Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

PENZI LA FUKARA MATESO - 3

  







    Simulizi : Penzi La Fukara Mateso

    Sehmu Ya Tatu (3)



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    naaam



    mwili wa madam s,ukiwa na kisu pembeni ya yalipo makazi ya moyo wake macho ya mshangao maumivu aliyatoa pima...



    kichwa alikielekeza juu ya bati akiegemea shingo katika kiti chake...



    dakika chache nlikuwa naongea naye...muda huu alikuwa ni marehemu...kaniachia zigo zito!



    don na mwenzake awakwepo,sikuwa na shaka ndo wahusika...



    wasichana walijongea wote hawakuweza kuzuia kilio kilio kikatapakaa.



    kwa mbali akatokea madam MERY akuwa peke yake alikuwa na wale wale vijana don g na mangeu



    Pindi nilipoviona viumbe vile mwili ukaanza kuntetemeka kijasho chembamba kuntoka...



    "wote nyamazeni! akuna siri ndani ya jumba hili huyu ni msaliti adhabu yake ndo hii mwili wake utazikwa na vijana wa kazi atakayefumbua domo lake naye yatamkuta haya haya atakayepanga kutoroka litamkuta hili ili."



    baada ya kumaliza kuongea maneno hayo akawapa ishara vijana wale wakaibeba maiti ile na kuondoka nayo...



    akukuwa na polisi, nilichoka...



    " bado kuna vimbelembele miili yao itatumika kusafirishia madawa ya kulevya.."



    madam yule akuogopa kusema...

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    alitueleza wazi!



    malengo yote yalokuwa kichwani kwangu yakayeyuka



    ni siku ya tatu yenye kuogofya tangu niingie ndani ya jengo ilo la kulelea watoto wa mtahani....



    "janeth nakuitaj hofisini!..."



    madam akanita



    Moyo ukanipasuka paaaa,Alikuwa kanikazia macho....



    Moyo ulintetemeka baada ya wito ule wa madam MERY madam katili,asiye na huruma hata chembe sikuwa na budi kwenda akaniangalia kwa muda kabla ajafumbua mdomo wake!



    "JANETH najua unasiku ya nne tangu umekuja! nadhani wenzako washakwambia kila kitu juu ya hapa kituoni siri baina yetu yaitajika na atakayejaribu kutoa siri atauwawa kikatili kama madam S alivyouwawa."



    nikagundua madam yule akugundua chochote juu yangu nikazidi kumsikiliza.



    "sasa ni zamu yako nawe kutumika!"



    nikashtuka akaendelea...



    "mh waziri anategemea kututembelea kuleta msaada hapa kituoni na katika malighafi mpya zilizoingia wiki hii wewe ni mmoja hapo alafu waonekana mjanja usije ukaniangusha kajiandae."



    madam mery aliongea.huku akiwa anatabasamu sikumjibu kitu nikajinyanyua na kuondoka.



    siku hiyo ndiyo siku niliyoandaliwa kwenda kumridhisha yule mwenye kitambi,mke na watoto kama mimi....



    ila mimi sikuwa kama alivyofikiria

    mheshimiwa aliingia na msafara wake kituoni pale akashuka na kuanza kutoa misaada sijui vitanda mashuka vyakula huku waandishi alokuja nao wakipiga picha na kurekodi yale,



    sahiyo miye nilikuwa ndani nikiandaliwa kuondoka na muheshimiwa.



    baada ya kumaliza nikaingia ndani ya gari aliyoko mheshimiwa tukaondoka,tulifika mpaka ofisini kwake ambapo aliacha msafara wake tukaondoka tukiwa wenyewe na mlinzi mmoja mpaka katika hoteli moja ya kifahari,



    akachukua chumba,tukaingia...baada ya kuingia akaitaji kwenda kwanza kuoga...



    wakati akiwa bafuni anaoga sikuichezea nafasi hiyo...nikaikwapua suruali yake na kuisarch nikatoka na simu na hela kwa uangalifu nikatoka nikipitia geti la nyuma nikatoweka maeneo yale bila mlinzi alokuwa pamoja na dereva wakipiga gumzo kwenye gari bila kugundua....



    Muheshimiwa waziri alichanganyikiwa baada ya kutoka bafuni na kunikosa,alizidi kuchanganyikiwa...zaidi pale alipogundua pia simu yake aipo



    alirudi mpaka mapokezi ambapo akuelezwa chochote cha maana,akajipakia ndani ya gari lake na safari kurudi kituo cha mkombozi ikafatia,njia nzima akuongea hasira zilikuwa zimemvimba,...



    simu yake ilikuwa na siri zake nyingi ambazo laiti kama ningeziona alijua lazima ingekuwa hatari kwake! kituoni akunikuta.



    baada ya taharifa ile viongozi wote wa kituo kile walichanganyiki

    wa,



    mimi sasa nilikuwa ni hatari kwa maisha yao,amri ikatolewa na kigogo,mmiliki wa kituo kile nisakwe kwa udi na uvumbi niletwe nikiwa maiti kuficha siri za wakubwa,



    vijana wa kazi! usalama wa taifa,na vijana maalum wakaingia kazini kunisaka!



    wewe awo vijana watano wa PATRICK sijui migambo ndo wanakutisha mimi nimesakwa na makomandoo! usalama wa taifa,na majambazi walokubuhu,...



    siku hiyo kulikuwa kuna giza tororo! kwa mwendo wa kunyata nikiwa nimevaa nikabu iloficha sura yangu nilikuwa kandokando ya nyumba moja ya kifahari mawazo yalikuwa yakikiandama kichwa changu macho yangu yalikuwa katika nyumba moja kubwa nikiitazama kwa umakini

    ilikuwa ni nyumba ya madamu mery,lengo la kwenda pale ni kuchukua ufunguo uliomo chumbani kwake ndani ya mto!



    kwa nini madam s aliamua kuja kuifadh huku? sikuwa na shaka kwamba madam yule katili akujua kuwa kuna ufunguo katika mto wake!



    na aliuwekaje?!!



    ilo swali sikulijua jibu lake lakin mpelelezi ni mpelelezi tu!



    nikaachana na mawazo hayo! nkafikiria mbinu ya kuingilia mule...kulikuwa na ulinzi mkali getini pale huku taa zenye mwanga mkali zikimulika eneo lile.



    pale hapakuwa mahali sahihi pa kupita.ghafla wazo likanijia kuizunguka ile nyumba na kupanda kwa nyuma.



    Ila je ntaweza kupanda ukuta na sijawah? ujasiri ukanivaa nikaona bora nijaribu nishindwe kuliko kutojaribu.



    nikazunguka bila kushtukiwa na walinzi wale...nikakusanya matofali kadhaa nikayapanga nikalikunja baibui kidogo nikapanda juu ya matofali nikaweka mkono juu ya ukuta



    "WI WU WI WU WI WU WI WU!!!....."



    ghafla kingora kikaanza kulia!.....



    King'ora kile kililia toka juu ya ukuta kilinishtua nikauachia ukuta ule na kuanza kukimbia



    Kumbe ule ukuta ulikuwa na waya wa ulinzi!...



    "Simama hapo hapo kabla atuja usambaratisha ubongo wako!"



    Nilisikia sauti toka nyuma yangu nilipogeuka niliona walinzi watatu wakija ule upande wangu kwa kasi kubwa



    Bastola wakizishika tayari kwa matumizi ikiwa nitakiuka matakwa yao!



    "Nimekwisha!"



    nikajiwazia huku nikiongeza mbio sikuwa tayari kuingia mkononi mwa vijana wale!



    nilikata mitaa miwili mitatu.



    nilipogeuka nyuma bado walikuwa nyuma yangu.ghafla nikaanza kusikia kwa mbali MAULIDI nikakata kwenye ule mtaa niliosikia matwari yakipigwa nikakuta bunge la sherehe nikajichanganya na wa mama.



    nikawa nimefanikiwa kuwakwepa walinzi wale...tuliendelea kusikiliza maulidi mpaka kulipopambazuka..watu wakaanza kusambaratika...nami nikajiondoa kuelekea katika gesti nilopanga kwa muda.nikajitupa kitandani nikitafakari ili na lile....ghafla nikakumbuka kitu! kitu kilichoamsha hari ya uhuru ulopoteya,njia yoyote ya kuingia katika nyumba ya madam mery aikwepo ilibidi nitumie plan b! kwenda kwa yule mama kule uswazi anipe namba za mtu atakayenisaidia! ni mtu gani huyo?



    hamu ya kutaka kujua ilinisukuma niamke kitandani hapo na kuondoka

    ilikuwa ni nyumba ya kifukara!,walevi walitawala katika nyumba ile makelele yakitawala.eneo lote kuzunguka nyumba ile ujio wangu pale uliwashtua watu wengi kutokana na juba nililovaa ila ilo sikujaliCHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "nimemkuta bi chau?"

    nikamuulizia mama mmoja alokuwa akiudumia hudumia wateja wake pombe

    "ndiyo ni mimi"

    alijibu yule bibi huku woga ukimvaa,

    "ok na ujumbe wako mama?"

    "ujumbe gani?" yule mama alizidi kudodosa

    "madam s kanipa ujumbe kanambia nije kuna karatasi utanipa,"

    "ooooh yaaah ni kweli" alijibu yule mama na kuingia ndani alipotoka alikuwa na kaupande cha karatasi kilichochafuka akanikabidhi...

    "msalimie sana SALOME shosti mwambie awe hata anakuja kusalimia maramoja moja"

    moyo uliniuma sana katu hakujua kuwa mwenzake kwa sasa ni marehemu,nami kwa kuwa sikuwa na majibu ambayo ningeulizwa na mam yule pindi ningemweleza ukwel



    Ilibidi niage tu na kuondoka zangu!,nilielekea mpaka SHEDRACK hotel,hotel nilopanga ile nikafikia mapokezi na kumsalimia dada yule

    "kuna mtu yoyote alokuja kuniulizia?"

    nkampachika swali!

    "yah walikuja kaka wawili walovaa makoti ya laizar na pikipiki baada ya kukukosa wamesema watarudi ukisharudi uwatafute!"

    "heee dada wameniulizia kwa jina gani?!"

    "mwanamke mwenye juba wa chumba namba 4"



    utata!



    wanaume wenye makoti ya laizar ni watu gan hao?



    wana nia gani na mimi?



    "dada kwani kuna matatizo?"



    muhudumu yule alinioji baada ya kuniona katika tafakuri kuu,woga,nimenyong'onyea



    "matatizo?! no amna matatizo!"



    nilijibu nikiondoka! pale apakuwa sehem salama tena nltaka kwenda chumbani lengo nichukue begi langu niondoke! nikakifikia chumba changu nikausweka ufunguo katika tundu la mlango nkauzunguka! mlango ukantii nkaingia chumbani



    shadaash!!!



    nilipigwa na butwaa baada ya kukuta chumba changu akipo kama nilivyokiacha! nguo zote katika begi langu zilisambazwa chini,..



    kuonesha kwamba kuna msako usiyorasmi ulikuwa ukiendelea humo.



    nlibaki pale mlangoni nimepanua mdomo kwa woga mikono ikiwa kichwani!



    nikagutuka!!



    iliitajika niondoke haraka sana pale.



    nikajua ilo!



    simu!



    nikakumbuka simu ya mheshimiwa waziri nlokimbia nayo,kwa hatua ndefu nikajongea katika begi langu na kuanza kuitafuta



    simu haikwepo!



    Ushahidi aukuwepo!....



    nkazidi kuchanganyikiwa,ushahidi wote umepotea,ntamtafuta huyu kiumbe mwenye namba hizi kwa kutumia simu gani?



    nikawaza nikijilaumu kwa nini nisingeondoka nayo,si simu tu,hata fedha zangu nilizochukua kwa mheshimiwa azikwepo,mambo yalinfikia shingoni kwa haraka sana nkakusanya nguo zangu zilizotawanyishwa.kuziweka katika begi lile...



    chumba kilikuwa shaghala baghala nguo zangu zilitupwa huku na huko,huko na huku,nkaziweka zote katika begi,mara ghafla macho yangu yakatua mlangoni kitasa kilikuwa kikifunguliwa.



    bila hodi



    "nimekwisha JANETH miye"



    niliwaza huku nikiwa bado natetemeka,chumba taratibu kikafunguliwa,na wakaingia vijana wawili walovaa makoti ya laizar..



    KAH!!!..







    Katika siku ambazo ZUBERI mpz wangu nilitetemeka hadi haja ndogo ikantoka ni siku hiyo...



    vijana wale walovaa makoti ya laizar myeusi walinitazama kwa matabasamu yao mapana!...



    muda wote walikuwa bado wapo mlangoni pale,ghafla mmoja wapo akachomoa risasi iliyokwepo kibindoni mwake na kunielekezea! mwenzake akashika simu yake na kupiga namba kadhaa



    "mheshimiwa tumefanikiwa kumkamata!...ndiyo mheshimiwa!..... sawa"



    Baada ya kumaliza kuongea vile akamgeukia mwenzake!



    "mheshimiwa kasema tumpeleke kwake..."



    yule mwenzake aliyeambiwa aliyekuwa bado kanioneshea silaha akanambia...



    "binti nadhani bado ujatujua sisi ni vijana wa usalama wa taifa upo chini ya ulinzi,kimya kimya kirafiki tutatoka na wewe mpaka nje katika gari yetu tutaingia na kuondoka kwa utulivu, tofauti na ivyo ukileta kujua ni ubongo wako tunausambaratisha!"



    akaweka kituo!,akaisweka bastola yake kibindoni,...



    "taratibu beba begi lako tuondoke..."



    sikuwa na uwezo wa kukataa,nikabeba begi langu na kutoka tukapitia mapokezi wenye ma laizar wakamuaga yule dada ambaye kwa upande mmoja au mwingine nilijua anausika kunchomea utambi!



    lakini kanijuaje wakati nilikuwa ndani ya juba muda wote? swali ili sikujiuliza sikujua kitendo cha kutozima simu ya mheshimiwa waziri ndicho kilichonigharimu..



    simu ile ilikuwa na GPS ambayo ilikuwa na uwezo wa kugundua mahala ilipo.



    ndipo muheshimiwa wazir alipotuma vibaraka wake waifatilie mpaka pale ambapo kwa bahati nzur awakunikuta nilikuwa kule uswazi kwa bi chau! kwa kutumia funguo zao wakatafuta,wali

    vyoitaji! baada ya kuridhika wakaondoka na ile simu yao...



    wakiacha ujumbe kwa dada wa mapokezi nikija nipewe taharifa zile na wakaacha namba.



    kitendo cha mimi kufika pale dada wa mapokezi akawapigia simu wazee wa laizar wakanivamia na wakanchukua kiulaini...



    makubwa...



    waliniingiza katika gari yao nyeusi na kuniweka katikati yao wenyewe....njia nzima ilikuwa ni vicheko



    "wewe msichana bado mdogo mrembo! kwa nini unagombana na watu wakubwa?! ...sasa leo waenda kufa katika shamba la mzee...."



    "hivi mzee kasema tumpeleke shambani kwake?!"



    aliuliza dereva akizidi kukanyaga mafuta.



    "ndiyo nje ya mji..."



    alijibu yule kijana huku mkono wake ukichezea mapaja yangu!



    alinishika hapa mara pale ilimradi kero katika mwili wangu,japo mikono yake ilikuwa ikigusa nguo lakini sikupendezeshwa na tabia hiyo!...



    kushikwa shikwa bila idhini ya mshikwaji ni karaha isiyokaraika...



    gari iliendelea kwenda kwa mwendo mkali ule ule mpaka katika hotel moja wale wanausalama wakashuka kwa lengo la kwenda kula wakinifungia milango kusudi nisitoke.



    nikangata mdomo kwa hasira!



    walikuwa wamenizidi tena akili,ghafla macho yangu yakatua katika kiti cha dereva.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nikaiona simu!



    moyo ukapiga paaa!



    nilikuwa na nafasi moja ya kuokoka!,sikuwaza mara mbili nikaikwapua ile simu na kujisachi zile namba



    "hawa watu ni wapumbavu sana hawa kuweka pin cord sijui ni kwa nini?"



    niliwaza huku nikipiga namba zile zikaita....



    "halooo!"



    nkapokelewa na sauti nzito



    "g next hotel,gari nyeus yenye vioo vya tinted,wavulana wawil wamevaa makoti ya laizar...wamenteka nsaidie kaka yangu."



    nkaweka tuo,baada ya kuongea msururu wa maneno simu upande wa pili ikakatwa.



    "heee! mbona sasa ajanijibu?!"



    nikawaza huku nikimpigia tena! heee!

    akakata!



    nkazidi kuchanganyikiwa nilipopiga nkaambiwa namba aipatikani!...



    "ooh shit!"



    nkalaani huku nikifuta ile namba nkairudisha simu ilipokuwa.



    huku tumaini la kupona sasa likiwa limetoweka...



    baada ya dakika chache wale vijana walovaa makoti ya laizar wakarejea wakiwa na kamfuko cha chipsi na kakopo ka juice!



    "kula mwanadada usiseme tumekukalisha na njaa bure"



    kitendo cha kuona kile chakula tumbo likaanza kuunguruma kwa njaa nkakumbuka tangia siku iyanze sijatia kitu mdomini nikapokea chakula kile na kukifakamia,muda huo dereva alikuwa barabarani....



    Duuuh Janeth kapiga namba alopewa na madam kabla ajafa akaambiwa ni ya msaada ameipiga imekatwa na wameianza safar je msaada huo utakuja!



    Na ni nani?!







    Baada ya kumaliza kula chipsi zile,nikakitupa nje kimfuko kile gari ikazidi kukata upepo



    "P2 naisi huyo mtu mwenye bodaboda nyuma yetu si mwema!...kama anatufatilia vile anaonekana yupo makini na gari hii..."



    aliongea dereva!,kitendo kilichonifanya na miye macho yangu niyakaze katika said mirrew ambapo nilimuona kijana akiwa kavaa kofia aina ya bushori,miwani mkononi alikuwa na gloves nyeusi ni kweli alikuwa makini na gari ile...



    "kata kushoto tuingie upande wa pili akiendelea kutufata ingia barabara yoyote ya vumbi!"



    aliongea yule mchezeaji wa mwili,safar hii akiwa kaacha kunishikashika.



    "huyu kidudu mtu atujuh we unamjua huyo?"



    yule jamaa akanibwatukia akiniangalia kwa macho yake makali! nikatingisha kichwa kukataa



    "nimshambulie na risasi nini?"



    "no tutajaza watu huyu anatekwa tu mwache afike usawa wetu! ntafanya anachostaili kufanyiwa!"



    aliongea jamaa yule,akimwangalia dereva kwa makini,kama mwendesha bodaboda alijua akawa anakuja ule upande wa yule jamaa.



    na kwa ghafla jamaa akafungua mlango na kujirusha mzima mzima kwa teke kali aina ya mbwambuko



    "mbwambuko" ni aina ya teke mrushaji hulipiga akiwa hewani hewani mara nyingi sana teke hili upigwa shingoni,tofauti na matarajio yake teke lake likapiga hewa! na mtarajiwa alikuwa kasimama kimapigano hatua mbili nyuma,mrushaji teke akaidondokea pikipiki ilomfanya aachie yowe dogo la maumivu! ila akasimama na kumwangalia mpikaji kwa ghadhabu



    "wewe ni nani? na unajua unapambana na nani?!"



    "sipaswi kujua nnachoitaji ni huyo mdada"



    jamaa yule akaongea kwa kiburi na dharau ilo jaa kejeli ndani yake



    "ati?" jamaa akauliza!



    mvamizi akuangaika kujibu zaidi ya kwenda kwa kasi na kumbatiza mateke mawili ya rasharasha,jamaa akaenda chini!



    ila katu akukubali kulala chini pale akajiamsha kwa haraka na mkono wake akiupeleka nyuma ile anaichomoa bastola yake kibindoni akakutana na teke moja kali liliiloirusha bastola ile pembeni...



    "nini kaka wakimbilia silaha? mwanaume kamili anapambana kwa mikono" akaongea jamaa yule kwa jeuri...dakika hiyo hiyo akajizungusha kwa mateke mawili double kebing! yalompeleka



    Jamaa chini!,yule dereva akafungua mlango wa upande wake na kushuka bastola ikiwa mkononi akaibonyeza kifyatulio,



    mlio wa risasi ukarindima!



    jamaa wa bushori alikuwa akimfata kwa kasi kwa stayle ya kukimbia upande upande risasi zikimkosa kosa!



    ghafla akainama na kuinuka na kipande cha mbao alichokirusha katika mikono ya mfyatua risasi,bastola ikamponyoka,jamaa mwenye bushori ghafla akageuka nyuma na kumrushia ngumi moja yenye ujazo wa kutosha jamaa alokuwa akimfata kwa nyuma! alafu akajiskumia nyuma kidogo kumkwepa yule aliyekuwa anamrushia risasi! akamvaa mwenzake.



    jamaa mwenye bushori ghafla akalirukia gari lile akaubamiza mlango ufunguo ulikuwa mahali pake akaliwasha gari na kuliondoa

    .

    ...bado sikumjua ni nani na lipi lengo lake kuu la kuniokoa.pikipiki ile akiacha mahali pale ambako wale usalama wa taifa walijipakia na kuanza kutufukuzia...



    "wewe ni nani na kwanini umeniokoa?"

    "usiniulize maswali mengi msichana fikiria nini hatma ya maisha yako!"

    yule kijana akanijibu kibabe zaidi,mtoto wa kike mimi sikutegemea jibu lile...

    "umewafanyeje hawa watu?"



    akanpachika swali huku akikata kona kuipotea ile pikipiki



    "ni historia ndefu kaka yangu!"



    "nipe kwa muhtasari!"



    kabla sijamsimulia ghafla akapiga break baada ya kulitoa gari barabarani akafungua mlango



    "shuka mwanamke..."



    akanipa amri nikamtwii nikashuka tukapiga hatua chache tukafika stendi tukajipakia ndani ya gari za buguruni na safari ya kuelekea huko



    ikaanza,tukashuka buguruni tukapanda gari za tmk magorofani! maeneo ya vetenary uswailini ndipo tulipoweka kambi katika gesti ilochoka!



    jamaa mwenye bushori akaenda kuoga alipotoka hapo ndipo nilipoweza kuusanifu mwili wake vizuri!



    alikuwa na kifua cha mazoezi kilichotawaliwa na garden love fupi,pia niliweza kuuona mikono yake ilojaa na kutengeneza misuli ilomzidishia umaridadi!



    nilizidi kumtathminisha macho yangu yakishuka miguuni ni kama miguu ya wacheza mipira "kiazi" kiliota miguuni kutokana na mazoezi ayafanyayo...

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    hakika alikuwa ni bonge la handsome



    JOhn CHAKA aingia mzigoni tena?!



    Je ataweza kumlinda janeth dhidi ya wana usalama au itakuwa kama Ktk MZIMU ULOREJEa?!



    Nadhani wengi mnamjua huyu jamaa kufanya vizuri ktk kitabu chake cha HEKA heka za komandoo Chaka



    Tunaye humu



    ****************





    "msichana,kaoge acha kunshangaa!"



    ghafla nkazinduliwa na sauti nzito,ilojaa kitetemeshi cha kiume!



    nikajinyanyua kiuchovu pale na kuelekea maliwaton kuoga!,fikra zangu zilikuwa juu ya yule mtu! kwa mara ya kwanza nilijikuta NIKIMPENDA!



    "Kaokoa maisha yangu! sina budi kumpa maisha yangu! kijana mzuri sana yule..."



    nilijiwazia huku nikipaka "dokidoki" sabuni....nkaoga haraka na kujifunga kaupande ka kanga!



    nkatoka...nkamkuta jamaa na ugali akiwa anakula! sikujua kautolea wapi! kwa sekunde chache akaacha zoezi lake lile la kula akintumbulia macho! macho ya tamaa!,nami kwa kulitambua hilo nkazidi kumdatisha kwa pozi makusudi! nikaitolea sauti yangu puani!...



    "mh wewe mkaka wala peke yako bila kumsubiri mwenzako!!"



    ni sauti yenye chembechembe za mahaba,nkamuona kijana yule akiachia tabasamu! tabasamu lililomuongezea umaridadi!...



    "usijali mwanamke chakula chako hiki hapa!"



    nusuru ningeangua kicheko,ila nikaishia kutabasamu zilikuwa ni chipsi mayai na soda tena mirinda.



    "mh! kwa hiyo wewe wala ugali mahalage wenye nguvu mimi nile chipsi soda"



    nikamuuliza huku nikifungua ka begi kangu na kutoa aina ya vipodozi na kuanza kujipodoa...



    "mwanamke! nimeamua kukuchagulia hiki na si hichi..."



    akaweka tuo huku akiendelea kula,baada ya kumaliza kujipodoa nikakaa pembeni yake! na kuanza kula



    "mwanamke!"



    akaniita,nkamwangalia huku kipande cha chipsi kikiwa mdomoni



    "unajua atujatambua mpaka saivi na sijajua una ugomvi gani na wale watu na nin lengo la kuniita nikusaidie na ninani alokupa namba zangu!"



    Kukuita?!.....



    ghafla nkashtuka,kumbukumbu za kumpigia simu mtu na namba nilizopewa na bi CHAU zikanijia...



    ikabidi nianze kumweleza stori yote ya maisha yangu toka nikiwa mtahani kuchukuliwa katika kituo kile....



    ,kutumika na vigogo hakika mwenye bushori alistaajabu na zaidi aliuzunika baada ya kugundua madam S kafariki



    "mchezo umeisha! janeth mimi naitwa JOHN CHAKA mtetezi wa kinte,mpelelezi asiye na mipaka,ni kweli taharifa ya kituo kile umoja wa mataifa wanayo wakamweka SALOME kama mpelelezi pale "....ila wanadiriki kumuua?! wameuchezea moto,moto usiozimika!



    umesema ufunguo upo chumbani kwa MERY naomba nielekeze mahali ilipo nyumba ile nianze kazi mara moja wewe utabaki hapa kwa ulinzi wako chakula utaletewa humu humu...bado unasakwa sana."



    alimalizia JOHN CHAKA kutoa maelezo...



    "mimi nitakuwa chumba kinachofuata!"



    "nop JOHN kwa nini tusilale chumba kimoja?" niliongea huku nikikaa kiasara hasara.chaka akanikata jicho kali



    "jiheshimu wewe mwanamke"



    akanyanyuka na kutoka, penzi lake liliushambulia moyo wangu! nilihisi kuonewa mawazo kichwani juu ya kijana yule ayakunitoka.



    **************



    makachero wa jeshi la polisi walishuka katika gari lao na kuuendea geti lililolindwa na walinzi wenye mitutu kutoka kampuni kubwa ya ulinzi barani africa,



    makachero wale walokuwa na vitambulisho vya umoja wa mataifa walipata ukinzani getini! ila baada ya walinzi wale kuongea na bosi wao MERRY aliwaruhusu kuingia.



    waliingia mpaka chumbani ambapo waliangalia kwenye makabati wakijidai kutafuta fedha haramu.



    katu MERY akumtilia shaka kijana alokuwa karibu na mto akauingiza kwa siri mkono wake katika mto ule na kuibuka na funguo...



    baada ya kukosa fedha zile wakaondoka wakitupiwa maneno machafu na dada yule.



    katu hakujua juu ya lengo la wanausalama wale....



    KACHERO PHILIP,aliingia katika kituo cha kati cha polisi...hakukaa sana countar baada ya kusaini akaingia katika landrova ya polisi na wenzake kuingia mtaani!...



    wakati akiwa ndani ya gari lao ghafla simu yake ikaita akapokea huku akiwa anatabasamu



    "yap JOHN CHAKA kila kitu nimefanikiwa nipo kitaa ntakushtua tukitoka site"



    kachero PHILIPO alizungumza...



    **********



    wakati kachero PHILIPO akizungumza na simu ile garini kulikuwa na kijana alokuwa akimchunguza pasina yeye kugundua.



    akaishika simu yake na kutuma msg



    "ni JOHN CHAKA BOSI..."



    akaifoward katika namba aloijua yeye.baada ya dakika chache msg ikaingia



    "akikisha unamfata na kumtia nguvuni kabla ajafika kwa huyo CHAKA"

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "sawa mkuu" afande yule aka ireply....





    ILIVYOKUWA....



    Kitu ambacho mtetezi wa kinte JOHN CHAKA akukijua ni juu ya mtandao wa vigogo wa kituo kile uloenda mpaka katika vituo mbalimbali vya polisi...



    baada ya chaka kupewa maelezo na JANETH juu ya ufunguo wa posta alitoka akaenda kuonana na rafiki yake KACHERO inspekta PHILIPO akamwelezea azma yake juu ya kuuhitaji ufunguo katika ngome ya madam MERY



    kachero philipo alipotaka kumpa kibali cha kupekua jengo lile,machale ya komandoo chaka yakacheza,akaisi kubainika haraka akapeleka wazo lake kwa kachero yule,..



    "usijali kumredi mi ntachukua maafande tutaenda kwa kisingizio cha kusachi noti bandia ntafanya ujanja kuchukua funguo huo katika mto usijali"



    kachero yule akachukua maafande kituoni bila kutambua kuwa wote siyo wema.



    ***********



    DUNGA MAJURA alokuwa na cheo cha koplo alikuwa ni kibaraka wa kituo kile kwa siri sana,



    alishangazwa na msako wa fedha haramu,kwa akili zake dunga alitambua kuna siri ilokuwa nyuma ya kapeti kwa kuwa alikuwa mmoja wapo wa ma afande walochukuliwa na inspekta philipo alishangazwa na wakati wenzao wakikagua katika makabati yeye alikaa katika kitanda kile.



    ndipo kwa siri akaanza kuzichunguza nyendo za mkubwa wake yule bila mafanikio.



    PHILIP aliuchukua ufunguo katika mto ule kwa siri sana bila kubainika na wale maafande alokuwa nao.



    ndipo walipoamua kuondoka.



    DUNGA alikuja kushtuka pale PHILIP alipopigiwa simu na kulitaja jina la CHAKA.



    naye bila kuchelewa akamtumia msg mheshimiwa waziri ambaye alimpa kazi ya kumwangamiza philip kabla ajaingia mikononi mwa chaka.



    dunga akakubali



    ********



    baada ya mwendo mrefu wakiwa bado maafande wale wakiwa mtaani kwenye doria inspekta PHILIP akaomba udhuru na kushuka,



    gari ikaendelea na mwendo mbele nako Dunga Naye akashuka....



    na kuelekea alipopaswa kuelekea ilikuwa ni kitendo cha dakika chache tayari koplo DUNGA alikuwa kabadilika alikuwa katika nguo nyeusi na maski nyeusi usoni akiwa katika gari ya wizara ya waziri mkuu tawala na tamisemi alishushwa hatua chache kidogo kutoka alipo INSPECTA filipo kwa hatua ndefu akapiga kujongea eneo alilopo inspekta philipo!



    katu akujali macho ya watu walokuwa wakimwangalia! philipo akakata kushoto palipokuwa na uchochoro!



    baada ya inspekta yule kukata kona dunga akakimbia alipofikia karibu na kichochoro kile akaanza kutembea!



    kitendo cha kuingia katika uchochoro ule akapokelewa na teke la kushtukiza lililompeleka chini!



    alikuwa ni inspekta philipo baada ya kuona akifatwa na mtu yule alofichwa sura yake akakata ile kona makusudi kwa lengo la kum "taget" mfatiliaji wake...



    ndo akampokea kwa teke lile.lililomwangusha.dunga kwa haraka alijinyanyua na kumvaa inspekta philipo kwa konde kali ambalo philipo aliliona na kujikunja kidogo kunde lile likapiga hewa,



    dunga akakosa mhimili na kupepesuka kitendo kilichopelekea philipo arushe ngumi ilompata dunga katika paji la uso na kumdondosha kabisa.



    dunga akaachia yowe la maumivu! inspekta akamfata koplo yule kwa speed akiwa na lengo la kumvua maski ile kitendo cha kuinama na kutaka kupeleka mkono wake kichwan kwa kasi ya ajabu mkono ule ulidakwa na kuviringishwa mpaka ukalia kaaaah!



    dunga akautumia kama mhimili wa kusimamia akimsindikiza na kipepsi cha goti maeneo ya sehemu za siri philipo akatoa mguno wa maumivu lakin tayar dunga alikuwa hewani akimjia kwa lengo la kumcharaza mateke...



    sekunde chache zilizobakia philipo alizitumia vizuri kumkwepa dunga akaja kupambana na ardhi...



    philipo akamuwah pale chini kwa kumpa ngumi zisizoesabika dunga akaanza kutema damu.



    kwa mara nyingine tena akaunyanyua mkono wake juu na kumvua lile alilovaa kichwani...



    hakika INSPEKTA philipo alistaajabu baada ya kumuona ni rafiki yake kipenzi akabaki kapigwa na butwaa



    "KOPLO ni wewe?"



    akamuoji akikumbuka dakika chache alimwacha kwenye gari...



    wakati akiwa bado katika bumbuwazi lile ghafla alipata msukumo asioutarajia ukiambatana na maumivu makali mbavuni koplo tayari alishanyanyuka na kumchoma kisu kidogo mbavuni,lilikuwa ni tendo la haraka.inspekta akabaki kashika jeraha lile akadondoka!!! Chini na kutulia



    Koplo yule msaliti akaachia cheko kwa haraka akampiga sachi Philipo na kutoka na ufunguo







    Nuru machoni ikaanza kutoweka!,kwa mbali akamuona hadui yake akimwangalia kwa jicho la jeuri,akitoa cheko la ushindi...



    giza likaanza kutawala machoni mwake! akajaribu kuunyanyua mkono wake ashike eneo la jeraha akashindwa!



    ghafla maumivu yakatawala! maumivu ambayo akuwahi kuyapata kabla akiona maruerue! miguu akawa anajaribu kuinyanyua akashindwa



    Akabaki "anatapapata" ghafla akatulia tuli!



    huo ndo ukawa mwisho wa inspekta PHILIP



    KOPLO DUNGA akatoa simu yake na kutafuta namba za mheshimiwa waziri akazipiga



    "ndiyo mh yule mtu tayari ayupo duniani"



    "good kijana! msachi chukua simu tafuta namba wasiliana na aliyekuwa anaitaji kuonana naye ,naye atoweke duniani! acount yako naiwezesha,ukiitaji msaada wa vijana toa taharifa mapema"



    "yah mh"

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    akaitikia koplo yule akipeleka mkono wake mfukoni mwa maiti ile akaibuka na simu! katu akuangaika na funguo kwa kutojua umuhimu wake kwa kuwa namba za JOHN CHAKA zilikuwa mwanzo akabonyeza kitufe cha kupigia na kusikiliza.



    simu ikaita mpaka ikakata, akapiga mara ya pili....ikaita kabla ya kupokelewa



    *****************



    Siku zote mwanaume huwa dhaifu kwa mwanamke,japo JOHN CHAKA alijitahidi kuzizuhia hisia zake kwangu,alishindwa na mitego nilomtega bila kuelewa akazama katika penzi langu!



    bila kujua najichoma msumari wa moto katika moyo wangu nikazama katika penzi lake.tukawa wapenzi!



    siku hiyo tukiwa pamoja kitandani ghafla simu yake ikaita,akachelea kuipokea kutokana na kunogewa vile nilivyompa! simu ikaita mpaka ikakata,iliporudia mara ya pili kuita akanyoosha mkono wake akaichukua simu na kuangalia mpigaji akatabasamu kabla ajaipokea



    "vipi comredy mmemaliza kupiga doria mitaa yote ya jiji?"



    baada ya chaka kuongea maneno yale ghafla akatoa macho ya mshangao kutokana na kile alichosikia...



    akajinyanyua kabla sijamdaka mkono



    "mpz unaenda wapi na unaniachaje hivi?!"



    niliongea kwa hisia nkimwangalia mwanaume yule kwa huruma, akujibu kitu akachukua suruali yake akaivaa,shati akalivaa na kutoka.

    silaha aliiweka kibindon

    kwa mwendo wa harak kuelekea kule

    Alikoelekezwa na mwelekezaji alotumia simu ya swaiba wake....



    JOHN CHAKA alitoka kwa kutojielewa,akiwa kachanganyikiwa,



    "njoo kichochoro cha mtaa wa kati kuchukua mzoga wa comredy wako!"



    akakumbuka sauti ya kukera aloambiwa na mpigaji simu,kule gest alimwacha JANETH katika bumbuwazi lililoubumbua ubongo wake,hali ya sintofahamu ikiyaandama mawazo yake.



    JOHN CHAKA alihtaji kufika haraka kabla wanausalama awajafika pale alipoitajika kufika!



    katu akujua uwepo wa koplo dunga mwenye uwezo katika kombi ya mapigano



    Chaka alifika eneo la tukio ambalo akupata tabu kuupata ufunguo ulokuwa pembeni ya mwili ule! watu waliuzingira ule mwili kwa mbali vingora vya gari la polisi vikisikika,



    chaka akutaka kuendelea kubaki pale akapiga hatua ndefu kuondoka maeneo yale katu akumtilia shaka kijana alokuwa akimfata nyuma yake kwa hatua fupi fupi,



    koplo DUNGA aliongeza mwendo kusudi kumkabili kijana yule,



    chaka akainama ishara ya kufunga viatu kamba kabla ajashtukia risasi ikichimba pembeni yake,



    Ikimkosakosa,chaka hakaruka kukwepa risasi zile...koplo dunga alikosa umakini kwa kupiga risasi hovyo chaka alizidi kumfata kwa stayle ya "shiraz" yani akikimbia bila uelekeo mahalumu akikimbia kwa kukata kata kona kabla ajaruka teke kuupiga mkono wa dunga risasi ikaruka mita kadhaa toka kijana yule alipo



    "bustard man"



    koplo akatukana sasa wote wakawa wanaangaliana! wamekaa mkao wa kimapigano dunga akakunja mkono na kuunda ngumi ambapo aliirusha kuelekea usoni,



    chaka akaiona wakati inakuja na kujikunja kidogo chini ngumi ile ikapiga hewani



    dunga akapepesuka,mpepesuko ambao chaka aliuwah kwa konde zito maeneo ya kwapani ambalo lilimfanya kijana yule akatoa kilio cha uchungu!



    bila shaka ni kutokana na mvunjiko wa mifupa chini kidogo ya kwapa,chaka akaachia tabasamu nukta hiyo hiyo akiruka teke aina ya samasoti lililotua kitovuni,ikamlazimu koplo yule ainame kwa maumivu makali ya tumbo aliyoyapata chaka akamfikia akiwa mkono wake kaunyoosha vidole kavikunja akaachia pigo lingine....



    Pigo alilolielekezea shingoni kwa kutumia ubapa wa mkono wake,pigo lile likampeleka Dunga mpaka chini,macho akayatoa







    Komandoo chaka akamfikia akiwa mkono wake kaunyoosha vidole kavikunja,akaachia pigo lingine



    Ilikuwa ni ngumi ya mbavuni,katika sehemu nyeti katika mwili ule



    Koplo akaachia yowe



    Chaka akakunjua vidole vyake na kuachia pigo lingine...



    Pigo alilolielekeza shingoni kwa kutumia ubapa wa mkono wake



    Pigo ilo likampeleka koplo Dunga mpaka chini!,macho akayatoa,CHAKA akutaka kumuoji maswali kutokana na watu kuanza kujaa kushughudia pambano lile akaanza kuondoka akiacha nderemo na vifijo kwa watu waliokuwa wakifurahia mapigano yale



    ,dunga akajinyanyua huku akichechemea na kutokwa na miguno hafifu ya maumivu akaiendea risasi yake na kuiokota,kichwani aliwaza....



    "wabongo bhana,pamoja na sare za jeshi la polisi nilizovaa,badala hata wapige simu kituoni wenyewe wanashangilia heti mi kupigwa dah duniani kuna mambo...."



    Kitendo cha JOHN CHAKA kuingia ndani mule alinikuta bado nimejilaza na kaupande cha khanga nilijinyanyua pale kitandani na kwenda kumkumbatia nikimpiga vibusu viwili katika papi za mdomo wake!

    nikamfungua vifungo vya shati alilovaa...



    akabaki kifua wazi,hakika niliona fahari kukipapasa kifua chake kilichotuna na kujengeka kimazoezi!



    kilichopendezeshwa na garden love fupifupi nikazipapasa taratibu huku nikimwangalia kwa macho yangu malegevu yaloitaji kitu...



    "nimefanikiwa kupata ufunguo wa posta japo haikuwa kazi nyepesi imegharimu maisha ya mtu na bado nawindwa!"



    CHAKA aliongea kwa sauti ya upole,sauti ya kuzidiwa na muamko wa kimahaba!



    "what?!"



    nilihamanika,nikikiacha kile kifua nilichoona raha kukipapasa.



    nikajinyanyua ila CHAKA alin daka mkono akanivuta nkadondokea kifuani mwake tukabaki tukiangangaliana kwa mita chache!



    macho yake yakiongea akatasua mdomo wake kutaka kusema kitu ila nikauhai mdomo wake na kuukutanisha na wangu tukazama katika tendo lile kabla atujadondokea kitandani!..."



    "COMMON JANETH! VITU VINGINE SI LAZIMA UNI ELEZEE UNA BOA ATI... "



    Nikamkatisha stori yake na kuangalia ukutani nikiivuta shuka langu kujifunika



    "zuberi.."



    janeth akaniita ila sikumuitika,



    "wacha wivu mpz wangu mi ni wako geuka bhana nkuendelezee"



    "siitaji naitaji kulala!"



    nilihitimisha na JANETH akaamua kuniachia....



    tukalala



    kila mtu akiangalia kivyake,nikiwa sina hamu tena ya kusikiliza stori ile iloshinikiza kupatwa na wivu mkali ulochomoza katika moyo wangu!



    "chaka yupo wapi kwa sasa?"

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nikamuoji naye JANETH akanijibu...



    "umekataa nikusimulie zuber inatosha..."



    "khaaaa!"



    nikaguna na kutulia!,mawazo kichwani yalinisonda kumbe huyu mwanamke anampenzi wake komandoo kwa nini sasa aingie katika mapenzi na mimi?.



    niliwaza kifala



    Kabla usingizi mnene ujanpitia...sikujua kilichoendelea juu ya kisa kile ambacho bado kiliniacha katika utata.



    SURA YA NNE



    JANETH alikaa katika ofisi yake nadhifu macho yakiwa katika laptop yake,akijaribu kupitia vifungu vya sheria kusudi amtie PATRICK hatiani hiyo ndiyo ilikuwa kiu yake kubwa akashika simu yake na kubonyeza vitufe kadhaa upande wa pili ukapokea



    "sady salim double s nakuitaji ofisini"



    akakata simu,na kungojea baada ya dakika chache kijana mrefu shombeshombe akaingia ndani JANETH akamwangalia kwa tabasamu pana



    "double s nnakazi naitaji ripoti baada ya masaa 24 mchunguze kijana PATRICK nyendo zake akikisha mpaka unapata makabrasha yenye ushahidi wa picha wa kumwingiza hatiani,"



    aliongea JANETH...double s akakubali moyoni mwake akiwa na faraja kwa kupata tenda ile ambayo alijua angeingiza kitita cha maana



    SADY SALIM au DOUBLE S alikuwa ni wakili mpelelezi aliyepitia jeshi kabla ajawa wakili katika campuny ya janeth alivumilia mafunzo muda wote jeshini,akaiva,siku ya kuitimisha yeye na wenzake watano waliitwa pasina kuambiwa makosa yao zaidi ya kuambiwa ni ukiukwaji wa sheria za jeshi akafukuzwa.



    uchungu alokuwa nao sitoweza kuueleza kwa maandishi! angetegemea angerudi nyumbani kama mwanajeshi ila alirudi kwa masikitiko,



    ndugu wakamtenga,kitendo kilichofanya aingie uraiani kufanya kazi za sulubu kazi ngumu akajisomesha uakili,ni kijana aloaminiwa na kupendwa sana na JANETH,ni kijana ambaye janeth alimtumia kuchunguza ushahidi kwa kesi mbalimbali zilizoitaji nguvu



    double s alifanikisha na kuipa sifa compuny ile ya uwakili.



    Ila kesi hii ilikuwa tofauti na kesi zote walizopitia kesi hii ilikuwa ngumu

    PATRICK alikuwa kiumbe mwingine,tofauti na walivyomtegemea





    ****



    JANETH alikaa katika ofisi yake nadhifu macho yakiwa katika laptop yake,akijaribu kupitia vifungu vwa sheria kusudi amtie PATRICK hatiani



    hiyo ndiyo ilikuwa kiu yake kubwa akashika simu yake na kubonyeza vitufe kadhaa upande wa pili ukapokea



    "sady salim double s nakuitaji ofisini"

    akakata simu,na kungojea lazima shone atambue kila kitu...



    na lazima zuber ajue kuwa shone yupo hai japo sijui atachukua maamuzi gani kati yangu na ya yule binti.....



    janeth aliongea kwa mawazo!



    "nenda na picha ya zuber mwoneshe usimfiche kitu ila kwa pale ofisin kwake si pazuri muitaji eneo faragha."



    "najua kazi madam"



    SADY alitamka akijinyanyua akaingia ndani ya gari yake



    alisimama mita kadhaa toka ilipo PATRICK CONSTRACTION kampuni kubwa ya ujenzi akashuka katika gari yake ile na kuliendea duka lililopo pembeni ya pale...



    akaagiza soda na kunywa taratibu huku macho yake yakiangalia eneo la compuny ile!



    "hivi mmiliki wa kampuni hile anaishi wapi?"



    akampachika swali dada mwenye duka lile



    "mtaa wa pili tu toka hapa!"



    dada yule alijibu kwa tabasamu!



    "dah hivi mke wake si ndo katibu muhtasar huku?"



    "dah kaka unamaswali mengi mi Sijui bwana..."



    sady akagwaya...



    akamalizia soda yake na kurudisha chupa akajongea taratibu katika jengo lile,



    katu akuwatilia mashaka vijana wawili walokuwa wamekaa mita kadhaa kutoka eneo lile kwa mpiga picha

    paspoti ambao macho yao na masikio yao yalikuwa kwake.



    kitendo cha kijana yule kuingia ndani ya ofisi ile vijana wale walijinyanyua wakapeana ishara na dada yule wa dukani wote walikuwa ni watu wa patrick waloizunguka kampuni ile kwa uchunguzi maalum double s kaingia kichwakichwa.



    wakaifata gari ile ya sady wakatoa funguo zao malaya wakafungua mlango wakajitoma ndani na kukaa siti za nyuma wakimsubiri kwa hamu kijana yule...



    DOUBLE S,sady akaingia ndani ya jengo lile ambalo alipokelewa na binti mrembo SHONAIZAR!



    ambaye macho yake yalikuwa bize katika luptop yake



    PATRICK muda huo alikuwa ndani ya ofisi yake ilozungukwa na camera zilizounganishwa na dstv nje ya jengo lile na ndani ya jengo lile



    yule mtu alikuwa makin naye sana toka alipoingia tayari msichana aliyempachika nje alishampigia simu kumtaharifu kuwa makini naye! akawa bize kufatilia maongezi yao



    "wewe ndo mrs PATRICK?"



    SADY alianza kwa kuoji,shone akamtupia jicho la mshangao!,akaachia tabasamu,akatingisha kichwa ishara ya kukubali

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "ok nilikuwa nakuitaji kwa maongezi sehemu yenye utulivu kuna vitu uvijui naitaji nkueleze"



    SADY kwa sauti ya upole aliongea...



    PATRICK kule ofisini kwake akashtuka,akaikwapua simu yake akapiga namba kadhaa



    "mnafanya nin mpaka mtu anaingia ofisini kwangu na kutaka kuaribu mipango yangu?"



    PATRICK aliuliza kwa ukali



    "basaaat bosi!..tupo ndani ya gari yake,tunamsubiri hana maisha huyo bosi"



    mmoja kati ya wale vijana waloingia ndani ya gari ya SADY aliongea



    "kabla amjamwangamiza mumtese aseme nani alomtuma kuna hisia ambazo sitaki niziamini zinanambia kuna mzoga unaishi?"



    "mzoga? upi bosi?" xy alioji



    "zuberi!"



    "bashaaat bosi...sitaki kuamini ilo!"



    "ok bashaat! ngoja nimuwah kumtoa kabla ajamwaga unga kwa malkia wangu mpelekeni shambani nikija nikikute kichwa chake akatwe kiungo kimoja kimoja mpaka aeleze aliyemtuma sawa?"



    "bashaaat bosi"



    "kwenda huko."



    PATRICK alimkejeli akakata simu na kujinyanyua akausogelea mlango na kushika kitasa.



    UPANDE WA PILI



    Shone akamwangalia sady kwa tuo,cheko likamkaba



    "ok mimi ni mke wa mtu hivyo sina muda wa kwenda kukaa mahali kupiga stori na nsiyemjua sady akatabasamu,tabu la kejeli kisha akaufungua mdomo wake mengi sana uyajui dada plz naomba muda wako ulipoteza kumbukumbu....



    kabla ajaendelea ghafla mlango wa ofisi ya bosi ikafunguliwa wote wakaiangalia kwa mashaka,



    patrick akatoka, uso wake ukiwa umejaa ghadhabu na hasira tosha!!...



    "nakuitaji ofisini haraka sana na yale ma file ya makandarasi..."



    patrick akaongea kwa ukali huku jicho likiwa kwa sady!



    jicho ambalo sady alilitambua si jicho jema, shone akanyanyuka kwa unyonge na kumfata mumewe ofisini,



    muda huo huo kengele ya hatari ikagonga katika kichwa chake...



    hakutaka tena kukaa hapo akajinyanyua na kulifata gari lake kwa mwendo wa speed akajipakia ghafla akashtushwa na kuguswa na kitu nyuma ya kisogo!,



    akupata tabu kujua ni mdomo wa bastola...



    macho akayapepesa pembeni katika said mirrow kabla ya kuwaona vizuri wale jamaa, mmoja aliyemnyooshea bastola alikuwa kwenye tabasamu pana,



    mdomoni akiwa na pande la sigara

    akukumbuka kama alishaiona katika nchi hii



    "bashaaaat tulia hivyo hivyo ufate maelekezo yetu"



    kijana aloshika pisto alitamka,uso ulikosa mzaha, tabasamu liliyeyuka.

    huyo ndo bashaat mpole kwa asiyoko ndani ya kazi mkali mwenye roho mbaya kwa aliyoko ndani ya kazi



    huyu ndiye aliyetoa idhini janeth aachwe porini kule na kuwachukuwa wale wasaliti mpaka porini.



    kuwafanyia jimai na kuwaua



    basaaaat wakati kijana sady akiwaza cha kufanya kupona katika kisanga kile ghafla kitu kizito kikatua kisogoni



    kilikuwa ni kitako cha bunduki!



    sady akapoteza fahamu wakamvuta kiti cha nyuma wakamfunga kamba na kumtupia kiti cha nyuma.







    *



    wakati kijana sady akiwaza cha kufanya kupona katika kisanga kile ghafla kitu kizito kikatua kisogoni



    kilikuwa ni kitako cha bunduki!



    sady akapoteza fahamu wakamfunga kamba na kumtupia kiti cha nyuma



    bashaat akaingia katika kiti cha dereva na kulitoa gari kwa kasi...kuondoka maeneo yale.



    ***********



    "tatizo ni nini mume wangu, mbona mafile hayo nimeyajaza vizur?!"



    "nop shone! sitaki vijana wa kiuni humu ofisini yule bwege nilimuona tangu akiwa anaingia"



    "ooops!"



    shone akahema,



    "sawa nmekuelewa mme wangu"



    "sawa kaendelee na kazi!"



    SHONE akanyanyuka na kutoka,



    mawazo kichwani mwake juu ya yule mtu yakazaliwa!



    'ni nani? nilipoteza kumbukumbu? lini na wapi? na kwa nini? kipi ambacho sikikumbuki?,lazima nijue! lazima nimtafute yule kijana anidadavulie? na kwa nini PATRICK akasirike?,naitaji kujua!'



    akawaza shone macho yakiwa katika lap top yake,ila mawazo yalikuwa mbali,katu akujua yule alotaka kumfumbua maisha yake yalikuwa

    hatarini!...

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    na hata shoni alipokuja kugundua ilo alikuwa kashachelewa



    Gari ilombeba double s ilifika ilipokusudiwa kupelekwa! katika mashamba makubwa ya katani huko kusikojulikana!



    mwili wa sady ukatolewa ukafungwa katika kiti! xy kijana akakabidhiwa panga penye makali! akaanza kumcharanga! huku basaaaaaat akimmwagia pilipili zilizochanganywa na chumvi!



    maumivu yakaambaa katika mwili wake...



    akazinduka



    akazinduka katika maumivu makali!,



    mbele yake walikwepo vijana wale katili wasiyo na huruma hata chembe...



    wakaanza kumsaili maswali! sady alipokaidi kujibu alicharangwa mapanga huku pilipili ile ikimwagiwa mwilini!



    akatoa siri zote!



    juu ya binti janeth!



    vya kurekodiwa vikarekodiwa,patrick aje aoneshwe...kwa kuwa akija aliitaji akute kichwa.



    ndivyo ilivyokuwa....



    sady akachinjwa kichwa chake,



    uhai ukauwacha mwili!



    akatumbukizwa mpaka katika pipa la kemikali!



    hata mfupa wake aukuonekana



    hiyo yote ni kupoteza ushaidi!



    patrick akapigiwa simu kuelezwa,dakika chache badaye alikuwa katika shamba lake lile akiwa kakishika kile kichwa...



    akaenda kukitumbukiza katika pipa lile lile,ishara ya kuzika uhai wa sady salim



    double s!



    huo ndo ukawa mwisho wake.



    "siitaji maiti hapa ila naitaji nione katika vyombo vya habari juu ya kifo cha huyo binti! siitaji kujua kwa nini ananifatilia.leo hii hi janeth awe maiti"



    "basaaaaaaaat!"



    "poteeni"



    vijana wale wakaingia katika gari tayari kuelekea ofisini kwa janeth,



    kusababisha mauaji yake....



    UPANDE WA PILI



    Upweke ulimuandama kijana ZUBER baada ya kukaa pasina kazi,kuchoka kuangalia tv n.k kwa mara ya kwanza akajiingiza katika maktaba ya JANETH kwa ajili ya kujisomea somea,



    Katu akujua juu ya watu ambao walikuwa njiani kuja huko kwa mauaji,akakaa na kuvuta kitabu kimoja kikubwa ni kitabu kilichomvutia,kitabu cheusi kilichonakshiwa maneno (my diary) ubavuni huku mbele ya kitabu kile kili printiwa maneno STORY YA KWELI YA MAISHA YANGU



    picha ya JANETH ikiwa nje ya kava ya kitabu kile..kitabu kile kikamvutia ZUBER kukifungua,ilikuwa ni ile ile stori ambayo Janeth alimsimulia



    Akafungua page zile haraka haraka na kuendelea kusoma kisa kile kwa utulivu!..



    "penzi langu na CHAKA likazidi kukomaa siku hadi siku!,nikiwa bado nipo mafichoni!,chaka alinifanya nijihisi uhuru zaidi...



    nikisema mafichoni simaanishi nilikuwa mtu wa ndani tu!! nop la hasha...



    nakumbuka vizuri siku hiyo tukiwa tumeelekea club nikavua jaketi langu la maradona na kuzama ndani ya clab chaka akiwa kanishika mkono! katu sikuwatilia shaka au pengine sikuwaona vijana wale wawili wenye makoti ya laizar walokaa countar...



    vijana wa kigogo waziri mkuu walikuwa na head forn katika maskio yeo asusa yetu ipo mawindoni mkuu any time twaja nayo!"



    "ok mpelekeni gofu death katutesa sana!"



    upande wa pili ukajibu.,wenye laizar wakawa makini kufatilia nyendo zangu!



    "beby ngoja niende toilet!"



    "ok beby usichelewe!"



    chaka akaniaga! akwenda toilet kumbe ni mtego alitega!



    ukanasa



    KIZAAZAA



    mwenye koti la laizar akanifata,akaitaji kucheza nami! kitendo cha kumuona tu nikamkumbuka akanishika kwa nguvu na kunivutia kwake! nkaiona kwa uwazi bastola!



    "chakufanya taratibu tunatoka bila kuwabughudi watu unafatana na mimi!"



    sikuwa na jinsi nikajitoa!,na kumfata akiwa kanishika kiuno kama mpz wake! usoni akiwa na tabasamu pana.



    mpaka nje,chaka kwa uangalifu pasina mimi kujua kumbe alikuwa yu anatufata nyuma!....



    tukafika nje wakanielekezea katika gari yao! yenye vioo vya tinted aliyoko nje amwoni wa ndani ila wa ndani anamwona wa nje wakaliondoa gari kwa speed



    JOHN CHAKA naye akajipakia ndani ya gari na kulifata gari lile kwa usiri mkubwa.



    ilo alifanikiwa



    sisi wa mbele atukujua kama tunafatiliwa...



    mpaka tulipoanza kutoka katikati ya mji ndipo dereva alipolitilia shaka gari lile ambapo kila alipokata lilikuwa nyuma.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    baada ya kubainika wakapitisha uamuzi wamjulishe mkuu! mkuu akawaidi kuongeza watu lakini walishachelewa.



    chaka akaanza kurusha risasi...



    yule mmoja akajibu, milio ya risasi ikarindima maeneo yale..kabla chaka ajapiga taili gari ikakosa muimili na kwenda kugonga mti!.





    *******************





    Kitendo kilichofanya wale wenye makoti ya laizar kujirusha toka katika magari,risasi zao zikicheua!,



    CHAKA naye alijirusha toka katika pikipiki yake akatua chini!



    akiacha pikipiki ikienda kivyake! naye akatua kivyake!, akaanza kukimbia kwa mtindo wa zig zag kuelekea upande wa maadui!



    kimuyemuye kikazuka!,kizaazaa kikashamiri,rusha nkurushie ikatawala maeneo yale,kila mtu akionesha uwezo wake wa kurusha na kukwepa silaha,



    mtindo wa zig zag ukimsaidia CHAKA kuwafikia maadui waloponzwa na ghadhabu zilizowapanda



    mita kadhaa kabla chaka ajawafikia akajirusha kumvaa kijana mmoja wakaserereka kwa haraka



    CHAKA akajinyanyua na kurusha teke kali lililompata kijana yule wa pili!



    bastola ikamponyoka! ,kijana yule wa pili,



    chaka kwa wepesi wa ajabu akajigeuza tena kwa kasi na kumcharaza teke yule jamaa wa kwanza alomvaa na kwenda naye chini hapo awali,



    kama mwenzake silaha naye ikamponyoka na kudondokea pembeni ya miguu ya chaka!



    chaka akuinama kuiokota akaigusa kwa miguu kama anataka kucheza nayo danadana akaidaka



    tayari mkononi kwa chaka kulikuwa na silaha tatu akazisweka kibindoni! wale watu walikuwa bado chini wakiugulia maumivu!



    "nani kawatuma mumteke huyu binti?"



    CHAKA alimuoji mmoja kabla ajajibu akamzawadia konde zito usoni...



    jamaa akatema jino!,



    jamaa likatoa cheko la dharau,cheko lililomuudhi chaka!,akamzawadia tena konde lingine,



    akajiandaa kumgeukia yule mwenzake kabla ajashtushwa na mlio wa gari za polisi!



    chaka hakuwa na budi kuondoka na kuwaacha hapo!...



    wakati wote janeth alikuwa ndani ya gari ile akitetemeka! chaka akamfata na kumfungulia mlango akampa amri atoke!



    akaifata pikipiki yake akainyanyua janeth akapanda nyuma.chaka akaiondoa kwa spidi...



    akiwaacha watuhumiwa wake wakibwabwaja matusi.



    Walifika salama hotelini japo walikuwa wamechoka wakiwa wameshikana mkono kuingia katika hoteli walofikia..janeth alikuwa bado anaongea na muhudumu



    chaka akatangulia chumbani, akatoa ufunguo na kufungua mlango ile anaingia AKAPOKEWA NA TEKE.lililompeleka chini.ninja 3 wakiwa

    Na upanga katika mikono yao walikuwa Mbele yake



    Kwa Mara nyingine tena maisha ya Chaka yalikuwa hatarini



    Ni vipi waliingia humo ndani akuwa na muda wa kuwaza hayo! wale ninja waloshika upanga walikuwa wamemzingira!...



    wakimwangalia kwa ghadhabu! mmoja hapo akaunyanyua upanga wake ile anaushusha CHAKA akajibinua sarakasi na kumpushi ninja mmoja akatoka katikati yao!



    ninja wale wakamfata kwa speed wakiachia mayowe! kwa wepesi wa ajabu JOHN CHAKA akakinyanyua kitanda na kuwatupia kishindo kikasikika!



    wakajinyanyua na kuangaza chaka akuonekana ghafla akatua katika mabega ya ninja mmoja!



    kumbe alikuwa juu ya paa la nyumba! kijendo cha kutua yule ninja akaenda chini chaka akajizungusha na kuachia mateke mawili ya double wale viumbe vyote vikaenda chini!...



    ila avikukubali kubaki pale vikajinyanyua na kujipanga upya vikamfata chaka alowakwepa wakajigonga wenyewe kwa wenyewe na kusambaratika chini! Kwa Mara nyingine....



    ghafla wakaangaliana na bastola ya chaka ilikuwa ni hatari kwao bastola ikacheua! kabla risasi zile azijawafikia tayari walishatoweka!!



    JANETH alipoingia alikuta chumba shaghala baghala.akujua kilichoendelea



    JAMHURI YA MUUNGANO KINTE

    KITUO KIKUU CHA POLISI



    Ni mara ya tatu sasa muungurumo wa simu ile iliendelea kuunguruma pasina kupokelewa! katika ofisi ya mkuu wa kituo kile...



    mkuu wa kituo kile si kwamba akuisikia simu ile no la asha! ila alizidiwa na kipigo alichokuwa akikitoa,ni mdada alovaa kombati za kiaskari! mkononi akiwa na kirungu akikishusha kwa watuhumiwa walokuwa mbele yake...

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    moyo wake ulijawa na hasira...akaendelea kuwaadhibu mpaka alipotosheka akatoa amri warudishwe palipostahiki! akarudi kukaa katika kiti chake!,..



    ile simu sasa ilishaacha kuita naye akuangaika nayo! mwili wote ulimloa jasho...



    usiku ilimkuta chumbani kwake! ni dakika chache alikuwa ametoka bafuni kukoga,alikuwa akijikanda! hisia za mapenz zikimsumbua!



    ni mwaka wa tatu sasa mume wake akwepo tangia ameenda TANZANIA kwa kazi maalumu,



    akuwa tayari kumsaliti mume wake kwa kuwa alimpenda! kila mara alitumia maji na kitambaa kumaliza shida zake

    HUYU alikuwa ni katarina mke wa JOHN CHAKA!!!....





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog