Search This Blog

Thursday, November 24, 2022

NILIVUNJA NDOA ZANGU 3 KULIPIZA KISASI - 4

 

     

     

     

    Simulizi : Nilivunja Ndoa Zangu 3 Kulipiza Kisasi

    Sehemu Ya Nne (4)

     

     

    SEHEMU YA SABA.

    Ilikuwa siku ya ijumaa, nilikuwa nimejikali nyumbani tu, siku hiyo nilikuwa nimeomba ruhusa ya kumpeleka mtoto shule kwa ajili ya sports day, na ilikuwa ni lazima kuhuwepo, hivyo niliongea na muajiri wangu na akanipatia likizo ya siku sita kama nilivyoomba. Kwani nisingeweza kupewa ruhusa ya siku moja kutokana na taratibu za kazi, akanishauri ni bora nichukue likizo ya siku saba kama kuna ambalo nataka kulifanya nilifanye kabisa.

    Zaidi ya kuwepo shuleni kwa siku moja hiyo kwa sports day sikuwa na jambo lingine la kufanya. Sijui ni furaha ya kulipiza kisasi ama ni nini, Nilipendeza sana na kunawiri mno, uzito uliongezeka, lakini kutokana na umbo langu bado nilionekana nimependeza sana na kunawiri, kila aliyeniona alinisifia sana na kuniambia nimependeza mno. Hii ilinifanya niendeleee kupata moyo, wasijue yanayonisibu.

    Ninazo siku 6 za kukaa tu nyumbani, hapana haiwezekani, nitasafari na Majid, kwani si kanihitaji mwenyewe, nitasafiri.

    Je nitaombaje ruhusa? Lazima nitafute ugomvi, Jones nikimuomba ruhusa hivi hivi hataniruhusu, hawezi, hawezi, ananilinda sana sasa hivi, lazima nitafute ugomvi.

    Ahaa, naweza kutafuta ugomvi, naweza hili halinishindi, naweza.

    Niliporudi kutoka shuleni, Jones alikuja na kunikuta nimekaa chumbani, alikuwa na furaha sana. Ama Kweli ashukuriwe Mungu ambaye mwanadamu huwezi kuona moyo wa mtu anavyokuwazia, tungechinjana sana.

    Aliingia ndani na kunikuta nimejibwaga kitandani, alikuwa na furaha sana,

    Aliniuliza habari za mtoto shule, na nilimueleza ni njema sana,

    Akaingia bafuni kuoga na akatoka, bado nilikuwa nimejilaza kitandani, kila nilipokuwa kimya nilikuwa nikitunga sheria, Kimya change siku zote kilikuwa sio cha kutulia tu hivi hivi la hasha, ni kimya cha kutunga shiria nitalipizaje kisasi ili wahusika waumie haswa.

    Jones alitoka na alipotoka ikawa kama alijua namtaka uchokozi. Cha kwanza aliniuliza mbona kama umechoka? Ama umekunywa pombe zako tena Charlote?

    Heeeee, alijuta,, nasema ungekuta nalumbana naye ungemhurumia.

    Nilikaa, nilikuwa nimefunga khanga ya kifuani tu na kwani nilihitaji kupigwa na upepo. Kwa umbo langu lilivyo kubwa nilisimama na kila kiungo cha mwili wangu kilitetemeka kwa namna nilivyokuwa naongea, sio makali, mapaja , wala mikono na matiti,, nilisimama na kushika kiuno.

    Nilimtazama na kumwambia,,, Jones, naona umenichoka,,hivi kwa nini huniamini? Nakuuliza hivi kwa nini huniamini? Kwa nini unapenda kuniambia sana kuhusu pombe? Si tumekubaliana ni ache na leo ni karibu wiki ya pili sinywi? Hivi mbona unapenda maneno wewe mwanaume? Khaaaa,,, nilikuwa nimeshika chupa ya perfume nikaipigiza chini, tena ile perfume aliyoninunulia.

    Jones alishikwa na butwaaaa. Akanishika mikono na kusema, Charlote,, sipaswi kukuliza mama? Sipaswi mke wangu kukuuliza lolote? Ni makosa? Aliongea kwa upole sana,, niliitoa mikono yake kwangu kwa kuirusha ili iiachane,,

    Kisha nikamtazama na kumuuliza,, hivi nikikuuliza Bado tu hujaachana na Husna utajiskiaje?

    Jones, alisema basi mama, basi mke wangu yaishe,, yaishe…

    Nilianza kulia na kulalamika ndoa gani hii ambayo haina furaha wala amani, ndoa gani hii jamani? Nililia sana na huwa nina machozi ya karibu sana.

    Lakini nilikumbuka kwamba kinachoniliza ni uchungu wa Jones kuwa na mahusiano na Husna, yani jambo hili liliumiza sana moyo wangu na kuwa na Donda kuu lisilopona. Ndicho kiliniliza, nilimpenda sana jones, sikutaka kusikia habari hizi kabisa, na kusamehe nilishindwa, isipokuwa ahueni nilikuwa naipata kwa mimi kulipiza kisasi, na ni ahueni ya kuniliwaza kwa muda tu, lakini sio ya kuniliwaza kwa moja kwa moja.

    Jones alinifuata na kuniambia mke wangu samahani, samahani Charlote mke wangu am sorry mami,, sikujua nimekuumiza samahani, yaishe.

    Nilikuwa nalia sana, kweli hakukuwa na pombe kabisa ndani kwani nilishaacha kabisa kunywa, kwa sababu niliona najiumiza maini yangu. Kwa namna nilivyokuwa nakunywa nyingi bila kipimo. Nikaogopa kuwa abused na alcohol.

    Ilifika saa mbili usiku bado tunalumbana, Jones aliniomba sana msamaha, nikawa siongei tena ila nalia tu.

    Jamani,, ni kukuuliza tu ama kuna jengine charlotte? Mbona un hasira hivi? Huwezi kusamehe na kuachilia mke wangu?

    Nilimtazama na kumwambia sio kirahisi hivi, Je wewe ukigundua nina mahusiano nje ya ndoa utajisikiaje? Nijibu nakuuliza utanisamehe?

    Jones alisema ndio nitakusamehe. , nitakusamehe charlotte.

    Nikamwambia, basi subiri siku niwe naye alafu nikuombe msamaha unisamehe.. mfyuuuu nikafyonza na kuondoka kuelekea chumba cha watoto ambacho hakitumini ila hutumika kwa waageni tu na kujifungia humo.

    Nilifyonza kwani ninajua waname wengi ambao hawawezi na hawakuwasamehe wake zao mara baada ya kusikia, kuhisi ama kuiona wana mahusiano na wanaume wengine, hivyo nilijua kusamehe kwa mwanaume ni ngumu sana.

    Nilikaa chumbani huko mpaka nikalala, nikiwa nimejifungia mlango. Jones alikuwa anajuta kwa nini alifanya mahusiano na Husna, ndoa yake sasa alianza kuiona achungu. Asijue mkewe nina agenda ya kulipiza kisasi na karibu sana mission yangu itatimia.

    Aligonga sana, badae mida ya saa saba usiku nilifungua na kuelekea chumbani, nilimkuta amekaa anasoma kitabu, ni mpenzi wa kusoma, hakuwa na usingizi.

    Aliniambia Charlote unanitesa sana, naumia sana juu yako.

    Nilimwambia … Jones, maumivu unayoyapata ni moja ya nane na yamumivu niliyo nayo mimi kuhusu wewe na Husna, na sijui hili donda litaponaje, kila nikijaribu kuliponya inakataa.

    Jones alinitazama na kuniambia,, kwa hivyo unataka kuniambia hukunisamehe?

    Kwa sauti kabisa nilijibu, NDIO NIMESHINDWA KUKUSAMEHE, NIMESHINDWA.

    Jones alifunga kitabu chake na kunitazama tena, Aliniambia Charlote niambie nifanye nini ili unisamehe juu yangu na kosa nililokukosea naomba uniambie nifanye nini/

    Nilimtazama na kumwambia,,, Iko siku na mimi nitakukosea pengine unaweza kushindwa kunisamehe, na itakuwa ni sehemu yaw ewe kupima na kujua je msamaha ni kitu RAHISI AMA KIGUMU???

    Unasemahe Charlote? Umepanga kunilipizia kisasi? Unataka kunilipizia kisasi?

    Nilimtazana na kumwambia umesema wewe ila ni lazima ukosewe ili ujue msamaha ni jambo rahisi ama gumu.

    Sina ninaloweza kukueleza zaidi, nilimaliza na kupanda kitandani na kulala.

    Jones hakuwa kashiba alikuwa na njaa. Alienda jikoni na nilimskia akiwasha microwave na kama anayepasha kitu.

    Alikuja chumbani na sahani na kuniambia, Charlote, hujala na mimi sijala usiku huu, tafadhali amka tule.

    Nilimhurumia sana Jones, ni mwanaume ninayempenda sana, lakini kwa nini KISASI kimenikali kooni? Kwa nini?

    Niliamka huku machozi yakinichuruzika. Nilimambai Jones kula, kula sitakula. Nilitoka chumbani na kwenda kukaa sebuleni.

    Nilitafakari mambo mengi sana muda ule, najiuliza hivi mwisho wa familia yangu ni nini?

    Mwisho wa ndoa yangu ni nini? Mbona nimejirahisi sana? Kwa nini lakini nimekuwa na mahusiano na Mzee Zuberi kwa nini? Na sasa nataka kuwa na Majidi kwa nini? MOyo wangu uliniuma sana,

    Nililia sana, wanangu je,, mume wangu je? Wazazi wangu je?

    Aghraaaaaa… niliendelea kuulia sana, Jones alikuja na kukaa kochi la pembeni, kisha wote tulipitiwa na usingizi mpaka ashb.

    Asbh huwa Jones huenda kazini na kufanya kazi nusu siku.

    Alipokuwa anaondoka nilimwambia, Jones nina likizo ya siku 6. Nahitaji kupumzika, nahitaji kwenda mahali kupumzika,

    Jones alinitazama na kuniambia ni haraka sana, unaenda wapi? Nilimwambia najua mwenyewe nitakapoenda mahali ambapo nitatuliza kichwa na akili yangu, najua itanisaidia.

    Jones aliniambia hapana hutaenda,

    Niliwambia je wewe nilikukataza kuwa na Husna? Nilikukataza?

    Jones alitingisha kichwa na kusema , Charlote naomba kosa nililofanya isiwe sababu ya kunikosesha amani na furaha kwenye maisha yangu, nimeshakuomba msamaha sana, nimejuta sana lakini huoni.

    Fanya utakavyo, na kama unataka ndoa hii ife na ife, nimechoka… siwezi kuwa mtumwa wa ndoa kisa kosa.

    Aliongea kwa hasira na kufoka sana.

    Nilimwambia ahaaa. Kwa hivyo unaona ni sawa u livyofanya mpaka unasema kama ndoa kufa na ife eee, okay.

    Niliingia ndani, Alipark gari na kuja ndani,

    Alinishika kwa nguvu mkono kwa nyuma na kuniambia unataka nini wewe mwanamke? Unataka nini?

    Nilianza kulia tena. Kisha alipigiwa simu ya ofcn akiambiwa anahitajika haraka sana.

    Aliondoka na kuniacha peke yangu.

    Nilianza kufungasha kibegi change cha safari. Na kisha baadae nilitoka na kumuaga dada kwamba nitarudi baada ya sikuu tano.

    Dada aliniaga na nikawabusu wanangu na kutoka.

    Nilichukua taxi mpaka hotel Fulani ambayondiyotulikutana na Majid mara ya kwanza.

    Nilipofika pale nilimpigia simu majidi na kumueleza kwamba ninahitaji kuonana naye.

    Kwanza alipenda kuniutii kwani alijua ni biashara, lakini pia alinitii kwa vile alinihitaji kimapenzi. Hangekuwa na ujanja wa kukataa kuja, hili nililitambua.

    Nilikua nimevalia blauzi nzuri na jeans ambayo ilishika mwili wangu vyema na kuonyesha umbo langu lilivyokaa.

    Nikiwa pale hoteli kabla majid hajafika tayari nilishasalimiwa na wanaume zaidi ya watatu wakitaka kuiongea na mimi kuhusu mapenzi. Niliwaona na kujua lengo lao.

    Lakini sikuwa kwa ajili ya hayo, ila kulipiza kisasi.

    Baada ya dakika 45, Majid alikuwa ameshawasili, Aliniona nikiwa nimevimba macho yakiwa mekundu. Na akaniulizakulikoni? Alipomaliza tu kuniuliza machozi yalinidondoka tena, nikamwambia tumepishana kauli na mume wangu, akaniambia pole.

    Huyu mwanaume ambaye haoni na kujua thamani yako anawezaje kukuudhi kiasi hiki? Niliendelea kulia, kisha nikamueleza nimeamua kutoka kwa siku 6 kwenda kutulia mahali. Ndo maana nimekuja kukuuliza kama una nafasi kutokana na ombi lako ili tuwe pamoja.

    Majid hakuamini, aliniambia sawa kabisa, sawa, Sasa naomba siku moja ya leo tu, na kesho jioni tusafiri na ndege ya saa tisa kuelekea Zanzibar ama unaonajee?

    Nilimueleza ni sawa.

    Hivyo akanilipia hotel night moja na kuniambia kesho saa tisa tutasafiri pamoja.

    Tulikaa pamoja muda wote huo, kuanzia saa sita mchana mpaka saa kumi na mbili jioni, huku tukizungumza, kula na kunywa, na akinisifia sana.

    Kilichonishangaza simu zake ziliuwa on lakini husna hakuwa akiongea naye wala kuwasiliana naye, hali kazalika na mimi pia sikuwa nawasiliana na Jones, japo mimi nilizima simu zangu.

    Niligundua wanawake tuna madhaifu katika mawasiliano, unawezaje kutowasiliana na mchumba wako ama mume mtarajiwa muda wote huo?

    Baadaye mida ya saa kumi na mbihli na robo aliniaga na kunieleza tukutane airport saa saba kwa ajili ya ndege ya saa tisa kwa safari ya Zanzibar.



    ***********************************************************************************************



    SEHEMU YA NANE:



    Simu zangu nilikuwa nimezima zote, hakuna ambayo ilikuwa iko available. Nilizima makusudi, sikutaka kusumbuliwa, nilijua tu Jones atakaponitafuta akinikosa ataongea na wadhamini wetu wa ndoa, kwani ndivyo tulikubaliana kwamba endapo kutakuwa na tatizo kabla ya kushrikisha wazazi ni lazima tuongee na wadhamini kwanza endapo tatizo litakuwa kubwa sana.

    Hivyo haraka nilitoka na kwenda kibanda cha simu, ambapo nilimpigia mdhamini wa kike kumueleza situation nzima. Nilimueleza kwamba nimtoka nyumbani kutokana na matatizo, hivyo nimeamua kupumzika na niko salama, na nitarudi nyumbani baada ya wiki.

    Mdhamini alipoendelea kuhoji na kunishauri kwa nini nimefanya hivyo nilimueleza kwamba nitakaporudi nitaeleza tatizo.

    Hata hivyo alinieleza kwamba Jones alishazungumza na mumewe na kumueleza kwamba tumekorofishana na kumueleza kisa kizima , sikutaka kuongea sana na mdhamini wa kike kwani sikutaka kupoteza mood yangu, lakini nilijua kumpa nafasi ya kuongea zaidi anaweza kunishauri jambo na nikajikuta nimeghairi ninachotaka kukifanya. Hiyo nilimkwepa.

    Sikia,,, niko salama, nitarudi nyumbani in 6 days, angalia watoto. Kwaheri.

    Nilimkatia simu na niliondoka, na hata angepiga tena ni lazima angeambiwa mteja ameshaondokana hatujui alipoeleokea kwani hapa ni kibanda cha simu tu.

    Nilifika hotelini, sikutaka kujishughulisha na lolote, zaidi ya kula, na kulala tu basi.

    Nilikula nikalala, na wala sikutumia pombe kwani nilijua Majidi sio mtumiaji wa pombe na ningemkwaza endapo asbh ningeamka na hangover.

    Usiku haukuwa mzuri sana, kwani nilifikiria familia yangu sana.

    Lakini mara nilipowaza niko kwenye kisasi usingizi ulikuwa mzuri na kujikuta Napata mbinu mpya kila mara ninapotafakari.

    Nilishangaa ni saa tatu na roho asbh. Dah,, nimechelewa sana kuamka. Nilianza kujiandaa, nilishuka chini kwa kifungua kinywa, nilikunywa na kushiba. Kisha nilipigiwa simu nikiwa chumbani na kuambiwa kuna mtu anataka kuzungumza na wewe. Nilijua fika ni Majidi na si mtu mwinigne yeyote Yule.

    Ni kweli ni Majid.

    Charlote,,, aliita… yes.. niliitika.

    Ninatuma mtu aje akupeleke airport… mh.. niliguna.

    Mbona unaguna? Nilishangaa kwa nini anatuma mtu.. nilimuuliza huyo unayemtuma ni salama?

    Aliniambai ni swaiba wangu hana shaka. Anakuja hapo Omary kukupeleka airport. Usijali.

    Niliitika sawa. Kisha baada ya muda mchache sana alikuja kijana na kuuliza.. aliniulizia, kisha nikaitwa kwani nilikuwa room.

    Nilishuka na begi langu, na kumkuta kijana reception akinisubiri.

    Habari dada,, bila shaka wewe ni Charlote… ndio niliitika.

    Basi nimeambiwa nikupeleke airport… asante nilijibu.

    Safari ya airport iliianza. Nilifika na kumsubiri Majidi afike.

    Baada ya muda mchache sana, majidi aliwasili. Nilimuona nikaburudika, nilisika faraja.

    Moyoni niliwaza kumkomesha, na kupanga kufanya kila kituto cha kimapenzi ili kumlobesha,,, nilitaka kumfanya achachawe haswa, na niache chapa ya penzi langu kwake.

    Ki umri tulikuwa tunalingana, lakini bado alionekana mdogo kwangu kutokana na nilivyojazia .

    Alionekana kuridhika na mimi.

    Nilijua tunaenda Zanzibar, hivyo nguo zote nilizobeba zilikuwa ni nguo zinazofaa kutumika sehemu za pwani, niliamua kumkomesha Majidi, asijue lengo langu ni nini.

    Muda wa kusafiri uliwadia. Tulisafiri salama, rubani wa ndege aliendesha ndege salama kabisa, na ndani ya dakika 30 tayari ndege ilikuwa imeshatua na tulikwua tukishuka.

    Mh,, Majid alikuwa akinibana sana, alinisogelea karibu sana, na kuniambai usiogope Charlote,, mh.. kuna wakati nilikuwa naogopa. Lakini nikasema nani ananiona huku Zanzibar, nani ananiona?

    Hakuna ambaye ananifahamu, na hata angenifahamu maisha yangu yanamhusu nini?

    Mimi peke yangu ndiye nilikuwa najipa moyo kwani sikuwa na wa kuweza kumshirikisha jambo na azma yangu.

    Tunaenda stone town,,,, Mkwezi hotel…. Majid alimpa maelezo dereva taxi.

    Haoo, ndani ya dak 10 tulikuwa ndani ya hotel ya mkwezi, hotel ya kifahari, nzuri, na ilikuwa na wazungu tu. Tuliingia kwenye room yetu, na moja kwa moja Majid alinikumbatia na kuniambia, Charlote nashukuru sana, kwa muda na nafasi hii ambayo umenipatia, umeniheshimu sana na sitakuangusha.

    Nilimwambia wala usijali, nashukuru pia kwa nafasi hii ambayo umejitolea kwangu, ni nafasi yap ekeee kwa bwana harusi mtarajiwa kuamua kutoka na mimi. Hii kwangu na hesabu ni heshima ya pekeee.

    Majid alitabasamu kisha akasema ama kwa hakika Charlote umeniteka moyo wangu na fahamu zangu. Mpaka sioni thamani ya ndoa dah?natamani ungekuwa hujaolewa ungenisababishia nifanye kituko cha duniani.

    Wote tulicheka, lakini alionekana mwenye furaha sana, sasa sijui ni kwa ajli yangu tu ama kwa ajili ya jambo gani.

    Baada ya kama muda wa nusu saa aliniambia Husna anapiga simu… nilinyamaza kimya,, na kumuacha azungumze na Husna.

    Alitumia tu dakika chache sana ambazo hazikuzidi 3. Na alikata simu na kumtakia usiku mwema.

    Dah.. nilishangaa inakuwaje…. Mume mmtarajiwa yuko safarini alafu ulale salama saa mbili na robo???

    Nilijua ndiyo maisha yao.

    Tulioga na akaniambia kwamba anataka kunitoa niutazama mji wa stone town usiku nione unavyofanania.

    Tulijiandaa na kwenda kutembea mjini usiku huo. Mji wa Zanzibar ulikuwa unavutia sana, mzuri sana, na wenye kupendeza. Tulitembea mpaka saa sita, tulipitia soko la zanzibari ambalo ni maarufu sana Forodhani, na nilikula chakula ambacho sikuwahi kukila hapo mwanzo. Mbatata za urojo,, ama kweli kilikuwa kitamu.

    Baada ya hapo tulirudi hotelini. Nilijua nitakuwa na kazi nzito usiku huo, hivyo nilikuwa nimejiandaa bara bara.

    Asbh tuliamka, na aliniaga na kuniambia anaelekea bandarini kwa ajili ya kucheki mizigo yake. Aliniacha hotelini nikiwa nimekaa tu chumbani. Baada ya muda mchache alikuja na kuniambia.. dah mwanamke una kismart sana wewe. Contena zangu zimefika salama salmin, na sio kawaida kuja siku moja na kukuta mambo sawia mara zote ninakaa zaidi ya siku tatu nakuendelea ila leo dah, niko na mwanamke mwenye ngekewa.. mambo swari.

    Jiandae tukapate chakula cha mchana mamiii.

    Nilijiandaa na kutoka kwa ajili ya chakula cha mchana.

    Tulipata lunch nzuri sana, kisha baada ya hapo tulitoka na kuelekea sehemu za kuutazama mji wa Zanzibar ambazo ni za makumbusho. Tulizunguka mji huo haswa , na baada ya hapo tulienda bandarini kuangalia contena zake ambazo zilikuwa zimewasili, kisha kukagua baadhi ya mizigo yake kuona kama imefika yote salama.

    Ilikuwa ni zoezi zito kidogo, lakini tulimaliza na aliita vijana ambao walimsaidia pia kuhesabu baadhi ya mizigo ambayo alikuwa akiiacha Zanzibar na mingine ya kuelekea dar.

    Tulitoka hapo tukiwa tumechoka wote, kwani hata na mimi nilimsaidia kuhesabu baadhi ya bidhaa.

    Siku zote tulizokaa Zanzibar zilikuwa nzuri sana, tulifurahiana wote wawili, ungetuona wala usingefikiri ni mtu na kimada, ila moja kwa moja ungejua ni mtu na mke wake tena wanaopendana sana. Majid alinipenda sana.

    Safari ya kurudi dar iliwadia, dah, moyo wangu ulianza kuniuma naenda kukutana na kero zngine, sikupenda kabisa mimi kuondoka Zanzibar mji wa maraha.

    Saa nne na nusu nilikuwa nimeshafika dar, moja kwa moja nilielekea nyumbani, nilfika nyumbani na kumkuta dada na watoto hawapo. Na funguo huwa kama nyumba imefungwa tunazichukua kwa jirani, nilienda kwa jirani na kuchukua funguo. Nilifungua nyumba, na mlangoni nilikuta ujumbe kwenye karatasi.

    NAOMBA USIINGIE NDANI KWANGU, RUDI ULIPOTOKA…. Nilicheka sana.

    Kisha na mimi nikachukua kalamu na karatasi na kuandika… UJUMBE NIMEUKUTA, SAWA NARUDI NILIKOTOKA TAKE CARE.

    Sijui ni kiburi gani nilikuwa nacho, sijui ni roho gani iliniingia. Niliingia na kuchukua nguo za kunitosha kama begi mbili hivi kwani niliweka na pochi na viatu kwa ajili ya kazini.

    Kisha nikafungu nyumba na kuondoka. Na hapo niliwasha simu zangu.

    Nilijiuliza ni hoteli gani ya bei rahisi? Nilipata na kulekea hotelini hapo ambapo chumba ni shilingi 35000 kwa siku. Nilimpigia mzee Zuberi simu kumsalimia na kumueleza nimerudi salama safari yangu, kwani nilimuaga na kumueleza niko nje kikazi. Na alinitumia pesa za safari. Kisha nikamueleza pia kwamba nimerudi salama isipokuwa mume wangu kanifukuza kwa vile ya wivu. Alinihurumia sana na kuniambia nisijali, kama nina tatizo nimueleze. Nilimueleza niko hotelini kwa sasa mpaka hapo nitakapomjulisha kitakachoendelea.

    Alinihurumia sana na kuniambia ninyi bado ni watoto hivyo kuonena wivu ni lazima.

    Nilijilaza hotelini wala nikiwa sijali, na niliamua kumpigia simu Majid kwa simu ya hotelini kumueleza kilichojiri.

    Haloo…. Aliitika,, niliongea kwa upole,,, uko mahali salama tunaweza kuongea ni mimi shalooo… mwenyewe aliniita baby shalo.

    Aliniambia ndio kuna tatizo? Kama aliyeshtuka. Ndio kuna tatizo,,,, ila sio kubwa,,

    Enhe… niambie nini shida? Dah.. kama aliogopa kidogo.. nilimueleza kwamba nimefika nyumbani na kukuta ujumbe kwamba nirudi nilikotoka,, hivyo nimeamua kuchukua hotel.

    Majid alisema sikia shalo, usiogope tuko pamoja, usiogope kabisa,,, wewe tulia hapo, kisha utanijulisha kitakachoendelea, kama ni pesa ya hotel nitalipa,, ila usipanick wala kusema lolote, sawa???

    Nilimwambia sawa kisha nikashanga imekuwaje hajali? Ni anavunga ama?

    Baada ya lisaa limoja niona Jones akipiga simu,, kwanza niliitazama sana simu, kisha ikakata,, nikasubiri ipigwe tena.

    Akapiga tena ikakata, nikasubiri apige tena.

    Akapiga tena nikapokea.. haloo….. Akapokea haloo…

    Hivi charlotte ni maisha gani haya? Nikamuuliza yapi? Wewe si umesema nirudi nilikotoka nimerudi.

    Mh.. akaguna akaniambia uko wapi? Nikamwambia nilikotoka. Kisha nikakata simu na kuzima kabisa.

    Ninafikiri alihangaika sana kunitafuta, nilikuwa sina la kumueleza kwani nilijua ana hasira sana, hivyo sikutaka hata tukutane tuongee maana tungepigana mpaka basi.

    Asbh nilijiandaa na kuelekea kazini. Nilipofika tu kazini huyu hapa, namuona Jones na wadhamini wa ndoa wako pamoja.

    Niliwasalimia,kisha wakataka kuzungumza na mimi, niliwaeleza naingia kazini kwanza, pengine wapange tuongee saa ngapi. Wadhamini hawakuamini, licha ya Jones.

    NIliwapiga nikaingia kazini na kufanya kazi zangu. Lunch time jones alipiga sikupokea, Jioni saa kumi na moja wakati natoka , nilitoka na hakukuwa na mtu, nilichukua taxi na kuelekea hotelini kwangu. Nilipofika tu, ni kama walikwua wananifuatilia, waliiingia na kunikuta niko reception.

    Charlote aliita Jones, niligeuka na kuitka, yes… ni wewe ama?

    Nikajiangalia na kumwambia yes ni mimi. Hata na mimi nakushangaa ni wewe ama?

    Wadhamini waliona kwamba wote tuna hasira hivyo walisogea na kusema yapaswa tuongee. Inatakiwa tuongee, tafadhali charlotte tunaomba utukaribishe chumbani kwako tukazungumze.

    Nilipaacha rafu naomba nikaparekebishe kwanza. Niliondoka na kuwaacha wamekaa,, kisha mdhamini wa kike akanifuata na tukaingia chumbani.

    Akaniambia Charlote wewe ni kiboko,, unawezaje kufanya haya lakini?

    Nilimwambia yakikufika utaweza, yakikufuka utaweza mama,, niache tu maana ni issue nzito.

    Akaguna.. mh… lakini mbona wala sio nzito mama yangu? Mbona mpaka na msamaha kakuuomba jamani? Si umsamehe kiishe? Angalia usije kujuta mama yangu, najua unapendwa na utapendwa na wengi ila utaishia pabaya.

    Mdhamini wa kike alikwua anaongea kama kameza kanda.

    Sikuwa namsikiliza hata kidogo maana sikuona sababu ya kuweka hayo maneno moyoni, na hayakuwa na nafasi.



    SEHEMU YA TISA:

    Baada ya dakika chake aliingia Jones na mdhamini wa kiume.

    Jones alionekana kuchoka sana, na hakuongea lolote zaidi ya mdhamini wa kiume na wa kike.

    Lengo lao ilikuwa ni kutupatanisha, walitueleza kwamba mtu unapokosewa na mwenzako anapoomba msamaha basi ni lazima umsamehe. Na akasema kukosa mara ya kwanza sio kosa bali kurudia ndio kosa.

    Mdhamini wa kiume alieleza kwa namna ya kueleweka kabisa, na akijaribu kumueleza Jones namna ambavyo wanawake wakikosewa na wakichefukwa wasivyoweza kurudi kwenye nafasi zao za kwanza zaidi ya kuumia sana, isipokuwa yeye kuonyesha kubadilika ndiko ambako kutamfanya mke aweze kuamini ameombwa msmaha na kuamua kusamehe. Hivyo alimtaka Jones kukirii kosa lake mbele yangu kwa mara ingine tena.

    Jones hakuonekana kuwa mgumu. Aliniomba msamaha na kusema anatamani tuendelee na maisha yale ya mwanzao.

    Mdhamini wa kiume alinigeukia na kuniambia Charlote ni lazima umsamehe mumeo. Nilimwambia ni ngumu kumsamehe kirahisi, ila nitajitahidi kumsamehe moja kwa moja na ninakiri kumsamehe ila asipobadilika basi msamaha unaweza usitoke kabisa.

    Mdhamini aliniomba sana nimsamehe, na nilikubali.

    Na alimwambia Jones, nivyema sasa ukawa karibu sana na mkeo ili aaminmi umemuombe msamaha kwa kumaanisha, vinginevyo ukikosea tena unazidi kumfanya awe na moyo mgumu na wakutosamehe na kusababisha madhara zaidi.

    Jones alikubali na kusema amebadilika kabisa na hana mahusiano na mtu yeyote Yule.

    Mdhamini wa kike alinitazama na kuniambia, Charlote unaivunja nyumba yako mwenyewe, huyo shetani aliyewaingilia ashindwe kwa jina la Yesu.

    Tulimaliza kuzungumza an kukubaliana kurudi nyumbani na kuendelea na maisha. Lakini kabla ya kuondoka tulikunywa na kula chakula hotelini kisha mdhamini wa kiume akaenda kuchukua watoto na msichana wa kazi na kuwaleta nyumbani.

    Nilikuwa niko tu okay, sikuwa natatizo lolote lile. Jones alikuwa karibu sana na mimi, akijiongelesha sana, lakini sikuwa namjibu kwa wakati, sio kama nilikuwa nampuuza la hasha, ila kuna hali Fulani iliniingia ya kumchukia tu na si vinginevyo, nikimuona na kumhesabu ni Msaliti mkubwa sana kwenye ndoa yangu.

    Maisha yaliendelea, Mtaani shamra shamra za Harusi ya Husna na Majid zilishamiri na kupamba moto.

    Kila kona ilikuwa ni story ya harusi yao.

    Kila mmoja alikuwa amejiandaa vyema kwa ajili ya harusi hiyo.

    Kwa vile sikutaka jambo lolote lijulikane la mahusiano kati yangu na Mzee Zuberi wala Majdi, nilijitahidi kufanya siri sana, tena siri kubwa sana.

    Mzee Zuberi tuliendelea kuwasiliana. Na siku moja aliniita ofcn kwake akinitaka niende kuchukua mzigo, ambao sikujua ni mzigo gani.

    Ilikuwa ni majira ya mchana. Niliondoka ofcn mara moja na kuelekea kwa mzee Zuberi.

    Nilifika ofcn kwake na alinikaribisha vyema kama kawaida, alizoea kuniita Bi mdogo. Nilifurahia sana jina hilo. Alinipenda sana.

    Nilifika na alinitazama na kuniambia,, wewe mtoto nakupenda sana na leo nina zawadi yako ambayo nataka usinisahau hata nikifa unikumbuke. Nilijiuliza ni zawadi gani? Sikuwa na idea hata kidogo. Kwani amekuwa akinipa pesa na viatu na nguo ila leo ananipa nini?

    Alivuta droo yake na kutoa bahasha kubwa ya A4 ya rangi ya khaki. Na kuniambia chukua fungua.Bado sikuwa nawaza ni nini.

    Niliichukua bahasha ile na kuifungua, Dah… waoo, nilijikuta nikitamka kwanguvu baada ya kufungua habasha ile.

    Uwiii, sikuamini nilichoona ndani yake.

    Nikiwa nimekaa kitini huku nikiwa ninashangaa karatasi ile iliyo mezani kwake, alisimama na kunisogelea karibu kabisa, na kuzunguka nyuma ya mgongo wangu na kunishika mabega, huku nikiwa nimegeuza uso wangu kwa nyuma nikimtazama.

    Alinibusu na kuniambia,Charlote wewe ni msichana mzuri sana, unayenipenda, unayeniheshimu na kunijali sana, na kukifanya kichwa change kitulie kwa penzi lako, unastahili zawadi nzuri kama hizi za maisha.

     

     

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog