Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

THE LOVE YOU HAD BEFORE (PENZI ULILOKUWA NALO KABLA) - 2

 







    Simulizi : The Love You Had Before (Penzi Ulilokuwa Nalo Kabla)

    Sehemu Ya Pili (2)



    Mama Evadia hakutaka kutulia nyumbani, alihisi hasira moyoni mwake, alichokifanya ni kuondoka nyumbani hapo na kuelekea kwa akina Dickson ambapo huko akawaambia wazazi wa kijana huyo kila kitu kilichokuwa kimeendelea. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wazazi hao hawakuamini, waliuliza mara mbilimbili kama alikuwa na uhakika na kile alichokizungumza, mwanamke yule aliwaambia kwamba kila kitu kilikuwa wazi, alipoona hiyo haitoshi, akampigia simu Evadia na kumtaka kuelekea nyumbani kwa kina Dickson ambapo alifanya hivyo haraka sana.

    “Ni kweli Evadia?” aliuliza baba yake Dickson.

    “Ni kweli! Ameniambia amepata mwanamke mwingine.”

    Wazazi hao wakashtuka, hawakutegemea kusikia kile walichokisikia mahali pale, walibaki wakimwangalia msichana yule, walipigwa na mshangao mkubwa. Walimfahamu kijana wao, waliyajua mapenzi mazito aliyokuwa nayo kwa msichana yule, leo hii kusema kwamba hakuwa akimhitaji kwa sababu alikuwa amepata mwanamke mwingine, mioyo yao ilisikia maumivu makali.

    “It is impossible,” (Haiwezekani)

    “Ndiyo hivyo!” alisema Evadia na kuanza kulia kwa uchungu. Maumivu yake ya moyo, hakika hayakuweza kupungua. Dickson alimchanganya mno.



    Kwa jina aliitwa Luciana Pentezel, msichana mrembo aliyetoka nchini Rwanda. Kwa kumwangalia tu, usingekuwa na wakati mgumu wa kusema kwamba Luciana alikuwa miongoni mwa wasichana wazuri waliowahi kuumbwa katika sayari hii.

    Alikuwa na sura nyembamba ya Kitusi, macho makubwa yaliyomuonyesha kwamba muda wowote ule usingizi mzito ungempata, alikuwa na lipsi nene huku meno yake yakiwa meupe kabisa.

    Kwa sura alivutia mno, kila mwanaume aliyemwangalia Luciana alibaki na kumbukumbu kwamba katika maisha yake aliwahi kumuona msichana aliyekuwa na urembo wa ajabu.

    Japokuwa nchini venezuela kulikuwa na wasichana wengi warembo lakini kwa Luciana kila msichana alikaa pembeni, chuoni hapo alikuwa gumzo, kila alipopita, wanaume walimwangalia kwa matamanio makubwa.

    Luciana hakuwa msichana wa tofauti, hakuwa na maringo, alipewa kuzungumza na kila mtu kitu kilichomfanya kupendwa mno.

    Katika mambo yote hayo, uzuri wote aliokuwa nao, Luciana alihusudu sana pesa, alipenda pesa sana zaidi ya alivyokuwa akimpenda Mungu. Kila alipokaa, alitamani pesa ziwe zimemzunguka, kila alipopita alitamani akanyage pesa kwenda sehemu yoyote aliyotaka kwenda.

    Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, hakuwahi kuwa katika uhusiano na mwanaume asiyekuwa na pesa. Alitoka katika familia ya kimasikini, alikwenda nchini Venezuela kama bahati tu hivyo alivyofika, alitaka kurudi nchini Rwanda huku akiwa na heshima ya juu kabisa, atafute pesa popote zilipo ili mwisho wa siku atakaporudi nchini Rwanda basi awe na utajiri wa kutosha.

    Uzuri wake ukawavuta wanaume wengi, walipogundua kwamba msichana huyo alihusudu sana pesa, wakamfuata na pesa zao na kisha kulala naye. Luciana hakuwa msichana mwenye kujali, alitembea na kila mtu aliyekuja kwake na kutanguliza pesa mbele.

    Kila alipopata mimba, kwake ilikuwa ni bahati mbaya tu, hivyo akatoa na maisha kuendelea kama kawaida. Siku zikakatika, wanaume wakazidi kutembea naye, wakampa pesa nyingi mpaka kufikisha kiasi cha dola milioni mbili, zaidi ya milioni mia nne.

    Alijiona kuwa tajiri, alijiona kuwa na sauti kubwa mara atakaporudi nchini Rwanda. Hakukoma, hakuacha, bado msururu wa wanaume uliendelea kujipanga huku kila aliyekuja kulikuwa na sharti kubwa la kuacha pesa mezani, kiasi kikubwa cha pesa ambacho hata wakati mwingine kilifika dola elfu tano, zaidi ya milioni kumi, kwa watu wenye pesa, hawakujiuliza, walitoa kiasi hicho cha fedha ili mradi mwisho wa siku walale naye tu.

    “Kuna mvulana amekuja chuo,” alisikika rafiki yake aitwaye Serena, msichana kutoka nchini Ethiopia aliyekuwa anamuunganishia kwa wanaume wengi hapo chuoni.

    “Mvulana gani?”

    “Ni Mtanzania, mzuri sana.”

    “Kweli?”

    “Ndiyo!”

    “Ana pesa?”

    “Mmmh! Sijui!”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa bila pesa, hata sidhani kama kuna mtu anaweza kuwa mzuri. Uzuri wa kweli ni pesa tu, hivyo vingine mbwembwe,” alisema Luciana huku akibinua mdomo wake.

    Hicho ndicho alichokifikiria, hakuamini kama duniani kulikuwa na wanaume wazuri, kwake aliamini katika pesa, kwamba unapokuwa na pesa, hata kama wewe ni mbaya bado utaonekana mzuri tu.

    Kila siku Serena alimwambia kuhusu mwanachuo mpya aliyekuja kujiunga chuoni hapo, mwanaume mwenye uzuri wa sura ambaye alitoka nchini Tanzania. Kila siku Luciana alikuwa bize na wanaume wenye pesa ambao walimfuata na magari ya thamani chuoni hapo.

    Alipelekwa katika kumbi za starehe, kulala kwenye hoteli za gharama ilikuwa kawaida yake, hakujuta kuwa mzuri, kila siku ilikuwa ni lazima kumshukuru Mungu kwa uzuri aliompa ambao muda huo aliona faida yake kubwa.

    “Luciana!”

    “Abeee!”

    “Kesho una ratiba gani?”

    “Nakwenda kwa Arnandro!”

    “Mmh! Yule si muuzaji wa madawa ya kulevya?”

    “Ndiyo! Kwani mimi nakwenda kuuza? Si nakwenda kuchuma pesa tu,” alisema Luciana.

    “Mmh! Ila kuwa makini.”

    “Usijali.”

    Alitembea na watu wengi mno, wenye pesa ambao walitamani kuwa na wanawake wazuri. Kwa Luciana hakutaka kujali kitu chochote kile, alichokuwa akikifikiria kwa wakati huo kilikuwa pesa tu.

    Hakujali kama mtu fulani alikuwa muuzaji wa madawa ya kulevya au alizipata pesa kwa njia haramu, alichokuwa akikiangalia ni mfuko wake kujaa pesa tu. Alizibabaikia pesa, utajiri mkubwa ukaanza kunukia maishani mwake, hakufikiria kurudi Rwanda, hata kulipokuwa na likizo, alihakikisha kwanza anatafuta fedha kwa juhudi zote na ndiyo arudi huko.



    “Ulikuwa unasemaje siku ile?” aliuliza Luciana.

    “Siku gani?”

    “Kuna siku uliniambia kwamba kuna mwanaume amefika chuo ni mzuri sana.”

    “Bado unakumbuka tu?”

    “Ndiyo! Ninataka kumuona.”

    “Yupo chuo.”

    “Leo lazima niende, sikwenda siku nyingi, nitataka kumuona,” alisema Luciana.

    “Basi usijali. Twende.”

    Alifanya mambo mengi, alifanya ufuska mpaka kufikia hatua kuona kwamba ilikuwa imetosha. Alikusanya kiasi kikubwa cha pesa, akaunti yake ikajaa pesa, hakukuwa na kitu alichokihitaji kwa wakati huo zaidi ya kuwa na mwanaume mmoja tu.

    Mtu aliyekuwa akimfikiria kwa wakati huo ni huyo mwanaume aliyeambiwa kwamba alikuwa mzuri wa sura, mvulana aliyewavutia wanawake wengi lakini hakukuwa na yeyote aliyefanikiwa kumpata.

    Kwake, Luciana hakuwa na tatizo lolote, alijua kwa namna moja au nyingine ilikuwa ni lazima mwanaume huyo amkubali kwa sababu tu alikuwa mzuri wa sura, msichana aliyependwa na wanaume wote, waliokuwa na fedha na hata wale ambao hawakuwa na kitu.

    Kilipita kipindi kirefu hakuwa amekwenda chuo. Siku ambayo alifika chuoni hapo, wanaume walipomuona, macho yakawatoka, msichana huyo alipotea kwa kipindi fulani na siku hiyo ambayo alifika chuoni hapo alionekana kuwa mrembo hasa, mara tano ya jinsi alivyokuwa kipindi cha nyuma.

    Alifika chuoni hapo kwa lengo la kumuona mwanaume aliyezungumzwa sana na rafiki yake, mwanaume aliyekuwa mzuri wa sura ambae aliamini kwamba hata yeye mwenyewe angeweza kumpenda.

    “Yupo wapi?”

    “Nani?”

    “Si huyo mwanaume uliyesema ni mzuri!”

    “Twende kule, nilimuona sehemu ya kulia chakula,” alisema Selina.

    Hawakutaka kubaki mahali hapo, walichokifanya ni kwenda sehemu iliyokuwa ikihusika na uuzaji wa chakula. Walipofika kule, wakaanza kuyapeleka macho yao huku na kule na kwa bahati nzuri macho yao yakatua kwa mwanaume waliyekuwa wakimtafuta.

    “Luciana....”

    “Abeee...”

    “Mwanaume mwenyewe yule pale,” alisema Selina huku akimuonyeshea Luciana sehemu aliposimama mwanaume huyo.

    Luciana alipomuona, kwanza akatoa mguno, hakuonekana kuamini kama duniani kulikuwa na mwanaume mzuri kama alivyokuwa yule ambaye alionyeshewa mahali pale. Moyo wake ukaanza kubeba kitu kizito, shauku kubwa ikamuingia moyoni mwake, akajikuta akiwa hajiwezi.

    “Selina...is that the one?” (Selina...yule ndiye mwenyewe?) aliuliza Luciana huku akionekana kutokuyaamini macho yake.

    “He is the one.” (Ndiye mwenyewe)

    Luciana hakutaka kubaki mahali hapo, hakuona kama alitakiwa kusimama zaidi, akili yake ilichanganyikiwa mno, hakuamini kama katika dunia hii kungekuwa na mwanaume mzuri kama alivyokuwa yule aliyeonyeshewa, tena kutoka barani Afrika.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akashindwa kuvumilia, akajikuta akianza kupiga hatua kumfuata. Mahali pale kulikuwa na gumzo, kitendo cha msichana Luciana kuonekana mahali hapo kilimchanganya kila mwanaume aliyemwangalia.



    Umaarufu wake, uzuri wake uliwadatisha watu wengi, wanaume wakabaki kimya huku wakimwangalia, hawakuamini kama yule Luciana ambaye kila siku alionekana kuwa mrembo, leo alikuwa mara tano ya zaidi ya urembo aliokuwa nao kabla.

    Alipomfikia kijana yule, akamshtua kwa kumshika bega, alipogeuka, macho ya mwanaume yule yakatua usoni mwa msichana aliyeonekana kuwa mrembo mno, msichana ambaye urembo wake alihisi kwamba hakuwahi kuuona sehemu yoyote ile.

    “My name is Luciana, a beautiful girl you have never met,” (Jina langu ni Luciana, msichana mrembo ambaye haujawahi kukutana naye) alisema Luciana huku akiachia tabasamu.

    “My name is Dickson.” (Ninaitwa Dickson).

    Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa wawili hawa kukutana, walipoonana kwa mara ya kwanza, kila mtu akatokea kumpenda mwenzake. Wasichana walichanganyikiwa na uzuri aliokuwa nao Dickson lakini kwa upande wa pili hata wanaume walichanganyikiwa na uzuri aliokuwa nao Luciana.

    Wawili hao wakatengeneza muunganiko wa hatari, kila aliyekuwa akiwaangalia alibaki akitabasamu tu kwani watu hao kama walijua jinsi walivyokuwa wazuri, hivyo waliamua kuchaguana.

    Katika kipindi cha kwanza Dickson alimkumbuka sana msichana wake aliyemuachana nchini Tanzania, Evadia, aliwasiliana naye mara chache chache lakini baada ya kuwa karibu na Luciana, akaanza kumsahau msichana huyo aliyekuwa nchini Tanzania.

    Penzi likamteka, hakuwa na sababu ya kumpenda msichana kama Evadia, kwake, alimuona msichana huyo kuwa wa kawaida sana, msichana masikini ambaye aliamini katika maisha yake asingeweza kumsaidia kwa lolote lile.

    Baada ya kuwa na Dickson, hata maisha ya Luciana yakabadilika, hakuwa kama jinsi alivyokuwa kipindi cha nyuma, akaacha tabia yake ya kufuata wanaume wengi, alijiahidi kwamba angekuwa mwaminifu na hicho ndicho kilichotokea.

    Kwa Luciana, akafika, hakutaka kusikia lolote lile kutoka kwa mwanaume yeyote yule. Wanaume wengi wakaendelea kumchombeza kwa maneno matamu tena wengine wakiweka pesa mezani lakini moyo wa Luciana ulibadilika kabisa, alichokifikiria kwa wakati huo hakikuwa pesa tena, yalikuwa ni mapenzi ya dhati ambayo aliyapata kutoka kwa Dickson ambaye alikuwa amemuacha msichana aliyekuwa naye nchini Tanzania, Evadia kwa ajili yake.



    Moyo wake ulijeruhiwa, kama ni mtu, tayari aliumwa na nyoka hivyo hata alipokuwa akiguswa na ujani, alishtuka. Moyo wake ukabadilika, kitendo alichofanyiwa na Dickson kilimuumiza mno na kujiahidi kwamba milele yote asingeweza kuwa na mwanaume hivyo alipaswa kumkatalia kila mwanaume aliyekuja mbele yake.

    Chuki kubwa ikamkamata moyoni mwake, hakuamini kama wanaume aliokuwa akiwachukia kipindi hicho, kulikuwa na mwanaume mwingine ambaye alianza kumfuatilia, mwanaume asiyemfahamu ambaye aliamua kuacha kazi zake kwa ajili yake.

    Alipomuona Laurence akimfuatilia, alichukia, aliyachukia mapenzi hivyo hakutaka kuwa na mwanaume yeyote yule. Mama yake alilifahamu hilo, kila alipomuona Laurence, alimfukuza kwa kumwambia aondoke kwani binti yake hakutaka kuonana naye.

    “Ninahitaji kumuona Evadia,” alisikika Laurence.

    “Evadia!”

    “Ndiyo mama!”

    “Huwezi kumuona.”

    “Kwa nini jamani?”

    “Nimesema huwezi. Hunielewi?”

    “Siwezi kukuelewa mpaka nimuone,” alisema Laurence.

    Japokuwa alikatawaliwa sana na Evadia lakini hakutaka kusikia, hakutaka kuacha kumfuatilia, kwake, msichana huyo alionekana kuwa kila kitu, alimpenda kwa mapenzi ya dhati kutoka moyoni, hakutaka kuwa na msichana mwingine zaidi ya Evadia tu.

    Mama yake Evadia alimkatalia kuonana naye tena huku akimtaka kuondoka nyumbani hapo lakini Laurence hakutaka kuondoka. Maisha aliyokuwa akiyaleta mahali hapo yalionekana kuwa kama filamu fulani ya kimapenzi lakini kile kilichokuwa kikitokea, alikimaanisha kwa asilimia mia moja.

    “Siondoki mpaka nimuone Evadia,” alisema Laurence huku akikaa nje ya nyumba ya kina Evadia.

    Mama Evadia hakutaka kujali sana, alichokifanya ni kuingia ndani na kuufunga mlango huku tayari ikiwa saa moja usiku. Laurence hakutaka kuondoka mahali hapo, wakati mwingine hata yeye mwenyewe alibaki akijishangaa kwamba ilikuwaje amng’ang’anie msichana mmoja namna hiyo, hakutaka kujali sana, aliendelea kusubiri zaidi na zaidi na hata kama ingewezekana kulala mahali hapo, alikuwa tayari.

    Mbu walimuuma, aliwaua na kuendelea kumsubiri msichana huyo. Alikuwa ndani, hakutaka kuingia kumfuata, alitaka msichana huyo atokea na kuzungumza naye kwani siku moja kwake pasipo kuona ilikuwa ni adhabu kali ya kaburi.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Muda ulizidi kuyoyoma, saa mbili ikaingia, saa tatu, saa nne, saa tano lakini bado Laurence hakuondoka mahali hapo.

    Ndani, Evadia alikuwa ametulia kitandani, moyo wake ulimuuma mno, bado alikuwa kwenye maumivu makali ya kukataliwa na mwanaume aliyempenda kwa moyo wa dhati.

    Alilia usiku kucha, kila siku akawa mtu wa kumlalamikia Mungu kwa kile kilichotokea, alijutia kitendo chake cha kuwa na mwanaume huyo ambaye mwisho wa siku alimsababishia maumivu makali ya moyo.

    Mama yake alipomwambia kwamba Laurence alikuwa nje akimsubiria, alikunja uso wake, alionekana kuwa na hasira kali mno. Hakutaka kuwa na mwanaume yeyote kwa kipindi hicho, alitaka kubaki peke yake, aishi peke yake na hata kama angezeeka, alitamani kuzeeka akiwa peke yake.

    Ilipofika saa tano na nusu usiku, Evadia akaelekea sebuleni ambapo akalifuata pazia chakavu na kuchungulia nje, alimuona Laurence amekaa kibarazani huku akiwa amejikunyata, baridi lilimpiga na mbu kumng’ata lakini hakutaka kuondoka mahali hapo.

    Huruma ikamuingia, akajikuta akiufuata mlango na kuufungua, akasimama mlangoni na kumwangalia Laurence ambaye naye alibaki akimwangalia machoni, tabasamu likaanza kuonekana usoni mwake.

    Laurence hakutaka kuishia hapo tu, alichokifanya ni kusimama na kumfuata Evadia pale mlangoni aliposimama na kuanza kuzungumza naye.

    “Hii yote kwa ajili yako,” alisema Laurence, alikuwa akianza kutetemeka kwa baridi kali la usiku.

    “Laurence...”

    “Nakusikiliza.”

    “Naomba uniache, sipo sawa,” alisema Evadia.

    “Najua Evadia. Macho mekundu, umenyong’onyea, ila naweza kukupa furaha maishani mwako,” alisema Laurence.

    “Najua Laurence....ila naomba uniache.”

    “Siwezi Evadia. Niambie tatizo nini.”

    “Basi tu.”

    “Hapana! Kuna kitu! Naweza kukupa mawazo pia, unachotakiwa ni kuniamini tu.”

    “Naomba tufanye siku nyingine. Rudi nyumbani.”

    “Unadhani nitakuwa na furaha? Unadhani nitakuwa katika hali ya kawaida? Evadia, ninakupenda, unalijua hilo, siwezi kurudi nyumbani huku nikikuacha katika hali hiyo, naomba uniambie, nini kinaendelea,” alisema Laurence huku akionekana kulengwa na machozi.

    “Mapenzi yanauma Laurence.....” alisema Evadia, hapohapo akaanza kububujikwa na machozi.

    Laurence akasikia maumivu makali moyoni mwake, alichokifanya ni kumsogelea zaidi Evadia kisha kumkumbatia, akaanza kumbembeleza kwa kumpigapiga mgongoni. Hakutaka kumuona msichana huyo akilia, akiumia kwa kitu chochote kile.

    Kwa jinsi alivyokuwa akiumia, hata naye maumivu yake yalikuwa vilevile. Machozi ya Evadia yakatiririka na kuulowanisha mgongo wake kwani bado walikuwa wamekumbatiana tu.

    “Usilie...”

    “Inauma Laurence....”

    “Ninaahidi kukupa furaha na kukusahaulisha kwa kila kitu,” alisema Laurence.



    Utajiri wake mkubwa aliokuwa nao ulikuwa siri kubwa, hakutaka Evadia afahamu au hata mama yake ajue hali halisi ya maisha yake. Jina lake lilikuwa kubwa nchini Tanzania lakini bahati mbaya watu hawakuwa wamemuona hivyo kuwa na shauku ya kutaka kujua kwamba huyu bilionea Laurence alikuwaje, alifananaje na aliishi vipi.

    Hakuacha kwenda nyumbani kwa kina Evadia, kidogo kwa wakati huo hali ilikuwa afadhali, msichana huyo hakuwa mtu wa kuwa na majonzi wakati wote, kwa Laurence, mwanaume huyo alijitahidi kumpa furaha.

    Hakumpa ruhusa msichana huyo kufika nyumbani kwake, alichokuwa akikifanya ni kumfuata kwao na kuzungumza naye, kama walitakiwa kutoka, walitoka kwenda sehemu, walizungukazunguka na kurudi.

    “Laurence...” aliita Evadia.

    “Naam.”

    “Hivi unaishi wapi?”

    “Kwani hupajui?”

    “Sipajui.”

    “Kweli?”

    “Kweli! Hujaniambia.”

    “Naishi Manzese Midizini.”

    “Na unafanya kazi wapi?”

    “Mmh! Mbona maswali mengi jamani?”

    “Kwani ni vibaya nikijua?”

    “Si vibaya sana, ila usijali. Nafanya kazi katika Ofisi ya Kata ya Manzese, nimeajiriwa pale kama fundi umeme,” alijibu Laurence.

    “Kumbeee!”

    “Ndiyo! Samahani kwa kukuficha kwa muda mrefu.”

    “Usijali.”

    “Leo wapi?”

    “Twende popote pale, nitakuwa na furaha kwa kuwa nipo pamoja nawe,” alijibu Evadia.

    Kwa kipindi chote hicho, Laurence hakutaka kumwambia ukweli Evadia namna alivyokuwa. Alijifanya kuwa mtu wa kawaida, hakutaka kujulikana kwa msichana huyo kama alikuwa bilionea.

    Waliondoka nyumbani kwa kina Evadia na kwenda Manzese Darajani, huko, walisimama juu na kupiga picha. Kwa Evadia ilikuwa ni furaha pekee, aliwahi kuwa na mwanaume mwenye fedha na matokeo yake kilichotokea ni kitu kilichomuumiza mno.

    Leo hii alikuwa na mwanaume mwingine, alikuwa bilionea mkubwa nchini Tanzania lakini Evadia hakufahamu hilo, kila alipomwangalia Laurence, jinsi alivyokuwa akivaa, simu aliyokuwa akiitumia, alionekana mtu wa kawaida sana.

    Walisimama katika daraja la Manzese, walikuwa wakiangalia huku na kule, kila mmoja alionekana kuwa na furaha mno. Evadia alifarijika sana, upendo wa dhati alioupata kwa mwanaume huyo ulikuwa tofauti kabisa.

    “Najifunza mengi sana kutoka kwako mpenzi,” alisema Evadia, Laurence akashtuka kusikia hivyo kwani kwa kipindi chote hicho hakuwahi kuitwa mpenzi.

    “Kama yapi?”

    “Ni bora kuwa na mpenzi asiyekuwa na kitu kuliko kuwa na mpenzi mwenye fedha,” alisema Evadia.

    “Kwa nini?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wenye fedha wanaringa, wanajiona wao ndiyo wao, ila mkikutana masikini msiokuwa na kitu kama tulivyo, kila kitu kinakwenda sawa,” alisema Evadia huku akiachia tabasamu.

    “Najua hilo mpenzi. Maisha ya mapenzi ni mapenzi, fedha haina nafasi katika mapenzi,” alisema Laurence.

    Walizungumza mambo mengi, bado Evadia hakujua mtu aliyekuwa naye alikuwa wa namna gani. Kitu alichokijua ni kwamba Laurence alikuwa masikini wa kutupwa, aliyaamini maneno yake kwamba alikuwa mtu asiyekuwa na fedha, yaani alikuwa fukara kama alivyokuwa.

    Baada ya kuzungumza naye kwa kipindi kirefu darajani, wakateremka na kuanza kuondoka mahali hapo. Walitakiwa kupanda daladala kutoka hapo Manzese mpaka Mburahati lakini hilo lilishindikana kwani kwa maneno ya Laurence, mfukoni hakuwa na kitu.

    “Kwa hiyo?” aliuliza Evadia.

    “Tutembee tu, au una hela yoyote hapo?”

    “Mmh! Sina.”

    “Basi tutembee, baadaye nitarudi hukuhuku Manzese,” alisema Laurence.

    Wakaanza kutembea huku wakizungumza mambo mengi. Ilikuwa ni ngumu mno kwa Evadia kugundua kwamba mtu aliyekuwa naye alikuwa bilionea mkubwa Tanzania, tena hata yeye mwenye alimsikia sana.

    Katika kipindi chote hicho Laurence alionekana kuwa na furaha mno, kuwa na Evadia katika maisha yake hakika kilikuwa kitu kilichompa furaha sana katika maisha yake. Walichukua dakika arobaini wakafika nyumbani kwa kina Evadia, wakamkuta mama Evadia akiwa nje.

    “Nimemrudisha nyumbani,” alisema Laurence mara baada ya salamu.

    “Sawa. Karibu tena Laurence.”

    “Asante mama.”

    Laurence akamsogelea Evadia na kumbusu shavuni, alipomaliza, akaondoka zake kurudi nyumbani. Alipofika njiani, akasimamisha bodaboda, akapanda na kuelekea nyumbani. Kila kitu alichokuwa akikifanya, alikifanya kimakusudi, hakutaka apendwe na msichana huyo kwa sababu ya fedha tu.



    Siku iliyofuata, asubuhi na mapema Laurence akajiandaa kwa ajili ya kwenda kumtembelea mpenzi wake. Kwa wakati huo, hata kazi hakutaka kufanya, alitaka kuweka mambo sawa kabisa, hakutaka kuwa bize na kazi kwani ukaribu wake na Evadia ulikuwa kitu cha muhimu kuliko vitu vingine.

    Alipomaliza kujiandaa, kama kawaida yake akachukua bodaboda na kuelekea huko. Njiani, mawazo yake yalikuwa kwa Evadia tu, alimuona kuwa na thamani mno, alipenda zaidi ya mtu yeyote katika dunia hii.

    Alipofika nyumbani kwa kina Evadia, kitu kilichomshangaza ni kwamba mlango ulikuwa umefungwa kitu ambacho hakikuwa kawaida kabisa. Laurence akachanganyikiwa, alijaribu kuufungua mlango ule, ulikuwa umefungwa kwa ufunguo, hakuishia hapo, alichokifanya ni kuanza kuita, ukimya mkubwa ulitawala ndani.

    “Evadiaaaa...Evadiaaaa...” aliita huku akiwa amesimama nje ya nyumba ile, hakukuwa na sauti yoyote iliyosikika kutoka ndani.

    Alijaribu kuzunguka mpaka nyuma ya nyumba ile huku akiendelea kuita lakini bado ukimya uliendelea kutawala mahali hapo. Hakujua ni kitu gani kilikuwa kimeendelea, alichokifanya ni kwenda kwa majirani na kuwauliza juu ya hali iliyokuwa ikiendelea mahali pale.

    “Walikwenda hospitali asubuhi sana,” alijibu jirani mara baada ya kuulizwa.

    “Nani anaumwa?”

    “Evadia. Ugonjwa wake uleule.”

    “Upi?”

    “Wanasema figo yake moja ina matatizo na ndiyo maana mara kwa mara anazimiazimia,” alijibu jirani huyo.

    “Wamekwenda hospitali gani?”

    “Mmh! Sijui! Ila nadhani Palestina, nenda huko kajaribu kumtafuta,” alijibu jirani huyo.

    Laurence akachanganyikiwa, kile alichoambiwa kilimchanganya kichwa chake. Akabaki akijiuliza juu ya ugonjwa uliokuwa ukimsumbua mpenzi wake, hakuwa ameambiwa kabla japokuwa kuna siku mama yake Evadia alimwambia kwamba alizimia.

    Hakutaka kubaki mahali hapo, alichokifanya ni kuondoka nyumbani hapo, kwa kasi kubwa na kuelekea huko hospitali. Akachukua bodaboda na kuelekea huko huku akionekana kuchanganyikiwa mno.

    Japokuwa dereva alikuwa akiendesha bodaboda kwa mwendo wa kasi, yeye aliona akiendesha kwa mwendo mdogo hali iliyomfanya kumwambia dereva huyo aongeze kasi.

    “Vuta moto kaka! Vuta moto mpaka pikipiki ipae,” alisema Laurence.

    “Kaka! Kwa magari haya, tutakufa.”

    “Kufa si tatizo, unaogopa kufa?”

    “Mmmh!”

    “Wewe ongeza kasi, hizi hospitali zimewekwa kwa ajili yetu.”

    Alisema Laurence na hivyo dereva wa bodaboda kufanya kama alivyotaka mteja wake.

    Kama kuchanganyikiwa, Laurence alichanganyikiwa mno, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea, msichana aliyempenda, aliyeonekana kuwa kila kitu katika maisha yake alikuwa hoi hospitalini.

    Hakukuwa na kitu kilichomuumiza kichwa kama hicho, kila alipomwambia dereva bodaboda aongeze kasi, aliona aliendesha kwa kasi ndogo japokuwa dereva huyo aliongeza kwa kiasi kikubwa.

    Baada ya dakika chache, wakafika katika Hospitali ya Sinza Palestina na hapohapo Laurence akaruka kutoka katika bodaboda na kuanza kukimbia kuelekea ndani, yaani hata kumlipa dereva hela yake hakukumbuka kabisa.

    “Nimekuja kumuulizia mgonjwa wangu,” alisema Laurence, alikuwa amemsimamisha nesi mmoja aliyekuwa akipita mbele yake.

    “Nani?”

    “Anaitwa Evadia.”

    “Mmmh! Nenda kule kwa upande wa magonjwa ya wakinamama,” alisema nesi yule, hapohapo Laurence akaanza kuelekea huko.

    “Braza, hujanilipa hela yangu,” alisema dereva bodaboda baada ya kumsogelea. Hapohapo Laurence akaingiza mkono mfukukoni na kutoa noti ya shilingi elfu kumi, hakutaka kusubiri chenji, akaondoka zake.

    Laurence alionekana kuwa na haraka. Hakutaka kupoteza muda mahali hapo, alichokifanya ni kuelekea kule alipokuwa ameelekezwa, alipofika, akakuta kundi la wanawake wakiwa wamekaa kwenye mabenchi yaliyokuwepo mahali pale, kila mmoja akaanza kumwangalia.

    Laurence akayapitisha macho yake huku na kule, yakagongana na macho ya mama yake Evadia, hapohapo akaanza kumfuata.

    “Kuna tatizo gani mama?” aliuliza Laurence.

    “Evadia anaumwa.”

    “Anasumbuliwa na nini?”

    “Figo yake moja haifanyi kazi vizuri, huwa inafeli,” alisema mama yake Evadia, Laurence akashusha pumzi ndefu na nzito.

    “Yupo wapi kwa sasa?”

    “Amelazwa ndani, daktari aliniambia nisubiri nje, wanamshughulikia,” alijibu mwanamke huyo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Laurence akaungana naye mahali pale. Wote wawili walionekana kuwa na mawazo lukuki, Laurence alikuwa akimfikiria mpenzi wake tu kwamba ni kwa namna gani angeweza kupata matibabu yanayotakiwa.

    Hakutaka kuonekana kama ana fedha nyingi, hakutaka ajulikane kama alikuwa bilionea lakini kwa jinsi hali ilivyokuwa ikienda, alionekana kuwa na wasiwasi kwamba ilikuwa ni lazima ijulikane kwani asingekubali kuona msichana aliyekuwa akimpenda kwa mapenzi ya dhati akifa.

    Walikaa kwa saa mbili ndipo walipofuatwa na daktari na kuambiwa kwamba waende ndani kumwangalia Evadia. Kitendo cha Laurence kumuona mpenzi wake akiwa kimya kitandani, moyo wake ukanyong’onyea, huzuni ikaanza kuugubika moyo wake, akashindwa kuvumilia, machozi yakaanza kumbubujika.

    “Amka mpenzi, amka unitazame,” alisema Laurence huku machozi yakiendelea kumbubujika.

    Evadia alikuwa kimya kitandani, kwa kumwangalia, lisingekuwa jambo jepesi kuamini kwamba mtu huyo bado alikuwa hai, kuna kipindi Laurence alionekana kuwa na hofu hivyo kusikiliza mapigo yake ya moyo ili kuona kama yalikuwa yakiendelea kudunda au yalisimama, aliyasikia yakidunda.

    Wakati wakiendelea kumwangalia msichana huyo kitandani pale, mlango ukafunguliwa na daktari mmoja, mwanamke aliyevalia koti refu jeupe kuingia ndani ya chumba kile.

    “Bado hajafumbua macho dokta,” alisema Laurence huku mashavu yake yakiwa yamelowanishwa na machozi.

    “Naomba nizungumze nanyi, mnaweza kunifuata,” alisema daktari yule.

    Hakukuwa na mtu aliyebisha, walichokifanya ni kusimama mahali pale na kisha kumfuata daktari yule ambaye safari yake iliishia ndani ya chumba kimoja, ilikuwa ni ofisi yake.

    Wakaingia ndani na kukaribishwa katika viti vilivyokuwa humo ndani. Walipokaa, daktari yule akachukua miwani yake iliyokuwa mezani na kuivaa, akachukua mafaili yaliyokuwa mezani mwake na kuyaangalia vilivyo.

    “Kuna nini?” aliuliza Laurence huku akionekana kuwa na hofu tele.

    “Mgonjwa wenu anatakiwa kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa uchunguzi zaidi,” alijibu daktari yule.

    “Tatizo nini?”

    “Anasumbuliwa na figo, haiwezi kufanya kazi kama inavyotakiwa,” alijibu daktari yule.

    “Sawa!Hakuna tatizo.”

    Laurence hakutaka kusikiliza sana daktari alisemaje, aliufahamu ugonjwa huo, watu wengi walikuwa wakifa kwa kukosa figo moja tu iliyokuwa na nguvu, aliuogopa ugonjwa huo, alikuwa tayari kuona lolote likitokea lakini si kumuona mpenzi wake huyo akifariki dunia.

    Siku iliyofuata, Evadia akarudiwa na fahamu, hawakutaka kuzungumza naye, waliambiwa kutokufanya hivyo, wakamchukua na kuelekea katika hospitali ya Taifa. Walipofika huko, msichana huyo akapewa kitanda na madaktari kuanza kazi yao.

    “Unajisikiaje?” aliuliza Laurence huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana.

    “Naendelea vizuri. Nashukuru kwa kuwa nami hatua kwa hatua,” alisema Evadia huku akijitahidi kutoa tabasamu pana.

    “Mbona haukuniambia kwamba unaumwa?”

    “Niliogopa kufanya hivyo.”

    “Kwa nini?”

    “Basi tu. Kwa jinsi ulivyokuwa ukinipenda, nilihisi kamba ungehuzunika zaidi,” alisema Evadia.

    “Hata kama mpenzi, ulitakiwa kuniambia.”

    “Naomba unisamehe.”

    “Usijali.”

    Walikaa na kuzungumza mengi, mama yake alikuwa pembeni yake, kila wakati alionekana kuwa mtu mwenye furaha mno, hakuamini kama binti yake kidogo angeendelea vizuri kama ilivyokuwa.

    Mara baada ya kukaa naye kwa dakika thelathini, mlango ukafunguliwa na daktari wa kiume kuingia, alikuwa mzee mwenye ndevu nyingi, alipoingia tu, akawataka kutoka nao nje.

    “Kuna nini?”

    “Njooni mara moja.”

    Akawachukua na kuelekea nao ofisini mwake. Tayari wawili hao walionekana kuwa na hofu, uso wa daktari yule ulionekana kuwa na jambo kubwa lililokuwa likitokea ambalo kwa namna moja au nyingine hakutaka kulizungumza mbele ya mgonjwa wodini mule.

    “Kuna nini?” aliuliza Laurence huku akionekana kuwa na hofu.

    “Figo moja ya mgonjwa wenu haifanyi kazi kama inavyotakiwa, ni lazima tufanye kidney transplant,” alisema daktari.

    “Ndiyo nini hiyo?” aliuliza mama yake Evadia.

    “Tumuwekee figo moja kwani kati ya mbili alizokuwa nazo, moja imeharibika na haifanyi kazi kama inavyotakiwa,” alijibu daktari huyo aliyeitwa Haji Mukhandi.

    “Hiyo figo nyingine tutaitoa wapi?” aliuliza mama yake Evadia.

    “Hilo ni swali gumu kwa sasa, figo haipatikani bure, ni lazima kitolewe kiasi cha fedha ili kumhamasisha mtu kutoa figo yake kwa ajili ya mgonjwa,” alijibu Dk. Mukhandi.

    “Kiasi gani?”

    “Si chini ya milioni ishirini.”

    “Unasemaje?” aliuliza mama yake Evadia huku akionekana kushtuka.

    “Ndiyo hivyo.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mama Evadia akachanganyikiwa, hakuamini kile alichoambiwa kwamba zilihitajika zaidi ya milioni ishirini ili binti yake aweze kuwekewa figo nyingine ili arudi katika hali yake ya kawaida.

    Moyoni mwake alifikiria ni kwa namna gani angeweza kupata kiasi hicho cha fedha kwani kilikuwa kikubwa sana ambacho kamwe asingeweza kukipata. Alihisi moyo wake ukimuuma sana, hakuwa na fedha, hakuwa na kitu chochote kile, kwa maana hiyo kitendo cha binti yake kuwa na figo moja inayofanya kazi kilionekana kuwa kitu cha hatari sana na ndiyo maana mara kwa mara alikuwa mtu wa kuzimiazimia tu.

    Mbele yake aliona giza, hakujua pa kuanzia, kitu pekee alichokifikiria ni kurudi mitaani na kuomba michango kutoka kwa watu wengine, ndugu, jamaa na marafiki, lakini hata kama angewachangangisha watu wengi, kiasi kilichohitajika kilikuwa kikubwa mno.

    “Kwa hiyo tufanyeje?” aliuliza Laurence huku akionekana kuwa mwenye majonzi.

    “Nitakwenda mitaani kuomba michango,” alijibu mwanamke huyo huku akijaribu kuyafuta machozi yaliyokuwa yakimbubujika mashavuni mwake.



    Japokuwa mama Evadia alijitahidi kwa nguvu zote kuzunguka huku na kule kwa ajili ya kutafuta mchango ili binti yake abadilishwe figo lakini kiasi alichokipata hakikuweza kufika kama kilivyotakiwa.

    Mbele yake aliona giza kubwa, hakujua ni kipi alichotakiwa kufanya kipindi hicho. Miaka ya nyuma alimpoteza mume wake, leo hii, binti yake pekee aliyebaki katika maisha yake alikuwa akiumwa mno na hali yake ilikuwa mbaya sana.

    Alishinda akilia, kila alipokwenda hospitalini, alikaa pembeni ya binti yake na kuanza kulia kama kawaida yake. Laurence hakuacha kufika hospitalini hapo, kila siku alifika, alishinda na Evadia, walizungumza mengi huku akimpa moyo kwamba angepona na kurudi katika hali ya kawaida kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

    Maneno hayo yalimtia nguvu Evadia, hakutegemea kupata mwanaume ambaye angejitolea kama alivyojitolea Laurence. Alifahamu fika kwamba mpenzi wake huyo alikuwa masikini wa kutupwa lakini hiyo haikuwa sababu ya kutaka kutokuwa naye, huyohuyo masikini ndiye ambaye leo hii alikuwa naye katika kila hatua aliyopitia hospitalini pale.

    Wakati wote watatu wakiendelea kuwa ndani ya chumba kile, ghafla mlango ukafunguliwa na Dk. Mukhandi kuingia ndani, uso wake ulikuwa tofauti na jinsi alivyokuwa kipindi cha nyuma, alionyesha tabasamu pana. Kila mtu aliyemwangalia daktari huyo akajua kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.

    “Kuna habari njema,” alisema daktari huyo, wote wakasimama na kumwangalia.

    “Habari gani?” aliuliza Laurence huku akijifanya kushtuka.

    “Kuna mtu amejitokeza na kutoa milioni thelathini kwa ajili ya Evadia,” alisema daktari huyo, kila mmoja akashtuka.

    “Milioni thelathini?”

    “Ndiyo!”

    “Nani?” aliuliza Laurence huku macho yake yakiwa na mshtuko mno.

    “Anaitwa Matilda John, mwanamke mmoja, alisema anafanya kazi Umoja wa Mataifa, alizipata taarifa za Evadia hivyo ameamua kumsaidia,” alijibu daktari.

    “Mwanamke? Mhh! Alijuaje kama Evadia anaumwa na anahitaji kiasi hicho cha fedha?” aliuliza Laurence.

    “Hata mimi sijui, imekuwa ni miujiza mno ambayo haikuwahi kutokea,” alijibu daktari huyo.

    Kila mmoja alibaki na maswali moyoni mwake, hakukuwa na mtu aliyefahamu hilo zaidi ya Laurence ambaye kiasi kile cha fedha alikitoa yeye kupitia kwa mfanyakazi wake aitwaye Matilda ambaye alifika hospitalini hapo na kujifanya msamaria mwema.

    Hakutaka kitu chochote kile kijulikane, na hata daktari alipokuwa akiwaambia kuhusu jambo hilo, hata yeye mwenyewe alijifanya kuwa na mshangao na aliuliza maswali mengi kama kuwapa upofu watu hao wasijue kitu chochote kile.

    Kwa kuwa kiasi hicho cha fedha kilitolewa, kilichofuata ni kuwekwa kwa matangazo katika baadhi ya magazeti ambapo wakaandika kwamba mtu yeyote aliyekuwa tayari kutoa msaada wa figo alitakiwa kufika hospitalini hapo.

    Wiki iliyofuata, zaidi ya watu mia moja wakawa wamefika hospitalini hapo tayari kwa kupimwa ili kuangalia vinasaba kama vinaendana na vinasaba vya Evadia.

    “Ila nitahitaji milioni ishirini,” alisema jamaa mmoja kwa kutoa figo yangu.

    “Hakuna tatizo, njoo ndani,” alisema Dk. Mukhandi.

    Waliwapima watu wote ili kuona kama vinasaba hivyo viliendana, kitu kilichomuumiza kila mtu, hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa tayari kutoa figo yake ambaye vinasaba vyake vilifanana na vinasaba vya Evadia.

    “Mungu wangu!” alisema Dk. Mukhandi.

    “Kuna nini?”

    “Hakuna mtu ambaye vinasaba vyake vinaendana na Evadia.”

    “Unasemaje?”

    “Ndiyo hivyo!”

    “Watu wote hao hakuna?”

    “Hakuna.”

    Kila mmoja alichanganyikiwa, hawakujua ni kitu gani kilichotakiwa kufanyika mahali hapo. Mama Evadia na Laurence wakaitwa ndani ya ofisi ya daktari na kuambiwa kile kilichokuwa kimetokea, kila mmoja alisikitika mno.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Imeshindikana?” aliuliza Laurence.

    “Ndiyo! Hakuna hata mmoja!” alijibu daktari yule. Kilio kikaanza kusikika kutoka kwa mama yake Evadia.



    ITAENDELEA

THE LOVE YOU HAD BEFORE (PENZI ULILOKUWA NALO KABLA) - 1

 





    IMEANDIKWA NA : NYEMO CHILONGANI



    *********************************************************************************



    Simulizi : The Love You Had Before (Penzi Ulilokuwa Nalo Kabla)

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    Glorious Worship Event (GWE) lilikuwa moja ya matamasha ya kusifu na kuabudu yaliyokuwa yakiandaliwa na kanisa kubwa nchini Tanzania, kanisa lililokuwa chini ya mchungaji mwenye upako, mchungaji mpakwa mafuta wa Bwana, Mchungaji Michael Yekonia wa Kanisa la Praise And Worship lililokuwa Mwenge jijini Dar es Salaam.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Vijana wengi kutoka katika makanisa mbalimbali walikuwa wakikutana katika Uwanja wa Taifa uliokuwa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusifu na kumuabudu Mungu kisha kusikiliza maneno ya Mungu kwa dakika kadhaa kabla ya sifa na kuabudu kuendelea.

    Wanachuo, wanafunzi waliosoma bweni waliomba ruhusa shuleni kwao ili kwenda kushiriki katika tukio hilo lililokuwa gumzo nchini Tanzania, tukio lililoripotiwa kila kona nchini Tanzania na kulifanya kuwafikia watu wengi zaidi na hivyo kuongeza idadi ya watu walioshiriki.

    Vijana zaidi ya laki mbili walikuwa wakikusanyika uwanjani hapo, waimbaji mbalimbali wa kimataifa kutoka Afrika Kusini, Marekani, Nigeria, Botswama na nchi nyingine nyingi walifika katika tukio hilo ambapo kulikuwa na kazi moja ya kusifu na kuabudu tu.

    Kwaya mbalimbali kutoka katika makanisa mengi jijini Dar es Salaam zilipewa nafasi za kuimba, waimbaji binafsi nao hawakuwa nyuma, kila mmoja aliyetaka kuimba siku hiyo ndiyo ilikuwa siku yake.

    Kupitia tukio hilo kubwa, vijana wengi walikuwa wakionana, walijenga urafiki na hata wengine kujikuta wakiwa kwenye uhusiano wa kimapenzi ambao moja kwa moja yalileta ndoa. Tukio hilo lilipendwa, makanisani, vijana walilizungumzia mno, kila mmoja alitaka kushiriki, akutane na vijana wenzake na kisha kuanza kumuimbia Mungu.

    Katika tukio la GWE la mwaka huo, zaidi ya vijana laki moja na nusu walikuwa wamefika uwanjani hapo, kila mmoja alifika akiwa na dhamira moja tu ya kumsifu na kumwabudu Mungu. Waliotaka kucheza kama watu waliochanganyikiwa, walifanya hivyo, waliotaka kusali mpaka kulia, wote walikuwa na uhuru.

    Hakukuwa na utulivu, kila mmoja alicheza na kurukaruka, uwepo wa Mungu ulionekana mahali hapo, waliokuwa wagonjwa, kupitia nyimbo za sifa zilizokuwa zikiimbwa uwanjani hapo wakajikuta wakipokea uponyaji hata kabla kipindi cha maombezi kufika.

    Miongoni mwa watu waliokuwa katika uwanja huo, ndani ya tukio hilo alikuwepo kijana mtanashati, kijana aliyekuwa na muonekano wenye fedha, sura ya upole, huyu aliitwa Laurence Mathew.

    Kwa kumwangalia mara moja, usingepata wakati mgumu kugundua kwamba kijana huyo alikuwa na fedha au alitoka katika familia yenye fedha. Alikuwa na muonekano wa bei na hata mavazi yake aliyoyavaa yalikuwa ni ya bei mbaya.

    Siku hiyo katika kipindi cha kusifu na kuabudu, hakutulia, alicheza mno, jasho lilimtoka, hakuangalia mavazi yake, hakuangalia kama alikuwa tajiri, alichokuwa akikifanya ni kucheza mpaka kuvua shati, alionekana kama kujitoa fahamu.

    Hakukuwa na mtu aliyemwangalia mwenzake, kila mmoja alijali yake. Kwa Laurence ilionekana kuwa nafuu kwani kulikuwa na watu wengine ambao walicheza, walirukaruka mpaka nguo kuwavuka, hawakujali, walichokuwa wakikifanya ni kumsifu Mungu aliye hai.

    “Bwana Yesu asifiweeeeee....” ilisikika sauti ya mchungaji Yekonia aliyesimama jukwaani.

    “Ameeeeeeeeeeeen....” zilisikika sauti za watu wote waliokuwa uwanjani hapo, wakaanza kupiga vigelegele huku mikono yao ikiwa hewani.

    “Leo ni siku ya kipekee sana, ni siku ambayo tumekuwa tukiisubiri kwa kipindi kirefu, leo ni siku ya kumkanyaga shetani, ni siku ya kuacha mizigo yetu msalabani, Yesu alipokufa, alibeba mizigo yetu na hata alipofufuka, bado akatuachia msaidizi ambaye ni Roho Mtakatifu,” alisema mchungaji Yekonia huku akiwaangalia watu waliokusanyika uwanjani hapo.

    Hakuzungumza sana, hakutaka kupoteza muda wa watu uwanjani hapo, aliongea kwa dakika chache sana, akamkabidhi mtu wa sifa kipaza sauti kile kisha kuendelea kumsifu Mungu.

    Wakati watu wakiendelea kumsifu Mungu, ghafla macho ya Laurence yakatua kwa msichana mmoja aliyesimama pembeni yake, kama hatua kumi kutoka alipokuwa, msichana huyo alikuwa akiimba huku akicheza, kwa kumwangalia usoni, alikuwa na uzuri wa ajabu.

    Alifanana na mwanamuziki wa Marekani, Alicia Keys, uso wake ulionyesha kuwa na tabasamu pana lililomfanya kumvutia zaidi Laurence aliyebaki akiyatuliza macho yake kwa msichana huyo tu.

    “Haleluyaaa...” alijikuta akisema Laurence, macho yake yaliganda kwa msichana yule.

    Tayari akili yake ilikwishahama, kila alipomwangalia, tayari akaanza kupata maono, akajiona akisimama mbele ya kanisa, alikuwa amevaa suti na msichana huyo alivalia shela jeupe, walikuwa kanisani hapo kwa ajili ya tukio moja tu, kufunga ndoa na hatimaye kuwa mume na mke.

    Akaulizwa kama alikuwa tayari kumuoa msichana huyo, jibu lake lilikuwa lilelile alilotaka kulitoa, ndiyo alikubali na hata alipoulizwa msichana huyo, hawakutofautiana jibu lake na Laurence, naye alikubali kuolewa.

    Ghafla akatoka katika maono yale, akamwangalia vizuri msichana yule, alionekana kuwa msichana mpole, mwenye maisha duni kwani hata mavazi aliyoyavaa yalionyesha dhahiri kwamba msichana huyo hakuwa na maisha mazuri hata kidogo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Laurence hakutaka kusimama pale aliposimama, akajikuta akianza kupiga hatua za taratibu, tena huku akicheza mpaka karibu na msichana yule ambapo alipomwangalia vizuri, akagundua kwamba machozi yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake.

    “Bwana Yesu asifiwe,” alisalimia Laurence, msichana yule hakusikia kutokana na kelele zilizokuwa uwanjani hapo.

    “Bwana Yesu asifiweeee...” alimsalimia tena kwa sauti ya juu.

    “Unasemaje?” aliuliza msichana yule.

    “Nimekusalimia.”

    “Sijambo,” alisema msichana yule huku akionekana kutokuisikia salamu ile.

    Laurence hakutaka kuendelea kuzungumza na msichana yule, akajifanya kuwa bize kuimba kama wengine. Mawazo yake yalivurugika kabisa, akili yake ikahama, alihisi kuwa na mapenzi mazito juu ya msichana yule, kila alipomwangalia, aliona akimpenda kuliko mtu yeyote yule.

    Alionekana kustahili kuwa mke wake wa ndoa, muonekano wake wa upole, sura nzuri vilikuwa vitu vilivyomchanganya vilivyo. Hakutaka kufuatilia tena kilichokuwa kikiendelea uwanjani hapo, mawazo yalimjaa juu ya msichana yule huku akiwa na hisia kali za mapenzi zikiutawala moyo wake.

    Tamasha lile liliendelea mpaka lilipomalizika majira ya saa moja usiku. Mchungaji Yekonia akasimama na kisha kufunga kwa maombi mazito na kuwaruhusu watu kuondoka uwanjani hapo.

    Laurence hakutaka kusubiri, alichokifanya ni kuanza kutafuta mazoea na msichana yule, kila alipoongea hiki au kuuliza kitu fulani, jibu alilopewa lilikuwa la kukatisha tamaa, lililoonyesha kwamba msichana huyo hakutaka kuulizwa zaidi.

    “Unasali kanisa gani?”

    “Mburahati.”

    “TAG, Pentekoste au Anglikana?”

    “TAG.”

    Kila alichouliza, alijibiwa kifupi, tena huku uso wa msichana huyo ukionekana kuwa siriazi, hakuonekana kuwa tayari kuzungumza zaidi. Kwa Laurence, hali ilionekana kuwa mbaya, alishindwa kuelewa kama kweli angeweza kufanikiwa kuwa na msichana huyo au la.

    Alichokuwa akikihitaji kwake si kuwa msichana wa kuwa naye siku kadhaa na kumuacha, alichokitaka ni kuwa naye, kufunga naye ndoa na kuwa mume na mke. Msichana huyo hakuonekana kuwa na habari, macho yake yaliangalia mbele, wakawa wamekwishafika nje, na walianza kuyafuata mageti na watu wengine.

    “Binti...” aliita Laurence, msichana yule hakuitikia, akayageuza macho yake na kumwangalia Laurence usoni.

    “Unaitwa nani?”

    “Ili?”

    “Kukufahamu tu mpendwa! Kwani kuna tatizo?” aliuliza Laurence.

    Msichana yule hakujibu kitu, aliendelea kusonga mbele. Hakutaka kuzungumza na Laurence, kila alimwangalia, alikasirika kwa kuona kwamba alipotezewa muda wake. Japokuwa alikuwa ameegesha gari lake katika eneo la uwanja huo lakini Laurence hakulikumbuka, aliendelea kwenda na msichana yule ambaye alifika kituoni na kuanza kusubiria daladala.

    “Unaishi wapi?” aliuliza Laurence.

    “Wewe kaka vipi?”

    “Jamani! Kwani kuna tatizo kama nikikufahamu zaidi mpendwa katika Bwana?”

    “Aya! Naitwa Evadia,” alijibu msichana yule.

    “Nashukuru kukufahamu. Ubarikiwe na Bwana,” alisema Laurence.

    Wote wakajikuta wakikaa kituoni hapo kusubiri daladala. Laurence hakujua msichana huyo alikuwa akisubiri daladala za wapi. Usafiri ulikuwa ni wa shida kwani kulikuwa na watu wengi mno. Kila gari lililokuja kituoni hapo, liligombaniwa hivyo kukosa nafasi.

    Waliendelea kusubiri. Evadia alikuwa akimshangaa Laurence, hakuwa akimfahamu mvulana yule, hakujua alihitaji nini. Japokuwa alionekana kuwa mvulana mwenye sura nzuri na ya upole lakini hakuwa amevutika.

    Kila daladala aliyolifuata kwa ajili ya kupanda, alifuatwa na Laurence, alipoliacha, naye Laurence aliliacha. Evadia akawa na wasiwasi mno, alichokifanya ni kusogea pembeni kabisa ya kituo kile na kutulia, alitaka kuona kama Laurence angemfuata.

    Moyo wa Laurence uliumia mno, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea. Moyo wake ulikuwa kwenye mapenzi ya dhati, hakuamini kuona kwamba msichana aliyekuwa akimpenda kwa mapenzi yote hakuwa akimtaka, hakuwa akitamani kuzungumza naye.

    Japokuwa ilikuwa ni mara ya kwanza kumuona msichana huyo lakini moyo wake ulikufa na kuoza. Alichokifanya ni kusimama, alimwangalia Evadia kwa jicho la wizi, ilipokuja daladala ya kwenda Manzese kupitia Kigogo, Evadia akaifuata, akaingia ndani, naye Laurence akaingia. Akasahau kama aliliacha gari lake la thamani ya shilingi milioni mia na hamsini katika eneo la kuegesha magari pale Uwanja wa Taifa. Alikuwa bize kumfuatilia msichana huyo tu ambaye hakujua aliishi wapi..

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Abiria walikuwa wengi ndani ya gari, Laurence alishikilia bomba huku pembeni yake akiwepo Evadia ambaye alikuwa na maswali mengi juu ya mwanaume yule aliyekuwa akimuwinda tangu walipokuwa ndani ya Uwanja wa Taifa.

    Hakutaka kuzungumza lolote na Laurence, alibaki kimya huku akisikilizia ni kitu gani kingefuata kwani kwa jinsi alivyoonekana Laurencce, hakuonekana kuwa mwanaume mwenye papara, kila alilokuwa akilifanya alionekana kuwa makini nalo.

    “Umependeza Evadia,” alisema Laurence, hakuwa na kingine cha kusema zaidi ya kumsifia msichana huyo kwa kuamini kwamba pindi unapomsifia mwanamke, una asilimia kubwa za kumpata.

    “Asante.”

    “Unashuka wapi?” aliuliza Laurence.

    “Mburahati.”

    “Oooh! Sawa, ningependa nikufahamu zaidi,” alisema Laurence, watu waliokuwa karibu nao waliyasikia mazungumzo hayo japokuwa Laurence alijitahidi kuongea kwa sauti ya chini.

    “Ili?”

    “Basi tu, kuna mengi ya kuzungumza nawe.”

    “Kuhusu nini?”

    “Usiogope, niamini.”

    “Hivi wewe kweli Mkristo au ulifika uwanjani kutafuta wanawake?” aliuliza Evadia huku akimkazia macho Laurence.

    “Mimi?”

    “Kwani naongea na nani?”

    “Mimi ni Mkristo, sikwenda pale kutafuta mwanamke, nilikwenda kumsifu na kumuabudu Mungu,” alijibu Laurence.

    “Sawa.”

    “Evadia naomba unielewe. Mimi si kijana mhuni, sikukufuata kihuni, nimekuja kwako kama mtu anayejitambua, hicho unachokifikiria kichwani mwako juu yangu si kile kilichopo kwangu. Naomba tukae sehemu tuzungumze, hata kama utataka nije nyumbani kwenu, hakuna tatizo,” alisema Laurence.

    “Uje nyumbani kwetu?”

    “Ndiyo!”

    “Kama nani?”

    “Evadia, naomba usinifikirie vibaya,” alisema Laurence.

    Kuanzia hapo Evadia hakutaka kuzungumza tena, alibaki kimya, kadiri muda ulivyozidi kwenda mbele Laurence alijitahidi kumuongelesha lakini msichana huyo akawa kimya kabisa. Kwa muonekano wa nje Laurence alionekana kuwa mtu mzuri lakini hiyo haikuwa sababu ya Evadia kumuamini.

    Safari iliendelea zaidi, Laurence hakunyamaza, alikuwa kinara wa kuongea japokuwa maswali yake yote aliyokuwa akiyauliza hakuwa akijibiwa. Gari lilipofika maeneo ya Mburahati Msikitini, Evadia akateremka, naye Laurence akateremka.

    “Unahitaji nini kutoka kwangu?” aliuliza Evadia huku akimwangalia Laurance usoni.

    “Kukuoa!”

    “Unasemaje?” aliuliza Evadia huku akionekana kushtuka.

    “Kwani haujanisikia mpendwa? Nahitaji kukuoa,” alisema Laurence.

    Evadia akaonekana kukasirika, hakutaka kuendelea kusimama mahali hapo alichokifanya ni kuondoka kuelekea katika njia iliyokuwa na michanga mingi. Laurence hakusimama, akaanza kumfuata msichana huyo kama mkia.

    Kila baada ya hatua ishirini, Evadia aligeuka nyuma, akaona bado Laurence alimfuatilia kwa nyuma. Safari iliendelea na baada ya dakika tano, msichana huyo akaanza kuifuata nyumba moja iliyochoka, kwa kuiangalia kwa nje tu ingekupa picha kwamba mtu aliyekuwa akiishi ndani ya nyumba hiyo alikuwa masikini mno.

    Nje ya nyumba ile kulikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa akisuka ukili. Laurence hakutaka kusogea zaidi, akabaki akiwa amesimama kule mbali alipokuwa, hali waliyokuwa nayo watu wale iliunyong’onyeza moyo wake, akajikuta akiingiwa na huruma mno.

    Msichana mwenye sura nzuri, msichana ambaye kwa kumwangalia tu hakutaka kujiuliza kama alistahili kuwa mke wake au la, maisha aliyokuwa akiishi yalikuwa ya kimasikini mno. Alipoiangalia nyumba ile, hakuamini kama kungekuwa na watu waliokuwa wakiishi humo.

    Ilionekana kuwa kama kibanda fulani cha kufugia kuku. Sehemu nyingine ilijengwa kwa udongo lakini sehemu nyingine ilijengwa kwa matofali yaliyoonekana kuchoka sana. Bati lililotumia kuezeka nyumba ile lilichakaa, lilikuwa na kutu nyingi, kila alipoiangalia nyumba ile, kwa kifupi, alijisikia vibaya moyoni mwake.

    Alipomuona Evadia akizungumza na mwanamke yule aliyekaa chini nje ya nyumba ile, hakutaka kusubiri zaidi, alichokifanya ni kugeuka na kurudi alipotoka. Hicho ndicho alichokuwa akikihitaji, alihitaji kupafahamu mahali alipokuwa akiishi Evadia.

    Moyo wake ulimpenda mno, alitaka awe mke wake wa ndoa, kila alipomwangalia, sura ya kuvutia, aligundua kwamba msichana huyo alistahili kuwa mpenzi wake. Hivyo akaondoka zake na kujiahidi kurudi tena siku nyingine.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Laurence alikuwa na mawazo kichwani mwake, kazi zake za kila siku hazikufanyika, muda wote aikuwa na mawazo tele, alikuwa akimfikiria msichana aliyekutana naye jana yake ambaye kwake alionekana kuwa kama malaika.

    Kila alipojigeuza huku na kule, taswira ya msichana yule ilionekana kichwani mwake, moyo wake ukavutwa, ukabuuzwa vilivyo, mapenzi mazito yaliendelea kuchipua moyoni mwake, hakutaka kitu kingine, hakuwa na hamu ya msichana mwingine, yule aliyekuwa akimfikiria alikuwa Evadia tu.

    Usiku wa siku hiyo hata usingizi haukumjia inavyotakiwa, alikuwa akimfikiria msichana huyo tu, kwake, alikuwa tayari kukosa kitu chochote kile, afilisike na kurudi kama zamani, maisha ya kimasikini yaliyokuwa yamemtesa kwa kipindi chote lakini si kumkosa Evadia.

    Alitaka kuwasiliana naye, alimuona siku moja tu lakini siku hiyohiyo ikaubadilisha moyo wake. Alikuwa msichana mrembo sana, aliyevutia, msichana mwenye umbo zuri, kitu kilichomhuzunisha ni kwamba msichana huyo alikulia katika maisha ya kimasikini.

    Mungu hakumnyima kila kitu katika maisha yake, alimnyima utajiri lakini alimpa uzuri, kitu ambacho angebaki nacho milele na si kama utajiri ambao ungeweza kupotea siku yoyote ile. Kila alipotaka kulala, usingizi bado ulikataa kuja, alibaki akigalagala huku na kule mpaka ilipofika saa nane usiku ndipo usingizi ukamchukua.

    Siku hiyo, kwa kuwa Evadia alimkaa sana kichwani, akafikia hatua ya kumuota msichana huyo, ndoto iliyomuonyesha kwamba walikuwa kanisani, alikuwa na suti nyeusi huku Evadia akiwa na shela jeupe lililomfanya kupendeza mno, ilikuwa siku ya harusi yao.

    Laurence alifurahi mno lakini mara baada ya kushtuka kutoka usingizini na kugundua kwamba ile ilikuwa ndoto, alibaki na mawazo tele, moyo wake ukakosa raha kabisa.

    Siku nyingine ilikuwa imeingia, Laurence akaamka kutoka kitandani, akajiandaa kwa ajili ya kwenda kazini. Alipomaliza kila kitu, akatoka ndani, akaelekea sehemu ya maegesho ya magari yake na kuchukua gari la kifahari, Ferrari Spider, gari ya gharama ambayo ilikuwa moja tu nchini Tanzania, akaingia ndani na kuondoka mahali hapo.

    Laurence Mathew alikuwa miongoni mwa watu waliofanikiwa sana katika maisha yao. Alikuwa mkurugenzi wa kampuni kubwa ya Amazon Tyre ambayo ilikuwa ikihusika na uuzaji wa matairi Afrika Mashariki.

    Kupitia biashara hiyo, akajikuta akitengeneza fedha, akanukia fedha na kuishi maisha ya kifahari. Katika maisha yake yote, alifikiria fedha, kila alipoamka asubuhi, kitu cha kwanza kabisa ambacho kilikuja kichwani mwake ni namna ambavyo angefanikiwa kupata fedha nyingi zaidi ya alizokuwa nazo kipindi hicho.

    Kiu yake ya mafanikio, kiu yake ya kutamani kuwa bilionea mkubwa duniani ikamfanya kupambana sana, mbali na kuwa na kampuni hiyo, pia Laurence akaanzisha kampuni nyingine iliyokuwa ikishughulika na watalii katika mbuga mbalimbali za wanyama.

    Kote huko, alikuwa katika harakati za kutafuta fedha, hakukubali kuona akishindwa, ili jambo lionekane kuwa kubwa na lililoshindikana, ilikuwa ni lazima alifanye, hakutaka kukata tamaa kwa kuliona jambo gumu na wakati hakuwahi kulifanya.

    Akawa na fedha nyingi, akawa bilionea kijana. Wanawake wengi warembo walivyoona hivyo, wakaanza kumpapatikia lakini Laurence hakutaka kabisa kuwasikiliza. Alijua fika kwamba wasichana wengi walimfuata kwa kuwa alikuwa tajiri, aliwafahamu vilivyo hivyo akaamua kuachana nao kabisa.



    Kiu yake ya mafanikio, kiu yake ya kutamani kuwa bilionea mkubwa duniani ikamfanya kupambana sana, mbali na kuwa na kampuni hiyo, pia Laurence akaanzisha kampuni nyingine iliyokuwa ikishughulika na watalii katika mbuga mbalimbali za wanyama.

    Kote huko, alikuwa katika harakati za kutafuta fedha, hakukubali kuona akishindwa, ili jambo lionekane kuwa kubwa na lililoshindikana, ilikuwa ni lazima alifanye, hakutaka kukata tamaa kwa kuliona jambo gumu na wakati hakuwahi kulifanya.

    Akawa na fedha nyingi, akawa bilionea kijana. Wanawake wengi warembo walivyoona hivyo, wakaanza kumpapatikia lakini Laurence hakutaka kabisa kuwasikiliza. Alijua fika kwamba wasichana wengi walimfuata kwa kuwa alikuwa tajiri, aliwafahamu vilivyo hivyo akaamua kuachana nao kabisa.



    Utajiri wake haukupungua, ulizidi kuongezeka kila siku. Hakujiona, alikuwa mtu wa kuwasaidia watu wengine. Ndani ya miaka mitano tu, alikuwa na utajiri uliokadiriwa kuwa shilingi trilioni tano, tajiri mkubwa kabisa.

    Kitu ambacho Laurence hakukitamani kabisa ni kujulikana, alihitaji kuwa huru, sura yake mitaani ilikuwa ngumu kujulikana. Siku nyingine ambazo alitamani sana kutembea mitaani, alivalia kawaida na kuingia mitaani, huko, alinunua karanga, alipanda daladala na kufanya mambo mengine pasipo watu kujua kwamba mtu waliyekuwa naye ndiye yule bilionea kijana aliyejijengea heshima.

    Gari yake hiyo ya zaidi ya milioni mia tano alikuwa akiitumia kwenda nayo ofisini tu, alipofika huko, aliingia ofisini, alipotoka na kwenda kwenye mizunguko yake ya kawaida, aliomba gari la kawaida la mfanyakazi yeyote na kisha kuelekea mitaani, alipotaka kurudi nyumbani, aliingia ndani ya gari lake la kifahari na kurudi nyumbani.

    “Hivi huyu Laurence ndiye nani? Sijawahi kumuona hata kidogo,” alisema jamaa mmoja, Laurence alikuwa pembeni ya meza ya magazeti, alikuwa akipitia magazeti.

    “Hata mimi mwenyewe simfahamu, sura yake imekuwa adimu sana, kama Bakhresa” alisema jamaa mwingine.

    “Kwani Laurence ndiye nani?” aliuliza Laurence huku akiwaangalia vijana wale usoni.

    “Bilionea huyo! Nasikia jamaa nuksi sana, ana hela mpaka anapagawa,” alijibu jamaa mmoja.

    “Kweli?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ndiyo! Kwani wewe haumfahamu?”

    “Hapana!”

    “Wewe mgeni nini hapa Tanzania?”

    “Ni mwenyeji. Ila si umesema hata wewe haumfahamu?”

    “Ndiyo! Nilimaanisha kwamba haujawahi kusikia chochote kuhusu yeye?”

    “Hapana.”

    “Basi umepitwa.”

    Laurence alikuwa kwenye mizunguko yake kama kawaida, hakutaka kujiweka kama mtu mwenye fedha, alitaka kujua mambo mengi sana hivyo kutembea huku na kule, kuwa huru kulimfanya kuamini kwamba angeweza kujifunza mambo mengi sana.

    Ombaomba waliokuwa mitaani walimsikitisha mno, hakuamini kama kulikuwa na watu waliokuwa na uhitaji wa namna ile, alihakikisha kwa kila ombaomba aliyekuwa akikutana naye, ilikuwa ni lazima kumsaidia kiasi fulani cha fedha.

    Katika kipindi chote hicho alikuwa akimfikiria msichana ambaye alikutana naye siku chache zilizopita, Evadia, msichana mrembo aliyekuwa akimpenda kwa moyo wa dhati, msichana ambaye hakuona kama kulikuwa na mwingine zaidi yake.

    Alizunguka sehemu mbalimbali pasipo kugundulika, alipoona kwamba alichoka sana, akaingia katika mghahawa wa chakula cha mama ntilie na kuanza kula. Alizungumza na watu wengi lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyegundua kwamba mtu huyo alikuwa bilionea, alipokula na kushiba tena huku akizungumza na watu mbalimbali kuhusu maisha kisha kuondoka zake.

    Safari yake wakati huo ilikuwa ni kwenda Mburahati, mahali alipokuwa akiishi Evadia, alizikumbuka sana njia, hakutaka kupanda daladala, alifurahi kutembea mitaani, kuangalia mazingira na jinsi watu wengine walivyokuwa wakiishi.

    Kutoka hapo alipokuwa mpaka Mburahati alichukua saa moja ndipo akafika Mburahati Msikitini na kisha kuingia mitaani. Alipita kwenye vichochoro vilevile, alipanda na kushuka, alizidi kusonga mbele mpaka alipofika katika nyumba ile kuukuu.

    Alipoiona kwa mara ya pili, moyo wake ukamuuma zaidi, aliiangalia huku akilengwa na machozi, msichana ambaye alimfanya kutokulala vizuri usiku, msichana aliyemfanya kumfikiria sana, alikuwa akiishi katika nyumba ile iliyokuwa mbele yake.

    “Shikamoo mama,” alimsalimia mwanamke aliyemkuta nje, mama yake Evadia ambaye alikuwa akisuka ukili.

    “Marahaba mwanangu, hujambo?”

    “Sijambo mama.”

    Akayatuliza macho yake kwa mwanamke yule, alionekana kupigwa na maisha, alionekana ‘kuchoka’ mno. Moyo wake ulizidi kuumia, maisha aliyokuwa akiishi mwanamke yule yalimuumiza pia.

    “Nimemkuta Evadia?” aliuliza Laurence.

    “Ametoka, alikwenda hospitali.”

    “Oooh! Sawa! Anaumwa?”

    “Ndiyo!”

    “Anaumwa nini?”

    “Kwani wewe nani?”

    “Rafiki yake.”

    “Mmh! Sasa rafiki yake ndiyo asikwambie anaumwa nini?”

    “Hahah! Sikutaka kumuuliza. Ila sidhani kama kuna tatizo endapo nikijua,” alisema Laurence.

    “Utamuuliza mwenyewe akija.”

    “Sawa! Atarudi muda gani?”

    “Bado sijajua, ila atarudi tu,” alijibu mama yake Evadia.

    Laurence hakutaka kuondoka mahali hapo, alibaki nyumbani hapo, alikaa katika mkeka huku akizungumza na mama yake Evadia ambaye muda wote alikuwa mtu wa mawazo tu, maisha aliyokuwa akiishi na binti yake yalimchanganya mno.

    Laurence hakuuliza kitu chochote kile, kila alichokuwa akiambiwa, alikubaliana nacho hata kama kililazimika kuuliziwa maswali, hakutaka kufanya hivyo. Mawazo yake yalikuwa kwa Evadia tu, hakuwa na kitu kingine alichokuwa akikihitaji zaidi ya kumuona msichana huyo tu.

    Muda ulizidi kwenda mbele, saa na dakika zilikatika, hakutaka kuondoka, alikuwa radhi kukaa hadi usiku wa manane lakini si kuondoka nyumbani hapo pasipo kumuona Evadia. Ilipofika saa mbili usiku, huku giza likiwa limetawala ndipo mama yake Evadia akamwambia kwamba alitakiwa kuondoka lakini Laurence akagoma.

    “Haiwezekani mama, ni lazima nionane na Evadia leo,” alijibu Laurence.

    “Kwani kuna nini?”

    “Nataka nionane naye tu, wala usijali.”

    “Sawa. Basi ngoja nikuletee chakula ule,” alisema mama yake Evadia.

    “Sawa.”

    Hakutaka kujivunga, aliletewa chakula, ulikuwa ugali na dagaa, pembeni kulikuwa na mchicha. Tangu awe bilionea hakuwahi kula chakula cha namna hiyo ila kwa sababu alikuwa amedhamiria kuishi maisha ya chini, akaamua kula.

    Bado mama Evadia alikuwa na maswali mengi, kila alipomwangalia Laurence alishindwa kufahamu vizuri mwanaume huyo alikuwa nani. Ni kweli Evadia alikuwa na marafiki lakini hakuwahi kumuona mwanaume huyo hata siku moja.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kila alipotaka kumuuliza, alibaki kimya, hakutaka kuuliza kitu chochote kile, akabaki na maswali yake moyoni.

    Ilipofika saa 3:18 usiku, ndipo Evadia akatokea mahali hapo. Aliona nje ya nyumba yao kukiwa na watu wawili, mmoja alikuwa mama yake, alimtambua lakini mtu wa pili hakuweza kumtambua. Alionekana kuwa na hofu, hakujua mtu yule alikuwa nani na alifika hapo kufanya nini.

    Akaanza kusogea karibu kwani kule mbali alipokuwa hakuwa akifahamu mtu huyo alikuwa nani. Mwanga wa koroboi uliokuwa ukiwaka ndiyo uliomfanya kugundua kwamba mtu aliyekuwa amekaa katika mkeka pamoja na mama yake alikuwa Laurence, mwanaume yule aliyemfuatilia siku chache zilizopita.

    “Karibu Evadia,” alimkaribisha Laurence, Evadia hakujibu kitu zaidi ya kusalimia na kuingia ndani.

    Moyo wa Laurence ukapoa, kitendo cha kumuona Evadia mahali hapo kiliufanya moyo wake kujisikia ahueni, hakuwa kwa siku kadhaa na kitendo cha kumuona tena mahali hapo kilimfanya kujisikia faraja.

    Alimpenda, alimthamini, alitamani kuwa naye maisha yake yote. Kitendo cha kumuona mahali hapo kilimfanya kujisikia faraja, mapenzi aliyokuwa nayo kwa msichana huyo yakaongezeka zaidi.

    “Kweli wewe ni rafiki yake?” aliuliza mama Evadia.

    “Ndiyo!”

    “Kweli?”

    “Kweli tena.”

    “Mbona hajazungumza hata na wewe?”

    “Sijui! Inawezekana amechoka. Si ametoka hospitali? Inaelekea hajisikii vizuri,” alijitetea Laurence huku akijitahidi kuonyesha tabasamu pana usoni mwake.

    Mama Evadia alionekana kuwa na wasiwasi, japokuwa Laurence aliongea kwa tabasamu pana tena huku akionekana kujiamini lakini mwanamke huyo akasimama na kuelekea ndani.

    Lengo lake kubwa lilikuwa ni kumuita binti yake kwa kuamini kwamba inawezekana hakuwa amemtambua Laurence pale nje alipokuwa. Huku nyuma, mapigo ya moyo wa Laurence yalikuwa yakidunda kwa nguvu. Wakati mwingine alitamani kukimbia.



    Walipendana kana kwamba hakukuwa na watu waliopendana kama walivyokuwa. Kila walipokuwa, walikuwa pamoja, walitembea pamoja huku wakati mwingine wakienda kutazama filamu pamoja.

    Muonekano wao wa nje, walionekana kuwa watu waliopendana kwa mapenzi ya dhati kiasi kwamba kila mtu akahisi kwamba hakukuwa na kitu ambacho kingekuja kuwatenganisha, ukaribu wao ungeweza kwenda mbele zaidi mpaka pale ambapo wawili hao wangeoana na kuishi kama mke na mume.

    Alikuwa ni kijana Dickson Maghembe na msichana aliyeitwa kwa jina la Evadia Johnson. Wawili hawa walikuwa gumzo kila walipokuwa. Japokuwa walikuwa wametoka katika familia tofauti lakini hakukuwa na mtu aliyeliangalia hilo, kila mtu alikuwa akimuona mwenzake sawa na alivyokuwa.

    Evadia hakuwa msomi, aliishia darasa la saba baada ya baba yake kufariki dunia. Kuanzia hapo, hakusoma tena, maisha yake yakawa ni nyumbani tu huku akimtegemea mama yake ambaye alikuwa akifanya biashara ya mikeka aliyokuwa akiifuma yeye mwenyewe.

    Kutokana na uzuri wake, wanaume wengi walimfuata Evadia, walimtaka kimapenzi kwa maneno matamu, kwa kutumia fedha lakini yote hayo yalionekana kuwa si lolote lile kwake. Alichokuwa akikiangalia ni mapenzi kwa Dickson tu, hakutaka kuwa na mwanaume yeyote yule katika maisha yake zaidi ya huyo mpenzi wake.

    Dickson ambaye alikuwa akisoma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kila alipotoka chuoni ilikuwa ni lazima kupita nyumbani kwa kina Evadia na kuzungumza naye. Alimpenda, hapo alipokuwa akifika, alimchukua na kisha kuondoka naye kuelekea nyumbani kisha baadaye kumrudisha.

    Wazazi walifahamiana, mara kwa mara walitembeleana, waliwahusia watoto wao kuhusu maisha, ni jinsi gani walitakiwa kuishi na kupenda mpaka pale watakapooana. Kila neno waliloambiwa, liliingia vichwani mwao na kutulia, ashki kubwa ya kupendana iliikamata mioyo yao, hawakuona kama kungekuwa na chochote kile ambacho kingewafanya kuachana.

    “Dickson...” aliitwa Evadia.

    “Ndiyo kipenzi.”

    “Ninakupenda.”

    “Najua hilo, ila haunishindi mimi!”

    “Kweli?”

    “Kwa nini nikudanganye. Ni lazima nikuoe, siwezi kukuacha maishani mwangu,” alisema Dickson huku akiachia tabasamu pana.

    Waliahidiana mambo mengi, waliahidiana kuishi milele, waliahidiana kila kitu walichokiona kustahili kuingia katika mahusiano yao ya kimapenzi. Hakukuwa na mtu aliyetaka kumwacha mwenzake, kila siku waliendelea kuwa pamoja.

    Wakati wakiyaongea hayo, walikuwa ufukweni, mapenzi yaliwachukua, walijikuta katika ulimwengu mwingine wa mahaba, wakiogelea katika dimbwi la mahaba na kila walipoangalia mbele, hawakuamini kama ingetokea siku moja wangeachana.

    Mara baada ya kupita miaka mitatu ya uhusiano wao wa kimapenzi, hapo ndipo harakati za ndoa zikaanza kufanyika. Wakajipanga kwani hakukuwa na kitu chochote ambacho kingeweza kuwatenganisha au kuwazuia wao kufunga ndoa na kuishi pamoja.

    “Evadia, ninakuahidi kwamba hakuna mwingine zaidi yako,” alisema Dickson huku akichia tabasamu pana.

    “Na iwe hivyo mpenzi, ninatamani kuolewa nawe,” alisema Evadia, wakakumbatiana na kupigana mabusu mfululizo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakati wakijiandaa na harusi, hapo ndipo baba yake Dickson alipomwambia kijana wake kwamba alitakiwa kuongeza elimu yake nchini Venezuela, hivyo alitakiwa kwenda huko haraka iwezekanavyo na mara atakaporudi nchini Tanzania basi mikakati ya ndoa iendelee na hatimaye wawili hao wafunge ndoa.

    “Nitabaki na unyonge mpaka utakapotudi,” alisema Evadia, macho yake yalikuwa yakikusanya machozi.

    “Najua mpenzi, hata mimi sitokuwa na furaha kamwe, hakika nitakuwaza wewe, sitoweza kuishi kwa furaha huku ukiwa mbali nami,” alisema Dickson, naye alionekana kuwa na huzuni mno.

    Japokuwa walihuzunika lakini mwisho wa siku Dickson akaondoka na kuelekea nchini Venezuela. Kuwasiliana ilikuwa ni kwa tabu sana, kutokana na Evadia kutokupata elimu ipasavyo, hakuwa na akaunti ya barua pepe, hakuwa akitumia mtandao wowote ule wa kijamii, kitu pekee alichokuwa akikifahamu ni kutumia simu kwa kupiga na kutuma meseji tu.

    Evadia alikosa raha, kila alipokuwa, alionekana kuwa na mawazo tele, hakuzoea kuwa mbali na mpenzi wake huyo, kila siku maisha yake yalikuwa ya huzuni mno. Wakati mwingine hakuwa akila chakula, mawazo yalitawala kichwani mwake, kila alipokaa, alimfikiria Dickson tu.

    Siku zikaendelea kukatika, ni mara chache Dickson alikuwa akimpigia simu na kuzungumza naye na kitu pekee alichokuwa akimwambia ni kuwa mwaminifu mpaka pale ambapo angerudi tena nchini Tanzania.

    “Nitakuwa muaminifu milele mpenzi,” alisikika Dickson.

    “Nami nakuahidi uaminifu wangu,” alisema Evadia huku machozi yakimbubujika mashavuni mwake, hakika alisikia moyo ukimchoma mno.

    Hayo ndiyo yalikuwa maneno waliyoambiana kila siku ambazo Dickson alipopiga simu. Mapenzi yaliendelea kuchipuka huku nchini Tanzania Evadia akiendelea kuwaambia marafiki zake wachache kwamba mara mpenzi wake atakaporudi nchini Tanzania basi wangeweza kuoana.

    Baada ya miezi mingine kupita hapo ndipo mabadiliko yalipoanza kutokea, Dickson hakuwa mpigaji wa simu kama zamani na hata pale alipokuwa akipiga, stori zake zilikuwa za kawaida sana na hata kwenye umaliziaji wake, haukuwa kama ule uliokuwa kipindi cha nyuma.

    “Nakupenda mpenzi,” alisema Evadia mara baada ya kuzungumza sana na Dickson ambaye kwa kumsikia tu, hakuonekana kuwa na raha.

    “Asante...”

    “Asante tena?”

    “Ndiyo! Unataka nijibu nini tena?”

    “Si kama zamani!”

    “Kivipi?”

    “Kwamba unanipenda pia,” alisema Evadia.

    “Yaani neno hilo kila siku, acha kukariri Evadia,” alisema Dickson.

    “Umeniita jina langu! Mungu wangu! Sijawahi kusikia ukiniita jina hilo miaka na miaka, imekuwaje?” aliuliza Evadia, alionekana kuchanganyikiwa.

    “We ulitaka nikuite vipi?”

    “Huwa unaniita mpenzi, imekuwaje tena?”

    “Potezea.”

    Aliposema neno hilo, Dickson hakutaka kuiacha simu hewani, alichokifanya ni kukata na kisha kuizima.

    Evadia akachanganyikiwa, hakuamini kile kilichotokea, mpenzi wake, aliyempa thamani kubwa moyoni mwake, leo hii alikuwa akizungumza mambo yaliyompa maswali mengi kichwani mwake.

    Akahisi kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake, machozi yakaanza kujikusanya machoni mwake na baada ya sekunde chache, yakaanza kububujika mashavuni mwake, hakika aliyasikia maumivu makali moyoni mwake.



    Alikuwa na ndoto za kuolewa, zikafutika, alikuwa na ndoto za kupata maisha bora, nazo zikafutika, alihisi kuchanganyikiwa, mapenzi aliyokuwa nayo juu ya Dickson yalimzuzua mno na hata pale mambo yalipoanza kubadilika, alihisi kuchanganyikiwa.

    Kauli za Dickson ambazo alizitoa siku hiyo zilimchanganya, akajiona kama akiukaribia uchizi, akabaki akibubujikwa na machozi, moyo wake ulimuuma mno. Hakujua kilichosababisha Dickson kubadilika ghafla namna hiyo, alibaki akijiuliza lakini mwisho wa siku hakupata jibu lolote lile.

    Alibaki na maumivu moyoni mwake, hakutaka kumwambia mtu yeyote kile kilichokuwa kimetokea, hakutaka kumwambia mama yake wala wazazi wa Dickson kwa kuamini kwamba inawezekana siku hiyo ambayo alizungumza naye Dickson hakuwa na wakati mzuri, hivyo kuamini kwamba kama angepiga siku nyingine basi mambo yangekwenda kama yanavyotakiwa kwenda.

    Usiri wenye kuumiza uliendelea kubaki moyoni mwake, hakutaka mtu yeyote yule afahamu. Baada ya kupita miezi miwili akapokea simu nyingine kutoka nchini Venezuela, alikuwa Dickson ambaye alimpa ujumbe mmoja mkubwa, ujumbe uliomsikitisha mno, alimwambia kwamba kama akipata mwanaume wa kumuoa, awe radhi kuolewa.

    “Unasemaje?” aliuliza Evadia huku akionekana kushtuka.

    “Kwani umesikia nini?”

    “Nataka uniambie tena!”

    “Kwani umekuwa kiziwi siku hizi?”

    “Hapana, ila...”

    “Hebu kuwa muelewa Evadia. Kama kuna mwanaume atajitokeza na kukwambia kwamba anataka kukuoa, usiichezee bahati hiyo, kuwa naye,” alisikika Dickson kwenye simu.

    “Dickson...”

    “Unasemaje?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwa nini unan....” aliuliza swali lakini hata kabla hajamaliza kuliuliza swali hilo, hapohapo akaanza kulia.

    “Hebu acha utoto, sasa kipi kinakuliza? Kwani wewe ndiye wa kwanza kukataliwa? Nyamaza bwana, nitakuja na Luciana mwezi ujao, utamuona tu wifi yako,” alisikika Dickson na kukata simu.

    Kulikuwa na watu wengi walioumizwa mioyoni mwao, wengine walilia na wengine kujiua kabisa, wengine wakakata tamaa ya kupendwa, hawakuyapenda mapenzi tena, waliwachukia wanaume na hata wanawake.

    Maisha yalibadilika, wengine wakatishia kunywa sumu kutokana na maumivu makali ya kuachwa mapenzini, tena kwa watu waliokuwa wakiwapenda mno. Ingawa kulikuwa na wengi waliowahi kuumizwa mapenzini lakini kwa Evadia akahisi kwamba hakukuwa na mtu aliyepatwa na maumivu makali moyoni mwake kama alivyopata kipindi hicho.

    Hakuamini kilichotokea, wakati mwingine alihisi kama yupo ndotoni na baada ya muda fulani angeamka kutoka usingizini, ukweli ni kwamba hakuwa ndotoni, kile kilichokuwa kikitokea, kilimtokea katika maisha yake, kilikuwa ni kitu halisi ambacho kilimuumiza mno.

    Akakonda kwa mawazo, hakutaka kula, kila siku alipokuwa akiulizwa na mama yake tatizo lilikuwa nini, hakutaka kumwambia zaidi ya kumdanganya kwamba alikuwa akiumwa.

    Moyo wake uliamini kwamba kuna siku Dickson angerudi na kumwambia kwamba alikuwa akimtania, alifanya vile kwa kuwa alitaka kujua ni kwa jinsi gani alikuwa akimpenda.

    Alijipa moyo kila siku lakini pamoja na kujifariji sana, majibu yalikuwa yaleyale kwamba mwanaume huyo hakutaka kuwa naye kwa kuwa alimpata msichana mwingine aliyeitwa kwa jina la Luciana.

    Hicho ndicho kilichokuwa kikimpa wakati mgumu Evadia, hali ya kuwa na mawazo mengi, wakati mwingine ikamfanya kuhisi kizunguzungu, alipokuwa akitembea mitaani, alianza kupepesuka na mwisho wa siku kuanguka chini, alipoinuka alijikuta akiwa kitandani tena huku amezungukwa na dripu zilizotundikwa juu yake.

    Hali hiyo haikutokea mara moja au mara mbili, ndani ya mwezi huo ambao aliambiwa na Dickson kwamba alikuwa amempata mwanamke mwingine, kuanzia siku hiyo alikuwa kwenye hali mbaya, kuanguka na kuzimia ilitokea kwa zaidi ya mara tano kitu kilichompelekea mama yake kuwa na wasiwasi kwamba kulikuwa na tatizo.

    “Evadia...”

    “Abee mama.”

    “Hebu niambie kuna nini.”

    “Hakuna kitu.”

    “Sasa kwa nini unaanguka mara kwa mara?”

    “Sijui. Huwa ninajisikia kizunguzungu tu.”

    “Mmmh!”

    “Ndiyo hivyo!”

    “Na umemwambia Dickson?’ aliuliza mama yake.

    Hata kabla Evadia hajajibu swali hilo, akaanza kulia, mama yake alishtuka, hakujua ni kitu gani kilichokuwa kikimliza mtoto wake kiasi kile. Alijaribu kuuliza ili ajue sababu lakini hakupewa majibu zaidi ya msichana huyo kulia zaidi.

    Siku zikaendelea kukatika, hakupokea simu nyingine kutoka kwa Dickson hali ilitoashiria kwamba kile kilichokuwa kimetokea, hakikuwa na utani hata mara moja, mwanaume huyo alikuwa amemaanisha alichokizungumza na kwamba alitakiwa kutafuta mwanaume mwingine wa kumuoa.

    “Mama!”

    “Unasemaje binti yangu?”

    “Kuna kitu nataka kukwambia.”

    “Kitu gani?”

    “Kuhusu Dickson.”

    “Amefanyaje?”

    Hata kabla Evadia hakujibu swali hilo akaanza kulia, kumbukumbu zake zikaanza kurudi nyuma, siku ambayo alipigiwa simu na mwanaume huyo kisha kuambiwa kwamba kama kungekuwa na mwanaume mwingine amemfuata kwa ahadi ya kumuoa basi akubaliane naye na huku siku nyingine akimwambia kwamba tayari alikuwa amepata mwanamke mwingine.

    Alilia na kulia, mama yake alijaribu kumbembeleza na kumuuliza nini kilikuwa kinaendelea lakini hakujibu, aliendelea kulia, na aliponyamaza baada ya dakika tano kupita, hapo ndipo alipoamua kumwambia mama yake juu ya kilichokuwa kimetokea.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mama yake hakuamini alichokuwa amekisikia, wakati mwingine alihisi kama alikuwa akimtania, alimjua vilivyo Dickson, jinsi alivyompenda binti yake, alifahamu ni kwa kipindi gani walikuwa wameweka ahadi ya kuoana na kuishi milele kama walivyokuwa wameambiana.

    Kuambiwa kwamba mwanaume huyo alikuwa amepata mwanamke mwingine, hakika ilimchanganya na akashindwa kumwamini Evadia moja kwa moja.

    “Haiwezekani,” alisema mama yake.

    “Ndiyo hivyo mama! Dickson amepata mwanamke mwingine, anaitwa Luciana,” alisema Evadia.

    “Dickson huyuhuyu?”

    “Ndiyo mama!”



    ITAENDELEA



MTU WA UFUKWENI (THE BEACH MAN) - 5

 







    Simulizi : Mtu Wa Ufukweni (The Beach Man)

    Sehemu Ya Tano (5)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilikuwa ni kesi ambayo ilikosa mahali pa kusimamia. Kesi Isiyo na ushahidi wowote wala mwelekeo hasa. Baadaye uchunguzi ulifanywa na Polisi haukuona kuwa Ramson alihusika kwa lolote. Ilionekana kwamba muuaji ni Dr. Jackson ambaye alimpiga risasi mkewe na kutaka kumuua Ramson badala yake risasi ikampiga ya mguuni. Baadaye alijipiga risasi ya kichwa mwenyewe. Uchunguzi wa alama za vidole kwenye bastola ile uliona kuwa mtumiaji wa silaha hiyo alikuwa ni Jackson mwenyewe.

    Wakati upelelezi wa haya yote unafanyika, Ramson alikuwa Hospitali akitibiwa akiwa chini ya ulinzi. Mpaka anapata nafuu kubwa kwenye jeraha lake la mguu, upelelezi ulimwondoa kwenye shutuma na baadaye walimwachia huru. Ramson alitoka Hospital asijue la kufanya. Ila alikumbuka kuwa karatasi zile alizificha sana baada ya kukabidhiwa na marehemu Dr Jackson.

    Alipoingia kwenye gari la Jackson aligundua picha na vyeti. Picha zile zilimwonyesha yeye akiwa na mke wa Dr. Jackson wakiogelea na nyingine zilizokuwa na ushahidi pia vitu vte hivyo alivificha pamoja na zile hela. Alifanya hivyo kusudi kuondoa ushahidi wa yeye kuhusishwa na vifo vya Dr. Jackson na mkewe.

    Hii pekee ndiyo iliyomweka mbali na kesi ya mauaji hayo. Baada ya yote hayo Wafanya kazi wake walipokuja aliwaaagiza wampeleke mtoto kwa mmoja wa rafiki zake. Simu aliyompigia rafiki yake huyo ilimfanya akubali kumtunza mtoto huyo, hadi hapo mambo yatakapotulia. Katika maficho alikozificha karatasi zile na fedha alizokabidhiwa na Marehemu Mary palikuwa salama. Baada ya kurudi akiwa huru alikuta vitu vikiwa vile vile kama alivyoweka.

    Alikaa na kuamua kusoma makaratasi yale aliyopewa na Dr. Jackson, maana tangu apewe hajawahi kuyapitia na hakujua kuwa yalihusu nini! Mwili ulimsisimka sana baada yakusoma kichwa cha habari! Maneno yaliyofuata yalimfanya apanue mdomo kwa mshangao! Kila hatua aliyoipiga katika kusoma maneno yaliyopo pale, vilimfanya aduwae! Ilikuwa ni zaidi ya habari! Ilimshangaza na kumshtusha kwani ndani ya karatasi zile Dr.Jackson alirudia kusema kuwa, hakuwa na budi kufa kwa sababu hataweza kustahimili kuishi bila Mary mkewe!

    Na pia asingevumilia kupata hukumu ya mauaji ya mkewe ambayo mwenyewe hakukusudia kufanya hivyo. Lakini jambo la msingi ni kwamba hakuwa na ndugu hata mmoja, ila wazazi wake tu ambao wako kijijini nao ni wazee sana. Kwa hiyo ameamua kumrithisha Ramson mali zake zote, ambazo ni pamoja na mahotel mawili ya kitalii yaliyopo Lushoto mjini.

    Makampuni ya usafirishaji iliyopo jijini Dar es Salaam. Mashamba mawili yenye heka kumi kila moja, moja likiwa Lushoto na jingine likiwa Korogwe Pia kulikuwa na nyumba tatu; Moja ikiwa hapo mjini Tanga na nyingine ikiwa Arusha na nyingine ilikuwa Ostabay Dar es Salaam.

    Fedha zilizoko Bank zilikuwa ni Shilingi milioni mia sita na hamsini. Mwisho wa yote akamwambia atafute wakili kwa sababu yeye pamoja na mali zote hizo hakuwahi kuweka wakili binafsi. Wakili atakayemweka amsimamie katika kubadilisha hati za umiliki wa mali zake, kutoka jina la Dr. Jackson Kigoi kwenda jina lake yaani Ramson. Hakujua aanzie wapi baada ya kuona mambo hayo.

    Alimshangaa sana Dr. Jackson kwa moyo wake wa ajabu! Alikaa na kuangalia jinsi ya kufuatilia mambo ya sheria kwa ajili ya kuwakilisha barua ile. Alijua kuwa ile ndiyo itakayomsaidia pindi atakapoifikisha kwa mwanasheria. Alijua kuwa huko atapata mwongozo wa namna ya kusimamia mali zile za Marehemu Dr.Jackson. Akili hazikutulia kabisa! Alikuwa na mchanganyiko wa mawazo.

    Moyo wake ulikuwa umejaa huzuni na mawazo mengi, kwa mtihani mkubwa sana aliopewa na Dr. Jackson. Kwa ujumla alikuwa hajui aanzie wapi ili kuziweka malizote zile chini ya himaya yake. Kichwa kilijaamambo mengi na baadaye alijikuta akipitiwa na Usingizi. Usingizi huu uliomchukuwa muda mrefu kabla ya kuamka na kutafuta jibu la mitihani iliyopo mbele yake.



    Ramson Aliingia ndani baada ya kufunguliwa mlango! Aliitikia salamu ya dada aliyemfungulia mlango na kuingia ndani. Sebuleni alimkuta mzee Kigoi akiwa amekaa na mkewe. baada ya salamu Ramson akaanza mazungumzo. “Wazee wangu naomba sana mnisamehe kwa kusababisha kifo cha Dr. Jackson!”

    Nikijieleza ni habari ndefu sana lakini naomba mnisamehe sana kwa yote wazee wangu.” Alisema hayo huku akilia machozi mbele ya wazee hao. ..kisha akaendelea: “Mimi ndiye Ramson mmiliki wa ufukwe wa mwahako ambako Dr. Jackson na mkewe walipofia. Nimetafuta sana nijue mahali mlipo wazee wangu mpaka nimefika leo. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baba na mama naombeni mnisamehe juu ya yote yaliyotokea.” Alihitimisha na kunyamaza kimya ili asikie kile wazee hao watakachosema. “Kijana Hebu inuka ukae na ufute kabisa machozi yako.” Alisema Mzee Kigoi na Ramson akanyanyuka na kukaa kwenye kochi lililokuwa kando yake; alipokuwa ametulia Mzee Kigoi aliendelea: “Huwezi kuomba msamaha kwa kazi ya Mungu kijana.

    Mimi ninavyojua ni kwamba Mwanangu Jackson alikufa kwa siku zake! Potelea mbali kama kulikuwa na sababu gani lakini ninachojua ni kwamba kifo chochote hakikosi sababu au mlango wa kupitia. Wewe uwe na amani kabisa sioni wapi umekosea katika msiba huu.” Alisema Mzee Kigoi na kumtazama mkewe aliyekuwa kimya wakati wote.

    “Kijana mimi na baba yako hapa ni wazee sasa. mambo mengi tumepitia na wasawahili wanasema: “Kuishi kwingi ni kuona mengi. Tunajua mengi na tumejifunza mambo ya ajabu sana katika maisha yetu haya. Tunajua kuwa kifo chochote kinapompata mtu kinatafuta pa kupitia tu. Pia kifo hicho hakiji hadi wakati wa mtu uwe umefika. Kama wakati haujafika kifo hukaa mbali kabisa na wala Jackson na mkewe wasingelikufa. Lakini ninavyojua ni kwamba kila jambo hupangwa na mwenyezi Mungu. Asingepanga mtoto wetu asingelikufa.

    Kwa hiyo mwanangu uwe na amani tu.” Alisema hivyo mke wa mzee Kigoi akimwondoa wasiwasi Ramson. “Asanteni sana wazazi wangu.” Baada ya hapo Ramson aliwasomea ile karatasi aliyopewa na Dr. Jackson kisha baada ya hapo akasema: “Wazazi wangu kuja kwangu hapa kuwatafuta ni ili pia niwaachie jukumu hili. Kwangu mimi sistahili kurithi hata shilingi moja. Nitasimama pamoja na wewe baba katika kuhakikisha kuwa mali hizi zote zinaingia mikononi mwako.” Alisema Ramson akiwa kashikilia karatasi ile. “Kijana wewe ni mtu wa ajabu sana!! Alifoka Mzee kigoi,

    “Sijaona mtu mwenye busara kama wewe katika maisha yangu! Wenzio wanalilia mali mpaka kudiriki kushikilia silaha na kumwaga damu za watu wewe unapewa kihalali mali hizi na unazikataa!” Aliongea kwa mshangao mkubwa Mzee Kigoi na kumgeukia mkewe ambaye naye aliishia kuguna tu na kutoa tabasamu la mshangao. .. kisha akaendelea “Mimi na mama yako tunakupokea rasmi leo kuwa mtoto wetu. Mali zote hizo utazisimamia wewe!”

    Kama marehemu Jackson amefikiria mpaka akaamua kukuandikia maneno haya juu ya mali zake zote, moja kwa moja amekuidhinisha kuwa mtoto wetu badala yake. Huna haja ya kutupa sisi mzigo ambao hatutauweza. Uzee tulionao huu tutaweza wapi kuingia kila mahali kutafuta sijui hati gani za umiliki wa vitu hivyo?

    Sisi kwa moyo wote tunakupa baraka zote, kama alivyofanya ndugu yako nenda kashughulikie hayo mambo. Ikiwa kuna mahali nitatakiwa kuja kudhibitisha lolote nitafanya hivyo. Jukumu lako litabaki kututunza sisi wazazi wako kama alikuwa akifanya marehemu kaka yako sawa?” Alihitimisha Mzee Kigoi na mama alimuunga mkono.Baada ya hapo Ramson akaagana nao na kuingia Rasmi katika michakato na majukumu mapya.



    Kila kitu kilienda kama kilivyopangwa. Wazazi wa Dr. Jackson walihamishwa kutoka kijijini na kupewa nyumba nzuri na ya kifahari Mjini. Ramson aliwawekea wafanyakazi wa kuwahudumia kwa kila kitu. Hoteli ziliendelea vizuri na makampuni yote. ufukwe nao ulitengenezwa na kuwa bora sana kwa kujengewa mahoteli ya kifahari ya kulala watalii.

    Maboti mapya na ya kisasa yalinunuliwa. Kijiji cha Tabu yanini mkutano mkubwa ulifanyika. Ramson aliamua kufanya mambo ya kimaendeleo; ikiwa ni pamoja na kuweka mabomba ya maji badala ya visima na kujenga Hospitali kubwa na nzuri kabisa. Historia iligeuka na kumfanya Ramson kuwa mtu wa thamani kubwa anayetegemewa kwa mambo mengi.

    Babu yake Ramson aliona fahari kubwa sana Baada ya kukamilishiwa nyumba yake mpya na nzuri kijijini hapo. Kwa ujumla Ramson alikuwa ndiye mfadhili katika kijiji cha Taabu yanini. Aligeuka na kuwa gumzo katika nchi yote, kwa kusababisha maendeleo na mabadiliko katika fukwe. Wengi walijaribu kuiga katika kutengeneza baadhi ya fukwe, hivyo alifanyika cheche yenye kuleta moto mkubwa wa maendeleo, katika fukwe za pwani ya bahari na hata katika maziwa makuu nchini Tanzania.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    * * *

    “Hiyo ndiyo Historia kamili ya maisha yangu!” Nilisema huku nikimtazama Jobiso Baro usoni. Alikuwa ameduwazwa na safari yangu ya maisha jinsi ilivyokuwa na mabonde na milima mikali! Hakutaka kabisa kuikatisha hadithi yangu ya maisha kwa kuonyesha uchomvu! Niliushangaa uvumilivu wake. “Pole sana Brother na hongera sana kwa mafanikio makubwa uliyoyapata.

    Ninakuahidi kwamba maandalizi ya Vipande vya Sinema yatakuwa tayari ndani ya wiki hii. Nitakuletea vipande vyako vya kuhusika na kazi itaanza mara moja.” Alisema Jobiso Baro kwa uhakika wakati akikusanya vifaa vyake vya kazi.” Kama tulioagana wote tulitazama saa. Mimi niliguna na mwenzangu alipiga mluzi wa mshangao! Kumbe nilitumia masaa kumi na mbili kusimulia Historia ya maisha yangu!



    MWISHO



MTU WA UFUKWENI (THE BEACH MAN) - 4

 







    Simulizi : Mtu Wa Ufukweni (The Beach Man)

    Sehemu Ya Nne (4)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilipita miaka miwili baada ya uhusiano wa Ramson na Mary. Mtoto alishazaliwa na tayari alikuwa na zaidi ya mwaka mmoja. Alikuwa ni mtoto wa kiume aliyeitwa Lameck. Mara kwa mara Mary alikuwa anaenda Ufukweni na mtoto huyo, akiwa kaongozana Irene rafiki yake. Hata uhusiano wa kimapenzi kati ya Mary na Ramson uliendelea kwa namna ya usiri. Siku moja walipokuwa ufukweni walikuwa na mazungumzo kuhusu mtoto.

    “Naona mtoto amekuwa mkubwa sasa, unafikiri ni lini utanimalizia hela zangu ili nimsahau kabisa?” Alisema Ramson huku akimwangalia mtoto wake aliyekuwa amebebwa na Irene. Irene na Lameck walikaa kwenye viti umbali wa mita mia moja, wakati Mary na Ramson wakiwa kwenye mazungumzo yao. “Hilo lisikupe shida Ramson nadhani yote tulishayamaliza kwenye mkataba wetu, nilikwambia usubiri kiasi kilichobaki nikupatie wakati Dr Jackson akirudi nchini.

    Ninaamini kuwa unakumbuka hilo.” Alisema Mary kwa namna ya umakini sana huku akimtazama Ramson machoni ili maneno yale yamwingie sawasawa. “Ni sawa Mary lakini jamaa amekaa sana huko au ameongeza tena muda wa masomo yake?” Ramson Aliropoka! “Ramson naamini wewe ni mtu makini sana na unajua kila kitu sina nilichokuficha! Nilikwambia kuwa Dr. Jackson atakaa nchini Uingereza kwa muda wa miaka mitatu.

    Mpaka sasa ana miaka miwili na miezi saba. Miezi mitatu tu imebaki atarudi na kila kitu kitaenda kama tulivyopanga sawa?” Alisema Mary. “Sawa Mary nimekuelewa.” Alisema Ramson. “Nashukuru kwa kunielewa Ramson sasa ninaona ni wakati wa kurudi nyumbani kwaheri tutaonana siku nyingine.” Alisema Mary na kusimama kisha akaanza kupiga hatua kumfuata Rafiki yake Irene.

    “Sawa nitakupigia simu tuangalie namna ya kuonana tena siku mbili hizi sawa?” Ramson Alimwambia Mary. “Sawa.” Alisema Mary bila kugeuka na baada ya hapo Mary na Irene walinyanyuka na kuelekea lilipo gari lao. Irene alimpungia Ramson Mkono wa kwaheri wakati Mary akilitoa gari ufukweni hapo.



    * * *

    Yalikuwa ni mapokezi mazuri sana yaliyofanywa na watu wachache na wa muhimu katika Uwanja wa ndege. Uwanja huu wa Mwalimu J.K.Nyerere, ulifurika watu wengi jioni hii miongoni mwa watu waliokuwa hapa walikuwa ni Dr.Mudy, Mary na Mtoto Lameck. Dr. Mudy ni rafiki yake Dr.Jackson alikuwepo uwanjani hapa pamoja na Mary na mtoto Lameck ili kumpokea Dr. Jackson. Leo ilikuwa ndiyo siku ya kurudi kwa Dr. Jackson nyumbani Tanzania.

    Alikuwa na furaha sana kurudi tena nyumbani, baada ya kuishi kwa muda mrefu mbali na familia yake. Zaidi sana kilichomfurahisha ni juu ya kuzaliwa kwa mtoto Lameck. Shauku ya kumwona mtoto wake ilikuwa kubwa sana. Moyo wake ulikuwa na shauku kubwa sana ya kumwona mkewe mpenzi Mary.

    Hakupata picha furaha atakayoipata pindi atakapowaona Mke wake na mtoto wake. Aliona kama ndoto na baraka ya pekee sana kwa familia yake kuongezeka. Shauku yake ilizidi baada ya ndege kutua katika uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere. Aliona mchakato wa kukaguliwa mizigo kama inayochelewesha kuonana kwake na familia yake.

    Uvumilivu wake ulimsaidia mpaka zoezi hilo likaisha, baada ya hapo akasogelea maeneo ya mapokezi na ndipo alipomwona mke wake na mtoto. Furaha yake ilikuwa kubwa sana kuwaona naye mkewe akiwa na mtoto wake alimkimbilia mumewe na kumkumbatia kwa furaha. “Woooooow!!! Mume wangu mpenzi! Nimefurahi sana kukutana tena.” Alisema Mary akimwachia mumewe baada ya kukumbatiana kwa muda mrefu.

    “Mimi ni zaidi mke wangu. Nilikuwa ninaona kama ndege imesimama angani maana nilikuwa na hamu sana ya kuwaona na mtoto wangu mpenzi.” Alisema Dr.Jackson huku akimchukuwa mtoto toka kwa mama yake. “Vipi baba hujambo?” Dr.Jackson alimsalimia mtoto wake. Mara hiyo hiyo alijitokeza Dr.Mudy!“Mzee UK imekukubali sana!” Alisema Dr.Mudy huku akimgusa rafiki yake begani.“Oooohoo! Dr. Mudy!” Alifoka Dr. Jackson kwa furaha!“Ee bwana nimekusahau ghafla naona kitambi kinaanza kutafuta njia mzee!! Inaelekea bongo mambo mazuri sana.” Alisema Dr.Jackson kwa furaha sana baada ya kumwona rafiki yake Mudy.

    “Karibu sana rafiki yangu tumekumiss sana mtu wangu.” Alisema Dr.Mudy huku wakiongozana kwenda kwenye gari aliyokuja nayo Mary. Baada ya Dr. Jackson na mkewe na mtoto wao kupanda ndani ya gari, Dr. Mudy naye aliifuata gari yake na kuingia ndani tayari kwa safari ya kwenda nyumbani kwa Dr. Jackson Ostabay mahali ambapo Dr.Jackson alipanga kukaa na mkewe kwa siku tatu ndipo warejee jijini Tanga. Walipofika walizungumza mawili matatu wakati wakipata vinywaji kisha Dr.Mudy aliaga.

    “Jamani sasa na mimi ngoja nirudi nyumbani tutaonana kesho baada ya wewe kupumzika ili tuulizane habari za UK. vizuri.” Alisema Dr. Mudy. “Sawa ndugu yangu wewe nenda ukalale kesho jioni itabidi uje ili tuogee mengi.” Alisema Dr. Jackson huku akinyanyuka na kuingia ndani baada ya muda alitoka na mfuko mdogo na kumkabidhi Mudy.“Hii ni zawadi yako Rafiki yangu.

    Ninajua kuwa wewe ni mlevi sana wa vitu hivi.” Alisema Dr. Jackson. “Aiiiiiisee Loptop!.. Kwakweli siamini macho yangu!” Alisema Dr.Mudy kwa mshangao wa furaha! “Ndio nimekuletea rafiki yangu japo ucheze cheze Game!” Alisema Dr. Jackson huku akicheka. “Usifanye utani rafiki yangu unajua umenipa zawadi nzuri sana? Hapa Internate kwa sana na Game inapigwa vilevile! Alisema Dr. Mudy kwa utani. “Sawa ndugu yangu tuonane kesho basi alisema Dr. Jackson huku akimtoa nje ya geti na baadaye rafiki yake huyo aliondoka akiwa na furaha tele.

    Dr.Jackson na mkewe walikuwa na furaha sana hasa Jackson kwa kumwona mtoto aliyeamini kuwa ni mtoto wake. “Nafurahi sana kumwona mwanangu mpendwa Lameck. Kwakweli hatimaye leo aibu ya kuwa hatuna mtoto imefutika kabisa. Nimepata mrithi wa mali hizi na mtu muhimu wa kuendeleza mali zetu.” Alisema Dr. Jackson kwa furaha isiyo na kifani. Alikuwa akicheza na mtoto wake kwa muda mpaka akaanza kusinzia. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alinyanyuka na kwenda kumlaza kwenye kitanda chake. Waliongea mambo mengi sana wakiulizana hiki na kile kwa zamu. Baada ya muda mrefu wote walijikuta wamepitiwa na usingizi. Kwa Jackson furaha ilikuwa kubwa sana kwa kuungana na mke na Mtoto wake. Aliyafurahia maisha kwa namna ya ajabu sana.

    Ila kwa mkewe alikuwa na siri moyoni mwake. siri nzito ambayo kama ikifichuka na kujulikana kwa Mumewe Italeta adhari kubwa sana katika maisha yake. Siri hii ilikuwa ni kama bomu. Bomu linaloweza kuangamiza kabisa familia yake iwapo litalipuka. Moyo wake haukuwa na raha hata pale ambapo mumewe alionyesha furaha yeye alikuwa akifanya maigizo tu.

    Roho yake ilikuwa inamsuta kila saa anapomwangalia mtoto wake na kumwangalia mumewe jinsi alivyokuwa akimfurahia. Kwa namna Alivyokuwa haikuchukuwa muda mrefu Dr. Jakson alimgundua mkewe kuwa hakuwa na furaha sana ila alichukulia tu kuwa labda ni hali ya uchovu, au alikuwa huenda hajisikii vizuri. Zawadi alizompa zilimfurahisha sana Mary hivyo kumfanya asahau ile hali ya mwanzoni.

    Kesho yake walifunga safari kurudi uwanja wa ndege tayari kwa safari ya Tanga ambako ndipo walipoweka makaazi yao ya kudumu. Walifurahia sana kuwepo Tanga baada ya dakika arobaini kuwepo angani wakielekea katika mji huo. Kwakuwa walifika mapema Siku yao ilikuwa ni njema sana na wakati wa jioni ulipofika waliamua kwenda kupunga upepo baharini. Mwahako ndiko walikojichagulia maana walipapenda sana. Walipofika walikuwa na wakati mzuri sana wa kupumzika ufukweni hapo, huku wakizungumza hili na lile kwa furaha. Mazungumzo yao kati yake na Mudy yalihusu masomo.

    Walikumbushana mengi baada ya hapo hasa walipokuwa wakisomea nchini India miaka kumi iliyopita. Ramson aliwahudumia kama kawaida kwa vinywaji huku akimtupia Mary jicho la wizi. Mary alikuwa mtulivu sana jioni hii. Baadaye waliondoka na kurudi mjini wenye furaha kubwa. Kwa Ramson alikuwa na kidonda moyoni cha wivu, ambacho hakufikiria hapo mwanzo kuwa mapenzi yalikuwa yamebeba vitu kama hivyo.

    Kwake kumwona Mary amekaa na mumewe na kukumbatiwa, moyo wake ulipata tabu sana kwa wivu wa kimapenzi. Tangu akiwa mdogo hakuwahi kushiriki mapenzi na mwanamke yeyote, kwa hiyo hakujua kuwa ndani ya mapenzi kuna kitu kibaya sana kiitwacho wivu. Alikuwa anasikia tu kwa watu kuhusu mambo ya wivu wa kimapenzi, kwake aliona ni ujinga wa hali ya juu sana kumwonea mwanamke wivu. Leo imekuwa zaidi ya kituko kwa kumwonea wivu mke ambaye hakuwa wa kwake. Alipotaka kupotezea hali hiyo iliibuka kama moto! Ilikuwa haiepukiki.

    Kingine kilikuwa ni mtoto wake Lameck. Hakupenda kumwona yuko mikononi mwa baba mwingine, wakati yeye yupo. Hali ile ilimsukuma aone heri kuhamia mahali pengine ili awe salama. Aliona kwamba ikiwa ataendelea kuwepo mahali hapo iko siku kingetokea kitu cha ajabu. Hizo zilikuwa ni fikra tu zilizopita kichwani kwake na kumpa namna ya kuondokana na shari.

    Alijua atakapokuwa nje ya Tanga atasahau taabu hizo, zinazosababishwa na wivu kwa Mary na Uchungu wa mtoto wake.“Lakini huyu mwanamke atakaponipatia hela zilizobaki kwake sitapata taabu kuwa mbali na ufukwe huu.” Alijisemea…“Kumwachia mtu mahali hapa apaendeleze na mimi kwenda mbali kwa miaka miwili ama mitatu kutanipa nafasi ya kusahau kila kitu.” Aliendelea kujipa ushauri ambao kwake ulikuwa wa busara sana.

    Ramson aliendelea na shughuli zake akiwa tayari katika kujipanga kuondoka, maana aliamini kuwa Mary hatakawia kumkabidhi kiasi cha shilingi millioni kumi zilizobaki kwenye mapatano yao. Kichwani kwake aliwafikiria marafiki zake na kuangalia japo ampate mmoja atakayemwamini ili amwachie biashara zake ufukweni hapo. Alipanga akipata hela zake kutoka kwa Mary na kuchanganya na nyingine zilizoko Bank, aweze kwenda kuanzisha biashara eneo jingine ndani ya nchi hii, au nje ya nchi ikibidi.

    Mawazo yake yaliendelea hadi alipokuwa kitandani usiku. Kutokana na mawazo mengi usiku huo aliotandoto nyingi sana za kutisha na zisizoeleweka vizuri. Ilimradi alikuwa katika changamoto ya pekee juu ya tatizo lake jipya. Hata ilipofika asubuhi hakuwa na raha hasa kwa kukosa japo simu kutoka kwa Mary ya kumjulisha kuhusu fedha zake kuwa atamletea lini. Kujitenga kwa Mary kulimpa mtihani mkubwa sana kwani alizoea ukaribu wake. Jambo jingine lililokuwa linampa shida ni juu ya Patano lao kuhusu kiasi cha fedha za malipo ya mwisho.

    Mary hakumjulisha hata juu ya mumewe kuwa alikuwa amerudi hivyo ilimpa shida kujua kuwa Dr.Jackson ameingia lini nchini. Mawazo yaliendelea kupandana kichwani kwake na kumfanya aone kuwa Mary anataka kumgeuka juu ya mpango waliopatana. Lililomtatiza ni kukosa mawasiliano na Mary, hasa kwa kujulishwa tu juu ya mpango wao baada ya mumewe kurudi.

    Kwa siku nzima alikosa rahasana na akashindwa kufanya jambo lolote la maana. Muda wote alikuwa akiguna tu na kukosa mwelekeo wa kufanya hata kazi zake kwa umakini. kazi muhimu alimpatia kijana wake azisimamie na kuwaongoza wafanyakazi wenzie wachache, kufanya usafi na kuweka eneo lile katika hali ya kuvutia wateja. Moyo wake ulikuwa ukimwuma sana kila alipokuwa akifikiria habari ya Mary na mtoto wake.

    * * *

    Ulikuwa ni usiku wa saa sita simu ya Mary ilipoita. Alikuwa kitandani, Mumewe alikuwa amelala fofofo! Mary alipoangalia kwenye kioo cha simu, alikutana na Jina Ramson! Haraka sana aliondoka kitandani hapo na kuelekea sebuleni na kuipokea simu ile. “Ramson unasemaje usiku huu wote? Aliuliza Mary kwa hamaki.

    “Unanilazimisha wewe Mary kufanya hiv,i sio makusudio yangu! Tangu mumeo amerudi huonyeshi hata dalili ya kutimiza ahadi tuliyowekeana, hupigi simu wala ujumbe mfupi hutumi.” Alisema Ramson kwa kulalamika. “Samahani sana Ramson kwa hilo lakini kumbuka kuwa simu na ujumbe mfupi kwangu ni hatari sana. Dr. anakuwa na simu yangu kila wakati. Sipati mpenyo mwingine wowote.” Alijibu Mary kwa kujitetea.

    “Kwa hapo Mary huwezi kunidanganya! ikiwa anakuwa na simu yako kila saa mbona umepokea wewe wakati huu? Potelea mbali kuhusu hayo yote, la msingi nahitaji uniambie ni lini utanipa hela zangu zilizobaki?” Aliuliza Ramson bila mzaha. “Naomba Ramson nivumilie ili nilifanyie kazi jambo hilo.” Alisema Mary kwa kubembeleza. “Siwezi kuvumilia zaidi ya hapa!” Alisema Ramson kwa hasira. “Ramson nitakuja kesho tutaongea vizuri sawa?” CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mary alisema maneno hayo kwa kunong’ona baada ya kusikia sauti ya mumewe kutoka chumbani akikohoa; kisha akakata simu. Ramson aliduwaa lakini ahadi ya kwamba Mary atakuja ufukwenikesho yake, ilimvutia japo bado kuna hatari alikuwa anaihisi katika jambo hilo. Alikuwa hana hamu tena kuendelea kuwepo mahali hapo, kutokana na matatizo yaliyopo.

    Alihofia maisha yake kukatizwa kutokana na uhusiano huo mbaya uliozaa matunda ya mtoto. Alijua kuwa kwa vyovyote Dr. Jackson anaweza kufanya vipimo vya DNA ikiwa tu atashtukia jambo fulani kwa mtoto. Baada ya kugundua lazima hatari ingefuata maana asingevumilia. Kwa mawazo hayo Ramson alikusudia apewe hela zake ili aondoke kabisa katika mji huo.

    Kuhusu biashara zake na mradi wake kwa ujumla ufukweni hapo, angeuacha kwa marafiki zake. Kuchelewa kwa Mary kumpatia hela zake ni kumfanya akaribie kwenye mdomo wa mamba; kitu ambacho ni hatari kubwa sana kwake. Alisubiri siku ya pili yake aone uaminifu wa Mary juu ya ahadi yake.

    Mapambazuko ya siku hii yaliambatana na hamu ya kumwona Mary. Kila wakati alikuwa anaangalia njia, kuona labda Mary angekuja wakati huo. Kila aliposikia muungurumo wa gari aligeuka upesi akifikiri ni Mary amekuja. Hali hii iliendelea kwa muda mrefu sana, mpaka kufikia mchana wa siku hiyo. Kuna muda alifikia kukata tamaa kabisa juu ya ujio wake ufukweni hapo.

    * * *

    Usiku kabla ya kulala Dr. Jackson alimwambia mkewe ajiandaye kwa safari ya kesho yake. “Mke wangu ni siku nyingi sana nimekuwa nje ya nchi. Alisema Dr. Jackson akakohoa kidogo kisha akaendelea.. “Natamani kesho twende Lushoto, Tukaangalie Hotel zetu na maendeleo yake. utakuwa wakati wetu mzuri sana wakwenda kupumzika, baada ya kutengana kwa muda mrefu.”

    Alitoa wazo Dr. Jackson.“Mume wangu nashukuru kwa wazo lako zuri, nadhani hilo halina tatizo kabisa nitajiandaa.” Alijibu Mary kisha akaenda kabatini kuandaa nguo chache za kwake na za mumewe. Baada ya kuzifunga vizuri kwenye mabegi alirudi kitandani na kuungana na mumewe. Waliongea mengi na hatimaye wote walipitiwa na usingizi.

    kilichomwamsha Mary ilikuwa ni simu iliyopigwa na Ramson. Alijua kuwa kama atayachukulia kimzaha malalamiko ya Ramson yangemharibia. Jambo aliloona ni la lazima ni kutafuta kisingizio cha kutokwenda Lushoto na mumewe. Mwisho wa yote akaona kujifanya mgonjwa ndiyo njia pekee itakayompa mwanya wa kubaki.

    Baada ya muda alianza kujiliza akijifanya anaumwa na Tumbo. Hata mumewe alipoamka alimkuta mkewe katika hali hiyo.Alipohoji tatizo Mary alisema kuwa anaumwa na tumbo. “Kama linakuuma sana basi nikupeleke ukapimwe Hospital ijulikane kuwa ni nini?” Alisema mumewe kwa msisitizo akimhimiza mkewe ajiandae waende Hospitali. “Usiwe na wasiwasi mume wangu hali hii sio ya kwenda Hospital.” Ni majira yake na halitadumu kwa muda mrefu zaidi ya siku mbili tu ya tatu linatulia kabisa. Alisema Mary na mumewe alimwelewa.

    “Sawa mke wangu nimekuelewa sasa itabidi basi Lushoto niende peke yangu? Nitakuja baada ya siku mbili kwa kuwa Hoteli zote mbili kuzikagua ni kazi kubwa.” Alisema Dr. Jackson. Sawa mume wangu ila siku mbili nitakukosa sana! Japo pia kuna umuhimu mkubwa wa kutembelea Hotel zetu, maana kwakweli taarifa za kupewa tu hazitoshi.” Mary aliongea hivyo na baada ya muda alimwandalia mumewe chai mezani. Baada ya kuoga na kunywa chai hiyo alipakiza begi lake kwenye gari na kumuaga mkewe na kumbusu mtoto kisha akaondoka zake.



    * * *

    Asubuhi baada ya mumewe kuondoka, Mary alimpigia Ramson Simu kuwa anakuja. Ramson alifurahi kuwa hatimaye atapewa fedha zake. Mnamo saa tano za asubuhi Mary alikuwa barabarani kwenda Mwahako Beach. Mwendo wake ulikuwa wa kasi sana lakini alipofika mwakidila alikutana na ajali ya pikipiki na baiskeli watu wengi walikusanyika mahali hapo kwa wingi.

    Kwakuwa waliogongana walikuwa wamelala barabarani aliteremka ili aone majeruhi hao. Baada ya muda majeruhi wale waliondolewa na kuruhusu magari kupita. Dr. Mudy aliyekuwa akitoka Pangani alipita mahali pale kwa kasi lakini macho yake yalimwona Mary Mke wa rafiki yake. Kwanza alianza kuiona gari yake na kisha baada ya kuangalia sana akamwona Mary akielekea iliko gari yake.

    Alipopita kidogo alisimamisha gari kando ya barabara na kuangalia mwelekeo wa shemeji yake. Alipomwona akipinda kushoto mahali ilipo Mwakidila sokoni alijua kuwa alikuwa akielekea Mwahako Beach. Baada ya kuona hivyo ilimsikitisha sana maana alijua kuwa rafiki yake Dr. Jackson alikuwa akiibiwa na Beach Man. Hali hiyo ilimtia uchungu kutokana na taarifa aliyopewa na rafiki yake Jackson, kuwa alikuwa aende Lushoto na mkewe lakini tatizo ni kwamba mkewe alikuwa akiumwa.

    Hali hii hakuivumilia badala yake alipiga simu ya Dr. Jackson. Halo ndugu yangu mambo vipi? Alisalimia Mudy baada ya simu kupokelewa. “Aisee ni nzuri sana kwema Pangani?” Aliuliza Dr. Jackson. “Pangani ni kwema nimeshamaliza shughuli zangu ila sasa niko hapa Mwang’ombe napita mahakamani hapa narudi Mjini.” Alisema Mudy.

    “Sawa ndugu yangu mimi nilishafika Lushoto kitambo ninapitia mahesabu na kukagua mazingira ya Hoteli zangu.“Jackson alisema na mara hiyo simu ikakatika. Alijaribu kuipiga lakini alikutana na ujumbe ukisema: “Asante kwa kutumia mtandao wa voda com. Namba unayopiga kwa sasa haipatikani tafadhali jaribu tena baadaye.”

    Dr. Mudy alitaka kuwakilisha ujumbe wake wa kimbea kuhusu kukutana na mke wa rafiki yake akielekea Beach. Ni mazungumzo mengi ya Jackson yaliyosababisha chaji yake iliyokuwa kidogo kwenye simu yake kwisha. Simu yake ilizima kabla hajawakilisha ujumbe huo. Aliendelea mbele akipania kuwa baada ya kuweka chaji kwenye simu yake basi angemweleza rafiki yake mambo yote.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    * * *

    Mary alifika ufukweni na Ramson alimpa mapokezi ya aina yake kwani walijumuika katika kukumbushia uhusiano wao. Baada ya zoezi lao Ramson aliuliza juu ya mpango wao waliopatana. “Mary uvumilivu unanishinda siwezi kuvumilia kukuona uko na mumeo na mtoto wangu. Ninachotaka kuanzia sasa nipate ule mzigo uliobaki nijue cha kufanya. Hiyo peke yake itakuwa ndio dawa ya kustiri siri yetu.” Alisema Ramson kwa Msisitizo.

    “Ramson nimekuelewa mpenzi wangu lakini nimekuja kukuambia kuwa naomba usubiri kidogo tu kuna mambo nayarekebisha kusudi nikupe ule uzigo tuliopatana.” Mary alisema kwa upole. “Lakini Mary kumbuka kuwa ulisema jamaa akija tu utanipatia na sasa tangu aje ni wiki imeshaisha sio mapatano yetu. ila kama unavyosema ni muda mfupi naombaufanye hivyo kabla mambo hayajawa mabaya.

    Nataka niondoke katika mji huu kwa muda usiojulikana.” Alisema Ramson.” “Usiwe na wasiwasi nitatimiza kila tulichoongea, nipe siku tatu tu tangu leo.” Alisema Mary kwa uhakika. “Kwa sababu umesema mwenyewe kuwa ni baada tu ya siku tatu naomba isivuke hapo. Kwa sababu sina amani moyoni mwangu juu ya maisha yangu.

    Utanielewa vibaya ikiwa hutatimiza ahadi yako ndani ya siku hizo. Najua niko hatarini kwa sababu nawaelewa madaktari walivyo! Iko siku atashtuka kuwa mtoto sio wa kwake na kama akienda kwenye vipimo vya vinasaba kitakakachotokea ni siri kuwa wazi.” Alisema Ramson huku akionyesha hofu katika macho yake. “Ramson nitajitahidi nifanikiwe ndani ya siku hizo.” Alisema Mary huku akinyanyuka na kuaga kuwa anarudi nyumbani.”

    “Zingatia hayo na uwe makini sana kwa kila jambo. usifanye papara katika kila pointi. Kosa moja tu litaifanya siri yetu kuwa hadharani.” Alitahadharisha Ramsoni. “Hakuna wasi wasi niko makini Ramson.” Alijibu Mary huku akiishilia ndani ya gari lake, baadaye akaliwasha na kuliondoa taratibu Ufukweni hapo. Mawazo yalipandana kwa Mary na kumsababisha kuwa na huzuni, iliyochanganyika na majuto.

    Siri hii imekuwa kikwazo sana ndani ya maisha yake. Hakuwa tena na raha katika maisha kama ilivyokuwa hapo mwanzo.Hitaji la kupata mtoto na tamaa ya kimapenzi, imemwingiza katika hatari kubwa katika maisha yake. Nisawa kabisa kuwa alimpenda sana Ramson, lakini haikuwa zaidi ya mapenzi tu aliyoyataka kwake. Ndoa yake hakutaka kuipoteza kabisa hivyo alitamani kuilinda, kwa namna yoyote ile ya gharama.

    Lakini dalili zinavyoonyesha mpaka hapo ni kwamba kuna dalili za siri hiyo kuvuja, kutokana na uharaka wa Ramson katika madai yake. Alijuta sana kumwambia Ramson kuwa alikuwa na mimba yake. Alikumbuka jinsi alivyopata furaha ya ghafla baada ya kupewa majibu ya vipimo na Daktari. Furaha yake ilimnyima simile hivyo akajikuta anaropoka na kumpa nafasi ya utawala Ramson, katika nafsi yake na maisha yake kwa ujumla.

    “Umefanya kosa kubwa sana rafiki yangu kumwambia Ramson kuhusu huo ujauzito. Hiyo inaweza kukugharimu mambo mengi katika kuilinda siri hii.”

    Alikumbuka maneno ya rafiki yake Irene, pindi tu alipomwambia kuwa amemjulisha Ramson juu ya ujauzito ule kuwa ni wake. Mpaka sasa kengele za tahadhari zilikuwa zikipigwa masaa ishirini na nne! Hali ya mashaka ilitawala kila wakati pindi tu anapofikiria jinsi ya kucheza katika pande zote mbili, kwa Ramson na mumewe.

    Alijikuta yuko njia panda kwa ujumla. “Zingatia hayo na uwe makini kwa kila jambo, Usifanye papara katika kila pointi! Kosa moja tu litaifanya siri yetu kuwa hadharani!” Aliyakumbuka maneno ya Ramson ya mwisho wakati wanaachana. Hakuwa na hakika kuwa hatafanya kosa katika harakati zake za kuihifadhi siri hii; hasa ukizingatia kuwa pande zote alikuwa anawindwa!

    Alikuwa na majukumu ya kawaida kwa mumewe na kwa Ramson. Kutoa Shilingi milioni kumi na kumpa Ramson halikuwa jambo kubwa sana wakati mumewe akiwa yuko masomoni. Lakini kutoa kiasi hicho cha fedha wakati mumewe akiwepo ni mtihani mkubwa sana, ambao umebeba hatari kubwa sana, kama hautafanywa kwa uangalifu.

    Ubaya wenyewe ni kwamba pande zote mbili zitamwangukia kwa hasira kubwa sana bila huruma. Hayo yalikuwa ni mawazo ya kweli yaliyokuwa yakipita katika kichwa cha Mary. Kwakweli hakuwa na nafuu wala faraja kwa yote hayo; bali yalimtaka kuwa macho sana katika pande zote mbili. Kwa wakati huu Presha ilikuwa kwenye kulilipa deni la Ramson. Baada ya hapo abaki salama akiyalea mapenzi yake kwa mumewe. Tatizo kubwa lilikuwa ni Ramson na deni lake peke yake. Mawazo yake yalikuwa juu sana kutafuta jinsi ya kutatua tatizo hilo kwa busara.

    * * *

    Dr. Mudy alipofika nyumbani jambo la kwanza alikimbilia kwenye soketi ya umeme, ili kuchaji simu yake kusudi aweze kumpa rafiki yake habari juu ya Shemeji yake. Moyo wake ulikuwa na dukuduku bayasana, ambalo lilihitajika kutolewa mahali husika ili apate nafuu. Jamaa huyu huwa hawezi kuvumilia anapoona neno. Rafiki zake wengi walikuwa wakimshauri aachane na kazi ya udaktari, badala yake awe mwandishi wa habari wa magazeti ya udaku! Pendekezo hilo la rafiki zake lilikuwa sahihi, kwa sababu Dr. Mudy alikuwa hakai na jambo.

    Anapoona jambo ambalo sio zuri, hulisimamia na kulitolea habari zake mahali husika. Mara tatu aliweza kutoa taarifa kuhusu Madaktari wenzake, waliokuwa wakijihusisha na kutoa mimba za wanafunzi. Madaktari hao walikamatwa na kufungwa kifungo cha miaka ishirini kila mmoja baada ya kubainika wakifanya tendo hilo. Leo hii yupo nyumbani kwake akiwa na harakati za kuchomeka simu kwenye chaji, lakini hali haikuruhusu kwani umeme ulikuwa umekatika.

    Kidogo alitahayari kutokana na zoezi lake kukwamishwa na kukosekana kwa umeme. “Lakini ni kwa muda tu, umeme ukirudi nitachaji na kumwambia rafiki yangu habari hizi.” Alijisemea kimoyomoyo huku akielekea chumbani kwake na kuingia bafuni ili ajimwagie maji kuondoa uchomvu wa safari.

    Baada ya kumaliza kuoga aliporudi chumbani kwake ili kuvaa nguo alikuta umeme umesharudi. Kwa haraka alichukuwa simu yake na kuiweka kwenye chaji. Baada ya hapo alirudi na kumalizia kuvaa, kisha akarudi na kuwasha simu ikiwa kwenye chaja na kutafuta namba ya Dr. Jackson. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hata hivyo bahati haikuwa upande wake, kwa sababu simu ilikuwa haipatikani alijaribu tena ikawa vile vile. “Mmmmmh! huu umbea utachacha sasa! kama angepokea ningempasha habari zikiwa bado za motomoto, lakini inavyoonekana leo sikulalia mkono mzuri. Jamaa tunapishana tu nikitaka kufikisha umbea wangu kunatokea vikwazo!” Alilalamika Dr. Mudy huku akijaribu kupiga kwa mara nyingine ambayo ilijibiwa vilevile kuwa namba haipatikani labda ajaribu tena baadaye! “Hakuna neno ataifungua tu simu yake.

    Na mimi sitaki kumtumia ujumbe mfupi wala nini! Nataka nimpigie na kumwambia kila kitu neno kwa neno.” Aliendelea kusema peke yake mawazoni huku akiwa ameshushuka kwa kukosa nafasi ya kubwagiza habari zile. Habari ambazo alizitunza kwa muda mrefu sana ila tu alikuwa akizitafutia ushahidi wa kutosha.

    Alitayarisha ushahidi wa namna zote na kupata vigezo mbalimbali vya kuusema umbea ule kwa Jackson. Uchunguzi wake wa kina na ufuatiliaji wa mambo na kuhifadhi ushahidi ni sehemu ya kipaji chake. Hii ndio maana baadhi ya marafiki zake walimpendekeza kuwa alifaa sana kuwa mwandishi wa habari.

    Kwa upande wa Mary aliweka ushahidi wa siku nyingi, hivyo kuifanya habari kamili juu ya kuibiwa kwa rafiki yakeiwe imeiva. Hii ndiyo sababu iliyopelekea kuhangaika sana ili kumpata Dr. Jackson, kusudi ampe habari kamili. Mahangaiko yake hayakufua dafu kwa siku ile, hivyo alilala nayo tena bila mafanikio.

    * * *

    Dr. Jackson alifika salama Lushoto na ukaguzi wa Hotel zake ulifanyika mara tu baada ya kufika. “Inaonekana mnafanya vizuri kazi zenu au sio Meneja?” Alisema Dr.Jackson baada tu ya kuingia kwenye Ofisi ya meneja wa Hotel mojawapo kati ya mbili alizonazo. Ni kweli Mzee tunajitahidi kufanya vizuri.” Alijibu Meneja kwa unyenyekevu. “Nimeona mazingira ya nje ni mazuri watu wa kukatia majani kwenye bustani wamefanya vizuri bwawa la kuogelea liko katika hali ya usafi, kadhalika bwawa la samaki pia naona linatunzwa vema, maana naona samaki wamekuwa wengi sana.

    Hayo ni machache ya mambo niliyoyaona mazuri. Hongera sana Meneja kwa kazi yako nzuri.” Alisema Dr. Jackson huku akimpa mkono Meneja kusindikiza pongezi zake. “Asante Bosi kwa kuyaona hayo. Tunajitahidi kufanya vizuri kwa sababu wageni ni wengi kutoka Ulaya; wanakuja kulala hapa wengine wanakaa kwa mkataba, wa mwezi mpaka miezi mitatu.

    Wanapokuja watu hawa kinachowavutia ni mazingira kwanza ya Hotel. Bwawa la kuogelea bwawa la samaki na vivutio vinginevyo, ikiwepo bustani ya mboga mboga na bustani ya matunda. Mpangilio wa vitu hivyo huwafanya waje hapa na kutaka kuishi hapa, ikiwa muda wao wa kukaa hapa ni mrefu.” Alisema Meneja kwa kirefu akielezea jinsi biashara zinavyoenda vizuri.

    “Unataka kuniambia kuwa tangu niondoke nchini wamekuja watalii mara ngapi kwenye Hotel zetu?” Aliuliza Dr. Jackson. “Unajua mzee miaka mitatu sio mchezo! Inabidi niangalie kwenye kitabu kusudi nikupe idadi hasa za wageni wetu.” Alisema Meneja na huku akifungua kabati la vitabu vya wageni na taarifa za kila siku. Kisha akaendelea… “Unaona sasa! Kwenye kitabu cha kupokea wageni kinaonyesha kuwa ni zaidi ya mara ishirini tumeingia mkataba na wageni toka nje ya nchi wa kukaa kwa muda mrefu. Wengine walikaa wiki mbili wengine walichukuwa Hoteli nzima kwa miezi mitatu.

    Hawa hapa walikaa kwa miezi miwili. waliokaa kwa muda wa miezi miwili miwili walikuwa watalii kutoka Nchini Marekani. Watalii hawa walikuja kuendesha semina za mambo ya ukimwi. Walichukuwa Hoteli nzima kwa muda wote huo. Wengine walitoka Austaralia hawa walikuja kufanya utafiti wa wadudu wanaoeneza magonjwa, kwa wanyama kama vile Ng’ombe, mbuzi na kondoo.

    Hawa walikuwa watu mia moja na kumi, hivyo iliwalazimu kuchukuwa Hotel nzima waliobaki tuliwapeleka kwenye Hotel yetu nyingine. Kwa ujumla Bosi hao ndio wageni wetu waliotutembelea katika kipindi chote hicho.” Alisema Meneja huku akimalizia kuweka idadi kamili, katika karatasi moja na kumkabidhi bosi wake.

    Kiasi cha fedha kwenye akaunt kimefikia shilingi ngapi kulingana na kazi zilizofanyika?” Aliuliza Dr. Jackson. Fedha zote zilizoko Bank nimekuwa nimeorodhesha kwenye kitabu cha mahesabu. Nimejitahidi kuhifadhi risiti za manunuzi ya vitu vya matumizi, faida nimeweka kwenye Akaunti. Kumbukumbu nimeweka kwenye kitabu hiki.” Alionyesha kitabu kikubwa cheusi. Alisema Meneja. Kiasi chote cha akiba iliyoko Bank ni hii hapa. Alimwonyesha kila kitu jinsi alivyotunza mahesabu.

    Baada ya kumpa kitabu cha akiba iliyopo, alimpa kitabu kingine cha mchanganuo wa mapato na matumizi. Mwisho wa yote Dr. Alimpongeza sana Meneja wake kwa kufanya kazi nzuri sana. “Kazi yako ni nzuri sana. Endelea na shughuli mimi ninataka nikamilishe kuangalia Hotel ile nyingine. Nahitajika nirudi mjini Tanga maana nahitajiwa kazini.” Alisema Dr. Jackson. “

    Ila bosi nimekuwa nikijiuliza kila siku mambo mengi sana ninakosa majibu. Wewe ni tajiri sana mwenye Miradi mingi kiasi hiki, lakini bado unafanya kazi ya kuajiriwa! Kwanini usitulie ukaangalia miradi yako?” Samahani bosi kama nitakuwa nimeingilia maisha yako binafsi.” Alisema Meneja wakati wanaagana.

    “Bila samahani ni watu wengi wananiuliza swali hilo sio wewe tu. Unajua kazi ya Udaktari ni sehemu ya wito kwa ajili ya kuwasaidia binadamu wenzetu? Aliuliza kisha akaendelea. “Wito ni kitu cha ajabu sana, humuendesha mtu kwa ndani ya nafsi yake na mtu huyo akakosa maamuzi sahihi zaidi ya kuutimiza wito huo. Ndani yangu ninasukumwa na huruma kwa watu wanaoteseka kwa magonjwa.

    Nikiwa nje ya kazi hii ninajiona kama sijakamilika, ikiwa tu sijafanya jukumu langu la kuwasaidia watu wanaoteseka. Hilo ndilo linalonisumbua na kunifanya niendelee kuwepo kazini. Hata kama ningekuwa na utajiri kiasi gani hauwezi kunifanya nikaacha kufanya kazi yangu ya Udaktari.” Alisema Dr. Jackson na kumalizia kwa kumpa mkono wa kwaheri Meneja wake. Asante mzee kwa kunijibu. Una moyo wa ajabu sana Bosi wangu.”

    Alimaliziakuzungumza wakati Dr. akifunga mkanda na kuliwasha gari kisha kuliondoa kwa mwendo wa taratibu. Njiani aliwapungia mkono wafanya kazi wake waliokuwa wakifanya usafi na kuendelea na safari yake. Ukaguzi wa hoteli yake nyingine, ulikuwa ni hali kadhalika na baada ya kumaliza kukagua kila kitu aliondoka jioni ya siku ya pili tangu afike Wilayani hapo.

    Fedha zilikuwa ni nyingi za faida alizozipata kwa kipindi chote hicho kiasi kwamba alifikiri kuanzisha mradi mwingine mkubwa sana. Alijaribu kufikiri akiwa kwenye gari lake, huku akipiga mluzi taratibu kufuatisha mziki uliokuwa ukipigwa na Mwanamuziki Mbiliabel.

    * * *CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mary baada ya kurudi kutoka ufukweni alijipanga na kumpigia rafiki yake Irene simu kusudi waonane. “Kwani una haraka sana ya kuonana na mimi sasa hivi? Kama unaweza kusubiri niende mara moja Bank maana kuna Fedha zinatakiwa za marejesho Pride.” Alisema Irene baada ya Mary kumwambia anataka waonane ndani ya muda huo. “Mazungumzo yangu ni marefu na yanahitaji tuyaongee mapema sijui utafanyaje?” Aliuliza Mary kwa sauti ya chini yenye dalili kuwa amebanwa sana na jambo.

    Irene kwa kuzingatia uzito huo aliouonyesha rafiki yake akamwambia: “Kwani kuna tatizo gani rafiki yangu? au mambo yameharibika?” Alisema Irene akisukumia na utani ambao ulifanana na ukweli. “Ninashukuru kama umekubali tuonane mengine tutaongea tukikutana.” Alisema Mary na kukata simu. Baada ya hapo aliingia kwenye gari lake na kuanza safari kuelekea kwa Irene.

    Alienda kwa mwendo wa kasi kusudi amwahi rafiki yake. muda haukuwa mrefu sana alifika nyumbani kwake na kumkuta Irene Sebulen akiwa kakaa mkao wa kutaka kuondoka. “Wooooow Mary” Alisema Irene na kumkubatia rafiki yake… “Karibu sana naona leo huko kwenye hali yako ya ucheshi unanini” Alisema Irene baada ya kumkaribisha Mary kwenye moja ya sofa.

    “Sio hali mbaya sana, ilibidi tu nikuone japo tupeane maarifa. Alisema Mary kwa unyonge. “Kuhusu nini sasa?” Aliuliza Irene akiwa na shauku ya kujua. “Rafiki yangu sasa hivi niko njia panda na sijui ni njia gani nitapita ili niokoke! Mpaka sasa Ramson ananidai kile kiasi cha shilingi millioni kumi, na amenikalia kooni kwelikweli hana utani kabisa. Lengo la Ramson anataka akimbie mji maana hana uhakika na maisha yake kama anavyodai mwenyewe. Nimempa siku tatu za kumlipa hela hizo, lakini mpaka sasa bado sijajua nitaanzia wapi kumwomba Mume wangu kiasi chote hicho.”

    Alisema Mary katika hali ya majonzi akihitaji ushauri kutoka kwa Irene rafiki yake. “Pole sana Mary! Labda utakuwa unakumbuka maneno yangu, nilikuambia tangu mwanzo kuwa hukupaswa kumwambia Ramson kuwa una mimba yake. Ungezingatia yote haya yasingelitokea.” Irene alimwambia Mary kwa masikitiko.

    “Ni kweli rafiki yangu lakini Waswahili wanasema: “Maji yakishamwagika hayazoleki.” Nimejuta sana juu ya hilo na kila wakati ninakumbuka ushauri wako, lakini majuto yangu hayawezi kubadilisha lolote kwa sasa. Kinachotakiwa ni kupata njia mpya ya jinsi ya kujikwamua kutokana na matatizo haya, nishauri ndugu yangu!” Alisema Mary kwa uchomvu wa mawazo. “Sawa rafiki yangu labda twende katika Pointi yenyewe.

    Jioni Mr. wako atakaporudi ongea naye umwambie kuwa, kuna biashara tumeamua kuifanya ya kuleta vipodozi na kuviuza kwa jumla. Na kwamba bidhaa hizo tunazitoa nchini China. Mpe mchanganuo mzima wa mtaji unaohitajika na faida zitakazopatikana kutokana na biashara hizo. Kwa sasa tuandae mchanganuo huo, kisha nitauprint na kukupatia ili ukampe mumeo.”… Alisema Irene kisha akameza mate wakati huo Mary alikuwa amemtazama tu usoni.

    “Kwenye huo mchanganuo nitaweka kiasi cha mtaji kama milioni Thelathini na tiketi itakuwa ni shilingi million tano. Mpaka kufikia hapo mimi hela zangu nitakuwa nazo tayari, kwa hiyo utamwambia kuwa ulikuwa unamsubiri kusudi umweleze jinsi tulivyopatana.” Alisema Ireni huku akimwangalia Mary usoni kuona kwamba maneno yale yamemwingia.

    “Hapo umenipa njia. Kweli ninavyomjua ni kwamba hawezi kugoma, ila anachotaka mara nyingi ni kupewa mchanganuo wa kile kinachohitajika kufanywa. Unanishauri baada ya kupewa hela hizo nifanyeje?” Aliuliza Mary. “Ufanyeje tena!?” Alisema Irene kwa kushangaa!...“Lengo la yote haya ni ili upate hela za kumlipa Ramson!

    Ninavyofahamu ni kwamba mumeo hakufuatilii katika miradi yako wala biashara zako. Kwa hiyo kwako ni njia nzuri sana ya kuondoa tatizo lililopo la huyu Ramson.Si ndiyo shida iliyopo kwa sasa?” Alisema Irene huku akitabasamu. “Hapo mwenzangu umenisaidia sana rafiki yangu.”

    Alisema Mary huku akiungana na rafiki yake katika kutabasamu. Wewe ni Mbunifu sana wa mambo! Hiyo ni mbinu kabambe ambayo itanisaidia kuniondoa kwenye matatizo, Asante sana rafiki yangu.” Alisema Mary huku akionyesha uso wa matumaini. Irene alinyanyuka na kuingia ofisini kwake.“Jichukulie mwenyewe juisi hapo Frijini wakati nikiandaa Mchanganuo sawa?” Alisema kabla hajaingia na baadaye akatokomea ndani.



    Ilikuwa ni ujumbe mfupi uliomshtua kwenye mawazo yake. Mawazo muhimu sana ya kupangilia namna ya kuanza mradi mkubwa, kulingana na fedha nyingi alizopata. Wimbo wa Mbiliabeli uliendelea kujirudia kweye Redio huku Dr. Jackson akiutolea kibwagizo kwa mluzi!Alichukuwa simu yake huku akiwa amekasirika kidogo. Baada ya kuifungua simu yake akakuta ujumbe mfupi kutoka kwa Dr.Mudy.

    Ujumbe wenyewe ulikuwa na maneno machache sana, yaliyosomeka hivi: “Rafiki yangu kama umerudi fanya kila njia tuonane kwenye Hoteli ya Mkonge jioni hii, kuna habari nyeti sana nikuambie. Zingatia kuwa ni muhimu.”

    Baada ya kusoma akairudisha simu mahali pake huku akiwaza ninini anachoitiwa na rafiki yake? “Ni jambo gani hilo la Muhimu tena?” Alijiuliza Dr. Jackson huku akikerwa na wito huo bila kujua kuwa unahusu nini.” Alifika nyumbani alasiri akiwa na uchomvu wa safari. Jioni hii alimkuta mkewe amechangamka sana. Lakini hakutaka kukaa sana maana wakati alioambiwa wakutane na Mudy ulikuwa umefika.

    “Mbona unaondoka mapema kiasi hiki hata hujapumzika? halafu nina mazungumzo mazuri sana ambayo ungeyafurahia mume wangu.” Alisema Mary kwa hali ya deko.“Sawa Honey nitakaporudi baadaye tutakaa tuongee sawa? Kwa sasa nimeitwa na rafiki yangu Mudy amesema kuwa ana mambo muhimu sana ya kuzungumza na mimi.” Dr.Jackson alisema kwa kusihi ili apate nafasi ya kwenda kumwona Mudy.

    “Mtoto yuko wapi?” Aliuliza kwa kumalizia akitaka kutoka. “Yuko chumba cha michezo anacheza.” Alijibu Mary. Mara hiyo Dr. Jackson akarudi na kuingia chumba cha michezo, alimkuta Lameck anachezea magari yake ya kitoto. Jambo Lameck? Alisema Dr. Jackson na Lameck akaitika na kumsalimia baba yake. Jackson alimbeba na kumpa zawadi alizomnunulia, kisha akatoka na kuingia kwenye gari kisha, akaiondoa kwa mwendo wa kasi kidogo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alifika mkonge baada ya muda mfupi maana kutoka mahali alipoishi na Hotelini hapo sio mbali sana. Baada ya kupaki gari mahali pake aliondoka na kwenda kwenye bustani iliyopo nyuma ya Hoteli hiyo kubwa. Kufika hapo alimkuta rafiki yake akiwa anamsubiri. “Kumbe umeshafika!” Jackson aliuliza huku akishangaa. “Zamani sana mbona?” Alisema Mudy huku akinyanyuka kwenye kiti na kumsalimia rafiki yake.

    Baada ya kupeana mikono walikaa na wakati huo huo mhudumu alikuwa ameshafika kutaka kuwahudumia. “Niletee Malta Guiness ile isiyo na kilevi sawa?” Alisema Dr. Jackson. “Na mimi vilevile aliagizia Mudy na mara hiyo mhudumu akaenda kuwachukulia vinywaji. “Habari za Lushoto rafiki yangu?” Mudy aliuliza wakati akijiweka sawa kwenye kiti. “Habari sio mbaya ni nzuri sana rafiki yangu.Lushoto ni kuzuri sana baridi ya kule kama Uingereza nilikotoka.

    Mazingira ya kijani na misitu vimenifanya nijisikie vizuri sana kwa siku hizi mbili. Ninatamani baada ya kustaafu kazi ya udokta nihamie Lushoto nikamalizie uzee wangu huko.” Alisema Dr. Jackson kwa hisia kali. Mara mhudumu alifika na makopo mawili ya Malta Guiness na kuwawekea na glasi kisha akaondoka. “Haya rafiki yangu nimekuja unipe habari ulizosema kuwa ni nyeti.

    Kiukweli nimechoka sana nilitakiwa niwe niko kitandani nimepumzika saa hizi.” Alisema Jackson. “Sawa kabisa naona ni vizuri kwenda katika jambo lenyewe.” Alisema Mudy kisha akakohoa kisha akaendelea….”Nina jambo ambalo kwa siku nyingi nimelifanyia utafiti na baadaye nikaona kuwa sio vema kukaa nalo bila kukuambia.” Alitulia kidogo kuona kama maneno yake yanapokelewa namna gani.

    kisha akaendelea tena… “Unajua yule Beach Man sio mtu mzuri kwako? Alianza kwa swali ili kuchokoza shauku ya Jackson ya kutaka kujua zaidi. “Sio Mtu mzuri kwangu kivipi?... Usizunguuke sema moja kwa moja hivyo ndivyo ninavyokuambiaga mara nyingi, kuwa kama una habari niambie kabisa. Namna hiyo unaweza kumsababishia mtu shinikizo la damu bila sababu ya msingi sawa?” Aling’aka Dr. Jackson kwa sauti ya juu kidogo. “Nimekuelewa ndugu yangu ila usiwe mkali. “ Habari yenyewe ni kwamba yule Jamaa ana uhusiano wa kimapenzi na shemeji yaani mkeo!” Alisema Mudy huku akimtazama Jackson jinsi atakavyozipokea habari zile.

    “Nashukuru rafiki yangu kwa kunipa hizo habari.” Alisema Jackson kwa kujikaza na kuzuia hasira ambayo haijulikani ikiwa ni kwa ajili ya Mudy, au huyo Ramson aliyeambiwa. “Lakini habari zenyewe hizo kwangu siwezi kuziamini kabisa, hata ungeniambia kwa Lugha gani. Mimi na Mary tumetoka mbali sana! Mbali kiasi kwamba chochote unachokisema kuhusu yeye kunisaliti ni kama unaongea Kichina, ambacho sikielewi hata ungefafanua namna gani! Labda nikuage kwa sababu sitaki kusikia zaidi kuhusu hilo ngoja nikapumzike…

    ”Kwa heri.” Alisema na kunyanyuka kwenye kiti na kuelekea kwenye gari lake. Dr. Mudy alijisikia vibaya sana kwa kutokueleweka kwa rafiki yake. Alijaribu kumzuia lakini haikusaidia lolote. Hata kinywaji Dr. Jackson alikiacha hapo bila hata kukifungua. “Rudi rafiki yangu sijawahi kuzusha jambo lolote kwako na habari hii nina ushahidi nayo.” Alisema Mudy lakini ilikuwa kama anayempigia mbuzi gitaa ili aserebuke, badala yake mbuzi aliendelea kula majani!

    Dr.Jackson alielekea kwenye gari yake, kisha baada ya kuingia aliiwasha na kuiondoa kwa kasi kuelekea nyumbani kwake. Njiani alikuwa anafikiria mengi sana kuhusiana na taarifa ile. Upendo wake kwa mkewe ulikuwa juu sana. Yuko tayari kupigana na mtu kama tu wataongea kinyume na mkewe. Dr. Mudy kwake aligeuka adui baada tu ya kumsikia akisema habari kuhusu mkewe.

    Maneno yake yalijirudia kwenye mawazo yake kama jinamizi: “Habari zenyewe ni kwamba yule jamaa ana uhusiano wa kimapenzi na shemeji yaani mkeo.”Maneno haya yalikuwa mafupi lakini yanayoumiza sana kuliko hata risasi. Moyo unaumia vibaya sana kuliko maumivu ya mwili. Moyo unapoumia kila kitu kinasimama, maana maumivu yake hushirikiana na kichwa chenyewe. Mudy alimuumiza sana kwa habari zake hizo. “Ningejua kuwa habari zenyewe ni za hivyo nisingeitikia wito wake.” Alijisemea moyoni wakati alipokuwa akipiga honi ya gari kwa ajili ya kuingia ndani ya nyumba yake.



    * * *

    Mazungumzo kati ya Dr. Jackson na mkewe yalifikia mwafaka kuwa Mary atapewa shilingi milioni kumi, kusudi aongezee mwenyewe kiasi kilichobakia; ili Irene aende kufungasha bidhaa nchini China. Hii ni baada ya Mary kujieleza sana na kuonyesha mchanganuo wote wa biashara hiyo. “Fedha yote nitakupatia kesho kutwa maana kesho nitakuwa kazini kuna mwanamke ambaye nimepangiwa kumfanyia upasuaji. Na kama zoezi hilo likimalizika mapema saa saba kamili nitakuwa na kikao na uongozi wa Hospital, kuna mambo muhimu ya kuweka sawa kikazi.

    “Ninakuahidi kuwa kesho kutwa mapema sana nitakwenda kukutolea hela hiyo kwenye Akaunti ya Hotel sawa?” Alisema Dr. Jackson kwa upole.“Sawa mume wangu mpenzi asante sana kwa kunijali.” Alisema Mary akifurahia mafanikio hayo na kumpongeza rafiki yake Irene kwa ushauri wake.

    “Usijali wewe ni mke wangu. Unadhani mali hizi zote ni za nani kama sio zetu wote pamoja na mtoto wetu?” Alisema Dr. Jackson kwa sauti ya upole sana. Alipotaja habari za mtoto alikuwa kama ametonesha kidonda kwa Mary. Mary alikumbuka vizuri tahadhari ya Ramson, isitoshe kesho yake ndio ulikuwa mwisho wa kumpelekea fedha zake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ila alijipa moyo kuwa mara tu ifikapo keshokutwa majira ya saa sita, atakuwa mbele ya Ramson akimpatia Fedha zake zote. Alijua tendo hilo litaondoa shida zote na kumfanya ayafurahie tena maisha yake na mumewe. Hilo ndilo jambo la muhimu sana kwa kuirejesha furaha yake na uhuru moyoni mwake.

    Dr. Jackson naye alihuzunika sana moyoni mwake kwa kupata habari za ajabu ajabu kutoka kwa Rafiki yake Mudy. Japokuwa hakuziamini kabisa lakini zilikuwa zinamsumbua kila saa. Moyo wake ulimwuma kwa uchungu kila anapofikiri kuhusu habari zile. Kila wakati alikuwa akijiuliza kama ikitokea kuwa ni kweli mkewe anamsaliti kwa Ramson angejisikiaje? Mahesabu hayo ya ndani kwa ndani yalimfanya kila wakati kukosa raha kabisa.

    Naye alijiwekea ahadi ya kutafiti habari zile kwa kina.Kwa fikra zake aliamini kuwa habari zile ni uongo mtupu hazina ukweli wowote. Lakini kwa kujiridhisha ilikuwa ni lazima azifanyie utafiti. Kila mmoja kati yake na Mary alikuwa na fikra zake tofauti na mwenziye.

    Fikra zao zikilenga kutafuta ubora wa maisha yao ya ndoa. Mawazo hayo yaliendelea hadi pale walipopotelea ndani ya usingizi mzito. Kila mmoja aliingia katika ndoto mbalimbali zilizousukuma usiku ule hata ikafikia asubuhi. Waliamka wenye mawazo tofauti japo kila mmoja alionyesha furaha kwa mwenzake. Kila mmoja alimpenda mwenzake, kwa dhati.

    Jackson aliona ili furaha yake itimie ni pale atakapofanya upelelezi na kugundua kuwa maneno ya rafiki yake yalikuwa ni majungu tu. Hakutaka kuyakubali moja kwa moja na pia hakutaka kuyachukulia mzaha. Kwa upande wa Mary alitaka amlipe Ramson hela zake, kusudi awe huru na vitisho vyake. Hakutaka ndoa yake iingie kwenye matatizo. Alijua kuwa pindi tu atakapomlipa Ramson itampa nafasi ya kuhama kama alivyomweleza mwenyewe. Ikitokea hivyo itampa nafasi nzuri ya kuyafurahia mapenzi yake huku moyoni akiwa huru kwa asilimia nyingi na mumewe.

    * * *

    Ulikuwa ni usiku wa matumaini kwa Mary. Usiku mwingine uliotanguliwa na mchana uliokuwa na mishemishe nyingi, zilizoambatana na kikao kati yake na Irene. Kikao hiki kilikuwa ni kwa ajili ya kutoa asante kwa ushauri alioupokea kutoka kwake. Ushauri uliosababisha Mumewe kuahidi kumpatia kiasi cha shilingi milioni kumi.

    “Rafiki yangu sina cha kufanya kwako zaidi ya kukushukuru kwa kunisaidia mbinu hizi. Shinikizo la damu liliniandama wakati wote, hivyo mawazo yalipandana kiasi kwamba sikuweza hata kuwaza kiusahihi.” Alisema Mary kwa furaha na matumaini. “Usijali rafiki yangu ni jukumu langu kukusaidia wakati wa taabu.” Alisema Irene.

    Kuna ule msemo usemao: “Akufaaye wakati wa dhiki ndiye rafiki wa kweli, Leo nimedhibitisha maneno hayo kwako. Alisema Mary.. Ila sasa mwenzangu leo ndio siku niliyotakiwa kumpelekea Ramson mzigo wake, wakati ahadi yenyewe nimepewa ya kesho. Sijui nifanyeje?” Alisema Mary kwa wasiwasi kidogo. “Usiwe na wasiwasi kesho sio mbali. Mtengenezee Mshtukizo au kwa lugha ya wenzetu Surprise!

    Vile anavyofikiri sivyo wakati anafikia kuona kama mambo yamekwama ndipo unapomtokea kwa ghafla na kumkabidhi mzigo wake sawa?” Alisema Irene na Mary akaona ushauri huo ni sawa tu kwa sababu hakukuwa na njia nyingine zaidi. Baada ya mazungumzo hayo waliagana. Mary alirudi nyumbani ikiwa tayari jioni imeshafika. Alimkuta msichana wa kazi akimwogesha mtoto naye aliingia jikoni na kuandaa chakula kwa ajili ya familia.

    Mengi yaliyofanyika ndani ya siku hiyo yalimchosha na kumfanya awe na usingizi. Lakini ilibidi ajikaze kwa ajili ya kumsubiri mumewe mpaka atakaporudi. Mnamo saa tatu kamili mumewe alirudi akiwa amebeba zawadi mbalimbali. Vitu hivyo walisaidiana kuviingiza ndani na baada ya kutulia alimwandalia mumewe chakula.

    Baada ya kumaliza kila kitu waliingia chumbani kwa ajili ya kupumzika. Hali ya uchomvu ilikuwa imemwandama Mary hivyo alitangulia kupitiwa na usingizini wakati mumewe akiingia kazini katika kupanga malengo yake ya miradi. Dr. Jackson alitaka kuanza mradi mwingine mkubwa lakini alikuwa hajapanga kuwa ni mradi gani.

    Usiku huo aliamua kupanga na kuamua kuwa ni mradi gani auanzishe baada ya kupata faida zilizojilimbikiza kwa miaka mitatu. Fedha za Hoteli zilikuwa ni nyingi hivyo zilitosha kufanyia mradi wowote mkubwa. Usingizi ulikata na pale ulipojaribu kuja aliuzimisha na kahawa chungu. Mawazo yake yaligombana ndani kwa ndani wakati alipokuwa akifikiria aina tofauti ya miradi, alizidi kuzama ndani ili kufanya uamuzi sahihi.

    Ilipofika saa sita na nusu alishtuliwa na mlio wa simu ya Mkewe. Alivumilia kuona kuwa mwenyewe ataamka kuipokea lakini Mary alikuwa amelala usingizi mzito. Ili kuondoa kero kutokana na kelele hizo aliamua kuichukuwa ili aone ninani mpigaji. Mwanzoni alidhani Irene anampigia rafiki yake kwa ajili ya mpango yao ya kibiashara. Lakini alishtuka alipoona Jina la Ramson kwenye kioo cha simu!

    Mawazo ya Dr. Jackson yalienda mbali sana! Iweje Ramson ampigie mkewe simu usiku huu?! Kabla hajaipokea akawa amekubaliana na maneno ya Mudy. Taratibu aliminya kitufe cha kupokelea na kuwa kimya ili asikie mpigaji anataka nini. Mara Sauti ya Ramson ikasikiika upande wa pili:

    “Mary Mpenzi hii ni mara ya pili kuniahidi na matokeo yake kumbe umeamua kunidanganya! Patano letu lilikuwa leo mchana uniletee shilingi milioni kumi zangu ili niondoke katika mji huu. Kumbuka nilikwambia kuwa zile Milioni kumi ulizonipatia miaka mitatu iliyopita bado nimeziweka kusudi zinisaidie huko nitakakokimbilia kuanzisha mradi mwingine. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tatizo ni kwamba huelewi kuwa ninakabiliwa na hatari kiasi gani nikiendelea kuwepo hapa. Sasa ninataka uchague mawili kwa sasa, kuniletea Fedha zangu mchana wa siku ya kesho au uniletee mtoto wangu. Sitanii Mary!..Labda utajua kuwa sifanyi utani pale utakaposhindwa kuniletea hela zangu hapo kesho kwaheri!”

    Baada ya maneno hayo makali simu ikakatika. Dr. Jackson alishituka sana kusikia maneno hayo! Moyo wake ulimuuma sana baada ya kugundua hata mtoto Lameck ni wa Ramson! Ujasiri na uvumilivu ndio uliomfanya asimwamshe mkewe wala yeye mwenyewe asifanye jambo la ajabu katika kipindi hicho kigumu kwake!

    Taratibu hasira zake zilitengeneza machozi huku moyo wake ukiachia maumivu ya aina yake! “Kumbe Lameck sio mtoto wangu, kumbe fedha nilizoambiwa kuwa ni za biashara ni kwa ajili ya kumpatia Ramson ili kuficha siri kuhusu mtoto! Kweli nimefanywa bwege kwa kiasi kikubwa sana!” Dr. Jackson aliendelea kujiwazia huku akiuguza moyo wake uliokuwa na maumivu kama kidonda.

    Mawazo ya kupanga miradi yakabadilika ghafla badala yake akaanza kupanga jinsi ya kufanya katika janga hili. Alijua kuwa busara ilihitajika kwa kiwango cha juu sana. Kuchukulia papara suala hili ilikuwa ni hatari sana. Kwa Jackson busara aliiwekea kiwango cha juu sana katika kufanya maamuzi. Aliona mengi yaliyofanywa na watu bila kufikiri jinsi yalivyoleta hasara, katika maisha ya watu hao.

    Alimkumbuka rafiki yake Chido aliyeamua bila busara kuua mkewe na hatimaye kujiua mwenyewe, eti kwa sababu alimfumania na House boy wao. Mawazo yake yalimkumbusha jamaa mmoja aliyeitwa Alen aliyekuwa akimiliki biashara nyingi zikiwepo vituo saba vya mafuta ya magari. Jamaa huyu aligundua kuwa rafiki yake mpenzi alikuwa na uhusiano na mkewe na kwamba kati ya watoto aliokuwa nao wanne, wawili walikuwa wa huyo rafiki yake.

    Huyo naye alichukuwa maamuzi ya kuwaua watoto wote wa jamaa yake na kumwua mkewe kwa bastola,kisha akakimbia. Baadaye Alen alikamatwa na Polisi akiwa mafichoni na kupelekwa mahakamani. Mahakama ilimkuta na hatia hatimaye alihukumiwa kifungo cha maisha Gerezani. Mali zake alizozisumbukia kwa muda mrefu kwa taabu, aliziacha huku maisha yake yakiwa nyuma ya nondo akiteseka bila kikomo. Haya yote yalipita katika kichwa cha Dr. Jackson. Alifikiria kwa kina kitu cha kufanya ili asilete madhara kwa mtu yeyote.

    Mwishowe akaona vema kuwa asubuhi akatoe hela zote alizozitaka mkewe na kumkabidhi. Hizo ndizo zitakazomfanya awabambe pale watakapokutana kwa ajili ya kukabidhiana. Kwa njia hiyo Wezi wake watajihukumu wenyewe na huo unaweza kuwa ndio mwisho wa mkewe kumsaliti. Busara aliyoibuni ni kwamba baada ya kuwakuta jinsi watakavyobabaika na kuomba msamaha mwisho wa yote atatangaza msamaha kwao, bila kusababisha madhara kwa yeyote.

    Moyo wa Dr. Jackson uliuma sana kwa fedheha atakayoipata hasa itakapojulikana kwa watu kuwa mtoto aliyekuwa anajivuna naye sio wa kwake. Hali hiyo tena ikaibua maumivu katika moyo wake na maamuzi ya kwanza yakatibuka na kukosa uamuzi sahihi, juu ya jambo hilo.

    Machozi yalimtoka pindi alipokuwa akimwangalia mkewe aliyekuwa katikati ya usingizi. Mwisho wa yote alipitisha uamuzi aliouona ni wa Busara zaidi. Alipoangalia saa yake alikuta ilikuwa ni saa kumi na moja alfajiri. Alikesha hapo kitini akiwa amechanganyikiwa kutokana na mlundikano wa mambo. Mary aliamka alifajiri hiyo baada ya simu yake kupiga Alam. Ulikuwa ni wakati wa kuanza majukumu yake ya kumwandalia mumewe chai kusudi awahi kwenda kwenye mizunguko ya siku hiyo.

    “Heey! inamaana leo hujalala kabisa! Mbona uko vilevile na nguo zako ulizotoka nazo kazini jana?” Aliuliza Mary kwa mshangao. “Ni kweli sijalala kabisa nimekuwa na mambo mengi sana usiku huu.” Alijibu kwa upole sana Dr. Jackson akiwa kajiinamia mezani, akijifanya kuwa anapitia mahesabu kwenye karatasi.

    Lengo lake lilikuwa kuficha uso wake uliokuwa na majonzi. Sawa mume wangu pole sana kwa kazi hiyo nzito, ila ungejipumzisha japo kidogo kazi haziishi. Mwili ndio huo huo, wenyewe hauna spea unatakiwa uupumzishe, kusudi upate nguvu kwa ajili ya kufanya mambo mengine.” Alishauri Mary na kuingia maliwatoni kujiandaa, kwa ajili ya kuanza majukumu yake.

    Jackson hakujibu neno ila baada ya mkewe kutoka bafuni,naye aliinuka na kwenda kuoga. kisha akajiandaa na kumuaga mkewe kuwa anaondoka. “Si usubiri kidogo nikuandalie chai mume wangu?” Alisema Mary. “Nina suala muhimu naenda kuweka sawa ofisini kusudi niwe huru baadaye kwenda Bank; nikichelewa naweza nisipate muda wa kufanya mapatano yetu.” Alisema Dr. Jackson na kutoka huku akielekea lilipo gari lake alipanda ndani na kuliondoa gari kwa mwendo wa taratibu.



    * * * *

    Dr. Mudy alifurahi kumwona rafiki yake amemtembelea asubuhi hiyo. “Karibu ndugu yangu mbona asubuhi sana kwema huko?” Aliuliza Mudy akijaribu kuchangamka kwa rafiki yake. “Kwema tu kwani ni mara ya kwanza kuja hapa asubuhi kama hivi?” Aliuliza Dr. Jackson kisha alinyoosha mkono ili kusalimiana na rafiki yake. Walishikana mikono na kusalimiana, kisha Mudy akamkaribisha rafiki yake sebuleni.

    Baada ya kukaa kwenye kiti Dr. Jackson alimwambia rafiki yake: “Rafiki yangu nimeamini kile ulichokisema. Nimefanya upelelezi baadaye nimedhibitisha jambo lile kuwa ni kweli.” Alisema hivyo kisha akatulia kidogo… kisha akamweleza kila kilichotokea usiku wa jana yake. Dr.Mudy alikuwa anasikiliza kwa makini sana. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Lakini rafiki yangu una moyo wa uvumilivu sana. mtu mwingine angeshafanya mambo ya ajabu kwa hasira. Sasa ulikuwa unataka nikupe ushirikiano gani baada ya kugundua mambo hayo?” Aliuliza Dr. Mudy kwa utulivu. “Kwako nimekuja ili unipe ushahidi ulionao juu ya swala hili kusudi nipate nyongeza ya hayo niliyoyashuhudia jana.” Alisema Dr. Jackson. “Sawa rafiki yangu.” Alisema Mudy kisha akaenda jikoni kumwita mkewe na kumtaka awaletee kahawa. Kisha akarudi kwenye kiti chake na baada ya hapo akaendelea na mazungumzo..

    ”Unajua tangu mtoto anazaliwa nilijua kabisa kuwa hakuwa wa kwako. Ila nilinyamaza sikutaka kukuchanganya maana ulikuwa masomoni. Hali hiyo ilininyima rahasana na baadaye nilifuatilia ili nijiridhishe katika mashaka yangu. Kufuatilia kwangu nyendo za shemeji za kila wakati za ufukweni, kukazaa matunda.Siku moja nilienda ufukweni nikawaona Ramson na shemeji wakiwa wanaogelea. Hali hiyo ikanifanya nichukuwe picha kadhaa za ushahidi.

    Haikuishia hapo niliendelea kupeleleza na kugundua mengi sana. Mengi ya kutosha ambayo nayo niliyapiga picha. Lakini pia baadaye nikakumbuka tukio la ajali mbaya uliyoipata nchini India, tulipokuwa pamoja masomoni. Baada ya ajali ile ya piki piki uliyoipata baada ya kugongwa na gari, ulipopimwa ulionekana kuwa hungeweza kupata mtoto katika maisha yako. Ushahidi wa hilo ni vyeti hivi vya Hospitali uliyotibiwa. Wakati unapatiwa matibabu ulikuwa hujitambui, kwa namna hiyo kila kitu nilihusishwa mimi kama ndugu yako.

    Majibu hayo ya vipimo usingelivikumbuka kwa sababu wakati yanatolewa wewe ulikuwa mahututi kitandani. Nilipewa vyeti vyako na kwa bahati nikasahau kukupatia, nilihifadhi kwenye begi langu. Nilishanga nilipopata habari kuwa Shemeji alikuwa mjamzito. Ndipo nikakumbuka maneno ya Daktari kule India. Kumbukumbu yangu ilinipeleka kwenye cheti nikaamua kukitafuta. Baadaye Mungu sio Athumani nilikipata.

    Hiki ndio cheti chako kinachodhibitisha kuwa huwezi kupata mtoto!” Dr. Mudy alimwonyesha rafiki yake cheti hicho… na kumfanya Dr. Jackson aendelee kupigwa na butwaa!..Kisha akaendelea.“Kwa hiyo mpaka hapo nyongeza yangu ni hiyo na ushahidi wangu ni huo hapo. Moyo uliniuma pindi nilipokumbuka jinsi mama alivyokuwa akimsema vibaya mkeo kuwa ni mgumba.

    Hali hii ikanipa kuona kuwa labda shemeji alifikia mahali akapimwa na kuonekana kuwa hakuwa na matatizo hivyo akaamua kuzaa nje ya ndoa na kuificha siri hiyo japo kwa fedha ili kuficha aibu yake na yako katika ndoa yenu. Ndio maana akaamua kufanya hivyo!” Alisema Mudy akiwa katika hali ya kumtetea Shemeji yake kusudi rafiki yake asimchukulie maamuzi magumu.”

    Hayo niachie mwenyewe acha kumtetea! Dr. Jackson alisema huku akikiangalia kile cheti na picha alizopigwa mkewe akiwa na Ramson Ufukweni. Mara alisikia nyayo za shemeji yake yaani mke wa Mudy akija mezani akaficha zile picha chini ya meza. Mke wa Mudy alimsalimia shemeji yake kwa uchangamfu sana na baadaye alimkaribisha kahawa. Baada ya kuwamiminia kwenye vikombe. Jackson alishukuru kwa kahawa na kuendelea na mazungumzo yake na Dr.Mudy.

    “Jambo hilo la kuanza kumtetea shemeji yako achana nalo kabisa. Niachie mimi mchezo mzima nitajua nifanyeje sawa?” Alisema Dr. Jackson wakati akimalizia kahawa yake na kisha alinyanyuka akiwa kashikilia ushahidi wa picha na cheti chake baadaye akaaga kuwa anaondoka. “Sawa rafiki yangu lakini hupaswi kuchukuwa hatua yoyote mbaya. Ninakuamini sana kuwa wewe ni mtu jasiri unayeweza kuvumilia mambo magumu katika maisha.

    Sitaamini macho yangu kama utaonyesha kubadilika katika tabia yako ya mwanzoni. Jikaze na uendelee kuwa jasiri na mvumilivu ili mambo haya yamalizike kwa usalama. Naamini baada ya hapo amani itakuwa kubwa katika maisha yenu.Ninasema hivyo kwa sababu ninajua hii ni bahati mbaya tu.” Alisema Mudy maneno ya busara sana kwa rafiki yake baada ya kumwona akiwa na hasira kali. “Okay nimekuelewa nitakuona jioni kukupa michapo kuhusu kile kitakachotokea maana nataka niwafanye wakutane leo.”

    Alisema Dr. Jackson huku akiingia ndani ya gari lake na kuliondoa baada ya kuangalia saa yake ya mkononi. Neno la mwisho alilosema Dr. Jackson, Mudy hakulielewa kuwa alikuwa na maanisha nini kusema kuwa alikuwa anataka awafanye wakutane ufukweni leo. Mudy alikumbuka kumpungia mkono rafiki yake wakati akiwaamechelewa sana; badala yake aliona vumbi kiasi lililoonyesha kuwa rafiki yake alishatokomea.



    * * *

    Mary alifurahi sana kupatiwa mzigo wa hela na mumewe. Woooow! nafurahi sana Mume wangu kuona kwamba unanijali kiasi hiki. Asante kwa kuwa Mume mwema kwangu.” Alisema Mary wakati akizipokea hela hizo. “Usijali ni kawaida tu kwa mume kumjali mkewe.

    Ila sikai kuna mahali nakimbia nimekuletea tu hizi hela kusudi umpelekee rafiki yako, awahi kufanya utaratibu wa safari ya China au sio?” Aliuliza Dr. Jackson wakati akitoka na kuelekea iliko gari yake. Kwa Mary ilikuwa ni nafuu kwake kuona Mumewe kaondoka ili apate mpenyo wa kupeleka hela zile kwa Ramson. Alijiandaa haraka haraka na baada ya muda alianza safari kuelekea Ufukweni.

    Mwendo wake ulikuwa wa kasi sana wakati akienda ufukweni kwani alijua kuwa huenda mumewe angerudi mapema nyumbani asije akamkosa kisha akamfuata kwa Irene nako akamkosa ikawa taabu.Baada tu ya kuondoka Dr. Jackson alipiga simu nyumbani kwa msichana wake wa kazi aitwaye Magreth: “Halo mage mama ameshatoka au bado yupo?” Aliuliza ili kuhakikisha. “Ametoka na gari Muda si mrefu.

    Kwani hukumpata kwenye simu yake?” Aliuliza Mage. “Simpati sijui kuna tatizo gani kwenye simu yake alijibu Dr.Jackson kisha akakata simu na kuingia kwenye gari tayari kwa safari ya nyumbani. Aliporudi nyumbani aliingia kwa haraka chumbani na kumchukuwa mtoto Lameck na kuingia naye kwenye gari hatimaye kuliondoa kwa mwendo wa kasi sana. Hali hiyo ilimchanganya sana Mage kwa sababu ndio alikuwa anamwandalia mtoto uji wake. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alikosa la kusema kwa sababu hakupata hata nafasi ya kuuliza, kutokana ana haraka aliyokuwa nayo bosi wake. Njiani watu walishangaa mwendo huo wa gari ilikuwa kama gari ya mashindano. Kwa mwendo huo aliwahi kufika maana kwa mbali aliona gari ya Mary ikiingia kwenye kibarabara kidogo ufukweni hapo.

    Baada ya Mary kupaki gari yake alitoka kwa haraka na kuelekea ilipo nyumba ya Ramson na wakati huo huo Dr. Jackson aliipeleka gari yake na kuipaki kando ya gari la mkewe. Taratibu alitoka ndani ya gari na kunyata huku akiwa amejawa na hasira kubwa sana. Alimwona mkewe akikumbatiana na Ramson baada ya Ramson kutoka kwenye nyumba yake. Ni ajabu kuwa hawakumwona kwa haraka Dr. Jackson akija labda ilikuwa ni kwa sababu ya shauku yao ya kuonana.

    Mfuko wa hela ulikuwa kwenye kiti wakati wao walipokuwa wakisalimiana. Kabla hawajamaliza kusalimiana walisikia sauti: “Hapo hapo mlipo msifanye jambo lolote wala kukimbia! Nataka maelezo ya kutosha kila mmoja ajieleze kwa zamu juu ya ubaya huu mnaonitendea.”Alisema Dr. Jackson kwa sauti nzito isiyo na mzaha hata kidogo. Mary na Ramson walipatwa na mshituko usio wa kawaida! Baada ya kugeuka walikutana na mtutu wa bastola! Mary alitamani ardhi ipasuke na kuingia! Alifedheheka sana kubambwa na mumewe katika hali ile akiwa na Ramson. Pamoja na kuiona bastola bado Ramson hakuvumilia aliamua kukimbia. “Simama hapo hapo kabla sijakumaliza!” Alisema Dr.Jackson kwa sauti kali lakini Ramson aliendelea kukimbia. Dr. Jackson alikasirika zaidi na kufyatua risasi iliyompata Ramson mguuni na kuanguka chini na kuachia kelele za maumivu.

    Baada ya kuanguka Dr. Jackson alimfuata kwa mwendo wa haraka akiwa na hasira kali, huku akiwa amemlenga na mtutu wa bastola yake. Ufukwe huo ulikuwa umetulia sana ila kelele za Ramson tu za maumivu. Wafanyakazi wote wa Ramson walitawanyika kwenda kufungasha mahitaji muhimu kwa ajili ya wateja. Kwa hiyo ufukweni hapo alikuwepo Ramson peke yake na wageni wake hao. Unafikiri unaweza kuniharibia familia yangu kisha unikimbie? Umefanya kosa kubwa sana.

    Heri ungesimama tu tukayaongea kuliko kunikimbia.”Alisema Dr. Jackson kwa hasira huku akimsogelea Ramson kwa hatua imara. Kuona vile Mary aliamua kuingilia kati na kwenda kumzuia mumewe. “Tafadhali usimuue Ramson hana kosa mimi ndio mwenye makosa yote mwache tafadhali.” Mary aliyasema hayo huku akimnyang’anya Dr. Jackson bastola yake.

    Wakati wakinyang’anyana kwa bahati mbaya risasi ikatoka kwenye bastola na kumpiga Mary kifuani, mara hiyo akaanguka chini! Jackson alihamaki sana na kuiweka bastola yak echini na kumwinania mkewe huku akipiga kelele.“Mary mke wangu usife! Mke wangu Mary Usife!! Nisamehe kwa hili lililotokea ni hasira tu. Na mimi nimekusamehe kwa yote uliyonitendea.

    Lakini Mary alikuwa tayari amekata roho. Uchungu wake uliongezeka na kutokwa na machozi mengi, huku moyo ukimwuma sana. Hakutaka kufanya hivyo tangu mwanzo; ni jambo lililotokea kwa bahati mbaya tu. Mary alikuwa kila kitu katika maisha yake. Kosa lile alikuwa tayari kumsamehe mkewe na kuendelea kuishi naye. Alizingatia sana maneno ya rafiki yake Mudy alipomwambia:

    “Moyo uliniuma pindi nilipokumbuka jinsi mama alivyokuwa akimsema vibaya mkeo kuwa ni mgumba. Hali hii ikanipa kuona kuwa labda shemeji alifikia mahali akapimwa na kuonekana kuwa hakuwa na matatizo hivyo akaamua kuzaa nje ya ndoa na kuificha siri hiyo japo kwa fedha ili kuficha aibu yake na yako katika ndoa yenu. Ndio maana akagharimika kufanya ujanja ili atoe fedha zote hizo!”

    Maneno hayo yalijirudia rudia katika akili zake huku akilia machozi mengi. Baadaye alikumbuka tena maneno ya mwisho aliyoambiwa na Dr. Mudy wakati wakiagana kuwa:

    “Ninakuamini sana kuwa wewe ni mtu jasiri unayeweza kuvumilia mambo magumu sana katika maisha. Sitaamini macho yangu kama utaonyesha kubadilika katika tabia yako ya mwanzoni. Jikaze na uendelee kuwa jasiri na mvumilivu ili mambo haya yamalizike kwa usalama. Naamini baada ya hapo amani itakuwa kubwa katika maisha yenu.”

    Maneno haya yalikuja kwa nguvu ya aina yake huku yakimsuta sana, kwa sababu tayari ameshafanya mambo ya ajabu kinyume na ushauri huo. Maisha yake aliyaona bure kabisa bila Mary mke wake. Mara hiyo hiyo akaamka na kuchukuwa bastola yake na kumsogelea Ramson aliyekuwa amejisogeza sana akitaka kutoroka. Alipomwona Dr. Jackson anakuja alipiga kelele za kuomba msamaha: “Nisamehe kaka, usiniue tafadhali! Ni ushawishi tu na ibilisi, nisamehe mkubwa wangu!”Sauti yake ilikuwa ya kutetemeka na macho alikuwa ameyatoa kwa woga akiogopa kifo!

    “Ukweli unastahili kufa tena kifo kigumu zaidi ya mtu yeyote, kumbuka makosa yako yote! Umenichukulia mke wangu na kuzaa naye, na ni wewe umesababisha kifo chake. Lakini Mimi sitakuua kama ulivyofikiri, Moyo wangu unauma sana kwa hukumu jinsi nilivyomwua mke wangu japo sikudhamiria!”Alitulia kidogo akiwa anatafakari jambo! Kisha kama aliyeshtuka akamwambia kwa sauti: “Nipe kalamu na karatasi upesi kabla sijageuza mawazo yangu!” Alifoka kwa hasira kali. “Viko pale mezani kwenye kibanda changu kaka!” Alisema Ramson huku akiendelea kutetemeka kwa hofu.

    “Subiri hapo usiondoke ukiondoka nitakuadhibu.” Alisema hivyo Dr.Jackson wakati akikimbilia kibandani. alikaa baada ya kukuta karatasi na kalamu, kisha akaandika mambo mengi sana kwenye karatasi kama mbili hivi. Baada ya hapo alinyanyuka na kwenda aliko Ramson na kumpa zikiwa zimekunjwa.

    “Chukuwa karatasi hizi na ufuate maelekezo yote yaliyopo humo!” Alisema Dr Jackson huku akiwa katika hali mbaya sana iliyotawaliwa na huzuni na hasira. Ramson alizipokea kwa mashaka huku akiwa anaendelea kusihi asamehewe. Hakujua maana ya karatasi hizo.“Ramson Mtoto wako uliyezaa na mke wangu yuko ndani ya gari yangu pale. Nimegundua mambo yote yaliyofanyika na ushahidi wote upo ndani ya dashboad kwenye gari. Sina tena thamani ya kuishi katika dunia hii bila mke wangu Mary!” Dr. Jackson aliyasema hayo huku akimwacha Ramson na kumsogelea mkewe. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alipofika ilipo maiti ya Mary alipiga magoti na kuishika huku akiongea maneno ambayo Ramson hakuyasikia kwa sababu ya umbali. Ghafla Ramson alimwona Dr. Jackson akinyanyua bastola kujielekezea kichwani! Alipiga kelele “Usifanye hivyo Brother!” Alijikongoja kujaribu kwenda kumzuia asijiue, lakini maumivu ya mguu yalikuwa makali sana kiasi cha kushindwa kusogeza hatua hata tatu mbele.

    Kelele zake za kutaka kumzuia asijiue hazikufua dafu, mlio wa bastola ulisikiika na mara hiyo Dr. Jackson alianguka kando ya mkewe na kufa hapohapo. Mshituko alioupata Ramson ulikuwa ni mkubwa sana, hivyo alipiga kelele za mfululizo kama kichaa! Ilikuwa wazimu hasa maana mambo yenyewe yalikuwa hayachukuliki katika akili za kawaida!



    ITAENDELEA

Blog