Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

JULIANA - 4

 







    Simulizi : Juliana

    Sehemu Ya Nne (4)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Zoezi lao lilichukua miezi mitatu lakini hakukuwa na majibu yoyote yale. Kila mmoja alishangaa, walijitahidi sana, walikuwa vyakula vingi vya kuirutubisha afya zao na vizazi vyao lakini Juliana hakufanikiwa kushika ujauzito.

    Walipoona kila kitu kimeshindikana ndipo wakaamua kwenda hospitalini kuona kama kulikuwa na tatizo lolote lile.



    Walipofika huko, daktari akawapima na baadaye kuwapa matokeo ambayo yaliwashtua wote wawili.

    “Hamtoweza kupata mtoto,” alisema daktari huku akiwaangalia wote wawili.

    “Kwa nini?”

    “Mkeo ana kansa ya kizazi,” alijibu daktari huyo huku uso wake ukionyesha huzuni kubwa.



    Hawakuamini kile walichokisikia, walimwangalia daktari yule, mioyo yao ilichoma kupita kawaida. Juliana akahisi moyo wake ukichoma kuliko kawaida, akayafumba machoo yake na kuanza kulia.

    Hakuamini kwamba alikuwa na kansa ya kizazi, daktari akawaambia kwamba haikuwa imekomaa hivyo kulikuwa na nafasi ya kuiwahi kitu kilichowafanya kuanza kuhangaikia tiba.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walikwenda kila kona, Juliana alitumia dawa za kila aina lakini kitu cha ajabu ni kwamba hakufanikiwa kupona kansa ile ambayo ilikuwa ikiendelea kumtafuna kila siku.

    Ugonjwa ukampa mawazo, kila alipokuwa akikaa, mawazo yake yalikuwa katika ugonjwa huo uliokuwa ukimtesa kila siku. Moyo wake ulimuuma mno, hakukuwa na mtu wa kumfariji zaidi ya mume wake mpendwa.



    Gideon alihuzunika, kila alipomwangalia mke wake, moyo wake ulimuuma mno. Juliana alimsikitisha, alikuwa akikonda, mawazo yalimtesa na kila wakati aliona kabisa kwamba angekufariki dunia.

    Alimuonea huruma mume wake, alikuwa akihangaika mno, kila kulipokuwa na tetesi kwamba dawa ilikuwa ikipatikana, alikwenda huko. Alinunua dawa za kila aina, kwa Wachina, Wakolea na nyingine za asili ilimradi mke wake apone kansa ile lakini haikusaidia kitu.



    Alihuzunika, wakati mwingine alipokuwa ofisini, aliufunga mlango na kuanza kulia. Moyo wake ulichoma mno, wakati mwingine alimwambia Mungu kwamba lile jaribu alilompa lilikuwa kubwa mno na asingeweza kulibeba peke yake.

    “Mungu! Hili ni jaribu kubwa sana! Nitawezaje kulibeba?” alimuuliza Mungu huku akiwa ofisini kwake.



    Kila alipokuwa alimfikiria mke wake, Juliana. Aliona kabisa hizo ndizo zilikuwa dakika za mwisho kumuona mke wake huyo akiendelea kupumua. Hakuacha kuomba, alisali kwa nguvu zote, aliamini kwamba kuna siku Mungu angetenda muujiza na mke wake kurudi kwenye hali ya kawaida.



    “Mke wangu! Una imani kwamba utapona?” aliuliza Gideon huku akimwangalia mke wake.

    “Nina imani nitapona, ila….” Alisema Juliana.

    “Unaposema ila inaonyesha huna imani! Naomba uwe na imani mke wangu!



    Mungu wetu ni mponyaji, kama alimponya mwanamke mwenye baada ya kushika vazi la Yesu Kristo, kama aliwaponya vipovu, kansa ni nini mbele yake? Amini kwamba Mungu ni mponyaji, unachotakiwa ni kuamini kwani mungu hufanya kazi na wanaoamini,” alisema Gideon huku akimwangalia mke wake huyo.



    Japokuwa aliambiwa maneno mengi na mume wake kwamba alitakiwa kuamini lakini moyoni mwa Juliana hali ilikuwa tofauti kabisa. Kichwani mwake zikaja picha za watu mbalimbali waliokuwa wakiugua kansa na mwisho wa siku kufariki dunia, hakuona kama angepona, aliamini kwamba mumewe alikuwa akimwambia maneno mengi kama kumtia moyo lakini ukweli ni kwamba asingeweza kupna.



    Alilia mchana kutwa, moyo wake uliendelea kulia. Kila alipomwangalia mtoto wake, Jesca moyo wake ulimuuma, alikuwa mtoto mdogo ambaye bado alihitaji malezi kutoka kwake, hakujua angefanyaje kama angekufa, hakujua ni kwa jinsi gani mtoto wake huyo angeumia usiku na mchana.



    Miaka ikakatika, hali yake ikazidi kuwa mbaya, ugonjwa ule ulimtesa na mwisho wa siku kuanza kutafuna nywele zake. Zinaanza kunyonyoka, akaanza kubaki na upara kichwani. Alitia huruma, aliumia mno kwani hizo zote zilikuwa ni dalili kwamba asingeweza kupona tena.

    “Mke wangu! Amini kwamba Mungu anaweza kukuponya,” aliisikia sauti ya mumewe moyoni mwake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akahisi akipata nguvu kubwa, akaanza kuingiwa na kumbukumbu za watu waliokuwa wakiumwa sana na mwisho wa siku kuponywa. Kama Mungu aliiumba dunia, kama Mungu aliumba binadamu wote duniani, ilikuwaje kuhusu ugonjwa wa kansa, angeshindwa vipi kumponya mtu aliyekuwa na ugonjwa huo?



    “Mungu naomba uniponye,” alisema Juliana huku akiwa amepiga magoti.

    Alimuomba Mungu kila siku, alimuamini kwamba kuna siku angemponya tena lakini hilo lilionekana kuwa gumu kutokea. Mwili wake ulizidi kudhoofika, kansa iliendelea kusambaa na mbaya zaidi wakati mwingine alikuwa akitoka damu nyingi sehemu za siri kama mwanamke aliyeingia kwenye simu zake.



    Hilo ndilo lililomtesa zaidi, likamfanya kukaa ndani, akajifungia, hakutaka kutoka kwani muda wowote ule damu zilikuwa zikimtoka sehemu za siri. Huo ndiyo ulikuwa msiba mkubwa, aliomboleza kila siku, wakati hali ikiwa imekuwa hivyo, wakati ambao alikuwa akihitaji sana msaada na faraja kutoka kwa mume wake, hapo ndipo Gideon akaanza kubadilika.



    Hakuwa karibu naye kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma, alichelewa kurudi nyumbani kitu kilichomfanya kuwa na maswali mengi juu ya kitu kilichokuwa kikiendelea kwa mumewe.

    Alitamani sana kuzungumza naye lakini mwanaume huyo hakuwa na muda. Moyo wa Juliana ulimchoma, japokuwa alikuwa na maumivu makali katika mwili wake lakini kufanyiwa vitu kama hivyo na mwanaume aliyempenda kwa moyo wa dhati kwake ilikuwa ni zaidi ya maumivu.





    Alilia, hakuna aliyemfuta machozi, alihuzunika, hakukuwa na wa kumfariji. Wakati mwingine aliisikia sauti moyoni mwake ikimwambia kwamba aachane na mumewe kwa kuwa alikuwa amepata mwanamke mwingine lakini Juliana hakutaka kukubaliana na hilo.

    “Gideon! Hapana! Hawezi kuwa na mwanamke mwingine,” aliibishia sauti aliyokuwa akiisikia moyoni mwake.



    “Aya! Utakapoletewa mwanamke ndani ya nyumba ndipo utakapoamini kwamba amepata mwanamke mwingine, tena mzuri zaidi yako, na ana afya nzuri sio kama wewe goigoi ambaye muda wowote ule unakufa,” aliisikia sauti hiyo maneno ambayo yaliuchoma moyo wake vilivyo.



    Kansa iliendelea kumtesa Juliana, hakuwa na furaha, muda wote alikuwa akilia, alimuomba Mungu kumponya kansa ile au kubadilisha kila kitu na mwisho wa siku kugundua kwamba kila kilichoendelea kilikuwa ndoto.



    Alimpenda sana mume wake, Gideon lakini kwa kipindi hicho mwanaume huyo alikuwa bize na mambo yake, upendo uliondoka, akawa anachelewa kurudi nyumbani, hakutaka kabisa kuona akiendelea kuwa na mwanamke mgonjwa kama alivyokuwa Juliana.



    Moyo wa mwanamke huyo ulimuuma kupita kawaida. Bado aliendelea kutoka damu sehemu za siri, aliumia, alihitaji msaada kutoka kwa mume wake lakini mwanaume huyo hakuwa na muda naye.

    Wakati mwingine akawa anampigia simu, hakuwa akipokea na hata alipomtumia ujumbe kwenye simu yake mwanaume huyo hakuwa anajibu kitu kilichomfanya kujisikia vibaya mno.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakati Juliana akiteseka kitandani, Gideon alikuwa kwenye penzi la mwanamke mwingine aliyeitwa Juliet. Lilikuwa penzi jipya, penzi lililochipukia kwa kasi kubwa, penzi ambalo lilimfanya kuanza kumsahau mke wake.



    Alihitaji faraja, alihitaji kulala na mwanamke, mkewe hakuwa akiweza kufanya kitu chochote kile, alionekana kama sanamu hivyo kwa hali aliyokuwa akipitia ilikuwa ni lazima kutafuta mwanamke mpya ambaye angeufanya moyo wake kuwa na furaha muda wote.

    Akawa akitoka na Juliet kwenda sehemu mbalimbali, alikuwa na pesa, alitumia pesa zake kumfurahisha msichana huyo pasipo kumkumbuka mwanamke ambaye alichuma naye.



    Kila alipokuwa na Juliet, Juliana alikuwa akipiga simu, aliichukua simu yake na kuangalia, alipoona jina la mke wake, alicheka sana na kumuonyeshea Juliet ambaye alimwambia amsahau mwanamke huyo kwani hakuwa chochote kile.

    “Achana naye!” alisema Juliet.

    “Ndiyo ninachofanya. Unajua namchukia sana yule mwanamke,” alisema Gideon huku akionekana kuwa na hasira.

    “Jamani! Basi tukampoteze,” alishauri Juliet.



    “Tumpotezaje?”

    “Tumuue!”

    “Sawa. Ngoja nikafanye mipango, mwanamke yule hatakiwi kuishi. Kwanza pale alipokuwa tayari maiti,” alisema Gideon.



    Hakukumbuka chochote kuhusu mke wake, alimchukia, kila alichosema Juliet alimsapoti, hakukumbuka kwamba zamani hakuwa na pesa lakini msichana huyo alimpenda hivyohivyo, hakukumbuka kwamba utajiri aliokuwa nayo, chimbuko lake lilikuwa kwa wazazi wa mwanamke huyo huyo, hakukumbuka kitu chochote kile, kitu pekee alichokuwa na hamu nacho kwa wakati huo ni kumuua Juliana tu.



    Akarudi nyumbani huku akiwa na muonekano mwingine kabisa. Akamkuta Juliana akiwa sebuleni amekaa akimsubiri. Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake kila siku, hakukubali kulala na wakati mume wake hakuwa amerudi nyumbani.



    Ilikuwa ni lazima kukaa sebuleni mpaka mwanaume huyo atakaporudi nyumbani hapo. Alipokuwa akija, hakuzungumza naye, alimsalimia mwanaume huyo lakini alikuwa kimya, hata salamu hakutaka kabisa.

    Siku hiyo Gideon alipoingia, alionekana kuwa tofauti, alipoufungua mlango na kumwangalia mke wake, tabasamu pana likaonekana usoni mwake.



    Juliana akashangaa, hakuamini alichokuwa akikiona, hakuwahi kuliona tabasamu la mume wake tangu alipoanza kuugua, leo iweje mwanaume huyo atoe tabasamu pana kiasi hicho?



    Kwa tabu sana akasimama na kumfuata mume wake, alipomfikia, akamkumbatia, kwa furaha aliyokuwa nayo moyoni, Juliana akaanza kulia, hatimaye mume wake wa zamani, mume wake yule aliyekuwa kipindi cha nyuma alikuwa amerudi pasipo kugundua kwamba mwanaume huyo alikuwa na jambo lake moyoni mwake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Nimekukumbuka mke wangu,” alisema Gideon huku akimwangalia Juliana.

    “Nimekukumbuka pia,” alisema Juliana huku akilia kwa furaha.

    Wakaongea mengi kama wanandoa, wakaondoka na kuelekea chumbani.



    Kila kitu alichokuwa akikifanya, moyo wake ulimuuma mno, hakutaka kumshika mkono Juliana lakini kwa kuwa alitaka kumuua, ilikuwa ni lazima kufanya hivyo.

    Akamuacha chumbani na kumwambia kwamba aende jikoni kuchukua chakula na kula. Akaondoka na kuelekea huko ambapo kitu cha kwanza kabisa ni kuchukua simu na kumpigia Juliet.



    “Vipi? Umemuua?” alisikika Juliet kwenye simu.

    “Bado!”

    “Acha ujinga. Unasubiri nini sasa?” aliuliza msichana huyo.

    “Ndiyo naandaa mazingira!”

    “Au bado unampenda?”

    “Walaaa!”

    “Au bado unampenda?”

    “Walaaa!”

    “Au unataka kuendelea kuwa na maiti yako hiyo?”

    “Hapana mpenzi!”

    “Sasa kwa nini unachelewa? Hebu muue bwana nije niishi na wewe na kukuuonyeshea jinsi mapenzi yanavyotakiwa kuwa,” alisema msichana huyo.



    “Sawa laazizi! Nipe dakika kadhaa!”

    Simu hiyo ni kama ilimuhamasisha kufanya kile alichoambiwa. Akachukua chakula na kurudi chumbani, akatulia kwa muda, alitakiwa kufanya hilo haraka iwezekanavyo lakini hakujua ni kwa namna gani angeweza kumuua Juliana.



    “Ngoja nitoke naye! Nikifika huko, namuua na kurudi na maiti yake,” alisema Gideon na hivyo kumgeukia mke wake.

    Alichokifanya ni kumwambia mke wake kwamba alitaka kutoka naye kwenda sehemu fulani kwa ajili ya kupumzika, alikuwa na mazungumzo naye juu ya hali yake na aliamini kwamba endapo angezungumza naye basi furaha aliyokuwa nayo kipindi cha nyuma ingerejea tena.



    Kwa Juliana hakukuwa na tatizo, alifurahia sana kwani hakukuwa na mwanaume aliyekuwa akimpenda kama ilivyokuwa kwa mume wake, akakubaliana naye pasipo kujua lengo la mwanaume huyo lilikuwa ni kumuua.



    Wakatoka nje huku Juliana akijikongoza mpaka ndani ya gari, akakaa na kutulia tuli. Akili yake ilikuwa ikifikiria mbali kabisa, ukaribu ambao mumewe alimuonyeshea siku hiyo ulimkumbusha jinsi walivyokuwa katika kipindi cha uchumba.



    Kabla ya kwenda kwenye gari, alichokifanya Gideon ni kuchukua kisu na kukiweka kiunoni, alitaka kumuua na kumshikisha kisu kile kuonyesha kwamba mwanamke huyo alikuwa amejiua.

    “Kwa mpango huu! Hakuna atakayebisha kama amejiua,” aliwaza huku akiingia garini.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hakutaka kugundulika hivyo kila wakati uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana lililomfanya Juliana kuona kwamba mumewe alikuwa na furaha kubwa, hata chuki aliyokuwanayo moyoni haikuwa ikionekana usoni.



    Gideon akaliwasha gari na kuondoka mahali hapo. Njiani, Gideon ndiye alikuwa mzungumzaji sana, alimchangamsha mkewe kwa mameno mengi, alitaka kumuonyeshea kwamba kila kitu kilichokuwa kimetokea kipindi cha nyuma kilitokea kwa bahati mbaya lakini mapenzi yake yalikuwa kwa mke wake huyo.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog