugulia, haifahamiki kama ni maumivu ama unono ilisikika vyema sikioni mwao. Na kuwapa ufahamu mguno huo unasababishwa na nini. Walitumia takribani dakika mbili kusikilizia, kiasi kwamba watu wenye imani ndogo walianza pandwa midadi kwa kutamani nao wawe katika ulimwengu wa huba.



    Kimya kilivyotawala, kilichowatambulisha kuwa washamaliza, haraka, walikimbilia mlangoni na kushauriana mmoja wao agonge. Zoezi la kumtafuta mmoja wa kugonga, likafuatia kwa muda mfupi kisha wengine walijibanza kiambazani ili atapotoka ndani baada ya kugongewa amuone mtu mmoja pekee. Halafu wengine wajitokeze baadaye. Liliwachukua dakika tatu, kila mmoja kukaa sawa katika nafasi yake, alipotayarika yule aliyepaswa kugonga mlango aliandaa mkono wake kwa kuusogeza taratibu sambamba na koo, ila kabla hajaanza, alishtushwa kuona mlango unafunguliwa na mtoto wa kike akijitokeza mbele yake. Ambaye ni Upendo.



    Upendo naye alishtuka, tena sana. Mshtuko uliomfanya akaribie kudondoka, ila alijikaza na kumsukuma kwa nguvu yule mtu aliyoko mbele yake akafanikiwa kupata nafasi ya kupita na kuendelea na safari. Lakini hakufika mbali, wale waliojificha walijitokeza wakamzuia.

    “Nimekwishwa...!” alijisemeza. Huku wale watu wakimmulika mulika na tochi zilizopo kwenye simu zao.



    Aliwekwa chini ya ulinzi akafungwa pingu. Kisha wengineo wakaingia ndani kumfuata Mchungaji Somola, ambaye kwa wakati huo alikuwa katika hali nyingine. Upendo alifanya kazi yake. Hali waliyomkutana nayo walishangaa, na kuwapa picha moja kwa moja Upendo ndiye kahusika. Wakati huo alishapoteza fahamu, uso ulianza kuharibika na sehemu ndogo ya ulimi ishakatwa. Wapo waliyemdhania, kuwa Upendo ni jini, wazo lililotupiliwa mbali baadaye walivyomfikisha kituoni. Kituo cha polisi cha Stakishari. Ambako walimfanyia uchunguzi wa kina usiku huohuo toka kwa wataalamu mbalimbali wa mambo ya afya. Alichukuliwa maelezo na kufunguliwa mashtaka ya kujaribu kusababisha vifo kwa watu aliowatenda, baada ya hapo alipelekwa mahabusu kusubiri kupambazuke hatua zingine ziendelee.



    Asubuhi kulivyopambazuka habari yake ndiyo ilikuwa habari ya jiji. Kwenye vyombo mbalimbali vya habari, alikesha kutangazwa yeye tu, si magazetini, redioni na runingani pia. Kwenye mitandao ya kijamii ndiyo kuzidi. Pindi habari yake inaenea mtaani, mwenyewe aliamkia kwenye mahojiano kwa mara ya pili kuhusu tukio na uchunguzi wa kina juu yake. Awamu hii Upendo alihadithia ukweli uliomo moyoni mwake. Kuanzia mwanzo hadi hapo alipofikia. Siku zijazo akapelekewa mahakamani, kujibu tuhuma zinazomkabili.



    Mahakamani kulifurika watu wengi mno. Asilimia kubwa walikuja kumshuhudia namna afananavyo na matukio aliyotenda. Alisomewa mashtaka akakiri, lengo kutoisumbua mahakama, apate hukumu mapema apelekwe gerezani atulie kwa amani asiwaze tena mambo ya uraiani. Mahakama ilivyohairishwa alirudishwa mahabusu kusubiri tarehe nyingine aliyopangiwa. Shauri lake lilisikilizwa kwa muda wa mwezi mmoja tu, ikafikiwa siku ya hukumu iliyojumuisha watu wengi mno toka miji mbalimbali. Wengi wao wakiwa ni wale wanaomfahamu. Siku hii ilihudhuriwa na wazazi wake, ndugu, marafiki na jamaa wengine wengi. Madam Cecy, Mwanjaa na Vumilia ni miongoni mwa watu waliohudhuria. Huku wakipata habari zake runingani. Hata Zamzam naye alihudhuria, tena alivyoambiwa kuwa Upendo ndiye kamfanyia hivyo, alilaani vibaya mno na kutoa chukizo la milele la kutomsamehe. Walio na roho za huruma wanaomfahamu hawakuacha kudondosha chozi. Kabadilika vipi? Ndivyo walivyokesha jiuliza mwanzo mwisho hadi alivyosomewa hukumu yake. Kifungo cha miaka sita kikamvaa, iliyoambatana na adhabu ngumu ndani yake. Hukumu iliyowaliza zaidi wanaomfahamu. Lakini hawakuwa na jinsi kwani, kilio chao hakikuweza kubadili maamuzi ya mahakama. Mahakama ilivyohairishwa, alifungwa pingu na kuongozwa ndani ya karandinga tayari kwa safari ya gerezani kutumikia kifungo chake. Ila kabla hajapanda, aliomba kuonana na Mwanjaa, akaruhusiwa. Mwanjaa aliitwa, na kusogea jirani naye, akainamisha kichwa na kutega sikio karibu na mdomo wake.



    Yalikuwa maongezi mafupi, yaliyomsukuma Mwanjaa kuyahangaisha macho yake kuangaza huku na kule jicho lililojaa kila uashirio wa kumtafuta mtu fulani. Baadaye, Upendo alipakizwa ndani ya gari, na safari ikaanza, huku Mwanjaa akiambatana na Madam Cecy walivutana chemba wakateta jambo kwa kunong’ona kisha wakasukumizana kukimbilia sehemu zilikopaki taksi, walivyoifikia moja wapo walipanda kwa uharaka na kumuamuru dereva aifuatilie moja ya gari iliyojichanganya katika foleni ikitokea viwanja vya Mahakama. Muda wote ndani ya gari walikesha kumshinikiza dereva, ikibidi avunje sheria za usalama barabarani ili wapate kuiwahi hiyo gari kabla haijawapotea. Lakini, haikuchukua muda. Walishindwa ifikia na kuwaacha umbali mrefu mno, ambao hata wangelijitahidi vipi, wasingelifanikiwa kuipata. Hawakuwa na budi, walikubaliana na matokeo, walimlipa dereva nauli iliyotakiwa kwa umbali waliotembea baada ya hapo waliendelea na kawaida.

    “Tutamtafuta siku zijazo,” alisema Madam Cecy.

    “Sahihi, na ikibidi kabla hatujamwambia tuanze na wazee wake kabla hawajaondoka kurudi mkoani kwao,” Mwanjaa alichangia.

    “Ni ushauri mzuri. Lini tutekeleze hicho kitu?”

    “Kesho! Siku ya wikendi. Nina hakika watakuwepo nyumbani kwa mjomba yake, maana hawezi kwenda kazini.”

    “Hamna shida, utanipitia nyumbani.”



    Wawili hao walikuwa na jukumu zito. La kukabiliana na ndugu wa Upendo, wawaeleze walichoambiwa. Achilia mbali wao. Vumilia pia alihusika. Na ndiye waliyekuwa wanamfukuzia ile siku ya hukumu punde walivyopatiwa ujumbe. Na ndiye mhusika mkuu wa kwanza aliyepaswa kuambiwa kabla ya wengine, ili awe na ufahamu mapema. Asije leta mtafaruku mbeleni atapokuja ambiwa. Siku waliyopanga ilivyowadia walielekea nyumbani kwa mjomba yake na Upendo. Ambaye alikuwa anaishi maeneo ya Masaki. Walipokelewa kwa bashasha, na kukaribishwa sebuleni ambako kulikuwa na kikao kilichowakutanisha baadhi ya wanandugu wa Upendo. Nao wakakaribishwa kushiriki, sababu Upendo alikuwa mtu wao wa karibu sana. Hawakusita, waliungana. Pale walipohusishwa kutoa mchango wa mawazo, walitoa, na kupokelewa kwa ukarimu kabisa.



    Mada za wenyeji zilivyohitimishwa, waliingiza ya kwao. Iliyopelekea kuteka hisia za wengi hata kabla neno halijatamkwa. Kila aliyoko alitega sikio lake vyema, ili kile kiongelewacho akisikie vizuri na kukielewa. Si akitoka hapo aanze kuuliza. Utulivu, uliochangiwa na ukimya ulitamalaki. Ni mara chache sana, sauti ilisikika, labda wakati wa kujihoza kuilainisha koo, maandalizi ya kuchangia hoja aonapo yafaa.

    “Aaah!...jana, nilibahatika kuonana na Upendo. Kabla hajasafirishwa kuelekea magereza. Na kunipatia ujumbe, alioniomba niwafikishie ndugu na kijana mmoja aitwaye Vumilia,” alisema Mwanjaa na kuweka pozi. Kisha alijikohoza kidogo, na kupiga fundo la juisi ya parachichi, akaendelea.

    “Upendo, kaniambia. Awali ya yote anaomba msahama, kwa ndugu wote. Anafahamu kuwa kadhalilisha familia, ila nguvu ya hisia za kimapenzi ndizo zilimbadili na kuangukia kule aliko leo. Kuna watu aliwaamini, akawakabidhi umiliki wa mwili wake, lakini mwishowe watu hao, waliishia kuuchezea mwili wake na kuuacha. Jambo lililomfanya aghafirike, na kutengeneza chuki dhidi yao yenye uhitaji wa kulipiza kisasi. Na kweli kalipiza, japo yupo mmoja aliyesalia. Huko aliko kwa sasa anajuta. Lakini juto lake litaisha, ninyi mtaporidhia kumsamehe. Pili...” Mwanjaa alikatishwa na kauli ya mjomba yake Upendo. Iliyoambatana na kitendo cha kutingisha kichwa, kulia kushoto akimaanisha kutomsamehe.

    “Mmmmh! Mmmmh! Hapana, katudhalilisha sana. Udini wote uliokuwa umemkwiva leo kawa vile? Haiwezekani. Binafsi siwezi msamehe, labda wenzangu,” alisema mjomba.

    “Endelea dada yangu,” mwingine alisikika.

    Mwanjaa alipiga fundo lingine kisha akasonga mbele na maongezi.

    “Pili, Upendo, anaenda gerezani akiwa m...” hata kabla hajamalizia kauli yake, sauti ya pamoja ilimkatisha.

    “Mjamzito?”





    “Ndiyo! Upendo anaenda gerezani akiwa mjamzito.”

    “Nani kampatia huo ujauzito?”

    “Kijana mmoja aitwaye Vumilia Matatizo,” alisema Mwanjaa. Fuadi ukiwa umejaa hofu, kauli yake itapokelewaje. Alivyojaribu kuwasaili alimuona kila mmoja akiongea kivyake. Akinong’ona, na kutikisa kichwa kuashiria hawakubaliani na hilo jambo.



    Sababu mjumbe hauwawi. Ujumbe wao ulipokelewa baadaye wakaondoka. Siku iliyofuata wazazi wa Upendo, wakiambatana na mjomba yake walizuru gerezani. Ukonga, nia, kuthibitisha ujumbe walioambiwa jana kama una ukweli wowote. Ila isivyo bahati, hawakufanikiwa kuonana naye. Kwani siku hiyo gerezani hapo palitembelewa na ugeni ulioongozwa na Waziri Mkuu. Hivyo wakaombwa kurejea siku nyingine. Hawakuchoka. Ushauri walioambiwa waliufanyia kazi. Wiki moja baadaye walirejea tena, lakini pia waliambulia patupu. Upendo alihamishwa gereza. Alipelekewa gereza la kilimo Kitengule mkoani Kagera. Mwishowe walihairisha, wazazi wake wakarejea makwao mkoani Katavi. Na ndugu wengine wakaendelea na shughuli zao pia. Tena kwa sababu walishamjengea chuki kwa kuchafua familia yao, hawakuwa hata na chembe ya huruma dhidi yake.

    ****



    Maisha ya gerezani daima huaminika ni magumu. Ila kwa Upendo ilikuwa tofauti. Upendo aliyafurahia, moyo wake ulijawa na amani na kutamani aishi humo milele. Yote ni kwa sababu ya utambuzi wa haraka alionao, kutokana na yale aliyoyatenda nduguze hawatomhitaji tena japo kumsikia. Mbali na hao, wale aliowatendea unyama wanaweza msaka nao walipize kisasi. Hivyo alilazimika kuligeuza gereza kuwa sehemu sahihi kwake. Alisongesha maisha, huku akitengeneza marafiki wengi waliokuwa wanashauriana mambo kadha wa kadha. Wafungwa wenzake wa kike, na baadhi ya askari magereza. Wakike kwa wakiume. Jambo lililopelekea kwenye baadhi ya shughuli za gerezani hapo kupumzishwa. Ilikuwa jambo la kawaida sana, kwake kuketi siku nzima kwenye chumba chao walalacho pasipo kufanya kazi yoyote. Siku nyingine kufanya kazi nusu siku kisha kupumzishwa. Hilo lilifanyika si kwa sababu ya urafiki pekee, hapana! Bali mwili wake ulichangia. Maana alikuwa mjamzito, na chakula cha wazee pia.



    Askari magereza wa kiume, walikesha kujilea unono alionao, huku wakijinasibu kuongeza na kuimarisha viungo vya mtoto aliye tumboni. Upendo alijiachia. Tena pasi na kuangalia afya yake ikoje, alichojalisha ni unafuu wa maisha. Kila atakaye, alidiriki kumvulia chupi yake na kumwachia goma asasambuke nalo atakavyo, akisharidhika amuache unafuu wa maisha uendelee kumwelemea. Gharama kubwa ya mapumziko apatayo ulikuwa mwili wake. Aliuachia tu. Na aliruhusu kufanyiwa sehemu yoyote. Huku sehemu kubwa ikiwa ni ofisini ama kwenye vyumba vya vyoo mara baada waondokapo wenzake kwenda kwenye shughuli mbalimbali. Alijiachia, mithili ya kuruta wa kike kwenye mafunzo mbalimbali ya kijeshi. Ambao waaminiao kuwa wakifanya hivyo hawatofanya mafunzo magumu kama wengine. Sasa rasmi alibadilika, na kuhalalisha kuwa hayo ndiyo maisha yake.



    Hakika! Alibadilika. Upendo huyu hakuwa yule wa mwanzo tena. Si tabia, hata umbo nalo lilibadilika. Alipungua, na kusalia na umbo ambalo mtu anayemfahamu hawezi kuamini kwamba ndiye yeye aliyekuwa anamfahamu kipindi cha nyuma. Ila mwenyewe aliona kawaida, sababu ndiyo maisha aliyoyachagua kwa sasa. Siku zote alizoko gerezani hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumtembelea. Si wazazi, ndugu ama marafiki. Wazazi wake walishindwa kwenda kwa sababu ya hali ya kiuchumi, huku ndugu sababu walishamkataa toka walivyotambua uovu alioufanya uliohaibisha familia na koo kwa ujumla. Ilifikia kipindi hata mwenyewe aliweka kiapo, kutoonana na mtu yeyote atokaye nje ya gereza atayethubutu kumtembelea. Dhima, asionwe alivyobadilika. Hali aliyonayo aonwe na walewale walioko ndani ya gereza. Kwani aliamini akitembelewa atakuja onewa huruma hali itayomsukuma kuwa mliaji ilhali asharidhika na maisha hayo.



    Hatimaye saa, siku, majuma na miezi ilizidi songa mbele. Ujauzito nao ukazidi chanua na kujiweka bayana kila amuonaye atambue. Akaanza hudhuria kliniki, kwa msukumo toka kwa maafisa wa magereza, maana kuna wakati mwenyewe alikuwa haitaji. Kila tarehe aliyopangiwa kuhudhuria, alipelekewa kwa lazima, na zile siku ambazo mwenyewe aliridhia kwa shauku binafsi iliyokithiri moyoni mwake, aliwahimiza maafisa hao wamwahishe apate huduma mapema. Hali ilikuwa hivyo, hadi ilivyosalia siku chache apate kujifungua. Huku ukiwekwa muda wa makadirio wa wiki moja. Akiwa katika matazamio hayo, uongozi wa gereza ulipata amri. Toka wizarani, ya kuwaamuru wapunguze baadhi ya wafungwa wapelekwe gereza la Kisongo mkoani Arusha, ambalo lilipungukiwa na wafungwa baada ya wengi wao kumaliza muda wa kifungo chao na wengine kusamehewa. Hivyo kutokana na upungufu uliojitokeza ikalazimu magereza yote yenye wafungwa wengi, wapunguze wafungwa wao kupunguzia gereza hilo. Gereza la kilimo Kitengule likawa moja ya gereza chaguliwa, huku likipewa nafasi kubwa ya kupunguza wafungwa wengi zaidi ya mengine sababu ya tetemeko lililopata kupiga miaka ya nyuma lililopelekea mazingira kutokuwa rafiki kwa wafungwa. Walikuwa wanarundikana wengiwengi chumba kimoja tofauti na inavyopaswa.



    Walichaguliwa watu husika, wapatao ishirini, kwa kujali jinsia zote japo wa kike walikuwa wachache. Watano tu. Upendo akiwa mmoja miongoni mwa hao watano. Akiondolewa kwa kigezo kwamba akawe karibu na mji mkubwa ataoweza kupata huduma nyingi za kiafya. Afya yake hawakuijadili, walichoamua ndicho waliona sahihi, kwa kuamini ule muda wa makadirio. Siku ya safari ilivyowadia haikusita kuanza. Tena mapema sana, saa kumi na moja alfajiri. Wakisafiri na basi linalomilikiwa na magereza, lililosheheni uchakavu, kwa kuwa ni la zamani na halipatiwi huduma ya marekebisho ipasavyo. Mwendo ulikuwa wa wastani, si wa taratibu na wala si wa kasi, kikubwa kilichojaliwa ni kufika, hata kama watachukua siku tatu. Ndani ya gari mlitawaliwa ukimya, sababu hawakuwa na ufahamu waendako kukoje. Kama kulitokea mazungumzo basi ni kwa wachache sana ambao walikuwa wanaoneshana jiografia ya maeneo wapitayo yalivyo. Furaha haikukosa kwa baadhi, kufurahia kubadilisha mazingira na wengine walifurahia kusafiri. Maana wengi wao toka walivyoingia gerezani safari ya vyombo vya moto walivisikia tu. Hawakukosekana waliochukizwa. Upendo mmoja wapo. Safari ilikuwa kero kwake, tamanio lake lilikuwa kusafiri kwa ndege na si njia hiyo watumiayo ambayo ilimkera mno, kutokana na matuta na mashimo yaliyopo barabarani japo ilikuwa na lami. Hali ya kudunda dunda, iliyosababishwa na basi ipitapo kwenye matuta ama shimoni, ilifamnya safari aione zaidi ya chungu na kuanza kuugulia maumivu yaliyobadilisha afya yake kabisa. Alianza kulalama, kwa kulalamika maumivu ya tumbo, kiuno na sehemu ndogo ya mgongo. Mwanzo alichukuliwa poa, kwa kupewa pole za hapa na pale na kumuomba ajikaze. Ila hali ilibadilika ghafla, walivyowasili mkoani Mwanza, ikabidi gari ipakiwe pembeni waanze kumshughulikia. Alipatwa na uchungu.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Wafungwa wote wakiume waliteremka wakasalia wa kike pekee na maafisa wa magereza wasindikizaji wa msafara huo ambao ni wakiume na wakike. Hata kama hawakuwahi kufanya shughuli ya ukunga kwa siku hiyo walilazimika kuwa wakunga kuhakikisha wanaokoa maisha ya wote wawili. Mama na mtoto. Walifanya kila jitihada, wengine kwa kukumbuka simulizi walizokuwa wanahadithiana kwenye vigenge vyao na wale wasio na uzoefu kabisa kazi yao kubwa ilikuwa usaidizi. Walilazimika kutekeleza hilo kwa wakati huo japo walishaufikia mji sababu hali ilishazidi kuwa mbaya mno kiasi kwamba wangelichelewa maisha ya wote wawili wangeliyapoteza. Ila isivyo bahati, kwa jitihada zote, walifanikiwa kuokoa maisha ya mmoja pekee. Mtoto! Mama alikwishatangulia mbele ya haki punde tu alivyojifungua. Kwani kiwango cha damu kilichomtoka kilikuwa kingi mno na hawakuweza izuia.



    Baadaye waliomba msaada, kwa raia walivyowataarifu waombewe gari ya wagonjwa na uongozi wa magereza pia. Haikuchukua muda mrefu, msaada ukawasili. Gari ya wagonjwa na maafisa wawili toka magereza, ambao walipatiwa mkasa mzima kisha kuachiwa majukumu kwa niaba ili wao waendelee na safari. Hilo halikuwa tatizo. Uongozi wa gereza la Butimba lilipokea majukumu kisha wale wa Kitengule waliendelea na safari baada ya gari kusafishwa zile damu. Upendo, ambaye kwa sasa alitambulika kwa jina lingine, marehemu. Alipakizwa ndani ya gari la wagonjwa pamoja na mwanaye, kisha safari ya kuelekea hospitali ikaanza. Safari yao iliishia hospitali ya rufaa Bugando, ambako mwili wake ulifanyiwa uchunguzi wa mwisho na kupelekwa chumba maalumu cha kuhifadhia miili ya wafu. Monchwari! Yule wanaye alifanyiwa tiba za hapa na pale kisha akawa chini ya uangalizi wa wale maafisa wa magereza.



    Pindi hayo yanaendelea yakafanyika mawasiliano baina ya uongozi wa gereza la Butimba na lile la Kitengule kuwaeleza kilichojiri na taratibu gani zifuatwe. Makubaliano yalivyopatikana yalitekelezwa tena kwa uharaka sana. Ambapo mwili wa Upendo walipanga kuuzika hapohapo jijini Mwanza wakati huo mtoto akifanyiwa taratibu za kupelekwa kwa ndugu aliowaandika Upendo enzi za uhai katika faili lake. Siku mbili baadaye alizikwa, katika makaburi ya Igoma yaliyopo jijini humo. Mtoto alitolewa hospitalini, akawa chini ya uangalizi wa magereza, wakahusika na huduma zote zitakiwazo kwa mtoto. Kama vile kunyonyeshwa, alikuwa ananyonyeshwa maziwa ya chupa, kliniki na nyingnezo. Siku za baadaye alisafirishwa hadi kwa ndugu aliyeandikwa kwenye faili. Waliandikwa wazazi, hivyo alisafirishwa hadi mkoani Katavi mji wa Mlele. Wazee hao walitaarifiwa habari zote namna ilivyokuwa hadi hapo ilipofikia. Walilia, walifutwa machozi mwishowe waliishia kubaki na maumivu moyoni na kumpokea yule mtoto waliyempatia jina siku za baadaye.

    ****



    Mwanjaa na Madam Cecy hawakutuliana. Kila leo walihangaika kumtafuta Vumilia. Kwa njia ya simu na mitandao mbalimbali ya kijamii katika akaunti zake lakini hawakubahatika kumpata. Kwani, kila walivyojaribu kumpigia simu, alikuwa hapatikani na kwenye mitandao ya kijamii jumbe walizokesha kutuma zilikuwa hazijibiwi. Na wala hazikuonyesha alama yoyote iliyoashiria jumbe zao zimepokelewa. Walivyojaribu kumuulizia kwa watu wanaofahamiana naye jibu wapatiwalo halikuwa la kuridhisha, lilikuwa sawa na yale waliyoambulia wenyewe awali. Jambo lililowasukuma kuomba likizo ya dharura kumfuata ili watimize ombi la rafiki yao, kwani waliona wakikaanalo, watakuwa hawajamtendea haki na mioyo yao haitokaa kwa amani. Walifunga safari hadi Dodoma, ambapo kwa wakati huo lilishakuwa jiji. Wakafikia hotelini kisha siku iliyofuata wakaanza rasmi kutekeleza kilichowapeleka. Kwa kuwa walikuwa na anuani yake ya kazi, wapi anapofanyia, walienda moja kwa moja huko. Kikosi cha FFU jijini hapo. Awali walipokelewa kwa mikwara mingi, toka kwa askari waliopo zamu, ila baada ya kujitambulisha, ndambo zote walizofanyiwa zilikata kisha wakaelekezwa ofisini kwa wakuu wao. Walivyofika huko walijitambulisha kwa mara nyingine. Viongozi waliowakuta nao, OC na kaimu wake, nao walijitambulisha baada ya hapo dhamira ya ujio wao ikawekwa bayana.



    Walihadithia kila kitu, kuanzia mwanzo, namna wawili hao Upendo na Vumilia walivyoingia kwenye mahusiano na hatma ilivyokuwa. Walivyohitimisha, mmoja wa viongozi aliendeleza. Kwa kutoa jibu kuhusu maelezo waliyopatiwa.

    “Aah!...Vumilia kaacha kazi,” alisema OC na kutulia. Akiwatazama kina Mwanjaa namna wapokeavyo kauli hiyo kisha akaendelea.

    “...ni muda mrefu sasa ushapita toka alivyoacha. Japo tulijitahidi kumzuia na kumsihi asichukue uamuzi huo ila tulishindwa, maana mwenyewe alishadhamiria.”

    “Kahamia wapi?” aliuliza Madam Cecy.

    “Kwa taarifa za awali tulizonazo, tuliambiwa kahamia Morogoro. Mji mmoja hivi, ufahamikao Ifakara.”

    “Na vipi kuhusu mawasiliano yake? Maana tumejaribu kumpigia simu mara nyingi sana haipatikani?”

    “Kuhusu hilo sina ufahamu nalo. Labda tujaribu kuwauliza wenziye.”



    Kaimu Kamanda wa Kikosi alitoka nje na kwenda kumuita mmoja wa askari walioko wanacheza mchezo wa Carrom akaongozana naye hadi chumba cha maongezi ambako walikuta ukimya umetawala wakisubiriwa. Walivyowasili na kutulia yalianza upya, kwa yule askari kuulizwa maswali lukuki kuhusu Vumilia. Hasahasa mawasiliano ya Vumilia kwa wakati huo ni yapi.

    “Ninachokumbuka, mara ya mwisho kuwasiliana, aliniomba nifute namba zake zote nilizonazo, kwa madai kwamba anauza simu. Hivyo hatokuwa hewani na hafahamu atakaa kwa muda gani hadi anunue simu mpya,” alisema yule askari alivyopatiwa nafasi ya kujibu.



    Madam Cecy na Mwanjaa waliishia kuduwaa, kwani matarajio yao hayakuwa hayo waliyokutana nayo. Walikuja wakiwa na imani kwamba wanakuja kukamilisha ombi la rafiki yao, ila matokeo hayo yanawafanya waendelee na zoezi la kumtafuta Vumilia ambapo kwa sasa iliwalazimu kutumia ubashiri ama kwenda Ifakara walikoambiwa au wapatikanapo wazazi na ndugu wengine wa Vumilia. Ila sehemu ya uharaka wa kufanikiwa kupata ni kule waliko kwa wingi ndugu wa Vumilia, lakini wao walipishana na dhana hiyo, wakasafiri hadi Ifakara. Sehemu yao ya kwanza, ni kwa mwenyekiti mmoja wa mtaa, walijitambulisha na kueleza nia ya ujio wao. Iliyoambatana na kuacha picha ya mhusika ambayo waliipakua mtandaoni na kuichapa katika moja ya maduka ya uchapaji jijini Dodoma.









    Makazi yao yakawa kwa huyo mwenyekiti, usiku walilala hapo, japo kwa tabu na chakula walikula hapo pia. Muda walioupanga kwa shughuli ya utafutaji walikesha mtaani kumtafuta huku wakitumia picha yake kuwaonesha watu wawaulizao. Walifanya zoezi hilo hadi karibu na siku za mwisho za likizo zao, pasipo hata chembe ya mafanikio ya aina yoyote. Kitendo kilichowakatisha tamaa na kuamua kurejea jijini Dar es salaam huku wakiacha tenda kwa mwenyekiti, endapo atafanikiwa kumuona wapamtaia donge nono. Kurejea jijini hapo haukuwa mwisho wa wao kusitisha zoezi walilonalo. Waliendelea, ila mara chache chache sana kutokana na muda kuwa finyu kwao. Awamu hii walikesha kwenye mawasiliano, kuwasiliana na mwenyekiti na watu mbalimbali waliopo mikoa ya kusini wenye ufahamu na kijiji atokacho Vumilia, Mangaka! Kwa mwenyekiti kazi yao kubwa ilikuwa kuuliza kama kashafanikiwa ama lah! Huku kwa watu wa kusini kazi yao kuuliza pia wale watu wanaofahamu Mangaka kama wanamfahamu Mzee Matatizo ama ndugu yeyote wa mzee huyo. Lakini matokeo yalikuwa bilabila. Juu ya jitihada zote walizoendelea nazo hawakupata dalili ya kuonana na Vumilia.



    Mwishowe walilazimika kupotezea, na kumwachia Mwenyezi Mungu atende miujiza yake. Yale mawasiliano ya mara kwa mara waliachana nayo, walisubiri kuona taarifa kutoka kwa mtu, akiwataarifu kwamba nimewasiliana na Vumilia, ama kaonekana sehemu fulani. Walielekeza nguvu zao kwenye majukumu ya awali, ya kiserikali kwenye idara walizoajiriwa na binafsi zihusuzo maisha yao.



    Sekunde, dakika, saa, siku, majuma na miezi ilikatika. Mwaka na hatimaye miaka, habari ya Vumilia ikasahaulika kabisa masikioni mwao. Hata ufahamu kwamba kuna mtu aitwaye Vumilia aliyewahi kuwa na mahusiano na rafiki yao ulishapotea. Si wote, ulibaki kwa uchache uliojitokeza siku mojamoja ilivyotokea wamemkumbuka Upendo. Ambaye tayari alishakuwa mfu ila wao hawakuwa na taarifa hiyo. Hata jamaa wa Upendo waliokesha kuonana onana kipindi cha nyuma hawakuonana tena, kwani walikuwa hawaendi tena kwao na wala kwenye mizunguko yao hawakubahatika kuonana nao. Ilikuwa jioni moja, yapata saa kumi na moja, jua likificha makali yake yaliyo tawala mchana na kuruhusu upoozi uliojiandaa kupokea kiza, punde Mwanjaa alivyotoka kazini. Alipata chakula, akabadili mavazi na kuondoka kuelekea mjini kubarizi. Mwendo wake ulikuwa taratibu, mithili ya kinyonga tawini, mikogo ikisheheni katika utembeaji wake, asipate kuchafuka. Huku kikubwa kilichochangia utembeaji huo, kichwa kilitawaliwa na mawazo lukuki aliyoshindwa kuyaamua. Hivyo alidiriki kuamini, akitembea namna hiyo anaweza yapatia ufumbuzi. Alivyouacha uga wa kambi yao alisimama pembeni kusubiri usafiri, ambao hakuchukua muda mrefu kumfikia. Bajaji! Akapanda na kumuamuru dereva ampeleke sehemu anayohitaji.



    Safari yake iliishia Kariakoo, ambako alienda kutafuta mahitaji fulani, alivyofanikiwa kupata safari ya kurudi atokako, kambini kwao ilianza. Alielekea kituo cha daladala, akaunga foleni ya kusubiri, kituo kilichukua watu wengi zaidi ya idadi hitajika. Daladala zilivyokuwa zinawasili abiria walikesha kusoma bango lililoandikwa mbele likionyesha gari lielekeako na litokako pia. Wale walioona daladala hiyo inaelekea wanakohitaji walikesha kugombaniana kila mmoja awahi kuingia apate siti, ama asimame sehemu nzuri kama siti zishajaa. Mwanjaa alikuwa kasimama pembezoni kidogo mwa banda lililojengwa maalumu kwa abiria kupumzikia pindi wanasubiri usafiri. Muda wote macho yake yalipepesa huku na kule, kuangaza gari zifikazo, ili atapoiona ile ielekeayo kule anakohitaji basi naye akaungane kwenye pambano la kuparamia. Akiwa katikati ya shughuli hiyo, iliyochangia kwa kiasi kidogo aanze kuhisi kizunguzungu, alishtushwa na mkono uliogusa begani tokea nyuma. Alivyotupa jicho kumuangalia ni nani, alikumbana na sura ya mke wa mjomba yake na Upendo. Mshangao ulitamalaki ghafla, ulioamaanisha kutoamini akionacho. Walikumbatiana, walipoachana walivutana pembeni wakaanza kuteta jambo.

    “Hee! Mwanjaa, za siku nyingi?”

    “Salama. Vipi huko utakako?”

    “Kwema. Umeadimika sana, toka alivyoondoka rafiki yako hujakanyaga kwetu kabisa.”

    “Mihangaiko shangazi. Isitoshe ninyi si mlishamkataa, sasa ningekuja kufanya nini?”

    “Haya tuachane na hayo. Una taarifa zozote zihusuzo juu yake?”

    “Hapana! Sifahamu chochote. Kuna nini?” Mwanjaa aliuliza, fuadi ukichanua tabasamu la kupokea umbeya. Hata habari za kusubiri gari aondoke muda huo akazipotezea. Moyo ukatamani umbeya kwanza kisha safari baadaye.



    Hadithi ikaanza. Tena walisogea pembeni zaidi ili waepukane na rabsha ziendeleazo. Shangazi alimhadithia kilichojiri, habari za kujifungua kwa Upendo na baadaye kupoteza maisha. Taarifa iliyopeleka na kuinua uchungu kwa Mwanjaa. Alishindwa kujikaza, alijikuta anadondosha chozi lililoambatana na kilio cha chinichini baadaye. Alilia, takribani muda wa robo saa, ndipo alipokuja tulia kisha kuongozwa kupanda kwenye usafiri, daladala ilivyowasili. Alivyofika kambini kwao naye aliwahadithia wenziye, wengi walisikitika na kuungana katika kilio. Hata Madam Cecy alivyopatiwa taarifa hakuacha kulia, sababu ya kumpoteza rafiki yao kipenzi ambaye walikesha kushirikiana katika shughuli mbalimbali. Umivu walilopata halikuisha siku moja. Liliendelea kutafuna nyoyo zao kila siku, hadi lilivyokuja kupoa, siku nyingi zilikata.



    Wiki moja baadaye, toka walivyofikiwa na taarifa ile, walichukua mapumziko mafupi ya siku nne, baada ya kusingizia ugonjwa wakasafiri hadi mjini Mlele. Wanakoishi wazazi wa marehemu Upendo. Dhamira ya ujio wao ikiwa ni kuhani pamoja na kumuona mtoto wa Upendo. Walivyowasili walipokelewa vizuri, wakaeleza nia yao, lakini majibu waliyokutana nayo hayakuwa tarajiwa. Walijiona kuwa watu wa nuksi, kwani kila wafanyalo halifanikiwi.



    “Mwanaye katoka miaka mingi sana mara baada ya kuhitimu elimu ya msingi. Kaenda Morogoro kufanya kazi, pia mama yake kazikiwa Mwanza si huku kwetu,” alisema mama yake Upendo.

    “Kwanini kazikiwa huko? Na mwanaye kaenda kufanya kazi gani?”

    “Kwa madai ya magereza alipatwa na tatizo pindi wako safari, walipofika hapo likazidi na ndipo alipoagia maisha. Kwa hiyo kuepuka gharama za kusafirisha safirisha wakaamua kumzika hapohapo. Pia huyo mwanaye sijajua kazi aifanyayo huko aliko, maana mtu mwenyewe hatuliani. Mara hii kesho ile, anabaki kuhangaika tu.”



    Hawakuwa na budi, sababu walichofuata hawakufanikiwa kukipata, walirejea jijini Dar es salaam. Huku wakiambulia kuchukua namba za simu tu, watazoweza kuwasiliana na mtoto wa marehemu Upendo. Ambaye kwa wakati huo alishafikisha miaka kumi na sita. Walivyowasili jijini wakawa wanawasiliana naye siku mojamoja. Walijitambulisha, naye akawatambulisha wapi apatikanako kwa wakati huo. Mkoani Ruvuma, katika mji mmoja ufahamikao Tunduru. Akifanya shughuli ya uuzaji wa vitabu, katika duka kubwa liitwalo Ubunifu.

    “Mama mdogo!”

    “Ndiyo mwanangu,” aliitika Mwanjaa, baada ya kuitwa na mtu wa upande wa pili, aliyekuwa anawasiliana naye kwa njia ya simu ya mkononi. Ambaye ni mtoto wa marehemu Upendo.

    “Mama, siku zote pindi tunawasiliana kuna jambo nilisahau kukuambia.”

    “Lipi tena hilo mwanangu?”

    “Mama, kesho kutwa naenda kuolewa.”

    “Mmh! Acha utani. Jambo la muhimu namna hiyo ushindwe kuniambia kweli? Wenzio siamini.”

    “Kweli mama.”

    “Lakini kwanini unaenda kuolewa mapema hivyo? Na nani anayeenda kukuoa?”

    “Maisha mama yangu. Unadhani nitafanyaje? Ilhali baba simjui, na walezi wangu ndiyo kama uwaonavyo.”

    “Haya, nani anayeenda kukuoa?”

    “Bosi wangu!”

    “Mmh! Mwenzangu? Mara hii?”

    “Ndiyo hivyo mama.”

    “Ni dini gani? Na anaitwaje mwanaume mwenyewe?”

    “Dini yangu. Ni muislam. Nakutumia picha hivi punde katika mtandao wa whatsapp umuone sambamba na jina lake,” alisema mtoto wa marehemu Upendo kisha akakata simu.



    Wala hakupoa, alivyokata tu simu, alifungua data, kisha kuingia katika moja ya faili alizohifadhi picha zake, akachagua picha moja nzuri ya mwanaume aendaye kumuoa. Kijana akaribiaye miaka arobaini na tano, mvi kiasi zikiwa zimenawiri kichwani. Aliipeleka katika mtandao husika, baada ya hapo akatuma.

    “Nina hakika watakufurahia,” alijisemeza baada ya kuona ishara ya tiki mbili zenye rangi ya kijivu zilizoashiria picha ishamfikia mlengwa ila bado hajaiona.







    Wakati huo Mwanjaa alikuwa ndani ya daladala, kaketi sitini akitokea nyumbani kwa nduguze, waishio maeneo ya Mbagala akielekea Ubungo. Gari ilifurika watu, walikuwa wengi mno, kiasi cha kuongeza joto na kuleta shida kwenye upumuaji, kwani kila mtu alivyopumua, pumzi iligonga kwenye mwili wa mtu mwingine. Hii ilikuwa hasahasa kwa watu waliosimama. Muito wa simu ulioashiria jumbe kuingia, ukamshtua Mwanjaa, aliyekuwa yuko bize akiteta jambo na jirani yake kuhusu adha waipatayo katika usafiri jijini hapo. Akasitisha maongezi, na kuhamishia akili yake kwenye jumbe hiyo aweze kumfahamu nani kutuma na ujumbe gani alioandikiwa. Alivyobaini kuwa ni mwanaye, mtoto wa rafiki yake, marehemu Upendo, shauku iliongezeka ya ufunguzi maradufu ya alivyokuwa mwanzo. Aliufungua mtandao husika, whatsapp na kuona jumbe mbili zilizooneka kutumwa naye kwa wakati mmoja.



    Pindi anasogeza kidole, dole gumba. Kwenye jina husika afungue na ajionee jumbe zilizotumwa, ghafla, zogo kali likaibuka garini. Lililomsukuma kila mmoja ahangaike huku na kule kutetea roho yake. Wengi wakiwa na uhitaji wa kuvunja vioo vya dirisha wapate nafasi ya kutoka. Watu wa kwanza kushuhudia hicho kitu kilichowafanya wengi wao wahangaike ni wale waliosimama na wachache walioketi siti za mbele. Walioketi siti za nyuma na kati hawakuona chochote, labda hadi wasimame. Hivyo Mwanjaa, akashawishika kusimama, mara baada ya kuizima simu hata kabla hajasoma zile jumbe. Alivyotupa macho mbele, alishikwa na mshangao, mapigo ya moyo yakaanza mwenda kasi na kijacho chembamba kumtiririka.

    “Mungu wangu!” alijisemeza. Mapigo ya moyo yakizidi ongezeka, huku akijaribu kuungana na watu wengine waliokuwa wanahangaika kujiokoa kwa kurukia nje.



    Kupoteza uelekeo wa gari yao ndicho kitu kilichowashtua wengi na kuwafanya waanze kuhangaika, mara baada ya kumuona dereva karuka punde usukani wa daladala waliyopanda kukatika. Gari iliyumba, na kuwayumbisha abiria pia, ilhali wakiendelea na jitihada zao. Wengine wakitokea mlangoni, wengine dirishani ili-mradi sehemu yoyote aionayo mtu inafaa. Habari ya kumtambua mume zikasahaulika, hapa kujiokoa kwanza, ndipo mengineyo yafuate. Kidogo, mbinu za kijeshi zikamsaidia, baada ya kuyumba huku na kule, mwishowe akapata mwanya uliomwezesha kukamata sehemu zianzianzo dirisha kisha akakanyaga siti na kuruka. Lakini bahati haikuwa upande wake. Kwani miyumbo kadhaa tu, gari ikaachia, na kuangukia kulekule alikorukia. Anatua tu, ardhini, gari nayo ikatua nyuma yake. Ikampiga, na kumbana sehemu kubwa ya mwili, kuanzia katikati ya mgongo hadi miguuni.

    ****



    Maisha yalienda vyema kwa Vumilia na familia yake. Kwani mtoto alizidi kukua na kuimarika afya kila uchao. Siku za baadaye wakaanzisha biashara, ya uuzaji wa nguo za jinsia zote za duka pamoja na viatu. Vumilia akawa msimamizi wa hiyo shughuli na shughuli za nyumbani pia. Kwa siku ambazo hawana mfanyakazi. Wakiwa naye, ama mtoto wao anapokuwepo ambaye walishamwanzishia masomo Morogoro mjini, Vumilia akawa anahusika na shughuli za dukani pekee. Hakika furaha ya maisha hawakuikosa. Kwani, shida ndogondogo kwao hazikutamba. Walizitatua kwa uharaka, hata kubwa pia, walizitatua kwa nafasi yao iliyosalia walishirikisha watu wengine.



    Ikawa hivyo, hadi walivyoukaribia uzee na kuongeza mwana mwingine. Pia biashara yao ilizidi kukua na kuitanua katika miji mingine, ila hawakufungua zinazowiana. Walifungua zihusuzo bidhaa nyingine. Walifungua tawi la biashara yao mjini Tunduru. Wakamwajiri msichana mmoja aitwaye Lalmaa. Ambaye alianza kufanya kazi hapohapo Ifakara, baadaye wakamhamishia Tunduru. Juu ya furaha iliyotawala kwenye familia, huzuni haikukosa. Ambayo ilisababishwa na kitu kimoja tu toka kwa Zamzam. Alikuwa anamshinikiza mumewe aowe mwanamke mwingine. Kwa kisingizio kwamba yeye hatimizi mahitaji yote kama mke kutokana na tatizo alilonalo. Hasa shughuli za nyumbani. Kila kukicha akawa anamlazimisha Vumilia afanye hivyo, lakini alipinga. Apingapo, baadhi ya siku akawa ananyimwa unyumba, jambo lililomsukuma siku za baadaye akubaliane nalo.



    Alivyokubali mkewe alifurahi sana. Tena katika kuonesha furaha yake akampendekezea mwanamke, akikubaliana naye, amuoe. Ambaye ni Lalmaa. Vumilia akautafakari ushauri wake kwa siku kadhaa. Huku akimtathmini na Lalmaa pia, wakati huohuo Zamzam akionesha hisia zake waziwazi kwa Lalmaa za kumtaka binti huyo awe mke mwenza kwa kumpatia maneno yenye ushawishi. Alitongoza kwa niaba.

    “Lalmaa, kwanini huamini maneno nikuambiayo?” aliuliza Zamzam, kwa shida sana, kutokana na tatizo la uongeaji alilonalo baada ya sehemu ndogo ya ulimi kukatwa, jioni moja alivyoketi na Lalmaa sebuleni baada ya kufunga mahesabu.

    “Mama! Acha masihara. Inawezekana vipi kuolewa na bosi wangu?”

    “Mimi ndiye mwenye uhitaji mume wangu awe na mke mwingine, ambaye ni wewe. Fanya tuishi pamoja hapahapa hadi mwisho wa maisha yetu. Hebu angalia, kwa kuvuta kumbukumbu nyuma umkutapo anafanya kazi ambazo zilipaswa kufanywa nami. Naomba unionee huruma katika hili.”

    “Mmmh! Yaani unanikazia hivyo kama kweli? Ama lengo lako uipime imani yangu, kwamba nina hisia gani na mumeo?”

    “Hapana! Namaanisha niongeacho.”

    “Mama, kama hutaki mimi niendelee kuwepo hapa, heri niondoke zangu mapema kabla mambo hayajaharibika zaidi huko mbeleni,” alisema Lalmaa, kisha kuinuka pale alipoketi akaenda chumbani kwake.



    Zamzam naye aliongoza, hukohuko ila hakufanikiwa kuingia chumbani, kwani Lalmaa alivyoingia alifunga mlango kwa ndani. Haikuwa shida, hapohapo aliposimama akaanza endeleza maongezi kwa kile kilichopo moyoni. Lalmaa akawa anasikia, ila hakutaka kutoa jibu lolote, zaidi ya kuwa kimya akiipa akili iwaze mambo mengine. Hasa ya kuacha kazi na kuondoka nyumbani hapo. Asubuhi kulivyopambazuka, Lalmaa alikawia kuamka. Tofauti na siku zote, kilichomchelewesha, jana alichelea kulala kwa sababu ya kupanga nguo zake tayari kwa kuondoka. Moyo uliruhusu hitajio la kutowepo tena mahala hapo. Vumilia ndiye alimfuata kumwamsha, walisabahiana kisha ukapatikana mwanya wa maongezi kueleza tatizo lililochangia uchelewaji.

    “Bosi, mimi nimeamua niache kazi,” alisema Lalmaa, macho akiwa kayatupa chini kwa haya.

    “He! Mbona ghafla hivyo? Nini tatizo?” aliuliza Vumilia, ila ghafla akapatwa na kumbukizi baina yake na mkewe usiku wa jana.

    “Mume wangu naomba uniwie radhi kama nitakuwa nimekukwaza. Hisia zilinizidi nguvu na hatimaye nikadiriki kumuambia Lalmaa ukweli, kwamba nahitaji awe mke mwenza, ila anaonekana kuchukia kwa kuhisi nampima,” aliikumbuka kauli hiyo.



    Alivyotupa jicho kumwangalia Lalmaa akamuona anajiuma uma kwa kubabaisha macho yake huku na kule.

    “Sikia Lalmaa,” Vumilia alinena. Kauli iliyomuinua Lalmaa na kuwafanya wagongane macho ana kwa ana.

    “Ulichoambiwa, kina usahihi. Hajafanya hivyo kwa ajili ya kukupima. Aliniomba nikueleze, ila baada ya kuniona sitekelezi ombi lake na siku zinazidi kusonga akaamua afunguke mwenyewe.”

    “Ina maana kweli unahitaji niwe mkeo?” aliuliza Lalmaa, macho pima kwa Vumilia akimtathmini.



    Tathmini yake ilikuwa inafikiri umri wake na huyo amuambiaye anahitaji amuoe, pia kuhusu usichana wake. Maana hajawahi ruhusu usichana wake kuingiliwa.

    “Nakupa muda, fikiri kisha utanipitia mrejesho,” alisema Vumilia na kuondoka.

    Suala la kuondoka akaachana nalo. Sasa akaanza fikiria jumbe aliyopatiwa. Ambayo alitumia muda wa wiki mbili pekee kisha kutoa jibu. Aliridhia!



    Mahusiano yakaanza, tena kwa kasi ya ajabu. Lalmaa akatolewa usichana wake, japo kwa shida siku za mwanzoni lakini siku za mbeleni uzoefu ukapatikana ulio poteza usumbufu aliokuwa anautoa siku za nyuma. Kila kukicha akawa anaongeza ujuzi katika ulimwengu huo, kwa kusoma makala gazetini na kuangalia vipindi runingani vihusiavyo mahusiano ya kimapenzi. Miezi kadhaa baadaye afya yake ikaanza badilika. Akawa mtu wa kutapika ovyo, kupenda vitu vichachu na kichefuchefu kila wakati. Alipoenda kupima afya, akabainika kuwa mjamzito. Tukio lililofurahiwa na watu wote nyumbani hapo.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa ni wakati mahususi wa sisi wawili kuwa mwili mmoja,” alisema Vumilia. Huku akichezea chezea tumbo la Lalmaa.



    Katika kufanikisha hilo walisafiri hadi kwa wazazi wa Lalmaa. Mjini Mlele, mkoani Katavi. Kikafanyika kikao kidogo, ambacho Vumilia alipata nafasi ya kujitambulisha na kutambulishwa pia. Akiwa kaambatana na mshenga wake. Vilevile alitoa mahari, na kupangwa siku ya tukio husika la ndoa. Ambalo lilipangwa kufanyika mwezi mmoja mbele toka siku hiyo.

    MWISHO


0 comments:

Post a Comment

Blog