Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

THE LOVE YOU HAD BEFORE (PENZI ULILOKUWA NALO KABLA) - 3

 







    Simulizi : The Love You Had Before (Penzi Ulilokuwa Nalo Kabla)

    Sehemu Ya Tatu (3)



    Mapenzi yalizidi kuwa motomoto, kila siku walikuwa pamoja huku wakisaidiana katika kila kitu. Luciana yule wa kipindi cha nyuma alibadilika kabisa, akawa si mtu wa kukosa chuo, kila siku ilikuwa ni lazima kuhudhuria huku akitamani kuwa karibu na Dickson kila wakati.

    Maisha aliyopitia nyuma, yalibaki na kuwa historia, hakuwa msichana yule wa kuhusudu fedha, alikuwa mtu aliyekuwa tayari kwa maisha ya kufunga ndoa na kuwa na mume wake.

    Kwa Dickson, alikuwa na mawazo mno, hakufikiria sana kuhusu Evadia, aliamua kwa moyo mmoja kuachana na msichana huyo, watu ambao walimuumiza sana kichwa chake walikuwa wazazi wake tu.

    Hakujua angewaambia nini, hakujua angeanzia wapi kuwaambia kwamba alipata msichana mwingine ambaye alionekana kustahili kuwa mke wake, alijua kwamba wangeongea sana lakini kama mwanaume, wakati mwingine akapiga moyo konde na kusonga mbele.

    “Mbona una mawazo?” aliuliza Luciana.

    “Hakuna kitu mpenzi.”

    “Hebu niambie ukweli kwanza.”

    “Hakuna kitu, niamini.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku ziliendelea kukatika, penzi likazidi kuchipuka, Dickson akawa si kitu pasipo Luciana na kwa msichana huyo ikawa hivyohivyo. Baada ya kukatika miezi kumi, hapo ndipo chuo kikafungwa kwa ajili ya likizo ndefu kwani napo kilikuwa kipindi ambacho nchi hiyo ya Venezuela ilikuwa ikielekea katika uchaguzi mkuu.

    Wakaondoka na kurudi barani Afrika. Kabla ya kurudi nchini Tanzania, Dickson aliataka kupitia nchini Rwanda, atambulike kwa wazazi wa Luciana hata kabla ya kufunga ndoa, baada ya saa kadhaa, wawili hao walikuwa nchini Rwanda.

    “Nimefurahi sana kufika nchini kwenu, hakika watu wenu ni wakarimu sana,” alisema Dickson huku akionekana kuwa na furaha mno.

    Walifika katika Jiji la Kigali, mishemishe ziliendelea kila kona, watu walionekana kuwa bize kuitengeneza nchi yao baada ya machafuko yaliyotokea mwaka 1994. Hakukuwa na mtu aliyekaa kiholelaholela, kila mmoja alionekana kuwa na kiu ya kuibadilisha nchi yake.

    Baada ya safari ya dakika thelathini, wakafika katika mtaa uliokuwa pembeni wa Jiji la Kigali, Mtaa wa Mwongozo ambapo gari likaingia katika barabara ya vumbi na baada ya dakika kadhaa likasimama nje ya nyumba moja iliyoonekana kuwa ya kawaida sana.

    Watu waliokuwa ndani ya nyumba hiyo walipoliona gari hilo likiingia ndani ya eneo la nyumba hiyo, wakatoka nje ili kushuhudia ni nani ambaye angeteremka, aliposhuka Luciana, wote wakamkimbilia na kumkumbatia kwa furaha.

    Majirani hawakutaka kuwa mbali, nao wakasogea kule kulipokuwa na gari lile na kuanza kumwangalia Luciana. Alionekana kuwa mrembo hasa, alipendeza machoni mwa kila mtu aliyekuwa akimwangalia, kwao, alionekana kuwa mrembo hata zaidi ya alivyokuwa kipindi cha nyuma.

    “Très proche soeur Luciana,” (Karibu sana Luciana) alimkaribisha mama yake, alizungumza Kifaransa kama ilivyokuwa nchini humo.

    “Thank you,” (Asante) Luciana aliitikia kwa Lugha ya Kingereza, hakutaka kumuacha mpenzi wake katika sintofahamu.

    Wote kwa pamoja wakaanza kuelekea ndani. Dickson hakuzungumza kitu, mahali hapo alikuwa kimya tu na muda wote ule uso wake ulijawa na tabasamu pana. Alionekana kufurahia kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo, kila mmoja alimchangamkia.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walipofika ndani, kitu cha kwanza alichokifanya Luciana ni kumtambulisha kwa wazazi wake kwamba alikuwa mpenzi wake ambaye walipanga mambo mengi kuhusu ndoa, wazazi, ndugu na jamaa wote wakakubaliana naye, wakampokea na kuwabariki kwa kila kitu ambacho wangekifanya likiwa hilo la kuishi milele.

    “Yeye ni Mtanzania?” aliuliza mama yake.

    “Ndiyo!”

    “Nimefurahi, nawapenda sana Watanzania,” alisema mama yake Luciana.

    Siku hiyo wakalala hapo na siku mbili baadaye wakaanza safari ya kuelekea nchini Tanzania. Njiani, Dickson alikuwa na mawazo tele, hakujua ni kitu gani alitakiwa kuwaambia wazazi wake kwani kitendo cha Luciana kuwa mpenzi wake, aliamini kwamba kisingepokelewa kwa mikono miwili.

    “Nitawaambia chochote tu, kwanza Evadia simtaki tena,” alisema Dickson.

    “Unasemaje?” aliuliza Luciana.

    “Kwani nimesema chochote?”

    “Nimesikia ukiongea!”

    “Hapana!Labda umesikia vibaya!”

    “Mhh!Sawa mpenzi,” alisema Luciana, hapohapo akamuegemea Dickson begani na kupitiwa na usingizi.

    Muda wote huo, Dickson alikuwa kwenye presha kubwa.





    *****

    **********

    ***********

    Safari iliendelea, japokuwa Luciana alilala njiani lakini kwa Dickson alikuwa macho safari nzima. Kichwa chake kilikuwa na mawazo tele, aliwafikiria wazazi wake kwa kuona kwamba wangekataa yeye kuwa na msichana huyo kwa kuwa alimwacha msichana waliyemfahamu, msichana mpole, asiyekuwa mzungumzaji, Evadia.

    Ndege ilichukua saa kadhaa ndipo ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambapo wakateremka na kufuata taratibu zote kisha kukodi teksi ambayo ikaanza kuwapeleka mpaka Msasani alipokuwa akiishi.

    Njiani, bado Dickson hakuonyesha uchangamfu ambao ulizoeleka machoni mwa Luciana, alionekana kuwa na kitu kilichokuwa kikimtatiza moyoni mwake, Luciana hakutaka kukubali kuiona hali hiyo kitu kilichompelekea kuuliza.

    “What’s wrong with you?” (Kimekukuta nini?) aliuliza Luciana.

    “What?” (Nini?)

    “I’m asking you! What’s wrong with you?” (Ninakuuliza kimekukuta kitu gani?)

    “Nothing.” (Hakuna kitu)

    “Are you sure?” (Una uhakika?)

    “Yes!” (Ndiyo!)

    “But, you look weird!” (Lakini unaonekana tofauti)

    “Luciana! Nothing wrong, trust me,” (Luciana! Hakuna tatizo, niamini) alisema Dickson.

    Luciana hakutaka kuuliza swali jingine, alichokifanya ni kuyapeleka macho yake nje na kuanza kuangalia mazingira. Hakuwa na raha, kitu alichohisi ni kwamba mpenzi wake huyo kulikuwa na kitu kilichomfanya kuwa katika hali ile ila alimficha tu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hakujali, alichokifanya ni kupuuzia na safari kuendelea. Walichukua dakika kadhaa na ndipo walipofika nje ya jumba moja la kifahari, dereva akapiga honi na mlinzi kutoka nje, akaenda kuongea na dereva, alipoona kwamba gari hilo lilimbeba Dickson, akafungua geti.

    “Karibu kaka!” mlinzi alimkaribisha Dickson.

    “Asante.”

    Wakaingia ndani huku mlinzi akitangulia na mabegi. Hapo ndipo Dickson alipoonekana dhahiri kwamba alikuwa na hofu moyoni mwake. Luciana aliendelea kuwa na wasiwasi lakini hakutaka kuuliza swali kwani majibu aliyopewa ndani ya gari yalionyesha kabisa kwamba mpenzi wake hakutaka maswali zaidi.

    Walipofika sebuleni, wakatulia, akamuita dada wa kazi ambaye akafika mahali hapo na kuambiwa kwenda kuwaita wazazi wake, mfanyakazi yule akafanya kama alivyoambiwa.

    Hazikupita dakika nyingi, wazazi wake wote wawili wakafika sebuleni hapo, walifurahi kumuona kijana wao lakini walipoyapeleka macho yao pembeni, wakamuona msichana ambaye alikuwa mgeni machoni mwao, wakahisi kwamba huyo ndiye alikuwa Luciana waliyeambiwa.

    Hawakuonyesha kinyongo, hawakuonyesha hali yoyote ya mshtuko kwani walijua hilo lingeweza kutokea, walichokifanya ni kuwakaribisha nyumbani hapo. Dickson hakutaka kunyamaza, alichokifanya ni kuwaambia wazazi wake juu ya Luciana.

    “Huyu ni mchumba wangu,” alisema Dickson.

    “Uchumba huo umeanza lini?” aliuliza mama yake.

    “Chuoni. Nimeona kwamba yeye ni msichana mzuri, mwerevu na anayejua kupenda ambaye kama tutatengeneza maisha pamoja, naamini itakuwa ni furaha yangu ya milele,” alisema Dickson.

    “Karibu sana Luciana.”

    “Asante mama.”

    Hakukuwa na maswali mengi, wazazi wake walipomuona msichana huyo wakaridhika naye, walimpenda kwa sababu alikuwa na sura nzuri ila mbali na hilo, walikuwa na majonzi mioyoni mwao kwani msichana pekee waliyekuwa wamemzoea alikuwa Evadia tu.

    Baba yake hakutaka kuvumilia, alichokifanya baada ya Luciana kuanza kuzoea mazingira ya humo ndani ni kumuita kijana wake pembeni kwa lengo la kuzungumza naye.

    “Hivi ulifikiria nini?” aliuliza baba yake.

    “Kivipi?”

    “Kuhusu huyu msichana.”

    “Hakuna kitu, nimegundua kwamba ni msichana mzuri, ana sifa zote za kuwa mke,” alijibu Dickson.

    “Una uhakika?”

    “Asilimia mia mbili.”

    “Sawa. Na vipi kuhusu Evadia?”

    “Nilimwambia ukweli kwamba nimempata msichana mwingine.”

    “Ila hukuona kama angeumia?”

    “Unafikiri ningefanyaje? Sikuwa na jinsi, ila nilimpa nafasi ya kuwa na mwanaume mwingine,” alijitetea Dickson.

    “Mmmh! Aya, hakuna tatizo. Uamuzi ni wako, kazi yetu kubwa ni kukuunga mkono,” alisema baba yake maneno yaliyomfanya Dickson kuwa na furaha mno, akashindwa kuvumilia, akamkumbatia baba yake.

    Laurence alipotea ghafla, hakuonekana tena hospitalini hapo. Kila mmoja alikuwa na hofu, walijiuliza mahali alipokwenda kijana huyo lakini hakukuwa na aliyejua, na hata alipouliza Matilda, jibu lake lilikuwa lilelile kwamba hakujua mwanaume huyo alielekea wapi.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku zikaendelea kukatika, Evadia aliendelea kubaki kitandani pale, kama kulia, alilia sana lakini hakukuwa na kitu chochote kilichobadilika. Hakukuwa na mtu ambaye alimfanya kuwa katika maumivu makali kama msichana huyo.

    Kuna wakati alikuwa akijuta kuonana na Laurence, chuki ya taratibu ikaanza kujitengeneza moyoni mwake, mapenzi aliyokuwa nayo juu ya mwanaume huyo yakaanza kupotea kabisa.

    Mama yake ndiye alikuwa mfariji pekee aliyebaki naye, ingawa Matilda alifika hospitalini hapo mara kwa mara na kumwambia kwamba inawezekana hapo baadaye Laurence akarudi tena lakini kwa msichana huyo jambo hilo halikuweza kumbadilisha chochote kile.



    Mikakati ya kutafuta figo kwa mtu mwingine ikaanza hospitalini hapo, watu mbalimbali walifika kwa ajili ya kutoa figo lakini kila walipopimwa majibu yalikuwa yaleyale kwamba vinasaba vyao havikuendana kabisa na vya Evadia jambo lililofanya upasuaji kutokufanyika hivyo Evadia kuwa kwenye hali mbaya.

    “Hivi nitapona kweli mama?” aliuliza Evadia.

    “Utapona tu, Mungu atakutia nguvu.”

    “Kweli?”

    “Niamini. Hujui kwamba Yesu ni Mponyaji?”

    “Najua.”

    “Basi amini hilo. Kama aliponya wengine, basi jua kwamba hata wewe atakuponya,” alimfariji mama yake.

    Siku zikaendelea kukatika, ulipofika mwezi wa pili tangu awe kitandani, Dk. Panzini akaingia ndani ya chumba kile huku uso wake ukionekana kuwa mwenye furaha tele.

    “Kuna nini?” aliuliza mama Evadia.

    “Laurence amerudi.”

    “Unasemaje?” aliuliza Evadia huku akijitahidi kukaa kitandani lakini akashindwa.

    “Laurence amerudi. Ngoja nimuite.”

    Badala ya kuwa na furaha, Evadia akaanza kulia kitandani pale. Moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kile alichokisikia kutoka kwa daktari yule. Alimchukia Laurence, hakumpenda kwa sababu tu alimtoroka hospitalini hapo na kwenda asipopafahamu.

    Baada ya dakika kadhaa, Laurence akaingia ndani ya chumba kile. Alionekana vilevile, mwanaume aliyepigwa na maisha ambaye uso wake ulijawa na tabasamu pana, alipomuona Evadia, hapohapo akaanza kumfuata pale kitandani kisha kumuinamia.

    “Mpenzi....” aliita.

    Evadia hakuitikia, alibaki akimwangalia Laurence mahali pale huku akionekana kuwa mwenye hasira. Uso wake ule, ndita alizokuwa amezikunja hazikumfanya Laurence kuliondoa tabasamu lake, aliendelea kulitoa huku akimwangalia msichana huyo kitandani pale.

    “Naomba uondoke Laurence,” alisema Evadia.

    “Niondoke? Niende wapi?”

    “Nimesema naomba uondokeeeee...” alisema Evadia kwa hasira.

    “Hapana! Siwezi kuondoka, siwezi kukuacha peke yako,” alisema Laurence huku akipiga magoti.

    Evadia hakuzungumza kitu chochote, alibaki akilia kitandani pale, moyo wake ulimuuma mno, kila alipomwangalia Laurence na jinsi alivyomtoroka hospitalini hapo alibaki akiumia na hakuona kama alitakiwa kumsamehe mwanaume huyo.

    Msimamo wake ulikuwa uleule kwamba Laurence alitakiwa kuondoka ndani mule kitu ambacho hakukubaliana nacho hata kidogo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa si uondoke,” alisema mama Evadia.

    “Mama! Siwezi kuondoka, ninampenda Evadia, siwezi kumuacha peke yake akiteseka.”

    “Hapana! Kama ungekuwa unampenda, usingemkimbia katika kipindi kigumu kama hiki. Mwangalie jinsi alivyo, angalia jinsi alivyokonda kwa ajili ya mawazo. Laurence, naomba uondoke na umuachae binti yangu,” alisema mama Evadia huku akionekana kumaanisha alichokisema.

    “Siwezi! Kwa sababu nina mapenzi mazito kwa Evadia, siwezi kuondoka,” alisema Laurence, akasimama, akavuta kiti na kutulia. Mara hapohapo Matilda akaingia, yeye mwenyewe kumuona Laurence wodini mule alishangaa.



    “Karibu Matilda,” alimkaribisha Laurence.

    “Laurence! Ulikuwa wapi?” lilikuwa swali lililotoka kwa Evadia.

    “Nani? Mimi?”

    “Ndiyo!”

    “Nilipata tatizo, nilikwenda mbali.”

    “Wapi?”

    “Mwanza!”

    “Kufanya nini?”

    Laurence alibaki kimya kwa muda, alionekana kuwa mtu mwenye mawazo mengi. Kichwa chake kikaanza kufikiria kwa haraka juu ya kitu alichotakiwa kukizungumza mahali hapo. Wote waliokuwa ndani ya chumba kile walibaki wakimwangalia, walitaka kusikia Laurence alikuwa wapi.

    “Nimekuwa nikimpenda sana Evadia, amekuwa msichana muhimu sana kwangu. Kumuona kitandani akiugua, kilikuwa kitu kilichoniumiza sana, sikupenda kumuona akiteseka, hivyo niliondoka kwenda Mwanza,” alisema Laurence.

    “Kufanya nini huko?”

    “Kutafuta pesa.”

    “Ila pesa zipo, si nimetoa pesa kwa ajili ya kuwasaidia?”

    “Najua. Ila wakati mwingine niliona bora nitafute pesa kama mwanaume, nisingeweza kukubali kuona msichana wangu akiteseka kitandani,” alisema Laurence.

    “Sawa. Kuna kingine?”

    “Ndiyo! Tena cha muhimu kabisa,” alijibu Laurence.

    “Kitu gani?”

    “Nataka kutoa figo yangu kumsaidia Evadia,” alisema Laurence, kila mmoja humo ndani akashtuka, mpaka Dk. Panzini.

    “Utoe figo yako?”aliuliza Dk. Panzini.

    “Ndiyo! Ninataka kumpa figo yangu moja Evadia.”

    “Mmmh!”

    Kwa kumwangalia tu usoni mwake, alionyesha ni kwa jinsi gani alimaanisha kile alichokisema mahali pale. Kichwa chake kilimuuma kila siku, alimfikiria msichana huyo aliyekuwa kitandani, jinsi alivyoteseka, hakupenda kuliona hilo likitokea hivyo kitu cha mwisho kabisa alichoamua kukifanya ili kumrudishia furaha msichana huyo ni kwamba alitaka kutoa figo yake ili ipandikizwe kwa Evadia.

    Evadia mwenyewe hakuonekana kuamini kile alichokisikia, ila swali kubwa likaja je, vinasaba vya figo lake vingeendana na vya mwanaume huyo au ingekuwa kama wale wengine?

    “Na vipi kuhusu vinasaba?” aliuliza Evadia.

    “Najua Mungu atafanya jambo, sidhani kama yupo tayari kukuona ukiteseka kitandani hapa,” alijibu Laurence.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwa hiyo unataka kumpa figo yako?” aliuliza Dk. Panzini.

    “Ndiyo! Ninataka kwa asilimia mia moja.”

    “Sawa.”

    Huo ndiyo uamuzi alioufikia, hakutaka kuona msichana wake akiendelea kuteseka kitandani pale. Alichokifanya Dk. Panzini ni kumwambia amfuate kwa ajili ya kupima ili kuona kama vinasaba vyake vingekuwa vinafanana na vya Evadia.

    Evadia alibaki chumbani mule na mama yake, japokuwa kwa kipindi kirefu aliahidi kwamba angemchukia Laurence lakini kwa kile alichojiwekea nadhiri kukifanya kikazifanya hasira zake kupungua kwa kiasi kikubwa hivyo kubaki chumbani mule wakifarijiana.

    Zilipita dakika arobaini na ndipo Laurence na daktari yule waliporudi ndani ya chumba kile. Kwa kuwaangalia tu ungejua ni kitu gani kilikuwa kimetokea, wote wawili nyuso zao zilijawa na tabasamu pana, tabasamu yaliyoonyesha kwamba kulikuwa na habari nzuri.

    “Kuna nini?” aliuliza Matilda.

    “Habari njema ni kwamba vinasaba vya Laurence vinaendana na vya Evadia,” alijibu Dk. Panzini.

    Hakukuwa na aliyeamini kile alichokisikia kutoka kwa Dk. Panzini, watu wengi walifika hospitalini hapo kwa ajili ya kumtolea figo Evadia lakini mwisho wa siku hakukuwa na mtu aliyefanikiwa katika hilo.





    Leo hii, baada ya watu zaidi ya mia mbili kufika hospitali hapo na kutokufanikiwa, mwanaume aliyekuwa akimpenda, aliyemthamini kumbe vinasaba vyake viliendana na vile alivyokuwa navyo yeye.

    Hasira zote zikatoweka, akauhisi moyo wake ukianza kumpenda tena Laurence. Siku hiyo ilikuwa ni furaha kwa kila mtu, Laurence hakujutia uamuzi wake wa kutoa figo kwa ajili ya msichana aliyekuwa akimpenda, alikuwa radhi kwa kila kitu na ndiyo maana aliamua kufanyika kwa jambo hilo.

    “Ninakupenda Evadia,” Laurence alimwambia Evadia.

    “Nashukuru mpenzi! Nashukuru kwa kila kitu,” alisema Evadia, akashindwa kuvumilia, machozi yakaanza kumtoka.

    “Usijali. Kwa maana hiyo, zile fedha zilizobaki, tutafanyia biashara nyingine kwa ajili ya maisha yetu,” alisema Laurence.

    “Hakuna tatizo.”

    Kiasi kilichokuwa kimebaki kilikuwa ni milioni ishirini na saba, milioni tatu zilitumika. Mama Evadia hakuchoka kumshukuru Laurence, kila wakati alimwambia dhahiri kwamba alimshukuru kwani alikuwa msaada mkubwa kwa binti yake.

    Siku iliyofuata, asubuhi na mapema Laurence akafika katika chumba hicho, siku hiyo alijiandaa kwa ajili ya upasuaji ambao ungemfanya kutolewa figo yake na kupandikizwa katika mwili wa msichana Evadia.

    Mara baada ya kufika, akaitwa katika ofisi ya daktari yeye na mama Evadia pamoja na Matilda na kuanza kupewa elimu juu ya kile ambacho kingekwenda kufanyika huku akipewa karatasi kwa ajili ya kusaini kwamba alikuwa tayari kwa kila kitu.

    “Unatakiwa kusaini hapa, hii ni oparesheni, chochote kinaweza kutokea,” alisema Dk. Panzini.

    “Hakuna tatizo.”

    Laurence akachukua karatasi hiyo na kuanza kusaini. Muda wote moyo wake ulikuwa na wasiwasi, hakuwahi kufanyiwa upasuaji na siku hiyo ndiyo ilikuwa siku ya kwanza hivyo kitendo cha kuambiwa kwamba alitakiwa kufanyiwa upasuaji huo kilimtia woga moyoni mwake.

    Alipomaliza kusaini, akachukuliwa na kupelekwa katika chumba maalumu, huko, akavuliwa nguo zake na kuvarishwa vazi maalumu kisha kulazwa katika machela ambayo ilisukumwa mpaka katika chumba kilichoandikwa Theatre (chumba cha upasuaji).CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wala hazikupita dakika nyingi, machela nyingine ikaingizwa ndani ya chumba kile na juu yake alikuwepo msichana Evadia. Alipomuona mpenzi wake chumbani mule huku akiwa tayari kwa ajili ya upasuaji ule, akatoa tabasamu pana. Alichokifanya Laurence ni kuunyoosha mkono wake kisha kuushika mkono wa Evadia.

    “Ninakupenda mpenzi,” alimwambia.

    “Ninakupenda pia mpenzi na asante kwa kila kitu.”

    “Ninafanya hivi kwa ajili yako, si unajua hilo?”

    “Najua mpenzi.”

    “Sawa.”

    Tayari Dk. Panzini na madaktari wenzake walikwishafika chumbani humo, kila mmoja alikuwa tayari kwa ajili ya upasuaji huo. Kazi hiyo ilitakiwa kufanywa kwa umakini mkubwa kwani endapo wangekosea hata sehemu moja basi ingemaanisha kwamba mmoja wapo au wote wawili wangefariki dunia.

    Kabla ya upasuaji kuanza, madaktari wale wakashikana mikono na kuanza kusali kila mtu kwa dini yake, walipomaliza, wakachukua nusu kaputi na kisha kuwawekea, wala hazikupita dakika nyingi, wawili hao wakapitiwa na usingizi mzito, kilichoendelea, hakukuwa na aliyekifahamu, upasuaji ukaanza kufanyika.

    Nje ya chumba kile, mama Evadia alikuwa na hofu, hakutulia, kila wakati alikuwa akiomba Mungu kwamba upasuaji ule ukamilike na hivyo binti yake arudi na kuwa kama alivyokuwa kipindi cha nyuma.

    Kwa Matilda, hakutulia, kichwa chake kilikuwa na maswali mengi kwamba ilikuwaje bosi wake, Laurence akubali kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya kutolewa figo kisa msichana?

    Alifahamu kwamba alikuwa na fedha nyingi, alikuwa na uwezo wa kuwatafuta watu wengine tena kwa gharama zozote zile na mwisho wa siku kumpata mtu ambaye vinasaba vyake vingeendana na vya Evadia kisha kumlipa na figo ya huyo mtu kutolewa.

    Kila kitu alichojiuliza alikosa jibu ila kwa sababu mapenzi yalikuwa na nguvu kuliko mauti, akaamua kuachana naye kwa kuamini kwamba bosi wake aliamua kutoa figo yake kwa kuwa alimpenda sana msichana Evadia.



    Madaktari waliendelea na kazi yao ya kutoa figo ya Laurence kwenda kwa msichana Evadia. Nje ya chumba kile bado mama Evadia alikuwa na mawazo tele. Saa ziliendelea kukatika huku akiendelea kubaki kwenye benchi pamoja na Matilda.

    Kwa kumwangalia Matilda, aliendelea kuwa kwenye hali ya sintofahamu kwani alionekana kujiuliza juu ya ujasiri alioufanya nao mwanaume huyo wa kuutoa figo yake na kumpa msichana aliyekuwa akimpenda sana, Evadia.

    Saa zilianza kukatika mahali pale, waliendelea kuvumilia, hali ilionekana tofauti na walivyotegemea kwani upasuaji ulikuja kumalizika saa tatu usiku, saa kumi na mbili tangu madaktari waanze upasuaji ndani ya chumba kile.

    Mara baada ya kila kitu kumalizika, Laurence akachukuliwa na kupelekwa nje, alikuwa kitandani, machela ilisukumwa kuelekea katika chumba cha wagonjwa mahututi, alipofikishwa humo akapewa muda wa mapumziko.

    Wala hazikupita dakika nyingi naye Evadia akatolewa ndani ya chumba kile, hakuwa akijitambua, alikuwa hoi juu ya machela na ilikuwa ikisukumwa kuelekea katika chumba cha mapumziko.

    Si mama Evadia wala Matilda ambaye aliruhusiwa kuingia ndani ya vyumba hivyo, walizuiliwa kwani wagonjwa walihitaji muda zaidi wa kupumzika kabla ya kuendelea na mambo mengine.

    Matilda alifika hospitalini hapo kila siku, kila kitu kilichokuwa kikiendelea kilitakiwa kuwa siri, hakutakiwa kufahamu mfanyakazi yeyote yule juu ya hali aliyokuwa nayo Laurence kwamba aliamua kutoa figo yake moja kwa ajili ya kumsaidia mpenzi wake.

    Siku zikakatika, baada ya wiki mbili, wote walikuwa wakiendelea vizuri. Walizungumza ingawa si kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma. Walionekana kuwa na afya nzuri kidogo. Mama Evadia alipata nafasi ya kuwatembelea wote wawili, tena kwa zamu, baada ya madaktari kuona mama huyo akihangaika huku na kule, wakaamua kuwaweka wagonjwa hao katika chumba kimoja.

    “Unajisikiaje?” aliuliza mama Evadia, alikuwa akimuuliza binti yake.

    “Najisikia vizuri kidogo,” alijibu Evadia kwa sauti ya chini.

    “Asante Mungu!”

    Hapohapo akamfuata Laurence ambaye naye alikuwa ndani ya chumba hichohicho, alipomfikia akamuuliza kuhusu hali yake, naye alikuwa kama Evadia, hakuwa akijisikia vizuri sana kwani bado mshono ulikuwa ukimuuma.

    Siku ziliendelea kukatika, kila siku Matilda alipoingia wodini na kumwangalia bosi wake machoni, aliyaona mapenzi yaliyokuwa yakionekana kwa msichana Evadia. Laurence alikuwa tayari kwa kila kitu na hakuonekana kama alikuwa tayari kumpoteza msichana huyo.

    “Bosi..” aliita Matilda.

    “Shiiiii....”

    “Samahani, nimesahau. Unajisikiaje?” aliuliza Matilda.

    “Najisikia vizuri kidogo, bado kidonda kinaponapona kwanza,” alijibu Laurence.

    “Pole sana.”

    “Asante sana.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya mwezi mmoja, wote wawili wakaruhusiwa kutoka hospitalini. Hakukuwa na mtu yeyote aliyeruhusiwa kufanya kazi zozote kwani walikuwa walitakiwa kupumzika kwa kipindi kirefu pamoja na kutofanya kazi zozote nzito kwani bila hivyo mishono waliyokuwa nayo ingeweza kuleta matatizo mengine.



    ITAENDELEA

THE LOVE YOU HAD BEFORE (PENZI ULILOKUWA NALO KABLA) - 2

 







    Simulizi : The Love You Had Before (Penzi Ulilokuwa Nalo Kabla)

    Sehemu Ya Pili (2)



    Mama Evadia hakutaka kutulia nyumbani, alihisi hasira moyoni mwake, alichokifanya ni kuondoka nyumbani hapo na kuelekea kwa akina Dickson ambapo huko akawaambia wazazi wa kijana huyo kila kitu kilichokuwa kimeendelea. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wazazi hao hawakuamini, waliuliza mara mbilimbili kama alikuwa na uhakika na kile alichokizungumza, mwanamke yule aliwaambia kwamba kila kitu kilikuwa wazi, alipoona hiyo haitoshi, akampigia simu Evadia na kumtaka kuelekea nyumbani kwa kina Dickson ambapo alifanya hivyo haraka sana.

    “Ni kweli Evadia?” aliuliza baba yake Dickson.

    “Ni kweli! Ameniambia amepata mwanamke mwingine.”

    Wazazi hao wakashtuka, hawakutegemea kusikia kile walichokisikia mahali pale, walibaki wakimwangalia msichana yule, walipigwa na mshangao mkubwa. Walimfahamu kijana wao, waliyajua mapenzi mazito aliyokuwa nayo kwa msichana yule, leo hii kusema kwamba hakuwa akimhitaji kwa sababu alikuwa amepata mwanamke mwingine, mioyo yao ilisikia maumivu makali.

    “It is impossible,” (Haiwezekani)

    “Ndiyo hivyo!” alisema Evadia na kuanza kulia kwa uchungu. Maumivu yake ya moyo, hakika hayakuweza kupungua. Dickson alimchanganya mno.



    Kwa jina aliitwa Luciana Pentezel, msichana mrembo aliyetoka nchini Rwanda. Kwa kumwangalia tu, usingekuwa na wakati mgumu wa kusema kwamba Luciana alikuwa miongoni mwa wasichana wazuri waliowahi kuumbwa katika sayari hii.

    Alikuwa na sura nyembamba ya Kitusi, macho makubwa yaliyomuonyesha kwamba muda wowote ule usingizi mzito ungempata, alikuwa na lipsi nene huku meno yake yakiwa meupe kabisa.

    Kwa sura alivutia mno, kila mwanaume aliyemwangalia Luciana alibaki na kumbukumbu kwamba katika maisha yake aliwahi kumuona msichana aliyekuwa na urembo wa ajabu.

    Japokuwa nchini venezuela kulikuwa na wasichana wengi warembo lakini kwa Luciana kila msichana alikaa pembeni, chuoni hapo alikuwa gumzo, kila alipopita, wanaume walimwangalia kwa matamanio makubwa.

    Luciana hakuwa msichana wa tofauti, hakuwa na maringo, alipewa kuzungumza na kila mtu kitu kilichomfanya kupendwa mno.

    Katika mambo yote hayo, uzuri wote aliokuwa nao, Luciana alihusudu sana pesa, alipenda pesa sana zaidi ya alivyokuwa akimpenda Mungu. Kila alipokaa, alitamani pesa ziwe zimemzunguka, kila alipopita alitamani akanyage pesa kwenda sehemu yoyote aliyotaka kwenda.

    Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, hakuwahi kuwa katika uhusiano na mwanaume asiyekuwa na pesa. Alitoka katika familia ya kimasikini, alikwenda nchini Venezuela kama bahati tu hivyo alivyofika, alitaka kurudi nchini Rwanda huku akiwa na heshima ya juu kabisa, atafute pesa popote zilipo ili mwisho wa siku atakaporudi nchini Rwanda basi awe na utajiri wa kutosha.

    Uzuri wake ukawavuta wanaume wengi, walipogundua kwamba msichana huyo alihusudu sana pesa, wakamfuata na pesa zao na kisha kulala naye. Luciana hakuwa msichana mwenye kujali, alitembea na kila mtu aliyekuja kwake na kutanguliza pesa mbele.

    Kila alipopata mimba, kwake ilikuwa ni bahati mbaya tu, hivyo akatoa na maisha kuendelea kama kawaida. Siku zikakatika, wanaume wakazidi kutembea naye, wakampa pesa nyingi mpaka kufikisha kiasi cha dola milioni mbili, zaidi ya milioni mia nne.

    Alijiona kuwa tajiri, alijiona kuwa na sauti kubwa mara atakaporudi nchini Rwanda. Hakukoma, hakuacha, bado msururu wa wanaume uliendelea kujipanga huku kila aliyekuja kulikuwa na sharti kubwa la kuacha pesa mezani, kiasi kikubwa cha pesa ambacho hata wakati mwingine kilifika dola elfu tano, zaidi ya milioni kumi, kwa watu wenye pesa, hawakujiuliza, walitoa kiasi hicho cha fedha ili mradi mwisho wa siku walale naye tu.

    “Kuna mvulana amekuja chuo,” alisikika rafiki yake aitwaye Serena, msichana kutoka nchini Ethiopia aliyekuwa anamuunganishia kwa wanaume wengi hapo chuoni.

    “Mvulana gani?”

    “Ni Mtanzania, mzuri sana.”

    “Kweli?”

    “Ndiyo!”

    “Ana pesa?”

    “Mmmh! Sijui!”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa bila pesa, hata sidhani kama kuna mtu anaweza kuwa mzuri. Uzuri wa kweli ni pesa tu, hivyo vingine mbwembwe,” alisema Luciana huku akibinua mdomo wake.

    Hicho ndicho alichokifikiria, hakuamini kama duniani kulikuwa na wanaume wazuri, kwake aliamini katika pesa, kwamba unapokuwa na pesa, hata kama wewe ni mbaya bado utaonekana mzuri tu.

    Kila siku Serena alimwambia kuhusu mwanachuo mpya aliyekuja kujiunga chuoni hapo, mwanaume mwenye uzuri wa sura ambaye alitoka nchini Tanzania. Kila siku Luciana alikuwa bize na wanaume wenye pesa ambao walimfuata na magari ya thamani chuoni hapo.

    Alipelekwa katika kumbi za starehe, kulala kwenye hoteli za gharama ilikuwa kawaida yake, hakujuta kuwa mzuri, kila siku ilikuwa ni lazima kumshukuru Mungu kwa uzuri aliompa ambao muda huo aliona faida yake kubwa.

    “Luciana!”

    “Abeee!”

    “Kesho una ratiba gani?”

    “Nakwenda kwa Arnandro!”

    “Mmh! Yule si muuzaji wa madawa ya kulevya?”

    “Ndiyo! Kwani mimi nakwenda kuuza? Si nakwenda kuchuma pesa tu,” alisema Luciana.

    “Mmh! Ila kuwa makini.”

    “Usijali.”

    Alitembea na watu wengi mno, wenye pesa ambao walitamani kuwa na wanawake wazuri. Kwa Luciana hakutaka kujali kitu chochote kile, alichokuwa akikifikiria kwa wakati huo kilikuwa pesa tu.

    Hakujali kama mtu fulani alikuwa muuzaji wa madawa ya kulevya au alizipata pesa kwa njia haramu, alichokuwa akikiangalia ni mfuko wake kujaa pesa tu. Alizibabaikia pesa, utajiri mkubwa ukaanza kunukia maishani mwake, hakufikiria kurudi Rwanda, hata kulipokuwa na likizo, alihakikisha kwanza anatafuta fedha kwa juhudi zote na ndiyo arudi huko.



    “Ulikuwa unasemaje siku ile?” aliuliza Luciana.

    “Siku gani?”

    “Kuna siku uliniambia kwamba kuna mwanaume amefika chuo ni mzuri sana.”

    “Bado unakumbuka tu?”

    “Ndiyo! Ninataka kumuona.”

    “Yupo chuo.”

    “Leo lazima niende, sikwenda siku nyingi, nitataka kumuona,” alisema Luciana.

    “Basi usijali. Twende.”

    Alifanya mambo mengi, alifanya ufuska mpaka kufikia hatua kuona kwamba ilikuwa imetosha. Alikusanya kiasi kikubwa cha pesa, akaunti yake ikajaa pesa, hakukuwa na kitu alichokihitaji kwa wakati huo zaidi ya kuwa na mwanaume mmoja tu.

    Mtu aliyekuwa akimfikiria kwa wakati huo ni huyo mwanaume aliyeambiwa kwamba alikuwa mzuri wa sura, mvulana aliyewavutia wanawake wengi lakini hakukuwa na yeyote aliyefanikiwa kumpata.

    Kwake, Luciana hakuwa na tatizo lolote, alijua kwa namna moja au nyingine ilikuwa ni lazima mwanaume huyo amkubali kwa sababu tu alikuwa mzuri wa sura, msichana aliyependwa na wanaume wote, waliokuwa na fedha na hata wale ambao hawakuwa na kitu.

    Kilipita kipindi kirefu hakuwa amekwenda chuo. Siku ambayo alifika chuoni hapo, wanaume walipomuona, macho yakawatoka, msichana huyo alipotea kwa kipindi fulani na siku hiyo ambayo alifika chuoni hapo alionekana kuwa mrembo hasa, mara tano ya jinsi alivyokuwa kipindi cha nyuma.

    Alifika chuoni hapo kwa lengo la kumuona mwanaume aliyezungumzwa sana na rafiki yake, mwanaume aliyekuwa mzuri wa sura ambae aliamini kwamba hata yeye mwenyewe angeweza kumpenda.

    “Yupo wapi?”

    “Nani?”

    “Si huyo mwanaume uliyesema ni mzuri!”

    “Twende kule, nilimuona sehemu ya kulia chakula,” alisema Selina.

    Hawakutaka kubaki mahali hapo, walichokifanya ni kwenda sehemu iliyokuwa ikihusika na uuzaji wa chakula. Walipofika kule, wakaanza kuyapeleka macho yao huku na kule na kwa bahati nzuri macho yao yakatua kwa mwanaume waliyekuwa wakimtafuta.

    “Luciana....”

    “Abeee...”

    “Mwanaume mwenyewe yule pale,” alisema Selina huku akimuonyeshea Luciana sehemu aliposimama mwanaume huyo.

    Luciana alipomuona, kwanza akatoa mguno, hakuonekana kuamini kama duniani kulikuwa na mwanaume mzuri kama alivyokuwa yule ambaye alionyeshewa mahali pale. Moyo wake ukaanza kubeba kitu kizito, shauku kubwa ikamuingia moyoni mwake, akajikuta akiwa hajiwezi.

    “Selina...is that the one?” (Selina...yule ndiye mwenyewe?) aliuliza Luciana huku akionekana kutokuyaamini macho yake.

    “He is the one.” (Ndiye mwenyewe)

    Luciana hakutaka kubaki mahali hapo, hakuona kama alitakiwa kusimama zaidi, akili yake ilichanganyikiwa mno, hakuamini kama katika dunia hii kungekuwa na mwanaume mzuri kama alivyokuwa yule aliyeonyeshewa, tena kutoka barani Afrika.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akashindwa kuvumilia, akajikuta akianza kupiga hatua kumfuata. Mahali pale kulikuwa na gumzo, kitendo cha msichana Luciana kuonekana mahali hapo kilimchanganya kila mwanaume aliyemwangalia.



    Umaarufu wake, uzuri wake uliwadatisha watu wengi, wanaume wakabaki kimya huku wakimwangalia, hawakuamini kama yule Luciana ambaye kila siku alionekana kuwa mrembo, leo alikuwa mara tano ya zaidi ya urembo aliokuwa nao kabla.

    Alipomfikia kijana yule, akamshtua kwa kumshika bega, alipogeuka, macho ya mwanaume yule yakatua usoni mwa msichana aliyeonekana kuwa mrembo mno, msichana ambaye urembo wake alihisi kwamba hakuwahi kuuona sehemu yoyote ile.

    “My name is Luciana, a beautiful girl you have never met,” (Jina langu ni Luciana, msichana mrembo ambaye haujawahi kukutana naye) alisema Luciana huku akiachia tabasamu.

    “My name is Dickson.” (Ninaitwa Dickson).

    Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa wawili hawa kukutana, walipoonana kwa mara ya kwanza, kila mtu akatokea kumpenda mwenzake. Wasichana walichanganyikiwa na uzuri aliokuwa nao Dickson lakini kwa upande wa pili hata wanaume walichanganyikiwa na uzuri aliokuwa nao Luciana.

    Wawili hao wakatengeneza muunganiko wa hatari, kila aliyekuwa akiwaangalia alibaki akitabasamu tu kwani watu hao kama walijua jinsi walivyokuwa wazuri, hivyo waliamua kuchaguana.

    Katika kipindi cha kwanza Dickson alimkumbuka sana msichana wake aliyemuachana nchini Tanzania, Evadia, aliwasiliana naye mara chache chache lakini baada ya kuwa karibu na Luciana, akaanza kumsahau msichana huyo aliyekuwa nchini Tanzania.

    Penzi likamteka, hakuwa na sababu ya kumpenda msichana kama Evadia, kwake, alimuona msichana huyo kuwa wa kawaida sana, msichana masikini ambaye aliamini katika maisha yake asingeweza kumsaidia kwa lolote lile.

    Baada ya kuwa na Dickson, hata maisha ya Luciana yakabadilika, hakuwa kama jinsi alivyokuwa kipindi cha nyuma, akaacha tabia yake ya kufuata wanaume wengi, alijiahidi kwamba angekuwa mwaminifu na hicho ndicho kilichotokea.

    Kwa Luciana, akafika, hakutaka kusikia lolote lile kutoka kwa mwanaume yeyote yule. Wanaume wengi wakaendelea kumchombeza kwa maneno matamu tena wengine wakiweka pesa mezani lakini moyo wa Luciana ulibadilika kabisa, alichokifikiria kwa wakati huo hakikuwa pesa tena, yalikuwa ni mapenzi ya dhati ambayo aliyapata kutoka kwa Dickson ambaye alikuwa amemuacha msichana aliyekuwa naye nchini Tanzania, Evadia kwa ajili yake.



    Moyo wake ulijeruhiwa, kama ni mtu, tayari aliumwa na nyoka hivyo hata alipokuwa akiguswa na ujani, alishtuka. Moyo wake ukabadilika, kitendo alichofanyiwa na Dickson kilimuumiza mno na kujiahidi kwamba milele yote asingeweza kuwa na mwanaume hivyo alipaswa kumkatalia kila mwanaume aliyekuja mbele yake.

    Chuki kubwa ikamkamata moyoni mwake, hakuamini kama wanaume aliokuwa akiwachukia kipindi hicho, kulikuwa na mwanaume mwingine ambaye alianza kumfuatilia, mwanaume asiyemfahamu ambaye aliamua kuacha kazi zake kwa ajili yake.

    Alipomuona Laurence akimfuatilia, alichukia, aliyachukia mapenzi hivyo hakutaka kuwa na mwanaume yeyote yule. Mama yake alilifahamu hilo, kila alipomuona Laurence, alimfukuza kwa kumwambia aondoke kwani binti yake hakutaka kuonana naye.

    “Ninahitaji kumuona Evadia,” alisikika Laurence.

    “Evadia!”

    “Ndiyo mama!”

    “Huwezi kumuona.”

    “Kwa nini jamani?”

    “Nimesema huwezi. Hunielewi?”

    “Siwezi kukuelewa mpaka nimuone,” alisema Laurence.

    Japokuwa alikatawaliwa sana na Evadia lakini hakutaka kusikia, hakutaka kuacha kumfuatilia, kwake, msichana huyo alionekana kuwa kila kitu, alimpenda kwa mapenzi ya dhati kutoka moyoni, hakutaka kuwa na msichana mwingine zaidi ya Evadia tu.

    Mama yake Evadia alimkatalia kuonana naye tena huku akimtaka kuondoka nyumbani hapo lakini Laurence hakutaka kuondoka. Maisha aliyokuwa akiyaleta mahali hapo yalionekana kuwa kama filamu fulani ya kimapenzi lakini kile kilichokuwa kikitokea, alikimaanisha kwa asilimia mia moja.

    “Siondoki mpaka nimuone Evadia,” alisema Laurence huku akikaa nje ya nyumba ya kina Evadia.

    Mama Evadia hakutaka kujali sana, alichokifanya ni kuingia ndani na kuufunga mlango huku tayari ikiwa saa moja usiku. Laurence hakutaka kuondoka mahali hapo, wakati mwingine hata yeye mwenyewe alibaki akijishangaa kwamba ilikuwaje amng’ang’anie msichana mmoja namna hiyo, hakutaka kujali sana, aliendelea kusubiri zaidi na zaidi na hata kama ingewezekana kulala mahali hapo, alikuwa tayari.

    Mbu walimuuma, aliwaua na kuendelea kumsubiri msichana huyo. Alikuwa ndani, hakutaka kuingia kumfuata, alitaka msichana huyo atokea na kuzungumza naye kwani siku moja kwake pasipo kuona ilikuwa ni adhabu kali ya kaburi.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Muda ulizidi kuyoyoma, saa mbili ikaingia, saa tatu, saa nne, saa tano lakini bado Laurence hakuondoka mahali hapo.

    Ndani, Evadia alikuwa ametulia kitandani, moyo wake ulimuuma mno, bado alikuwa kwenye maumivu makali ya kukataliwa na mwanaume aliyempenda kwa moyo wa dhati.

    Alilia usiku kucha, kila siku akawa mtu wa kumlalamikia Mungu kwa kile kilichotokea, alijutia kitendo chake cha kuwa na mwanaume huyo ambaye mwisho wa siku alimsababishia maumivu makali ya moyo.

    Mama yake alipomwambia kwamba Laurence alikuwa nje akimsubiria, alikunja uso wake, alionekana kuwa na hasira kali mno. Hakutaka kuwa na mwanaume yeyote kwa kipindi hicho, alitaka kubaki peke yake, aishi peke yake na hata kama angezeeka, alitamani kuzeeka akiwa peke yake.

    Ilipofika saa tano na nusu usiku, Evadia akaelekea sebuleni ambapo akalifuata pazia chakavu na kuchungulia nje, alimuona Laurence amekaa kibarazani huku akiwa amejikunyata, baridi lilimpiga na mbu kumng’ata lakini hakutaka kuondoka mahali hapo.

    Huruma ikamuingia, akajikuta akiufuata mlango na kuufungua, akasimama mlangoni na kumwangalia Laurence ambaye naye alibaki akimwangalia machoni, tabasamu likaanza kuonekana usoni mwake.

    Laurence hakutaka kuishia hapo tu, alichokifanya ni kusimama na kumfuata Evadia pale mlangoni aliposimama na kuanza kuzungumza naye.

    “Hii yote kwa ajili yako,” alisema Laurence, alikuwa akianza kutetemeka kwa baridi kali la usiku.

    “Laurence...”

    “Nakusikiliza.”

    “Naomba uniache, sipo sawa,” alisema Evadia.

    “Najua Evadia. Macho mekundu, umenyong’onyea, ila naweza kukupa furaha maishani mwako,” alisema Laurence.

    “Najua Laurence....ila naomba uniache.”

    “Siwezi Evadia. Niambie tatizo nini.”

    “Basi tu.”

    “Hapana! Kuna kitu! Naweza kukupa mawazo pia, unachotakiwa ni kuniamini tu.”

    “Naomba tufanye siku nyingine. Rudi nyumbani.”

    “Unadhani nitakuwa na furaha? Unadhani nitakuwa katika hali ya kawaida? Evadia, ninakupenda, unalijua hilo, siwezi kurudi nyumbani huku nikikuacha katika hali hiyo, naomba uniambie, nini kinaendelea,” alisema Laurence huku akionekana kulengwa na machozi.

    “Mapenzi yanauma Laurence.....” alisema Evadia, hapohapo akaanza kububujikwa na machozi.

    Laurence akasikia maumivu makali moyoni mwake, alichokifanya ni kumsogelea zaidi Evadia kisha kumkumbatia, akaanza kumbembeleza kwa kumpigapiga mgongoni. Hakutaka kumuona msichana huyo akilia, akiumia kwa kitu chochote kile.

    Kwa jinsi alivyokuwa akiumia, hata naye maumivu yake yalikuwa vilevile. Machozi ya Evadia yakatiririka na kuulowanisha mgongo wake kwani bado walikuwa wamekumbatiana tu.

    “Usilie...”

    “Inauma Laurence....”

    “Ninaahidi kukupa furaha na kukusahaulisha kwa kila kitu,” alisema Laurence.



    Utajiri wake mkubwa aliokuwa nao ulikuwa siri kubwa, hakutaka Evadia afahamu au hata mama yake ajue hali halisi ya maisha yake. Jina lake lilikuwa kubwa nchini Tanzania lakini bahati mbaya watu hawakuwa wamemuona hivyo kuwa na shauku ya kutaka kujua kwamba huyu bilionea Laurence alikuwaje, alifananaje na aliishi vipi.

    Hakuacha kwenda nyumbani kwa kina Evadia, kidogo kwa wakati huo hali ilikuwa afadhali, msichana huyo hakuwa mtu wa kuwa na majonzi wakati wote, kwa Laurence, mwanaume huyo alijitahidi kumpa furaha.

    Hakumpa ruhusa msichana huyo kufika nyumbani kwake, alichokuwa akikifanya ni kumfuata kwao na kuzungumza naye, kama walitakiwa kutoka, walitoka kwenda sehemu, walizungukazunguka na kurudi.

    “Laurence...” aliita Evadia.

    “Naam.”

    “Hivi unaishi wapi?”

    “Kwani hupajui?”

    “Sipajui.”

    “Kweli?”

    “Kweli! Hujaniambia.”

    “Naishi Manzese Midizini.”

    “Na unafanya kazi wapi?”

    “Mmh! Mbona maswali mengi jamani?”

    “Kwani ni vibaya nikijua?”

    “Si vibaya sana, ila usijali. Nafanya kazi katika Ofisi ya Kata ya Manzese, nimeajiriwa pale kama fundi umeme,” alijibu Laurence.

    “Kumbeee!”

    “Ndiyo! Samahani kwa kukuficha kwa muda mrefu.”

    “Usijali.”

    “Leo wapi?”

    “Twende popote pale, nitakuwa na furaha kwa kuwa nipo pamoja nawe,” alijibu Evadia.

    Kwa kipindi chote hicho, Laurence hakutaka kumwambia ukweli Evadia namna alivyokuwa. Alijifanya kuwa mtu wa kawaida, hakutaka kujulikana kwa msichana huyo kama alikuwa bilionea.

    Waliondoka nyumbani kwa kina Evadia na kwenda Manzese Darajani, huko, walisimama juu na kupiga picha. Kwa Evadia ilikuwa ni furaha pekee, aliwahi kuwa na mwanaume mwenye fedha na matokeo yake kilichotokea ni kitu kilichomuumiza mno.

    Leo hii alikuwa na mwanaume mwingine, alikuwa bilionea mkubwa nchini Tanzania lakini Evadia hakufahamu hilo, kila alipomwangalia Laurence, jinsi alivyokuwa akivaa, simu aliyokuwa akiitumia, alionekana mtu wa kawaida sana.

    Walisimama katika daraja la Manzese, walikuwa wakiangalia huku na kule, kila mmoja alionekana kuwa na furaha mno. Evadia alifarijika sana, upendo wa dhati alioupata kwa mwanaume huyo ulikuwa tofauti kabisa.

    “Najifunza mengi sana kutoka kwako mpenzi,” alisema Evadia, Laurence akashtuka kusikia hivyo kwani kwa kipindi chote hicho hakuwahi kuitwa mpenzi.

    “Kama yapi?”

    “Ni bora kuwa na mpenzi asiyekuwa na kitu kuliko kuwa na mpenzi mwenye fedha,” alisema Evadia.

    “Kwa nini?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wenye fedha wanaringa, wanajiona wao ndiyo wao, ila mkikutana masikini msiokuwa na kitu kama tulivyo, kila kitu kinakwenda sawa,” alisema Evadia huku akiachia tabasamu.

    “Najua hilo mpenzi. Maisha ya mapenzi ni mapenzi, fedha haina nafasi katika mapenzi,” alisema Laurence.

    Walizungumza mambo mengi, bado Evadia hakujua mtu aliyekuwa naye alikuwa wa namna gani. Kitu alichokijua ni kwamba Laurence alikuwa masikini wa kutupwa, aliyaamini maneno yake kwamba alikuwa mtu asiyekuwa na fedha, yaani alikuwa fukara kama alivyokuwa.

    Baada ya kuzungumza naye kwa kipindi kirefu darajani, wakateremka na kuanza kuondoka mahali hapo. Walitakiwa kupanda daladala kutoka hapo Manzese mpaka Mburahati lakini hilo lilishindikana kwani kwa maneno ya Laurence, mfukoni hakuwa na kitu.

    “Kwa hiyo?” aliuliza Evadia.

    “Tutembee tu, au una hela yoyote hapo?”

    “Mmh! Sina.”

    “Basi tutembee, baadaye nitarudi hukuhuku Manzese,” alisema Laurence.

    Wakaanza kutembea huku wakizungumza mambo mengi. Ilikuwa ni ngumu mno kwa Evadia kugundua kwamba mtu aliyekuwa naye alikuwa bilionea mkubwa Tanzania, tena hata yeye mwenye alimsikia sana.

    Katika kipindi chote hicho Laurence alionekana kuwa na furaha mno, kuwa na Evadia katika maisha yake hakika kilikuwa kitu kilichompa furaha sana katika maisha yake. Walichukua dakika arobaini wakafika nyumbani kwa kina Evadia, wakamkuta mama Evadia akiwa nje.

    “Nimemrudisha nyumbani,” alisema Laurence mara baada ya salamu.

    “Sawa. Karibu tena Laurence.”

    “Asante mama.”

    Laurence akamsogelea Evadia na kumbusu shavuni, alipomaliza, akaondoka zake kurudi nyumbani. Alipofika njiani, akasimamisha bodaboda, akapanda na kuelekea nyumbani. Kila kitu alichokuwa akikifanya, alikifanya kimakusudi, hakutaka apendwe na msichana huyo kwa sababu ya fedha tu.



    Siku iliyofuata, asubuhi na mapema Laurence akajiandaa kwa ajili ya kwenda kumtembelea mpenzi wake. Kwa wakati huo, hata kazi hakutaka kufanya, alitaka kuweka mambo sawa kabisa, hakutaka kuwa bize na kazi kwani ukaribu wake na Evadia ulikuwa kitu cha muhimu kuliko vitu vingine.

    Alipomaliza kujiandaa, kama kawaida yake akachukua bodaboda na kuelekea huko. Njiani, mawazo yake yalikuwa kwa Evadia tu, alimuona kuwa na thamani mno, alipenda zaidi ya mtu yeyote katika dunia hii.

    Alipofika nyumbani kwa kina Evadia, kitu kilichomshangaza ni kwamba mlango ulikuwa umefungwa kitu ambacho hakikuwa kawaida kabisa. Laurence akachanganyikiwa, alijaribu kuufungua mlango ule, ulikuwa umefungwa kwa ufunguo, hakuishia hapo, alichokifanya ni kuanza kuita, ukimya mkubwa ulitawala ndani.

    “Evadiaaaa...Evadiaaaa...” aliita huku akiwa amesimama nje ya nyumba ile, hakukuwa na sauti yoyote iliyosikika kutoka ndani.

    Alijaribu kuzunguka mpaka nyuma ya nyumba ile huku akiendelea kuita lakini bado ukimya uliendelea kutawala mahali hapo. Hakujua ni kitu gani kilikuwa kimeendelea, alichokifanya ni kwenda kwa majirani na kuwauliza juu ya hali iliyokuwa ikiendelea mahali pale.

    “Walikwenda hospitali asubuhi sana,” alijibu jirani mara baada ya kuulizwa.

    “Nani anaumwa?”

    “Evadia. Ugonjwa wake uleule.”

    “Upi?”

    “Wanasema figo yake moja ina matatizo na ndiyo maana mara kwa mara anazimiazimia,” alijibu jirani huyo.

    “Wamekwenda hospitali gani?”

    “Mmh! Sijui! Ila nadhani Palestina, nenda huko kajaribu kumtafuta,” alijibu jirani huyo.

    Laurence akachanganyikiwa, kile alichoambiwa kilimchanganya kichwa chake. Akabaki akijiuliza juu ya ugonjwa uliokuwa ukimsumbua mpenzi wake, hakuwa ameambiwa kabla japokuwa kuna siku mama yake Evadia alimwambia kwamba alizimia.

    Hakutaka kubaki mahali hapo, alichokifanya ni kuondoka nyumbani hapo, kwa kasi kubwa na kuelekea huko hospitali. Akachukua bodaboda na kuelekea huko huku akionekana kuchanganyikiwa mno.

    Japokuwa dereva alikuwa akiendesha bodaboda kwa mwendo wa kasi, yeye aliona akiendesha kwa mwendo mdogo hali iliyomfanya kumwambia dereva huyo aongeze kasi.

    “Vuta moto kaka! Vuta moto mpaka pikipiki ipae,” alisema Laurence.

    “Kaka! Kwa magari haya, tutakufa.”

    “Kufa si tatizo, unaogopa kufa?”

    “Mmmh!”

    “Wewe ongeza kasi, hizi hospitali zimewekwa kwa ajili yetu.”

    Alisema Laurence na hivyo dereva wa bodaboda kufanya kama alivyotaka mteja wake.

    Kama kuchanganyikiwa, Laurence alichanganyikiwa mno, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea, msichana aliyempenda, aliyeonekana kuwa kila kitu katika maisha yake alikuwa hoi hospitalini.

    Hakukuwa na kitu kilichomuumiza kichwa kama hicho, kila alipomwambia dereva bodaboda aongeze kasi, aliona aliendesha kwa kasi ndogo japokuwa dereva huyo aliongeza kwa kiasi kikubwa.

    Baada ya dakika chache, wakafika katika Hospitali ya Sinza Palestina na hapohapo Laurence akaruka kutoka katika bodaboda na kuanza kukimbia kuelekea ndani, yaani hata kumlipa dereva hela yake hakukumbuka kabisa.

    “Nimekuja kumuulizia mgonjwa wangu,” alisema Laurence, alikuwa amemsimamisha nesi mmoja aliyekuwa akipita mbele yake.

    “Nani?”

    “Anaitwa Evadia.”

    “Mmmh! Nenda kule kwa upande wa magonjwa ya wakinamama,” alisema nesi yule, hapohapo Laurence akaanza kuelekea huko.

    “Braza, hujanilipa hela yangu,” alisema dereva bodaboda baada ya kumsogelea. Hapohapo Laurence akaingiza mkono mfukukoni na kutoa noti ya shilingi elfu kumi, hakutaka kusubiri chenji, akaondoka zake.

    Laurence alionekana kuwa na haraka. Hakutaka kupoteza muda mahali hapo, alichokifanya ni kuelekea kule alipokuwa ameelekezwa, alipofika, akakuta kundi la wanawake wakiwa wamekaa kwenye mabenchi yaliyokuwepo mahali pale, kila mmoja akaanza kumwangalia.

    Laurence akayapitisha macho yake huku na kule, yakagongana na macho ya mama yake Evadia, hapohapo akaanza kumfuata.

    “Kuna tatizo gani mama?” aliuliza Laurence.

    “Evadia anaumwa.”

    “Anasumbuliwa na nini?”

    “Figo yake moja haifanyi kazi vizuri, huwa inafeli,” alisema mama yake Evadia, Laurence akashusha pumzi ndefu na nzito.

    “Yupo wapi kwa sasa?”

    “Amelazwa ndani, daktari aliniambia nisubiri nje, wanamshughulikia,” alijibu mwanamke huyo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Laurence akaungana naye mahali pale. Wote wawili walionekana kuwa na mawazo lukuki, Laurence alikuwa akimfikiria mpenzi wake tu kwamba ni kwa namna gani angeweza kupata matibabu yanayotakiwa.

    Hakutaka kuonekana kama ana fedha nyingi, hakutaka ajulikane kama alikuwa bilionea lakini kwa jinsi hali ilivyokuwa ikienda, alionekana kuwa na wasiwasi kwamba ilikuwa ni lazima ijulikane kwani asingekubali kuona msichana aliyekuwa akimpenda kwa mapenzi ya dhati akifa.

    Walikaa kwa saa mbili ndipo walipofuatwa na daktari na kuambiwa kwamba waende ndani kumwangalia Evadia. Kitendo cha Laurence kumuona mpenzi wake akiwa kimya kitandani, moyo wake ukanyong’onyea, huzuni ikaanza kuugubika moyo wake, akashindwa kuvumilia, machozi yakaanza kumbubujika.

    “Amka mpenzi, amka unitazame,” alisema Laurence huku machozi yakiendelea kumbubujika.

    Evadia alikuwa kimya kitandani, kwa kumwangalia, lisingekuwa jambo jepesi kuamini kwamba mtu huyo bado alikuwa hai, kuna kipindi Laurence alionekana kuwa na hofu hivyo kusikiliza mapigo yake ya moyo ili kuona kama yalikuwa yakiendelea kudunda au yalisimama, aliyasikia yakidunda.

    Wakati wakiendelea kumwangalia msichana huyo kitandani pale, mlango ukafunguliwa na daktari mmoja, mwanamke aliyevalia koti refu jeupe kuingia ndani ya chumba kile.

    “Bado hajafumbua macho dokta,” alisema Laurence huku mashavu yake yakiwa yamelowanishwa na machozi.

    “Naomba nizungumze nanyi, mnaweza kunifuata,” alisema daktari yule.

    Hakukuwa na mtu aliyebisha, walichokifanya ni kusimama mahali pale na kisha kumfuata daktari yule ambaye safari yake iliishia ndani ya chumba kimoja, ilikuwa ni ofisi yake.

    Wakaingia ndani na kukaribishwa katika viti vilivyokuwa humo ndani. Walipokaa, daktari yule akachukua miwani yake iliyokuwa mezani na kuivaa, akachukua mafaili yaliyokuwa mezani mwake na kuyaangalia vilivyo.

    “Kuna nini?” aliuliza Laurence huku akionekana kuwa na hofu tele.

    “Mgonjwa wenu anatakiwa kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa uchunguzi zaidi,” alijibu daktari yule.

    “Tatizo nini?”

    “Anasumbuliwa na figo, haiwezi kufanya kazi kama inavyotakiwa,” alijibu daktari yule.

    “Sawa!Hakuna tatizo.”

    Laurence hakutaka kusikiliza sana daktari alisemaje, aliufahamu ugonjwa huo, watu wengi walikuwa wakifa kwa kukosa figo moja tu iliyokuwa na nguvu, aliuogopa ugonjwa huo, alikuwa tayari kuona lolote likitokea lakini si kumuona mpenzi wake huyo akifariki dunia.

    Siku iliyofuata, Evadia akarudiwa na fahamu, hawakutaka kuzungumza naye, waliambiwa kutokufanya hivyo, wakamchukua na kuelekea katika hospitali ya Taifa. Walipofika huko, msichana huyo akapewa kitanda na madaktari kuanza kazi yao.

    “Unajisikiaje?” aliuliza Laurence huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana.

    “Naendelea vizuri. Nashukuru kwa kuwa nami hatua kwa hatua,” alisema Evadia huku akijitahidi kutoa tabasamu pana.

    “Mbona haukuniambia kwamba unaumwa?”

    “Niliogopa kufanya hivyo.”

    “Kwa nini?”

    “Basi tu. Kwa jinsi ulivyokuwa ukinipenda, nilihisi kamba ungehuzunika zaidi,” alisema Evadia.

    “Hata kama mpenzi, ulitakiwa kuniambia.”

    “Naomba unisamehe.”

    “Usijali.”

    Walikaa na kuzungumza mengi, mama yake alikuwa pembeni yake, kila wakati alionekana kuwa mtu mwenye furaha mno, hakuamini kama binti yake kidogo angeendelea vizuri kama ilivyokuwa.

    Mara baada ya kukaa naye kwa dakika thelathini, mlango ukafunguliwa na daktari wa kiume kuingia, alikuwa mzee mwenye ndevu nyingi, alipoingia tu, akawataka kutoka nao nje.

    “Kuna nini?”

    “Njooni mara moja.”

    Akawachukua na kuelekea nao ofisini mwake. Tayari wawili hao walionekana kuwa na hofu, uso wa daktari yule ulionekana kuwa na jambo kubwa lililokuwa likitokea ambalo kwa namna moja au nyingine hakutaka kulizungumza mbele ya mgonjwa wodini mule.

    “Kuna nini?” aliuliza Laurence huku akionekana kuwa na hofu.

    “Figo moja ya mgonjwa wenu haifanyi kazi kama inavyotakiwa, ni lazima tufanye kidney transplant,” alisema daktari.

    “Ndiyo nini hiyo?” aliuliza mama yake Evadia.

    “Tumuwekee figo moja kwani kati ya mbili alizokuwa nazo, moja imeharibika na haifanyi kazi kama inavyotakiwa,” alijibu daktari huyo aliyeitwa Haji Mukhandi.

    “Hiyo figo nyingine tutaitoa wapi?” aliuliza mama yake Evadia.

    “Hilo ni swali gumu kwa sasa, figo haipatikani bure, ni lazima kitolewe kiasi cha fedha ili kumhamasisha mtu kutoa figo yake kwa ajili ya mgonjwa,” alijibu Dk. Mukhandi.

    “Kiasi gani?”

    “Si chini ya milioni ishirini.”

    “Unasemaje?” aliuliza mama yake Evadia huku akionekana kushtuka.

    “Ndiyo hivyo.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mama Evadia akachanganyikiwa, hakuamini kile alichoambiwa kwamba zilihitajika zaidi ya milioni ishirini ili binti yake aweze kuwekewa figo nyingine ili arudi katika hali yake ya kawaida.

    Moyoni mwake alifikiria ni kwa namna gani angeweza kupata kiasi hicho cha fedha kwani kilikuwa kikubwa sana ambacho kamwe asingeweza kukipata. Alihisi moyo wake ukimuuma sana, hakuwa na fedha, hakuwa na kitu chochote kile, kwa maana hiyo kitendo cha binti yake kuwa na figo moja inayofanya kazi kilionekana kuwa kitu cha hatari sana na ndiyo maana mara kwa mara alikuwa mtu wa kuzimiazimia tu.

    Mbele yake aliona giza, hakujua pa kuanzia, kitu pekee alichokifikiria ni kurudi mitaani na kuomba michango kutoka kwa watu wengine, ndugu, jamaa na marafiki, lakini hata kama angewachangangisha watu wengi, kiasi kilichohitajika kilikuwa kikubwa mno.

    “Kwa hiyo tufanyeje?” aliuliza Laurence huku akionekana kuwa mwenye majonzi.

    “Nitakwenda mitaani kuomba michango,” alijibu mwanamke huyo huku akijaribu kuyafuta machozi yaliyokuwa yakimbubujika mashavuni mwake.



    Japokuwa mama Evadia alijitahidi kwa nguvu zote kuzunguka huku na kule kwa ajili ya kutafuta mchango ili binti yake abadilishwe figo lakini kiasi alichokipata hakikuweza kufika kama kilivyotakiwa.

    Mbele yake aliona giza kubwa, hakujua ni kipi alichotakiwa kufanya kipindi hicho. Miaka ya nyuma alimpoteza mume wake, leo hii, binti yake pekee aliyebaki katika maisha yake alikuwa akiumwa mno na hali yake ilikuwa mbaya sana.

    Alishinda akilia, kila alipokwenda hospitalini, alikaa pembeni ya binti yake na kuanza kulia kama kawaida yake. Laurence hakuacha kufika hospitalini hapo, kila siku alifika, alishinda na Evadia, walizungumza mengi huku akimpa moyo kwamba angepona na kurudi katika hali ya kawaida kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

    Maneno hayo yalimtia nguvu Evadia, hakutegemea kupata mwanaume ambaye angejitolea kama alivyojitolea Laurence. Alifahamu fika kwamba mpenzi wake huyo alikuwa masikini wa kutupwa lakini hiyo haikuwa sababu ya kutaka kutokuwa naye, huyohuyo masikini ndiye ambaye leo hii alikuwa naye katika kila hatua aliyopitia hospitalini pale.

    Wakati wote watatu wakiendelea kuwa ndani ya chumba kile, ghafla mlango ukafunguliwa na Dk. Mukhandi kuingia ndani, uso wake ulikuwa tofauti na jinsi alivyokuwa kipindi cha nyuma, alionyesha tabasamu pana. Kila mtu aliyemwangalia daktari huyo akajua kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.

    “Kuna habari njema,” alisema daktari huyo, wote wakasimama na kumwangalia.

    “Habari gani?” aliuliza Laurence huku akijifanya kushtuka.

    “Kuna mtu amejitokeza na kutoa milioni thelathini kwa ajili ya Evadia,” alisema daktari huyo, kila mmoja akashtuka.

    “Milioni thelathini?”

    “Ndiyo!”

    “Nani?” aliuliza Laurence huku macho yake yakiwa na mshtuko mno.

    “Anaitwa Matilda John, mwanamke mmoja, alisema anafanya kazi Umoja wa Mataifa, alizipata taarifa za Evadia hivyo ameamua kumsaidia,” alijibu daktari.

    “Mwanamke? Mhh! Alijuaje kama Evadia anaumwa na anahitaji kiasi hicho cha fedha?” aliuliza Laurence.

    “Hata mimi sijui, imekuwa ni miujiza mno ambayo haikuwahi kutokea,” alijibu daktari huyo.

    Kila mmoja alibaki na maswali moyoni mwake, hakukuwa na mtu aliyefahamu hilo zaidi ya Laurence ambaye kiasi kile cha fedha alikitoa yeye kupitia kwa mfanyakazi wake aitwaye Matilda ambaye alifika hospitalini hapo na kujifanya msamaria mwema.

    Hakutaka kitu chochote kile kijulikane, na hata daktari alipokuwa akiwaambia kuhusu jambo hilo, hata yeye mwenyewe alijifanya kuwa na mshangao na aliuliza maswali mengi kama kuwapa upofu watu hao wasijue kitu chochote kile.

    Kwa kuwa kiasi hicho cha fedha kilitolewa, kilichofuata ni kuwekwa kwa matangazo katika baadhi ya magazeti ambapo wakaandika kwamba mtu yeyote aliyekuwa tayari kutoa msaada wa figo alitakiwa kufika hospitalini hapo.

    Wiki iliyofuata, zaidi ya watu mia moja wakawa wamefika hospitalini hapo tayari kwa kupimwa ili kuangalia vinasaba kama vinaendana na vinasaba vya Evadia.

    “Ila nitahitaji milioni ishirini,” alisema jamaa mmoja kwa kutoa figo yangu.

    “Hakuna tatizo, njoo ndani,” alisema Dk. Mukhandi.

    Waliwapima watu wote ili kuona kama vinasaba hivyo viliendana, kitu kilichomuumiza kila mtu, hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa tayari kutoa figo yake ambaye vinasaba vyake vilifanana na vinasaba vya Evadia.

    “Mungu wangu!” alisema Dk. Mukhandi.

    “Kuna nini?”

    “Hakuna mtu ambaye vinasaba vyake vinaendana na Evadia.”

    “Unasemaje?”

    “Ndiyo hivyo!”

    “Watu wote hao hakuna?”

    “Hakuna.”

    Kila mmoja alichanganyikiwa, hawakujua ni kitu gani kilichotakiwa kufanyika mahali hapo. Mama Evadia na Laurence wakaitwa ndani ya ofisi ya daktari na kuambiwa kile kilichokuwa kimetokea, kila mmoja alisikitika mno.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Imeshindikana?” aliuliza Laurence.

    “Ndiyo! Hakuna hata mmoja!” alijibu daktari yule. Kilio kikaanza kusikika kutoka kwa mama yake Evadia.



    ITAENDELEA

THE LOVE YOU HAD BEFORE (PENZI ULILOKUWA NALO KABLA) - 1

 





    IMEANDIKWA NA : NYEMO CHILONGANI



    *********************************************************************************



    Simulizi : The Love You Had Before (Penzi Ulilokuwa Nalo Kabla)

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    Glorious Worship Event (GWE) lilikuwa moja ya matamasha ya kusifu na kuabudu yaliyokuwa yakiandaliwa na kanisa kubwa nchini Tanzania, kanisa lililokuwa chini ya mchungaji mwenye upako, mchungaji mpakwa mafuta wa Bwana, Mchungaji Michael Yekonia wa Kanisa la Praise And Worship lililokuwa Mwenge jijini Dar es Salaam.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Vijana wengi kutoka katika makanisa mbalimbali walikuwa wakikutana katika Uwanja wa Taifa uliokuwa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusifu na kumuabudu Mungu kisha kusikiliza maneno ya Mungu kwa dakika kadhaa kabla ya sifa na kuabudu kuendelea.

    Wanachuo, wanafunzi waliosoma bweni waliomba ruhusa shuleni kwao ili kwenda kushiriki katika tukio hilo lililokuwa gumzo nchini Tanzania, tukio lililoripotiwa kila kona nchini Tanzania na kulifanya kuwafikia watu wengi zaidi na hivyo kuongeza idadi ya watu walioshiriki.

    Vijana zaidi ya laki mbili walikuwa wakikusanyika uwanjani hapo, waimbaji mbalimbali wa kimataifa kutoka Afrika Kusini, Marekani, Nigeria, Botswama na nchi nyingine nyingi walifika katika tukio hilo ambapo kulikuwa na kazi moja ya kusifu na kuabudu tu.

    Kwaya mbalimbali kutoka katika makanisa mengi jijini Dar es Salaam zilipewa nafasi za kuimba, waimbaji binafsi nao hawakuwa nyuma, kila mmoja aliyetaka kuimba siku hiyo ndiyo ilikuwa siku yake.

    Kupitia tukio hilo kubwa, vijana wengi walikuwa wakionana, walijenga urafiki na hata wengine kujikuta wakiwa kwenye uhusiano wa kimapenzi ambao moja kwa moja yalileta ndoa. Tukio hilo lilipendwa, makanisani, vijana walilizungumzia mno, kila mmoja alitaka kushiriki, akutane na vijana wenzake na kisha kuanza kumuimbia Mungu.

    Katika tukio la GWE la mwaka huo, zaidi ya vijana laki moja na nusu walikuwa wamefika uwanjani hapo, kila mmoja alifika akiwa na dhamira moja tu ya kumsifu na kumwabudu Mungu. Waliotaka kucheza kama watu waliochanganyikiwa, walifanya hivyo, waliotaka kusali mpaka kulia, wote walikuwa na uhuru.

    Hakukuwa na utulivu, kila mmoja alicheza na kurukaruka, uwepo wa Mungu ulionekana mahali hapo, waliokuwa wagonjwa, kupitia nyimbo za sifa zilizokuwa zikiimbwa uwanjani hapo wakajikuta wakipokea uponyaji hata kabla kipindi cha maombezi kufika.

    Miongoni mwa watu waliokuwa katika uwanja huo, ndani ya tukio hilo alikuwepo kijana mtanashati, kijana aliyekuwa na muonekano wenye fedha, sura ya upole, huyu aliitwa Laurence Mathew.

    Kwa kumwangalia mara moja, usingepata wakati mgumu kugundua kwamba kijana huyo alikuwa na fedha au alitoka katika familia yenye fedha. Alikuwa na muonekano wa bei na hata mavazi yake aliyoyavaa yalikuwa ni ya bei mbaya.

    Siku hiyo katika kipindi cha kusifu na kuabudu, hakutulia, alicheza mno, jasho lilimtoka, hakuangalia mavazi yake, hakuangalia kama alikuwa tajiri, alichokuwa akikifanya ni kucheza mpaka kuvua shati, alionekana kama kujitoa fahamu.

    Hakukuwa na mtu aliyemwangalia mwenzake, kila mmoja alijali yake. Kwa Laurence ilionekana kuwa nafuu kwani kulikuwa na watu wengine ambao walicheza, walirukaruka mpaka nguo kuwavuka, hawakujali, walichokuwa wakikifanya ni kumsifu Mungu aliye hai.

    “Bwana Yesu asifiweeeeee....” ilisikika sauti ya mchungaji Yekonia aliyesimama jukwaani.

    “Ameeeeeeeeeeeen....” zilisikika sauti za watu wote waliokuwa uwanjani hapo, wakaanza kupiga vigelegele huku mikono yao ikiwa hewani.

    “Leo ni siku ya kipekee sana, ni siku ambayo tumekuwa tukiisubiri kwa kipindi kirefu, leo ni siku ya kumkanyaga shetani, ni siku ya kuacha mizigo yetu msalabani, Yesu alipokufa, alibeba mizigo yetu na hata alipofufuka, bado akatuachia msaidizi ambaye ni Roho Mtakatifu,” alisema mchungaji Yekonia huku akiwaangalia watu waliokusanyika uwanjani hapo.

    Hakuzungumza sana, hakutaka kupoteza muda wa watu uwanjani hapo, aliongea kwa dakika chache sana, akamkabidhi mtu wa sifa kipaza sauti kile kisha kuendelea kumsifu Mungu.

    Wakati watu wakiendelea kumsifu Mungu, ghafla macho ya Laurence yakatua kwa msichana mmoja aliyesimama pembeni yake, kama hatua kumi kutoka alipokuwa, msichana huyo alikuwa akiimba huku akicheza, kwa kumwangalia usoni, alikuwa na uzuri wa ajabu.

    Alifanana na mwanamuziki wa Marekani, Alicia Keys, uso wake ulionyesha kuwa na tabasamu pana lililomfanya kumvutia zaidi Laurence aliyebaki akiyatuliza macho yake kwa msichana huyo tu.

    “Haleluyaaa...” alijikuta akisema Laurence, macho yake yaliganda kwa msichana yule.

    Tayari akili yake ilikwishahama, kila alipomwangalia, tayari akaanza kupata maono, akajiona akisimama mbele ya kanisa, alikuwa amevaa suti na msichana huyo alivalia shela jeupe, walikuwa kanisani hapo kwa ajili ya tukio moja tu, kufunga ndoa na hatimaye kuwa mume na mke.

    Akaulizwa kama alikuwa tayari kumuoa msichana huyo, jibu lake lilikuwa lilelile alilotaka kulitoa, ndiyo alikubali na hata alipoulizwa msichana huyo, hawakutofautiana jibu lake na Laurence, naye alikubali kuolewa.

    Ghafla akatoka katika maono yale, akamwangalia vizuri msichana yule, alionekana kuwa msichana mpole, mwenye maisha duni kwani hata mavazi aliyoyavaa yalionyesha dhahiri kwamba msichana huyo hakuwa na maisha mazuri hata kidogo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Laurence hakutaka kusimama pale aliposimama, akajikuta akianza kupiga hatua za taratibu, tena huku akicheza mpaka karibu na msichana yule ambapo alipomwangalia vizuri, akagundua kwamba machozi yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake.

    “Bwana Yesu asifiwe,” alisalimia Laurence, msichana yule hakusikia kutokana na kelele zilizokuwa uwanjani hapo.

    “Bwana Yesu asifiweeee...” alimsalimia tena kwa sauti ya juu.

    “Unasemaje?” aliuliza msichana yule.

    “Nimekusalimia.”

    “Sijambo,” alisema msichana yule huku akionekana kutokuisikia salamu ile.

    Laurence hakutaka kuendelea kuzungumza na msichana yule, akajifanya kuwa bize kuimba kama wengine. Mawazo yake yalivurugika kabisa, akili yake ikahama, alihisi kuwa na mapenzi mazito juu ya msichana yule, kila alipomwangalia, aliona akimpenda kuliko mtu yeyote yule.

    Alionekana kustahili kuwa mke wake wa ndoa, muonekano wake wa upole, sura nzuri vilikuwa vitu vilivyomchanganya vilivyo. Hakutaka kufuatilia tena kilichokuwa kikiendelea uwanjani hapo, mawazo yalimjaa juu ya msichana yule huku akiwa na hisia kali za mapenzi zikiutawala moyo wake.

    Tamasha lile liliendelea mpaka lilipomalizika majira ya saa moja usiku. Mchungaji Yekonia akasimama na kisha kufunga kwa maombi mazito na kuwaruhusu watu kuondoka uwanjani hapo.

    Laurence hakutaka kusubiri, alichokifanya ni kuanza kutafuta mazoea na msichana yule, kila alipoongea hiki au kuuliza kitu fulani, jibu alilopewa lilikuwa la kukatisha tamaa, lililoonyesha kwamba msichana huyo hakutaka kuulizwa zaidi.

    “Unasali kanisa gani?”

    “Mburahati.”

    “TAG, Pentekoste au Anglikana?”

    “TAG.”

    Kila alichouliza, alijibiwa kifupi, tena huku uso wa msichana huyo ukionekana kuwa siriazi, hakuonekana kuwa tayari kuzungumza zaidi. Kwa Laurence, hali ilionekana kuwa mbaya, alishindwa kuelewa kama kweli angeweza kufanikiwa kuwa na msichana huyo au la.

    Alichokuwa akikihitaji kwake si kuwa msichana wa kuwa naye siku kadhaa na kumuacha, alichokitaka ni kuwa naye, kufunga naye ndoa na kuwa mume na mke. Msichana huyo hakuonekana kuwa na habari, macho yake yaliangalia mbele, wakawa wamekwishafika nje, na walianza kuyafuata mageti na watu wengine.

    “Binti...” aliita Laurence, msichana yule hakuitikia, akayageuza macho yake na kumwangalia Laurence usoni.

    “Unaitwa nani?”

    “Ili?”

    “Kukufahamu tu mpendwa! Kwani kuna tatizo?” aliuliza Laurence.

    Msichana yule hakujibu kitu, aliendelea kusonga mbele. Hakutaka kuzungumza na Laurence, kila alimwangalia, alikasirika kwa kuona kwamba alipotezewa muda wake. Japokuwa alikuwa ameegesha gari lake katika eneo la uwanja huo lakini Laurence hakulikumbuka, aliendelea kwenda na msichana yule ambaye alifika kituoni na kuanza kusubiria daladala.

    “Unaishi wapi?” aliuliza Laurence.

    “Wewe kaka vipi?”

    “Jamani! Kwani kuna tatizo kama nikikufahamu zaidi mpendwa katika Bwana?”

    “Aya! Naitwa Evadia,” alijibu msichana yule.

    “Nashukuru kukufahamu. Ubarikiwe na Bwana,” alisema Laurence.

    Wote wakajikuta wakikaa kituoni hapo kusubiri daladala. Laurence hakujua msichana huyo alikuwa akisubiri daladala za wapi. Usafiri ulikuwa ni wa shida kwani kulikuwa na watu wengi mno. Kila gari lililokuja kituoni hapo, liligombaniwa hivyo kukosa nafasi.

    Waliendelea kusubiri. Evadia alikuwa akimshangaa Laurence, hakuwa akimfahamu mvulana yule, hakujua alihitaji nini. Japokuwa alionekana kuwa mvulana mwenye sura nzuri na ya upole lakini hakuwa amevutika.

    Kila daladala aliyolifuata kwa ajili ya kupanda, alifuatwa na Laurence, alipoliacha, naye Laurence aliliacha. Evadia akawa na wasiwasi mno, alichokifanya ni kusogea pembeni kabisa ya kituo kile na kutulia, alitaka kuona kama Laurence angemfuata.

    Moyo wa Laurence uliumia mno, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea. Moyo wake ulikuwa kwenye mapenzi ya dhati, hakuamini kuona kwamba msichana aliyekuwa akimpenda kwa mapenzi yote hakuwa akimtaka, hakuwa akitamani kuzungumza naye.

    Japokuwa ilikuwa ni mara ya kwanza kumuona msichana huyo lakini moyo wake ulikufa na kuoza. Alichokifanya ni kusimama, alimwangalia Evadia kwa jicho la wizi, ilipokuja daladala ya kwenda Manzese kupitia Kigogo, Evadia akaifuata, akaingia ndani, naye Laurence akaingia. Akasahau kama aliliacha gari lake la thamani ya shilingi milioni mia na hamsini katika eneo la kuegesha magari pale Uwanja wa Taifa. Alikuwa bize kumfuatilia msichana huyo tu ambaye hakujua aliishi wapi..

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Abiria walikuwa wengi ndani ya gari, Laurence alishikilia bomba huku pembeni yake akiwepo Evadia ambaye alikuwa na maswali mengi juu ya mwanaume yule aliyekuwa akimuwinda tangu walipokuwa ndani ya Uwanja wa Taifa.

    Hakutaka kuzungumza lolote na Laurence, alibaki kimya huku akisikilizia ni kitu gani kingefuata kwani kwa jinsi alivyoonekana Laurencce, hakuonekana kuwa mwanaume mwenye papara, kila alilokuwa akilifanya alionekana kuwa makini nalo.

    “Umependeza Evadia,” alisema Laurence, hakuwa na kingine cha kusema zaidi ya kumsifia msichana huyo kwa kuamini kwamba pindi unapomsifia mwanamke, una asilimia kubwa za kumpata.

    “Asante.”

    “Unashuka wapi?” aliuliza Laurence.

    “Mburahati.”

    “Oooh! Sawa, ningependa nikufahamu zaidi,” alisema Laurence, watu waliokuwa karibu nao waliyasikia mazungumzo hayo japokuwa Laurence alijitahidi kuongea kwa sauti ya chini.

    “Ili?”

    “Basi tu, kuna mengi ya kuzungumza nawe.”

    “Kuhusu nini?”

    “Usiogope, niamini.”

    “Hivi wewe kweli Mkristo au ulifika uwanjani kutafuta wanawake?” aliuliza Evadia huku akimkazia macho Laurence.

    “Mimi?”

    “Kwani naongea na nani?”

    “Mimi ni Mkristo, sikwenda pale kutafuta mwanamke, nilikwenda kumsifu na kumuabudu Mungu,” alijibu Laurence.

    “Sawa.”

    “Evadia naomba unielewe. Mimi si kijana mhuni, sikukufuata kihuni, nimekuja kwako kama mtu anayejitambua, hicho unachokifikiria kichwani mwako juu yangu si kile kilichopo kwangu. Naomba tukae sehemu tuzungumze, hata kama utataka nije nyumbani kwenu, hakuna tatizo,” alisema Laurence.

    “Uje nyumbani kwetu?”

    “Ndiyo!”

    “Kama nani?”

    “Evadia, naomba usinifikirie vibaya,” alisema Laurence.

    Kuanzia hapo Evadia hakutaka kuzungumza tena, alibaki kimya, kadiri muda ulivyozidi kwenda mbele Laurence alijitahidi kumuongelesha lakini msichana huyo akawa kimya kabisa. Kwa muonekano wa nje Laurence alionekana kuwa mtu mzuri lakini hiyo haikuwa sababu ya Evadia kumuamini.

    Safari iliendelea zaidi, Laurence hakunyamaza, alikuwa kinara wa kuongea japokuwa maswali yake yote aliyokuwa akiyauliza hakuwa akijibiwa. Gari lilipofika maeneo ya Mburahati Msikitini, Evadia akateremka, naye Laurence akateremka.

    “Unahitaji nini kutoka kwangu?” aliuliza Evadia huku akimwangalia Laurance usoni.

    “Kukuoa!”

    “Unasemaje?” aliuliza Evadia huku akionekana kushtuka.

    “Kwani haujanisikia mpendwa? Nahitaji kukuoa,” alisema Laurence.

    Evadia akaonekana kukasirika, hakutaka kuendelea kusimama mahali hapo alichokifanya ni kuondoka kuelekea katika njia iliyokuwa na michanga mingi. Laurence hakusimama, akaanza kumfuata msichana huyo kama mkia.

    Kila baada ya hatua ishirini, Evadia aligeuka nyuma, akaona bado Laurence alimfuatilia kwa nyuma. Safari iliendelea na baada ya dakika tano, msichana huyo akaanza kuifuata nyumba moja iliyochoka, kwa kuiangalia kwa nje tu ingekupa picha kwamba mtu aliyekuwa akiishi ndani ya nyumba hiyo alikuwa masikini mno.

    Nje ya nyumba ile kulikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa akisuka ukili. Laurence hakutaka kusogea zaidi, akabaki akiwa amesimama kule mbali alipokuwa, hali waliyokuwa nayo watu wale iliunyong’onyeza moyo wake, akajikuta akiingiwa na huruma mno.

    Msichana mwenye sura nzuri, msichana ambaye kwa kumwangalia tu hakutaka kujiuliza kama alistahili kuwa mke wake au la, maisha aliyokuwa akiishi yalikuwa ya kimasikini mno. Alipoiangalia nyumba ile, hakuamini kama kungekuwa na watu waliokuwa wakiishi humo.

    Ilionekana kuwa kama kibanda fulani cha kufugia kuku. Sehemu nyingine ilijengwa kwa udongo lakini sehemu nyingine ilijengwa kwa matofali yaliyoonekana kuchoka sana. Bati lililotumia kuezeka nyumba ile lilichakaa, lilikuwa na kutu nyingi, kila alipoiangalia nyumba ile, kwa kifupi, alijisikia vibaya moyoni mwake.

    Alipomuona Evadia akizungumza na mwanamke yule aliyekaa chini nje ya nyumba ile, hakutaka kusubiri zaidi, alichokifanya ni kugeuka na kurudi alipotoka. Hicho ndicho alichokuwa akikihitaji, alihitaji kupafahamu mahali alipokuwa akiishi Evadia.

    Moyo wake ulimpenda mno, alitaka awe mke wake wa ndoa, kila alipomwangalia, sura ya kuvutia, aligundua kwamba msichana huyo alistahili kuwa mpenzi wake. Hivyo akaondoka zake na kujiahidi kurudi tena siku nyingine.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Laurence alikuwa na mawazo kichwani mwake, kazi zake za kila siku hazikufanyika, muda wote aikuwa na mawazo tele, alikuwa akimfikiria msichana aliyekutana naye jana yake ambaye kwake alionekana kuwa kama malaika.

    Kila alipojigeuza huku na kule, taswira ya msichana yule ilionekana kichwani mwake, moyo wake ukavutwa, ukabuuzwa vilivyo, mapenzi mazito yaliendelea kuchipua moyoni mwake, hakutaka kitu kingine, hakuwa na hamu ya msichana mwingine, yule aliyekuwa akimfikiria alikuwa Evadia tu.

    Usiku wa siku hiyo hata usingizi haukumjia inavyotakiwa, alikuwa akimfikiria msichana huyo tu, kwake, alikuwa tayari kukosa kitu chochote kile, afilisike na kurudi kama zamani, maisha ya kimasikini yaliyokuwa yamemtesa kwa kipindi chote lakini si kumkosa Evadia.

    Alitaka kuwasiliana naye, alimuona siku moja tu lakini siku hiyohiyo ikaubadilisha moyo wake. Alikuwa msichana mrembo sana, aliyevutia, msichana mwenye umbo zuri, kitu kilichomhuzunisha ni kwamba msichana huyo alikulia katika maisha ya kimasikini.

    Mungu hakumnyima kila kitu katika maisha yake, alimnyima utajiri lakini alimpa uzuri, kitu ambacho angebaki nacho milele na si kama utajiri ambao ungeweza kupotea siku yoyote ile. Kila alipotaka kulala, usingizi bado ulikataa kuja, alibaki akigalagala huku na kule mpaka ilipofika saa nane usiku ndipo usingizi ukamchukua.

    Siku hiyo, kwa kuwa Evadia alimkaa sana kichwani, akafikia hatua ya kumuota msichana huyo, ndoto iliyomuonyesha kwamba walikuwa kanisani, alikuwa na suti nyeusi huku Evadia akiwa na shela jeupe lililomfanya kupendeza mno, ilikuwa siku ya harusi yao.

    Laurence alifurahi mno lakini mara baada ya kushtuka kutoka usingizini na kugundua kwamba ile ilikuwa ndoto, alibaki na mawazo tele, moyo wake ukakosa raha kabisa.

    Siku nyingine ilikuwa imeingia, Laurence akaamka kutoka kitandani, akajiandaa kwa ajili ya kwenda kazini. Alipomaliza kila kitu, akatoka ndani, akaelekea sehemu ya maegesho ya magari yake na kuchukua gari la kifahari, Ferrari Spider, gari ya gharama ambayo ilikuwa moja tu nchini Tanzania, akaingia ndani na kuondoka mahali hapo.

    Laurence Mathew alikuwa miongoni mwa watu waliofanikiwa sana katika maisha yao. Alikuwa mkurugenzi wa kampuni kubwa ya Amazon Tyre ambayo ilikuwa ikihusika na uuzaji wa matairi Afrika Mashariki.

    Kupitia biashara hiyo, akajikuta akitengeneza fedha, akanukia fedha na kuishi maisha ya kifahari. Katika maisha yake yote, alifikiria fedha, kila alipoamka asubuhi, kitu cha kwanza kabisa ambacho kilikuja kichwani mwake ni namna ambavyo angefanikiwa kupata fedha nyingi zaidi ya alizokuwa nazo kipindi hicho.

    Kiu yake ya mafanikio, kiu yake ya kutamani kuwa bilionea mkubwa duniani ikamfanya kupambana sana, mbali na kuwa na kampuni hiyo, pia Laurence akaanzisha kampuni nyingine iliyokuwa ikishughulika na watalii katika mbuga mbalimbali za wanyama.

    Kote huko, alikuwa katika harakati za kutafuta fedha, hakukubali kuona akishindwa, ili jambo lionekane kuwa kubwa na lililoshindikana, ilikuwa ni lazima alifanye, hakutaka kukata tamaa kwa kuliona jambo gumu na wakati hakuwahi kulifanya.

    Akawa na fedha nyingi, akawa bilionea kijana. Wanawake wengi warembo walivyoona hivyo, wakaanza kumpapatikia lakini Laurence hakutaka kabisa kuwasikiliza. Alijua fika kwamba wasichana wengi walimfuata kwa kuwa alikuwa tajiri, aliwafahamu vilivyo hivyo akaamua kuachana nao kabisa.



    Kiu yake ya mafanikio, kiu yake ya kutamani kuwa bilionea mkubwa duniani ikamfanya kupambana sana, mbali na kuwa na kampuni hiyo, pia Laurence akaanzisha kampuni nyingine iliyokuwa ikishughulika na watalii katika mbuga mbalimbali za wanyama.

    Kote huko, alikuwa katika harakati za kutafuta fedha, hakukubali kuona akishindwa, ili jambo lionekane kuwa kubwa na lililoshindikana, ilikuwa ni lazima alifanye, hakutaka kukata tamaa kwa kuliona jambo gumu na wakati hakuwahi kulifanya.

    Akawa na fedha nyingi, akawa bilionea kijana. Wanawake wengi warembo walivyoona hivyo, wakaanza kumpapatikia lakini Laurence hakutaka kabisa kuwasikiliza. Alijua fika kwamba wasichana wengi walimfuata kwa kuwa alikuwa tajiri, aliwafahamu vilivyo hivyo akaamua kuachana nao kabisa.



    Utajiri wake haukupungua, ulizidi kuongezeka kila siku. Hakujiona, alikuwa mtu wa kuwasaidia watu wengine. Ndani ya miaka mitano tu, alikuwa na utajiri uliokadiriwa kuwa shilingi trilioni tano, tajiri mkubwa kabisa.

    Kitu ambacho Laurence hakukitamani kabisa ni kujulikana, alihitaji kuwa huru, sura yake mitaani ilikuwa ngumu kujulikana. Siku nyingine ambazo alitamani sana kutembea mitaani, alivalia kawaida na kuingia mitaani, huko, alinunua karanga, alipanda daladala na kufanya mambo mengine pasipo watu kujua kwamba mtu waliyekuwa naye ndiye yule bilionea kijana aliyejijengea heshima.

    Gari yake hiyo ya zaidi ya milioni mia tano alikuwa akiitumia kwenda nayo ofisini tu, alipofika huko, aliingia ofisini, alipotoka na kwenda kwenye mizunguko yake ya kawaida, aliomba gari la kawaida la mfanyakazi yeyote na kisha kuelekea mitaani, alipotaka kurudi nyumbani, aliingia ndani ya gari lake la kifahari na kurudi nyumbani.

    “Hivi huyu Laurence ndiye nani? Sijawahi kumuona hata kidogo,” alisema jamaa mmoja, Laurence alikuwa pembeni ya meza ya magazeti, alikuwa akipitia magazeti.

    “Hata mimi mwenyewe simfahamu, sura yake imekuwa adimu sana, kama Bakhresa” alisema jamaa mwingine.

    “Kwani Laurence ndiye nani?” aliuliza Laurence huku akiwaangalia vijana wale usoni.

    “Bilionea huyo! Nasikia jamaa nuksi sana, ana hela mpaka anapagawa,” alijibu jamaa mmoja.

    “Kweli?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ndiyo! Kwani wewe haumfahamu?”

    “Hapana!”

    “Wewe mgeni nini hapa Tanzania?”

    “Ni mwenyeji. Ila si umesema hata wewe haumfahamu?”

    “Ndiyo! Nilimaanisha kwamba haujawahi kusikia chochote kuhusu yeye?”

    “Hapana.”

    “Basi umepitwa.”

    Laurence alikuwa kwenye mizunguko yake kama kawaida, hakutaka kujiweka kama mtu mwenye fedha, alitaka kujua mambo mengi sana hivyo kutembea huku na kule, kuwa huru kulimfanya kuamini kwamba angeweza kujifunza mambo mengi sana.

    Ombaomba waliokuwa mitaani walimsikitisha mno, hakuamini kama kulikuwa na watu waliokuwa na uhitaji wa namna ile, alihakikisha kwa kila ombaomba aliyekuwa akikutana naye, ilikuwa ni lazima kumsaidia kiasi fulani cha fedha.

    Katika kipindi chote hicho alikuwa akimfikiria msichana ambaye alikutana naye siku chache zilizopita, Evadia, msichana mrembo aliyekuwa akimpenda kwa moyo wa dhati, msichana ambaye hakuona kama kulikuwa na mwingine zaidi yake.

    Alizunguka sehemu mbalimbali pasipo kugundulika, alipoona kwamba alichoka sana, akaingia katika mghahawa wa chakula cha mama ntilie na kuanza kula. Alizungumza na watu wengi lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyegundua kwamba mtu huyo alikuwa bilionea, alipokula na kushiba tena huku akizungumza na watu mbalimbali kuhusu maisha kisha kuondoka zake.

    Safari yake wakati huo ilikuwa ni kwenda Mburahati, mahali alipokuwa akiishi Evadia, alizikumbuka sana njia, hakutaka kupanda daladala, alifurahi kutembea mitaani, kuangalia mazingira na jinsi watu wengine walivyokuwa wakiishi.

    Kutoka hapo alipokuwa mpaka Mburahati alichukua saa moja ndipo akafika Mburahati Msikitini na kisha kuingia mitaani. Alipita kwenye vichochoro vilevile, alipanda na kushuka, alizidi kusonga mbele mpaka alipofika katika nyumba ile kuukuu.

    Alipoiona kwa mara ya pili, moyo wake ukamuuma zaidi, aliiangalia huku akilengwa na machozi, msichana ambaye alimfanya kutokulala vizuri usiku, msichana aliyemfanya kumfikiria sana, alikuwa akiishi katika nyumba ile iliyokuwa mbele yake.

    “Shikamoo mama,” alimsalimia mwanamke aliyemkuta nje, mama yake Evadia ambaye alikuwa akisuka ukili.

    “Marahaba mwanangu, hujambo?”

    “Sijambo mama.”

    Akayatuliza macho yake kwa mwanamke yule, alionekana kupigwa na maisha, alionekana ‘kuchoka’ mno. Moyo wake ulizidi kuumia, maisha aliyokuwa akiishi mwanamke yule yalimuumiza pia.

    “Nimemkuta Evadia?” aliuliza Laurence.

    “Ametoka, alikwenda hospitali.”

    “Oooh! Sawa! Anaumwa?”

    “Ndiyo!”

    “Anaumwa nini?”

    “Kwani wewe nani?”

    “Rafiki yake.”

    “Mmh! Sasa rafiki yake ndiyo asikwambie anaumwa nini?”

    “Hahah! Sikutaka kumuuliza. Ila sidhani kama kuna tatizo endapo nikijua,” alisema Laurence.

    “Utamuuliza mwenyewe akija.”

    “Sawa! Atarudi muda gani?”

    “Bado sijajua, ila atarudi tu,” alijibu mama yake Evadia.

    Laurence hakutaka kuondoka mahali hapo, alibaki nyumbani hapo, alikaa katika mkeka huku akizungumza na mama yake Evadia ambaye muda wote alikuwa mtu wa mawazo tu, maisha aliyokuwa akiishi na binti yake yalimchanganya mno.

    Laurence hakuuliza kitu chochote kile, kila alichokuwa akiambiwa, alikubaliana nacho hata kama kililazimika kuuliziwa maswali, hakutaka kufanya hivyo. Mawazo yake yalikuwa kwa Evadia tu, hakuwa na kitu kingine alichokuwa akikihitaji zaidi ya kumuona msichana huyo tu.

    Muda ulizidi kwenda mbele, saa na dakika zilikatika, hakutaka kuondoka, alikuwa radhi kukaa hadi usiku wa manane lakini si kuondoka nyumbani hapo pasipo kumuona Evadia. Ilipofika saa mbili usiku, huku giza likiwa limetawala ndipo mama yake Evadia akamwambia kwamba alitakiwa kuondoka lakini Laurence akagoma.

    “Haiwezekani mama, ni lazima nionane na Evadia leo,” alijibu Laurence.

    “Kwani kuna nini?”

    “Nataka nionane naye tu, wala usijali.”

    “Sawa. Basi ngoja nikuletee chakula ule,” alisema mama yake Evadia.

    “Sawa.”

    Hakutaka kujivunga, aliletewa chakula, ulikuwa ugali na dagaa, pembeni kulikuwa na mchicha. Tangu awe bilionea hakuwahi kula chakula cha namna hiyo ila kwa sababu alikuwa amedhamiria kuishi maisha ya chini, akaamua kula.

    Bado mama Evadia alikuwa na maswali mengi, kila alipomwangalia Laurence alishindwa kufahamu vizuri mwanaume huyo alikuwa nani. Ni kweli Evadia alikuwa na marafiki lakini hakuwahi kumuona mwanaume huyo hata siku moja.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kila alipotaka kumuuliza, alibaki kimya, hakutaka kuuliza kitu chochote kile, akabaki na maswali yake moyoni.

    Ilipofika saa 3:18 usiku, ndipo Evadia akatokea mahali hapo. Aliona nje ya nyumba yao kukiwa na watu wawili, mmoja alikuwa mama yake, alimtambua lakini mtu wa pili hakuweza kumtambua. Alionekana kuwa na hofu, hakujua mtu yule alikuwa nani na alifika hapo kufanya nini.

    Akaanza kusogea karibu kwani kule mbali alipokuwa hakuwa akifahamu mtu huyo alikuwa nani. Mwanga wa koroboi uliokuwa ukiwaka ndiyo uliomfanya kugundua kwamba mtu aliyekuwa amekaa katika mkeka pamoja na mama yake alikuwa Laurence, mwanaume yule aliyemfuatilia siku chache zilizopita.

    “Karibu Evadia,” alimkaribisha Laurence, Evadia hakujibu kitu zaidi ya kusalimia na kuingia ndani.

    Moyo wa Laurence ukapoa, kitendo cha kumuona Evadia mahali hapo kiliufanya moyo wake kujisikia ahueni, hakuwa kwa siku kadhaa na kitendo cha kumuona tena mahali hapo kilimfanya kujisikia faraja.

    Alimpenda, alimthamini, alitamani kuwa naye maisha yake yote. Kitendo cha kumuona mahali hapo kilimfanya kujisikia faraja, mapenzi aliyokuwa nayo kwa msichana huyo yakaongezeka zaidi.

    “Kweli wewe ni rafiki yake?” aliuliza mama Evadia.

    “Ndiyo!”

    “Kweli?”

    “Kweli tena.”

    “Mbona hajazungumza hata na wewe?”

    “Sijui! Inawezekana amechoka. Si ametoka hospitali? Inaelekea hajisikii vizuri,” alijitetea Laurence huku akijitahidi kuonyesha tabasamu pana usoni mwake.

    Mama Evadia alionekana kuwa na wasiwasi, japokuwa Laurence aliongea kwa tabasamu pana tena huku akionekana kujiamini lakini mwanamke huyo akasimama na kuelekea ndani.

    Lengo lake kubwa lilikuwa ni kumuita binti yake kwa kuamini kwamba inawezekana hakuwa amemtambua Laurence pale nje alipokuwa. Huku nyuma, mapigo ya moyo wa Laurence yalikuwa yakidunda kwa nguvu. Wakati mwingine alitamani kukimbia.



    Walipendana kana kwamba hakukuwa na watu waliopendana kama walivyokuwa. Kila walipokuwa, walikuwa pamoja, walitembea pamoja huku wakati mwingine wakienda kutazama filamu pamoja.

    Muonekano wao wa nje, walionekana kuwa watu waliopendana kwa mapenzi ya dhati kiasi kwamba kila mtu akahisi kwamba hakukuwa na kitu ambacho kingekuja kuwatenganisha, ukaribu wao ungeweza kwenda mbele zaidi mpaka pale ambapo wawili hao wangeoana na kuishi kama mke na mume.

    Alikuwa ni kijana Dickson Maghembe na msichana aliyeitwa kwa jina la Evadia Johnson. Wawili hawa walikuwa gumzo kila walipokuwa. Japokuwa walikuwa wametoka katika familia tofauti lakini hakukuwa na mtu aliyeliangalia hilo, kila mtu alikuwa akimuona mwenzake sawa na alivyokuwa.

    Evadia hakuwa msomi, aliishia darasa la saba baada ya baba yake kufariki dunia. Kuanzia hapo, hakusoma tena, maisha yake yakawa ni nyumbani tu huku akimtegemea mama yake ambaye alikuwa akifanya biashara ya mikeka aliyokuwa akiifuma yeye mwenyewe.

    Kutokana na uzuri wake, wanaume wengi walimfuata Evadia, walimtaka kimapenzi kwa maneno matamu, kwa kutumia fedha lakini yote hayo yalionekana kuwa si lolote lile kwake. Alichokuwa akikiangalia ni mapenzi kwa Dickson tu, hakutaka kuwa na mwanaume yeyote yule katika maisha yake zaidi ya huyo mpenzi wake.

    Dickson ambaye alikuwa akisoma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kila alipotoka chuoni ilikuwa ni lazima kupita nyumbani kwa kina Evadia na kuzungumza naye. Alimpenda, hapo alipokuwa akifika, alimchukua na kisha kuondoka naye kuelekea nyumbani kisha baadaye kumrudisha.

    Wazazi walifahamiana, mara kwa mara walitembeleana, waliwahusia watoto wao kuhusu maisha, ni jinsi gani walitakiwa kuishi na kupenda mpaka pale watakapooana. Kila neno waliloambiwa, liliingia vichwani mwao na kutulia, ashki kubwa ya kupendana iliikamata mioyo yao, hawakuona kama kungekuwa na chochote kile ambacho kingewafanya kuachana.

    “Dickson...” aliitwa Evadia.

    “Ndiyo kipenzi.”

    “Ninakupenda.”

    “Najua hilo, ila haunishindi mimi!”

    “Kweli?”

    “Kwa nini nikudanganye. Ni lazima nikuoe, siwezi kukuacha maishani mwangu,” alisema Dickson huku akiachia tabasamu pana.

    Waliahidiana mambo mengi, waliahidiana kuishi milele, waliahidiana kila kitu walichokiona kustahili kuingia katika mahusiano yao ya kimapenzi. Hakukuwa na mtu aliyetaka kumwacha mwenzake, kila siku waliendelea kuwa pamoja.

    Wakati wakiyaongea hayo, walikuwa ufukweni, mapenzi yaliwachukua, walijikuta katika ulimwengu mwingine wa mahaba, wakiogelea katika dimbwi la mahaba na kila walipoangalia mbele, hawakuamini kama ingetokea siku moja wangeachana.

    Mara baada ya kupita miaka mitatu ya uhusiano wao wa kimapenzi, hapo ndipo harakati za ndoa zikaanza kufanyika. Wakajipanga kwani hakukuwa na kitu chochote ambacho kingeweza kuwatenganisha au kuwazuia wao kufunga ndoa na kuishi pamoja.

    “Evadia, ninakuahidi kwamba hakuna mwingine zaidi yako,” alisema Dickson huku akichia tabasamu pana.

    “Na iwe hivyo mpenzi, ninatamani kuolewa nawe,” alisema Evadia, wakakumbatiana na kupigana mabusu mfululizo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakati wakijiandaa na harusi, hapo ndipo baba yake Dickson alipomwambia kijana wake kwamba alitakiwa kuongeza elimu yake nchini Venezuela, hivyo alitakiwa kwenda huko haraka iwezekanavyo na mara atakaporudi nchini Tanzania basi mikakati ya ndoa iendelee na hatimaye wawili hao wafunge ndoa.

    “Nitabaki na unyonge mpaka utakapotudi,” alisema Evadia, macho yake yalikuwa yakikusanya machozi.

    “Najua mpenzi, hata mimi sitokuwa na furaha kamwe, hakika nitakuwaza wewe, sitoweza kuishi kwa furaha huku ukiwa mbali nami,” alisema Dickson, naye alionekana kuwa na huzuni mno.

    Japokuwa walihuzunika lakini mwisho wa siku Dickson akaondoka na kuelekea nchini Venezuela. Kuwasiliana ilikuwa ni kwa tabu sana, kutokana na Evadia kutokupata elimu ipasavyo, hakuwa na akaunti ya barua pepe, hakuwa akitumia mtandao wowote ule wa kijamii, kitu pekee alichokuwa akikifahamu ni kutumia simu kwa kupiga na kutuma meseji tu.

    Evadia alikosa raha, kila alipokuwa, alionekana kuwa na mawazo tele, hakuzoea kuwa mbali na mpenzi wake huyo, kila siku maisha yake yalikuwa ya huzuni mno. Wakati mwingine hakuwa akila chakula, mawazo yalitawala kichwani mwake, kila alipokaa, alimfikiria Dickson tu.

    Siku zikaendelea kukatika, ni mara chache Dickson alikuwa akimpigia simu na kuzungumza naye na kitu pekee alichokuwa akimwambia ni kuwa mwaminifu mpaka pale ambapo angerudi tena nchini Tanzania.

    “Nitakuwa muaminifu milele mpenzi,” alisikika Dickson.

    “Nami nakuahidi uaminifu wangu,” alisema Evadia huku machozi yakimbubujika mashavuni mwake, hakika alisikia moyo ukimchoma mno.

    Hayo ndiyo yalikuwa maneno waliyoambiana kila siku ambazo Dickson alipopiga simu. Mapenzi yaliendelea kuchipuka huku nchini Tanzania Evadia akiendelea kuwaambia marafiki zake wachache kwamba mara mpenzi wake atakaporudi nchini Tanzania basi wangeweza kuoana.

    Baada ya miezi mingine kupita hapo ndipo mabadiliko yalipoanza kutokea, Dickson hakuwa mpigaji wa simu kama zamani na hata pale alipokuwa akipiga, stori zake zilikuwa za kawaida sana na hata kwenye umaliziaji wake, haukuwa kama ule uliokuwa kipindi cha nyuma.

    “Nakupenda mpenzi,” alisema Evadia mara baada ya kuzungumza sana na Dickson ambaye kwa kumsikia tu, hakuonekana kuwa na raha.

    “Asante...”

    “Asante tena?”

    “Ndiyo! Unataka nijibu nini tena?”

    “Si kama zamani!”

    “Kivipi?”

    “Kwamba unanipenda pia,” alisema Evadia.

    “Yaani neno hilo kila siku, acha kukariri Evadia,” alisema Dickson.

    “Umeniita jina langu! Mungu wangu! Sijawahi kusikia ukiniita jina hilo miaka na miaka, imekuwaje?” aliuliza Evadia, alionekana kuchanganyikiwa.

    “We ulitaka nikuite vipi?”

    “Huwa unaniita mpenzi, imekuwaje tena?”

    “Potezea.”

    Aliposema neno hilo, Dickson hakutaka kuiacha simu hewani, alichokifanya ni kukata na kisha kuizima.

    Evadia akachanganyikiwa, hakuamini kile kilichotokea, mpenzi wake, aliyempa thamani kubwa moyoni mwake, leo hii alikuwa akizungumza mambo yaliyompa maswali mengi kichwani mwake.

    Akahisi kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake, machozi yakaanza kujikusanya machoni mwake na baada ya sekunde chache, yakaanza kububujika mashavuni mwake, hakika aliyasikia maumivu makali moyoni mwake.



    Alikuwa na ndoto za kuolewa, zikafutika, alikuwa na ndoto za kupata maisha bora, nazo zikafutika, alihisi kuchanganyikiwa, mapenzi aliyokuwa nayo juu ya Dickson yalimzuzua mno na hata pale mambo yalipoanza kubadilika, alihisi kuchanganyikiwa.

    Kauli za Dickson ambazo alizitoa siku hiyo zilimchanganya, akajiona kama akiukaribia uchizi, akabaki akibubujikwa na machozi, moyo wake ulimuuma mno. Hakujua kilichosababisha Dickson kubadilika ghafla namna hiyo, alibaki akijiuliza lakini mwisho wa siku hakupata jibu lolote lile.

    Alibaki na maumivu moyoni mwake, hakutaka kumwambia mtu yeyote kile kilichokuwa kimetokea, hakutaka kumwambia mama yake wala wazazi wa Dickson kwa kuamini kwamba inawezekana siku hiyo ambayo alizungumza naye Dickson hakuwa na wakati mzuri, hivyo kuamini kwamba kama angepiga siku nyingine basi mambo yangekwenda kama yanavyotakiwa kwenda.

    Usiri wenye kuumiza uliendelea kubaki moyoni mwake, hakutaka mtu yeyote yule afahamu. Baada ya kupita miezi miwili akapokea simu nyingine kutoka nchini Venezuela, alikuwa Dickson ambaye alimpa ujumbe mmoja mkubwa, ujumbe uliomsikitisha mno, alimwambia kwamba kama akipata mwanaume wa kumuoa, awe radhi kuolewa.

    “Unasemaje?” aliuliza Evadia huku akionekana kushtuka.

    “Kwani umesikia nini?”

    “Nataka uniambie tena!”

    “Kwani umekuwa kiziwi siku hizi?”

    “Hapana, ila...”

    “Hebu kuwa muelewa Evadia. Kama kuna mwanaume atajitokeza na kukwambia kwamba anataka kukuoa, usiichezee bahati hiyo, kuwa naye,” alisikika Dickson kwenye simu.

    “Dickson...”

    “Unasemaje?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwa nini unan....” aliuliza swali lakini hata kabla hajamaliza kuliuliza swali hilo, hapohapo akaanza kulia.

    “Hebu acha utoto, sasa kipi kinakuliza? Kwani wewe ndiye wa kwanza kukataliwa? Nyamaza bwana, nitakuja na Luciana mwezi ujao, utamuona tu wifi yako,” alisikika Dickson na kukata simu.

    Kulikuwa na watu wengi walioumizwa mioyoni mwao, wengine walilia na wengine kujiua kabisa, wengine wakakata tamaa ya kupendwa, hawakuyapenda mapenzi tena, waliwachukia wanaume na hata wanawake.

    Maisha yalibadilika, wengine wakatishia kunywa sumu kutokana na maumivu makali ya kuachwa mapenzini, tena kwa watu waliokuwa wakiwapenda mno. Ingawa kulikuwa na wengi waliowahi kuumizwa mapenzini lakini kwa Evadia akahisi kwamba hakukuwa na mtu aliyepatwa na maumivu makali moyoni mwake kama alivyopata kipindi hicho.

    Hakuamini kilichotokea, wakati mwingine alihisi kama yupo ndotoni na baada ya muda fulani angeamka kutoka usingizini, ukweli ni kwamba hakuwa ndotoni, kile kilichokuwa kikitokea, kilimtokea katika maisha yake, kilikuwa ni kitu halisi ambacho kilimuumiza mno.

    Akakonda kwa mawazo, hakutaka kula, kila siku alipokuwa akiulizwa na mama yake tatizo lilikuwa nini, hakutaka kumwambia zaidi ya kumdanganya kwamba alikuwa akiumwa.

    Moyo wake uliamini kwamba kuna siku Dickson angerudi na kumwambia kwamba alikuwa akimtania, alifanya vile kwa kuwa alitaka kujua ni kwa jinsi gani alikuwa akimpenda.

    Alijipa moyo kila siku lakini pamoja na kujifariji sana, majibu yalikuwa yaleyale kwamba mwanaume huyo hakutaka kuwa naye kwa kuwa alimpata msichana mwingine aliyeitwa kwa jina la Luciana.

    Hicho ndicho kilichokuwa kikimpa wakati mgumu Evadia, hali ya kuwa na mawazo mengi, wakati mwingine ikamfanya kuhisi kizunguzungu, alipokuwa akitembea mitaani, alianza kupepesuka na mwisho wa siku kuanguka chini, alipoinuka alijikuta akiwa kitandani tena huku amezungukwa na dripu zilizotundikwa juu yake.

    Hali hiyo haikutokea mara moja au mara mbili, ndani ya mwezi huo ambao aliambiwa na Dickson kwamba alikuwa amempata mwanamke mwingine, kuanzia siku hiyo alikuwa kwenye hali mbaya, kuanguka na kuzimia ilitokea kwa zaidi ya mara tano kitu kilichompelekea mama yake kuwa na wasiwasi kwamba kulikuwa na tatizo.

    “Evadia...”

    “Abee mama.”

    “Hebu niambie kuna nini.”

    “Hakuna kitu.”

    “Sasa kwa nini unaanguka mara kwa mara?”

    “Sijui. Huwa ninajisikia kizunguzungu tu.”

    “Mmmh!”

    “Ndiyo hivyo!”

    “Na umemwambia Dickson?’ aliuliza mama yake.

    Hata kabla Evadia hajajibu swali hilo, akaanza kulia, mama yake alishtuka, hakujua ni kitu gani kilichokuwa kikimliza mtoto wake kiasi kile. Alijaribu kuuliza ili ajue sababu lakini hakupewa majibu zaidi ya msichana huyo kulia zaidi.

    Siku zikaendelea kukatika, hakupokea simu nyingine kutoka kwa Dickson hali ilitoashiria kwamba kile kilichokuwa kimetokea, hakikuwa na utani hata mara moja, mwanaume huyo alikuwa amemaanisha alichokizungumza na kwamba alitakiwa kutafuta mwanaume mwingine wa kumuoa.

    “Mama!”

    “Unasemaje binti yangu?”

    “Kuna kitu nataka kukwambia.”

    “Kitu gani?”

    “Kuhusu Dickson.”

    “Amefanyaje?”

    Hata kabla Evadia hakujibu swali hilo akaanza kulia, kumbukumbu zake zikaanza kurudi nyuma, siku ambayo alipigiwa simu na mwanaume huyo kisha kuambiwa kwamba kama kungekuwa na mwanaume mwingine amemfuata kwa ahadi ya kumuoa basi akubaliane naye na huku siku nyingine akimwambia kwamba tayari alikuwa amepata mwanamke mwingine.

    Alilia na kulia, mama yake alijaribu kumbembeleza na kumuuliza nini kilikuwa kinaendelea lakini hakujibu, aliendelea kulia, na aliponyamaza baada ya dakika tano kupita, hapo ndipo alipoamua kumwambia mama yake juu ya kilichokuwa kimetokea.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mama yake hakuamini alichokuwa amekisikia, wakati mwingine alihisi kama alikuwa akimtania, alimjua vilivyo Dickson, jinsi alivyompenda binti yake, alifahamu ni kwa kipindi gani walikuwa wameweka ahadi ya kuoana na kuishi milele kama walivyokuwa wameambiana.

    Kuambiwa kwamba mwanaume huyo alikuwa amepata mwanamke mwingine, hakika ilimchanganya na akashindwa kumwamini Evadia moja kwa moja.

    “Haiwezekani,” alisema mama yake.

    “Ndiyo hivyo mama! Dickson amepata mwanamke mwingine, anaitwa Luciana,” alisema Evadia.

    “Dickson huyuhuyu?”

    “Ndiyo mama!”



    ITAENDELEA



MTU WA UFUKWENI (THE BEACH MAN) - 5

 







    Simulizi : Mtu Wa Ufukweni (The Beach Man)

    Sehemu Ya Tano (5)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilikuwa ni kesi ambayo ilikosa mahali pa kusimamia. Kesi Isiyo na ushahidi wowote wala mwelekeo hasa. Baadaye uchunguzi ulifanywa na Polisi haukuona kuwa Ramson alihusika kwa lolote. Ilionekana kwamba muuaji ni Dr. Jackson ambaye alimpiga risasi mkewe na kutaka kumuua Ramson badala yake risasi ikampiga ya mguuni. Baadaye alijipiga risasi ya kichwa mwenyewe. Uchunguzi wa alama za vidole kwenye bastola ile uliona kuwa mtumiaji wa silaha hiyo alikuwa ni Jackson mwenyewe.

    Wakati upelelezi wa haya yote unafanyika, Ramson alikuwa Hospitali akitibiwa akiwa chini ya ulinzi. Mpaka anapata nafuu kubwa kwenye jeraha lake la mguu, upelelezi ulimwondoa kwenye shutuma na baadaye walimwachia huru. Ramson alitoka Hospital asijue la kufanya. Ila alikumbuka kuwa karatasi zile alizificha sana baada ya kukabidhiwa na marehemu Dr Jackson.

    Alipoingia kwenye gari la Jackson aligundua picha na vyeti. Picha zile zilimwonyesha yeye akiwa na mke wa Dr. Jackson wakiogelea na nyingine zilizokuwa na ushahidi pia vitu vte hivyo alivificha pamoja na zile hela. Alifanya hivyo kusudi kuondoa ushahidi wa yeye kuhusishwa na vifo vya Dr. Jackson na mkewe.

    Hii pekee ndiyo iliyomweka mbali na kesi ya mauaji hayo. Baada ya yote hayo Wafanya kazi wake walipokuja aliwaaagiza wampeleke mtoto kwa mmoja wa rafiki zake. Simu aliyompigia rafiki yake huyo ilimfanya akubali kumtunza mtoto huyo, hadi hapo mambo yatakapotulia. Katika maficho alikozificha karatasi zile na fedha alizokabidhiwa na Marehemu Mary palikuwa salama. Baada ya kurudi akiwa huru alikuta vitu vikiwa vile vile kama alivyoweka.

    Alikaa na kuamua kusoma makaratasi yale aliyopewa na Dr. Jackson, maana tangu apewe hajawahi kuyapitia na hakujua kuwa yalihusu nini! Mwili ulimsisimka sana baada yakusoma kichwa cha habari! Maneno yaliyofuata yalimfanya apanue mdomo kwa mshangao! Kila hatua aliyoipiga katika kusoma maneno yaliyopo pale, vilimfanya aduwae! Ilikuwa ni zaidi ya habari! Ilimshangaza na kumshtusha kwani ndani ya karatasi zile Dr.Jackson alirudia kusema kuwa, hakuwa na budi kufa kwa sababu hataweza kustahimili kuishi bila Mary mkewe!

    Na pia asingevumilia kupata hukumu ya mauaji ya mkewe ambayo mwenyewe hakukusudia kufanya hivyo. Lakini jambo la msingi ni kwamba hakuwa na ndugu hata mmoja, ila wazazi wake tu ambao wako kijijini nao ni wazee sana. Kwa hiyo ameamua kumrithisha Ramson mali zake zote, ambazo ni pamoja na mahotel mawili ya kitalii yaliyopo Lushoto mjini.

    Makampuni ya usafirishaji iliyopo jijini Dar es Salaam. Mashamba mawili yenye heka kumi kila moja, moja likiwa Lushoto na jingine likiwa Korogwe Pia kulikuwa na nyumba tatu; Moja ikiwa hapo mjini Tanga na nyingine ikiwa Arusha na nyingine ilikuwa Ostabay Dar es Salaam.

    Fedha zilizoko Bank zilikuwa ni Shilingi milioni mia sita na hamsini. Mwisho wa yote akamwambia atafute wakili kwa sababu yeye pamoja na mali zote hizo hakuwahi kuweka wakili binafsi. Wakili atakayemweka amsimamie katika kubadilisha hati za umiliki wa mali zake, kutoka jina la Dr. Jackson Kigoi kwenda jina lake yaani Ramson. Hakujua aanzie wapi baada ya kuona mambo hayo.

    Alimshangaa sana Dr. Jackson kwa moyo wake wa ajabu! Alikaa na kuangalia jinsi ya kufuatilia mambo ya sheria kwa ajili ya kuwakilisha barua ile. Alijua kuwa ile ndiyo itakayomsaidia pindi atakapoifikisha kwa mwanasheria. Alijua kuwa huko atapata mwongozo wa namna ya kusimamia mali zile za Marehemu Dr.Jackson. Akili hazikutulia kabisa! Alikuwa na mchanganyiko wa mawazo.

    Moyo wake ulikuwa umejaa huzuni na mawazo mengi, kwa mtihani mkubwa sana aliopewa na Dr. Jackson. Kwa ujumla alikuwa hajui aanzie wapi ili kuziweka malizote zile chini ya himaya yake. Kichwa kilijaamambo mengi na baadaye alijikuta akipitiwa na Usingizi. Usingizi huu uliomchukuwa muda mrefu kabla ya kuamka na kutafuta jibu la mitihani iliyopo mbele yake.



    Ramson Aliingia ndani baada ya kufunguliwa mlango! Aliitikia salamu ya dada aliyemfungulia mlango na kuingia ndani. Sebuleni alimkuta mzee Kigoi akiwa amekaa na mkewe. baada ya salamu Ramson akaanza mazungumzo. “Wazee wangu naomba sana mnisamehe kwa kusababisha kifo cha Dr. Jackson!”

    Nikijieleza ni habari ndefu sana lakini naomba mnisamehe sana kwa yote wazee wangu.” Alisema hayo huku akilia machozi mbele ya wazee hao. ..kisha akaendelea: “Mimi ndiye Ramson mmiliki wa ufukwe wa mwahako ambako Dr. Jackson na mkewe walipofia. Nimetafuta sana nijue mahali mlipo wazee wangu mpaka nimefika leo. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baba na mama naombeni mnisamehe juu ya yote yaliyotokea.” Alihitimisha na kunyamaza kimya ili asikie kile wazee hao watakachosema. “Kijana Hebu inuka ukae na ufute kabisa machozi yako.” Alisema Mzee Kigoi na Ramson akanyanyuka na kukaa kwenye kochi lililokuwa kando yake; alipokuwa ametulia Mzee Kigoi aliendelea: “Huwezi kuomba msamaha kwa kazi ya Mungu kijana.

    Mimi ninavyojua ni kwamba Mwanangu Jackson alikufa kwa siku zake! Potelea mbali kama kulikuwa na sababu gani lakini ninachojua ni kwamba kifo chochote hakikosi sababu au mlango wa kupitia. Wewe uwe na amani kabisa sioni wapi umekosea katika msiba huu.” Alisema Mzee Kigoi na kumtazama mkewe aliyekuwa kimya wakati wote.

    “Kijana mimi na baba yako hapa ni wazee sasa. mambo mengi tumepitia na wasawahili wanasema: “Kuishi kwingi ni kuona mengi. Tunajua mengi na tumejifunza mambo ya ajabu sana katika maisha yetu haya. Tunajua kuwa kifo chochote kinapompata mtu kinatafuta pa kupitia tu. Pia kifo hicho hakiji hadi wakati wa mtu uwe umefika. Kama wakati haujafika kifo hukaa mbali kabisa na wala Jackson na mkewe wasingelikufa. Lakini ninavyojua ni kwamba kila jambo hupangwa na mwenyezi Mungu. Asingepanga mtoto wetu asingelikufa.

    Kwa hiyo mwanangu uwe na amani tu.” Alisema hivyo mke wa mzee Kigoi akimwondoa wasiwasi Ramson. “Asanteni sana wazazi wangu.” Baada ya hapo Ramson aliwasomea ile karatasi aliyopewa na Dr. Jackson kisha baada ya hapo akasema: “Wazazi wangu kuja kwangu hapa kuwatafuta ni ili pia niwaachie jukumu hili. Kwangu mimi sistahili kurithi hata shilingi moja. Nitasimama pamoja na wewe baba katika kuhakikisha kuwa mali hizi zote zinaingia mikononi mwako.” Alisema Ramson akiwa kashikilia karatasi ile. “Kijana wewe ni mtu wa ajabu sana!! Alifoka Mzee kigoi,

    “Sijaona mtu mwenye busara kama wewe katika maisha yangu! Wenzio wanalilia mali mpaka kudiriki kushikilia silaha na kumwaga damu za watu wewe unapewa kihalali mali hizi na unazikataa!” Aliongea kwa mshangao mkubwa Mzee Kigoi na kumgeukia mkewe ambaye naye aliishia kuguna tu na kutoa tabasamu la mshangao. .. kisha akaendelea “Mimi na mama yako tunakupokea rasmi leo kuwa mtoto wetu. Mali zote hizo utazisimamia wewe!”

    Kama marehemu Jackson amefikiria mpaka akaamua kukuandikia maneno haya juu ya mali zake zote, moja kwa moja amekuidhinisha kuwa mtoto wetu badala yake. Huna haja ya kutupa sisi mzigo ambao hatutauweza. Uzee tulionao huu tutaweza wapi kuingia kila mahali kutafuta sijui hati gani za umiliki wa vitu hivyo?

    Sisi kwa moyo wote tunakupa baraka zote, kama alivyofanya ndugu yako nenda kashughulikie hayo mambo. Ikiwa kuna mahali nitatakiwa kuja kudhibitisha lolote nitafanya hivyo. Jukumu lako litabaki kututunza sisi wazazi wako kama alikuwa akifanya marehemu kaka yako sawa?” Alihitimisha Mzee Kigoi na mama alimuunga mkono.Baada ya hapo Ramson akaagana nao na kuingia Rasmi katika michakato na majukumu mapya.



    Kila kitu kilienda kama kilivyopangwa. Wazazi wa Dr. Jackson walihamishwa kutoka kijijini na kupewa nyumba nzuri na ya kifahari Mjini. Ramson aliwawekea wafanyakazi wa kuwahudumia kwa kila kitu. Hoteli ziliendelea vizuri na makampuni yote. ufukwe nao ulitengenezwa na kuwa bora sana kwa kujengewa mahoteli ya kifahari ya kulala watalii.

    Maboti mapya na ya kisasa yalinunuliwa. Kijiji cha Tabu yanini mkutano mkubwa ulifanyika. Ramson aliamua kufanya mambo ya kimaendeleo; ikiwa ni pamoja na kuweka mabomba ya maji badala ya visima na kujenga Hospitali kubwa na nzuri kabisa. Historia iligeuka na kumfanya Ramson kuwa mtu wa thamani kubwa anayetegemewa kwa mambo mengi.

    Babu yake Ramson aliona fahari kubwa sana Baada ya kukamilishiwa nyumba yake mpya na nzuri kijijini hapo. Kwa ujumla Ramson alikuwa ndiye mfadhili katika kijiji cha Taabu yanini. Aligeuka na kuwa gumzo katika nchi yote, kwa kusababisha maendeleo na mabadiliko katika fukwe. Wengi walijaribu kuiga katika kutengeneza baadhi ya fukwe, hivyo alifanyika cheche yenye kuleta moto mkubwa wa maendeleo, katika fukwe za pwani ya bahari na hata katika maziwa makuu nchini Tanzania.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    * * *

    “Hiyo ndiyo Historia kamili ya maisha yangu!” Nilisema huku nikimtazama Jobiso Baro usoni. Alikuwa ameduwazwa na safari yangu ya maisha jinsi ilivyokuwa na mabonde na milima mikali! Hakutaka kabisa kuikatisha hadithi yangu ya maisha kwa kuonyesha uchomvu! Niliushangaa uvumilivu wake. “Pole sana Brother na hongera sana kwa mafanikio makubwa uliyoyapata.

    Ninakuahidi kwamba maandalizi ya Vipande vya Sinema yatakuwa tayari ndani ya wiki hii. Nitakuletea vipande vyako vya kuhusika na kazi itaanza mara moja.” Alisema Jobiso Baro kwa uhakika wakati akikusanya vifaa vyake vya kazi.” Kama tulioagana wote tulitazama saa. Mimi niliguna na mwenzangu alipiga mluzi wa mshangao! Kumbe nilitumia masaa kumi na mbili kusimulia Historia ya maisha yangu!



    MWISHO



Blog