Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

USALITI WA KIAPO - 2

 







    Simulizi : Usaliti Wa Kiapo

    Sehemu Ya Pili (2)

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Asubuhi na mapema Tony akaamka baada ya kuchangamsha mwili kwa mazoezi mepesi na kuweka mwili safi bafuni akaingia jikoni walau kuandaa kifungua kinywa kwa ajili ya mgeni wake ambaye hadi muda huo alikuwa bado amelala. Wakati Tony yupo jikoni simu yake ikawa inaita na mlio wa simu ukasababisha Jamilah aamke, akaiangalia ile simu akakuta Jina ni Tedy, akaiacha hadi ikakata, baada ya muda mfupi ukaingia ujumbe mfupi,

    “Hello mpenzi! Bado umelala tuu”.



    Ujumbe ule ukamshtua sana Jamilah, uvumilivu ukamshinda akaamua apekue zaidi simu ya Tony ili kujua zaidi habari za huyo Tedy, wakati akiendelea kupekua ukaingia ujumbe mwingine mfupi toka kwa Vanessa,

    “Jamani bae, toka jana umenichunia shida nini, alafu mwenzio nimekumiss sana nataka nije kwako leo”



    Jamilah akahisi kama anaota vile hakuamini yale aliyoyashuhudia, ikabidi ajifinye ili aone kama alikuwa ndotoni au la, japo hiyo haikubadili ukweli juu ya aliyoyashuhudia, akajikuta akitokwa na machozi kama mtoto mdogo,

    “Siamini kama penzi langu la kwanza laweza kuwa chungu kiasi hiki, kwanini nimekuwa mpumbavu kumuamini mtu kirahisi hivi, kumbe hivi ndivyo maumivu ya mapenzi yalivyo,” aliendelea kusema Jamilah huku akilia, hakika hakuwa na nguvu hata ya kutoka pale kitandani hakutaka kuyakubali yale anayoyashuhudia.



    Tony akamaliza kuandaa kifungua kinywa na akaingia chumbani kumuita Jamilah akaribie mezani, alipoingia hakika naye alishikwa na bumbuazi. Alikuta Jamilah akilia mithiri ya mtu aliyepata msiba wa mtu wake wa karibu, akasogea kujua kulikoni lakini Jamilah hakuongea kitu zaidi ya kumpa ile simu. Tony akaishiwa nguvu akajua tayari amesababisha ajali, Jamilah akamkunja Tony na kumpiga piga kifuani,

    “Kwanini umenifanyia hivi Tony, katika siku yangu ya kwanza ya kujuana na mwanaume wewe umenifanyia ukatili huu, hakika sitokusamehe,” Jamilah akaongea kwa uchungu mno.

    “Kwani nimekufanyia kipi kibaya?” Tony akauliza.

    “Kwanini umenilaghai na kunifanya nikupende hadi kufikia hatua ya kulala na wewe wakati una mpenzi mwingine mbaya zaidi sio mmoja wawili Tony”

    “Mhmh! Jamilah sasa mimi kuwa na wapenzi inahusiana nini na kilichotokea kati yetu?”

    “Kwa iyo unanifanya mimi mtoto kunichanganya na wanawake wengine”

    “Binafsi sikumbuki kama ulishawahi kuniuliza kama nina mpenzi au la, pia katika kinywa changu sijawahi kutamka neno nakupenda kwako”

    “Tony..!”

    Jamilah alijikuta akikosa neno la kuzungumza, hakuamini kama Tony angeweza kucheza na akili yake kiasi kile.

    “Twende tukapate kifungua kinywa,” Tony alisema.

    Jamilah akamuangalia Tony kwa hasira sana, hakujua nini afanye Zaidi ya machozi kumbubujika, hakuwa na nguvu hata ya kuinuka pale kitandani,

    “Tony niambie kuwa niliyoyaona na niliyoyasikia kuwa si kweli”

    “Unataka nikuambie nini Jamilah?”

    “Niambie kuwa unanipenda na utaachana na hao wapenzi wako”

    “Hahahahahahaha! You can’t be seriously! How could I do that? (Unamasihara wewe! Nawezaje kufanya hivyo)”

    Jamilah akanyanyuka kitandani bila kusema neno, akaingia bafuni na baada ya kumaliza kuoga akavaa nguo zake na kuondoka lakini kabla hajatoka akageuka na kumtazama Tony kisha akamwambia,

    “Usihisahau hii siku ipo siku utailipia, nitayafanya maisha yako kuwa ya shida Zaidi”



    Tony alicheka sana aliposikia kauli ile, akamsogelea na kumshika kiuno, Jamilah akasogea nyuma na kumsukuma Tony, lakini jamaa alionekana kuwa imara kwani hakuweza kutikisika. Akamtazama Jamilah machoni na kumwambia,

    “Usiwe mjinga wa kusahau ubaya unaoufanya kwa mtu, ile siku uliyonidhalilisha kwa ajali ndogo ya gari lako, niliumia sana na niliapa nitafanya lolote kukupata sasa uko mikononi mwangu huna la kufanya. Nilikwambia kamwe usisahau ile siku ila kwakuwa siku zote wanawake mnaongozwa na hisia kwanza bila kufikiria Zaidi, nikakutega ukategeka kwa hiyo bila bila nenda tu na usifikirie kunitafuta tena”.

    Baada ya maneno hayo mazito akamuachia Jamilah ambaye kwa kiasi kikubwa aliduwaa huku machozi tuu yakimtoka, kiburi chake kimemuingiza pabaya.



    ********************



    Baada ya kuwa na mafanikio makubwa kama balozi wa kampuni ya Kikorea Martha akawa ni miongoni mwa wasichana ambao habari zao kila siku zinatangazwa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii. Wanaume wengi walitamani kuwa na mwanamke mwenye sifa kama alizonazo Martha, achilia mbali uzuri na urembo wake linapokuja swala la kazi Martha ni mtu anayependa kuwajibika kwa wakati na kuhakikisha kila kitu kimeenda kama kilivyopangwa. Wanaume wachache waliopata bahati ya kuwa karibu na mrembo huyo walishindwa kuzuia hisia zao na kila mmoja akijaribu kutupa karata yake kwa wakati wake. Kati ya wote hao hakuna hata mmoja aliyebahatika kuusimamisha moyo wa msichana yule.



    Joseph huyu ni mmoja kati ya vijana wachache waliojaliwa stara na wenye mafanikio makubwa, hakuwahi kuwa katika mausihano ya kimapenzi na alijenga Imani kuwa hamna mapenzi ya kweli duniani, lakini toka amefahamiana na Martha taratibu mawazo yale yakaanza kufutika na akajikuta akivutiwa sana na msichana yule. Kutokana na kufanya kazi katika kitengo kimoja wakajikuta wakiwa karibu Zaidi hasa baada ya kupewa kazi ya kuandaa Makala itakayoonesha utamaduni wa watu wa pwani hasa wale waishio Tanga.



    Iliwalazimu kufanya kazi mchana na usiku kuandaa mpango kazi, jinsi ya kuanza hadi utakapoishia, Jospeh alijisikia furaha sana kuwa na mwanadada yule ambaye muda wote aliwaza kazi tuu,

    “Martha naweza kukuliza jambo?” alisema Jose.

    “Uliza tuu!”CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Umekuwa bize sana na kazi! Nawaza huyo shemeji yangu anapata muda gani nawe?”

    “Hahahahahaha! Kwanini umeuliza?”

    “Nimeuliza tuu maana inaitaji moyo”

    “Kwani wewe mkeo akiwa bize hivi utafanyaje?”

    “Binafsi siwezi kusema kitu kwasababu sijawahi kuwa nae”

    “Ooh! Real? (Kweli?)”

    “Ndio”

    “What are you waiting for? (Unasubili nini?)

    “Namsubiri yule atakayeufanya moyo wangu kusimama walau kwa dakika na kuacha kufikiria yote na kumuwaza yeye tuu”

    “Keep on praying u will find her soon, (endelea kuomba utampata hivi karibuni)”

    “Thanks for your advice (akhsante kwa ushauri wako)”

    “Your welcome, (karibu)”

    “Lakini bado hujanibu swali langu”

    “Ooh! Ukweli kwamba sina muda na mapenzi kwa sasa, moyo wangu upo kwenye kazi yangu, hivyo tuu Jose”

    “Mhmhmh! Haya”



    Jose alijikuta akikatishwa tamaa na jibu alilopewa na Martha aliwaza Zaidi afanye nini walau mrembo yule arudishe hisia za mapenzi japo hakuwa anajua historia yake ya nyuma iko vipi, akajiuliza Zaidi je mrembo yule alishawahi kuwa kwenye mapenzi nini kilimtokea hadi leo kusema kuwa hana muda na mapenzi, kama hakuwai kuwa kwanini aogope kuingia katika ulimwengu huo wa huba.







    Baada ya mipango yote kukamilika, wafanyakazi wote wakiongozwa na Martha wakaanza safari ya kuelekea mkoani Tanga kwa ajili ya kuandaa Makala itakayoonesha utamaduni wa mkoa huo ambao kwa hakika unasifika kwa mahaba.

    “Sasa jamani nani ataongoza upigwaji wa picha maana Tony simuoni!” aliuliza Jose.

    “Mimi nitaongoza,” Martha akajibu.

    “Hiyo si sawa,” akasema Jose.

    “Kwanini?”

    “Umekuwa ukifanya kazi nyingi zinazomuhusu Tony, kwa nini azembee kiasi hiki hata kama yeye ni mkurugenzi lazima hawajibike sehemu yake,” aliongea Jose.

    “Lakini alichosema Jose ni kweli, yeye ni muongozaji na anajua kila kitu kuhusiana na hii safari sasa kwanini hasiwepo,” alisema mfanyakazi mwengine.

    “Jamani tuachane na hayo kila mtu achukulie hii safari kama sehemu ya kutuliza akili mbali na kazi inayotupeleka, tujitahidi kufanya vizuri bila kujali mtu flani hayupo”

    Ikabidi wote wakubaliane na Martha japo kishingo upande, maswali mengi yakazuka vichwani, inakuaje mkurugenzi amtete Tony kwenye maswala ya uwajibikaji au kuna mambo yanayoendelea nyuma ya pazia ambayo wao hawayajui.



    **************************



    Safari ya kuelekea jijini Tanga ikaanza huku wote wakiamini kuwa Tony anaingiza maswala ya kibinafsi kwenye kazi, sababu mara nyingi walishuhudia wakurugenzi hao wawili wakitofautiana kimitazamo na utendaji pia, japo wote walikuwa na nia moja ya kufanya kampuni kukua na kuingiza faida maradufu.

    Safari ilikua nzuri na yenye kuburudisha sana, wengi wao ilikuwa mara ya kwanza kwenda mkoa huo hivyo kwao ilikuwa kama kufanya utalii wa ndani,

    “Samahani bosi sijajua tunafikia wapi?” aliuliza Jose.

    “Tanga beach resort,” alijibu Martha.

    “Aah! Sasa kwani uliwapa taarifa mapema?”

    “Hilo ni jukumu la Tony”

    “Sasa Tony mwenyewe hakuja tutafanyaje!”

    “Usijali! Tutajua tukifika”



    ***************************



    Wakati msafara wa wafanyakazi ukikaribia kabisa kuingia jijini Tanga, Tony alifika mapema sana na akawa ashafanya mipango yote ya hotelini. Tony toka amefika hotelini hapo hakutulia sehemu moja, uwepo wa warembo wengi eneo hilo ulimfanya ajihisi yupo paradiso ndogo,

    “Braza eenh! Naona huku mambo sio mabaya,” alisema Tony baada ya kusogea katika kibanda cha mlinzi wa getini ambaye alikuwa zamu kwa wakati huo.

    “Kwanini?”

    “Braza! Huku kuna warembo kama wameshushwa hivi”

    “Hahahahaha! Hii ndio Tanga sasa”

    “Daah! Braza wee acha tuu nahisi mtaji wangu wa kuuza matunda nitaufirisi huku”

    “Hahahahaha! Angalia utakosa hata nauli ya kurudi Dar”

    “Ila broo kwani sehemu nyingine zipi ambazo kuna watoto wakali kama hawa na kumechangamka sana tofauti na hapa?” aliuliza Tony.

    “Mhmhmh! Sehemu zilizochangamka ni nyingi kama utaenda Usagara, Chumbageni au kule Raskazone ndio balaa maeneo ya ufukwe nini unaweza kusahau kabisa kurudi kwenu, alafu watoto wakule wanajua mahaba kweli,” alijibu Mlinzi.

    “Duuh! Broo uko vizuri kona zote unazijua”

    “Hahahahaha! Kawaida tuu”

    “Hivi broo umeoa kweli maana daah si mchezo”

    “Hahahahahaha! Unafurahisha sana dogo na maswali yako, ukweli mimi nina mke na mtoto mmoja wa kiume, lakini si unajua tena kila siku uwezi kula mboga moja lazima ubadirishe kesho nyama, kesho kutwa maharage japo vyote ni protini” alisema Mlinzi.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tony alijikuta akijenga Urafiki na Mlinzi yule ndani ya muda mfupi sana, sababu walionekana wote kupenda vitu vinavyofanana. Walizungumza vitu vingi sana, hii ikamsaidia Tony kujua picha nzima ya mkoa huo japo kwa uchache.

    Tony akarudi sehemu ya beach na kupunga upepo wa eneo lile, hakuacha kusifia uumbaji wa Mungu kwa hakika alishuhudia warembo walioumbwa wakaumbika, alijisikia furaha sana moyoni mwake.



    “Sasa huu si mtihani hata sijui nimsemeshe yupi kati ya hawa, kila mtu ni mzuri na ana kitu cha utofauti ambacho mwenzake hana,” alisema Tony kwa sauti ya chini ambayo haikusikika na yeyote yule.



    Baada ya muda mfupi wafanya kazi wenzake wakawa wamefika hotelini Pale, Tony alipigiwa simu baada ya wao kuambiwa kuwa tayari kuna mtu aliyewaandalia sehemu ya kufikia. Tony akawafata na kuwakaribisha kwa tabasamu zito, tabasamu lile likakata hasa baada ya macho yake kukutana na ya Martha. Wawili hao wanasiri nzito sana ambayo kila mtu hataki kuikumbuka na ndio maana mara zote wanazokuwa karibu mmoja wao anajikuta akishindwa kuuficha ule mfukuto wa moyo.

    “Daah! Sisi tulijua ndio umetuacha kwenye mataa,” alisema Jose.

    “Nadhani unanifahamu vizuri linapokuja swala la kazi masihara uwa naweka pembeni”

    “Maana kila tukikutazamia hukutokea kumbe mwenzetu umetuwahi huku au ndio vile nini!”

    “Hahahah! Kama kawaida si unajua jiji la mahaba hili,” alisema Tony.

    “Kwa hiyo ushachukua namba za wangapi?” Jose aliendelea kuuliza,

    “Wengi tuu!”

    “Jamani mtaongea mambo yenu mkiwa wenyewe tupo kwa ajili ya kazi, tuambie umechukua vyumba vingapi?” alisema Martha.

    “Vyumba 6 tuu”

    “Nini! Tunawezaje kulala kwenye vyumba 6 wakati sisi tupo 12?”

    “Tutalala wawili wawili”

    “No thanks! Siwezi kulala na mtu naomba uongeze vyumba”

    Kauli ile ilimfanya Tony ajisikie vibaya mno kwani hakupenda pesa nyingi itumike kwa ajili ya malazi wakati pesa ile inaweza ikagaiwa kwa wafanyakazi kwa ajili ya kuwaongezea pesa za kujikimu kwa kipindi ambacho watakuwepo katika jiji hilo. Akawaangalia wafanyakazi wengine na kuwauliza,

    “Na ninyi mnasemaje?”



    Wote wakaunga mkono kauli ya Martha, hivyo Tony akapiga simu mapokezi na baada ya muda mfupi mhudumu akafika akiwa na funguo nyingine 6. Martha na Tony wakakosa vyumba upande ule ikabidi waende ghorofa moja Zaidi na huko wakapata vyumba ambavyo milango yao ikawa inatazamana.

    “Samahani mhudumu! Siwezi kupata chumba tofauti na hiki?” alisema Tony.

    “Hapana kaka yangu vyumba vya hadhi yenu ni hivi tuu na vingine vyote vinawatu si unajua tena msimu wa sikukuu huu,” alisema Mhudumu.

    “Sawa akhsante”

    “Mkiwa na shida yeyote mtapiga simu mapokezi”



    Mhudumu akaondoka na kuwaacha Tony na Martha wakiingia vyumbani mwao kila mmoja. Katika ulimwengu huu wakidigitali mambo mengi hufanyika kwa njia ya mtandao, hii ikampa fursa Martha ya kutoa taarifa ya kikao kitakachofanyika jioni ya siku hiyo. Wafanya kazi wote wakaipata taarifa hiyo sababu kampuni hiyo ilihakikisha wafanyakazi wake wote wanakua na simu zenye uwezo wa internet hii imerahisisha kwa kiasi kikubwa ufikiwaji wa taarifa za dharula kwa wafanya kazi wote.

    Tony alipohakikisha kuwa kila mmoja yupo katika chumba chake, hakuwa na kazi tena kwa wakati huo kama kawaida yake ikabidi ashuke kwa swahiba wake wa Muda mfupi ambaye ni mfanyakazi katika hoteli hiyo kama mlinzi.

    “Braza nimerudi tena!”

    “Aah! Karibu asee tupo tunavuta masaa tuu hapa”

    “Sasa broo mi shida yangu unielekeze huko Raskazone maana vya kuadithiwa sitaki nataka nikathibitishe kwa macho yangu”

    “Hahaha! Kumbe unamaanisha kweli, ila mbona msafara wenu unawarembo tuu tena kama yule sijui ni meneja sijui nani asee acha tuu”

    “Aaah! Wale kila siku nawaona nataka sura mpya”

    “Poa basi kuna tax apo nje pia kuna bajaji mbele kidogo, hivyo uamuzi wako juu ya usafiri wa kuutumia ukiwatajia jina la Raskazone hamna hasiyepafahamu”

    “Poa broo shukrani”

    “Karibu tena!”





    Tony akatoka tayari kwa safari ya huko Raskazone, akasogea zilipo Tax na kuanza kumpa dereva maelekezo,

    “Huko napafahamu vizuri, usiwe na shaka,” alisema dereva wa tax.

    “Sasa inakuwa shilingi ngapi?”

    Kabla dereva hajajibu simu ya Tony ikaita, kuangalia akakuta ni namba ngeni ikabidi haipokee,

    “Uko wapi kuna vitu tunahitaji kuviweka sawa kabla ya kikao cha jioni,” ilisema sauti ya upande wa pili.

    Tony akaisikiliza vizuri na kugundua kuwa ni Sauti ya Martha mwanamke ambaye kiukweli hakupenda kuwa karibu naye hata kidogo.

    “Samahani siwezi kuja nimetoka sipo Hotelini,” alijibu Tony.

    “Ulisema linapokuja swala la kazi, masihara unaweka pembeni, sasa nini hiki ambacho unaniambia. Mimi nawe tu wakurugenzi na kabla ya kukaa na wenzetu jioni lazima tukutane tuwe na mipango inayoshabihiana,” alisema Martha.



    Tony akamsikiliza mrembo yule kwa makini kisha akaamua kuvunja safari yake na kurejea hotelini ambapo akapanga akutane na Martha katika fukwe iliyopo hotelini hapo. Haikuchukua muda wawili hao kukutana tayari wakaka na kuanza kujadili mpango kazi.

    “Makala yetu lazima ioneshe utamaduni, vivutio vya asili na sehemu za kihistoria katika mkoa huu, hivyo nafikilia tufanye maojiano na hawa waongozaji wanaokuwa katika sehemu hizi za kihistoria awe anasimulia na sisi tunamrekodi,” alisema Martha.

    “Wazo zuri lakini mimi ninafikiri tofauti kidogo” alisema Tony baada ya kumsikiliza Martha kwa makini mno.

    “Wewe unataka iweje?”

    “Mimi naona tusimrekodi huyo muongozaji badala yako tuchukue clip za sehemu tunazozitaka alafu wengine wafanye kazi ya kuchukua historia ya hizo sehemu kisha, tutaingia studio na kutengeneza audio zenye kuelezea hayo maeneo tutakuja kuzichanganya na hizo picha”.

    Martha hakuwa na la kupinga juu ya wazo lile, akamuunga mkono Tony kwa asilimia zote,

    “Sawa nadhani tumemaliza tutaonana jioni,” alisema Tony.

    Wakati wawili hao wakiongea kwa mbali Jose akawa anaangalia, akaanza kuhisi wivu na kwa kuwa alimjua vyema Tony kuwa huwa afanyi makosa akiachwa karibu na msichana sio yeyote ila mrembo ndio kigezo kikubwa. Jose akahisi kuwa endapo ukaribu huo utazidi basi ni wazi hatoweza kumpata Martha mwanamke ambaye alitokea kumpenda kwa muda mrefu toka alipotua nchini ila akakosa tuu ujasiri wa kuelezea hisia zake.

    “Nina nini Mimi? Mbona moyo wangu unaenda kasi kuliko kawaida, je nina hisia zozote juu ya mrembo huyu, ooh! Tony kwa wengine wote sawa ila kwa huyu hapana,” alisema Tony moyoni huku bado akimtazama Martha.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Martha akagundua kuwa Tony anamtazama kwa macho ambayo hayakuwa ya kawaida na yaliyojaa maswali mengi. Wakati akiendelea kutafakari yale Jose akafika na kuingilia maongezi,

    “Vipi mabosi mna kikao au!”

    Tony akamtazama Jose kisha akachukua tarakishi (laptop) yake na kuinuka,

    “Hapana tushamaliza! Karibu upige stori na bosi mimi ngoja niende misele”

    “Mhmhmhm! Ushampata nini wa kuzuga naye”

    “Bado ndio naenda kumsaka,” alisema Tony na kuondoka.

    “Hivi kwa nini mnapenda sana kuongea habari hizo kila mkikutana?” aliuliza Martha.

    “Tofauti na kazi ndicho kitu ambacho Tony anakipenda,” alijibu Jose.

    Martha akamtazama sana Jose, ambaye alikuja na sura ya tofauti kidogo na siku zote.

    “Tony ni mlaghai sana katika mapenzi nimeshuhudia wasichana wengi wakilia kwa sababu yake”

    “Kwanini unaniambia haya?” Martha akauliza.

    “Sitaki yakukute kama yaliyowakuta wao”

    “Jose! Do you think am cheap eenh!, (Jose! unahisi kuwa mimi ni mrahisi hivyo!)”

    “Hapana ila ni kama tahadhari tuu”

    “Kuna vitu vingi ambavyo wewe huvijui kuhusu Tony, kwa hiyo ni afadhali tukaacha kumzungumzia yeye, Je! Unalingine la kusema nahitaji kwenda kupumzika!”

    “Martha kuna kitu naomba tuzungumze kwa kirefu zaidi”

    “Ya kiofisi au binafsi?”

    “Binafsi tuu”

    “Naomba unitafute baada ya kikao sababu akili zangu kwa sasa zipo kwa ajili ya hiko”

    “Sawa bosi”



    Kadri ya muda ulivyozidi kwenda ndivyo Jose akajenga ujasiri wa kutaka kuelezea hisia zake kwa bosi wake japo ni mkubwa kikazi lakini mapenzi hayaangalii matabaka. Aliweka Imani kuwa ipo siku mrembo yule atamuelewa japo hakujua ni wakati upi hasa. Tony alionekana kuwa tishio kidogo katika harakati zake za kumpata Martha japo hawakugombana ila taratibu akajikuta akijenga chuki moyoni mwake.

    Muda wa kikao ukawadia kila mmoja akachukua nafasi yake kusikiliza kile walichoitiwa, Martha akawa wakwanza kuzungumza,

    “Jamani leo ni jumatatu, mategemeo yetu kuimaliza hii kazi ijumaa mapema walau mpate nafasi ya kuburudika, safari ya kurudi Dar es salaam itakuwa jumapili na jumatatu ofisini kama kawaida. Kikubwa naomba tushirikiane na kujituma katika hili,” alisema Martha kisha akampa Tony nafasi ya kuongea.

    “Tumekuwa marafiki sana lakini hiyo isiwe sababu ya kuweka ulegevu katika kazi, kesho ndio tunaanza rasmi hivyo majukumu ya kila mtu yapo katika faili ambayo muda si mrefu nitatuma kwenye anuani ya barua pepe zenu. Hatutofanya mahojiano kama ilivyokuwa awali ila sasa hivi jitahidi kuandika kila tukio kwa usahihi na mimi nitajitahidi kupata kila picha, baadaye tutaingia studio na kuingiza sauti kisha kazi yetu itakuwa imekamilika,” alisema Tony.



     Maongezi yalikuwa ya kirefu Zaidi kila mmoja alikumbushiwa majukumu yake, hari ya kazi ikajaa mioyoni mwao. Mambo yakawa tofauti kidogo kwa Joseph ambaye tayari alisharuhusu hisia za mapenzi zitawale akili yake muda wote alimtazama Martha bila kuzingatia kile kilichokuwa kikizungumzwa,

    “Leo lazima nimueleze hisia zangu, siwezi kusubili hata kidogo,” alisema Jose.

    Kikao kikafungwa kwa wote kupata chakula cha usiku, wengi walionekana kuufurahia msosi huo kwa kiasi kikubwa.

    “Jamani eenh! Mimi ngoja nikacheze buzuki kidogo, kama mjuavyo napenda sana muziki kwa hiyo nyie endeleeni tuu,” alisema Tony na kuanza kuondoka.

    “Mhmhmh! Kama kawaida yako wee nenda, tushakuzoea,” alisema Jose.



    Tony alijivuta hadi eneo la muziki, akakuta watu wa kila namna wakisakata rhumba, baada ya muda Dj akabadili muziki na kuweka ule wa taratibu, asilimia kubwa ya waliobaki uwanjani walikuwa wawili wawili. Tony akawaza ni namna gani ataucheza mziki ule akakosa jibu, akili ikamtuma atafute mtu wa kucheza naye, akatazama huku na huko kwa mbali akamuona msichana mrembo akiwa amekaa peke yake akinywa mvinyo. Ikabidi atumie dakika kadhaa kuhakikisha kama yule msichana yuko peke yake au yupo na mtu, dakika 5 zikapita bila mtu yeyote kusogea eneo lile. Tony akatumia fursa hiyo bila kupoteza muda,

    “Excuse me miss! May I join you? (Samahani! Naweza ungana nawe?),” alisema Tony.

    Mrembo yule alitumia sekunde kadhaa kumtazama Tony kabla ya kujibu, alishangazwa na tabasamu zito aliloichia kijana yule. Akajikuta akivutika Zaidi kutaka kujua nini Tony anataka kusema,

    “Ofcourse yes! (bila shaka ndio!),” alijibu yule msichana.

    Tony akasogeza kiti na kukaa, akamuita mhudumu na kuagiza kinywaji kisha akafungua maongezi na msichana yule,

    “Umekuja mwenyewe au uko na mtu?”

    “Nimekuja na rafiki yangu, ambaye ni yule aliyevaa blauzi ya pinki,” alisema msichana yule huku akimuonesha Tony sehemu ambayo watu wanacheza muziki.

    “Sasa mbona wewe huendi kucheza?”

    “Mhmhmh! Sina ujasiri wa kucheza mbele za watu”

    “Kwanini?”

    “Basi tuu sijazoea”

    “Unaonaje ukizoea kuanzia leo”

    “What do you mean? (Unamaana gani)”

    “May i dance with you? (Naweza kucheza nawe?)”

    “No thanks!, (hapana!)

    “Usikatae tafadhali! Nahisi upweke kidogo walau twende tukacheze kidogo na nafikiri tutazidi kufahamiana kadri ya muda unavyoenda”





    Msichana yule akafikiri kidogo, kisha akaongeza mvinyo wake kwenye bilauri na kunywa kwa haraka, alipomaliza akasimama na kumwambia,

    “Twende!”

    Tony hakuamini kama ingekuwa rahisi kwa msichana yule kukubali, akajenga Imani kuwa kama amekubali kucheza naye hayo mengine hawezi kuchomoa hata iweje.



    **********CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Jamani nyie hivi kazi kweli itafanyika kesho, maana director wetu ni balaa, mwangalieni kule,” alisema mmoja wa wasichana ambao wanafanya kazi katika kampuni ambayo Martha ndiye meneja.

    “Aaah! Yule jamaa ni kumbakumba asee, alafu kama mchawi vile yeye ananasa warembo tuu,” alisema Jose kwa sauti kidogo ambayo ilimfanya Martha naye kusikia.

    Martha akatazama alipo Tony, akakuta amemshika msichana yule ambaye wote hawakumfahamu, kwa mbwembwe za Dj taratibu walionekana kuufurahia muziki ule.

    “Bosi eenh! Muda umeenda sana, na nidhamu ya kazi ni bora Zaidi, kamwambie Tony akapumzike asije tukwamisha kazi kesho,” Jose alisema.

    “Mwacheni sie tuondokeni,” alijibu Martha.



    Mabadiriko yale yaliwashtua wengi kidogo, wakashangaa kwa nini bosi wao huyo muda mfupi uliopita alikuwa akicheka na kufurahi, sasa amekasirika na kuondoka kama amegombana na mtu.

    “Nyie sio bure mjue! Nahisi bosi Martha anampenda Tony”

    “Nini! Acha kuongea vitu usivyovielewa wewe,” alisema Jose.

    “ila hata mimi nahisi hivyo maana mara nyingi Martha anaonekana kumtetea sana Tony na tukianza kuongelea habari za Tony kuwa na wanawake wengi tunamuona wazi kama anaumia hivi japo hataki kuweka wazi maumivu yake, mfano mdogo ni sasa hivi,” alisema Bosco ambaye naye pia ni mfanyakazi wa kampuni ila yeye yupo katika kitengo cha kuseti mwanga.



    “Martha hawezi kumpenda mtu kama yule,” alikazia Jose.

    “Mhmhmh! Vipi ndugu mbona kama unatetea sana au nawe tayari ushamzimia bosi,” alisema Bosco.

    “Ilo alikuhusu,” alijibu Jose na kuondoka.

    “Jamani eenh! Huyo ndiyo Tony asije fanya tukazidi kukosana wenyewe kwa wenyewe, hata hivyo ana uhuru wa kufanya hivyo, nadhani itakuwa busara kama sisi sote tukaenda kupumzika na akili zetu tuziweke kwa ajili ya kazi kesho,” alisema Bosco.

    Kila mmoja akakubaliana na shauri la Boso, bila kupoteza muda wakaelekea vyumbani mwao tayari kwa kupumzisha akili na miili yao.



    *****************



    “Japo tumecheza kwa takribani dakika 20 sasa lakini sijalifahamu jina lako,” alisema Tony kwa sauti ya chini.

    “Ooh! Ni kweli nimenogewa na muziki kiasi cha kujisahau, mimi naitwa Leilah”

    “Ooh! Leilah sina wasiwasi na jina lako, maana linalandana sawia na uzuri Mungu aliokujalia, mimi naitwa Tony”

    “Jamani hata wewe una jina zuri”

    Maongezi ya hapa na pale yakaendelea huku wakisindikizwa na muziki wa taratibu ambao kwa hakika uliwafanya wajisahau. Kadri muda ulivyozidi kwenda ndipo hisia za kila mtu zikaanza kubadirika, Leilah akaligundua hilo akaomba kwenda kupumzika. Tony bila hiyana akaridhia,

    “Tony I have to go, am out of time, (Tony acha niende muda umekimbia sana)”.

    “Owky! Can I have your phone number? (Sawa! Je naweza kupata namba yako?)”.

    “No need of it! We shall meet if we destinied to, (haina haja, tutaonana Mungu akipenda)”.



    Tony hakutegemea jibu lile toka kwa msichana yule, akafikiri kama atakuwa amekosea mahali lakini hakupata jibu, na kwake ilikuwa mara ya kwanza kujibiwa vile.

    “Kweli haina haja! Je naweza kukusindikiza?”

    “Haina haja pia rafiki yangu ametangulia na ananisubili”

    “Sawa ukikaribia kwa rafiki yako nitakuacha uende”

    Leilah hakuongea kitu Zaidi ya kupiga hatua ndefu kuelekea sehemu yalipo magari, kabla hajafika Zaidi akasimama na kumtazama Tony,

    “Naomba tuishie hapa! Sihitaji rafiki yangu akuone!”

    Tony hakuongea kitu Zaidi ya kumvuta mrembo yule karibu yake, akahakikisha hakuna umbali wowote kati yao,

    “Unataka kufanya nini?” aliuliza Leilah.

    “Je uwezi kunyamaza na kutulia walau kwa dakika mbili?”

    “Hapana! Mwenzangu ananisubili isitoshe muda umeenda sana”

    “Stay calm, I promise to let you go after few seconds, (Tulia, nitakuacha uende baada ya sekunde kadhaa),” alisema Tony.



    Leilah akafurukuta kutaka kujinasua mikononi mwa mwanaume yule lakini alishindwa akajikuta akikubali kutulia kwa muda huo. Tony hakumfanya lolote msichana yule Zaidi ya kumkumbatia na kumtazama usoni kwa macho yenye uhitaji. Leilah naye akamtazama Tony kwa macho malegevu,

    “Sihitaji namba yako wala sitotaka kukuona tena, kama sekunde hizi chache zitaisha hivi hivi,” alisema Tony.

    Mapigo ya moyo yakamuenda mbio sana Leilah akajikuta katika wakati mgumu wa kushindana na nafsi yake. Akahisi kuvutiwa Zaidi na kijana yule, machozi ya kushindwa yakaanza kutiririka mashavuni mwake. Akaiunua mikono yake na kulikubali kumbatio lile la Tony, ndani ya dakika mbili tuu hakuna aliyeelewa nini kimetokea Zaidi ya kujikuta wakiwa katika hali nzito ya ndimi zao kuungana. muda waliopanga ukaisha Leilah hakushtuka wala hakutamani kumuachia tena Tony. Tony alifanikiwa Kwa kiasi kikubwa kucheza na akili ya Leilah hadi kuugundua udhaifu wake, wakati wakiendelea kukisi ghafla rafiki yake na Leilah akawakuta katika hali ile. Rafiki yule hakuliamini hilo hata kidogo, ikabidi aangushe chupa ili kuwashtua na hapo ndipo akili ikamrejea Leilah. Akajikuta akilia Zaidi na kukimbia, hakutamani kumtazama Tony usoni. Tony akabaki ameduwaa yule rafiki wa Leilah akamsogelea Tony na kumwambia,



    “Leilah ni mke wa mtu, anampenda sana mume wake, hana muda mrefu toka aolewe na hakuwahi kufikilia kumsaliti mumewe hata siku moja, mimi nimebeba dhamana ya kuja huku baada ya mumewe kusafiri kikazi. Kwa hiyo tafadhali naomba ukae mbali naye acha kuuyumbisha msimamo wa Leilah”.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kauli ile ikawa kama amemwagiwa maji ya baridi, pamoja na kuchezea wasichana ila hakuwahi kufikiri kufanya ukatili huo kwa mke wa mtu, kwa mara ya kwanza Tony akajihsi mkosaji,

    “Sawa nimekuelewa dada yangu hili alitotokea tena”.

    Tony alijibu na kuondoka eneo lile, huku akili yake bado haikukaa sawa, akashindwa kuamini ukweli wa mambo kuwa Leilah ni mke wa mtu maana ndani ya muda mfupi ule alijihisi kuwa yupo sayari nyingine, akatamani kulipata penzi la Leilah.

    Huku nyuma Leilah naye hakuamini kilichotokea muda mfupi uliopita, akawa analitaja jina la mumewe huku akiomba msamaha.



    “Usijali rafiki yangu hayo mambo huwa yanatokea, nitakutunzia hii siri,” alisema rafiki yake Leilah.

    “Najua wajua kiasi gani mume wangu ananipenda name nampenda ila kilichotokea kwa kweli hata sielewi yaani”

    “Basi yameisha hayo kikubwa ni kuwa makini siku nyingine”



    *********************



    Usiku ukapita na siku nyingine ikaanza, watu wote wakakusanyika tayari kwa kwenda kazini isipokuwa Tony pekee,

    “Mmeona kile nilichosema jana, huyu jamaa lazima atatuchelewesha tuu,” alisema Jose.

    “Twendeni bhana anajua tunapoanzia,” alisema Bosco.

    “Acheni papara muda tuliokubaliana ni saa 2 kamili na sasa ni saa 1.55, bado dakika 5 nzima tuvute subira kidogo,” alisema Martha.

    Jose taratibu akaanza kusadiki maneno ya wafanyakazi wenzake kuwa Martha inawezekana akawa kweli anampenda Tony maana kila jambo haachi kumtetea. Kabla ya dakika 5 hazijaisha Tony akawa amefika eneo hilo, alionekana amepooza kidogo.

    “Bila shaka kila mtu ni mzima, ni wakati wetu wa kuwajibika sasa akili zetu ziwe kwenye kazi,” alisema Tony.

    Wote kwa pamoja wakaingia kwenye gari na safari ya kwenda amboni ikaanza, njiani wakaongea mengi juu ya mipango ya kazi. Lakini Tony hakuonekana kuwa sawa kabisa jambo lile liliwashtua wengi mno. Kila mmoja akatamani kujua nini hasa kinachomsibu.



    Akili ya Tony kwa muda huo ilikuwa juu ya mrembo Leilah, mtoto wa kitanga ambaye kwa muda mfupi tuu tayari alishauyumbisha moyo wake. Tony mwanaume ambaye kiukweli hakuweza kumuacha mwanamke mzuri kama Leilah akikatiza mbele yake. Mtihani ni kwamba msichana yule tayari ni mke wa mtu hivyo ni hatari sana kama angelazimisha ukaribu.







    Siku zikazidi kuyoyoma hatimaye kazi iliyowapeleka Tanga ikakamilika, ilikuwa ni siku ya ijumaa hivyo ikabidi wafanyakazi wapewe uhuru wa kufanya mambo yao binafsi.

    “Jamani leo usiku tutafanya sherehe ya kupongezana kwa kazi nzuri tuliyoifanya hivyo kila mmoja akapumzike na saa 3 usiku tukutane tunapokutanaga siku zote,” alisema Martha.

    Kila mmoja akausubili muda huo kwa hamu Zaidi lakini hali ikawa sio shwari kwa Tony, tamaa ya kumpata Leilah ikazidi kumuingia,

    “Daah! Kwanini namuwaza sana msichana huyu, nitamuona wapi! Sijui anapokaa wala sina namba zake” alisema Tony kwa sauti ambayo hakuna mtu aliyeweza kuisikia.



    *************



    Muda uliokuwa ukisubiliwa ukawadia, wafanyakazi wote wakawa sehemu moja, keki maalumu ya kupongezana ikaandaliwa, Tony na Martha wakaikata keki ile na kuwarisha wafanyakazi wao. Hakika ilikuwa siku ya furaha mno, wakafungua shampeni na kila mmoja akamiminiwa baada ya hapo ukafata wasaa wakucheza muziki. Ilikuwa vituko katika uwanja wa muziki maana asilimia kubwa tayari walishalewa hawakufata stepu ila kila mmoja alicheza vile alivyoona inafaa.



    Chakushangaza Zaidi Martha naye alikunywa pombe siku hiyo, alionekana akiwa mwenye furaha kuliko siku zote zile. Wakajikuta wote wakiwa chakali hakuna aliyeweza kumsaidia mwenzie, Tony akawa wa kwanza kuondoka eneo lile na kwenda chumbani kwake kupumzika. Alitembea kwa kupepesuka na alipofika moja kwa moja akajitupa kitandani, fikra zikaenda mbali akahisi kama vile yupo karibu na Leilah. Huku nyuma kila mmoja naye akajikokota kuelekea chumbani kwake, hali ilikuwa ngumu kwa Martha ambaye hakuzoea kunywa kilevi, alijitahidi kutembea hadi kufika juu hakuelewa chumba chake kipi, kila chumba alichogusa kilikuwa kigumu, akapapasa na kutoa funguo yake, hakukumbuka hata namba ya chumba chake. Akasogea katika chumba chake ila kila alipojaribu kufungua akashindwa akahisi labda amekosea, akageuka nyuma na kukisogelea chumba cha Tony alipogusa kitasa mlango ukafunguka. Bila kusita akaingia chumbani na kuufunga mlango, kisha naye moja kwa moja akapanda kitandani alipo Tony.



    Tony aliendelea kuweweseka na kuhisi tayari Leilah amemkaribia pale kitandani, akajikuta akimkumbatia Martha bila kujua, Martha naye hakuwa anaelewa akajikuta anatoa ushirikiano kwa Tony. Muunganiko wa wawili hao ukafanya hali ya hewa nje kubadilika, radi ikapiga na upepo mkali mithili ya kimbunga ukawa unavuma,

    “Hata kama wewe ni mke wa mtu lakini nimetokea kukupenda sana, naomba usiku huu usisahaulike vichwani mwetu,” alisema Tony.

    “Nakupenda pia,” Martha alijibu.

    Tony alijiona mshindi kwa kiasi kikubwa, kilichofata hakuna anayeelewa. Maana wote wakapitiwa na usingizi mzito.



    *****************

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ni Asubuhi nyingine tena, Tony akawa wa kwanza kuamka, kichwa kilikuwa kizito mno kutokana na uchovu wa jana, akataka kutoka kitandani lakini akagundua kuwa hakuwa na nguo, akajaribu kuvuta kumbukumbu lakini alichokumbuka ni kuwa aliingia chumbani kwake na kulala akiwa na nguo zote. Alipotazama pembeni hakuyaamini macho yake alipoona Martha akiwa pale,

    “Mungu wangu! Nini tena hii, huyu mwanamke amefata nini chumbani kwangu?”

    Tony alijikuta akijiuliza mfululizo bila kupata majibu ya maswali yake, wakati akiendelea kufikilia hayo Martha naye akaamka, alishikwa na bumbuwazi baada ya kuona akiwa amelala na Tony kitanda kimoja. Akakurupuka lakini alishindwa kunyanyuka hasa baada ya kuona nguo zake zote zikiwa chini, alihisi kuchanganyikiwa asijue nini la kumfanya mwanaume yule,

    “Tony kwanini umenifanyia haya tena chumbani kwangu bila ridhaa yangu,” alisema Martha.

    “Nikuulize wewe Chumbani kwangu umefata nini, na kwanini umenifanyia haya,” Tony alijibu.



    Martha alivyotazama vizuri akagundua kweli hakuwa chumbani kwake, nguvu zikamuisha akajikuta akidondosha chozi asijue nini la kufanya. Tony akachukia mno kwani pamoja na kujua kuwachezea wanawake lakini hakufikilia kama hatakuja lala na msichana yule, akaingia bafuni na kumuacha Martha pale kitandani. Martha akaamua atumie muda huo kurudi chumbani kwake ile anatoka mlangoni akakutana na Bosco, alishtuka mno, uso wa aibu ukamjaa. Bosco hakutaka akashikwa na kigugumizi asijue amwambie nini Bosi wake huyo,

    “Bosi! Jana uliisahau funguo yako hivyo wamenipa nikuletee na sikujua kama utakuwa umelala kwa Tony,” alisema Bosco.

    Martha akafungua mkoba wake na kugundua ile funguo aliyokuwa akiitumia usiku ulopita haikuwa ya hapo. Akaichukua funguo ile aliyopewa na Bosco bila kusema lolote, akaingia chumbani kwake na kujifungia humo. Bosco ikabidi arudi kwa wenzie akiwa anacheka jambo ambalo liliwafanya wawe na shahuku la kutaka kujua kilichojili,

    “Hahahahaha! Jamani Tony sio mtu mzuri walah!” alisema Bosco.

    “Kwanini wasema hivyo!” Jose akauliza.

    “Mhmhm! Mlivyonipa ile funguo nikawa naelekea kwa Tony kumuuliza uenda akawa anafahamu lolote ila nilichokutana nacho nikaishiwa pozi”

    “Umekutana na nini wewe”

    “Nimemkuta bosi Martha akitoka chumbani kwa Tony na inavyoonesha walilala pamoja”

    Kauli ile ikawa kama mwiba mkali kwenye kidonda kibichi ilipotua masikioni mwa Jose akajikuta anainuka na kuondoka bila kuaga.



    ***************



    Tony alipotoka bafuni hakumkuta Martha, hakutaka kujishughulisha kujua alipo msichana yule japo ukweli hakuwa na ujasiri pia wa kuonana naye, akaamua kuama hoteli siku hiyo akapanga vitu vyake na kuondoka bila kumtaarifu yeyote.

    Muda wa kukutana ukafika, wote wakakusanyika kasoro Tony pekee, Martha akajiuliza alipo mtu yule ila akashindwa kupata jibu, akatamani ampigie simu lakini hakuwa na ujasiri huo.

    “Leo ni siku ya kuwa huru, nendeni popote mpendapo ila kumbukeni kesho asubuhi na mapema tutaanza safari ya kurejea Dar,” alisema Martha.



    Kila mtu alifurahi isipokuwa Jose ambaye ni wazi hakuwa na raha hasa baada ya kusikia kuwa mwanamke anayempenda amelala na mwanaume mwingine tena asiyejua thamani ya mapenzi. Martha aliamua kutumia muda wake kukaa ufukweni na kuangalia mawimbi ya bahari, huku akifikiri mambo mengi ambayo yalikwisha tokea katika maisha yake, hakutaka kwenda popote siku hiyo. Jose aliona kuwa hiyo ndiyo nafasi pekee ya kuelezea hisia zake. Akajisogeza hadi alipo Martha,

    “Tone moja la maji haliwezi badili ladha ya maji chumvi haya, ingawa kwa uweza wa Mungu yawezekana, ndivyo ilivyo kwa neno langu moja kutoweza kubadili msimamo wako ingawa kwa thamani halisi ya neno lile inawezekana,” alisema Jose.

    “Unamaanisha nini kusema hivyo?” aliuliza Martha.

    “Naomba hifadhi ndani ya moyo wako, naahidi kuwa mwema na muwazi siku zote”

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Martha alishtuka mno kusikia kauli ile ya Jose hakuwahi kufikilia kama itatokea siku ataambiwa maneno yale.

    “Martha nakupenda na nahitaji uwe wangu”

    “Nadhani nilishakuweka wazi msimamo wangu juu ya mapenzi, tafadhali naomba uelewe siwezi kuwa na mtu kwa sasa”

    “Sijali! Hata kama hutonipenda kwa sasa ipo siku utakuja nipenda huko baadae, tafadhali Martha!”

    “Am sorry Jose! I can’t give you what you want, (Samahani Jose! Siwezi kukupa utakacho)”

    “Why! Is it because of Tony?, (Kwanini! Je ni kwasababu ya Tony),” alisema Jose kwa hasira kidogo na kumfanya Martha ashtuke.







    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog