Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

LAITI NINGEJUA - 1

 





    IMEANDIKWA NA : FRANK SILAA



    *********************************************************************************



    Simulizi : Laiti Ningejua

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    Saa 11.00 alfajiri nazinduka usingizini baada ya kusikia mlio wa alamu niliyokuwa nimeitegesha kwenye simu yangu, ili niweze kujiandaa mapema niwahi shule. Macho yangu yanashindwa kuangaza vema kwasababu bado nilikuwa nahisi usingizi, kwasababu usiku nilikuwa na chati na marafiki zangu wa facebook kwa simu ambayo nilikuwa nimeikota barabarani miezi kadhaa iliyopita wakati nilipokuwa nimetoka dukani.

    Ingawa bado nilikuwa nikihisi usingizi sana lakini ilinibidi nijikaze niamke nijandae kwasababu wazazi wangu huwa ni wakali sana pindi ninapoonyesha kuwa mzembe katika mambo ya shule.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Baada ya kujiandaa nilimimina uji kwenye kikombe ili niweze kunywa niwai shule. Uchumi wa pale nyumbani ulikuwa ni mbovu sana kiasi kwamba ilikosekana hela ya kununulia sukari kwahiyo mara nyingi asubuhi huwa nakunywa uji ambao huwa natia ndimu pamoja na chumvi ili kuleta ladha. Mara bada ya kumimina uji kwenye kikombe nilisikia sauti ya rafiki yangu Glory ikiniita kwa sauti ya juu.

    “Teddy”

    “Abee” niliitikia nikiwa ndani

    “Twendee”

    “Nakuja.” Nilijibu wakati naweka kile kikombe cha uji chini ili niweze kuondoka kwasababu nilikumbuka kuwa jana yake niliadhibiwa kwa kosa la uchelewaji kwahiyo sikuwa tayari kupata adhabu kwa mara nyingine.

    Niliwaaga wazazi wangu ambao nao walikuwa tayari wameshaamka ili wameze kuwai kwenda shamba, na baada ya hapo kwa mwendo wa haraka niliongozana na rafiki yangu hadi shuleni ambapo tulifanikiwa kufika kwa wakati.

    Baada ya kukusanyika paredi kabla ya kuingia madarasani mkuu wa shule alitangaza kwa wale ambao hawajalipa ada warudi nyumbani wakalete ada, nilijisikia vibaya sana baada ya kauli ile kwasababu na mimi nilikuwa miongoni mwa wanafunzi ambao wanadaiwa ada. Na pia kama mkuu wa shule angeweza kutangaza mdaiwa sugu pale shuleni pengine mimi ndie ningeweza kuibuka kinara kwasabaabu nilikuwa na malimbikizo mengi ya madeni ya shule. Sikuwa na namna ya kufanya ili niendelee kuwepo shuleni pale kwasababu mkuu wa shule alitangaza kwamba endapo akimkuta mwanafunzi ambae hajalipa darasani basi ataweza kumuadhibu vibaya sana, nilianza safari ya kurudi nyumbani asubuhi ileile.

    Nilipokuwa njiani nikirudi nyumbani nilisikia mngurumo wa gari nyuma yangu ikanibidi nitembee kando kabisa ya barabara ili kulipisha gari lile lililokuwa likija kwa mwendo wa kawaida, mara baada ya kunifikia dreva wa gari lile alipunguza mwendo kabisa na kuanza kuniongelesha.

    “Mambo vipi.”

    “Safi.”

    “Mbona unarudi mapema hivyo, unaumwa?”

    ***

    Niliona aibu kumweleza kuwa nilikuwa nimerudishwa kwasababu sijalipa ada kwahiyo nilimdanganya kuwa nilikuwa mgonjwa.

    “Pole sana basi twende nikusogeze.”

    “Hapana we tangulia tu kaka mimi nakuja polepole.”

    “Hapana dadangu, naomba nikusaidie tafadhali.”

    Nilikosa ujanja wa kuendelea kumkatalia kwasababu nilikuwa nimemdanganya kuwa nilikuwa naumwa kwahiyo nilifungua mlango wa gari lile na kuingia ndani na kukaribishwa na mziki mlaini uliokuwa umefunguliwa kwa sauti ya wastani.

    “Unasikia wapi ndio panakuuma zaidi?”

    “Tumbo.”

    “Jamani pole sana, umekula nini au ndio yale mambo yenu wakina dada.”

    Yule kaka aliniuliza swali ambalo lilinifanya nipoteze kujiamini kabisa na kuishia kunyamaza kimya bila kujibu chochote.

    “Ok mimi naitwa Enrique.”

    “Sijui wewe mwenzangu unaitwa nani.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    “Naitwa Teddy.”

    “Jina lako zuri sana, nafurahi kukufahamu.

    “Unasoma kidato cha ngapi?”

    “Cha nne.”

    “Hongera sana kwasababu ndio upo ukingoni.”

    “Unaishi wapi?” Kaka yule alizidi kuniadama kwa maswali.

    “Mtaa wa Moshono.”

    “Duuh inamana unatoka kote huko unakuja shuleni Oldadai?”

    “Ndipo nilipofaulia kidato cha kwanza.”

    “Pole sana kwasababu ni umbali mrefu sana.”

    “Nimeshazoea.”

    “Basi usijali nitakupeleka hadi nyumbani kwenu.”

    ***

    Baada ya kunifikisha maeneo ya jirani na nyumbani kabla ya kushuka kwenye gari aliniomba namba zangu za simu na bila hiyana nilimpatia kwasababu alionekana kuwa ni kijana mstaarabu kwani barabarani hakuzungumza neno lolote lakuonyesha kuwa ananitaka kama ilivyo kwa vijana wengine akikutana na wewe kabla hata hajajua jina lako tayari ameshakutongoza. Nilivutiwa pia na namna anavyozungumza kwa ustaarabu bila mapepe.

    Niliaagana na Enrique nikishangaa sana kwa jinsi alivyoonekana kuwa na moyo wa huruma wa kunisaidia kwasababu alinifikisha hadi maeneo ya karibu na nyumbani na nilimuonyesha nyumba yetu kwa mbali kwasababu sikuthubutu kwenda nae hadi nyumbani kwavile isingeleta picha nzuri kwa familia yangu na kwa majirani pia kwasababu nilikuwa nasifika kwa kuwa binti mwenye heshima na adabu sana pale mtaani kwetu.

    Baada ya kufika nyumbani nilibadilisha nguo za shule huku nikijihisi kuwa na furaha sana baada ya kukutana na kaka yule na kuwafuata wazazi wangu shambani ili nikaweze kuwasaidia kwasababu nilijua hawatarudi nyumbani hadi jioni kabisa lakini pia nilifahamu kwamba hata ningekwenda kuwaeleza kuwa nilikuwa nimerudishwa kwaajili ya ada bado isingesaidia chochote kwasababu nilikuwa nafahamu hali halisi ya pale nyumbani.

    “Teddy mbona umerudi mapema?” mama aliniuliza baada ya kutia timu shambani nikiwa nimevaa nguo kuukuu kwaajili ya kuungana nao katika kilimo cha kuandaa shamba kwaajili ya kupanda mahindi na maharage ambapo kama kawaida huwa hatupati mazao ya kutosha kwasababu shamba halikuwa na rutuba kwasababu ya kulima kila mwaka.

    “Wanafunzi ambao hatujalipa ada tumerudishwa nyumbani.”

    “Yani na hivi maisha yalivyo magumu sijui hata hizo pesa zitapatikana vipi.”

    “Inamana mama hakuna namna kabisa ya kuweza kuniwezesha nikamalizia hili darasa moja lililosalia ili niweze kupata cheti cha form four?”nilizungumza na mama bila baba kusikia mazungumzo yetu kwasababu baba alikuwa akilima mbali kidogo kumalizia sehemu ambayo jana yake walishindwa kumalizia kutokana na kwamba giza liliwakuta shambani.

    “Kiukweli hakuna mzazi ambae hapendi mwanae asifanikiwe ila maisha yamekuwa magumu sana sioni njia yeyote itakayoweza kuleta hizo pesa za shule ili uweze kuendelea na masomo yako, kwasababu wewe mwenyewe ni shahidi kwamba jana tulilala bila kula, sasa embu niambie kama kupata tu hela ya chakula ni tabu, pesa za kupeleka shuleni zitapatikana kwa njia ipi.” Mama alizungumza maneno ambayo kiukweli yaliniumiza sana kwasababu niliona moja kwa moja malengo yangu ya shule yalikuwa ndio yanapotea kwaajili ya umasikini mkubwa ulikuwa umeandama familia yetu.

    “Teddy niletee maji ya kunywa.” Sauti ya baba ilivuma kutokea pale alipokuwepo.

    Nilikwenda chini ya mti mkubwa uliokuwa pale shambani ambapo kulikuwa na dumu lilokuwa limehifadhiwa maji ya kunywa na kummiminia baba maji kwenye kikombe na kumpelekea.

    ***

    “Pole baba.” Nilimpa baba pole wakati nilipokuwa nampa maji ya kunywa, alionekana kuchoka kwasababu lile shati alilokuwa amevaa lilikuwa limelowa jasho lote.

    “Asante binti yangu.”

    “Mbona umerudi?”

    “Wameturudisha kwasababu hatujalipa ada.”

    “Yaani kiukweli mwaka huu sijui itakuwaje kwasababu pesa hakuna kabisa.”

    “Tumuombe tu Mungu afungue milango yake ya baraka.”

    “Kweli kabisa, kwasababu moja haikai mbili haikai.”

    “Ndani ya muda mfupi mmelima sehemu kubwa kweli baba.”

    “Ni kweli mwanangu ila naona mvua inataka kunyesha kwahiyo hatuna budi kusitisha kazi hii kwa leo hadi kesho.”

    “Kweli kabisa kwasababu mvua ikitukuta huku porini tutalowana sana kwahiyo ni bora tusitishe kwa leo tuweze kuondoka.

    “Teddy nyanyua hizo kuni hapo njoo changanya na hizi ufunge tuweze kuondoka huku shambani kwasababu kunadalili ya mvua.” Mama alizungumza na mimi wakati alipokuwa akichuma mchicha iliyokuwa imejiotea kule shambani.

    “Sawa mama.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Baada ya muda mfupi niliweka furushi langu la kuni kichwani tuliondoka kule shambani na kurejea nyumbani, nilikuwa nikihisi njaa sana kwasababu asubuhi nilishindwa kunywa ule uji niliokuwa nimeuandaa kutokana na haraka niliyokuwa nayo.

    Njiani nilikuwa nawaza kwamba nitakapofika nyumbani niende nikanywe ule uji niliokuwa nimeuacha kwasababu hapakuwa na dalili ya kula kwa siku zile ingawa mama alikuwa akichuma mboga za majani lakini nyumbani hapakuwa na mafuta ya kupikia wala unga.

    Wakati tulipokuwa tukikaribia kufika nyumbani mvua kubwa iliyokuwa ikiambatana na radi ilianza kunyesha na kutufanya tuongeze kasi ya kutembea ili tuweze kufika nyumbani kwa haraka bila ya kulowana sana. Ingawa hapakuwa na umbali mrefu hadi kufika nyumbani tangu mvua ilipoanza kunyesha lakini tulijikuta tumelowana sana kutokana na kwamba mvua ile ilikuwa ni kubwa sana.

    Nilihisi kukasirika sana baada ya kufika nyumbani na kukuta ule uji niliokuwa nautegemea nikaunywe kumbe mende na sisimizi walikuwa wameniwai. Nilihisi kudondokwa na machozi baada ya kwenda jikoni kuangalia maparachichi ambayo nilikuwa nimeyavundika darini na kukuta yameharibiwa na panya wengi ambao walikuwa ni kero pale nyumbani.

    ***

    Baada ya kukosa kabisa namna ya kuweza kutuliza ile njaa iliyokuwa ikinisumbua nilisikia sauti ya baba ikiniita kutokea sebuleni.

    “Teddy.”

    “Abee baba”

    “Njoo”

    “Chukua hii shilingi elfu mbili, nenda dukani kwa Meku kanunue unga kilo moja na mafuta ya kupika ya shilingi mia tano, fanya haraka uje upike.”

    “Sawa baba” nilijiaandaa kidogo na kujiweka katika hali ya usafi kwasababu nilikuwa nimetoka shamba, halafu isitoshe palikuwa pana umbali mrefu kutokea pale nyumbani hadi dukani kwahiyo isingependeza kwa mtoto wa kike kutembea barabarani nikiwa katika hali ile niliyokuwa nimetoka nayo shambani. Baada ya kujiandaa nilikwenda mara moja dukani, nilipofika kwa bahati mbaya au nzuri Meku alijichanganya na kunizidishia chenchi kwasababu nilikuwa nimempa shilingi elfu mbili akafikiri kuwa nilikuwa nimempa shilingi elfu kumi. Kutokana na dhiki niliyokuwa nayo sikuthubutu kumweleza kuwa alikuwa amenizidishia hela zaidi sana nilikaa kimya nikisubiri kwa hamu amalize kunihudumia niweze kuondoka.

    Nilichelewa kupika na pia kuni nilizokuwa napikia zilikuwa mbichi baada ya kunyeshewa na mvua ilipelekea kutenga chakula mezani jioni ya saa kumi na moja baada ya kuchelewa kuiva, kusema kweli hatukuwa na ratiba inayoeleweka katika masuala ya chakula kwasababu muda mwingine ndio kama hivyo chakula cha mchana kilikuwa kinaliwa jioni.

    Japo kuwa wazazi wangu walitamani sana binti yao niweze kusoma lakini nilikumbana na vikwazo vingi sana japokuwa ada iliyokuwa ikihitajika shule ilikuwa ni ndogo sana lakini kutokana na ugumu wa maisha ilikosekana kabisa na kunifanya nibaki njia panda bila kuelewa msaada nitaupata wapi.

    Hayo ndio maisha Mzee Baruti na mkewe Tina ambapo walibahatika kupata mtoto mmoja ambae ndie Teddy, ingawa kabla ya Mzee Baruti kuoana na Tina alibahatika kuzaa watoto watatu ambao ni Kazimoto, Maridadi na Rehema, lakini pia Tina (mama Teddy) alibahatika kuzaa watoto wawili wa kike kabla ya kuoana na Mzee Baruti ambao ni Cheusi na Ameni. Kwa bahati nzuri watoto wote kwa upande wa Mzee Baruti na mkewake walikuwa wanajitegemea na familia zao ingawa bado maisha yao yalikuwa sio mazuri kabisa katika suala zima la uchumi isipokuwa Kazimoto kidogo alikuwa na maisha mazuri kidogo kuliko ndugu zake.

    Hali ya maisha ilizidi kuwa ngumu na kupelekea kushindwa kuhitimu elimu yangu ya sekondari na kubaki nyumbani nikibangaiza maisha na wazazi wangu kwa kufanya vibarua vya kulima katika mashamba ya watu ili angalau tuweze kupata chochote kitu cha kupeleka kinywani.

    Nilizidi kuwasiliana na Enrique kama marafiki japokuwa sikumweleza kuwa nilikuwa nimeacha shule kutokana na kukosa ada. Kwakadiri nilivyokuwa nikizungumza na kaka yule ndivyo alivyozidi kuniingia kwenye moyo wangu kwa jinsi alivyokuwa wakipekee kwasababu licha ya kwamba alikuwa anaonekana kuwa anajiweza kipesa lakini hakuwa mtu wa makuu, na wala hakuwa mtu wa kujionyesha kama ilivyo tabia ya vijana wengi kupenda kumshawishi msichana kutokana na pesa zao.

    ***

    Ilifikia kipindi nisipowasiliana na Enrique najihisi kuumwa kabisa kwajinsi nilivyokuwa nampenda japo kuwa nilikuwa naogopa kumweleza kuwa nimetokea kumpenda kwasababu pengine angeniona Malaya kumbe sivyo.

    Kabla ya kwenda kibaruani siku moja nilibandika kande jikoni na kumuomba mtoto mmoja wa pale jirani aweze kunisaidia kuchochea hadi yaive kipindi mimi na wazazi wangu tutakapokuwa kwenye utafutaji wa riziki. Baada ya kurudi nyumbani mida ya alasiri niliyaunga kwa kitunguu na mafuta na kutenga chakula mezani. Ilipofika usiku nilikuwa sijisikii kula tena kwasababu kile nilichokuwa nimekula baada ya kutoka shambani hakikuwa kimeisha tumbo. Kwahiyo niliwahi kwenda kitandani kujipumzisha kwasababu nilikuwa najihisi kuchoka sana.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    “Natamani angekuwa ndie mwanaume wangu wa kwanza nimpe zawadi ya bikira yangu lakini tayari nimeshaipoteza kwa mtu ambae alikuwa na maneno matamu kama asali kumbe alikuwa ananilaghai ama kweli wanaume wakati mwingine sio watu wa kuwaamini kwasababu wakati wanapokuwa wanakuhitaji wanajua sana kunyenyekea na kubembeleza lakini wakipata walichokuwa wakikitafuta wanakutelekeza na tena wengine hudiriki kukutukana ukiendelea kujipendekeza ili kuokoa penzi. Ila sio mbaya sijutii sana kwasababu nimejifunza namna ya kuishi na hawa viumbe.” Niliwaza nilipokuwa nikijigeuza geuza kitandani nikisubiri muda wake wa kunipigia uweze kufika kwasababu aliniahidi atanipigia simu usiku ule.

    Moyo ulianza kunienda mbio baada ya kuona simu yangu ikiita na aliekuwa akinipigia alikuwa ndio yule alinikuwa kwenye akili yangu kwa wakati ule.

    “Hello Enrique.”

    “Mambo vipi.”

    “Safi tu.”

    “Samahani nimechelewa kukupigia kwasababu nilikuwa napika, ila kwa bahati nzuri ndio kimeiva kwa sasa na tayari nimesha kitenga mezani kwahiyo nakukaribisha ili tuweze kujumuika pamoja katika chakula hiki cha usiku.” Ilisikika sauti ya Enrique ikitekenya hisia zangu kwa namna alivyokuwa akizungumza kwa utaratibu wa hali ya juu.

    “Asante sana jamani unakula nini leo.”

    “Leo nakula makaroni (tambi) kwa nyama.”

    “Ooh jamani I wish ningekuwa hapo ninge enjoy, ila asante sana.”

    “Vipi wewe umeshakula?”

    “Ndio nmekula tu mda sio mrefu.”

    ***

    “We mchoyo kwanini hukunikaribisha au umeona hutashiba nikishiriki na wewe?”

    “Hapana sio hivo jamani nilikupigia simu muda hule hukupokea nikajua labda utakuwa bize.”

    Kweli kabisa nisamehe kwasababu nilipotoka bafuni nilikuta missed call yako nikasema ngoja kwanza niandae chakula ndio nitakutafuta. Vipi umekula nini leo?” alizungumza Enrique kwa sauti ambayo ilionyesha alikuwa ameweka chakula mdomoni.

    “Nimekula kiporo cha kande.” niliona nimweleze ukweli kijana wa watu na nisimdanganye kwasababu pengine ipo siku atafahamu maisha yangu yalivyo ya kuungaunga. Kwasababu hata kama kwetu kulikuwa na dhiki sana lakini nilikuwa naishi.

    Nilijitahidi kumwonyesha Enrique kuwa natokea katika familia masikini lakini nilifurahi kwasababu alizidi kuonyesha moyo wa kunijali na kunithamini bila kujali nilikuwa nimetokea katika familia gani. Alisikitika sana baada ya kuja kubaini kuwa nilikuwa nimeacha shule kwasababu nilikosa ada pia isitoshe alinilaumu sana kwanini sikumshirikisha katika suala lile ili aweze kulitafutia ufumbuzi lakini tayari nilikuwa nimeshachelewa kwasababu wenzangu walikuwa tayari wameshaitimu.

    Urafiki wetu ulizidi kukua siku hadi siku ingawa hatukuwai kuonana tena tangu ile siku aliyonipa lifti kwenye gari lake baada ya kumdaanganya kuwa nilikuwa najihisi kuumwa. Nilifurahi sana siku moja baada ya kunieleza kuwa kuna jambo alikuwa anahitaji kunieleza kwahiyo alikuwa anahitaji tuweze kuonana, japo kuwa niliweka pingamizi kwakumbembeleza sana aweze kunieleza kwenye simu lakini alikataa kabisa na kunieleza kwamba ingependeza zaidi kama tungeweza kuonana ana kwa ana kwasababu alikuwa amenimiss sana.

    Siku moja ya juma pili nilimuomba mama ruhusa ya kwenda kumtembelea rafiki yangu Glory. Nilitumia upenyo ule ili niweze kwenda kuonana na Enrique. Nilikwenda moja kwa moja hadi kwenye ziwa moja linaloitwa duluti lipo nje kidogo ya jiji la Arusha ambapo ndipo alinieleza nikamkute.

    Nilifika na kukutana nae kiukweli alifurahi sana kuniona na pia nilifurahi sana kumwona kwa mara nyingine.

    “Umependeza sana Teddy.”

    “Asante.” Kiukweli hata mimi mwenyewe nilikuwa najua kuwa nimevunja kabati (nimependeza) kwasababu mara nyingi ninavyovaa nguo ile huwa nasifiwa sana na watu wengi kuwa nimependa. Na hata ile siku nilikuwa nimeshasifiwa zaidi ya mara 20 wanaume kwa wanawake. Kiukweli umaridadi uficha umasikini kwasababu kwajinsi nilivyokuwa nimependeza sio rahisi mtu kufahamu kuwa nilikuwa naogelea katika dimbwi la umasikini.

    Nilifurahia upepo mzuri uliokuwa ukivuma pale ziwani kuja katika ile hoteli nzuri tulipokuwa tumekaa mimi na Enrique.

    Unapendelea chakula gani dada.” Aliniuliza muudumu mmoja wa kiume aliekuwa amependeza sana.

    “Chochote utakachokula mwenzangu.”

    “Kinywaji je?”

    “Naomba Alvaro.”

    Baada ya kuletewa tulichokuwa tumeagiza tuliaanza kula na kunywa huku tukipiga stori na mkaka yule ambae uso wake ulikuwa umeandamwa na tabasamu kila mara pindi anapokuwa ananitazama.

    Teddy nimekuita hapa kwasababu kunajambo nahitaji kukueleza.”



    Saa 11.00 alfajiri nazinduka usingizini baada ya kusikia mlio wa alamu niliyokuwa nimeitegesha kwenye simu yangu, ili niweze kujiandaa mapema niwahi shule. Macho yangu yanashindwa kuangaza vema kwasababu bado nilikuwa nahisi usingizi, kwasababu usiku nilikuwa na chati na marafiki zangu wa facebook kwa simu ambayo nilikuwa nimeikota barabarani miezi kadhaa iliyopita wakati nilipokuwa nimetoka dukani.

    Ingawa bado nilikuwa nikihisi usingizi sana lakini ilinibidi nijikaze niamke nijandae kwasababu wazazi wangu huwa ni wakali sana pindi ninapoonyesha kuwa mzembe katika mambo ya shule.

    Baada ya kujiandaa nilimimina uji kwenye kikombe ili niweze kunywa niwai shule. Uchumi wa pale nyumbani ulikuwa ni mbovu sana kiasi kwamba ilikosekana hela ya kununulia sukari kwahiyo mara nyingi asubuhi huwa nakunywa uji ambao huwa natia ndimu pamoja na chumvi ili kuleta ladha. Mara bada ya kumimina uji kwenye kikombe nilisikia sauti ya rafiki yangu Glory ikiniita kwa sauti ya juu.

    “Teddy”

    “Abee” niliitikia nikiwa ndani

    “Twendee”

    “Nakuja.” Nilijibu wakati naweka kile kikombe cha uji chini ili niweze kuondoka kwasababu nilikumbuka kuwa jana yake niliadhibiwa kwa kosa la uchelewaji kwahiyo sikuwa tayari kupata adhabu kwa mara nyingine.

    Niliwaaga wazazi wangu ambao nao walikuwa tayari wameshaamka ili wameze kuwai kwenda shamba, na baada ya hapo kwa mwendo wa haraka niliongozana na rafiki yangu hadi shuleni ambapo tulifanikiwa kufika kwa wakati.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Baada ya kukusanyika paredi kabla ya kuingia madarasani mkuu wa shule alitangaza kwa wale ambao hawajalipa ada warudi nyumbani wakalete ada, nilijisikia vibaya sana baada ya kauli ile kwasababu na mimi nilikuwa miongoni mwa wanafunzi ambao wanadaiwa ada. Na pia kama mkuu wa shule angeweza kutangaza mdaiwa sugu pale shuleni pengine mimi ndie ningeweza kuibuka kinara kwasabaabu nilikuwa na malimbikizo mengi ya madeni ya shule. Sikuwa na namna ya kufanya ili niendelee kuwepo shuleni pale kwasababu mkuu wa shule alitangaza kwamba endapo akimkuta mwanafunzi ambae hajalipa darasani basi ataweza kumuadhibu vibaya sana, nilianza safari ya kurudi nyumbani asubuhi ileile.

    Nilipokuwa njiani nikirudi nyumbani nilisikia mngurumo wa gari nyuma yangu ikanibidi nitembee kando kabisa ya barabara ili kulipisha gari lile lililokuwa likija kwa mwendo wa kawaida, mara baada ya kunifikia dreva wa gari lile alipunguza mwendo kabisa na kuanza kuniongelesha.

    “Mambo vipi.”

    “Safi.”

    “Mbona unarudi mapema hivyo, unaumwa?”

    ***

    Niliona aibu kumweleza kuwa nilikuwa nimerudishwa kwasababu sijalipa ada kwahiyo nilimdanganya kuwa nilikuwa mgonjwa.

    “Pole sana basi twende nikusogeze.”

    “Hapana we tangulia tu kaka mimi nakuja polepole.”

    “Hapana dadangu, naomba nikusaidie tafadhali.”

    Nilikosa ujanja wa kuendelea kumkatalia kwasababu nilikuwa nimemdanganya kuwa nilikuwa naumwa kwahiyo nilifungua mlango wa gari lile na kuingia ndani na kukaribishwa na mziki mlaini uliokuwa umefunguliwa kwa sauti ya wastani.

    “Unasikia wapi ndio panakuuma zaidi?”

    “Tumbo.”

    “Jamani pole sana, umekula nini au ndio yale mambo yenu wakina dada.”

    Yule kaka aliniuliza swali ambalo lilinifanya nipoteze kujiamini kabisa na kuishia kunyamaza kimya bila kujibu chochote.

    “Ok mimi naitwa Enrique.”

    “Sijui wewe mwenzangu unaitwa nani.”

    “Naitwa Teddy.”

    “Jina lako zuri sana, nafurahi kukufahamu.

    “Unasoma kidato cha ngapi?”

    “Cha nne.”

    “Hongera sana kwasababu ndio upo ukingoni.”

    “Unaishi wapi?” Kaka yule alizidi kuniadama kwa maswali.

    “Mtaa wa Moshono.”

    “Duuh inamana unatoka kote huko unakuja shuleni Oldadai?”

    “Ndipo nilipofaulia kidato cha kwanza.”

    “Pole sana kwasababu ni umbali mrefu sana.”

    “Nimeshazoea.”

    “Basi usijali nitakupeleka hadi nyumbani kwenu.”

    ***

    Baada ya kunifikisha maeneo ya jirani na nyumbani kabla ya kushuka kwenye gari aliniomba namba zangu za simu na bila hiyana nilimpatia kwasababu alionekana kuwa ni kijana mstaarabu kwani barabarani hakuzungumza neno lolote lakuonyesha kuwa ananitaka kama ilivyo kwa vijana wengine akikutana na wewe kabla hata hajajua jina lako tayari ameshakutongoza. Nilivutiwa pia na namna anavyozungumza kwa ustaarabu bila mapepe.

    Niliaagana na Enrique nikishangaa sana kwa jinsi alivyoonekana kuwa na moyo wa huruma wa kunisaidia kwasababu alinifikisha hadi maeneo ya karibu na nyumbani na nilimuonyesha nyumba yetu kwa mbali kwasababu sikuthubutu kwenda nae hadi nyumbani kwavile isingeleta picha nzuri kwa familia yangu na kwa majirani pia kwasababu nilikuwa nasifika kwa kuwa binti mwenye heshima na adabu sana pale mtaani kwetu.

    Baada ya kufika nyumbani nilibadilisha nguo za shule huku nikijihisi kuwa na furaha sana baada ya kukutana na kaka yule na kuwafuata wazazi wangu shambani ili nikaweze kuwasaidia kwasababu nilijua hawatarudi nyumbani hadi jioni kabisa lakini pia nilifahamu kwamba hata ningekwenda kuwaeleza kuwa nilikuwa nimerudishwa kwaajili ya ada bado isingesaidia chochote kwasababu nilikuwa nafahamu hali halisi ya pale nyumbani.

    “Teddy mbona umerudi mapema?” mama aliniuliza baada ya kutia timu shambani nikiwa nimevaa nguo kuukuu kwaajili ya kuungana nao katika kilimo cha kuandaa shamba kwaajili ya kupanda mahindi na maharage ambapo kama kawaida huwa hatupati mazao ya kutosha kwasababu shamba halikuwa na rutuba kwasababu ya kulima kila mwaka.

    “Wanafunzi ambao hatujalipa ada tumerudishwa nyumbani.”

    “Yani na hivi maisha yalivyo magumu sijui hata hizo pesa zitapatikana vipi.”

    “Inamana mama hakuna namna kabisa ya kuweza kuniwezesha nikamalizia hili darasa moja lililosalia ili niweze kupata cheti cha form four?”nilizungumza na mama bila baba kusikia mazungumzo yetu kwasababu baba alikuwa akilima mbali kidogo kumalizia sehemu ambayo jana yake walishindwa kumalizia kutokana na kwamba giza liliwakuta shambani.

    “Kiukweli hakuna mzazi ambae hapendi mwanae asifanikiwe ila maisha yamekuwa magumu sana sioni njia yeyote itakayoweza kuleta hizo pesa za shule ili uweze kuendelea na masomo yako, kwasababu wewe mwenyewe ni shahidi kwamba jana tulilala bila kula, sasa embu niambie kama kupata tu hela ya chakula ni tabu, pesa za kupeleka shuleni zitapatikana kwa njia ipi.” Mama alizungumza maneno ambayo kiukweli yaliniumiza sana kwasababu niliona moja kwa moja malengo yangu ya shule yalikuwa ndio yanapotea kwaajili ya umasikini mkubwa ulikuwa umeandama familia yetu.

    “Teddy niletee maji ya kunywa.” Sauti ya baba ilivuma kutokea pale alipokuwepo.

    Nilikwenda chini ya mti mkubwa uliokuwa pale shambani ambapo kulikuwa na dumu lilokuwa limehifadhiwa maji ya kunywa na kummiminia baba maji kwenye kikombe na kumpelekea.

    ***

    “Pole baba.” Nilimpa baba pole wakati nilipokuwa nampa maji ya kunywa, alionekana kuchoka kwasababu lile shati alilokuwa amevaa lilikuwa limelowa jasho lote.

    “Asante binti yangu.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    “Mbona umerudi?”

    “Wameturudisha kwasababu hatujalipa ada.”

    “Yaani kiukweli mwaka huu sijui itakuwaje kwasababu pesa hakuna kabisa.”

    “Tumuombe tu Mungu afungue milango yake ya baraka.”

    “Kweli kabisa, kwasababu moja haikai mbili haikai.”

    “Ndani ya muda mfupi mmelima sehemu kubwa kweli baba.”

    “Ni kweli mwanangu ila naona mvua inataka kunyesha kwahiyo hatuna budi kusitisha kazi hii kwa leo hadi kesho.”

    “Kweli kabisa kwasababu mvua ikitukuta huku porini tutalowana sana kwahiyo ni bora tusitishe kwa leo tuweze kuondoka.

    “Teddy nyanyua hizo kuni hapo njoo changanya na hizi ufunge tuweze kuondoka huku shambani kwasababu kunadalili ya mvua.” Mama alizungumza na mimi wakati alipokuwa akichuma mchicha iliyokuwa imejiotea kule shambani.

    “Sawa mama.”

    Baada ya muda mfupi niliweka furushi langu la kuni kichwani tuliondoka kule shambani na kurejea nyumbani, nilikuwa nikihisi njaa sana kwasababu asubuhi nilishindwa kunywa ule uji niliokuwa nimeuandaa kutokana na haraka niliyokuwa nayo.

    Njiani nilikuwa nawaza kwamba nitakapofika nyumbani niende nikanywe ule uji niliokuwa nimeuacha kwasababu hapakuwa na dalili ya kula kwa siku zile ingawa mama alikuwa akichuma mboga za majani lakini nyumbani hapakuwa na mafuta ya kupikia wala unga.

    Wakati tulipokuwa tukikaribia kufika nyumbani mvua kubwa iliyokuwa ikiambatana na radi ilianza kunyesha na kutufanya tuongeze kasi ya kutembea ili tuweze kufika nyumbani kwa haraka bila ya kulowana sana. Ingawa hapakuwa na umbali mrefu hadi kufika nyumbani tangu mvua ilipoanza kunyesha lakini tulijikuta tumelowana sana kutokana na kwamba mvua ile ilikuwa ni kubwa sana.

    Nilihisi kukasirika sana baada ya kufika nyumbani na kukuta ule uji niliokuwa nautegemea nikaunywe kumbe mende na sisimizi walikuwa wameniwai. Nilihisi kudondokwa na machozi baada ya kwenda jikoni kuangalia maparachichi ambayo nilikuwa nimeyavundika darini na kukuta yameharibiwa na panya wengi ambao walikuwa ni kero pale nyumbani.

    ***

    Baada ya kukosa kabisa namna ya kuweza kutuliza ile njaa iliyokuwa ikinisumbua nilisikia sauti ya baba ikiniita kutokea sebuleni.

    “Teddy.”

    “Abee baba”

    “Njoo”

    “Chukua hii shilingi elfu mbili, nenda dukani kwa Meku kanunue unga kilo moja na mafuta ya kupika ya shilingi mia tano, fanya haraka uje upike.”

    “Sawa baba” nilijiaandaa kidogo na kujiweka katika hali ya usafi kwasababu nilikuwa nimetoka shamba, halafu isitoshe palikuwa pana umbali mrefu kutokea pale nyumbani hadi dukani kwahiyo isingependeza kwa mtoto wa kike kutembea barabarani nikiwa katika hali ile niliyokuwa nimetoka nayo shambani. Baada ya kujiandaa nilikwenda mara moja dukani, nilipofika kwa bahati mbaya au nzuri Meku alijichanganya na kunizidishia chenchi kwasababu nilikuwa nimempa shilingi elfu mbili akafikiri kuwa nilikuwa nimempa shilingi elfu kumi. Kutokana na dhiki niliyokuwa nayo sikuthubutu kumweleza kuwa alikuwa amenizidishia hela zaidi sana nilikaa kimya nikisubiri kwa hamu amalize kunihudumia niweze kuondoka.

    Nilichelewa kupika na pia kuni nilizokuwa napikia zilikuwa mbichi baada ya kunyeshewa na mvua ilipelekea kutenga chakula mezani jioni ya saa kumi na moja baada ya kuchelewa kuiva, kusema kweli hatukuwa na ratiba inayoeleweka katika masuala ya chakula kwasababu muda mwingine ndio kama hivyo chakula cha mchana kilikuwa kinaliwa jioni.

    Japo kuwa wazazi wangu walitamani sana binti yao niweze kusoma lakini nilikumbana na vikwazo vingi sana japokuwa ada iliyokuwa ikihitajika shule ilikuwa ni ndogo sana lakini kutokana na ugumu wa maisha ilikosekana kabisa na kunifanya nibaki njia panda bila kuelewa msaada nitaupata wapi.

    Hayo ndio maisha Mzee Baruti na mkewe Tina ambapo walibahatika kupata mtoto mmoja ambae ndie Teddy, ingawa kabla ya Mzee Baruti kuoana na Tina alibahatika kuzaa watoto watatu ambao ni Kazimoto, Maridadi na Rehema, lakini pia Tina (mama Teddy) alibahatika kuzaa watoto wawili wa kike kabla ya kuoana na Mzee Baruti ambao ni Cheusi na Ameni. Kwa bahati nzuri watoto wote kwa upande wa Mzee Baruti na mkewake walikuwa wanajitegemea na familia zao ingawa bado maisha yao yalikuwa sio mazuri kabisa katika suala zima la uchumi isipokuwa Kazimoto kidogo alikuwa na maisha mazuri kidogo kuliko ndugu zake.

    Hali ya maisha ilizidi kuwa ngumu na kupelekea kushindwa kuhitimu elimu yangu ya sekondari na kubaki nyumbani nikibangaiza maisha na wazazi wangu kwa kufanya vibarua vya kulima katika mashamba ya watu ili angalau tuweze kupata chochote kitu cha kupeleka kinywani.

    Nilizidi kuwasiliana na Enrique kama marafiki japokuwa sikumweleza kuwa nilikuwa nimeacha shule kutokana na kukosa ada. Kwakadiri nilivyokuwa nikizungumza na kaka yule ndivyo alivyozidi kuniingia kwenye moyo wangu kwa jinsi alivyokuwa wakipekee kwasababu licha ya kwamba alikuwa anaonekana kuwa anajiweza kipesa lakini hakuwa mtu wa makuu, na wala hakuwa mtu wa kujionyesha kama ilivyo tabia ya vijana wengi kupenda kumshawishi msichana kutokana na pesa zao.

    ***

    Ilifikia kipindi nisipowasiliana na Enrique najihisi kuumwa kabisa kwajinsi nilivyokuwa nampenda japo kuwa nilikuwa naogopa kumweleza kuwa nimetokea kumpenda kwasababu pengine angeniona Malaya kumbe sivyo.

    Kabla ya kwenda kibaruani siku moja nilibandika kande jikoni na kumuomba mtoto mmoja wa pale jirani aweze kunisaidia kuchochea hadi yaive kipindi mimi na wazazi wangu tutakapokuwa kwenye utafutaji wa riziki. Baada ya kurudi nyumbani mida ya alasiri niliyaunga kwa kitunguu na mafuta na kutenga chakula mezani. Ilipofika usiku nilikuwa sijisikii kula tena kwasababu kile nilichokuwa nimekula baada ya kutoka shambani hakikuwa kimeisha tumbo. Kwahiyo niliwahi kwenda kitandani kujipumzisha kwasababu nilikuwa najihisi kuchoka sana.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    “Natamani angekuwa ndie mwanaume wangu wa kwanza nimpe zawadi ya bikira yangu lakini tayari nimeshaipoteza kwa mtu ambae alikuwa na maneno matamu kama asali kumbe alikuwa ananilaghai ama kweli wanaume wakati mwingine sio watu wa kuwaamini kwasababu wakati wanapokuwa wanakuhitaji wanajua sana kunyenyekea na kubembeleza lakini wakipata walichokuwa wakikitafuta wanakutelekeza na tena wengine hudiriki kukutukana ukiendelea kujipendekeza ili kuokoa penzi. Ila sio mbaya sijutii sana kwasababu nimejifunza namna ya kuishi na hawa viumbe.” Niliwaza nilipokuwa nikijigeuza geuza kitandani nikisubiri muda wake wa kunipigia uweze kufika kwasababu aliniahidi atanipigia simu usiku ule.

    Moyo ulianza kunienda mbio baada ya kuona simu yangu ikiita na aliekuwa akinipigia alikuwa ndio yule alinikuwa kwenye akili yangu kwa wakati ule.

    “Hello Enrique.”

    “Mambo vipi.”

    “Safi tu.”

    “Samahani nimechelewa kukupigia kwasababu nilikuwa napika, ila kwa bahati nzuri ndio kimeiva kwa sasa na tayari nimesha kitenga mezani kwahiyo nakukaribisha ili tuweze kujumuika pamoja katika chakula hiki cha usiku.” Ilisikika sauti ya Enrique ikitekenya hisia zangu kwa namna alivyokuwa akizungumza kwa utaratibu wa hali ya juu.

    “Asante sana jamani unakula nini leo.”

    “Leo nakula makaroni (tambi) kwa nyama.”

    “Ooh jamani I wish ningekuwa hapo ninge enjoy, ila asante sana.”

    “Vipi wewe umeshakula?”

    “Ndio nmekula tu mda sio mrefu.”

    ***

    “We mchoyo kwanini hukunikaribisha au umeona hutashiba nikishiriki na wewe?”

    “Hapana sio hivo jamani nilikupigia simu muda hule hukupokea nikajua labda utakuwa bize.”

    Kweli kabisa nisamehe kwasababu nilipotoka bafuni nilikuta missed call yako nikasema ngoja kwanza niandae chakula ndio nitakutafuta. Vipi umekula nini leo?” alizungumza Enrique kwa sauti ambayo ilionyesha alikuwa ameweka chakula mdomoni.

    “Nimekula kiporo cha kande.” niliona nimweleze ukweli kijana wa watu na nisimdanganye kwasababu pengine ipo siku atafahamu maisha yangu yalivyo ya kuungaunga. Kwasababu hata kama kwetu kulikuwa na dhiki sana lakini nilikuwa naishi.

    Nilijitahidi kumwonyesha Enrique kuwa natokea katika familia masikini lakini nilifurahi kwasababu alizidi kuonyesha moyo wa kunijali na kunithamini bila kujali nilikuwa nimetokea katika familia gani. Alisikitika sana baada ya kuja kubaini kuwa nilikuwa nimeacha shule kwasababu nilikosa ada pia isitoshe alinilaumu sana kwanini sikumshirikisha katika suala lile ili aweze kulitafutia ufumbuzi lakini tayari nilikuwa nimeshachelewa kwasababu wenzangu walikuwa tayari wameshaitimu.

    Urafiki wetu ulizidi kukua siku hadi siku ingawa hatukuwai kuonana tena tangu ile siku aliyonipa lifti kwenye gari lake baada ya kumdaanganya kuwa nilikuwa najihisi kuumwa. Nilifurahi sana siku moja baada ya kunieleza kuwa kuna jambo alikuwa anahitaji kunieleza kwahiyo alikuwa anahitaji tuweze kuonana, japo kuwa niliweka pingamizi kwakumbembeleza sana aweze kunieleza kwenye simu lakini alikataa kabisa na kunieleza kwamba ingependeza zaidi kama tungeweza kuonana ana kwa ana kwasababu alikuwa amenimiss sana.

    Siku moja ya juma pili nilimuomba mama ruhusa ya kwenda kumtembelea rafiki yangu Glory. Nilitumia upenyo ule ili niweze kwenda kuonana na Enrique. Nilikwenda moja kwa moja hadi kwenye ziwa moja linaloitwa duluti lipo nje kidogo ya jiji la Arusha ambapo ndipo alinieleza nikamkute.

    Nilifika na kukutana nae kiukweli alifurahi sana kuniona na pia nilifurahi sana kumwona kwa mara nyingine.

    “Umependeza sana Teddy.”

    “Asante.” Kiukweli hata mimi mwenyewe nilikuwa najua kuwa nimevunja kabati (nimependeza) kwasababu mara nyingi ninavyovaa nguo ile huwa nasifiwa sana na watu wengi kuwa nimependa. Na hata ile siku nilikuwa nimeshasifiwa zaidi ya mara 20 wanaume kwa wanawake. Kiukweli umaridadi uficha umasikini kwasababu kwajinsi nilivyokuwa nimependeza sio rahisi mtu kufahamu kuwa nilikuwa naogelea katika dimbwi la umasikini.

    Nilifurahia upepo mzuri uliokuwa ukivuma pale ziwani kuja katika ile hoteli nzuri tulipokuwa tumekaa mimi na Enrique.

    Unapendelea chakula gani dada.” Aliniuliza muudumu mmoja wa kiume aliekuwa amependeza sana.

    “Chochote utakachokula mwenzangu.”

    “Kinywaji je?”

    “Naomba Alvaro.”

    Baada ya kuletewa tulichokuwa tumeagiza tuliaanza kula na kunywa huku tukipiga stori na mkaka yule ambae uso wake ulikuwa umeandamwa na tabasamu kila mara pindi anapokuwa ananitazama.

    Teddy nimekuita hapa kwasababu kunajambo nahitaji kukueleza.”



    Usiku kucha sikufumba mboni za macho yangu nilikuwa kama nimerukwa na akili kwa jinsi nilivyokuwa sijielewi.

    Palipokucha mama alikuja chumbani kwangu kunijulia hali na kuzidi kunisisitiza nisiendelee kulia kwasababu pengine haikuwa riziki yangu na kwa kawaida kisicho riziki huwa hakiliki.

    “Kama kweli ameamua kukuacha endelea kumnyenyekea Mungu akujalie umpate ambae ndie kusudi lake.”

    Mama alizungumza na mimi mambo ya msingi sana lakini niliona kama alikuwa akinipigia kelele kwasababu sikuwa tayari kuamini kuwa Enrique niliekuwa nimempenda na kumpa moyo wangu kuwa ndie alikuwa ameniacha kwenye mataa.

    Kila baada ya sekunde kadhaa nilikuwa napiga simu yake lakini sikuambulia kumpata hewani. Nilizidi kuteseka katika wimbi kubwa la mawazo lililokuwa likirindima kichwani mwangu.

    “Kama kweli alikuwa hanitaki kwanini aliniambia kuwa anakuja nyumbani kwetu kujitambulisha halafu asitokee na simu azime? Alichonifanyia ni zaidi ya unyama kwasababu kwanza amenidhalilisha sana kwa wazazi wangu hata kama sikuwa nimemwalika mtu yeyote lakini hii fedhea aliyonisababishia kwa wazazi wangu ni kubwa mno.” Mawazo yalizidi kutikisa kichwa changu hadi nikaaza kuhisi maumivu makali ya kichwa. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Nilishindwa kutoka ndani kutokana na aibu kubwa iliyokuwa imenijaa, ilipofika kwenye mida ya saa kumi jioni nikiwa bado ndani nilisikia mngurumo wa gari nje ya nyumba yetu, mapigo ya moyo yalibadilika na kuanza kwenda mbio kwasababu sikujua gari lile lilikuwa ni gari la nani kwasababu haikuwa kawaida ya gari lolote kufika pale nyumbani.

    Mama alikuwa nje akitwanga mboga aina ya kisamvu kwaajili ya chakula cha jioni, nilikuwa nikichungulia dirishani ili niweze kumwona yule ambae atashuka kwenye gari ni nani. Baada ya gari kusimama pale nje alishuka dereva wa gari lile na kuzunguka upande wa pili na kufungua mlango, nilipatwa na mshutuko mkubwa hadi nikahisi haja ndogo ghafla baada ya kumwona yule mtu ambae nilikuwa simfahamu akimsaidia Enrique kuteremka kwenye gari kutokana na majeraha mbalimbali aliyokuwa ameyapata mwilini mwake.

    ***

    Nilitoka kwa kasi kama ya mwanga na kwenda pale nje kumjulia hali mpenzi wangu ambae nilikuwa nadhani ameniacha njia panda kumbe alikuwa amepatwa na matatizo.

    Baada ya kufika pale nje licha ya kwamba Enrique alikuwa mgonjwa hata asieweza kuzungumza vizuri alimpigia mama yangu magoti akimwomba radhi kwa kushindwa kufika jana kutokana na ajali mbaya ya gari aliyokuwa ameipata jana alipokuwa anakuja nyumbani na rafiki yake na kwa bahati mbaya sana yule rafiki yake aliweza kupoteza maisha palepale.

    Taarifa ile iliniumiza sana na kuongeza maumivu juu ya maumivu na kusababisha macho yangu kuanza kudondosha machozi kutokana na kile alichokuwa akikizungumza Enrique.

    “Pole sana dia.” Nilimpa pole huku nikiwa nimemshika begani kumpa msaada kumpeleka ndani.

    “Asante sana mpenzi ila naomba unisamehe sana kwasababu sikudhamiria kutokufika siku ya jana.”

    “Usijali nimekwelewa Enrique wangu.”

    “Kwani ilikuwaje.” Nilipatwa na shauku ya kutaka kujua ajali ile ilitokea vipi kwasababu alionekana kuwa na majeraha makubwa mwilini mwake.

    “Ni kwamba tulipokuwa tunakuja kuna gari moja la mchanga (fuso) lilikuwa linalipita lingine na kwabahati mbaya likakutana na gari letu uso kwa uso na kupelekea umauti wa rafiki yangu kwasababu hakuwa amefunga mkanda na kusababisha kurushwa nje ya gari na kupoteza maisha mda uleule.” Alisimulia Enrique mbele yangu mimi na mama.

    “Jamani poleni sana.” mimi na mama tulijikuta tumetamka kwa pamoja maneno hayo.

    “Na hivi ninavyozungumza na wewe ndio nimeruhusiwa kutoka hospitali, ila nikaona nibora nimwambie huyu rafiki yangu mwingine ambae anaitwa Daudi aweze kunipitisha hapa kwenu ili nije niwajulishe kilichokuwa kimenikwamisha ili kuondoa wasiwasi mwingi ambao nadhani mliupata baada ya kushindwa kufika.”

    “Umefanya vizuri kwasababu kweli hata na sisi tulipatwa na wasiwasi na huyu mwenzio usiku kucha alikuwa analia.” Mama aliaamua kumweleza Enrique namna ambavyo nilikuwa kwenye wakati mgumu pindi aliposhindwa kufika jana yake.

    “Jamani pole sana mpenzi wangu, ndio maana anaonekanaa amevimba macho kumbe alikuwa analia.” Maneno ya Enrique yalinipa wasiwasi kidogo juu ya muonekano wangu kwa wakati ule kwasababu nilishtuka sana baada ya kukumbuka kuwa ile siku sikuwa nimeswaki, wala kujipodoa na mbaya zaidi sikuwa hata nimeoga kutokana na kisirani nilichokuwa nacho.

    “Asante sana dia.”

    “Simu yako je iko wapi?”

    “Baada ya ajali kutokea hata sikujua habari za simu kiukweli na sijaikariri namba yako kichwani ndio sababu nikaona nibora nije kuwapa taarifa.”

    “Pole sana baba.” Mama alizungumza kwa huruma kumpa pole Enrique ambae kiukweli alikuwa akitia huruma sana kwajinsi alivyokuwa akizungumza.

    “Asante mama, najua kwa namna moja au nyingine nimewakwaza lakini ninaomba radhi kwasababu mambo mengine ni mipango ya Mungu pengine labda Mwenyezi Mungu hakupanga nije jana bali nije leo ingawa ujio wangu wa leo sio wa kujitambulisha.”

    “Usijali mwanangu chamsingi nikumwomba Mungu atujalie uzima.”

    Muda huohuo sauti ya baba ilisikika ikibisha hodi kwasababu hakuwepo nyumbani kipindi tumepata wageni, mama alimkaribisha kwa kumpisha kwenye kiti.

    “Shkamoo baba.” Alisalimia Enrique na mwenzie kwa heshima.

    “Marahaba hamjambo vijana.”

    “Hatujambo baba.”

    ***

    “Baba huyu ndie yule mchumba wangu ambae nilikueleza jana kuwa atakuja lakini hakuweza kufika kwasababu alipata ajali mbaya alipokuwa anakuja yeye na rafiki yake na kwabahati mbaya yule rafiki yake alipoteza maisha katika ajali ile.”

    “Pole sana kijana kwa matatizo.”

    “Asante sana, naomba mnisamehe kwa ujio wangu wa ghafla ingawa ndio nimeruhusiwa kutoka hospitali mda huu nikaona ni bora nije moja kwa moja kutoa taarifa ya mimi kushindwa kufika jana kwasababu simu yangu yenyewe nimeipoteza kwenye ajali ile na namba ya Teddy sikuwa nayo sehemu nyingine yeyote kwahiyo sikupata namna ya kuweza kuwasiliana nae isipokuwa kuja hapa nyumbani.”

    “Hakuna tatizo kijana wangu naomba uwe na amani kabisa maisha ndivyo yalivyo.”

    “Nashukuru sana wazazi wangu basi naomba niwaage niweze kuondoka, ila nitapanga siku nyingine rasmi nitakuja tena naomba msivunjike moyo kwasababu mimi ni kijana wenu sikupenda yaliyotokea yatokee ila ni kwasababu ya mipango ya Mungu.”

    “Usijali kijana wetu tunakukaribisha sana kwani hapa ni nyumbani mda wowote unaruhusiwa kufika.” Alizungumza baba huku akipeana mikono na Enrique.

    “Karibu sana jamani, mmekuja wakati mbaya kwasababu ndio tunaandaa chakula cha jioni.” Sauti ya mama ya ukarimu ilisikika wakati alipokuwa akipeana mikono na wageni wale.

    “Hamna shida mama, tutakula siku nyingine.”

    “Asanteni sana, muwafikishie salamu zetu za pole kwa msiba.”

    “Zimefika kabisa wazazi wangu.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Kigizagiza cha usoni Enrique waliondoka pale nyumbani na kuelekea kwake. Baada ya wao kuondoka nilibaki nahuzuni sana ndani ya nafsi yangu kutokana na mkasa aliyokuwa amepitia kipenda roho wangu.

    “Kweli mama uliniambia nisimuhukumu kijana wa watu kwasababu pengine anaweza akawa amepatwa na tatizo na kumbe ni kweli kabisa.” nilizungumza na mama huku nikihisi amani ndani ya moyo wangu kwasababu nilikuwa tayari nimekwisha kumuwazia vibaya kijana wa watu kumbe masikini hana hatia.

    “Ni kweli kabisa tena na mimi nilijawa na wasiwasi mwingi kwa kuwaza ni kwanini simu yake ilikuwa haipatikani nikaona basi pengine panaweza pakawepo na jambo zito.”

    “Ila nimemuonea huruma sana Enrique.”

    “Kiukweli inatia simanzi.”

    “Alafu anaonekana ni kijana mzuri tu mnyenyekevu na mstaarabu sana.” mama alitoa dukuduku lake la moyoni kuhusu mwonekano wa Enrique kwa mara ya kwanza machoni mwake tena akiwa katika hali ya ugonjwa.

    ***

    “Yaani mama huyu kijana hana shida kabisa ni mtu wa watu ila ndio hivyo anapitia mambo magumu sana kwasasa, kwasababu kuondokewa na rafiki mkubwa vile ni pigo kubwa sana kwake ila ndio hivyo kazi ya Mola haina makosa, mbele yake nyuma yetu hatuna budi kumuombea apumzike kwa amani.” Nilizungumza na mama kwa majonzi ndani ya moyo huku nikipembua mchele uliokuwa umeletwa na Enrique ili niweze kupika wali kwa mboga ya kisamvu ambayo mama alikuwa ameuandaa kwaajili ya kupikia ugali.

    Niliendelea kuandaa chakula na kilipoiva nilikwenda kukitenga mezani ili tuweze kula kwasababu mimi mwenyewe nilikuwa nikihisi njaa kutokana na kwamba tangu jana yake sikuwa nimeweka kitu chochote kinywani mwangu kama chakula, vyote viligoma kupita kwenye koo langu hadi maji ya kunywa kweli mapenzi mabaya sana asikwambie mtu.

    Tulipokuwa tunakula.

    “Mwanangu yule kijana anaonekana ni mtu mzuri kabisa tena asie na kasoro yeyote, yani nimemtazama kwa mara ya kwanza tu lakini nikaona ni mtu mzuri kabisa.” Ulikuwa ni mda wa baba kumwagia sifa Enrique kutokana na kwamba ni kijana ambae anaadabu kipita maelezo.

    “Ahsante sana baba.”

    “Amenifurahisha sana kwasababu vijana wa siku hizi wengi hawana adabu tunawaozesha tu mabinti zetu kwasababu hakuna namna ila huyu nimempenda kiukweli na nawaombea baraka nyingi maishani Mungu akawajalie familia yenye furaha na upendo.”

    “Asante.”

    “Siku nyingine atakaposema anakuja itabidi tummalizie kumchinja yule kuku mmoja aliebakia kusudi tuweze kumwonyesha kuwa na sisi tunampenda na kumjali na tumefurahishwa na ujio wake wa katika familia yetu.”

    “Mh sasa baba kwa maana hiyo lile banda la kuku si tutalifunga?”

    “Hilo sio tatizo, Mungu atatuletea kuku wengine.”

    “Sawa baba asante sana.” tulimaliza kula na kwenda kulala.

    Baada ya kimya cha wiki moja siku moja usiku wa manane siku yangu iliita na kunifanya nizinduke usingizini na kukuta ni Enrique ndie alikuwa akinipigia mda ule, japo kuwa nilifurahi kuona mpenzi wangu akinipigia lakini nilipatwa na wasiwasi kwanini amenitafuta usiku mnene namna ile.

    “Mambo vipi darling.”

    “Po…..a kabisa vipi unaendeleaje?” nilimjibu huku nikipiga miayo.

    “Naendelea vizuri kabisa.”

    “Jamani siku zote hizo kwanini hujanitafuta mapema kama ulivyokuwa umeniahidi.”

    ***

    Kiukweli nimenunua simu siku nne zilizopita baada ya mazishi ya rafiki yangu Richard ila nilikuwa nimesahau nilipokuwa nimeweka kile kikaratasi ulichokuwa umeniandikia namba zako siku zile nilipokuja nyumbani kwenu ila ndio nimekipata nikaona nikupigie usiku huuhuu ili niweze kusikia sauti yako mpenzi wangu.

    “Poleni sana, vipi mlimaliza mazishi salama.”

    “Tunamshukuru Mungu tumemaliza salama.”

    “Nilikuwa nasubiri uweze kunipigia simu ili tuweze kufahamu utaratibu wa mazishi unakuwaje kusudi tuweze kushiriki lakini ndio ukawa kimya.”

    “Kiukweli imeshindikana kwasababu hiyo niliokueleza mpenzi wangu ila hakuna tatizo kabisa tayari tumeshamlaza kwenye nyumba yake ya milele.”

    “Ok.”

    “Natumani unaendelea vema kabisa kwa sasa.”

    “Naam bila shaka nipo vizuri kabisa.”

    “Nafurahi kusikia hivyo.”

    “Vipi wazee hawajambo?”

    “Ni wazima kabisa hofu kwa hao wa kwako.”

    “Wanaendelea vizuri kabisa.”

    “Poa.”

    “Basi nikutakie usiku mwema tutawasiliana kesho.”

    “Asante usiku mwema na kwako pia.”

    “Nashukuru sana sweety.”

    Mawasiliano yetu yalianza rasmi tena kwa mara nyingine na nilizidi kuwa na furaha ndani ya moyo wangu kwasababu afya ya mpenzi wangu ilizidi kuimarika kila kukicha jambo ambalo lilizidi kunifanya niwe wa furaha kila siku ya maisha yangu. Nilizidi kuushuhudia upekee wa mpenzi wangu kwa namna ambavyo alikuwa akinipenda, kunithamini pamoja na kunijali sana, sikuchoka kumuombea kwa Mungu azidi kumpa afya njema na siku moja aje nyumbani rasmi kujitambulisha kuwa ndie mpenzi wangu na hatimae tufunge pingu za maisha.

    Mara baada ya kupona kabisa alinipigia simu na kunieleza kuwa muda wa kuja nyumbani kwetu ulikuwa umewadia kwa mara nyingine tena. Tulikubaliana na kupanga siku ili aweze kuja nyumbani, na baada ya kufikia muwafaka wa siku ya kuja alikuja kweli siku ilipofika.

    ***CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Nilijisikia furaha sana baada ya Enrique kijana ni mpendae kuliko kitu chochote kuja nyumbani kujitambulisha rasmi kuwa ndie mwanaume ambae anataka kunioa.

    Halikuwa na kipingamizi kwasababu baba na mama walikuwa wameshaonyesha kumridhia tangu walipomuona mara ya kwanza. Taratibu zote zilifuatwa za yeye kutoa mahari na mipango ya harusi ilianza. Kiukweli kilikuwa ni kipindi kizuri sana ambacho kilinifanya niwe na furaha kubwa ndani ya moyo wangu kuliko matukio yote yaliokuwa yamewai kupita katika maisha yangu.

    Tulizidi kusonga mbele katika safari yetu ya uchumba huku mipango ya harusi ikifanyika na kizuri zaidi ni kwamba ile ahadi yetu mimi na Enrique ya kutokufanya tendo la ndoa hadi muda wa kuoana utakapofika lilikuwa linakwenda kutimia kwasababu hakuna hata siku moja alionyesha kutaka kuivunja ile ahadi tuliyokuwa tumekubaliana baada ya kuingia kwenye mahusiano.

    “Ama kweli huyu kaka anakila sifa za kuitwa mwanaume kwasababu hatetereki katika maamuzi yake na pia habadili kiurahisi kile anachokuwa amekidhamiria.” Niliwaza siku mmoja baada ya kumaliza kuzungumza nae kwenye simu.

    Kutokana na hali ngumu ya maisha iliyokuwa ikiikabili familia yangu suala la wao kunifanyia sherehe ya mwago (send off) lilionekana kuwa mzigo mkubwa kupita kiasi, jambo ambalo liliniumiza sana kichwa kwa kuwaza itawezekana vipi wakati hali ya uchumi pale nyumbani ilikuwa ni tete sana.

    Enrique alinigharamia mavazi ya kuvaa ile siku ya mwago (send off) pamoja na wazazi wangu jambo ambalo lilinipa faraja sana. Niliogopa kumweleza kuwa kamati ya maandalizi kwa upande wa familia yangu ilikuwa kwenye wakati mgumu wa kukusanya mchango kutokana na kwamba watu wengi pia waliokuwa wanatuzunguka ni watu wa tabaka la chini kwahiyo ilikuwa ni changamoto kubwa na pia niliona isingeleta picha nzuri ya yeye kugharamia hadi sherehe yangu ya mwago.

    Nilishtuka sana siku moja alivyonipigia simu na kuniuliza.

    “Vipi maandalizi yamefikia wapi?”

    “Yanaendelea vizuri kiukweli.” Kwa aibu nilizungumza kwa kumuongopea kwasababu huku watu walikuwa wanalia shida vibaya sana.

    Safi sana jitahidini kufanya maandalizi mazuri kwasababu nitakuja na watu wangu wa heshima sana na kama kunasehemu mmekwama nijulisheni ili niweze kutafuta namna ya kufanya ufumbuzi mapema ili kila kitu kiweze kwenda sawa sawia.

    “Mmh!”

    “Mbona umeguna?”

    “Amna.”

    “Au kuna tatizo?”

    ***

    “Kiukweli maandalizi ya hapa nyumbani kwetu ni ya kawaida sana kwasababu wewe mwenyewe unafahamu hali ya hapa kwetu kuwa sio nzuri kiuchumi.”

    “Kwani mmekwama wapi?”

    “Mambo ni mengi yaliyoshindikana kutokana na pesa kidogo iliyopatikana kwenye mchango.”

    “Basi msijali nitawapatia kiasi kidogo ambacho kitaweza kuwasaidia katika hiyo bajeti yenu kusudi muweze kufanya kitu kitakachopendeza na wewe ufurahi mpenzi wangu au unasemaje laazizi wangu.”

    “Nimekwelewa Enrique lakini mbona naona kama kwa namna fulani utakuwa unajitesa?”

    “Usiwe na wasiwasi kwasababu siku zote hakuna mtu ambae kwa ridhaa yake anataka kufanya jambo ambalo lipo nje ya uwezo wake, namaanisha kuwa ninauwezo huo ndio maana nataka nitowe mchango wangu ili uweze kuwasaidia wala msiwe na wasiwasi kabisa.”

    “Nashukuru sana dia.”

    “Usijali.”

    Baada ya siku moja nilikutana na Enrique na alinipatia fedha taslimu milioni 8 na kunieleza kuwa zile ndio zitumike kuongezea bajeti ya fedha tuliyokuwa nayo ili kuandaa sherehe ambayo ilikuwa ifanyike wiki mbili baadae. Nilishikwa na butwaa ile siku aliyokuwa ananikabidhi zile pesa kwasababu pamoja na kwamba alitoa kwaajili ya kuongezea ile bajeti ya kwenye familia yangu bado ilikuwa imezidi sana pesa zilizokuwa zimepatikana katika familia yangu kwani kulikuwa na kiasi cha shilingi milioni mbili na laki tatu tu.

    Wazazi ndugu jamaa na marafiki walifurahi sana baada ya kijana yule kuzidi kuonyesha moyo wake wa kipekee katika kuwachangia kiasi kikubwa namna ile.

    Maandalizi yalizidi kufanyika na siku ilizidi kukaribia kwenye tukio la kihistoria katika maisha yangu jambo ambalo lilifanya afya yangu izidi kuwa nzuri kwasababu ya furaha niliyokuwa nayo ndani ya nafsi yangu ya kuolewa na kijana ambae ndie niliekuwa nimemwona ananifaa katika maisha yangu.

    Namshukuru sana Mungu siku ya mwago (send off) yangu ilifika na baadhi ya wageni kwa upande wa mme wangu mtarajiwa walifika pale nyumbani kwetu na walionekana kufurahi kupita kiasi kwa namna watu walivyokuwa na nyuso za furaha juu ya tukio lile la kipekee.

    Watu walikula na kunywa, nilifarijika sana kwasababu ulijitokeza umati mkubwa pale nyumbani ambao hakuna aliekuwa akitegemea na jambo jema zaidi ni kwamba watu wote waliofika pale nyumbani walipata chakula pamoja na vinywaji jambo ambalo liliwafanya wanitakie baraka nyingi kwenye ndoa yangu.

    Nilipata zawadi nyingi sana, kiukweli kunasherehe nyingi za mwago zilikuwa zimeshafanyika pale mtaani lakini ile yangu kila mtu alikuwa akisifia na kusema kwamba ndio sherehe ambayo ilikuwa ni nzuri kuliko zingine zote zilizowai kupita.

    ***

    Baada ya sherehe kumalizika ulikuwa ni muda maalumu kwa watu kucheza mziki, DJ aliekuwa akipiga mziki pale nyumbani ile siku alikuwa ni mahiri sana katika kazi ile kwasababu aliweza kuukonga moyo wa kila mtu aliekuwepo pale kwenye ile sherehe ambayo ilifanyikia nyumbaani kwetu.

    Vumbi lilifuka pale umbumbini pale ambapo vijana walipokuwa wanacheza mziki kwa mtindo wa wakuvutia sana unaoitwa kingaleloo ambao ni maarufu sana kwa mikoa ya kanda ya kaskazini, nilishindwa kujizuia na kujisogeza uwanjani baada ya DJ kuanza kupiga nyimbo za twisti. Nilifurahi sana ile siku na sikutamani hata kidogo ile siku iweze kupita kwasababu laiti ningekuwa nauwezo ningezuia ile siku isiishe kwasababu ilikuwa ni njema sana kwa upande wangu pamoja na ndugu zangu.

    Watu walicheza mziki hadi asubuhi pale nyumbani ingawa mimi niliwai kwenda kulala kwasababu nilikuwa nimechoka sana. Alibaki kaka yangu ambae aliamua kusimamia mziki ule ambao ulipigwa hadi saa kumi na mbili asubuhi.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Palipokucha ilikuwa ni siku ya ijumaa kwahiyo tulianza maandalizi mengine ya harusi ambayo ilikuwa inafanyika kesho yake siku ya jumamosi katika ukumbi maarufu sana mjini arusha ambao upo ndani ya viwanja vya nanenane unaoitwa Palace hall. Haikuweza kufanyika nyumbani kwa Enrique kwasababu hakuwa na eneo kubwa lakuweza kutosheleza wingi wa wageni ambao walikuwa waudhurue sherehe ile ya harusi. Nilitamani ile siku ifike haraka ili niingie katika maisha ya ndoa ambayo huwa nasikia wengine wakisema ni matamu na wengine walikuwa wakisema ni machungu kwahiyo nilikuwa njia panda sielewi kwamba mimi nitakapoingia katika ndoa yangu nitafurahia ama la, ila nilijipa moyo kwasababu mwanaume niliekuwa nimempata kwa mda wote niliokuwa nae nimemwona anakila sifa ya kuitwa mme.

    Sikupata usingizi kabisa siku ya kuamkia sherehe yangu ya arusi, kila mara nilikuwa nashtuka usingizini nachungulia dirishani kama pamekucha au bado, niliona usiku wa siku zile ulikuwa ni mrefu sana kuliko kawaida kwasababu nilikuwa nikizinduka kila mara. Hakika nilikuwa na shauku sana ya kuvaa shela la harusi ambalo lilikuwa limeagizwa pamoja na suti ya mme wangu mtarajiwa kutoka Nairobi Kenya.

    ***

    Siku ya harusi ilifika, kwenye mida ya saa nne nilikwenda saluni kutengeneza nywele zangu pamoja na kuwekwa katika hali ya mvuto zaidi kwa vipodozi mbalimbali, wale waudumu wa ile saluni niliyokuwa nimekwenda walionekana kuwa na ustadi mkubwa sana katika kazi ile ya kumremba binti akarembeka. Baada ya hapo nilidumbukia ndani shela huku nje nikiwa nasubiriwa na gari ambalo lilionekana kuwa la kifahari sana ambalo lilitumwa na mme wangu lije kunichukua linipeleke kanisani, kusema kweli licha ya kwamba kila mtu alikuwa akinisifia kuwa shela lile lilikuwa limenikaa barabara lakini hata mimi mwenyewe niliridhika kwa namna ambavyo nilikuwa nimependeza, japokuwa uzuri nao niliokuwa nimejaliwa na Mungu ulichangia kwa kiasi kikubwa kuonekana kama malaika alietorokaa peponi.

    Baada ya kuvaa shela lile ambalo lilimfanya kila aliekuwa ananiona anitamani kwajinsi nilivyokuwa na mvuto kama pesa, nilivishwa mkufu wa dhahabu shingoni mwangu, hereini, pamoja na saa ya mkononi ambavyo vilikuwa vya gharama kubwa na vyote vilikuwa ni vya dhahabu, chini nikavalia viatu ambavyo vilikuwa virefu kiasi lakini vyenye mvuto sana ambavyo vyote vilinunuliwa nje ya nchi, na baada ya hapo nilijipulizia marashi yenye harufu nzuri sana iitwayo Annick Goutal Eud’Hadrien marashi ya bei ghali sana niliyokuwa nimeletewa na mpenzi wangu siku chache kabla ya harusi na kunieleza kuwa alitaka siku ya harusi yangu ninukie marashi yale ambayo alinieleza alinunua kwa gharama zaidi ya laki saba.

    Nilipendeza hadi nikawa najionea wivu mwenyewe. Nilipomaliza kujiandaa nilikwenda nje na kupanda kwenye gari ambalo lilikuwa limerembwa sana kwa kutiwa nakshi kila kona, na ndani ya gari kulikuwa na harufu nzuri sana, pamoja na mziki mlaini wa injili, na ubaridi wa AC uliokuwa ukipuliza taratibu. Nilihisi kama nipo peponi vile kwajinsi nilivyokuwa najiona nakujisikia murua kuliko siku zingine nilizokuwa nimepitia katika maisha yangu.



    Kabla dereva hajawasha gari nilimweleza kuwa asubiri kwanza niwasiliane na mchumba wangu ili niweze kufahamu kama ameshamaliza kujiandaa.

    “Haloo dia habari ya wewe.”

    “Njema tu vipi tayari umeshajiandaa?” Ilisikika sauti ya Enrique ikiwa na kila dalili ya furaha.

    “Yeah, nipo tayari mpenzi wangu.” Nilimjibu huku nikijiangalia kwenye kioo kidogo nilichokuwa nacho kwenye pochi japokuwa muda huohuo nilikuwa nimetoka kujiangalia kwenye kioo kikubwa cha saluni lakini nilikuwa natamani niwe najiona kila saa kwa naamna ambavyo nilikuwa nimependeza.

    “Ok fine yani kama nakuona vile umependeza sana angalia wasikuibe mpenzi wangu kwasababu nitachanganyikiwa kwa jinsi ninavyokupenda.” Alizungumza kwa kunitania kwasababu alikuwa hanioni ila kwasababu alikuwa anafahamu kuwa huwa ninapovaa huwa napendeza kupita kawaida, kwahiyo moja kwa moja alijua ile siku ya harusi kwasababu nitakuwa nimeongeza na kujipodoa kwahiyo alijua lazima kila mwanaume atakaenitazama ni lazima moyo ubadili mapigo.

    “Hahaha!” nilijikuta nacheka kwasababu Enrique alikuwa anapenda sana utani japokuwa pia alikuwa anawivu.

    “Ok sawa basi tukutane kanisani, kwasababu na mimi ndio nimemaliza kujiandaa muda sio mrefu.”

    Gari liliwashwa kwa mwendo wa taratibu sana tulianza safari ya kuelekea kanisani kwenda kufunga pingu za maisha. Baada ya kufika katika kanisa la Lutherani njiro ambapo ndio alipokuwa akisali mme wangu nilimkuta tayari ameshafika na tulikumbatiana kwa furaha sana kwasababu tuliona lile lengo letu la kuona lilikuwa linatimia.

    “Oo my God you have shine like a morning star.” (Unangara kama nyota ya alfajiri.) sauti ya mume wangu mtarajiwa ilisikika ikinimwagia sifaa lukuki juu ya muonekano wangu kwa wakati ule.

    Thanks baby, you have shine too.” (Asante sana umependeza pia mpenzi.)

    “Thank you.” (Asante)

    Kengele iligongwa ya kuingia kanisani kiukweli nilikuwa na furaha sana kwasababu mme wangu alikuwa amependeza sana pamoja na wazamini wetu wa ndoa na kusababisha kila mtu alikuwepo pale kanisani kusuprise kwa namna ambavyo tulikuwa na muonekano mzuri wa kuvutia. Tulipendeza sana na pia tulikuwa tunaendana sana na Enrique kwasababu mimi nilikuwa mweupe kama theluji na yeye alikuwa mweusi wa kuteleza na pia alikuwa mrefu kidogo kuliko mimi na hakuwa mnene wala mwembamba alikuwa wa wastani.

    ***

    Ibada ilianza na Mungu alizidi kuwa upande wetu kwasababu kila kitu kilikuwa kinakwenda vizuri kabisa. Na furaha yangu ilivuka kiwango baada ya kumaliza kula viapo vya ndoa na watu waliokuwepo kanisani walishangilia kwa furaha sana. ilikuwa ni siku ambayo nilikuwa ya kipekee sana kwasababu watu wengi huwa wanatamani sana kufanya lakini kutokana na sababu mbalimbali ilishindikana kwahiyo nilikuwa na kila sababu ya kufurahi na kumtukuza Mungu wangu kwa baraka ile njema aliyoishusha maishani mwangu ya kukutana na kijana niliempenda na yeye kunipenda na kuamua kufunga nae pingu za maisha.

    Mchungaji alitutakia baraka nyingi maishani na tuliondoka kanisani kuelekea katika ukumbi uliokuwa umeandaliwa na kwaajili ya tukio lile la kihistoria katika maisha yetu. Wapiga picha walituandama sana katika kutuchukua picha mbalimbali kwaajili ya kumbukumbu.

    Nilijisikia vizuri sana hasa kwajinsi tulivyokuwa tukisifiwa kwa namna ambavyo tulikuwa tumependeza kupita kiasi. Tulipiga picha mbalimbali katika maeneo tofauti tofauti kabla ya kufika ukumbini. Kila mtu aliekuwa amejumuika na sisi katika simu ile kiukweli walionekana kuwa na nyuso za furaha sana jambo ambalo lilinifanya na mimi nisiishiwe na tabasamu usoni mwangu.

    Tuliingia ukumbini jioni kabisa kwenye kigizagiza cha usoni huku mziki mnene ukiwa unatumbuiza ukumbini pale lakini nilishikwa na butwaa kwa namna ukumbi ule ulivyokuwa umepambwa kwa namna ambayo sikuwai kushuhudia katika sherehe yeyote tangu nizaliwe.

    Nilifurahi sana na kumkumbatia mpenzi wangu kwa ile heshima aliyokuwa amenionyesha kwani ilikuwa ni sherehe ya kipekee sana.

    “Asante sana mme wangu kwa namna ambavyo umejitahidi kuifanya hii siku iwe siku ya tofauti na zingine maishani mwangu hakika nashukuru sana.” nilizungumza kwa kwa sauti ya chini sana na mume wangu tulipokuwa tumekaa mbele ya ukumbi ule uliokuwa umepambwa kwa namna ya kisasa kabisa.

    “Usijali baby.”

    Mshehereshaji (MC) alikuwepo pale ukumbini alikuwa ni mcheshi sana na alionekana kuwa na uzoefu mkubwa na kazi yake kutokana na namna ambavyo alikuwa akizikonga nyoyo za wageni waliekuwepo ukumbini pale kwa kuwavunja mbavu kwa namna alivyokuwa fundi wa kuchekesha. Mimi mwenyewe nilikuwa nikicheka hadi machozi yananitoka kwa namna ambavyo yule mshehereshaji alivyokuwa mtundu.

    Meza zote zilizokuwepo pale ukumbini zilikuwa zimepambwa kwa vinywaji mbalimbali na kuzungukwa na viti vizuri vilivyokuwa vimerembwa na namna ya kuvutia sana. ile siku ilikuwa ni siku nzuri japo kuwa siku ya mwago wangu niliona ni siku nzuri sana lakini hii siku ya harusi ndio ilikuwa na kila sababu ya kusifiwa na namna ilivyokuwa nzuri.

    ***CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Muda wa zawadi ulifika na nilizidi kushangaa kwa namna ambavyo watu walituonyesha upendo wao kwa kutuzawadia zawadi mbalimbali. Baba mkwe na mama mkwe walitupa zawadi ya vyumba vitano vya biashara vilivyopo mjini Arusha, pamoja na shamba la maji hekari mbili. Wafanyakazi wenzake na mume wangu walitoa fedha taslimu milioni 7 pamoja na kutugharamia fungate (honeymoon) kwa muda wa wiki moja katika hoteli yeyote mkoa wa Arusha.

    Ndugu jamaa na marafiki walituzawadia sana fedha taslimu pamoja na zawadi zingine kama majokofu, mashine ya kufulia nguo, music system pamoja na vitu vingine vingi sana vyenye thamani kubwa.

    “Kweli mume wangu ni mtu wa watu.” Niliwaza kwa namna ambavyo msururu wa watu walivyokuwa unamiminika mbele ya ukumbi kuja kutuzawadia.

    Licha ya kwamba nilifurahi sana lakini pia hata ndugu zangu ambao walikuwa wamefika ukumbini pale walionekana kuwa na nyuso za furaha sana kwa namna ambavyo sherehe ilivyokuwa imeandaliwa kwa namna ya kisasa. Kamati ya harusi ilionekana kuwa makini sana katika kuhakikisha mambo yanakwenda sawa pale ukumbini.

    Baada ya zawadi ulikuja mda mwingine mzuri sana ambao ni mtu wa chakula, mahadhi ya mziki yalibadilika na kuanza kwenda kwa mdundo wa taratibu, bwana na bibi harusi ndio tulipewa nafasi ya upendeleo kuwa wa kwanza kusogea kwenye meza ya kuchukulia chakula halafu ndio wakafuata na watu wengine. Ingawa ukumbi ulikuwa umefurika watu lakini kila mtu aliefika ukumbini pale alikula na kusaza na pia vyakula na vinywaji vilibaki.

    Watu walipomaliza kula ulifuata muda wa watu kulisakata rumba kwa muda pale ukumbini, Mshehereshaji (MC) alimuamuru DJ afungue mziki mmoja mzuri halafu bwana na bibi harusi wafungue kwa kunyanyuka na kuanza kucheza.

    Nilikuwa naona aibu lakini baada ya DJ kuweka wimbo wa wasanii maarufu wa Nigeria maarufu kwa jina la P square “no one like you” nilijikuta napandwa na morali na kunyanyuka na mme wangu na kuanza kuzungusha nyonga zangu kwa madaha. Nilijisikia raha sana pindi mme wangu alivyokuwa anacheza huku amenishika kiunoni, ilipendeza sana na kusababisha ukumbi unyanyuke kwa nderemo na vifisho.

    “Its true baby no one like you.”(kweli kabisa mpenzi hakuna mwingine kama wewe.) mpenzi wangu alininong’oneza wakati tulipokuwa tunacheza mziki.

    “Thank you sweety.” (asante mpenzi.)

    “I love you.”

    “I love you too honey.”

    ***

    Baada ya wimbo huo mshehereshaji aliwakaribisha watu wote ambao walikuwa tayari kuja mbele kucheza pamoja na bwana na bibi harusi na ndipo watu walisogea mbele na kujumuka nasi katika kucheza mziki, ilikuwa ni siku ya furaha sana kwasababu nilifurahi mno mimi pamoja na mme wangu. Tulicheza kwa muda mfupi na tulirudi kukaa katika viti vyetu na kushuhudia jinsi ambavyo watu walikuwa wakicheza kwa mitindo tofautitofauti ya kuvutia.

    Baada ya sherehe kumalizika ilikuwa muda wa mimi na mme wangu kuondoka ukumbini pale kwenda fungate (honeymoon) ambayo ilikuwa ni sehemu ya zawadi ya kampuni aliyokuwa akifanya kazi mume wangu.

    Mume wangu alichagua hoteli nzuri ya kitalii iitwayo “Ngurdoto mountain lodge” iliyopo nje kidogo ya jiji la arusha.

    Simu ilipigwa usiku hulehule kuulizia kama tutapata nafasi katika ile hoteli ambayo mume wangu alikuwa ameichagua na kwabahati nzuri nafasi zilikuwepo.

    Nilifurahi sana baada ya kusikia kuwa nafasi itakuwepo katika ile hoteli ambayo mume wangu alikuwa ameichagua kwasababu ni hoteli ambayo nilikuwa natamani siku moja kufika kwasababu ni hoteli ambayo huwa inasifiwa sana kwa kuwa na huduma nzuri na mazingira ya kuvutia sana tofauti na hoteli zingine.

    Mkurugenzi wa mume wangu alitukabidhi hundi ya milioni ishirini kwaajili ya kugharamia fungate yetu kwa muda wa siku saba katika hoteli ile tuliyokuwa tumeamua mimi na mume wangu kwenda kupumzika na kufurahia uchanga wetu kwenye maisha ya ndoa.

    Mimi na mume wangu, na wazamini wetu wa ndoa pamoja na dereva aliekuwa amekodishwaa kutuendesha kwa siku ile maalumu tulianza safari kutokea pale ukumbini mida ya saa sita usiku kuelekea hotelini huku sura zeru zikidhihirisha furaha kubwa iliyokuwepo mioyoni mwetu.

    Macho yangu yalivutiwa sana na mazingira ya pale hotelini jambo ambalo lilinifanya niwe nashanga sana mambo mengi mageni niliyokuwa nayaona pale hotelini. Nilifurahishwa zaidi kwa namna ambavyo wahudumu wa ile hoteli walivyokuwa wakarimu sana.

    “Karibuni sana.” ilisikika sauti ya binti mmoja mrembo na wakuvutia aliekuwepo mapokezi.

    “Asante sana.”

    “Nahitaji chumba kizuri cha kupumzika mimi na mpenzi wangu kwa muda wa wiki moja.” Alizungumza mme wangu.

    “Karibuni sana, hapa gharama za vyumba vimegawanyika mara tatu yaani daraja la chini la kati na la juu.”

    Sasa wewe sijui ungependelea daraja lipi.”

    “Ningefahamu gharama pamoja na sifa ya kila daraja ili niweze kujua ningependezwa na daraja lipi.” Mume wangu alizidi kutoa maelezo pale mapokezi huku nikiwa pembeni na wadhamini wetu walioamua kutusindikiza hotelini pale usiku ule.

    ***

    “Sawa kwa daraja la kawaida yaani daraja la chini chumba cha kulala ninyi watu wawili ni dola 180 kwa siku ambayo ni sawa na shilingi 378,000, ila kwasababu mnataka kwa wiki itakuwa ni dola 1,260 ambayo kwa pesa zetu ni shilingi 2,646,000”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    “Kwa daraja la kati chumba pamoja na huduma ya breakfast ni dola 220 kwa siku ambayo kwa pesa za kitanzania ni shilingi 462,000 kwa wiki itakuwa ni dola 1,540 ambayo kwa pesa za kitanzania ni shilingi 3,234,000”

    “Daraja la juu kabisa ambayo ni (presidencial class) gharama ya chumba pamoja na breakfast kwa siku ni dola 1200 ambayo kwa pesa zetu ni shilingi 2,520,000 kwa wiki itakuwa ni dola 8400 ambayo kwa pesa za kitanzania ni shilingi 17,640,000”

    “Karibuni sana.” hivyo ndivyo muudumu alivyomaliza kutoa muhtasari wa malipo, kiukweli nilikuwa nashtuka sana nilipokuwa nikisikia anavyotaja zile gharama kwasababu ilikuwa ni pesa nyingi sana ambazo zilikuwa zinatakiwa kutumika kwa muda mfupi mno.

    Embu tushaurini wadhamini wangu kati ya daraja la kati na la juu tuchukue lipi?” mume wangu alizungumza kuomba ushauri.

    “Hii ni siku yenu ya pekee na haitajirudia tena kwenye maisha yenu kwa maana hiyo mimi nawashauri mchukue daraja la juu kabisa kwasababu gharama zake tunaweza kuzimudu kabisa.” Sauti ya baba mdhamini ilisikika ikitutaka tuchukue daraja la juu kutokana na upekee wa siku ile katika maisha yetu.

    Nilijisikia furaha sana kwasababu sikuwai kutegemea kwamba ipo siku hata mimi binti nilietoka katika familia masikini na pia nisie na elimu kabisa kwamba ipo siku nitalala katika hoteli yenye hadhi ya kulala raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania.

    Au unasemaje mke wangu.” Enrique alinijumuisha kwenye maongezi.

    “Sawa ila hizo gharama ni kubwa mno kwanini tusichukue hilo daraja la kati.” Nilizungumza ingawa moyoni nilikuwa natamani kulala katika lile daraja la juu kabisa kwasababu nilijua hata kwenye ukoo wetu ningekuwa nimeweka rekodi ya kuwa mtu wa kwanza kulala katika sehemu ya bei ghali kuliko ndugu zangu wote ila nilijishauwa ili nisionekane napenda starehe.

    “Usijali mke wangu kwasababu hizi gharama nalipiwa na kampuni ninayofanya kazi sisi tutagharamia chakula cha mchana na usiku kila siku na ninauwezo huo kabisa.” Alizungumza mume wangu kama kunikumbusha kuwa zile gharama tulikuwa hatulipi wenyewe.

    “Sawa nimekwelewa.” Nilionyesha kukubali kwa shingo upande ingawa moyoni nilikuwa nafuraha.

    Baada ya kukamilisha malipo, tuliagana na wadhamini wetu wa ndoa na wao walianza safari ya kurudi nyumbani kwao sanawari.

    “Tunashukuru sana jamani kwa upendo wenu hatuna cha kuwalipa ila tunawaombea kwa Mungu azidi kuwabariki.” Alizungumza mume wangu kuwashukuru wale wadhamini wetu.

    ***

    “Msijali kabisa tunawatakia fungate njema na Mungu awabariki sana.” mama mdhamini alizungumza kwa furaha wakati alipokuwa akituaga kwa kutushika mikono.

    Wakati tulipokuwa tukielekea katika chumba ambacho tulikuwa tumekilipia niliona nimshukuru mume wangu kwa kunipenda na kunijali.

    “Asante sana mume wangu.” Nilimshukuru kwa moyo mkunjufu kwa namna ambavyo aliweza kuifanya ile siku yangu kuwa siku ya kihistoria kabisa katika maisha yangu.

    Baada ya kufika chumbani nilifurahi sana kwasababu chumba kilikuwa ni kizuri kuliko kawaida, pamoja na kwamba ilikuwa ni usiku mnene lakini sikuhisi kabisa usingizi kutokana na furaha kubwa niliyokuwa nayo mimi na mume wangu mpenzi.

    Mara baada tu ya kuingia chumbani Enrique alionyesha kuwa na hamu sana na mimi kwasababu alianza kunitomasa sehemu mbalimbali za mwili wangu huku akininyonya dend*, mzuka ulizidi kunipanda na kusababisha nimvue koti la suti alilokuwa amevaa ili tuweze kupeana raha, bila kuchelewa alianza kuzisasambua zile nguo nilizokuwa nimevaa moja baada ya nyingine kitendo kile kilisababisha mapigo yangu ya moyo kubadili mwendo nakuanza kwenda kasi kwanamna ambavyo hisia za kimapenzi zilivyokuwa zikinipanda kwa kasi ya ajabu.

    Baada ya kunivua nguo zote na yeye alionyesha kupagawa sana kwasababu alimalizia kuzivua za kwake ndani ya sekunde kadhaa na kwa mara ya kwanza nikashuhudia muhogo wa mume wangu ukiwa umesimama kama mnara.

    “Ooh baby come over me please.”(tafadhali njoo juu yangu mpenzi) Nilijikuta natamka baada ya kuutamani muhogo wa Enrique uliokuwa umenyanyuka kwa manjonjo ya kunilaki.

    Enrique hakunisikiliza kwani alikuwa bize akicheza na ch*chu zangu na kizidi kunichanganya kabisa kwasababu huwa napandwa na mzuka sana mwanaume anavyokuwa akicheza na maziwa yangu.

    Aliposhuhudia kuwa nilikuwa nimelegea kupita kiasi aliingia katikati ya miguu yangu na kuanza kujimegea kitumbua polepole bila papara, nilikuwa najisikia msisimko mkali sana zaidi wa ule wa cocacola kwa namna ambavyo nilikuwa nafaidi penzi la mume wangu. Kutokana na utamu niliokuwa nikiuhisi nilinyanyua miguu juu na kuzidi kupanua mapaja yangu kuusikilizia muhogo ule ambao ulikuwa ukipasua mawimbi ipasavyo.

    “Oo yeah oo yeah.” Nilishindwa kuzuia pumzi na sauti za kimahaba zilizokuwa zikinitoka kutokana na utamu niliokuwa nikiuhisi kutokana na ule mchezo tuliokuwa tukiucheza pale kitandani na mwanaume wa ndoto zangu.

    Baada ya muda mfupi mume wangu alipata goli lake la kwanza wakati mimi nilikuwa namzidi kwa bao moja zaidi. Alionyesha kuchoka sana baada ya kuupata ushindi ule ingawa mimi bado nilikuwa nahitaji kuendelea kupata magoli mengine kwasababu mechi ile ilisubiriwa kwa muda mrefu sana na pia imegharimu maandalizi makubwa mno hadi wachezaji tukaingia uwanjani.

    ***

    Mume wangu alitoka uwanjani akidai awezi kuendelea tena na mechi kwasababu alikuwa amechoka sana nilijisikia vibaya kidogo kwasababu bado nilikuwa nauhitaji lakini kwasababu ni kweli ile siku tulikuwa tumechoka kweli nilijitahidi kumwelewa na hatimae tulikwenda bafuni kuoga na tulirudi kulala.

    “Kumbe fungate ndio huwaga hivi!” nilijisemea kimyakimya wakati tulipokuwa tukicheza na mume wangu kitandani baada ya kutoka kuoga.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Sababu ya uchovu tuliokuwa nao na pia tulichelewa sana kulala tuliamka mida ya saa tatu asubuhi tukiwa bado na uchovu. Tulipata breakfast na tukapanda tena kitandani, kwasababu usiku sikutosheka nilianza kumchokoza mume wangu kwa kushika muhogo wake ambao ulikuwa bado umelala lakini baada ya kuushika ulianza kunyanyuka taratibu.

    “Bwana mimi jana sikutosheka nataka tena.” Nilizungumza na mume wangu kwasauti ya chini na ya kudeka.

    Mume wangu alinivua lile pajama nililokuwa nimevaa nakuanza kunipagawisha kwa namna ambavyo alikuwa fundi wa kumwandaa mwanamke kwa muda mrefu kabla ya kumuingilia.

    Duu! asikwambie mtu nilipandwa na mashetani kwasababu maandalizi ya asubuhi ile yalikuwa ni makubwa kuliko ya jana kwani alinikoj*za viwili na ndipo akaanza kumega kitumbua kwa ustadi wa hali ya juu.

    Zoezi lilionekana kuwa gumu tena baada ya goli la kwanza la mume wangu kwani alishindwa kabisa kuendelea na mechi lakini alijitetea na kunieleza kuwa bado alikuwa anajihisi mchovu.

    Kiukweli ilikuwa ni wakati mgumu kwangu kwasababu goli lake la kwanza ndio kwanza lilikuwa linanisisimua na kunifanya nimkumbatie kwa nguvu ili namimi angalau niweze kufaidi zaidi lakini ilishindikana.

    “Kwanini aishie kwenye goli la kwanza wakati mimi sijatosheka?” Niliwaza wakati nilipokuwa nikimtazama Enrique wangu akiwa amejilaza kando yangu akionekana kuchoka sana.

    “Mmh hawezekani ngoja niendelee kuuchezea muhogo wake pengine unaweza kunyanyuka tena.” Niliwaza huku mkono wangu nikiupeleka katika karoti lake na kuanza kuuchezea ili uweze kunyanyuka lakini haikuwezekana.

    “Ngoja nimwache kwasababu labda niuchovu kama alivyonieleza.” Nilizidi kuwaza baada ya jitihada zangu kugonga ukuta.

    Hoteli ile ilikuwa na mazingira mazuri sana gadeni zilikuwa na ukijani ulikoza bwawa kubwa na zuri sana kwaajili yaa kuogelea na maua yalionekana kuchanua na kusababisha hali ya hewa kuwa nzuri sana, vinywaji vya aina mbalimbali pamoja na vyakula cha kila aina vilipatikana achilia mbali yote hayo palikuwa na ulinzi wa hali ya juu kuhakikisha kwamba wageni wanakuwa katika hali ya ulinzi na usalama. Licha ya kupatikana kwa hayo yote furaha yangu ilishindwa kukamilika kutokana na kwamba mume wangu alishindwa kunitimizia haja yangu ya mapenzi kwa ule mda mfupi ambao tulikuwa tumefika pale hotelini.

    Licha ya kuhakikisha kuwa anashiba kabisa lakini bado hali ilionekana kuwa ileile nakunisababishia kujiuliza maswali mengi sana akilini mwangu.

    “Au ni haya mazingira ndio hajayozoea?”

    “Au ni kwamba mimi ndio sina ufundi?”

    “Au pengine labda mume wangu hapati chakula cha kushiba?”

    “Au ni mgonjwa anaumwa halafu anaogopa kunieleza?”

    “Mbona yule kijana niliekuwa nae mwanzoni alikuwa anauweza mchezo vizuri hadi namwambia mwenyewe nimetosheka lakini hapa sivyo?” nilijiuliza maswali mengi sana ndani ya kichwa changu lakini sikupata jibu la mume wangu kushindwa kunitimizia kwa zile ssiku chache tulizokuwa pale hotelini. Kwasababu nilijua ni mara ya kwanza yeye kulala na mimi katika kitanda kimoja ndivyo ambavyo nilifikiri atakuwa na hamu na mimi zaidi kama ilivyokuwa kwa upande wangu.



    Wiki moja ilikatika pale hotelini nikiwa katika msongo mkubwa wa mawazo kwasababu ya uwezo hafifu ya mume wangu kitandani. Haikuwa kama nilivyokuwa nikihadithiwa na mashoga zangu jinsi fungate yao ilivyokuwa nzuri japo kuwa mazingira yalitofautiana. Ujuzi wote niliopewa katika sherehe mfundo niliutumia ili kuhakikisha nampagawisha mume wangu kitandani ila bado uwezo wa muwe wangu ulishindwa kujibainibisha katika hali ya kuridhisha.

    Kiukweli mume wangu alikuwa na maisha mazuri sana na alinipenda na kunijali sana kwasababu nilipata kila kitu nilichokuwa nakihitaji, na nilikwenda popote nilipohitaji kwenda, nilikula na kunywa chochote nilichohitaji, maisha yalikuwa ni mazuri japo kuwa nafsi yangu haikuridhika kabisa kwa kukosa kitu kimoja cha muhimu sana ambacho ni penzi la kuniridhisha kutoka kwa mume wangu kwasababu nilijifananisha na mtu mwenye kiu sana ambae anahitaji maji ya kunywa lakini kwa bahati mbaya akapata maji machache ambayo hayatoshi kukata kiu yake.

    Nilijitahidi kuwa mbunifu sana ili mume wangu aweze kuongeza ufanisi lakini ilishindikana kabisa na kunisababishia kutingwa na mawazo kila wakati ndani ya ubongo wangu.

    “Je nikimweleza atanielewa vipi?”

    “Naogopa kumweleza kuwa sitosheki kwa penzi lake ila sina budi kuzungumza nae ili tutafute suluhisho. Kwasababu haiwezekani awe na tabia za jogoo angali ni binadamu na tena wakati mwingine jogoo huonekana kuwa na bidii ili aweze kumridhisha kuku mtetea.” yalikuwa ni mawazo yangu siku moja baada ya kuagana na mume wangu alipokuwa anakwenda kazini.

    Jioni aliporudi akitokea kazini bado nilikosa ujasiri wa kuweza kumshirikisha katika lile suala kutokana na hofu iliyokuwa imenijaa kwa kuwaza kwamba ataniona vipi au atanielewa vipi. Ilinibidi niendelee kutengeneza mazingira ya kumweleza ili nisimuathiri kisaikolojia baada ya kumweleza.

    ***

    Baada ya miezi mitatu bado nilikuwa sijaona dalili kabisa ya ujauzito katika mwili mwangu ingawa nilikuwa situmii kinga yeyote ya kuzuia mimba. Kichwa changu kilishindwa kupumzika kuwaza kwasababu niliona kama lile lilikuwa ni tatizo lingine ambalo sikujua dhahiri litakuwa ni tatizo lake au langu.

    Siku moja nilikerekeka sana baada ya kuona kwamba mume wangu kutoniridhisha kimapenzi imekuwa kama tabia kwahiyo niliamua kuzungumza nae ili tuweze kutafuta suluhisho kwa wataalamu wa afya kwasababu haikuwa hali ya kawaida.

    “Mume wangu yani pale unapoanzaga kunikuna ndio unasitisha zoezi inamana ni unashindwa kabisa kuendelea au tatizo ni nini kipenzi changu kwasababu kama hivi sijatosheka kabisa.” Nilizungumza kwa sauti ya kimahaba wakati nilipokuwa nimelaza kichwa changu juu ya kifua chake baada ya tendo la ndoa.

    “Mke wangu unajua raha ya hili tendo lifanyike kwa afya na sio kama kukomoana au kama kazi.”

    “Nikweli mume wangu lakini tendo hili ni sehemu ya maisha yetu ya ndoa kwahiyo kila mtu ana budi kuhakikisha kwamba anamridhisha mwenzie.”

    “Inamana unataka uniambie kuwa haujaridhika?”

    “Ndio mume wangu sijaridhika kabisa.”

    “Lakini mbona siku zingine ndio huwa tunafanya hivi iwaje leo uniambie kuwa hujaridhika?”

    “Hapana sijamaanisha kuwa leo tu ndio sijaridhika ila ni mara kwa mara huwa siridhiki.”

    “Sasa mbona siku zote hizo hujanieleza kuwa huridhiki leo baada ya miezi kadhaa ndio unazungumza jambo kama hilo.?”

    “kwasababu mara ya kwanza ulikuwa unaniambia kuwa ni uchovu ndio ulikuwa unasababisha usinitosheleze.”

    “Naomba unielewe tafadhali mapenzi yetu tufanye kwa afya na sio kukomoana.”

    “Sawa nimekwelewa.” Nilimwitikia ingawa nilikuwa najisikia uchungu mkubwa ndani ya moyo wangu kutokana na lile jibu alilokuwa amenipatia.

    Kutokana na hasira iliyokuwa imenipanda nilishindwa kabisa kupata usingizi na kupelekea akili yangu kudumbukia katika mawazo mengi sana ambayo yalinipelekea kuumwa kichwa sana usiku ule.

    “Sasa kama hali itakuwa ndio hivi itakuwaje?” niliwaza wakati mume wangu alipokuwa pembeni yangu akikoroma baada ya kupitiwa na usingizi. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Ee mungu nisaidie kwasababu sipo tayari kumsaliti mume wangu kabisa hata siku moja katika maisha yangu kwasababu ninampenda kuliko kitu chochote hapa duniani na yeye naamini ananipenda sana kwahiyo sina budi kuvumilia hali hii kwa kadiri ya uwezo wangu.

    ***

    Nilijitahidi kukabiliana na hali ya mume wangu kwa kile kidogo aalichokuwa ananipatia kwa mtazamo wake kwamba ni kwa afya ingawa kwa upande wangu niliona kama alikuwa ananinyanyasa kwa kutonipatia haki yangu ya ndoa ipasavyo.

    Siku zilizidi kwenda nikijitahidi kuwa mwaminifu kwa mume wangu ingawa nilikuwa kwenye wakati mgumu sana. Akili yangu haikuwa imetulia ipasavyo kwasababu siku zilizidi kusonga bila kuona dalili yeyote ya kuwa na mimba.

    Nilikosa amani kabisa ndani ya moyo wangu kibaya zaidi ni kwamba nilianza kusikia chokochoko za maneno kutoka kwa ndungu wa mume wangu wakinisema kwamba mimi ni mgumba ambae namfilisi ndugu yao kwa kula na kunywa bure.

    “Hivi inamana kweli mimi ni mgumba au tatizo ni la mume wangu?” nijiuliza siku moja nilipokuwa chumbani kwangu peke yangu nikilia kwa uchungu baada ya kusikia kuwa ndugu wa mume wangu wamechachamaa kwa maneno hususani wifi zangu.

    Mume wangu nae nilimwona kaanza kubadilika kwasabaabu alianza kutonijali tena, nikimuuliza jambo ananijibu kwa kifupi sana wakati mwingine anadiriki kunifokea bila sababu ya msingi jambo ambalo halikuwa la kawaida kabisa kwake. Pamoja na yote hayo nilijitahidi kuwa mpole na sikujaribu kufungua kabisa mdomo wangu kwa ndugu wa mume wangu wala kwa mume wangu kwasababu ya upendo wa dhati niliokuwaa nao kwa mume wangu kwahiyo nilizidi kumpenda na kumuheshimu.

    Muda wa mume wangu kurejea nyumbani kutokea kazini kwa kawaida ni jioni ya saa kumi na mbili na akichelewa sana ni jioni saa moja ila siku moja nilishangaa sana kwasababu ilitimu mida ya saa tano usiku hajarudi nyumbani na wala simu yake ya mkononi ilikuwa haipatikani, niljaribu kuwasiliana na rafiki yake mkubwa ambae alikuwa akifanya nae kazi sehemu moja lakini nae simu yake haikupatikana. Niliingiwa na wasiwasi mwingi ndani ya nafsi yangu kwa kuwaza mume wangu atakuwa amepatwa na tatizo gani ile siku hadi achelewa kurudi nyumbani kiasi kile.

    Sikukata tamaa nilizidi kusubiri nikiwa nimekaa sebuleni huku akili yangu ikakataa kutoa ushirikiano kwa macho yangu ambayo yalikuwa yakitazama runinga.

    Ilitimu saa sita kamili usiku mume wangu akiwa bado hajarejea nyumbani na simu yake bado haikupatikana, nilipata wazo nimpigie mdogo wake ili niweze kumweleza kuwa Enrique alikuwa hajarudi nyumbani hadi mda ule. Lakini wakati nilipokuwa nikitafuta namba ya huyo shemeji yangu kwenye simu yangu ya mkononi nilisikia gari ikipiga honi kwa fujo sana getini.

    “Piii pipiiiiiii, piiiiiii, piiiiii.”

    “Mmh!” niliguna.

    “Pippiiiiiiiiii….”

    Huyu kapatwa na tatizo gani mbona anapiga honi kwa fujo namna hiyo.” Niliwaza huku mapigo ya moyo yakinienda mbio sana kwasababu haikuwa kawaida ya mume wangu kuwa mtu wa fujo namna ile.

    ***

    “Au atakuwa sio yeye?” nilizidi kuwaza.

    Baada ya dakika chache mlinzi wa getini alifungua geti baada ya kuhakikisha kuwa lile lilikuwa ni gari la bosi wake kwasababu hata yeye alipatwa na wasiwasi kidogo kutokana na ujio wa bosi kwa siku zile kuwa tofauti kabisa na siku zingine.

    Nilikuwa nikichungulia kwa dirishani, moyo wangu ulizidi kunienda kasi baada ya kushuhudia gari la mume wangu likiingizwa ndani kwa kasi ya ajabu ambayo haikuwa kawaida yake ya uendeshaji.

    “Kwanini anaendesha gari vibaya hivyo.” Nilijishtukia nazungumza peke yangu wakati nilipokuwa nikilitengenezea vizuri pazia ambalo nilikuwa nikilifunua kuchungulia kushuhudia yale maajabu yaliokuwa yakitendwa kwa mara ya kwanza na mume wangu.

    Bado wasiwasi ulizidi kunitanda baada ya kusikia mume wangu akibamiza kwa nguvu sana mlango wa gari baada ya kushuka kwenye gari.

    “Mmh! Hapa kuna usalama kweli!” nilizidi kuwaza kutokana na ujio wa mume wangu kuwa wa tofauti sana kwa siku zile.

    Baada ya dakika kadhaa aliingia ndani na nilipatwa na mshtuko mkubwa sana nilipomuona kwa mara ya kwanza akiwa amelewa kupita kiasi. Nilipata majibu ya maswali niliyokuwa nikijiuliza peke yangu kwasababu pengine ingekuwa kawaida yake kunywa pombe basi nisingeweza kuwa na wasiwasi wa yeye kuchelewa nyumbani na pamoja na kufanya matukio yasiokuwa ya kistaarabu.

    Moyo wangu ulijawa na simanzi sana baada ya kumuona mume wangu akiwa katika hali ile ya ulevi wa kupindukia.

    “We mwanamke hujalala hadi saa hizi unasu….biri nini?” alizungumza mume wangu kwa sauti ya kilevi huku akiyumbayumba kuzidi kusogea pale nilipokuwa nimekaa.

    “Nakuuliza wewe tasa naomba unipe jibu tafadha…tafadhali.” alizungumza huku akicheua.

    Nilishindwa kumjibu chochote nikawa namwangalia tu huku machozi yakinichuruzika kama maji.

    “Kwanini huzai?” bado alizidi kuniandama kwa maswali mazito yaliyokuwa nje ya uwezo wangu.

    “Kweli hakuna kizuri kisichokuwa na kasoro yaani binti mzuri kama wewe uliekamilika kila idara lakini bado unamatatizo jambo ambalo hakuna mtu anaeweza kuamini unaweza ukawa miongoni mwa wagumba kwajinsi ambavyo umeumbwa kwa upendeleo wa hali ya juu, Kijana wa watu najitahidi kutikisa nyavu lakini wapi, sioni mabadiliko yeyote isipokuwa tunakodoleana tu mimacho kama ngendere waliotimuliwa kwenye shamba la mahindi.”

    “Hainiingii hakilini kabisa kwanini haushiki mimba au umeshatoaga mimba nyingi sana kipindi ukiwa huko kwenu ndio maana leo hii inashindikana.” Hisia za majonzi zilifunika moyo wangu na kunisababishia maumivu makali mno kutokana na maneno niliyokuwa nayasikiliza kutoka kwa mwanaume ambae ndie chaguo langu.

    ***CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Nilishindwa kabisa kutamka neno lolote kwasababu nilikuwa nalia sana kwasababu niliona kama mume wangu aliamua ile siku aninywee pombe ili aweze kuzungumza na mimi maneno ambayo kwa hakika naamini asingeweza kunieleza akiwa na akili timamu.

    Nilizidi kuumia zaidi baada ya kujiuliza ni kwanini hakukaa na mimi chini ili kuweza kuzungumza juu ya suala lile hadi kufikia hatua ya kwenda kunywa pombe ndio aje kuzungumza na mimi. Isitoshe alizungumza maneno mengi sana ambayo yaliniumiza sana na kunifanya nijiulize maswali mengi sana juu yake.

    Maumivu yangu yaliambatana na maswali mengi sana.

    “Inamana ndio maisha ya ndoa yalivyo?”

    “Mbona kabadilika ghafla?

    “Mbona aliniambia kuwa hajawai kunywa pombe iwaje leo aje amelewa kupindukia?”

    “Na ni kwanini ananitupia mimi lawama kuwa ndie mgumba kwani yeye hawezi kuwa na tatizo?”

    wakati najiuliza maswali hayo simu ya mume wangu iliita na aliipokea muda huohuo na nilizidi kuumia baada ya kusikia mume wangu akiongea na mtu ambae nilihisi kuwa atakuwa ni mwanamke na kibaya zaidi alikuwa akiongea nae kwa lugha ya kiingereza ambayo ilikuwa inanipiga chenga kwa kiasi fulani.

    Sikuweza kuelewa kabisa kile kilichokuwa kikizungumzwa kwasababu mume wangu alikuwa na uwezo mzuri sana wa kuzungumza lugha ya kiingereza, katika mazungumzo yake yote nilisikia maneno kadhaa ambayo ndio niliweza kuyaelewa.

    “Yes I have arrived safe my dear.” (nimefika salama mpenzi.)

    “Mh huyo dia mwingine anaezungumziwa kwenye simu ni nani?” nilijiuliza huku nikizidi kutokwa na machozi nikijiuliza kwa nini mume wangu alikuwa ananitendea jambo la kuniumiza moyo wangu.

    Baada ya maongezi yake mume wangu alizungumza kauli ambayo ilikuwa ni kama mshale wa sumu uliotuwa katika mwili wangu.

    “We endelea kuzubaa kama wenzio hawajakupiku.”

    Macho yalivimba kutokana na kilio nilichokuwa nikikiangua kutokana mvua ya maneno iliyokuwa ikininyeshea kutoka kwa mume wangu. Baada ya kuhakikisha kwamba dukuduku lililokuwa limemjaa ndani ya moyo wake amemaliza aliamua kuondoka zake na kwenda chumbani kulala. Nilibaki sebuleni nikizidi kulia kutokana na uchungu mkubwa uliokuwa umejikusanya ndani ya moyo wangu ndani ya muda mfupi.

    Sikuhisi usingizi kabisa, badala yake niliendelea kukaa pale sebuleni nikiwaza ni namna gani nitaweza kuokoa ndoa yangu ambayo ilikuwa ndio inaanza kuzama. Ilipotimu saa kumi kamili mume wangu alinifuta sebuleni na kunichukua na kwenda nae chumbani. Pombe ilikuwa imepungua kichwani mwake kwa kiasi kikubwa sana.

    ***

    Licha ya kwenda kitandani kulala lakini bado usingizi ulikataa kabisa kunijia kutokana na msongo wa mawazo uliokuwa umenitanda.

    Kadri siku zilivyozidi kusonga ndivyo nilivyokuwa nikizidi kupoteza amani ndani ya moyo wangu kwasababu wifi zangu nao walizidi kuniandama kwa maneno yaliyojaaa dharau na masimango, sikuwa na pakupatia afueni kwasababu mume wangu nae alizidi kunywa pombe kupita kiasi na wakati mwingine zilikuwa zinapita siku mbili hajaonekana kabisa nyumbani na ukimuuliza anakuwa mkali kama mbogo.

    Mume wangu naomba twende hospitali tukatafute ufumbuzi wa hili tatizo linalopoteza amani ya ndoa yetu.” Nilijaribu kuzungumza nae siku moja asubuhi kabla hajaondoka kuelekea kazini.

    “Sasa unataka mimi niende hospitali nikafanye nini? Kwani mimi ndie ninatumbo la kubeba mimba? Wa kwenda hospitali ni wewe ambae ndie unapaswa kubeba mimba halafu inashindikana.

    Lakini suala la kutokubeba ujauzito linaweza likasababishwa hata na mwanaume sio mwanamke pekee.

    “Mimi ni mwanaume na nimekamilika kila idara sasa wewe endelea kuchelewa hapo kama sijamleta mtoto na mama yake humu ndani.” Nilihisi kuchanganyikiwa baada ya kusikiliza majibu ya mume wangu.

    Baada ya yeye kuondoka kuelekea kazini niliamua kwenda hozpitali kucheki ni kitu gani kilikuwa kinanifunga nisishike ujauzito ingawa sikuwa na wasiwasi sana kwasababu sikuwai kushika ujauzito nikatoa labda iwe mapenzi ya mungu mimi kuwa mgumba lakini sikuwai kufanya jambo lolote ambalo pengine lingeweza kunitia wasiwasi wa kutokushika ujauzito.

    Vipimo vya daktari vilionyesha kuwa sina kasoro yeyote ambayo ingeweza kusababisha nikashindwa kubeba mimba kwahiyo daktari alinitaka nimpeleke mume wangu akachunguzwe pengine tatizo lingeweza kuwa kwa upande wake.

    Nilipomweleza mume wangu kuwa vipimo vimeonyesha nipo safi kabisa bado alionekana kuwa na kichwa kigumu cha kunielewa kwasababu alizidi kukaidi wito wa daktari kufika hospitali akafanyiwe uchunguzi wa kiafya.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Amani ilizidi kutoweka katika familia yangu na niliona ni muda muwafaka wa kumshirikisha mama yangu ili aweze kunisaidia katika yale magumu niliyokuwa nikipitia kwa wakati ule ingawa mama alinishauri nijaribu kuwashirikisha wazamini wangu wa ndoa pamoja na wazazi wa mume wangu. Nililifanyia kazi wazo la mama kwa kuamua kumshirikisha mama mdhamini wa ndoa yangu ili nipate ushauri wake kwasababu amani ndani ya ndoa ayangu ilizidi kwenda mrama.

    Pamoja na kwamba wadhamini walijaribu kutafuta suluhisho kwa kutuweka wote chini na kuzungumza na sisi katika maongezi ambayo yalitawaliwa na neno la Mungu ndani yake kwamba tuzidi kumuomba Mungu atujalie kwasababu Mungu wetu ni mwaminifu na hashindwi na jambo lolote



    Nilijitahidi kuwa mvumilivu kwasababu watu wote niliowashirikisha walinishauri nijaribu kuvumilia kwasabaabu ndoa inahitaji uvumilivu wa hali ya juu hivyo sikuwa na namna nyingine ya kufanya isipokuwa nilizidi kumuheshimu mume wangu kwasababu ya nafasi kubwa na ya kipekee niliyokuwa nimempatia ndani ya moyo wangu.

    Tabia yake ilizidi kubadilika na ilifikia sehemu ikawa hata haki yangu ya ndoa sipati tena, na kila nilipojaribu kuulizia haki yangu alikuwa akinipa majibu ambayo yalikuwa yakiutengua moyo wangu kila mara.

    “Siwezi kutikisa nyavu ambayo haitikisiki kwahiyo naomba usinikondeshe bure mtoto wa mwanamke mwenzio.”

    Nilizidi kusononeka kwa mawazo na kusababisha kila mtu ambae alikuwa akinifahamu alipokutana na mimi ashtuke na aniulize swali.

    “Mbona umekonda hivyo?” lilikuwa ni swali ambalo nilikuwa nakumbana nalo kwa takribani mara mbili kila siku. Nilijitahidi kuwaficha ukweli halisi wa mimi kudhoohofu kimwili kwasababu sikupenda kila mtu afahamu mambo ya nyumbani kwangu.

    Palikucha siku moja nikiwa najihisi kuumwa kutokana na kichapo kikali nilichokuwa nimekipokea kutoka kwa mume wangu usiku alipokuwa amerudi amelewa sana akinitaka niende kwetu kwani ahitaji kuendelea kuishi na mimi tena kwasababu nimeshindwa kumzalia mtoto. Baada ya yeye kwenda kazini nilikuwa bado nimejilaza kitandani nikiwa najihisi maumivu kila kona ya mwili wangu, nilijitutumua na kushuka kitandani na ndipo sura yangu ilikumbana na kioo kilichokuwepo pale chumbani na kujitazama uso wangu jinsi ulivyokuwa umeharibika kwa hali ya kutisha.

    Mashavu yote yalikuwa yamevimba kutokana na makofi ya nguvu aliyonipiga mume wangu, lipsi zangu zilikuwa zimepasuka, na pia mwili wangu wote ulijawa na michirizi iliyosababishwa na mkanda aliokuwa anautumia kuniadhibu. Isitoshe bado nilikuwa nasikia maumivu ya ndani kwa ndani kwenye tumbo langu ambalo alikuwa analipiga mateke kwa hasira akidai kwamba ndio lilikuwa linastahili zaidi kupewa adhabu kwasababu ndio chanzo cha matatizo yote.

    Alinipiga na kuniumiza sana ila sikuthubutu kufungua mdomo wangu kuomba msaada kwasababu alikuwa ananitishia kuwa ataniua endapo nitajaribu kujaza watu nyumbani kwake kwa kelele zangu. Alinipiga kwa muda mrefu sana hata zile kwikwi zangu za kilio hazikuweza kufika getini kwa mlinzi kwasababu tulikuwa ndani chumbani na pia hata mlinzi angesikia asingekuwa na uwezo wa kuniombea msamaha kwasababu kibarua chake kingeota nyasi.

    Nilichukua uamuzi wa kwenda kwa nesi anaeitwa Doroth ambae ni rafiki yangu mkubwa niliekuwa nimezoeana nae pale mtaani kwangu ili akanipatie dawa ya kutuliza maumivu kwasababu mwili wangu ulikuwa na majeraha kila mahali, nilihofia kwenda hospitali kwasabaabu niliona mume wangu wangemchukulia hatua za kisheria ingawa sikuwa tayari kufanya hivyo lakini nilihofia pia usalama wangu kwasababu aliniambia kuwa endapo atasikia kwa majirani kwamba natangaza ananinyanyasa adhabu atakayonipa ni ya kifo.

    ***

    Nilimkuta nesi yule na kumweleza yote yaliyokuwa yamenisibu na alinionea huruma sana na kunitaka nisikate tamaa bali nizidi kumuomba Mungu ili aweze kunijalia mtoto na hatimae furaha ya ndoa yangu iweze kurudi, nilipata moyo kidogo kwasababu Doroth alinieleza kuwa tatizo lililokuwa linaninyima amani ndani ya ndoa yangu ameshawai kukumbana nalo katika maisha yake ya ndoa kwa muda wa miaka 8 na hatimae Mungu alisikia kilio chake. Alinipatia dawa aina ya paracetamol kwaajili ya kutuliza maumivu niliyokuwa nikihisi ndani ya mwili wangu na pia alinitibu yale majeraha yaliyokuwa sehemu mbalimbali ya mwili wangu, na mwishowe nilirejea nyumbani kwangu.

    Mara baada ya kufunguliwa geti na mlinzi nilipoingia ndani nilikutana na sura za mawifi zangu wawili Flora na Zubeda wakiwa wamefunga vibwebwe kama walikuwa wamekuja kucheza ngoma ya kizaramo pale nyumbani kwangu huku wakinitazama kwa macho ya dharau wakitema mate mfululizo kana kwamba walikuwa wamekutana na mzoga.

    “Duuh! hapa kuna amani kweli.”nilijiuliza baada ya macho yangu kugongana na macho za wifi zangu wakinitazama kana kwamba nilikuwa ninatia kinyaa.

    “Bibiweye tumechoka kukuvumilia leo tumeona tukutolee dukuduku lililojaa ndani ya mioyo yetu kama wana ndugu.” Ilisikika sauti ya Zubeda.

    “Basi karibuni muingie ndani.”

    “Sikiliza we tasa usie na tumbo lenye rutuba ya kumstawisha mtoto tunaomba uondoke humu ndani ili kaka yetu aweze kuoa mwanamke mwenye tumbo linaloweza kubeba mtoto.” Zubeda alianza kunichoma kwa jua la maneno huku mwenzie akitengenezea kibwebwe chake barabara ili aweze kunifikishia ujumbe mubashara (live) bila chenga.

    “Jamani kwani nimewakosea nini hadi mzungumze maneno makali kiasi hicho.” Nilizungumza huku machozi yakianza kunibubujika kwasababu ya maneno makali ambayo nilikuwa nikiyasikia kutoka kwa wifi zangu yalikuwa hayana utu ndani yake.

    “Tusikilize wewe kunguru hatutaki nuksi katika ukoo wetu kwahiyo fanya fasta usepe tuachie kaka yetu.” Flora ambae ndie alikuwa mkubwa kwa Zubeda nae alianza kuniporomoshea mzigo wa maneno yaliyokuwa yakigusa hisia zangu moja kwa moja. Kilichoniumiza na kunishangaza zaidi ni kwamba hawa wifi zangu wote walishaolewa na kuachika kwahiyo wote walikuwa wanaishi nyumbani kwao baada ya kutimuliwa kwa waume zao.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    Kutokana na maneno waliyokuwa wakizungumza yalikuwa yakiniumiza sana niliamua kuanza kuondoka kuelekea ndani ili kukwepa yale maneno ya mawifi zangu ambao kwa hakika ile siku walikuwa wameniamulia kunichamba sawasawa.

    Nilipokuwa naondoka nilisikia mmoja wao akisema kwamba.

    “Siunaona jinsia alivyo na dharau huyu Malaya mshenzi.”

    ***

    “Ngoja leo tumwonyeshe sisi ni nani hawezi kutuletea uchuro sisi mtu mwenyewe kaja mshamba hata kufungua mlango wa friji alikuwa hajui.” Alizungumza Zubeda huku akinifuata kwa kasi yeye na mwenzie.

    Baada ya kunifikia walinikamata na kuniangusha chini na kuanza kunipiga na kuning’ata sehemu mbalimbali za mwili wangu, ingawa niliwaambia kuwa nilikuwa naumwa lakini hawakujali isipokuwa waliendelea kunichangia kunipiga hadi mlinzi wa getini alipoingilia na kunichomoa mikononi mwa wale ma wifi zangu ambao walikuwa wanataka kunitoa roho yangu.

    Kitendo cha mlinzi kuniokoa kilizua tafarani zaidi kwasababu walimuwakia yule mlinzi kwa maneno makali sana.

    “We pimbi tu huna lolote unaingilia ugomvi wa wanawake unakuhusu nini?” sauti ya Flora ilisikika ikionyesha dharau kwa mlinzi wa nyumbani kwangu.

    “Litazame kwanza wakati wenzio wanakwenda shule kutafuta maarifa ya kuwasaidia maishani wewe ulikuwa unavuta shuka ukiogopa umande matokeo yake unakuja kusimama getini kwa mwanaume mwenzio kama sanamu.” Maneno ya kutia hasira yalizidi kumiminwa kwa yule mlinzi ambae alidiriki kunichomoa kwenye mikono ya wifi zangu ambao walikuwa wamenipania kama wametumwa.

    Niliwaza nipige simu polisi kutoa taarifa kuwa kuna watu walikuwa wamekuja kuniletea fujo nyumbani kwangu lakini niliwaza upande wa pili nikaona kwamba ningeweza kufanya vile basi ile ndio ingeweza kuwa tiketi ya mimi kuondoka pale nyumbani kwasababu pengine mume wangu asingenielewa kabisa kwahiyo ilinibidi kukaa kimya nikizidi kulia kwa uchungu sana.

    Mwili wangu ulizidi kuumia kwa maumivu mengine makali niliyokuwa nimeyapata muda mfupi baada ya kupigwa na mawifi zangu, zile dawa nilizokuwa nimetoka nazo duka la dawa zilikuwa zimesagika zote kutokana na kashikashi niliyokuwa nimeipata kutoka kwa mawifi zangu ambao walikuwa wananigombania kama mpira wa kona.

    Yule mlinzi alinichukua na kunipa msaada wa kunipeleka ndani ili wale mawifi zangu wasiweze kuendelea kunichangia kunipa kipondo. Walibaki nje wakiendelea kunitolea maneno ya kunivunja moyo ila sikudiriki kuwajibu kwa kuwatolea maneno mabaya bali nilinyamaza kimya kama mjinga nikiamini kwamba ukimya pia ni moja kati ya kuonyesha busara ya mtu pale ambapo anakuwa amekumbana na jambo ambalo kwa namna moja au nyingine kulivumilia ni vigumu.

    “Tunakwambia utang’ooka tu huwezi kuwa king’ang’nizi kama kupe.” Ilisikika sauti ya Flora wifi yangu ikizungumza kwasauti ya juu ambayo iliweza kunifikia mle ndani nilipokuwa nimepelekwa na mlinzi kwenda kujificha.

    “Wasikuumize kichwa nafikiri ni ujinga uliojaa kwenye vichwa vyao ndio unawasumbua.” Mlinzi alizungumza pale ambapo sauti za wifi zangu zilisikika zikizidi kuzungumza maneno ya kunivunja moyo.

    Niliona ni bora ni mpigie mama yao simu nijaribu kumweleza kuwa wanae wapo nyumbani kwangu wananifanyia fujo.

    ***

    “Sh..ka..moo mama!” nilizungumza kwashida kwasababu kwikwi za hasira zilikuwa zinaninyima uwezo wa kuzungumza vizuri.

    “Marahaba! Unalia nini?”

    “Flora na Zubeda wamenipiga.”

    “Kisa nini?”

    “Kiukweli hata mimi mama sielewi sababu ya wao kujaku…ni..piga tena nyu..mba..ni kwangu.” Nilizidi kuzungumza kwa uchungu sana moyoni huku nikidondokwa na machozi katika macho yangu ambayo yalikuwa yamevimba kwa kuparuliwa na kucha cha wifi zangu.

    “Sasa kuna mtu anapigwaga bila kosa?”

    “Au pengine wewe mama unafahamu kosa langu uniambie kwasababu mimi sifahamu chochote.”

    “Wee koma tena ukome ukomae kunishirikisha katika mambo yasiyokuwa na kichwa wala miguu.”

    “Sawa mama naomba unisamehe.”

    “Tena nikusikie ukitangaza kuwa eti umepigwa na wifi zako ndio utanitambua mimi ni nani, unajifanyisha umepigwa kwani wewe huna mikono ya kupigana au ndio umepata pa kudekea kwahiyo ndio unajiachia kwa raha zako.” Maneno ya mamamkwe yalizidi kunimaliza nguvu kwanamna ambavyo yalikuwa yakinichoma kama moto wa gesi.

    Simu ilikatika katika mazingira ya kutatanisha nikawaza labda yeye ndie atakuwa amekata baada ya kuona labda nazungumzaa nae maneno ya kumkera.

    Niliona ni bora nirudi duka la dawa nikachukue dawa zingine za kunisaidia kutuliza maumivu kwasababu nilizidi kujihisi vibaya, niliacha simu yangu pale kwenye kiti nilichokuwa nimekaa na kwenda chumbani kuchukua kanga ili niweze kujifunga kwasababu kanga niliyokuwa nimejifunga mara ya kwanza ilikuwa imechanika baada ya misukosuko ya kuvutwavutwa na wifi zangu.

    Baada ya kutoka chumbani niliporudi sebuleni nilikutana na missed call mbili kutoka kwa mamamkwe wangu na meseji moja ambayo ilisomeka.

    “WE MWALI SIKUJUA UNATABIA MBAYA KIASI HICHO YAANI UNADIRIKI KUNIKATIA SIMU MIMI MAMA WA MUMEO HALAFU NAKUPIGIA SIMU HUPOKEI, AMA KWELI UMDHANIAE NDIE KUMBE SIE, OK SAMAHANI KWA USUMBUFU.”

    Meseji ile iliniongezea uchungu zaidi na kunifanya nikose raha kabisa hivyo ilinibidi nimpigie simu ili niweze kumweleza ukweli lakini alionekana kususa kupokea simu yangu. Nilimtumia ujumbe mfupi wa maandishi kumweleza sababu ya kutokupokea simu yake.

    ***CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    “Samahani mama nadhani simu ilikatika kwasababu ya netiweki, halafu pia sikupokea simu ulipopiga kwasababu nilikuwa nimeacha simu kwenye kiti sebuleni na kwenda chumbani kuchukua kanga ya kujifunga ili niweze kwenda hospitali kupata matibabu kwasababu nimeumia.”

    Baada ya kutuma ujumbe ule niliamua kutoka ili niende kwa Doroth akanipatie dawa zingine za maumivu. Nilipofika getini nilikutana na mume wangu anakuja nyumbani ingawa haukuwa muda wake wa kurudi nyumbani kwasababu ilikiwa bado ni majira ya mchana na huwa anarudi jioni, lakini cha kushangaza mume wangu aliegesha gari pale gatini na kuteremka na kunifuata akionekana kuwa na hasira sana ingawa sura yake ilionyesha yupo vizuri kabisa hajanywa pombe.

    “We Malaya leo nakuvunja kiuno haiwezekani mbwa kama wewe umuonyesha mama yangu dharau.” Ilisikika sauti ya mume wangu ikizungumza kwa kwa hasira sana na ghafla akaanza kinishushia mkong’oto wa maana palepale nje ya geti la nyumba yetu.

    Kibaya zaidi alikuwa akinipiga makofi, ngumi na mateke kama vile alikuwa akipigana na mwanaume mwenzie jambo ambalo lilinifanya niwe naona nyotanyota kwa namna ambavyo makofi na ngumi vilivyopokuwa vikitua kwa mfululizo usoni mwangu.

    Ilinibidi nipige mayowe ili kuomba msaada kwasababu niliona Enrique alikuwa anataka kuniua kwasababu alikuwa na hasira sana kutokana na taaarifa aliyopewa na mama yake kwamba nilikuwa nimemdharau kwa kumkatia simu na kumsusia kupokea simu yake ingawa haikuwa kweli kabisa.

    Mlinzi alinionea huruma sana lakini hakuthubutu kufungua mdomo wake wala kusogea kuniokoa kwasababu bosi wake alionekana kufura hasira kama chatu kitu ambacho kingeweza kusababisha afukuzwe kazi muda uleule endapo angejaribu kufanya chochote.

    Kwabahati nzuri alifika jirani wa nyumba ya pili baada ya kusikia yowe nilizokuwa nikiangua kuomba msaada.

    “Kunanini tena jirani mbona mnadhalilishana kiasi hiki.” Ilisikika sauti ya jirani yetu Nasibu akizungumza huku akimvuta mume wangu ambae alikuwa anazidi kunitwanga mangumi na mateke bila huruma ingawa alikuwa ameshaniumiza sana kwasababu nilikuwa natokwa na damu nyingi puani na mdomoni.

    “Jirani wacha kwanza nimfundishe adabu huyu mwanamke hawezi kumkosea adabu mama yangu alienizaa.” Alizungumza kwa jazba sana huku akihema juujuu kwa nguvu alizokuwa anazitumia kunipa kipigo cha aina yake.

    “Brother wewe ni mtu ambae unaheshimika sana hapa mtaani kwajinsi ambavyo ni mstaarabu, kufanya haya yote ni kijishushia heshima yako mbele ya jamii inayokuzunguka, isitoshe mnagombana kwasababu ya mambo ya kifamilia ambayo mngepaswa kuyamaliza ndani ya nyumba yenu bila hata ya mlinzi kufahamu kinachoendelea baina yenu.”

    “Ni kweli kabisa kaka ila huyu mwanamke ni pasua kichwa mno, mwanamke gani ambae anadharau ndugu wa mume wake kama sio shetani.” Enrique alizidi kuzungumza kwa hasira sana maneno ambayo yalisababisha machozi yasikauke katika macho yangu kwasababu halikuwa kosa nililolitenda bali niliona ni njama tu za wale ndugu wa mume wangu walikuwa wameamua kuzitengeneza ili kuvunja ile ndoa yangu ambayo bado ilikuwa inaharufu ya upya.

    ***

    “Hata kama amekuudhi namna gani unapaswa kuwa makini wakati wa kumuadhibu kwasababu huyu ni mtoto wa kike ukimpiga kama unapigana na mwanaume mwenzio unaweza kumsababishia umauti kwahiyo nakuomba tafadhali jaribu kutafuta suluhisho la tatizo hili kwa namna nyingine ambayo ni ya amani zaidi, kwasababu suluhisho jema hupatikana kwa njia ya amani na si vinginevyo.”

    Jirani yule kwa maneno yake ya busara alifanikiwa kuituliza hasira za mume wangu na baada ya hapo alinipeleka hospitali moja ya mtu binafsi inayojulikana kwa jina la Faraja hospital inayomilikiwa na rafiki yake aitwae Petro.

    Tulipofika hospitalini kwa bahati nzuri tulimkuta Petro ambae alituhudumia vizuri sana ingawa sikujua kuwa mume wangu alimueleza kuwa nilikuwa nimeumizwa na kitu gani kwasababu hakuniuliza kabisa chanzo cha yale majeraha aliyokuwa akinitibu ndani ya mwili wangu jambo ambalo sio la kawaida, zaidi sana yule daktari alikuwa akinipa pole mara kwa mara alipokuwa akiniudumia.

    Baada ya kupata matibabu tulianza safari ya kurudi nyumbani ambapo licha ya kwamba nilikuwa na maumivu makali nilikumbana na maswali mengi kutoka kwa mume wangu ambayo yalinihitaji niweze kuyaatolea ufafanuzi unaoeleweka.

    “Nilipokutana na wewe pale getini ulikuwa unakwenda wapi?”

    “Nilikuwa nakwenda kwa Doroth kununua dawa za maumivu.”

    “Ulikuwa unaumwa.?”

    ”Ndio.”

    “Tangu lini?”

    “Tangu jana uliponipiga usiku.”

    “Ndio nilivyoamua sasahivi ni mwendo wa kichapo hadi kieleweke.”

    “Kwanini hukunipigia simu kunieleza kuwa ulikuwa unaumwa.”

    “Samahani mume wangu kwa kutokutaarifu.”

    “Ndio mana nakwambia kwasasa sintakuwa nazungumza kwa maneno bali kwa vitendo tu.”

    “Mama yangu nae umemfanyaje?”

    “Nilikuwa nazungumza nae kumweleza kuwa Flora na Zubeda walikuja nyumbani kwangu na kunichangia kunipiga bila mimi kufahamu nilichokuwa nimewakosea, kwa bahati mbaya sana wakati nilipokuwa nikizungumza nae simu ilikatika, ndio nikaacha simu sebuleni na kwenda chumbani kuchukua kanga ili niweze kujifunga niende kutafuta dawa za kutuliza maumivu. Nilipokwenda chumbani na kurudi nilinyanyua simu yangu ili niweze kuondoka ndipo niliona kuwa mama alikuwa amenipigia simu mara mbili na pia kulikuwa na ujumbe mfupi wa maandishi ambavyo vyote viliingia kile kipindi ambacho nilikuwa chumbani, ingawa meseji ya mama iliniumiza sana kwasababu niliona kuwa alipata mtazamo kuwa nilikuwa nimemdharau lakini haikuwa kweli. Nilijaribu kumpigia simu ili kumweleza hali halisi lakini simu haikupokelewa.” Nilizungumza kwa kwa masikitiko makubwa ndani ya moyo wangu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com

    “Kwanini ni fikie hatua ya kumdharau mama? Na pia achilia mbali mama mimi siwezi kumdharau mtu yeyote kwasababu nimelelewa katika misingi ya kumuheshimu kila mtu bila kujali umri, jinsia, kabila wala dini.” nilizungumza kwa hisia kiasi kwamba machozi yalianza kunidondoka tena kwa mara nyingine.

    “Uliona ugumu gani kunijulisha kwanza mimi kabla ya mama yangu au yeye ndie kakuoa?”

    “Niliogopa kukujulisha kwasababu uliondoka asubuhi angali hapakuwa na maelewano mazuri kati yetu.”

    “Ninyi wanawake mimi nawafahamu vizuri sana nitabia yenu mkishaolewa mnakuja kuharibu uhusiano wa mume na ndugu zake jambo ambalo sintaweza kulivumilia hata japo kwa sekunde moja, kama huwezi kuelewana na ndugu zangu hata mimi utakuwa unanidanganya vilevile kwahiyo mimi nakushauri ufungashe virago vyako uondoke nyumbani kwangu siwezi kuendelea kuishi na wewe kwa mtindo huu.”



    ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

Blog