Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

USALITI WA KIAPO - 3

 







    Simulizi : Usaliti Wa Kiapo

    Sehemu Ya Tatu (3)





    “Tayari kuna mtu aliyeujaza moyo wangu, hivyo sizani kama nitaweza kumkubali mwingine yeyote”

    “Sawa siwezi kuulazimisha moyo wako uniangukie ila ipo siku utagundua ni kiasi gani nakupenda na kwa ushauri tu, kaa mbali na Tony, ni mchezeaji tuu yule,” alisema Jose.

    “Nimekuelewa,” Martha akajibu.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Naomba tuwe hata Marafiki wa karibu”

    “Tulishakuwa hivyo toka siku nyingi”

    Maongezi yakaendelea baina ya wawili hao, kila mmoja alizungumzia jinsi kazi ilivyokua na kiasi kikubwa walifurahia,

    “Hivi siku ya leo tutaimalizia hapa?” Jose akauliza.

    “Yeah! Mimi sioni pa kwenda!” Martha akajibu.

    “Twende tukatembee Raskazone”

    “Aah! Sasa mazingira ya kule si yanafanana na ya huku”

    “kule kuna fukwe nyingi na pamechangamka Zaidi, twende huko naamini kila mmoja ukimwambia atafurahi”

    Ikabidi wawataarifu wenzao, wote kwa pamoja wakakubaliana na ilo wazo na kwa haraka wakaanza safari ya kuelekea Raskazone.



    ***********************************



    Tony hakutamani kuuona uso wa Martha hasa baada ya kilichotokea usiku uliopita, akaamua atoke na kwenda Raskazone, huko akakodi chumba kwenye Lodge moja iliyo karibu kabisa na ufukwe. Kwa kuwa hakuwa na kazi ikabidi asogee hadi sehemu ya ufukwe, alishuhudia watu wa kila namna, aliduwazwa na uzuri wa wasichana waliyekuepo eneo hilo,



    “Mwanamke siku zote yupo kwa ajili ya kumburudisha mwanaume, sio dhambi kama nitamtafuta wa kupumzika naye kwa siku ya leo, nitampata bila shaka,” alisema Tony huku akipiga hatua fupi fupi kuzunguka eneo la ufukweni.



    Wakati anaendelea kuzunguka eneo hilo akazidi kuona vitu vilivyomvutia macho yake, watu walikuwa wakicheza na wengine kuogelea. Kilichomvutia Zaidi ni kuona wapenzi wakiwa wanakimbizana na kumwagiana maji,

    “Daaah! Mapenzi kama uchizi yaani, kuna wakati unaweza kufanya jambo ambalo ukikaa na kufikili lazima ucheke,” alisema Tony huku akiendelea kuduwaa.



     Akaendelea kuwatazama wapenzi wale huku akitembea, kufumba na kufumbua akajikuta akipigana kikumbo na mwanadada ambaye Tony alijikuta akitumia dakika moja nzima kumtazama, hakuwa mwingine ila ni Leilah mwanamke aliyetokea kuunyanyasa moyo wa Tony, jamaa hakuamini aliona ni kama ndoto, Leilah mwenyewe akabaki anashangaa kumuona Tony eneo lile,

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Leilah!”

    “Tony!”

    “Nafikiri Mungu anampango mzuri kati yetu hadi akaamua kutukutanisha katika hali kama hii na kwa mara nyingine tena,” alisema Tony.

    “Mhmhmh! Acha kumshirikisha Mungu katika mambo yasiyofaa,” alijibu Leilah.

    “Hahahah! Inaonekana ni muumini mzuri katika maswala ya Imani, hata hivyo siitaji kufahamu Zaidi, je naweza kupata muda wako hili tuzungumze japo kwa ufupi”

    “Hakuna la kuzungumza kati yetu Tony, nadhani kila kitu kilikuwa wazi siku ile na sihitaji kurudia makosa”

    “Unaonaje tukiongea sehemu ya wazi ambayo kila mtu atatuona”

    “Ili iweje?”

    “Nahitaji kukuondoa wasiwasi, nakuhaidi sitokugusa ila nipe muda kidogo tu nizungumze nawe”

    Leilah akafikiri kidogo kisha akakubali ombi la Tony, wakaelekea sehemu iliyo na watu wengi lakini Leilah hakuipenda sehemu hiyo,

    “Nadhani eneo lililo na watu wachache ni salama Zaidi kwangu,” alisema Leilah.

    “Na iwe kama ulivyosema”

    Tony akaongozana na Mrembo huyo ambaye muda wote tabasamu zito lilijaa kwenye sura yake,

    “Mwanaume aliye kuoa wewe ni mwenye bahati sana,” alisema Tony.

    “Kwanini?”

    “Rangi yako angavu sioni haja ya taa nyakati za usiku, sura yako ya kupendeza sina haja ya kuangalia tv. una mwendo wa madaha Zaidi ya wanaogombania urembo wa nchi hata dunia, mbaya Zaidi uhusiano wangu na wako ni kama wa kiumbe na jua, kadri nitamanivyo kukusogelea ndivyo ninavyozidi kuungua,” alisema Tony baada ya kufika sehemu nzuri na kukaa na mrembo huyo.

    “Naomba hifadhi Leilah japo kibarazani maana najua chumbani tayari kuna mtu kakaa”



    Tony aliendelea kutoa maneno makali ambayo kiukweli yalizidi kumchanganya Leilah akawa akishindana na nafsi yake, upande unamwambia amkubali upande unamwambia akatae.

    “Nalitamani busu lako Zaidi na Zaidi, hakika nashindwa kukutoa kwenye ufahamu wangu. Nakuona kila sehemu niendayo, wakati wakula, wakufanya kazi na hata wakati wa kulala taswila yako hunijia”.

    “Tony usinifanyie hivi nashindwa kuvumilia,” alisema Leilah.

    Kauli ile ikawa kama ushindi kwa Tony, akazidisha ukaribu kwa binti yule na akasahau kabisa kwamba anacheza na mali ya watu, safari hii aliamua kutumia viganja vyake kumtomasa Leilah hapa na pale. Maskini leilah hakuweza kuimili ushawishi wa mwanaume huyo, akajikuta kwa mara ya pili akimsaliti mumewe kwa kuunganisha ulimi wake na wa Tony.



    Upepo wa bahari ukawa mkali Zaidi, mawimbi yakaongezeka ukubwa na kuwafanya watu waliokuwa wakiogelea kutoka sehemu hiyo. Tony baada ya kuhakikisha kuwa amecheza na akili ya Leilah vya kutosha akaamua abadili uwanja wa mapambano, safari ya kueleka chumbani ikaanza huku Leilah akiwa kama kuku wa kizungu asiyeweza kujinasua kwa mwanaume yule. Tony kila alipomuangalia Leilah ndipo alitamani afike kwa haraka chumbani hili aweze kutimiza haja ya moyo wake. Leilah hakuweza sema lolote kwa hakika alipagawishwa mno na Tony, wakafika chumbani bila kupoteza muda wakakumbatia kwa pupa na kuanza kupeana mabusu mazito. Tony taratibu akawa anapunguza nguo za mrembo yule, hapo Leilah akashtuka kidogo na kurudi nyuma,



    “No Tony! We can’t do this, (hapana Tony! Hatuwezi fanya hivi),” alisema Leilah.

    “Ooh! Come on Leilah! Am so excited to have you, (acha hizo Leilah! Nina hamu sana ya kuwa nawe)”

    “This is wrong! Please try to understand, (hii si sawa, jaribu kuelewa tafadhali)”

    Tony hakutaka kuongea Zaidi ya kumsogelea Leilah na kumgusa sehemu ambazo kwa kiasi kikubwa ziliamsha upya hisia za Leilah,

    “Am somebody wife Tony! You will be in danger if my husband found out, (Mimi ni mke wa mtu Tony, utakuwa matatani mume wangu akigundua)”



    Tony alizidisha kumkoleza mrembo huyo, akajikuta anashindwa kutoa sentensi zilizokamilika, na ikawa nafasi ya Tony kuamishia mashambulizi yake kitandani. Leilah hakuwa na kipingamizi chochote kwa Tony alionesha ushirikiano wote.



    Baada ya shughuli iyo nzito kila mmoja akapitiwa na usingizi, huku nje Martha pamoja na wengine wakawa katika mazingira hayo wakiendelea kushangaa na kuburudika kila mmoja na namna yake.

    ***************************

     Zay ambaye ni rafiki wa Leilah akaangaika kumtafuta rafiki yake asijue wapi alipoelekea, kila alipopiga simu ilikuwa ikiita bila kupokelewa mbaya Zaidi mume wa Leilah naye akaamua aje eneo hilo baada ya kuona simu ya mkewe haipokelewi. Zay aliogopa mno hakuelewa rafiki yake yupo katika mazingira yapi na alimuogopa Zaidi mume wa Leilah sababu si mtu mwenye utani wala masihara linapokuja swala la mkewe. Alimpenda sana mkewe na akamgharamia kila kitu na kwa kuwa haikuwa kawaida kwa Leilah kutopokea simu akaamua afike eneo hilo la Raskazone ajaribu kumtafuta.



    “Samahani kaka yangu, kuna mdada namtafuta, ni mrefu kiasi, mweupe pia anashepu flani hivi,” alisema Zay.

    “Mhmhmh! Ni yule mdada aliyevaa jinsi la blue hivi na blauzi flani panapana,” alijibu huyo mkaka ambaye ni muhudumu eneo hilo.

    “Yeah! Ndiye yeye nambie alipo”

    “Asee! Dada yangu mimi nilimuona akiwa na jamaa flani hivi sijui ndiye mumewe, walikaa muda mrefu hapo na baadae nikawaona wanaelekea ndani”





    “Ndani!” Zay alishtuka sana.

    “Ndio dada yangu”

    “Unaweza kujua chumba walichopo”

    “Aah! Ilo lipo nje ya uwezo wangu maana ni mambo binafsi ya mteja”

    “Tafadhali kaka yangu naomba unisaidie huyo mwanaume aliyekuwa naye si mumewe na mumewe hivi tunavyoongea anakaribia hapa. Tukizubaa inaweza kuwa hatari kubwa mno,” aliongea Zay.



    *******************



    Baada ya saa kadhaa kupita Leilah akaamka, akajikuta akilia kwa kile kilichotokea, hakuamini kama siku hiyo aliweza kumvulia nguo mwanaume mwingine tofauti na mumewe. Wakati akiendelea kulia Tony naye akaamka na kumsogelea mrembo yule,

    “Umenipa raha ambaye naweza kusema sijawahi ipata toka nilivyoanza kuingia ulimwengu wa mapenzi”

    “Tony do you real love me? (Je unanipenda kweli Tony?)”

    “Why? (Kwanini?)”

    “I need to know, (naitaji kujua)”

    “Mhmhmh! Vipi kama nitakwambia nilikutamani tuu na kwa kuwa shida yangu imeisha unaweza kwenda,” alijibu Tony.

    “What…!? You can’t be serious!”CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Am seriously! Sina hata chembe ya utani juu ya hili akshante kwa penzi ulilonipa na uondoke zako”



    Leilah akajikuta anaishiwa nguvu, akajiona Kama yupo ndotoni kile ambacho anakisikia, aliamini kuwa kadri ya muda unavyoenda ataamka na kusahau. Alishtushwa na mlio simu yake kuja kuiangalia akachanganyikiwa Zaidi baada ya kukuta missed call 17 za mumewe na 33 na rafiki yake kipenzi Zay, mapigo ya moyo yakaenda mbio Zaidi hasa baada ya kuiona meseji ya zay,

    “Shoga umeniweka katika majanga, hapa nipo na mumeo tunakusaka, nimeambiwa na muhudumu kuwa upo chumbani na mwanaume mwingine kwa hiyo utajua mwenyewe namna ya kufanya”

    Baada ya kusoma ule ujumbe akamgeukia Tony na kumwambia,

    “Nakupenda sana Tony tena kuliko nilivyokuwa nampenda mume wangu japo nimekufahamu kwa kipindi cha muda mfupi, aidha nashukuru kwa kuaribu maisha yangu, mume wangu amejua kuwa nipo hapa na yupo nje ananisaka bila shaka atakuwa na watu wengine. Sina la kulipia ovu hili Zaidi ya kifo, Mume wangu ananipenda sana na wala sijakosa chochote toka kwake, ila umefanikiwa kuuteka moyo huu japo sikufikilia kama mwisho wake utakuwa hivi. Acha hii tabia Tony usitumie uzuri wako kuwachezea watu wasio na hatia, ondoka eneo hili utakuwa salama”



    Maneno hayo yalimchoma sana, akajikuta akijutia sana kosa alilofanya. Kwa mara ya kwanza huruma ikamjia akawaza ni kwa namna gani atamsaidia msichana yule, machozi yakamtiririka mfadhaiko mkubwa ukamshika,

    “Nifanye nini Leilah kukusaidia!”

    “Niambie unanipenda walau mara moja tuu”

    “Sasa hiyo ndiyo itasaidia nini?”

    “Nitakufa nikiwa nakumbukumbu nzuri”



    Kabla hawajaongea Zaidi mlango wa chumba walichomo ukagongwa, Tony akaogopa mno, jamani mke wa mtu ni kama asidi ambayo ukiichezea inakuunguza na kukutokomeza bila kubakisha hata kipande cha nguo yako. Tony alijenga ujasiri na kuufungua mlango akaduwaa Zaidi alipokutana Martha,

    “Martha..! Wafata nini hapa?” Tony aliuliza kwa mshangao.

    “Hakuna muda wa maswali chukua kilicho chako na tuondoke,” alisema Martha.

    “Hapana siwezi kuondoka wewe nenda tuu,” alisema Tony.

    “Acha ubishi unadakika 5 tuu za kuwa hapa,” ilikuwa sauti ya msichana mwingine ambayo haikuwa ngeni sana masikioni mwa Tony alipomtazama vizuri akagundua kuwa ni rafiki yake na Leilah.

    “Nilikwambia kila kitu siku ile Tony, kweli mtu hawezi acha asili yake umeharibu maisha ya Leilah”

    Zay hakutaka kusubili jibu lolote toka kwa Tony akaingia ndani na kumtaka Leilah avae nguo zake haraka kisha wakatoka kupitia mlango wa uani,

    “Siwezi kumkimbia mume wangu Zay, nipo radhi kupokea adhabu inayonistahili”

    Wakati akiongea hayo mume wa Leilah akafika akiwa amefura kwa hasira sana, hakutaka kuuliza akampiga vibao mfululizo Leilah hadi Zay akaogopa na kuhisi uenda mwanaume huyo atamua mkewe.

    “Huu ndio upuuzi unaoufanya siku zote unapoaga kuwa unatoka?” aliongea mwanume huyo kwa hasira sana.

    “Zay nilikuwa nakuheshimu kama mdogo wangu na kama shemeji yangu ila siamini kama nawe umeweza kushirikiana na mwanamke huyu kusaliti kiapo ambacho tulikiweka mbele ya sheikh, wazazi ndugu na jamaa”

    “Ukweli nimekukosea sana mume wangu, naomba unisamehe japo najua sistahili tena kuitwa mkeo,” alisema Leilah huku akilia kwa kwikwi.

    “Na huyu mpuuzi uliyekuwa naye yuko wapi?”



    Mume wake Leilah aliuliza kwa ghazabu Zaidi kutaka kujua alipo Tony mwanaume aliyesababisha usaliti kwa mkewe. Wakati hali ikiwa hivyo upande wa pili ilikuwa aibu nzito kwa Tony kwani wafanyakazi waliomueshimu kama bosi wao leo wameshuhudia ujinga alioufanya, aliumia Zaidi alipomtazama Martha ambaye mbali na usiku uliopita kulala naye alihimili aibu ile ya kumfumania Tony na kumuokoa kwenye balaa ambalo angeweza kulipata kama wasingekuepo.

    “Sikilizeni! Ratiba imebadilika tunaondoka usiku huu hatuwezi kusubili hadi kesho,” alisema Marthaa.

    Jose alimchukia Zaidi Tony hadi kufika hatua ya kuomba bora angepigwa hadi afe kwenye fumanizi lile, Martha alijitahidi kuwa karibu na Tony na kumsihii atulize akili yake,

    “Martha kwanini unanifanyia haya mimi kwa sasa sidhani kama nastahili,” alisema Tony.

    “Mpumbavu wewe! Usifikiri kama nimefurahishwa na nimeridhishwa na uchafu ulioufanya, ila wewe una kazi ya mamilion kama ikipotea ni wazi kampuni zetu zitafirisika ndio maana nilikwambia nahitaji uwe hai,” alisema Martha.



    *******************



    Ilikuwa majira ya saa 2 usiku Leilah na mumewe wakiwa nyumbani. Mume wa Leilah alijaribu kumdodosa maswali kadhaa mkewe lakini hakuna hata moja alilojibu Zaidi ya kulia na kuomba msamaha huku akisisitiza kuwa yupo tayari kupokea adhabu yeyote ile.

    “Nakupenda sana mke wangu siwezi kufanya jambo lolote la kukudhuru ila huyo mwanaume uliyekuwa naye hatoweza kutoka nje ya Tanga hii akiwa salama”

    Kauli hiyo ilimtisha Zaidi Leilah akatamani amtetee Tony lakini kufanya hivyo kungesababisha mambo kuwa magumu Zaidi upande wake.

    “Kitakachomkuta hatokaa akisahau katika maisha yake,” alizidi kuongea mume wa Leilah.

    “Mimi ni mzigua hawezi kucheza na mke wangu nikabaki namtazama japo simfahamu ila ipo siku kama si yeye au ndugu zake watanitafuta kuniomba radhi”



    ************************CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Safari ya kurejea Dar ikaanza usiku huo huku kila mmoja akiwa na hofu nyingi juu ya safari hiyo, kila mtu alianza kuomba kwa Mungu wake waweze kusafiri bila shida yeyote. Dereva alikuwa makini sana hakutaka kwenda mwendo wa kasi ila alichojali ni usalama wa watu aliowapakia. Mungu akawasaidia wakapita Tanga na viunga vyake salama ila mauzauza yakaanza pale tuu walipolikaribia daraja la Mto wami. Wakaona kundi kubwa la viumbe vya ajabu vyenye umbo mithili ya nusu binadamu nusu sokwe likiwa juu ya maji ya mto wami. Chakushangaza Zaidi ni pale walipoona moto ukiwa umekolezwa juu ya maji na ukiwaka bila shida yeyote.



    “Mungu wangu nini kile!” alisema Martha kwa hofu kuu.

    “Mungu tusaidie tuvuke salama eneo hili” Jose akasema.





    Wakati huo wote Tony alijua kuwa yeye ndiye mtu anayewindwa kutokana na uovu alioufanya, roho ilimuuma Zaidi hasa baada ya kuona hatari ambayo ingeweza kusababisha wengine kupata madhara,

    “Hapa itabidi nitembee mwendo wa taratibu sana, msiangalie nje tutapita salama,” alisema dereva.

    Mungu mkubwa wakavuka daraja lile bila shida yeyote, safari ikaendelea lakini kabla hawajafika mbali Zaidi gari ikazima ghafla, ikabidi Tony, dereva na wanaume wengine washuke ndani ya gari kuangalia tatizo ni nini. Mazingira waliyokuepo yalikuwa yakuogofya sana kwani hakukuwa na dalili za makazi ya watu jirani na hapo, ulikuwa ni msitu huku sauti za ndege na wanyama mbalimbali zikisikika.



    Baada ya kuangalia vizuri gari hawakuona tatizo lolote, dereva ikabidi aingie ndani na kujaribu kuliwasha likawa linawaka na kuzima ila baadae likakubali. Wote wakaanza kuingia ndani ili kuendelea na safari, huku nyuma Tony akaanza kusikia kitu kama kinatembea kwenye kichaka, ikabidi ageuke kutazama hakuweza kuona chochote. Akasogea ulipo mlango wa gari na kuanza kupiga hatua kuingia ndani na kabla hajamalizia mguu mwingine akatokea nyoka mmoja mweusi na mrefu sana akamgonga, Tony alitoa yowe la mshtuko lilochanganyika na maumivu, ikabidi Bosco na Jose watazame kilichomkuta Tony. Wote walijaa na uoga hasa baada ya kumshuhudia nyoka mkubwa vile na mwenye kung’aa akiwa karibu na Tony, nyoka yule alivyoona watu wanashuka akaingia kwenye vichaka na kutokomea. Wakasaidia kumuingiza Tony kwenye gari na kumfanyia huduma ya kwanza huku dereva akiongeza mwendo walau kufikia eneo lenye huduma za afya.



    Hali ya Tony ilibadirika ndani ya muda mfupi, wote walishuhudia mguu wa Tony ukianza kubadirika rangi na kuwa mweusi kama mkaa. Tony hakutaka kulalamika kwa Mungu sababu alijua kuwa ni wazi yanayomkuta sasa ni malipo ya dhambi zake,

    “Msihuzunike juu yangu, kuweni na Amani tuu haya yamenistahili,” alisema Tony.



    Martha alishindwa kujizuia akajikuta akidondosha chozi, hali ilikuwa tofauti kidogo kwa wengine kwani waliona hata adhabu hiyo ni ndogo. Dereva alitembea kwa kasi sana bila kupata shida yeyote na wote waliamini kwa kuwa walishampata mtu wao hivyo kusingekuwa na madhara mengine kwenye safari hiyo. Saa mbili baadaye wakawa wamefika wilayani Bagamoyo ikiwa ni karibu kabisa na nyumbani kwa Tony. Martha ikabidi awapigie Yassir na Darmy ambao ni marafiki wa karibu sana wa Tony. Wakafika na kumkimbiza Tony hospitali,

    “Amekutwa na nini?” Yassir aliuliza baada ya safari ya Hospitali kuanza.

    “Ameumwa na nyoka usiku huu”

    “Inaonekana nyoka huyu ana sumu kali sana, ila mmefanya vizuri kumfanyia huduma hii ya kwanza,” alisema Darmy.



    *******************



    Ni katika maeneo ya Sahare mkoani Tanga ambapo Leilah na mumewe wanaishi, Asubuhi hiyo mume wa Leilah alionekana kuwa na furaha sana,

    “Mke wangu kazi iliyokuwa ikiniumiza kichwa nimeimaliza na hapa nasubili siku 9 ili nimalize kila kitu,” alisema mumewe Leilah.

    “Kazi gani tena mume wangu?” akauliza Leilah.

    “Yule mpuuzi aliyesababisha usaliti wa agano letu, maisha yake yapo matatani kwa sasa na hata akinusurika kwa hili basi atakuwa mtu wa kitandani na hatoweza kunyanyuka hadi umauti”.

    Kauli ile ilimtisha sana Leilah, akajikuta akiangusha chozi kwa kumuhurumia Tony,

    “Mume wangu haya utayafanya mpaka lini? Kila siku ukiendelea kukumbushia ilo jambo mimi nakosa Amani na najiona mkosaji nisiyefaa kusimama mbele yako”.

    “Ingawa nimekusamehe lakini yule mpuuzi atalipa kwa aliyoyafanya na ndio ameanza sasa, zikifika siku 9, nitafikiria kama kummaliza kabisa au kumuacha hivyo hivyo,’ alisema mume wa Leilah.



    **************************



    Baada ya vipimo kufanyika, Daktari akatoa majibu ambayo yanashtua na kuhuzunisha nyoyo za wengi huku kwa baadhi ikiwa ni furaha na sherehe yenye kufana,

    “Nasikitika kuwaambia kuwa sumu imemuathiri sana Tony na hatuna namna ya kufanya zaidi ya kuukata mguu huu ili kuzuia sehemu nyingine ya mwili kudhurika aidha upande wake mmoja umepooza hatoweza kuinuka wala kufanya lolote kila kitu atakifanya akiwa kitandani,” alisema daktari.

    Taarifa ile ilikuwa ni Zaidi ya msiba kwa Yassir na Darmy, hawakujua maisha yatakuaje bila rafiki yao huyo ambaye walishirikiana naye katika mambo mengi,

    “Msijali jamaa zangu hii ni mitihani ya dunia,” alisema Tony.

    Walishindwa kumwambia chochote maana mara nyingi walijitahidi kumshauri atulie hakuwaelewa, taarifa ya fumanizi liliwaumiza mno.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Naomba mnipeleke kwangu sitaki kuwa mzigo kwenu ila kikubwa naomba muiangalie sana kampuni naiacha mikononi mwenu maana lolote laweza kutokea”



    ***********



    Wakamchukua Tony na kurudi nae nyumbani, siku zikaenda na hakuna yeyote aliyejitokeza kuja kumtazama wengi waliamini kuwa Tony ni muovu na amestahili adhabu ile. Shughuli za kampuni ya Studio 7 Media Ltd. Zikaendelea kama kawaida japo hakuwa na uwezo wa kushika chochote aliwapa maelekezo rafiki zake ambao waliacha shughuli zao na kuamua kujikita katika kampuni ya swahiba wao kipenzi.



    “Project iliyofanyika Tanga lazima tuihariri na iwe nzuri mimi sina uwezo wa kushika chochote lakini akili yangu bado inafanya kazi hivyo nendeni ofisini kachukueni data na sauti ambazo zimesharekodiwa”

    Yassir ikabidi aende ofisini na kuonana na Martha ambaye hata hivyo alikataa kata kata kutoa data zikafanyiwe kazi,

    “Tony hawezi kwa sasa acheni kazi tutaifanya hapa,” alisema Martha.

    “Mie nafata maelekezo ya Tony tuu, hii kazi ni ya mamilioni ya pesa, hata kama mwili wake haufanyi kazi lakini bado akili yake ni nzima, naomba tafadhali,” alilisisitiza Yassir.

    “Nenda bhana! Wewe umeona wapi maiti ikafanya kazi,” Jose akaingilia kati maongezi yale.

    Yassir alijisikia vibaya sana kwa kauli aliyoitoa Jose akabaki anamtazama Martha asikie atamwambiaje lakini hakuambiwa lolote,

    “Martha kumbuka wewe ndiye sababu ya haya yote, Tony hadi kuwa vile wewe ndiyo chanzo ila tumekuvumilia tuu na hata yeye hakutaka lolote lifanyike juu yako, leo hii bado anaendelea kupokea adhabu kutokana na kosa ulilolifanya wewe,” Yassir aliongea kwa hasira mno.



    Jambo lile likazua maswali mengi kichwani mwa Jose ambaye ni wazi hakuwa anaelewa vitu vingi kuhusu wawili hao,

    “Sitaki kusikia lolote juu ya Tony, na sina kosa la kujutia juu yake, mwambie mkataba hautovunjwa japo hatofaidika na chochote kutokana na yeye kuharibu kazi,” aliongea Martha.

    “Sawa zimemfikia,” alijibu Yassir na kuondoka eneo hilo.



    **************



    Taarifa za kuugua kwa Tony zilifika masikioni mwa wengi sana, kila mmoja akajaribu kuchimba ila kujua kiini cha tatizo. Wengi walitofautiana na majibu wapo waliosema amelogwa na wapo walioamini ni ajali tuu ambaye inaweza kumtokea yeyote. Habari ya ugonjwa wa Tony ikatua masikioni mwa mjomba wake kipenzi na kumtaka apelekwe nyumbani kwake haraka iwezekanavyo.

    Baada ya mipango kukamilika Tony akapelekwa kwa mjomba yake ambaye anaishi Mkoani Mbeya wilaya ya Tukuyu, Mjomba wake huyo alioa mke wa kinyakyusa hivyo akabahatika kumiliki mashamba kadhaa ya mpunga pamoja na mifugo kama ng’ombe, mbuzi, kuku na nguruwe. Mbali na kuwa na mali hizo hakutamani kabisa kuishi katika jiji la Dar es Salaam. Tony alifikishwa Tukuyu akiwa bado na hali mbaya sana, mguu ulizidi kuwa mweusi na kufanya hata sehemu nyingine za mwili kuanza kuwa nyeusi,

    “Huyu si nyoka wa kawaida,” alisema Mjomba.





    “Wengi walisema hivyo, na tumejaribu kuhangaika katika mahospitali na kauli yao ya mwisho ni kwamba Tony akatwe mguu jambo ambalo yeye mwenyewe hakuridhia,” alisema Darmy.

    “Sawa! Kwanza niwashukuru sana kwa moyo wenu wa upendo hadi hapa mlipofikia naomba niwasaidie kumuuguza huyu mpwa wangu hili ninyi shughuli zenu zisilale, tutajitahidi kadri Mungu atakavyotujalia naamini kwa uweza wake atapona,” alisema Mjomba.



    **************



    Ndani ya kipindi hiko kifupi habari zikasambaa mtandaoni juu ya kuugua kwa Tony, mume wake Leilah akawa mmoja kati ya watu aliyeona habari ile, kwa haraka Zaidi akamuita mkewe na kumuonesha kuwa yule ndiye au la. Maskini Leilah alishindwa kuvumilia akajikuta akitoa machozi mbele ya mumewe.

    “Mume wangu basi yatosha muache kijana wa watu, mimi sitorudia kosa naamini hata yeye hatorudia kosa hilo”

    “Hahahahaha! Mimi nimemalizana naye kuna dawa ilikuwa nimmalize na mbele yako leo naichoma moto, ataishi hivyo alivyo sababu hakuna dawa ya kumtibu Zaidi ya kumuangamiza,” alisema mume wa Leilah kwa dharau mno.



    BAADA YA MIEZI 4



    Afya ya Tony iliziidi kudhoofika kwa kiasi kikubwa, matumaini ya kuishi yakadidimia mno, mjomba wake hakukata tamaa Zaidi ya kuangaika na dawa za mitishamba, aliwafata wazee wa kila aina na kila mmoja akawa na maoni tofauti. Swala la kupiga lamli likawa likiongelewa na wengi ila mjomba huyo hakuwa kabisa na Imani hizo, alimuamini Mungu wake na kama amepanga mpwa wake aendelee kuishi basi hakuna litakalopangua.



    ***********************



    Kutokana na Tony kushindwa masharti ya mkataba waliowekeana kati ya kampuni yake na kampuni ya Tae Xhiang Sung Group ambayo inaongozwa na Martha kama balozi akiwakilisha Makao makuu ambayo yapo nchini Korea ya Kusini. Maamuzi yakafikiwa kuwa mkataba lazima uvunjwe na Tony anapaswa kulipa hasara yote ambayo imejitokeza,



    “Hapana hii sio haki! Tony hawezi kuwapa chochote ninyi, hapa tunapoongea anapigania uhai wake, msimfanyie hivyo tafadhali,” aliongea Yassir kutetea hoja.

    “Ni kweli Tony lazima alipe hasara iliyopatikana, hana pesa lakini ana nyumba nzuri ambayo ikiuzwa tunaweza kufidia hasara hii,” aliongea Bosco.

    “Tatizo bosi unaingiza maswala binafsi katika kazi, mtu Malaya kama yule, wewe bado unataka kumtetea hili iweje!” Jose akasema kwa ghadhabu.

    Darmy na Yassir wakajikuta wakisimama kwa hamaki, wote walishindwa kusema neno. Martha akasimama na kuwataka wakae chini na kisha akasema,

    “Hasara yote hii nitailipa mimi, na mkataba kati ya Studio 7 Media LTD. Na Tae Xhiang Sung Group utaendelea kama kawaida”.



    Watu wote walishangaa sana, wengi wakapinga swala lile. Hata hivyo Martha akabaki na msimamo huo huo,

    “Sijaona kampuni ya ajabu kama hii, mimi nakuwa wakwanza kuacha kazi,” alisema Jose.

    “Mimi pia naacha,” Bosco akadakia.

    Martha akawatazama wengine hili kujua kuwa nao msimamo wao uko vipi. Nusu ya wafanyakazi wakaungana kuachana na kampuni hiyo kama mkataba utabaki vilevile.

    “Hatufanyi kwa ajili ya pesa tuu, ila tuna mapenzi ya kile tunachofanya, hatuwezi kuvumilia upuuzi wa mtu mmoja ukiharibu kazi”.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Kabla ya Martha kujibu akataokea mzee mmoja wa makamo ambaye yeye alipewa nafasi ya kufanya kazi kama mshauri katika kampuni hiyo, akasogea hadi mbele na kuwaomba wote wakae na kumsikiliza kile ambacho anataka kuwaambia. Wote wakatii na mzee akaanza kuongea,

    “Mnajua nini kuhusu Tony ninyi! Bosi wenu yupo sahihi katika maamuzi haya, mnafikiri Tony alikuwa na tabia hii?”

    Watu wote wakakaa kimya, minong’ono ya hapa na pale ikaendelea ila kwa busara za mzee wote wakaona haya na kuamua kumsikiliza.

    “Badala ya kujadili ni namna gani tunaweza kumsaidia mwenzetu ninyi mnajadili namna ya kumdidimiza na kutaka kumyang’anya hata kile alichokuwa nacho”

    Mzee akavuta kiti na kukaa na kuwataka wamsikilize kwa makini kisha baada ya simulizi atakayowapa, wana uhuru wa kufanya lile watakaloona ni sawa. Mzee akaanza simulizi yake kama ifuatavyo..



    *********************



    Miaka 5 iliyopita Tony hakuwa na ndoto za kuwa director kitu pekee alichokipenda katika maisha yake muziki alijua kuimba hata kutunga pia, alikuwa ni mtu mwenye nidhamu na heshima kwa kila mwanadamu, hakujua kutumia kilevi wala hakujua starehe ya wanawake. Kutokana na kipaji kikubwa alichokuwa nacho wengi wakamshauri ashiriki mashindano ambayo hufanyika kila mwaka kumsaka mtu mwenye kipaji cha uimbaji. Alifata ushauri wa wengi na kuingia katika mashindano hayo.

    “Mabibi na mabwana ule wakati tuliokuwa tukiusubiria sasa umewadia, ivyo kwa heshima na tahadhima namkaribishaa…”

    Kabla ya mc hajamalizia tayari mashabiki wakawa wanataja jina la kijana ambaye ameteka hisia za wengi toka shindano lenye kusaka watanzania wenye vipaji mbali mbali kuanza “Tanzania Got Talent”.



    “Tony! Tony..! Tony..!”

    “Kijana huyu ni tishio kwa ushindi wangu,” akaongea mshiriki mwenza wa shindano ilo katika kipengele cha uimbaji.

    “Jinsi anavyoimba, sauti na mpangilio wake wa mashairi hakika hamna kitachomnyima ushindi”.



    Kila mmoja aliongea lake kumuhusu kijana huyo, tupia mbali kipaji chake, muonekano tuu ulizidi kuwavuruga wengi, kwa hakika Tony ni miongoni mwa vijana watanashati tena asiopitwa na wakati, mwenye kujiamini na ubunifu wa hali ya juu katika kila anachokifanya. Uwezo wake wa kuona mbali ndio ulimfanya aonekane mpya na wakipekee kila apandapo jukwaani.

    “Yalinikuta kama yako rafiki, aliuteka moyo wangu nikajiweka usoni pake kabla ya macho yangu. Akaukataili moyo huu na kuniacha kilema, kwani ukumbuki tulivyokutana na akanikiss, sasa kwanini aniache bila kuangalia nyuma, ila rafiki nimeamua kutompenda yeyote tena”.



    Yalikua baadhi ya maneno yaliyokuwa kwenye nyimbo ambayo Tony alikuwa akiimba, ukumbi mzima ulizizima kwa nderemo na vifijo baada ya kuona Tony ameingia katika 10 bora za shindano ilo.

    “Mhm! Hongera jamaa yangu leo umekamua kichizi” 

    “Hahaha! Kwani siku zote hujui shughuli yangu iko vipi?”

    “Ila jamaa ulivyoimba kama umetendwa kweli yale mahisia nini daah! Nikaona watu wanalia huku”

    “Duuh! Kumbe walilia eenh!”

    “Sana tuu yaani”

    “Basi kikubwa ngoja nijipange maana shindano limefika patamu” yalikua maongezi kati ya maswahiba wawili, Darmian akimpa pongezi zake Tony.

    Kisha kwa pamoja wakawa wanatoka ukumbini tayari kwa kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwao, wakafika nje na kusimama kidogo,

    “Hivi Yassir yukwapi si alikuja leo?” Tony akauliza

    “Daah! Bora ulivyonikumbusha tungemwacha”

    “Yupo wapi kwani” CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Twende hivi tukamcheki”

    “Sawa”.

    Tony akakubaliana na Darmy taratibu wakawa wanaelekea alipo lakini kabla hawajafika mbali, wakasikia mtu akiita

    “Tony! Darmy!”



    Walipogeuka wakakuta Yassir akiwa na msichana ambaye kwa hakika alikuwa mrembo Zaidi, mwanga hafifu wa mbalamwezi haukuweza kuuficha ung’aavu wa sura yake. Hakuwa na umbile kubwa la kutisha, umbo lake la wastani lilifanya Darmy na Tony kutumia dakika kadhaa kumtazama mrembo yule, hakuna aliyeweza kuuzuia moyo wake usiende mbio hasa msichana yule alivyotoa tabasamu. Vishimo vidogo vilivyojitokeza mashavuni mwake vilizidi kumpa sifa ya kuwa mwanamke ambaye kila mwanaume anaweza kuota kuwa naye.

    “Tony, Darmy huyu anaitwa Martha ni rafiki yangu,” Yassir akatoa utambulisho mfupi ambao vichwani mwa jamaa zake ukawa bado umeacha maswali mengi.







    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog