Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

SINGIDANI - 4

 







    Simulizi : Singidani

    Sehemu Ya Nne (4)





    ILIONEKANA kama ni siku mpya kwao. Ilikuwa kama ndiyo kwanza wamekutana kwa mara ya kwanza katika mazingira waliyokuwa asubuhi hiyo.

    Kila mmoja alijitahidi kumfanya mwenzake aone hakukosea kuwa naye katika muunganiko huo. Walionyeshana kazi!CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Asubuhi hiyo upepo ulipuliza kwa kasi na kukifanya chumba kiwe baridi kabisa kama vile waliwasha kiyoyozi!

    Hawakuhitaji blangeti! Wenyewe walitosha kwa kila kitu. Wote wakamiminiana misifa, ahadi kibao zikawatoka vinywani mwao.

    Waliwaza ndoa tu!

    Walishinda siku nzima ndani ya chumba hicho. Jioni, Chris alilazimika kuondoka na kurudi Mkalama. Mazungumzo ya usiku huo yaliendelea kuwa yaleyale. Laura alitawala.

    “Mjukuu wangu, usiache kumuoa huyo msichana. Ni mzuri na anakufaa kwa maisha yako,” alisema bibi.

    “Usijali bibi, hilo nakuahidi. Halafu kesho ndiyo narudi Dar. Najua unataka kusema kitu... bibi kazi nyingi lazima niondoke ila nitakuacha vizuri,” akasema Chris akitoa bahasha ya khaki na kumkabidhi.

    “Ni laki moja bibi, tena nimezichenji kabisa. Zipo noti za elfu mbilimbili, najua hizi zitakusaidia mpaka siku nitakapokuja tena huku kijijini.”

    Bibi aliachia mdomo wazi kwa furaha. Alisimama kwa tabu na kumkumbatia mjukuu wake.

    “Mungu akubariki mume wangu, kwenye riziki zako kuongezeke,” akasema bibi.

    “Ahsante sana bibi, nashukuru sana.”

    Chris aliachana na bibi, akatenga muda wa kutosha kuzungumza na baba yake mdogo, Shamakala. Kama ilivyokuwa kwa bibi, ndivyo alivyofanya kwa Shamakala.

    Alimpatia kiasi cha shilingi laki moja kama ahsante ya mambo yote aliyomsaidia.

    “Kuondoka?” akauliza Shamakala.

    “Kesho.”

    “Sasa mwenzako?”

    “Nimeshampa maelekezo, nimemwambia mhudumu wa pale amwamshe usiku saa tisa, hata mimi nitampigia. Huyo atamsaidia kumpakia kwenye gari ambapo atanikuta kituoni Mkalama.”

    “Wazo zuri.”

    Uzuri ni kwamba, gesti aliyokuwa amefikia Laura ilikuwa barabarani kabisa. Ilikuwa ni kiasi cha kuamshwa na kuwa barabarani mapema.

    Kwa kawaida, magari ya kwenda mjini hutoka kituo cha Ibaga, usiku wa saa tisa na nusu. Kila siku kulikuwa na gari moja tu, likikukuacha, inabidi usibiri mpaka kesho yake au ukodi pikipiki, gharama yake wengi huikimbia.

    Usafiri wa kutokea Ibaga, huwa ni kwenda Singida Mjini, Arusha kupitia Hydom, Igunga na Meatu kwa magari tofauti. Jambo hilo Laura alijulishwa mapema na mpenzi wake, kwa hiyo alijiandaa!

    ***

    Chris alidamka mapema sana. Saa nane na nusu, tayari alikuwa macho. Haraka akampigia Laura ambaye alipokea na kumjulisha kuwa ameshaamka muda mrefu uliopita.

    Alijiandaa haraka kisha akatoka na kwenda kumgongea baba yake mdogo, ambaye alitoka nje haraka. Tayari ilikuwa nimeshafika saa tisa kamili usiku.

    Kwa msaada wa tochi, waliweza kutembea taratibu kuelekea barabarani. Walitumia robo saa kufika eneo hilo. Ilipotimia saa kumi kasorobo usiku, mlio wa gari ulianza kusikika kwa mbali, walikuwa na uhakika kuwa basi la kwenda mjini lilikuwa linakaribia kufika.

    “Gari hilo linakuja,” akasema Chris.

    “Ni kweli, ndiyo mida yake hii. Mimi nakutakia kila la kheri, hakikisha unatimiza yote tuliyokubaliana.”

    “Sawa baba mdogo, nakutegemea.”

    Basi lilisimama mbele yao, Chris akaingia. Hakupata shida kujua alipokuwa amekaa mpenzi wake, maana tayari alikuwa ameshakata tiketi mapema.

    “Pole na usingizi mpenzi,” akasema Chris.

    Laura akatabasamu, akamjibu: “Ahsante.”

    Ni kama alikuwa anasubiri shuka katikati ya usiku wenye baridi kali. Alijitupa kifuani mwa Chris, akatulia. Robo saa baadaye, alikuwa ameshapitiwa na usingizi.

    Alishtuka walipofika Iguguno! Tayari kulikuwa kumekucha! Muda mfupi baadaye walishuka Singida Mjini. Hapo ndipo walipoachana kwa majonzi mazito.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Chris alipanda basi lililotoka Kahama kwenda Dar na Laura akapanda basi lililotoka Dodoma kwenda Mwanza. Walishindwa kuficha hisia zao, muda mfupi kabla hawajaachana, walikumbatiana kwa muda mrefu. Kila mmoja alimhitaji mwenzake.

    Mapenzi matamu kiasi gani?



    WA kwanza kuingia kwenye basi alikuwa Chris aliyeingia kwenye Basi la NBS. Chris alitoa kichwa dirishani, akampungia mkono Laura, naye akafanya hivyo. Chris alisisimka alipoona mashavu ya mpenzi wake yakitiririsha machozi!

    Hakuweza kuvumilia zaidi, akarudisha kichwa chake ndani kisha haraka akachukua simu yake na kumwandikia ujumbe uliosomeka: “Usilie mama, unanifanya nijisikie vibaya. Najua unanipenda sana Laura, nakupenda pia!”

    “Najua Chris, lakini maumivu. Nimekuzoea sana, kwa siku chache nilizokaa nawe kijijini zimekuwa za tofauti sana kwangu, nahisi kama tayari umeshanioa. Nakupenda sana.”

    “Nakupenda pia.”

    Waliendelea kuwasiliana kwa muda mrefu. Tayari Laura alishangia kwenye Basi la Mohammed lililotokea Dodoma kuelekea Mwanza.

    Safari nzima kwao ilikuwa yenye furaha kubwa. Ni kama walikuwa wakisafiri umbali mfupi tu kutokana na kuwekana karibu kwa mawasiliano.

    Ahadi yao ilikuwa moja tu; ndoa. Wote waliazimia kuungana katika ndoa takatifu.

    ***

    Chris aliingia Dar es Salaam saa mbili usiku akiwa amechoka sana. Alichokifanya ni kuchukua teksi iliyompeleka nyumbani kwake Kijitonyama.

    Kweli alikuwa na hamu sana ya kukutana na wasanii wenzake akina Jaybee, Ramsey na Chika lakini kwa uchovu aliokuwa nao ilikuwa lazima apumzike kwanza.

    Alijimwagia maji, akatafuta chakula kwenye mgahawa wa jirani, kisha akarudi nyumbani alipofungua jokofu lake na kutoa kinywaji. Ilikuwa lazima ajitoe uchovu kidogo!

    Bia tatu zilitosha kumwondolea uchovu aliokuwa nao awali. Akajilaza kitandani akiendelea kutafakari siku yake mpya itakayofuata!

    ***

    Mapokezi ya Laura nyumbani kwao Nyakato, Mwanza yalikuwa mazuri sana. Usiku mzima alikuwa akizungumza na ndugu zake ambao hakuonana nao kwa muda mrefu alipokuwa masomoni.

    Sebule yao ilichangamka sana. Mpaka usiku sana, wengi walikuwa wameshaingia vyumbani kulala, wakabaki Laura na mama yake tu.

    Hapo ndipo Laura alipoamua kutumia nafasi hiyo vizuri kwa ajili ya kuzungumza na mama yake. Walikuwa wawili tu.

    “Mama kuna kitu nataka kukuambia!” akasema Laura akimwangalia mama yake usoni.

    “Niambie mwanangu, ni nini tena hicho?”

    “Nimepata mchumba... anataka kunioa.”

    “Unasema?”

    “Nimepata mchumba mama.”

    “Ni nani?”

    “Yupo Dar.”

    “Umekutana naye wapi?”

    “Singida.”

    “Naye ni mwanafunzi?”

    “Hapana mama. Nipe nafasi nikueleze vizuri, tatizo una haraka sana. Kwa nini hutaki kunisikiliza kwanza? Halafu tatizo si huyo mvulana, kuna shida kidogo kwa upande wa wazazi wake.”

    “Shida kivipi?”

    “Wazazi wake wamemwambia lazima aoe kijijini lakini sisi tumependana na yupo tayari kunioa.”

    “Hata kama mmependana na yupo tayari kukuoa, itawezekana vipi wakati wazazi wake hawataki?”

    “Kuna mpango tumeshafanya. Hivi ninavyoongea na wewe, tayari nimeshafika hadi kijijini kwao na wamenikubali.”

    “Mh!”

    “Usigune mama, ngoja nikueleze vizuri.”

    Laura alimsimulia mchezo mzima ulivyokuwa, jinsi jambo hilo alivyoshirishwa baba yake mdogo na Chris, Shamakala, bila bibi na ndugu zake wengine kufahamu.

    “Mh! Una hatari wewe mtoto. Enhee, huyo kijana mwenyewe ni nani hasa? Na kweli umri wake unamruhusu kuoa?” akauliza mama Laura.

    “Hana shida, ni mtu mzima. Ana miaka 35 sasa, nayaamini maamuzi yake mama.”

    “Anaitwa nani?”

    “Ni Dk. Chris yule msanii wa filamu, kwa sababu ni maarufu najua utakuwa unamfahamu,” akasema Laura akitabasamu.

    Alitegemea mama yake angefurahia jambo hilo, alichokutana nacho kilikuwa tofauti kabisa:

    “Unasemaje wewe?” mama Laura akasema kwa sauti ya ukali sana.

    “Vipi tena mama?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sitaki matatizo na baba yako, unataka kuolewa na hao wahuni wa filamu? Huo ujinga wako uishie hapahapa,” alisema mama Laura kwa hasira kisha akaondoka sebuleni na kumuacha Laura peke yake!

    Huzuni mpya!



    ALIHISI moyo wake kama umeingiwa na ubaridi mkali, Laura alichanganyikiwa kwa hakika. Kwa urafiki wake na mama yake, alijua jambo lile angelipokea kwa urahisi sana.

    Kinyume na matarajio hayo, mama yake aligeuka mbogo! Maneno yake yakamchanganya sana. Wasanii ni wahuni? Aliumia sana kichwani mwake.

    “Wasanii ni wahuni? Mbona simwelewi mama lakini? Labda ni kweli ni wahuni lakini si kwa Chris wangu. Chris si mhuni. Kwanza ni daktari. Mama lazima akubaliane na mimi.

    “Siwezi kukubali kuishi na mtu mwingine tofauti na Chris. Sijamwelewa mama hata kidogo. Hapo nitapingana naye,” aliwaza Laura.

    Furaha aliyokuwa nayo moyoni mwake iliyeyuka ghafla. Alimtegemea mama yake ndiye angemuunga mkono na ugomvi na baba yake usingekuwepo lakini imekuwa tofauti.

    Aliinuka kwa hasira na kwenda zake chumbani kwake. Hakufanya chochote zaidi ya kujitupa kitandani na kulala kama alivyotoka sebuleni.

    Kitu pekee alichokumbuka ilikuwa ni kuchukua simu yake. Akaiweka karibu yake, pembeni ya mto. Alitakiwa kupunguza mawazo yake, mtu pekee ambaye angemsaidia kupunguza mawazo yaliyokuwa yamemvaa kwa kasi muda ule alikuwa ni mpenzi wake tu – Chris.

    Lakini vipi kama angemwambia Chris kuhusu mama yake kugoma?

    “Itakuwa tatizo lingine, sitakiwi kumwambia chochote,” akawaza.

    “Pia sitakiwi kumpigia,” akawaza tena.

    Sauti ya Chris pengine ingeweza kuwa dawa ya usingizi na kumpunguzia maumivu makali ya moyo lakini kwa namna hali ilivyokuwa, aliona ni bora aache kumpigia.

    Alipitisha azimio hilo.

    Akaamua kulala bila kuzungumza na mpenzi wake; si juu ya tukio lililotokea muda mfupi uliopita, bali hakutaka kuzungumza naye kitu chochote.

    Akiwa anajitahidi kuubembeleza usingizi, simu yake iliita. Haraka akatupa macho yake kwenye kioo cha simu yake, akakutana na jina la ‘My Love’.

    Alikuwa ni Chris. Alisita kupokea. Alishindwa kuelewa kama angepokea angezunguza nini na mpenzi wake. Habari alizokuwa nazo, hazikuwa nzuri hata kidogo. Ni habari ambazo asingependa kuzisikia kabisa.

    “Lakini sijui anataka kuniambia nini...acha tu nimpokelee,” mwisho akapitisha uamuzi huo.

    Akapokea.

    “Hello darling,” ilikuwa sauti ya Chris.

    “Niambie mpenzi wangu,” Laura alijitahidi kuzungumza kwa upendo akiweka pembeni tatizo lilitokea.

    “Nimeshindwa kulala kabisa bila kuzungumza na wewe. Nimeshtuka muda huu mpenzi, nikakukumbuka,” akasema Chris.

    “Kweli mpenzi wangu?”

    “Kabisa dear.”

    “Nashukuru kusikia hivyo, wazee hawajambo?”

    “No! Kwa muda niliofika, ilikuwa vigumu sana kwenda nyumbani. Nipo kwangu Kijitonyama. Vipi huko, wewe?”

    “Hawajambo.”

    “Umewagusia suala letu?”

    “Hapana mpenzi, nimeona nilale kwanza, niwaambie kesho. Ulipenda iwe leo mpenzi wangu?”

    “Kabisa.”

    “Mh! Una haraka? Unatamani hata hiyo ndoa yenyewe ingekuwa kesho. Mimi ni wako tu mpenzi, wala usiwe na wasiwasi wowote. Mimi ni mali yako.”

    “Kweli?”

    “Kwa nini usiamini maneno yangu?”

    “Nakuamini mpenzi.”

    “Nashukuru kusikia hivyo, nakutakia usiku mwema, nitakutafuta kesho mpenzi wangu sawa.”

    “Sawa baba.”

    “Usiache kunijulisha chochote kitakachotokea kuhusu mambo yetu.”

    “Sawa mpenzi wangu.”

    Wakakata simu zao.

    Kitendo cha kukata tu simu, ilikuwa kama ndiyo tiketi ya Laura kuanza kulia. Alilia kuliko kawaida. Aliumizwa sana na maneno ya Chris ambaye hakujua kilichokuwa kikiendelea Mwanza!

    Ukweli ni kwamba, Chris hakutakiwa kwa sababu tu alikuwa msanii wa filamu.

    Kwa mama yake na Laura, msanii wa filamu ni mhuni tu, asiye na sifa ya kummiliki mwanaye.

    Ulikuwa mwiba mkali sana kwa Laura ambaye aliugulia mwenyewe. Hakuwa na wa kumwambia kuhusu kilichokuwa kikiendelea.

    Alilia sana.

    Mto wote ulikuwa chapachapa! Ulilowanishwa na machozi ya Laura. Alikuwa na jeraha kubwa sana moyoni mwake. Jeraha bichi kabisa. Jeraha linalovuja damu!

    ***CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Niambie ulipofikia,” mzee Shila, baba yake na Chris alimwambia mwanaye jioni hiyo walipokuwa wamepumzika bustanini.

    Siku nzima Chris aliamua kushinda nyumbani kwao, Mbezi Beach. Hakwenda kazini wala hakukutana na rafiki zake. Aliamua kujipumzisha na ndugu zake nyumbani.

    “Hatua nzuri baba. Bibi ameshamaliza kila kitu. Imebaki ndoa tu,” akasema Chris.

    “Kweli?”



    MOYONI Chris alikuwa na woga ambao hauna kipimo, alijua wazi jibu ambalo angemjibu baba yake, lilikuwa la uongo lakini alilazimika kufanya hivyo kwa sababu ya kutimiza lengo lake.



    Ni kweli alikuwa akidanganya lakini hata baba yake hakumtendea haki kumchagulia mahali na mtu wa kumuoa. Jambo hilo liligoma kabisa kuingia ubongoni mwake.

    “Niamini baba, nasema kweli kabisa.”



    Chris aliyatuliza macho yake usoni mwa baba yake, aliona milima midogomidogo iliyokuwa usoni mwa Mzee Shila ikiwa kama inaporomoka! Makunyanzi yake yakayeyuka taratibu.



    Tabasamu likachanua!

    Alitamani sana kuona mwanaye akioa! Siyo kuoa tu; aoe msichana kutoka kijijini! Kilichoendelea Mwanza, hakuna aliyejua!

    Si Chris wala baba yake, mzee Shila.



    Ni fumbo!

    “Ahsante sana mwanangu. Naamini hujaniangusha, namwamini sana baba yako mdogo, najua hawezi kufanya makosa. Vipi, umeweza kuja na picha yake?”



    “Hapana baba, ungependa kumuona?” akauliza Chris akitabasamu.

    “Kabisa...natamani kumuona.”

    “Nitafanya mpango wa picha, ngoja nifanye mawasiliano nitakujulisha.”

    “Sawa mwanangu.”



    Furaha ya mzee Shila ilikuwa wazi kabisa, ugomvi wa kwanza na mwanaye ulikuwa umeisha, ulibaki mmoja tu; kuigiza! Kwa mzee Shila, kuigiza ilikuwa ni uhuni na kujidhalilisha.



    Kila alipokutana na skendo za wasanii mbalimbali katika magazeti, alijua kwa sababu mwanaye pia ni msanii, lazima angekuwa na tabia kama hizo. Siku zote alipata tabu sana kumfanya Chris akubaliane naye.



    Hata hivyo, kwa hatua hiyo ya awali, kwa mzee Shila yalikuwa mafanikio makubwa. Moyoni akasema: “Acha kwanza hili lipite, mengine yataendelea. Hanishindi, huyu ni nimemzaa mwenyewe.”



    Ilikuwa furaha kubwa sana kwa familia hiyo, siku nzima walishinda wakiwa wenye amani, kitu kikubwa kilichojadiliwa, ilikuwa ndoa ya Chris na Njile (Laura).



    “Sikupatii picha mwanangu...siku hiyo, nakuona umevaa suti yako safi na mkeo amependeza, ukumbi mzima unasubiri kusikia utambulisho wa wazazi wako. MC sasa anasema: Baba mzaa chema, Profesa Shila naomba usimame watu wakuone....” alisema mzee Shila akicheka.



    “Hatimaye Dk. Chris ameoa, ah! Mwanangu kwa kweli itakuwa furaha kubwa sana kwetu,” akadakia mama yake.



    Hakutaka kabisa vurugu siku hiyo, vikao vyake vya pombe na rafiki zake akina Jaybee, Ramsey na Chika, alivisamehe kwa siku hiyo.

    ***

    Usiku mzima, Laura hakupata usingizi. Mawazo yake yalikuwa kwa Chris ambaye sasa ndoto za kuoana zilikuwa zimeanza kuyeyuka. Tegemeo pekee wa kumsaidia katika hilo alikuwa ni mama yake ambaye hakutaka kuwa upande wake kabisa.



    Asubuhi aliamka mapema na kukaa sebuleni akijifanya anaangalia taarifa ya habari ya Runinga ya ITV. Baba yake, mzee Moses Ngeleja alitoka akiwa ameshajiandaa kwenda kazini.

    Alipomuona mwanaye sebuleni, alitabasamu...



    “Morning dad!” Laura akasalimia kwa Kimombo.

    “Morning to you daughter. Vipi za masomo?”

    “Nzuri tu baba, nimebakiza kipindi kifupi cha mwisho nimalize masomo kabisa.”

    “Ni kweli. Naona Singida si kubaya, kumekupenda sana mwanangu.”

    “Mh! Baba bwana...”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Laura, acha mimi nikimbie kazini, jioni nitawahi kurudi kwa ajili yako. Nina mengi ya kuzungumza na wewe mwanangu.”



    Hayo yalimfanya Laura aamini kuwa mpaka muda huo, mama yake alikuwa hajamwambia chochote baba yake.

    “Ila dad, natamani uniruhusu nije nikuone ofisini kwako mchana, naona jioni ni mbali, nami nina yangu ya kuzungumza na wewe.”

    “Sawa...karibu mwanangu!”



    Mzee Ngeleja akatoka nje. Akaingia kwenye gari yake aina ya Toyota VX, akaelekea kazini kwake, katikati ya Jiji la Mwanza, Jengo la Kaijage ilipokuwa ofisi yake.

    ***

    Laura hakutaka kuzungumza na mama yake chochote kuhusiana na suala la Chris. Hata mchana alipotoka kwenda ofisini kwa baba yake, hakumwambia ukweli, zaidi ya kumdanganya kuwa anakwenda kumuona rafiki yake.



    Akiwa mbele ya meza ya baba yake, Laura alijikaza na kumweleza baba yake ukweli: “Baba nimekua sasa, nimempata mkweo. Kuna mwanaume anataka kunioa.”

    Mzee Ngeleja akatabasamu!



    “Habari njema kiasi gani binti yangu. Vipi, umeshazungumza na mama yako kuhusu hili?” akasema mzee Ngeleja akiachia tabasamu mwanana usoni mwake.



    USO wa Laura ulisawagika. Alionekana dhahiri kuwa na hofu ya ghafla. Mabadiliko yake yalikuwa wazi. Mzee Ngeleja alijua kwa vyovyote vile, kuna jambo lilimsumbua mwanaye.

    “Laura...” Mzee Ngeleja akaita.

    “Abee baba.”

    “Vipi, mbona kama umebadilika kidogo?”

    “Hapana.”



    “Mh!” mzee Ngeleja akaguna.

    “Mbona unaguna baba?”

    “Mimi nakujua vizuri mwanangu, kuna kitu unanificha.”

    “Hakika hakuna kitu baba.”

    “Sawa, hebu turudi katika suala lako. Umeshazungumza na mama yako?” akamwuliza tena.

    “Yaani baba hiyo ndiyo sababu iliyonifanya nije kuzungumza na wewe huku kazini kwako.”

    “Kivipi?”



    “Jana usiku nilijaribu kumweleza juu ya jambo hilo lakini cha ajabu, akapingana na mimi. Amesema hataki kusikia hizo habari.”



    “Hawezi kusema hivyo ikiwa hana sababu. Hebu kuwa wazi, niambie tatizo ni nini?”

    “Ukweli baba tatizo ni juu ya mwanaume mwenyewe. Unajua baba, huyo jamaa anayetaka kunioa ni msanii wa filamu, lakini siyo mhuni kama mama anavyofikiri.

    “Ni msomi, tena daktari na anafanya kazi hospitalini kabisa ila anafanya filamu kama sehemu yake ya kujifurahisha tu.”



    “Ni nani?”

    “Jina lake halisi ni Christopher Joseph Shila, kwenye kazi zake za filamu anajiita Dk. Chris. Tumechunguzana kwa muda mrefu sana, namjua vizuri baba. Nimewahi kufika hadi kijijini kwao.

    “Ni mwanaume sahihi kabisa baba, lakini mama ananikataza kwa vile tu ni msanii wa filamu, ndiyo maana nimeamua kuja kukushirikisha hili suala ili unisaidie,” alisema Laura mfululizo, baba yake akiwa kimya akimsikiliza.

    “Ok! Nimekuelewa vizuri sana. Umesema nyumbani kwao ulikwenda. Ilikuwaje?”



    “Hiyo ni habari nyingine baba, unajua kwao, wazazi wake nao walimpa masharti kuhusu mwanamke wa kuoa. Wakamwambia ni lazima mkewe atokee kijijini tena vijiji vya nyumbani kwao. Lakini kwa sababu sisi tunapendana ikabidi atumie mbinu nyingine ili kuwafanya wazazi wake waamini kuwa mimi ni wa kijijini.”

    “Mkafanyaje sasa?”



    Laura akamsimulia kila kitu kilivyokuwa bila kumficha chochote. Mzee Ngeleja alikuwa kimya akimsiliza mwanaye ambaye hakuna alichodanganya. Alionekana kumuelewa binti yake.

    “Kwa hiyo huyo kijana anaishi Dar?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ndiyo.”



    “Na wazazi wake?”

    “Dar pia.”

    “Anaishi nao?”

    “Hapana. Chris yeye amepanga kwake.”

    “Hoja za mama yako zinaweza kuwa na maana lakini na wewe pia maelezo yako ni ya msingi. Sitaki kuwa dikteta katika hili. Kitu pekee ambacho nakitaka, ni kukutana na huyo kijana kwanza. Anaweza kuja hapa Mwanza nikaonana naye?” akasema mzee Ngeleja.

    Laura akashtuka sana!



    Lilikuwa wazo zuri sana, kwa jinsi baba yake alivyozungumza, alionekana wazi kukubaliana naye lakini alitaka kuonana na Chris ili wazungumze na kufahamiana.

    “Anaweza baba, hilo halina shida.”

    “Sawa, nadhani hili tumemaliza, nenda zungumza naye, mpange siku ya kuja. Iwe mapema kabla hujarejea chuoni Singida.”



    “Sawa baba, kazi njema.”

    “Ahsante binti yangu.”

    Laura akaondoka ofisini kwa baba yake, angalau kichwani akiwa amepunguza mawazo. Sasa alikuwa na mwanga kuwa Chris angeweza kuwa mwanaume wa maisha yake.



    ***

    Aliposhuka chini ya Jengo la Kaijage, kitu cha kwanza Laura kufanya ilikuwa ni kumpigia Chris. Alipiga simu mara moja tu – ikapokelewa.

    “Baby vipi?” Laura aliongea.

    “Poa, mambo?”

    “Safi kabisa.”



    “Afadhali umenipigia, nilikuwa nakupigia sasa hivi.”

    “Kuna nini tena?”

    “Nilitaka unitumie picha zako kwenye WhatsApp. Nilizungumza na wazee kuhusu wewe, wanatamani kukuona japo katika picha tu,” akasema Chris.

    “Mh! Haina shida mpenzi wangu, mimi nina kubwa zaidi.”

    “Kubwa gani?”



    “Ni stori ndefu sana mpenzi lakini kikubwa, baba yangu anataka kuonana na wewe. Nimeongea naye kwa kirefu sana kuhusu mimi na wewe!” akasema Laura.

    “Dah! Kwani hukuzungumza na mama?”

    “Mama ndiyo amesababisha yote hayo lakini hakuna tatizo, dalili ni nzuri,” akasema Laura.

    “Unamaanisha nini?”



    “Mama alianza kuleta vikwazo ndiyo maana nikaamua kumwambia baba, hivi tunavyoongea nimetoka ofisini kwake,” akasema Laura kwa sauti ya taratibu kabisa.

    Chris alishtuka sana!





    Ni Mkristo, sijawahi kuwa na mtoto na sina mke na sijawahi kuoa. Naamini nimejieleza vizuri kiasi mzee wangu, lakini kama utaona kuna kitu nimeacha unaweza kuniuliza,” akasema Chris.

    “Ahsante sana, nimekuelewa vizuri Chris, napenda kukuita Dk. Chris. Naomba kwanza uniruhusu!”

    “Ndiyo taaluma yangu mzee, ruksa kutumia.”

    “Ahsante sana Dk. Chris, kwa hakika unajua kujieleza vizuri sana, nataka kukuambia kwa maelezo yako mafupi, nakuhakikishia kuwa binti yangu umempata!” akasema mzee Ngeleja.

    Chris akatabasamu!SASA ENDELEA...

    LAURA naye akafanya hivyo. Kwa furaha Chris alisimama na kunyoosha mkono wake kuelekea kwa mzee Ngeleja. Kitu cha ajabu ni kwamba, mzee huyo hakupokea mkono wake, zaidi akasema...

    “Lakini kuna tatizo kidogo Dk. Chris.”

    “Tatizo gani?” Chris akauliza haraka akionekana kushtuka sana.

    Tayari matumaini ya kumpata Laura yalianza kufutika tena. Kitendo cha mzee Ngeleja ambaye ni kama alikuwa mtetezi wake kusema kuna tatizo kidogo, kulimaanisha kumkwamisha kwenye zoezi lililokuwa mbele yake.

    Mzee Ngeleja alibaki kimya!

    Chris alikuwa bado amesimama vilevile. Akamwuliza tena: “Kuna tatizo gani mzee wangu?”

    “Tuliza moyo Dk. Chris,” akasema mzee Ngeleja akiachia tabasamu mwanana.

    “Nimeshtuka sana.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Lazima iwe hivyo.”

    “Lakini ni nini hasa?”

    “Naona njia mliyotumia haikuwa sahihi. Kwa nini mliwadanganya wazazi?”

    “Unamaanisha kule kijijini?”

    “Ndiyo.”

    “Kulikuwa hakuna kitu kingine cha kufanya zaidi ya hivyo baba. Kumbuka msimamo wa baba yangu ulikuwa huo; kwamba lazima nioe kijijini. Laura siyo wa kijijini baba, ningefanyaje?”

    Mzee Ngeleja akakaa kimya.

    “Naomba utusamehe baba, lakini tulilazimika.”

    “Tena baba, naomba uwe upande wetu katika hili. Sisi tunajua tunachotengeneza. Lengo letu ni zuri na najua litamfurahisha kila mmoja baadaye. Kwa sababu tumeshalianza kwa mtindo huu, naomba liishe hivyohivyo kwanza,” akadakia Laura.

    “Wazo zuri sana Laura,” akasema Chris.

    “Kwahiyo mnanishawishi nijiunge nanyi kusema uongo?” mzee Ngeleja akasema kwa hamaki.

    “Si kwa maana hiyo baba. Lakini kama tulivyosema lengo letu ni zuri.”

    Mzee Ngeleja akatulia tena.

    “Sawa. Nimekubaliana nanyi, endeleeni na taratibu nyingine. Mimi kwa upande wetu huku mniachie sawa?”

    “Sawa baba.”

    “Basi sawa, yangu mimi yalikuwa ni hayo mwanangu Chris. Laura unaweza kumsindikiza mwenzako. Vipi ratiba yako? Utakuwa hapa leo ukiendelea kula sangara na sato au unaondoka leoleo?” akauliza mzee Ngeleja.

    “Leo nipo, nina tiketi ya ndege ya kesho jioni maana sikujua mazungumzo yetu yangechukua muda gani.”

    “Sawa, Laura msindikize mwenzako ili apate hoteli, maana najua kwa hapa mjini si mwenyeji.”

    “Hakika baba, mimi nakwenda, ila nina zawadi yako!” akasema Chris akimkabidhi mzee Ngeleja begi dogo.

    “Kuna nini humu?” akasema akitabasamu.

    “Utaona ukifungua mwenyewe.”

    “Ahsante sana dokta, nashukuru.”

    Wakaagana.

    **

    Ilikuwa siku nyingine mpya kwa Chris na Laura. Waliongozana hadi hotelini ambapo mazunguzo ni kama yalianza upya kabisa. Chris hakuamini kama mambo yangekuwa rahisi kiasi kile hasa baada ya kuambiwa na Laura kuwa kulikuwa na tatizo kwa wazazi wake.

    “Siamini dear,” akasema Laura.

    “Siamini pia, lakini hapa mambo yanatakiwa kwenda harakaharaka kama ambavyo imepangwa. Mambo mengine yatajulikana baadaye.”

    “Sawa baby.”

    Chris alicharuka, Laura akasisimka. Ni kama damu zilikuwa zikiwaka moto. Ghafla walirukiana na kukutanisha ndimi zao. Kazi ya kufyonzana ikaanza. Waligalagala kitandani kwa muda mrefu kabla ya habari kuhamia kwenye upande wa kimataifa!

    Wote walikuwa na uchu kama ndiyo kwanza walikuwa wamekutana siku hiyo. Jioni kabisa, Laura alirudi nyumbani kwao. Ilikuwa lazima awahi kabla baba yake hajarudi.

    Chris alilala akiwa na uhakika wa kuingia kwenye ndoa na mwanamke wa maisha yake. Mwanamke ambaye alijihakikishia kumpenda kwa dhati ya moyo wake.

    ***

    Mzee Ngeleja alirudi nyumbani akiwa na furaha sana. Alizungumza na mkewe chumbani kuhusu Chris na binti yao Laura. Mkewe hakuwa tayari kabisa kumwelewa kwa maelezo yaleyale; wasanii ni wahuni!

    “Mke wangu achana na mawazo hayo, mimi nimekutana na Chris na kuzungumza naye.

    Mimi ni mtu mzima, naelewa vizuri haya mambo. Yule kijana ni mtu mzuri sana, hana shida na anafaa kabisa kuoana na binti yetu,” akasema mzee Ngeleja.

    Mkewe akashtuka!



    MAMA Laura hakutegemea kuwa mumewe angeweza kuwa ameshakutana na Chris na kuzungumza naye. Kwake, Chris alikuwa kijana mhuni kwa vile tu alikuwa msanii wa filamu.

    Kitendo cha kumwambia kuwa alikutana naye, kilimshangaza sana. Mama Laura alitoa macho na kumwuliza mumewe:



    “Umekutana naye wapi?” akauliza kwa hamaki.

    “Ofisini kwangu, leo hii amekuja Mwanza na kesho asubuhi anaondoka. Naomba ukubaliane na mimi, maana siwezi kukubali binti yangu akaolewa na kijana mpuuzi!”

    Mama Laura akatulia.



    Baadaye akasema: “Lakini mume wangu unapaswa kufikiri zaidi kuhusu hili. Naona kama utakuwa umeamua harakaharaka sana.”

    “Hapana, mimi ni mtu mzima na nina uelewa mzuri. Najua ninachokifanya,” akasema mzee Ngeleja kwa kujiamini.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Mama Laura alikaa kimya tena. Safari hii utulivu ulikuwa wa hali ya juu zaidi.

    Mzee Ngeleja akafungua lile begi na kutoa zawadi alizopewa na Chris. Kulikuwa na mashati mawili ya kitenge, saa, mkanda na tai mbili. Pia kulikuwa na doti tatu za vitenge vya gharama.



    “Ona hizi ni zawadi alizotuletea. Ndiyo nafungua muda huu hapa. Chukua na vitenge vyako,” akasema mzee Ngeleja akimkabidhi mkewe.



    Taratibu mama Laura akaonekana kuanza kuelewa somo, si kwa sababu ya zawadi bali utii alioanza kuhisi Chris anao.



    “Nakubaliana na wewe mume wangu! Nakubali Chris amuoe binti yetu. Nimeanza kuhisi kitu tofauti sasa, bila shaka nimebadili uamuzi wangu.”

    “Ahsante sana mke wangu!”



    Wakakumbatiana kwa furaha. Tayari upande wa Laura hapakuwa na pingamizi. Ilibaki upande wa Chris tu.

    ***

    Chris aliingia Dar es Salaam akiwa na matumaini mapya. Hakuwa na shaka yoyote kuhusu kumpata Laura. Alipozungumza na baba yake, alimwambia amwachie kila kitu yeye, anachotaka ni kuona anaoa!



    “Zungumza na baba yako mdogo akamilishe kila kitu kuhusu ndoa. Kama mtaamua mnaweza kufunga ndoa ya kimila kijijini halafu kanisani mje mfunge huku Dar. Kutokana na majukumu yangu, namwachia jukumu hilo baba yako mdogo.



    “Tafadhali lifanyike haraka sana. Mimi nimeshazungumza na marafiki zangu kuhusu ndoa yako. Wapo tayari kunisaidia. Wewe niachie mimi kila kitu, sawa?” akasema mzee Shila kwa kujiamini.

    “Sawa baba, nimekuelewa!” akajibu Chris akiachia tabasamu.

    Wasiwasi wa nini?

    ***

    Siku zilikwenda haraka sana, hawakuwa na kitu cha kusubiri. Kwa kuwa Shamakala alikuwa anajua kila kitu kinachoendelea, kilichofanyika ilikuwa ni kupeleka posa kwa mzee Ngeleja.



    Walilazimika kusafiri kutokea Singida mpaka Mwanza na kukamilisha zoezi la posa. Kila kitu kilikwenda sawa kabisa, posa ilikubaliwa na mahari ikapagwa. Vitu vidogovidogo vya kimila vilikamilishwa na mzee Ngeleja akawa tayari binti yake aende kufunga ndoa ya kimila kijijini.



    Zoezi hilo lilifanyika bila wazazi wa pande zote mbili. Ndoa ilisimamiwa na Shamakala, baba mdogo wa Chris na wawakilishi wa mzee Ngeleja kutoka Mwanza. Baada ya hapo Laura alirudi chuoni kumalizia mitihani yake ya mwisho.



    Mzee Shila alijulishwa na mdogo wake, Shamakala kuhusu mwenendo wa kila kitu kilivyokuwa kijijini. Alifurahi sana lakini kichwani mwake alijua kuwa, kijana wake alioa mwanamke wa nyumbani kwao jambo ambalo halikuwa la kweli.

    ***

    Mipango yote ilivyokamilika, zoezi la mahari liliachwa mikononi mwa Shamakala. Yeye na washenga wa Chris ndiyo waliosafiri tena hadi Mwanza kulipa mahari kisha ikafanyika hafla fupi ya Laura kuvalishwa pete ya uchumba.



    Kutokea hapo, Laura akawa mchumba rasmi wa Chris. Hadi kufikia muda huo, baba na mama wa Chris walikuwa hawajamuona Laura zaidi ya picha tu.



    Mzee Shila hakutaka kusumbua watu, alikuwa ameshatayarisha fedha za kutosha kwa ajili ya sherehe ya mwanaye. Aliitisha kikao cha watu wachache tu, marafiki zake wa karibu kwa ajili ya kupeana mawazo ya namna harusi ya mwanaye itakavyokuwa na michango waliyoahidi.



    Huko Mwanza vikao vya sherehe ya kumuaga Laura viliendelea. Taarifa ambazo mzee Shila alizipata ni kwamba, sherehe ya kumuaga Laura ingefanyika jijini Mwanza kwa baba yake mdogo ambapo aliishi na kusoma huko kwa muda mrefu.



    Hata hivyo, baadaye siri ilivuja! Mzee Shila akagundua kuwa Laura hakuwa Mnyiramba, wala hakuwahi kuishi Mpambala kama ilivyoelezwa lakini pia hakuitwa Njile.

    Ni Msukuma wa Mwanza!



    Mzee Ngeleja alikasirika sana. Ilibaki wiki chache sana kabla ya ndoa. Alimwita Chris nyumbani kwake ambaye alimkuta baba yake amewaka kwa hasira.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Chris unawezaje kunifanyia maigizo?” akafoka kwa hasira mbele ya mwanaye Chris.

    “Kivipi baba?” Chris aliuliza lakini alianza kuhisi kuwa tayari mambo yalishaharibika.

    “Huyo mchumba wako ni mtu wa wapi?”



    “Baba jamani... si ni Singida!”

    “Mpuuzi wewe! Singida ndiyo Mwanza siku hizi siyo? Halafu unanidanganya mimi kama mtoto mdogo? Pumbavu kabisa, sasa hiyo ndoa hesabu haipo.



    Potelea mbali fedha nilizopoteza, lakini safari hii nitaongozana na wewe hadi kijijini na nitahakikisha unaoa mwanamke kutoka kijijini!” akasema mzee Shila kwa hasira.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog