Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

JULIANA - 2

 







    Simulizi : Juliana

    Sehemu Ya Pili (2)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alishindwa kuvumilia, moyo wake ulikufa na kuoza. Penzi likautafuta moyo huo vilivyo, akawa hajiwezi tena, akashindwa kujificha na hivyo kumwambia Gideon hali halisi.

    Kwa upande wa Gideon, alifurahi, aliona kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wa msichana huyo. Alipoambiwa, akaingizia maneno ya dini lakini wakati mwingine alikuwa akijilaumu kwamba kwa nini alikuwa akimtesa msichana huyo na wakati yeye mwenyewe alimpenda na kumtaka tangu zamani?



    “Hapa nikiremba kibwegebwege mtoto ataondoka. Hainaga kuremba, ngoja nifanye kweli. Kama mambo ya kanisani tutakwenda Mbinguni,” alisema Gideon.

    Akakaa kitandani, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria Juliana tu. Wakati mwingine alihisi kwamba huo ulikuwa utani kwamba msichana huyo alikuwa akimtania na haikuwa kweli kwamba alikuwa akimpenda. Usiku huo, Juliana hakutulia, kila wakati alikuwa akimtumia meseji Gideon kwamba asimtese kwani yeye ndiye alikuwa kimbilio lake na kwamba kama angemtesa basi angejiua.

    “Ujiue?”



    “Gideon! Naomba usinitese mpenzi. Nakuomba!”

    “Tutaongea hiyo kesho wala usijali!”

    “Sawa. Nakupenda.”

    “Ahsante!”

    “Jamaniiiii!”

    “Sasa unataka nisemeje?”

    “Kwani hunipendi?”

    “Daah!”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nijibu! Hunipendi?”

    “Nakupenda!”

    “Naomba usinisaliti mpenzi!”

    “Kwani tayari tushakubaliana?”

    “Gideon! Hata kama ila naomba usinisaliti!”



    “Daaah! Aya!” baada ya hapo, akazima simu yake na kulala.

    Asubuhi ilipofika, akachukua simu yake na kuiangalia, akakutana na ujumbe murua kutoka kwa Juliana, alizielezea hisia zake ni kwa jinsi gani alikuwa akimpenda, jinsi moyo wake ulivyokuwa kwenye mapenzi ya dhati, hakuwa akijiweza, kwake, mwanaume huyo alikuwa kila kitu.



    Gideon akatabasamu, akainuka kutoka kitandani, akachukua taulo lake na kwenda bafuni kuoga. Huko alichukua muda mwingi kumkumbuka Juliana, alimpenda sana lakini hakutaka kujilainisha kwake kwani kwa kipindi chote cha nyuma yeye ndiye alikuwa akihangaika sana lakini msichana huyo hakujali.



    Alipofika chuo, Juliana akamfuata, kabla ya kuzungumza kitu chochote kile, akamkumbatia. Wanachuo wengine wakabaki wakishangaa, hali hiyo ikazua maswali mengi na wengine kuamini zile tetesi zilizokuwa zikisema kwamba watu hao walikuwa wakitoka kimapenzi.



    “Juliana! Huogopi macho ya watu?” aliuliza Gideon huku akiwa amekumbatiana na msichana huyo.

    “Sijali!”

    “Unahisi watasemaje? Wapendwa kukumbatiana na kugandana namna hii kama ruba?” aliuliza Gideon kwa sauti ya kunong’ona.

    “Hata Biblia imeandika salimianeni kwa busu takatifu!”

    “Ila si kukumbatiana!”



    Juliana akatoka mikononi mwa Gideon na kubaki wakiangaliana. Sura ya msichana huyo ikabaki kwenye tabasamu pana lililomchanganya zaidi mwanaume huyo kiasi kwamba moyo wake ukazidi kumpenda japokuwa kwa kipindi hicho hakutaka kumwambia kitu chochote kile.

    Hayo ndiyo yalikuwa maisha yao. Wakati mwingine Juliana alikuwa akienda nyumbani kwa Gideon ambapo huko walipata muda wa kuzungumza sana na kila Juliana alipotaka kulala na mwanaume huyo kitandani akawa akikataa.



    “Sasa mimi nitalala na nani?” aliuliza Juliana, alionekana kukasirika kwani kila kitu alichokuwa akikihitaji, Gideon hakukubaliana nacho kabisa.

    “Muda bado!”

    “Una uhakika?”

    “Ndiyo!”



    “Basi ngoja niwafuate watu wanaoona muda tayari,” alisema na kuanza kuvaa nguo zake harakaharaka.

    Gideon alimwangalia Juliana, msichana huyo hakuonekana kutania hata mara moja, alionyesha kumaanisha kwamba alikuwa radhi kulala na mwanaume mwingine kama tu Gideon asingekuwa radhi.



    Hakuwa na jinsi, alimuumiza sana msichana huyo, alipokuwa akivaa, akamshika mkono na kumvutia kwake, akamwangalia machoni na kutoa tabasamu.

    Juliana alishindwa kuyatuliza macho yake usoni mwa Gideon, alikuwa akijisikia aibu na hivyo kuangalia chini. Gideon akaanza kuzitoa nguo zake na hatimaye baada ya dakika chache zikaanza kusikika sauti za kitanda kikilalamika.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuwa wapenzi, hawakulala siku moja bali waliendelea kufanya hivyo kila siku. Mapenzi yao yakawa radhi, wakasahau kuhusu Biblia, hata mafundisho ya kanisani hawakuyakumbuka kabisa.

    Walipendana kwa mapenzi ya dhati, kwa kuwa Gideon hakuwa na uwezo mzuri kifedha, msichana Juliana ambaye alitoka katika familia yenye uwezo ndiye aliyekuwa akigharamia kila kitu, kuanzia kodi ya nyumba ya mwanaume huyo mpaka chakula.



    “Gideon! Ninahitaji kuwa nawe maisha yangu yote,” alisema Juliana huku akimwangalia Gideon.



    “Hakuna shida mpenzi. Ninakupenda, nipo tayari kuishi nawe mpaka kifo kitakapotutenganisha,” alisema Gideon huku akimwangalia msichana huyo.

    “Kweli?”



    “Niamini mpenzi. Ninakupenda sana!”

    Wakati wakilifurahia penzi lao jipya, nyuma ya pazia kulikuwa na watu ambao waliumia sana kuwaona wawili hao wakipendana na hivyo kuanza figisufigigu na miongoni mwa watu hao alikuwa msichana Halima.



    Kwa kumwangalia, alikuwa msichana mrembo, mwenye ngozi ya maji ya kunde, alikuwa na uzuri wa ajabu na wanaume wengi walikuwa wakimpenda mno.

    Halima hakuwa msichana mwepesi, alikuwa mgumu, watu wengi walimfuata kwa pesa na magari bado hawakuweza kumpata, wengine walimtumia zawadi mbalimbali lakini hawakuweza kufanikiwa kulipata penzi la msichana huyo.



    Halima alikufa na kuoza kwa Gideon, alimpenda, kwake alikuwa mwanaume mwenye taswira ya ajabu, aliuburuza moyo wa msichana huyo kiasi kwamba kuna wakati akawa hajiwezi.



    Alichukia mno alipoona Juliana akiwa na mwanaume aliyekuwa akimpenda kwa moyo wa dhati. Usiku alipokuwa kitandani alikuwa akilia sana, alimuomba Mungu ampate Gideon katika maisha yake kwani ndiye mwanaume aliyeonekana kuzaliwa kwa ajili yake.



    Mapenzi yalimliza, wivu ukamchoma mno moyoni mwake, akawa hajiwezi na muda mwingi alikuwa akiziangalia picha za Gideon zilizokuwa katika simu yake ambazo alimpiga kisiri na kuzibusu.

    Alikuwa tayari kufanya chochote kile lakini mwisho wa siku awe na mwanaume huyo, alikuwa tayari kupoteza kila kitu lakini awe na mwanaume huyo aliyekuwa wa ndoto katika maisha yake.



    Baada ya kuvumilia sana, baada ya kulia sana akaamua kuupiga konde moyo wake na kumfuata mwanaume huyo. Hakuogopa tena, alikuwa tayari kukataliwa lakini mwisho wa siku awe amemwambia mwanaume huyo kuhusu hisia zake, kwa nini aogope? Kwa nini ateseke? Kwa nini aumwe na wakati kulikuwa na daktari wake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Akamuomba Gideon muda wake, alitaka kuonana naye sehemu, wazungumze mawili matatu lakini siku za kwanza mwanaume huyo alimkatalia kwa kumwambia kwamba hilo lisingewezekana, na kama alitaka lifanyike basi aende na Juliana.

    “Gideon!”

    “Nimemaanisha Halima! Siwezi kuja peke yangu, ukitaka nije na Juliana,” alisema Gideon kwani alijua ni kitu gani kingetokea huko.

    “Hapana Gideon! Ninahitaji uje wewe tu!”

    “Haliwezekani!”

    “Gideon!”



    “Nimesema haiwezekani!”

    Gideon hakutaka kubaki mahali hapo, akaondoka zake na kumuacha msichana huyo akimwangalia tu. Halima aliumia moyoni mwake, alitamani kumsimamisha mwanaume huyo lakini halikuwezekana kabisa.

    Alimpenda, hakutaka kumuacha hivyohivyo, hakutaka kukata tamaa, aliamini kwamba kama angeendelea kumuomba sana mwanaume huyo mwisho wa siku angemkubalia na hivyo kukutana faragha na kuzungumza.



    Halima alijua kusumbua, alijua kupiga simu kiasi kwamba ikaonekana kuwa kero kwa Gideon hali iliyomfanya kukubali kuonana naye kwani kwa jinsi alivyokuwa akisumbua, alijua kabisa kuna siku Juliana angejua kile kilichokuwa kikiendelea.



    “Aya nimekuja! Unahitaji nini?” aliuliza Gideon baada ya kuonana na msichana huyo.

    “Gideon! Nimeshindwa kuvumilia. Ninakupenda mno. Nimekuwa nikitamani sana kuwa nawe, umenitesa sana moyoni mwake, sijiwezi, nimekuwa mtu mwenye mawazo sana juu yako, najua kwamba una mtu lakini sidhani kama Juliana anaweza kukuondoa moyoni mwangu,” alisema Halima huku akimwangalia Gideon aliyeonekana kushangaa.



    Halima alikuwa msichana mrembo sana, tena zaidi ya Juliana. Gideon alishangaa, ilikuwaje msichana mrembo kama huyo amtongoze na wakati kulikuwa na wanaume wengi waliokuwa wakimfuata? “Unanichanganya Halima,” alisema Gideon.



    “Gideon! Nakuchanganya!”

    “Inakuwaje msichana mrembo kama wewe uniambie kwamba unanipenda? Kuna wanaume wengi wanakufuata na kukuhitaji, inakuwaje uje kwangu?” aliuliza Gideon.

    “Kwa sababu nakupenda.”

    “Lakini nina mtu!”

    “Hata kama Gideon! Ninakupenda, ninakuhitaji, naomba uwe wangu,” alisema msichana huyo.



    Gideon alibaki kimya, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria mpenzi wake, Juliana. Ni kweli Halima alikuwa mzuri wa sura, alipendeza na kuvutia machoni mwake lakini kumsaliti Juliana kwa ajili yake aliliona jambo gumu sana.

    Alikumbuka jinsi alivyoteseka kwa ajili ya Juliana, zaidi ya miezi mitatu alijifanya mlokole akishinda na Biblia, iweje leo aje kumsaliti msichana huyo kiwepesi namna hiyo?



    “Haiwezekani!” alisema Gideon.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Huo ndiyo ulikuwa msimamo wake, hakutaka kabisa kuwa na Halima, moyoni mwake, hakukuwa na msichana aliyekuwa na nafasi kubwa kama Juliana.

    Siku ziliendelea kwenda mbele, msichana huyo hakutulia, aliendelea kumsisitizia mwanaume huyo kwamba alikuwa akimpenda sana lakini Gideon hakuwa mwepesi kukubaliana naye. Moyoni mwake kulikuwa na msichana mmoja tu, Juliana ambaye kwake alikuwa kila kitu.



    Juliana akaanza kuingiwa na hofu, kila alipokuwa akimwangalia mpenzi wake aliona kabisa kukiwa na utofauti, hakuwa na furaha kama kipindi cha nyuma, hakuwa amechangamka kama siku chache zilizopita.

    Alimzoea sana, mabadiliko hayo yakamtia hofu na kuanza kumuuliza, kama mpenzi wake alitakiwa kujua kila kitu. Alipomuuliza, Gideon hakumwambia ukweli, alimwambia kwamba hakukuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea, alikuwa kawaida kama zamani.



    “Hapana! Hebu niambie mpenzi wangu. Kuna nini?” aliuliza Juliana huku akimwangalia Gideon.

    “Hakuna kitu!”

    “Una uhakika?”

    “Ndiyo mpenzi! Naomba uniamini,” alisema Gideon, hapohapo akamsogelea Juliana na kumkumbatia, akampiga mabusu mfululizo kwenye paji la uso wake na mdomo.



    Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, Gideon hakutaka kabisa kumsogelea Halima, kila alipokuwa akimuona alikuwa akimkwepa. Msichana huyo hakuwa na jinsi, alichokifanya ni kuchukua simu yake na kuanza kuwasiliana na mwanaume huyo huko.



    Bado Gideon hakutaka kuelewa, hakuwa tayari kuona akitembea na msichana mwingine zaidi ya Juliana. Halima alijitahidi, alipambana kwa nguvu zote kulichukua penzi la Gideon lakini ikashindikana kabisa, hivyo alichokifanya ni kuanza kumtumia picha mbalimbali.



    Zilianza picha za kawaida ila kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele msichana huyo akabadilisha picha zake na kumtumia picha za nusu utupu mpaka zile za utupu kabisa. Gideona aliziona, akachukia mno moyoni mwake kwani alijua madhara ya kuwa na picha zile katika simu yake. Hapohapo akampigia Halima.



    “Ndiyo unafanya nini?” aliuliza Gideon huku akionekana kuwa na hasira sana.

    “Kwani nimefanyaje mpenzi?



    “Nani mpenzi wako? Hivi unaona mimi ni mjinga mpaka kunitumia mapicha yako. Wewe mwanamke nielewe. Usinitumie tena picha zako,” alisema Gideon kwa hasira. “Nitashindwa kujizuia. Ukikata simu, nakutumia tena!” alisema Halima na kukata simu.

    Gideon alifikiri ulikuwa utani, msichana huyo hakukoma, akamtumia tena na tena kitu kilichomfanya kuwa na hasira kupita kawaida.



    Hofu yake kubwa ilikuwa ni mpenzi wake, Juliana, alijua kwamba endapo msichana huyo angeendelea na tabia yake ya kumtumia picha hizo kila siku basi kuna siku ingetokea balaa endapo tu msichana huyo angeziona.

    Hakutaka hilo litokee kwani kwenye kitu ambacho hakutaka kabisa kuona kikipotea mikononi mwake kilikuwa ni mpenzi wake, Juliana, msichana mpole, mnyenyekevu na aliyekuwa na mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kazi kubwa ya Gideon ilikuwa ni kuzifuta picha za msichana huyo. Alizituma nyingi tena huku zikimuonyesha akiwa kama alivyozaliwa na nyingine zikiwa ni video ambazo zilimuonyesha akicheza mtupu na wakati mwingine akifanya matendo yasiyoandikika hadithini.



    Gideon alichukia lakini hakuwa na jinsi, moyo wake ulishikwa na ghadhabu kiasi kwamba akaamua kuiblock namba ya msichana huyo ili asiweze kupokea ujumbe wowote kutoka kwake.

    “Gideon! Nahisi kuna kitu kinaendelea, hebu niambie kuna nini,” alisema msichana Juliana huku akimwangalia mpenzi wake.



    “Hakuna kitu!” “Umekuwa ukiniambia hivyo mara nyingi na kila ninapokuangalia nagundua kwamba kuna kitu, naomba uniambie, kuna nini mpenzi wangu!” alisema Juliana.

    Majibu yake hayakubadilika, hakutaka kumwambia kuhusu msichana Halima kwa kuamini kwamba wawili hao wangeweza kugombana. Siku zikaendelea kukatika huku ugomvi baina yake na Halima ukiendelea kila siku.



    “Ngoja nifanye kitu,” aliwaza Gideon, alipata njia ya kumzuia msichana huyo asimfanyie mchezo ule tena.

    Akamfuata rafiki yake aliyeitwa Fred na kumwambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Fred hakuamini, alimjua Halima, alikuwa msichana mrembo aliyekuwa akitongozwa na wanaume wengi na kuwakatalia, hakuamini kama msichana huyo angeweza kufanya vitu vya kipumbavu kama hivyo.



    “Kwa Halima! Hapana Gideon! Labda useme wakina Stella lakini si Halima huyu,” alisema Fred huku akimwangalia Gideon.

    “Niamini! Huyu msichana mchafu sana. Alinitumia mapicha yake mengi sana ya utupu utupu,” alisema Gideon.

    “Kwanza hebu nizione.”

    “Uone nini?”

    “Hizo picha. Nataka nione akiwa mtupu anafananaje!” alisema Fred huku akionekana kuwa na mshawasha wa kuona picha hizo.



    “Nilizifuta!”

    “Gideon! Unapata picha za utupu za Halima unazifuta! Daah! Sasa huo si ndiyo ushahidi wenyewe! Halafu picha za Halima kweli unazifuta kaka, tena unaniambia mimi bila kunificha! Haki ya Mungu ningekuwa Syria, ningevivisha mabomu nije kujilipua mbele yako, hutakiwi kuishi kabisa, Mungu kakupa pumzi za kuishi, wewe unazitumia kufuta picha za utupu za Halima! Haupo siriazi kabisa,” alisema Fred huku akimwangalia Gideon kwa macho yaliyoonyesha mshangao mkubwa.



    Gideon hakutaka kujali, alichokuwa akihitaji ni kusaidiwa na kijana huyo tu, alimwambia dhahiri kwamba walitaka kufanya mchezo ambao ungemfanya msichana huyo kutokutuma picha tena au kumsumbua na jambo zuri ambalo lilitakiwa kufanywa ni kumfuata na kumwambia kuhusu picha hizo za utupu.



    Kwa Fred wala hakukuwa na tatizo, akakubaliana na Gideon kwamba kitu hicho kingefanyika kwa haraka sana na hivyo baada ya kuachana, jioni ya siku hiyo akamtafuta msichana huyo na kumuomba kuonana naye kwa ajili ya kuzungumza.

    “Uzungumze na mimi?” aliuliza Halima, kama kawaida yake akabinua kidogo midomo.



    “Ndiyo!”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hapana! Nipo bize sana,” alisema huku akichukua mkoba wake na kuanza kuondoka.

    “Sawa. Tutakutana kwenye Mtandao wa Global Publishers kwa ajili ya kuzioa picha zako za utupu,” alisema Fred, hakutaka kubaki mahali hapo, huyo akaanza kuondoka zake.



    Halima akashtuka, hakuamini kile alichokisikia, alihisi kwamba alisikia vibaya alichokuwa ameambiwa na mwanaume huyo, akahisi damu yake ikianza kuzunguka kwa kasi mwilini mwake, mapigo ya moyo yakaanza kudunda kwa nguvu, hakutaka kubaki mahali hapo, kwa kasi akaanza kumfuata Fred.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog