Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

SINGIDANI - 2

 







    Simulizi : Singidani

    Sehemu Ya Pili (2)





    Ni saa nne na dakika zake usiku. Chris alikuwa anatoka kwenye Baa ya G8, Kibaoni. Kutoka hapo hadi ilipo hoteli yake ni jirani mno, ni mwendo wa dakika mbili tu kwa miguu. Njiani akakutana na mmoja wa wahudumu wa hoteli aliyofikia.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akamwambia: “Kaka unatafutwa na maaskari. Kumbe yule mwanamke uliyekuwa naye chumbani ni mke wa polisi, tena ni mkuu pale Central. Wamekuja maaskari wanne na silaha wanakutafuta. Mimi nakushauri usirudi tena. Tafuta mahali ulale mpaka asubuhi wakati tukitafuta ufumbuzi wa hili jambo,” alisema akionekana kujawa na wasiwasi mwingi.Pombe yote ilimruka!



    I kama alikuwa hajanywa hata tone moja la pombe. Kichwa kilikuwa tupu kabisa. Bado alikuwa na maswali mengi kichwani mwake; inawezekana kweli Laura akawa mke wa mtu? Labda inawezekana lakini vipi amwache mumewe na kwenda kujirusha klabu?

    Kichwa kiliwaka moto. Aliumizwa na mengi. Achana na kukamatwa na pengine kufunguliwa mashitaka lakini alijilaumu kwa kujichelewesha kumpata. Angalau angekuwa amefaidi uzuri wake, kidogo ingepooza maumivu ya kile alichoelekea kukikabilia.

    Alimwangalia yule msichana kwa jicho lenye maswali lukuki, lakini alionekana kama ambaye hana majibu sahihi ya maswali yaliyozunguka kichwani mwake.

    “Sikia dada, mimi huwa sipendi mizaha kabisa. Hebu niambie ukweli, kuna maaskari wamekuja pale?”

    “Ndiyo!”

    “Wamevaa nguo za polisi?”

    “Ndiyo, tena kuna mwingine amevaa koti jeusi.”

    Moyo wa Chis ukalipuka.

    “Wamenitaja jina?”

    “Ndiyo. Wamesema wanamtaka Dk. Chris. Tena alitaka tuwafungulie mlango ili wakague chumba chako, tukakataa. Kwa inavyoonekana itakuwa ni kweli. Hili ni tatizo kaka yangu, tafuta mahali pengine pa kulala.”

    Chris akatulia kidogo.

    Mawazo yakazidi kumwandama. Kuna kitu aliwaza; iweje leo hii Laura awe mke wa mtu? Mbona hakuwa na pete kidoleni? Laura si mwanafunzi?

    “Au kuna mchezo nachezewa?” akajiuliza Chris.

    “Halafu kama ni mchezo mtu wa kunisaidia hapa ni mmoja tu, Maulanga.”

    Ni kweli Maulanga, dereva taksi aliyekuwa akimtumia kwa mizunguko yake pale mjini ndiye ambaye angeweza kumsaidia kujua ukweli wa tukio lile. Ni Maulanga huyohuyo ndiye aliyempeleka Laura kwenye nyumba anayoishi.

    “Kwahiyo dada unanishauri nisije kabisa pale?”

    “Huna haja ya kufanya hivyo, lakini kama unaona nakudanganya nenda. Wamesema watarudi tena baadaye, maana wameagizwa na mkuu wao, ukamatwe kabla ya asubuhi.”

    Moyo wa Chris ukapiga.

    “Sawa, ahsante kwa taarifa. Ngoja nitulize kichwa, nitajua cha kufanya. Kwa sasa naomba tu unisaidie namba yako ya simu tafadhali,” akasema Chris, yule dada akatekeleza.

    “Unaitwa nani vile?”

    “Mwanjaa.”

    “Ok.”

    Palepale Chris akaamua kubadilisha kiwanja ili atulize kichwa chake wakati akitafakari cha kufanya. Mwanjaa alirudi zake alipotoka, Chris akachukua bodaboda na kumwambia dereva ampeleke Baa ya Serengeti iliyokuwa katikati ya mji.

    ***

    Chris akiwa Serengeti Bar, alimpigia simu Maulanga na kumwambia amfuate pale haraka sana. Maulanga hakuwa mbali na eneo, alikuwa ameegesha jirani na Benki ya CRDB, lilipo Jengo la TRA la Mkoa wa Singida. Dakika mbili baadaye alikuwa pale.

    “Hivi yule msichana uliyempeleka hosteli jana usiku unamfahamu?”

    “Namuona sana klabu karibu kila wikiendi, huwa anakuja na rafiki zake.”

    “Unajua kuwa ni mke wa mtu?”

    “Mke wa mtu? Sina hakika kwa kweli.”

    “Kivipi?”

    “Yaani sifahamu chochote ingawa nahisi kwamba atakuwa ni mwanafunzi. Si anasoma chuo?”

    “Kwanini unasema unahisi? Kwani siku ile hukumfikisha hosteli?”

    “Kuna nyumba aliingia, akasema anaishi hapo na dada yake.”

    “Lakini mimi aliniambia anaishi hosteli. Dah! Sijui hii ishu ikoje! Nasikia wamekuja maaskari pale gesti, wananitafuta.. eti wanasema niliingia na mke wa mtu mle ndani na mumewe ni askari.”

    “Mh! Mbona majanga haya kaka. Sasa unafanyaje?”

    “Niachie mwenyewe, nitajua cha kufanya. Wewe nenda, nitakuita baadaye.”

    “Poa.”

    Chris alianza kunywa upya kabisa. Baadaye akapata wazo. Alitakiwa kupumzika ili siku inayofuata aweze kwenda zake kijijini kwao. Wazo la Laura alishalifuta kabisa. Aliona tatizo likiwa mbele yake waziwazi kabisa!

    Akatoka pale Serengeti Bar na kutafuta gesti nyingine jirani na eneo lile, akalala. Katikati ya usiku, simu yake ikapigwa. Alipoangalia kwenye kioo cha simu, alishtuka sana.

    Alikuwa ni Laura anampigia!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MACHO ya mshangao yalimtoka. Woga ukamjaa moyoni mwake. Alibaki akiingalia ile simu bila kuipokea. Mara simu ikakatika. Hapo sasa akapata nafasi ya kuangalia simu yake vizuri.

    Alikuta meseji nne, zote zilitoka kwa Laura. Alipoifungua ya kwanza tu, simu ikaanza kuita tena. Chris akazidi kuogopa. Akili yake ilimtuma kwamba, huenda aliyekuwa akipiga alikuwa ni mume wa Laura au walikuwa pamoja na alilazimishwa kufanya hivyo ili aingie mtegoni.

    Hakuwa tayari!

    Simu ilipokatika, mara moja akaanza kusoma ile meseji. Maneno aliyoyasoma yalimchanganya sana. Hakuamini alichokiona. Meseji ile iliandikwa: “Kwa muda mfupi sana umeuteka moyo wangu, tafadhali Chris usinitese. Mbona hujanitafuta wakati tulikubaliana tukutane klabu?”

    Inawezekana vipi mwanamke ambaye aliambiwa ni mke wa mtu ampigie simu usiku ule tena akimwambia kuwa anatakiwa kwenda kukutana naye klabu? Jambo hilo lilimchanganya sana kichwa chake.

    Akaendelea kusoma nyingine mfululizo: “Baba vipi jamani? Mbona kimya? Acha kunitesa.”

    “Chris nimekuwa tayari kukukabidhi moyo wangu wote kwako, mbona sasa huonyeshi kuwa upo tayari?”

    “Sikia, tayari mimi nipo klabu hapa, kama huji niambie nirudi zangu hosteli nikapumzike. Nimekuja hapa kwa ajili yako Chris.”

    Meseji ya mwisho ndiyo iliyomchanganya zaidi. Anamwambia anataka kwenda hosteli? Ni hosteli gani wakati alishaambiwa kuwa ni mke wa mtu?

    Kwa hakika usingizi wote ulipotea. Pamoja na yote hayo, alijua alikuwa mtegoni na kama angejibu chochote angeweza kukamatwa mara moja. Kwa mtu mkubwa kama mkuu wa kituo cha polisi, maana yake ni kwamba, kama angeamua kumfanyia chochote kwa kosa la kutembea na mke wake, angeweza!

    Wazo moja la haraka likamvamia kichwani mwake; alitakiwa kuvunja kabisa line yake. Hakutakiwa kupatikana tena kwa namba ile. Hilo ndilo wazo lililomwingia kwa kasi sana. Hakutaka kufikiria sana kuhusu hilo.

    Akavunja ile line na kuitupilia mbali!

    “Shiiit! Tuone sasa, watanipata wapi! Kwanza mimi sijafumaniwa. Najua wakiamua kunitafuta watanipata, lakini natakiwa kuwa mjanja sana kwenye eneo hilo. Hawawezi kunikamata asilani.”

    Hasira ilimjaa moyoni. Alishindwa kuelewa ni kwa nini Laura aliamua kumdanganya kuwa hajaolewa wakati alikuwa mke wa mtu, tena wa askari kabisa. Jambo hilo lilimuumiza sana.

    Akajilazimisha kulala.

    ***

    Nani asiyemjua Dk. Chris, msanii wa filamu za Kibongo? Kila kona alijulikana. Hilo lilimaanisha kuwa, kama polisi mkoani Singida wangeamua kumtafuta kwa dhati kabisa, wangemkamata mapema sana asubuhi hiyo.

    Chris alilijua hilo. Mara baada ya kuamka, alikwenda moja kwa moja mapokezi na kumuomba mhudumu akamnunulie kofia ya kapero. Yule mhudumu hakuwa na maswali mengi, alichukua fedha kwa Chris kisha akaenda kununua kofia na kumpelekea.

    Chris akaichukua na kuivaa baada ya kujiandaa kikamilifu. Alitoka nje ya gesti hiyo na kutembea kwa mwendo wenye tahadhari zote. Taratibu akiwa ameuficha uso wake kwa kapero, alikodi teksi na kumtaka dereva ampeleke stendi kuu ya mabasi mkoani Singida, Misuna.

    Dakika tano tu zilitosha kumfikisha kituoni hapo. Alishuka na kumlipa dereva kisha akatembea hadi katika ofisi za basi la Beffe, linalofanya safari zake kutoka mjini kwenda wilayani Mkalama kupitia Iguguno na Nduguti.

    “Gari linaondoka saa ngapi?” Chris akamwuliza dada aliyekuwa akimkatia tiketi.

    “Saa tano kamili, kwa sababu leo tunapita hadi Meatu.”

    “Sawa, nipatie tiketi lakini kuna shughuli zangu nazifanya hapa mjini, sitapandia hapa. Mtanikuta kwenye mizani huo muda.”

    “Tafadhali usije kulalamika umeachwa, saa tano juu ya alama uwe pale, sisi tutakukuta hapo.”

    “Haina shida dada.”

    Chris akalipa kisha akaondoka zake na kwenda kuchukua teksi nyingine iliyompeleka Kibaoni, ambapo ndipo gesti iliyokuwa na begi lake na vitu vyake vingine. Gari liliingia eneo hilo na kuegesha mbele ya geti.

    “Naomba ukaniitie mhudumu tafadhali,” Chris akamwomba yule dereva ambaye alitii.

    Sekunde chache sana, Mwanjaa alitokea, akakutana na swali kutoka kwa Chris: “Vipi, jamaa walirudi tena jana?”

    Chris alisubiria jibu la Mwanjaa akiwa mwenye wasiwasi mwingi sana. Bado hakuijua hatma yake.



    WASIWASI ulimjaa moyoni akiwa hajui kabisa kilichotokea usiku wa kuamkia siku hiyo. Macho yake aliyatuliza usoni mwa Mwanjaa akisubiri kusikia jibu lake. Mwanjaa alionekana kusita kidogo.

    “Vipi... walikuja? Naomba uniambie haraka maana natakiwa kuondoka.”

    “Hapana,” Mwanjaa akajibu.

    “Asubuhi hii?”

    “Pia hawajaja.”

    “Sikia... naomba unichukulie begi langu pale ndani, kuna vitu vyangu vingine vidogovidogo vipo kwenye kabati.”

    “Sawa kaka.”

    Mwanjaa akatoka haraka na kwenda ndani. Dakika tatu baadaye, alitoka ndani akiwa na begi la Chris. Ghafla Mwanjaa akaonekana kusimama na kuonyesha kuwa na mshangao mkubwa sana.

    Chris alipoangalia barabarani, akashtuka sana baada ya kuwaona maaskari wanne wenye silaha wakivuka mfereji mdogo uliokuwa pembeni mwa barabara kuu ya Dodoma – Mwanza. Pembeni waliegesha karandinga lao. Kufumba na kufumbua, taksi ilikuwa imezungukwa na maaskari wale.

    “Nimekwisha!” Chris akajisemea moyoni.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hamtakiwi kufanya chochote kwa sasa,” mmoja wa maaskari wale akasema.

    “Tumefanya nini?” Chris akauliza.

    “Haya mikono juu,” akasema yule askari.

    Wakafanya hivyo.

    Maaskari wawili kati yao, waliingia garini na kuanza upekuzi, baadaye wakamuamuru dereva afungue buti. Wakakagua lakini pia hawakuona walichokuwa wakikitafuta ambacho pia hawakusema ni nini.

    “We’ dada, hiyo mizigo ni ya nani?” mmoja wao akauliza.

    “Wa huyo hapo...” Mwanjaa akajibu haraka akimsonza kidole Chris.

    “Lete.”

    Mizigo ikapelekwa.

    Haraka ikaanza kukaguliwa, Chris alikuwa akipewa maelekezo na kuambiwa atoe nguo moja baada ya nyingine na vitu vingine vilivyokuwa ndani ya begi lake.

    “Wewe unaitwa nani?”

    “Naitwa Dk. Christopher.”

    “Unatokea wapi?”

    “Dar es Salaam.”

    “Unaelekea wapi?”

    “Nakwenda Kiomboi,” akadanganya Chris.

    “Tunaweza kuona kitambulisho chako?”

    “Bila shaka.”

    Mara moja Chris akatoa na kuwapa. Wasiwasi ulikuwa moyoni lakini kwa namna fulani ulianza kuondoka akiwa na imani kuwa walichokuwa wakikifuatilia kwake hakikuwa kuhusu Laura tena.

    Wakakagua kitambulisho chake kisha wakamrudishia.

    “Wewe dada ni nani?” askari mmoja akamwuliza Mwanjaa.

    “Mhudumu.”

    “Nahitaji kuona kitabu chako cha wageni,” akasema yule askari akiongozana na Mwanjaa ndani.

    Alipofika getini yule askari ambaye alionekana ndiye kiongozi wao, aligeuka na kusema: “Ninyi mnaweza kwenda.”

    Chris akaingia kwenye gari, dereva akawasha moto, akaondoa gari.

    ***

    Maswali yalikuwa mengi kuliko majibu, lakini jambo kubwa kwa Chris wakati ule ni kwamba alikuwa amefanikiwa kuondoka mikononi mwa hatari ya kuingizwa kwenye kashfa ya kutembea na mke wa mtu. Yaliyoendelea nyuma hayakuwa na maana kwake.

    Ndani ya Basi la Beffe, Chris alikuwa kimya kabisa, akitafakari mtihani wake uleule; kwenda kuoa kijijini.



    ***

    Laura alikuwa akitengeneza nywele zake saluni iliyokuwa Ginnery. Hisia zake za ndani bado ziliendelea kumhakikishia kuwa Chris ndiye angekuwa mwanaume wa maisha yake. Hakutaka kusikia mwanaume mwingine zaidi yake.

    Alijiuliza, kwanini hakupokea simu yake? Kwanini hakuonekana klabu kama walivyokubaliana? Kwanini hapatikani hewani?

    “Kwanini naingia kwenye mateso makubwa kiasi hiki? Nampenda Chris, nina hakika na hisia zangu. Sikutegemea kama hili lingetokea kirahisi hivi, lakini inanipasa nikubali kuwa nimeshatekwa na ninampenda. Nitahakikisha nampata Chris, lazima,” aliwaza Laura.



    SAA 10:00 alasiri, Basi la Beffe lilifunga breki katika kituo cha Mkalama - Shuleni. Dk. Chris alishuka na mizigo yake. Akakodisha baiskeli iliyomfikisha nyumbani kwao.

    Alipokelewa kwa shangwe na bibi yake aliyekuwa akisuka jamvi kwa kutumia  ukindu kiambazani mwa nyumba yao mpya. Walikuwa na eneo kubwa lililozungushwa kwa uzio wa michongoma. Maboma mawili makubwa ya mifugo yalikuwa pembeni mwa nyumba zao.

    Walifuga ng’ombe, mbuzi na kondoo. Nyumba yao mpya iliyojengwa kwa matofali ya kuchoma na kuezekwa kwa bati haikuwafanya wabomoe nyumba yao ya asili ambayo ilijengwa kwa fito na udongo na kuezekwa kwa tembe.

    “Aaaah! Mume wangu huyoo...” bibi alitamka kwa sauti kuu, akijaribu kumkimbilia mjukuu wake.

    Alikuwa ajuza hasa, akiwa na umri wa miaka themanini na tatu, alimudu kufanya shughuli zake ndogondogo za kila siku. Aliishi na wanaye wawili; Shamakala ambaye alikuwa na mke na watoto wawili na Maria aliyekuwa na mtoto mmoja.

    Ilikuwa famili yenye upendo mkubwa. Dk. Chris aliongeza mwendo na walipokutana na bibi yake alimpokea na kumlaza kifuani mwake.

    “Ooh! Daktari wangu huyo... karibu sana baba,” bibi alisema, akishindwa kuficha furaha yake.

    “Ahsante bibi, shikamoo.”

    “Marhaba mume wangu, habari za nyumbani?”

    “Nzuri kabisa.”

    Pamoja na kuzaliwa na kukulia kijijini Mkalama, bibi huyo alimudu vizuri sana kuzungumza Kiswahili japo kuna wakati huchanganya na lugha yao ya Kinyiramba.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mara moja bibi aliingia ndani, akatoka na kipeyu kilichojaa togwa kisha akamkabidhi Dk. Chris apooze koo na kinywaji hicho cha asili. Salamu zikaendelea.

    ***

    Sura ya mwanamke mrembo ilimchanganya Dk. Chris, alimwangalia umbo lake. Akatazama hipsi zilizochomoza vyema pembeni ya mapaja yake, akazidi kutibuka! Matiti madogo yaliyosimama yenyewe kifuani kama embe bolibo, ilikuwa kishawishi kingine kwa Chris.

    Nyongo ya huba ikapasuka. Alikiri kweli mwanamke yule alikuwa mrembo. Chris aliumia moyoni alipogundua kuwa, hawezi kumpata mwanamke yule tena. Ni Laura alikuwa akimjia mawazoni kwa kasi sana.

    Akiwa amekaa chini ya mti, Chris alidongosha machozi kwa kumbukumbu za mwanamke huyo. Alitamani sana kubadilisha ukweli, awe hajaolewa lakini haikuwezekana.

    “Vipi wewe?” Shamakala, baba yake mdogo alitamka akimgusa begani.

    Chris alishtuka na kugeuza shingo  kumwangalia aliyemgusa. Hapo akakutana na sura ya baba yake mdogo. Shamakala akashangazwa na machozi ya Chris.

    “Vipi, mbona unalia?” Shakamala akamwuliza.

    Shamakala na Chris walipishana kidogo sana kiumri. Alikuwa kitindamimba katika uzao wa babu na bibi yake. Sababu hiyo iliwafanya wawe marafiki na kuelezana siri zao zote. Chris hakuona sababu ya kumficha. Alimweleza kila kitu kuhusu kisa cha Laura.

    “Tulia Chris, imekuwa vizuri umegundua mapema.”

    “Lakini kuna tatizo lingine kubwa zaidi.”

    “Lipi?”

    “Mke. Baba amesema natakiwa kurudi Dar na jibu linaloeleweka. Ameniagiza nije huku kutafuta mke, amesisitiza kwamba lazima nioe huku kwa sababu mke bora anapatikana huku kijijini.”

    “Uamuzi wako ni nini juu ya hili?” akauliza Shamakala.

    “Sitaki kuongozwa katika suala hili. Natakiwa kutafuta na kuamua mwenyewe nimuoe nani na wapi. Hata hivyo nilipokutana na huyo Laura, nikaona ndiye mke wangu, imekuwa tofauti.

    “Si neno sana, maana siwezi kubadili ukweli ila baba sitaki kuoa huku kwa sasa, lazima nitulie kwa muda, nirudi mjini nitafute mwanamke mwingine,” akasema Chris.

    “Wazo zuri, lakini mzee atakuelewa? Maana Joseph namjua vizuri sana misimamo yake.”

    “Hapo ndipo ninapohitaji msaada wako baba mdogo. Itabidi tufanye mchezo. Mimi nitamwambia baba nimeshapata mke, wewe ndiye uliyenitafutia. Muda huo nitautumia kuanza kutafuta mwanamke mwingine. Unaonaje?”

    “Sawa kabisa, nipo upande wako. Kaka naye pamoja na kusoma kote huko bado ana mawazo ya kizamani sana. Nitakusaidia, nipo kwa ajili yako!”

    “Ahsante sana baba mdogo.”

    Kilichompeleka kijijini ni kama alikuwa ameshakamilisha. Kilichokuwa mbele yake kwa wakati huo ilikuwa ni kupanga safari ya kurudi Dar. Alitakiwa kurudi haraka kwa sababu  alikuwa ameshasaini mikataba  miwili ya filamu na alitakiwa  kurekodi.

    “Inabidi nirudi Dar keshokutwa.”

    “Mara hii? Mbona imekuwa haraka sana?”

    “Nina vimeo vingi baba mdogo, lakini usijali nitakuacha vizuri.”

    “Songela sana!” (Ahsante sana) alisema Shamakala.

    “Iiiza!” (Ahsante kushukuru)

    ***

    “Jambo moja muhimu ninalohitaji kujua kutoka kwako ni kama umefanikiwa nilichokuagiza kijijini au lah!” mzee Joseph Shila alimwambia mwanaye Chris, alipomkuta nyumbani usiku huo baada ya kurudi kutoka kazini.

    “Nimefanikiwa baba,” akajibu Chris, akitengeneza tabasamu la uongo usoni mwake.

    “Vizuri sana. Moyo wangu sasa una amani. Bila shaka sasa tunatakiwa kufikiria kuhusu mipango ya ndoa tu!” mzee Shila akauliza tena.

    Chris hakujibu!



    ALIKANYAGA mafuta kisawasawa, foleni ni kama ilikuwa hakuna kabisa usiku huo. Dakika kumi tu zilitosha kabisa kumfikisha Mzalendo Pub. Akaegesha gari lake kisha akapanda hadi ghorofa ya kwanza ilipo Pub hiyo.



    Hakupata shida kujua Ramsey alipokuwa amekaa maana walikuwa na kawaida ya kukaa sehemu moja ndani ya Pub hiyo kila walipokwenda. Alimfuata akiwa ameachia tabasamu mwanana.

    “Vipi kaka?” Ramsey akamsalimia.

    “Poa, mambo?”



    “Fresh kabisa... vipi za kijijini?”

    “Daaah! Huko acha tu. Yaani habari ndefu sana kaka. Nimekutana na mengi sana huko.”

    “Usiniambie umepata mwanamke wa ukweli tayari... ni Mnyiramba au Mnyaturu?” akauliza Ramsey.

    “Mh! Wapi ndugu yangu? Majanga tu mzee.”

    “Imekuwaje?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Ngoja nikusimulie.”

    Chris akakaa sawasawa... ni muda huo mhudumu alifika mezani kwake na kutaka kumsikiliza. Aliagiza pombe kali. Wakati mhudumu anakwenda kaunta kumchukulia kinywaji chake, Chris alianza kumsimulia Ramsey.



    Hakuna alichomficha, alimweleza yote yaliyotokea Singida Mjini. Mipango waliyopanga na baba yake mdogo, Shamakala na namna alivyozugumza na baba yake baada ya kuingia Dar usiku huo.

    “Aisee una kazi kaka. Yote hayo nimekusikia lakini sasa nahisi mzee mzima unaweza kuingia kwenye skendo!”



    “Skendo?” Chris akahamaki.

    “Ndiyo! Kama huyo mwanamke wa Singida kweli ni mke wa mtu, tena wa polisi, kuna nini tena kaka? Utachafuka!” Ramsey akasema kwa msisitizo.

    Chris akabaki kimya.



    Maneno yale yalimwingia akilini. Alitulia akifikiria kwa kina, akajikuta akipoteza furaha. Ni kweli alikuwa maarufu kiasi kwamba, mtu yeyote akitaka kumpata muda wowote ingekuwa rahisi tu.

    “Lakini kaka, ukweli ni kwamba sikutembea naye!” Chris akamwambia Ramsey.

    “Sawa ila si ulikuwa naye chumbani?”



    “Kaka kuna mambo ya kisheria hapo. Hata kama nilikuwa naye chumbani, hakuna mtu aliyenikuta nikiwa naye huko chumbani. Kama ningekuwa nimefumaniwa ingekuwa sawa, lakini maneno tu ya mtaani yanaweza kunikamatisha na kuniweka ndani?”

    “Kaka tunywe tu bwana!” akasema Chris kwa sauti ya kilevi.



    “Ndicho kilichobaki mkubwa. Aisee nina majukumu mengi sana wiki hii. Sijui itakuwaje lakini nitajipanga,” akasema Chris.

    Pombe zikaendelea. Haikuwa rahisi kwa Chris kukaa pale muda mrefu hasa kwa sababu ndiyo kwanza alikuwa ameingia Dar. Bado mawazo juu ya Laura yaliendelea kumzonga.

    Alitamani sana Laura asingekuwa mke wa mtu!



    ***

    Laura alipoteza amani ya moyo kabisa... mwanaume aliyempenda ghafla haonekani tena mbele yake. Alifikiria sana namna ya kumpata lakini alikosa majibu.

    Alijiuliza maswali mengi sana, lakini mwisho alipata wazo zuri. Lilikuwa jambo gumu sana kwake lakini alikuwa tayari mradi ampate Chris.



    “Lazima niende Dar es Salaam...” akawaza Laura.

    Lilikuwa wazo zuri lakini lingetumia muda mwingi sana kukamilika. Alikuwa tayari kupoteza masomo japo kwa wiki moja ili aweze kumpata Chris, mwanaume wa maisha yake.

    Mara moja akaanza kupanga mipango ya safari ya kwenda Dar es Salaam.



    ***

    Laura alikuwa amedhamiria hasa. Wiki moja baadaye alikuwa jijini Dar es Salaam. Saa 11:00 jioni alikuwa anashuka ndani ya Basi la ABC katika kituo kikuu cha mabasi ya mikoani na nchi jirani, Ubungo jijini Dar es Salaam.



    Alikuwa amechoka sana. Hakuwa mgeni wa Dar es Salaam. Alikuwa na ndugu zake wawili waliokuwa wakiishi jijini humo ambao kuna wakati huwa anakwenda kuwatembelea.

    Mama yake mdogo aishiye Kurasini na mjomba wake anayeishi Gongo la Mboto ndiyo ndugu zake jijini Dar. Hakutaka kabisa wajue uwepo wake jijini Dar kwa sababu alikwenda kwa sababu maalum.



    Alichukua taksi na kumwambia dereva ampeleke Manzese. Huko aliamini angepata gesti ya bei nafuu ambayo angeishi hapo kwa wiki nzima wakati akimtafuta Dk. Chris.

    Wakiwa wanakaribia mataa ya Shekilango, Laura akavunja ukimya, alijua kwa kumtumia dereva yule angepata mwanga wa wapi pa kuanzia ili aweze kumpata Chris.



    “Kaka hivi nawezaje kumpata Dk. Chris, yule mcheza filamu?” Laura aliuliza kwa sauti laini, akiyalegeza macho yake na kumfanya dereva apoteze umakini barabarani.

    “Vipi unataka kumwa mwigizaji au umeshampenda bibie?” dereva yule akajibu huku akiachia tabasamu, macho yake akiwa ameyatuliza kwa Laura.



    Aliporudisha macho yake barabarani, alishangazwa sana na kitu kilichotokea!

    “Nakufaaa....” Laura akapiga kelele

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    UZURI wa Laura ulikuwa tishio, dereva alishachanganywa na uzuri wa Laura. Pamoja na urembo wa sura yake, hakuweza kuficha ushamba wake wa jiji kubwa la Dar es Salaam. Ingawa alikuwa na ndugu zake, lakini hakuwa akienda Dar mara kwa mara.

    Macho ya kuangaza kila mahali, hakuweza kuyaepuka! Ni sababu hiyo ndiyo ilimfanya dereva achanganyikiwe na kutokuwa makini barabarani. Gari lilikuwa mbele yake kwenye mataa ya Shekilango hakuliona. Aliliona likiwa mita chache sana mbele yake.

    Alifunga breki kwa nguvu... Laura akafumba macho ili asishuhudie ile ajali. Kwa bahati nzuri, akiwa anakaribia kabisa kuligonga lile gari, tayari magari yalishaanza kutembea... taa ya kijani ilishawaka! Hiyo ndiyo ikawa salama yao!

    Taratibu wakateleza. Laura alifumbua macho, akahema kwa kasi sana.

    “Weweee jamaniiii!” akasema kwa sauti dhaifu, akijaribu kuvuta pumzi ndefu sana...

    Akazishusha taratibu kabisa!

    “Kumbe wewe mwoga sana?” dereva yule akasema, safari hii akiwa makini sana barabarani.

    “Kwani we huogopi?”

    “Naogopa pia... lakini usijali. Tatizo ni wewe bwana!”

    “Tatizo mimi, kivipi?”

    “Tuachane na hayo, kuhusu hawa jamaa wa Bongo Movies, ukitaka kuwapata kwa urahisi ni Jumamosi mara nyingi wanakutana Leaders Club.”

    “Kinondoni?”

    “Ndiyo.”

    “Huwa wanafanya nini hapo?”

    “Si unajua tena mambo ya wasanii, wanakutana na kujadiliana mambo yao tu. Kiukweli sijui mambo yao vizuri zaidi ya hapo.”

    “Ahsante, najua nitaweza kuanzia hapo. Ingia hapo kushoto, nataka kushukia hapo Tip Top.”

    “Barabarani kabisa au unataka nikuingize ndani?”

    “Hapana, hapo barabarani tu panatosha kabisa.”

    Dereva akapinda kushoto na kuegesha nyuma kidogo ya kituo cha daladala, Tip Top. Laura akamlipa yule dereva na kubaki hapo amesimama kwa muda. Dereva akaondoa gari.

    Laura aliangaza macho huku na huko, kisha akaamua kuifuata barabara ya vumbi iliyokuwa ikielekea Manzese – Uzuri. Alitembea taratibu kwa mtindo wa kuangaza huko na huko. Mbele kidogo akaona bango dogo juu ya nyumba limeandikwa Waridi Lodge.

    Laura akatabasamu. Akaenda mpaka hapo, akapita moja kwa moja Mapokezi. Akapokelewa na dada mrembo sana, lakini alijihakikishia kuwa, pamoja na urembo wa dada huyo, bado hakufua dafu mbele yake! Yeye alikuwa mzuri kuliko huyo msichana!

    “Nahitaji chumba,” akasema Laura.

    “Umepata mrembo!”

    Laura akaandikisha kwenye kitabu cha wageni. Kisha akepelekwa kwenye chumba chake.

    ***

    Ilikuwa Jumamosi, wasanii wengi wa filamu walikuwa wamekaa kwenye viti vya plastiki, pembeni mwa uwanja wa mpira wa pete katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam. Eneo karibu lote lilikuwa na watu wengi sana.

    Mapema sana!

    Saa tano asubuhi!

    Supu ilinywewa kwa fujo, wengine nyama choma na bia. Kifupi watu walikuwa kwenye mapumziko ya mwisho wa wiki. Wengi wa wasanii wale walikuwa ni wanachama wa klabu yao ya Bongo Film. Wasanii wa klabu hiyo hukutana hapo kila Jumamosi kwa ajili ya kuweka mikakati yao ya kisanii.

    Ilibaki nusu saa tu kikao rasmi kianze.

    ***

    Aliteremsha mguu wa kwanza chini kutoka kwenye gari alilokuwa amepanda. Kisha ukafuata mwingine. Baadaye, mwili mzima ulitoka ndani ya gari. Akasimama na kusukuma mlango kwa nguvu wa gari kwa nguvu. Akapunga mkono kumuaga dereva, ambaye aligeuza gari na kuondoka.

    Alikuwa msichana mrembo kuliko kawaida. Namna yake ya kutembea ikawa kivutio kingine kwa watu waliokuwa wakimtazama wakati akitembea kwa madaha. Macho yote yalikuwa kwake. Si wanaume wala wanawake.

    Wote walishangazwa na uzuri wa msichana yule. Kwa alivyoonekana alijua alichokuwa akikifanya. Alijua alipokuwa anakwenda na alimjua aliyekuwa akimfuata. Alinyoosha moja kwa moja hadi walipokuwa wamekaa wasanii wa filamu.

    Wasanii wote wakapagawishwa na uzuri wake. Akasimama katikati yao, akawaangalia kwa zamu, kisha akavua miwani yake myeusi iliyokuwa usoni mwake. Macho yake mazuri yakawa tatizo lingine!

    “Samahanini jamani... samahani sana ndugu zangu. Nimekuja hapa kwa sababu ya mtu mmoja tu; Chris!” akasema msichana yule.

    Alikuwa ni Laura.

    Dk. Chris alishtuka sana alipomuona Laura eneo lile. Akasimama na kumwangalia kwa hasira.

    “Kaa mbali kabisa na maisha yangu. Sitaki matatizo. Kama umetumwa, mnajidanganya, mimi ni daktari kitaaluma, tena nimesoma nje ya nchi, mimi siyo bwege!” alisema Dk. Chris kwa hasira.



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    CHRIS alikuwa anatetemeka kwa hasira. Kichwani mwake aliamini kwamba, Laura alikuwa akimchezea mchezo. Aliamini alikuwa kwenye mtego ili atapeliwe. Hakuwa tayari kwa jambo hilo hata kidogo. Chris alikuwa amefura kwa hasira.

    Kitu ambacho hakukijua ni namna msichana yule alivyokuwa akimpenda. Alikuwa akimpenda kwa moyo wake wote, ndiyo maana alifunga safari kutokea Singida kumfuata yeye. Kilichompeleka Dar kilikuwa ni mapenzi tu!

    Dk. Chris!

    Hilo tu!

    Hakutaka kulipa nafasi jambo hilo kichwani mwake. Alidhamiria kukaa naye mbali kabisa. Hisia za mapenzi zilishahama. Hakutaka kumuendekeza. Ramsey rafiki yake kipenzi, akamwangalia yule msichana kwa makini.

    Alishawishika sana na urembo wake. Kwa stori za Chris kuhusu mwanamke aliyetaka kumwingiza kwenye matatizo mjini Singida, alianza kuamini kuwa ndiye aliyekuwa mbele yao. Alichokifanya ilikuwa ni kumtuliza rafiki yake kwanza...

    “Kaka tulia tafadhali... lakini ni nani huyu msichana?” Ramsey akauliza kwa sauti ndogo.

    “Ni yule mwanamke wa Singida niliyekuambia. Anataka kuniharibia maisha yangu huyu. Sikia wewe... umekosea njia, ondoka kwenye maisha yangu,” akasema Dk. Chris kwa hasira na sauti ya juu.

    Laura alikuwa analia machozi. Hakuwa anaigiza, alikuwa analia machozi ya kweli kabisa...

    Kama angekuwa mbele ya kamera akirekodi filamu, angekuwa amefanikiwa kuvaa uhusika katika kiwango cha mwisho kabisa. Laura aliweza kuonesha kilichotakiwa kufanyika. Lakini haikuwa hivyo... ilikuwa halisi.

    Laura alikuwa analilia mapenzi!

    “Chris nina kosa gani mimi? Wewe ndiye umekuja kwenye maisha yangu, ukasema unanipenda, nakiri kweli mwanzoni sikuwa na hisia hizo, lakini sasa nimegundua upendo wangu kwako, ndiyo maana nimetoroka chuoni na kuja huku kwa ajili yako.

    “Nakupenda Chris. Nakupenda sana baba. Usinifikirie vibaya baba. Ni mapenzi tu. Nakupenda mpenzi wangu. Naomba unipe nafasi, nipe pumziko la moyo ndani yako...” maneno haya yalisikika huku machozi yakiendelea kutiririka machoni mwake.

    “Acha uongo wewe... unajifanya mwanafunzi, wewe ni mwanafunzi au mke wa mtu? Nimesema sitaki mawasiliano yoyote na wewe.”

    Laura akazidi kulia.

    Chika, Katibu Mkuu wa Bongo Film Club, aliingilia kati. Alimshika mkono Laura, akamsihi anyamaze, akatulia kidogo. Chika akaanza kuzungumza: “Maneno ya huyu binti si ya kupuuzwa, anahitaji kusikilizwa. Tafadhali Chris, Ramsey na Jaybee naomba tuzungumze pembeni. Naamini tutapata ufumbuzi.”

    “Sitaki!” Dk. Chris akajibu kwa hasira.

    “Utataka!” Jaybee, mwenyekiti wa nidhamu wa klabu hiyo alisema.

    Dk. Chris akanywea!

    Isingekuwa rahisi hata kidogo kumpinga Jaybee, msanii mwenye jina kubwa na sauti Bongo Film Club. Heshima yake ndiyo hasa iliyosababisha akabidhiwe kofia ya kusimamia nidhamu klabuni hapo. Ramsey alijua alichotakiwa kufanya.

    Alitoka na kusogea pembeni, Chika akafuta, Jaybee ndiye aliyekuwa wa kwanza akitangulizana na Laura. Dk. Chris akawa wa mwisho. Walitembea mpaka pembeni kidogo na kaunta iliyokuwa ndani. Wakaketi jirani na runinga.

    “Wakati mwingine huwa inanilazimu kutumia ukali kidogo ili mambo yaende sawa. Sikuwa na lengo la kukudhalilisha ila nilipenda haya mambo yajadiliwe kwa staha na siri. Chris lazima tuzungumzie huku pembeni,” alisema Jaybee, safari hii kwa sauti tulivu.

    “Nimekuelewa...” akasema Chris.

    “Huyu msichana unamfahamu?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ndiyo... lakini hafai huyu. Unajua...” akaanza kuzungumza kwa hasira lakini Jaybee akamkatiza.

    “Tulia, swali nililokuuliza ni moja tu; unamfahamu?”

    “Ndiyo.”

    “Utapenda haya mambo tuzungumze pamoja au mtayajadili wenyewe?” akauliza tena Jaybee.

    Dk. Chris alitulia kwa muda, alionekana akitafakari jambo kwa kina kidogo. Kichwa chake kilifanya kazi kama umeme. Pamoja na yote hayo, bado hakutaka mazungumzo yale yasikike na kila mtu. Haraka akajibu:

    “Nataka tuzungumze mimi na yeye tu!”

    “Si unaona mambo hayo?” Chika akasema na wote kwa pamoja wakasimama na kuwaacha Dk. Chris na Laura peke yao.

    ***

    “Nataka uniambie ukweli, umeolewa au hujaolewa?”

    Chris akamwuliza Laura.

    “Mbona maajabu tena mpenzi wangu? Niolewe na nani sasa?”

    “Jibu swali, wewe ni mke wa mtu au sivyo?”

    “Sivyo. Sijaolewa mimi.”

    “Ndiyo maana nakuambia unataka kunichezea mchezo... mbona mimi nilikuja kutafutwa na maaskari wakisema nimetembea na mke wa mtu... tena mke wa mkuu wa kituo?”



    LAURA alihisi kizunguzungu kikali. Yeye awe mke wa mtu? Tangu lini ameolewa? Alihisi kichwa chake kikigonga kwa kasi sana. Ukweli alioujua yeye ni kwamba hakuwahi kuolewa achilia mbali mchumba wa uhakika.

    Hakuposwa!



    Hakuwa na pete ya uchumba. Hata mwanaume wa uhakika pia hakuwa naye. Ni kweli hakuwa ameolewa. Ilikuwa ni yeye na masomo na starehe tu. Mara chache kuna wakati alikuwa akitoka na wanaume tofauti kwa ajili ya liwazo la moyo wake. Hivyo tu!

    Laura alishtuka si mchezo!!!



    “Aaaaah! Sasa naanza kupata picha. Hata mimi pia nilifuatwa nikaambiwa kwamba, wewe ni mume wa mtu na mkeo yupo palepale Singida. Nilikwenda hadi kituoni kutafuta ukweli, lakini cha kushangaza, wakasema hakuna kitu kama hicho na wala hakuna maaskari waliotumwa kunitafuta mimi kwa madai ya kutembea na mume wa mtu!” akasema Laura kwa sauti tulivu akionekana dhahiri kuwa na uhakika na alichokuwa akikizungumza...



    Chris alibaki mdomo wazi. Hata hivyo, bado hakumwamini Laura hata kidogo.

    “Nitaaminije?” akauliza Chris akimkazia macho Laura.

    “Subiri,” Laura akasema kwa sauti ya chini.



    Alichokifanya ilikuwa ni kufungua pochi yake, kisha akatoa kitambulisho chake cha chuo na kumkabidhi. Baada ya hapo alitoa kitambulisho cha kupigia kura nacho akamkabidhi. Chris akaonekana akivitazama vile vitambulisho kwa makini sana.

    “Kwahiyo sasa hii inathibitisha nini?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwamba mimi ni mwanafunzi wa chuo.”

    “Kwani mwanachuo hawezi kuolewa?”

    “Anaweza, lakini uliambiwa mimi siyo mwanachuo ni mke wa mtu tu.”

    Chris akatulia kwa muda.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog