Search This Blog

Thursday, July 21, 2022

SINGIDANI - 3

 







    Simulizi : Singidani

    Sehemu Ya Tatu (3)





    “Na hiki kitambulisho cha kura?”

    “Angalia nimejiandikishia wapi? Nilishakuambia mimi kwetu siyo Singida, natokea Mwanza. Naona hata kitambulisho changu kimekuthibitishia hilo sasa.”

    “Siyo kigezo sana Laura, lakini naomba nikuulize kitu.”

    “Uliza tu.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Kwanini umekuja Dar?”

    “Nimekuja kwa ajili yako Chris. Nakupenda sana, huwezi kuamini jambo hili hasa kutokana na mwanzo wetu ulivyokuwa, lakini nataka uamini kuwa umeingia moyoni mwangu kama cheche za umeme. Unaniumiza baba. Mapenzi yako yananitesa sana ndiyo maana nikaamua kuja hadi huku kwa ajili yako.



    “Usinione tapeli au mwenye nia mbaya na wewe, amini moyo wangu baba. Nakupenda sana. Nahitaji kutengeneza familia na wewe. Najua ni kiasi gani una wasiwasi na mimi. Ni haki yako kuwa na mashaka kutokana na mazingira yenyewe na hata mimi niliingiwa na wasiwasi kidogo baada ya kufuatwa na maaskari eti natembea na mume wa mtu.



    “Najua ni jambo gumu kidogo kupenya kichwani mwako mpenzi lakini nakuomba sana utambue kuwa moyoni mwangu, mwanaume pekee aliyejaa ni wewe. Niamini na unipe pumziko tafadhali,” Laura alizungumza kwa dakika tatu peke yake bila kupumzika.

    Kwa kiasi kikubwa, maneno ya Laura yalimwingia Chris taratibu ubongoni mwake. Alianza kumwamini taratibu kabisa...



    “Una uhakika na unayozungumza Laura?”

    “Zaidi ya uhakika.”

    “Kweli?”

    “Niamini.”



    Chris alitulia kwa muda tena. Akamwangalia Laura sasa kwa macho ya kawaida yasiyo na hasira. Moyo wake ulilipuka. Laura alikuwa mwanamke mrembo kuliko kawaida. Alihisi mpangilio wa mapigo ya moyo wake ukibadilika kabisa.



    Alijilamba midomo yake, akamwangalia kwa makini Laura ambaye sasa macho yake yalishaanza kuchuruzisha machozi mepesi. Chris akasimama na kumshika mikono Laura kisha akamwonyesha ishara asimame. Laura akasimama. Chris kama aliyechanganyikiwa, alimvutia kwake, Laura akaenda mzima-mzima.

    Wakakumbatiana!



    “Nakupenda sana Laura, nakupenda mama.”

    “Nakupenda pia Chris.”

    “Tafadhali usiniumize moyo wangu mama, usiniingize kwenye matatizo mama. Isije kuwa unatumiwa na watu ili uniharibie. Tafadhali sana mpenzi wangu, naomba unipende kwa moyo wako.”



    “Sijui niseme nini ili uelewe hili ninalosema lakini itoshe tu kukuambia kuwa, linatokea ndani ya moyo wangu!”

    Waliangaliana kwa muda mrefu, macho ya wote yakapoteza uwezo wa kutazama vyema, wakakutanisha midomo yao kisha wakaanza kubadilishana mate.



    Walidumu katika zoezi hilo kwa dakika mbili nzima, kila mmoja akionyesha hisia kali kwa mwenzake.

    “Pwaaaa! Pwaaaa! Pwaaaa! Pwaaaaaaa....” makofi yasikika yakipigwa!



    MSHTUKO wa ghafla ukawapata Laura na Chris waliokuwa wamezama kabisa kwenye ulimwengu wa mapenzi. Walikuwa kwenye dunia ya peke yao kabisa, wakiwa hawana habari na watu walikuwa eneo lile.

    Makofi yaliyopigwa kama vile watu walikuwa wakishangilia tukio fulani muhimu yaliwachanganya kwa hakika. Haraka wakaachiana. Walishangaa kuona kundi zima la Bongo Film Club likiwa limewazunguka wakiwapigia makofi.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Chris akatabasamu.

    “Naomba mnisamehe sana rafiki zangu kwa yote yaliyotokea. Laura, pia naomba unisamehe mama. Ndugu zangu, naomba sasa niwatangazie rasmi kuwa huyu ndiye mama watoto wangu mtarajiwa!” akasema Chris akiachia tabasamu!

    Mlipuko wa shangwe ukaendelea.



    “Kikao cha kwanza ni wiki ijayo hapa hapa Leaders. Mimi ndiye mwenyekiti na mchango wangu ni milioni tatu,” akasema Jaybee, wenzake wakimshangilia.

    “Hayo ndiyo maneno sasa ya kuzungumza... kuhusu usafiri wa maharusi, wazazi na wahudhuriaji wengine kutoka kanisani hadi ukumbini, itakuwa juu yangu,” akasema Chika, wote wakicheka na kuachia shangwe.



    Lilikuwa tukio la kufurahisha sana. Jaybee akajitolea ofa ya vinywaji kwa wenzake wote, kisha wakamimina kwenye glasi na kugongesha kwa furaha. Kikao cha kikazi kikabadilika, hawakujadiliana tena kuhusu filamu, walizungumzia ujio wa shemeji yao mpya; Laura.

    ***

    Giza jepesi lilichukua nafasi katika chumba hicho kikubwa chenye hewa safi iliyotoka moja kwa moja kutokea nje kupitia madirisha makubwa mawili kila upande. Pamoja na hewa hiyo nzuri iliyopenya kwenye mapazia mepesi, feni ilisaidia kupooza joto na kuwafanya viumbe hawa kusahau kabisa kama Dar es Salaam ni mji wenye joto kali.



    Macho ya Chris yalikuwa yamemwelekea Laura aliyekuwa kitandani na gauni jepesi la kulalia. Chris alikuwa amevaa bukta pekee. Alimwangalia sana kama anayemfananisha na mtu anayemfahamu! Laura alikuwa kimya akijilamba midomo yake.



    Hapo sasa, Chris aliamini kweli Laura alikuwa mwanamke mrembo. Macho yake yalizidi kumchanganya Laura na hivyo kushindwa kuvumilia na kumwangushia Chris swali: “Vipi dear, mbona unaniangalia hivyo?”

    “Siamini tu kama nipo na wewe.”

    “Kwanini mpenzi wangu?”



    “Basi tu... sikia darling, kama kuna wanaume wenye bahati duniani, mimi ni mmoja wao. Ni vigumu sana kumpata mwanamke wa ndoto zako katika mazingira kama tuliyokutana mimi na wewe. Kiukweli najisikia faraja sana.”

    “Usijali baba, wewe ni wangu, imeshapangwa iwe hivyo.”

    “Ahsante mama.”



    Chris alivuta shuka, akalitupa juu ya mwili wa Laura, naye akaingia ndani yake. Akamvutia Laura karibu yake, akamkumbatia. Hakuwa na haja ya kuzima, chumba kilikuwa na giza jepesi, mwanga hafifu kutoka taa iliyokuwa nje, ukisaidia kukifanya chumba kiwe katika mwonekano wa kimahaba.



    Chris aliuchoropoa ulimi wake kinywani, akausogeza jirani na mdomo wa Laura, kwa fujo akaanza kulambalamba midomo yake. Zoezi hilo halikudumu kwa muda mrefu sana, Chris akaupeleka ulimi wake kinywani mwa Laura, akaupokea!

    Hawakuwa na sababu za kuzima taa, mwanga mwepesi kutoka taa iliyokuwa nje ya chumba kile uliwatosha kabisa... wakaamua kuendelea na mambo yao wenyewe!

    ***

    Alihisi mwili wake ukiguswa lakini alifikiri alikuwa ndotoni. Mwili uliendelea kutingishwa kwa kasi, mwisho akaamua kufumbua macho. Alikutanisha macho na uso wa mwanamke mrembo sana; Laura. Kwa mara nyingine aliushangaa uzuri wa Laura.



    Laura alikuwa amevaa kanga moja tu kifuani, akionekana alikuwa kwenye pilikapilika za usafi wa asubuhi. Chris alitabasamu, akamwambia: “Vipi dear, umeamkaje?”

    “Salama baba, nilikuwa nafanya usafi... nimeshakuandalia kifungua kinywa. Mbona unachelewa sana kuamka? Unatakiwa kwenda kazini.”



    “Najua darling, ngoja niingie bafuni nikajimwagie maji kwanza, ahsante sana mpenzi wangu,” akasema Chir.

    Haraka akainuka na kwenda bafuni, aliporejea alikwenda moja kwa moja kwenye meza ya chakula.



    Wote kwa pamoja wakaanza kupata kifungua kinywa! Uzuri mwingine wa Laura ukaonekana! Alikuwa mtaalamu sana jikoni.

    “Mh! Kweli hapa nimepata mke,” akajisemea moyoni mwake Chris.





    HISIA za kuwa ndani ya ndoa zilimvamia Chris kwa kasi sana, ni kweli alikuwa anakimbia kuoa muda mrefu kwa sababu hakupata mwanamke ambaye amempenda kwa dhati ya moyo wake, lakini safari hii alikiri kuwa kweli Laura alikidhi vigezo vyote.

    “Kama sijawahi kukuambia, naomba nikuambie leo kutoka moyoni mwangu, nakupenda sana Laura,” akasema Chris.

    Laura akacheka sana!

    “Mbona unacheka?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ni mara ngapi baby umeniambia kuwa unanipenda? Mara nyingi tu... hata jana usiku uliniambia neno hilo.”

    “Basi kama ndivyo, naomba nibadilishe maneno, leo utambue kuwa ninasema kwa kumaanisha kuliko siku zote; nakupenda sana Laura, sijajuta kuwa na wewe na kamwe sitajuta mpenzi wangu.”

    “Ahsante sana mpenzi wangu kwa maneno yako mazuri.”

    Kimya kifupi kilipita, wote wakiendelea kula. Kila mmoja kichwani mwake alikuwa na mawazo yake. Laura alikuwa akiota ndoa na Chris. Kijana mtanashati kama yule, maarufu anayejulikana ndani na nje ya Tanzania kwa kazi yake ya sanaa lakini zaidi ya yote daktari!

    Chris yeye alikuwa akifikiria zaidi kuhusu baba yake, ni kweli amempenda sana Laura, lakini maelekezo ya baba yake ilikuwa lazima mkewe atokee kijijini kwao. Tayari alimshamdanganya kuwa mchumba amepatikana kijijini.

    “Itakuwaje? Mbona naanza kuona dalili mbaya za kumkosa Laura?” akawaza Chris.

    “Lakini nitajua cha kufanya, hawezi kunisumbua. Kichwa changu kinafanya kazi sawasawa,” akajiliwaza kwa maneno hayo.

    Ukimya huo wa mawazo ya ndani kwa ndani huku kila mmoja akiwaza lake, ulivunjwa na Laura: “Halafu dear, kuna jambo nataka kukuuliza.”

    “Uliza tu mama.”

    “Imekuwaje wewe daktari mzima, ukaingia kwenye mambo ya filamu?”

    “Kwanza kwa nini umesema daktari mzima? Inamaana hupendi mimi kuwa msanii?”

    “Sina maana hiyo mpenzi wangu. Ninavyojua mimi, wengi wanaoingia kwenye sanaa huwa hawana elimu ya kutosha lakini wewe kitaaluma uko vizuri kabisa. Kwa nini sasa ukaingia kwenye filamu?”

    “Ni habari ndefu Laura lakini jambo kubwa ambalo nataka kukuambia ujue, napenda sana sanaa na siku zote ndiyo imekuwa chanzo cha ugomvi kati yangu na mzee wangu. Baba alitaka sana niwe daktari, ndiyo maana alinilazimilisha nikazanie masomo ya Sayansi.

    “Alijua kunishawishi, kweli nikajikuta taratibu nimeanza kupenda masomo ya Sayansi na nikayamudu vizuri. Baada ya kumaliza kidato cha sita, mzee alinipeleka Uingereza kusomea udaktari. Nimeishi huko kwa miaka saba.

    “Pamoja na hayo, bado ndani yangu kulikuwa na chembechembe za sanaa, ndiyo maana nikaamua kurudi nchini kwa lengo hilo, lakini kwa sababu kiu ya mzee ni kutaka kusikia nikiitwa daktari tena nikiwatibu watu, nikaamua kuomba kazi Hospitali ya Kinondoni.

    “Mpaka sasa nafanya kazi hapo, lakini nikiendelea na sanaa kama kawaida. Bosi wangu hana tatizo na hilo, maana nilimweleza hali halisi kabla ya kuanza kazi. Naijua vizuri taaluma yangu lakini napenda sana sanaa, vyote vinanipa fedha na ninafanya vyote kwa wakati mmoja,” alisema Chris.

    “Hongera yako.”

    “Ahsante.”

    Walipomaliza kula, wote walitoka kwa pamoja na kuingia kwenye gari la Chris, wakaenda moja kwa moja kazini kwa Chris, akamtambulisha kwa baadhi ya wafanyakazi wenzake kisha akamruhusu aendelee na mizunguko yake mingine.

    Laura hakuwa na mambo mengi sana siku hiyo, kikubwa hasa ilikuwa ni kwenda Kariakoo kufanya manunuzi ya mavazi na vitu vingine vya kwenda navyo Singida.

    ***

    Laura alikaa Dar kwa wiki nzima akipoteza vipindi vyote kwa muda huo. Siku ya kurejea Singida ilikuwa ya huzuni sana kwake. Chris alimsindikiza mpaka kituoni, Ubungo ambapo alikuwa ameshamkatia tiketi kwenye basi la ABC.

    Laura aliagana na Chris wakiwa wamekumbatiana kwa muda mrefu sana. Ilikuwa ni kama hawakuwa na mpango wa kuachiana. Mwili wa Laura ulisisimka sana, alitamani kuendelea kubaki Dar lakini haikuwezekana, alipaswa awahi masomo Singida.

    Muda wa safari ulipowadia, hakuwa na jinsi – aliingia garini na kumwacha Chris akiwa anamtazama kupitia dirishani. Saa 12:00 asubuhi, gari lilianza kuondoka. Laura akampungia Chris mkono huku akitoa machozi, ni kama walikuwa wanarekodi filamu lakini ilikuwa kweli.

    Waliendelea kupungiana mikono mpaka gari lilipofika mbali. Chris akaenda kwenye maegesho, akaingia kwenye gari lake, akaondoka. Ilikuwa safari ya kuelekea kazini kwake. Saa 3:00 asubuhi hiyo alikuwa na kazi ngumu sana ya kumfanyia mtu upasuaji mkubwa!



    USO wa mzee huyu ulionyesha dhahiri kuwa hauna masihara; alitaka kujua jambo moja tu tena lenye hakika kutoka kwa mwanaye. Alitaka kujua kuhusu ndoa. Chris alitulia akimwangalia baba yake, kichwani akitafakari ni jibu gani lingemfaa baba yake.

    “Chris niambie ukweli, umefikia wapi?” baba yake akamwuliza.

    “Baba nilishakuambia kuwa lazima nitaoa mwaka huu kwa sababu tayari nimeshapata mchumba.”

    “Sasa mbona unachelewesha mambo?”

    “Si kuchelewesha baba, ni suala la mipango tu. Nipe muda.”

    “Muda gani?”

    “Miezi miwili inatosha kabisa, nipatie muda huo baba nitakamilisha hili suala.”

    “Nataka iwe hivyo.”

    Mzee Shila, baada ya kuzungumza hayo, alitoka haraka na kuelekea chumbani kwake, sebuleni alibaki Chris na mama yake tu. Waliangaliana kwa muda, kisha kila mmoja akajikuta akiinamisha uso wake chini.

    “Lakini mwanangu, kwa nini usioe ili kuachana na haya manenomaneno ya baba yako?”

    “Mama kwani nimekataa kuoa? Si tayari nimeshasema nimepata mchumba mama, kikubwa hapo ni muda tu.”

    “Sawa.”

    “Mama ngoja mimi niondoke, nina ratiba nyingi sana kesho asubuhi. Acha tu niende sasa,” akasema Chris akimtulizia macho mama yake.

    “Sawa baba, usiku mwema.”

    “Nanyi pia.”

    ***

    Kichwa kilitaka kupasuka. Alitulia kitandani mwake akiwaza sana, dalili za kumpoteza mrembo Laura zilianza kuonekana waziwazi. Alitamani sana kumuoa Laura, hakuwa mwanamke wa kucheza naye kwa usiku mmoja tu!

    Laura alikuwa mke!

    “Lakini itawezekanaje wakati mzee naye analazimisha mke atokee kijijini?” akawaza Chris.

    “Kuna kitu natakiwa kufanya hapa, lazima nimpate Laura maishani mwangu, siwezi kukubali akaolewa na mwanaume mwingine, haitawezekana hata kidogo,” akazidi kuwaza Chris.

    Akiwa mawazoni, simu yake iliita. Haraka akaichukua na kuangalia kwenye kioo; akakutana na jina la Laura lilitokea. Akapokea haraka sana...

    “Haloo mpenzi wangu...” sauti tulivu ya Chris ilitoka.

    “Yes darling, za huko?”

    “Nzuri tu mama. Unaendeleaje huko?”

    “Nipo vizuri tu, nimekukumbuka mpenzi, hata usingizi umekata kabisa.”

    “Kweli mpenzi?”

    “Kweli kabisa.”

    “Nataka kuuliza kitu dear maana naona dalili mbaya.”

    “Dalili mbaya za vipi mpenzi?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kuhusu mapenzi yetu.”

    “Mh! Mbona sikuelewi? Hebu niulize.”

    “Unanipenda kweli mama?”

    “Nakupenda sana.”

    “Unakumbuka nilikuambia nini kuhusu mzee wangu?”

    “Nakumbuka.”

    “Sasa hapo ndipo kwenye tatizo. Baba ameendelea kushikilia msimamo kuwa nioe mwanamke kutoka kijijini kwetu. Kuna kitu tunatakiwa kufanya mpenzi wangu ili tuweze kufanikisha jambo hili.”

    “Mh! Kweli kuna kazi, kwa hiyo hutanioa Chris kwa sababu hiyo? Kumbuka mimi nakupenda na nimekuwa tayari kufanya kila kitu kwa ajili yako. Sipo tayari kukupoteza.”

    “Najua, ndiyo maana nimekuambia, kuna jambo inabidi lifanyike ili tufanikishe.”

    “Ni jambo gani mpenzi wangu?”

    “Nimeshamwambia baba kuwa nimepata mchumba kijijini, sasa unachotakiwa kufanya.

    Itabidi nikazungumze na baba mdogo kuhusu jambo hili ili wewe uende kijijini, ukakae kwa muda, mzee ajue unatokea kule. Lengo langu ili mambo yaweze kwenda bila matatizo, itawezekana kweli mpenzi wangu?” akasema Chris.

    “Kwa nini ishindikane wakati nakupenda baba?”

    “Sasa itakuwa lini?”

    “Panga wewe. Wiki mbili zijazo tunamalizia muhula, tunafunga chuo kabla ya kurudi tena kumalizia chuo kabisa.”

    “Safi kabisa, ngoja nijipange ndani ya muda huo mama. Vipi, nyumbani hakutakuwa na tatizo?”

    “Hapana, nitajua cha kufanya. Niamini mimi.”

    “Sawa mpenzi wangu, angalau sasa nina amani. Naweza kupata usingizi wangu vizuri nashukuru sana mama, usiku mwema.”

    “Nawe pia.”

    Mwanga wa ndoa yake na Laura ulionekana wazi kabisa. Moyo wake ukagubikwa na furaha ya ajabu. Haikuwa kazi ngumu tena kupata usingizi. Kilichobaki ilikuwa ni utekelezaji tu!



    DK. Chris aliandika maneno fulani kwenye kadi alilokuwa nalo mkononi kisha akayarudisha tena macho yake kwa mgonjwa aliyekuwa ameketi mbele yake. Alikuwa mwanamke anayeelekea kuwa na umri si zaidi ya miaka 30. Alikuwa mpole, mkimya na anayeonekana kuhitaji huduma ya haraka sana. Hiyo ilikuwa ni muda mfupi baada ya kwenda maabara kutoa vipimo



    . Aliitwa Sandra.



    “Kuna tatizo kwenye mkojo wako. Una maambukizi. Kitaalamu tunaita Urinary Tract Infection, kwa kifupi UTI. Pia una malaria kali. Kwa namna hali yako ilivyo, ni lazima tukulaze ili tukuanzishie drip za kwinini mara moja ambayo inaweza kutibu malaria vizuri na haraka zaidi. Nitakupa na Antibiotics kali kwa ajili ya UTI.



    “Hata hivyo lazima uwe makini sana matumizi ya vyoo, ambavyo hasa ndiyo chanzo kikuu cha maambuzi ya UTI. Pole sana Sandra,” alisema kwa sauti tulivu sana Dk. Chris.



    “Ahsante dokta.”

    “Ngoja nimuite sista aje kukuchukua,” akasema Dk. Chris.

    Akainua mkonga wa simu iliyokuwa mezani kisha akabonyeza namba fulani na kuanza kuzungumza na upande wa pili. Muda mfupi baadaye alifika na kukabidhiwa kadi la Sandra, kisha akaongozana naye wodini. Mgonjwa mwingine akaingia.



    Ndivyo siku ya Dk. Chris ilivyokuwa kazini kwake, Hospitali ya Kinondoni siku hiyo. Ilikuwa siku ambayo alidili na wagonjwa wa kawaida tu. Hakuwa na ratiba ya upasuaji siku hiyo.

    ***

    Ilikuwa lazima apange safari ya Singida haraka iwezekavyo. Baba yake mzee Shila asingemwelewa hata kidogo kama angeendelea kuchelewa kuoa. Tayari alishatengeneza mazingira mazuri ofisini kwake.

    Ni muda ambao hata Laura naye alikuwa ameshafunga chuo baada ya kumaliza mitihani. Ilikuwa ni kipindi cha likizo fupi ya wiki mbili. Hizo zilitosha kabisa kukamilisha mpango waliokubaliana.



    Chris alisafiri hadi Singida ambapo alikutana na Laura na kuweka mipango yao sawa. Hakuwa na hofu tena, alishaamini kabisa kuwa Laura hakuwa mke wa mtu kama alivyojulishwa awali.

    Hata hivyo kwa hofu ya usalama wake, hakuwa tayari kukutana naye katika hoteli ileile ya awali. Alifikia hoteli nyingine iliyokuwa nje kidogo ya mji.



    “Laura unanipenda kweli? Kumbuka hapa nakwenda kufanya usaliti lakini ni kwa ajili ya penzi letu.”

    “Najua baba, nakupenda, niamini.”

    “Ahsante mama, sidhani kama tunatakiwa kutoka, maana kesho asubuhi tunakwenda kijijini. Mipango yote nitakuambia hukohuko, sawa mpenzi wangu?”



    “Nimekuelewa baba.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walilala wakiwa na matumani makubwa ya kufanikisha mpango uliokuwa mbele yao; mpango wa ndoa. Safari haikuwa mbali sana.

    Ni kesho tu!

    ***

    Walishuka katika kituo cha Ibaga saa kumi jioni ikiwa ni safari ya takribani saa tano kutoka Singida Mjini hadi hapo katika mji mdogo wa Ibaga.

    Kama miundombinu ingekuwa mizuri, ni safari ya saa mbili tu tena kwa mwendo wa kawaida. Walikuwa wachovu sana kwa safari hiyo. Walitafuta nyumba ya wageni na kulipia. Hapo ndipo filamu ilipotakiwa kuanza rasmi.



    “Lazima mavazi yako yabadilike sasa, utavaa zile nilizokununulia mjini. Unapaswa kufanana na watu wa huku. Mchezo ulivyo ni kwamba, leo mimi nitakwenda nyumbani - Mkalama, wewe utalala hapa hadi kesho.

    “Nitakwenda kuzungumza na baba mdogo ambaye anajua kila kitu kuhusu wewe, halafu yeye atazungumza na bibi kwamba, wewe utakuja kututembelea. Pale ndiyo sehemu ya kuchukua pointi, usilaze damu, ujitahidi kuendana na kila kitu cha pale nyumbani.



    “Kwa bahati nzuri, hakuna shida sana, halafu kipindi hiki si cha kilimo kwa hiyo hawatakupeleka shamba. Kifupi uonyeshe heshima na mwonekano wa mtu wa kijijini usiyejua mambo ya mjini sana.

    “Lakini itabidi tudanganye kuwa, hufahamu vizuri lugha yetu kwa sababu wazazi wako walihamia Mwanza tangu ukiwa mdogo lakini sasa wameamua kurudi tena kijijini. Mambo mengine utaniachia mimi.



    Umenipata?” akasema Chris.

    “Nimekuelewa vizuri sana.”

    Mpango mzima ukawa umekamilika, ilibaki utekelezaji tu!

    ***

    Chris alikodi baiskeli kutokea Ibaga hadi Mkalama, kijijini kwao. Alifika baada ya nusu saa tu. Alipokelewa vizuri na baba yake mdogo ambaye alimpa mpango mzima ulivyokuwa.

    “Wazo zuri sana Chris, acha nizungumze na bibi. Naamini naye atafurahi. Hatajua mchezo wetu na inabidi iwe siri yetu tu,” akasema Shamakala.

    “Sawa baba mdogo.”



    “Zoezi linafanyika lini?”

    “Hakuna kusubiri, ni kesho tu baba mdogo.”

    “Sawa.”



    CHRIS hakutaka kupoteza muda, kilichokuwa akilini mwake ni mke tu. Hakutaka mwanamke mwingine zaidi ya Laura. Baba yake mdogo, Shamakala alikubaliana na wazo lake.

    Hakuwa na sababu ya kupoteza muda. Alimfuata mama yake, alipokuwa amekaa kisha akaketi kwenye kigoda jirani yake.



    “Mkombi...” (Mama) Shamakala aliita kwa Kinyiramba.

    “Shamakala unasemaje?”

    “Kuna jambo zuri nataka kukuambia.”

    “Zuri? Hebu nikae vizuri sasa. Haya niambie ni nini?”

    “Ni kuhusu Chris... anataka kuoa.”



    “Jambo zuri sana hilo. Ameshapata huyo mwali mwenyewe sasa?”

    “Ndiyo, tena ni mtu wa hukuhuku kwetu.”

    “Wa wapi?”



    “Anatokea Kijiji cha Mpambala.”

    “Safi sana, sasa mmefikia wapi?”

    “Anataka kesho amlete hapa nyumbani aje kututembelea, kama tena taratibu zetu, tukikaa naye hapa japo kwa siku mbili tutaweza kumchunguza japo kidogo unavyojua na sisi ili tujiridhishe kuwa anafaa kuingia kwenye familia yetu.”



    “Ni wazo zuri, utaongozana naye sasa au?”

    “Ndiyo... mimi ndiyo mwenyeji wake pale, lazima niende naye.”

    “Mimi naunga mkono mwanangu, sina matatizo na hilo.”



    “Sawa mama, nilisema nikujulishe tu maana ungeshangaa kuona mtu amekuja nyumbani bila taarifa yako, tukaona si busara.”

    “Mmefanya vizuri.”



    Shamakala alifurahishwa sana na majibu ya mama yake. Alimfuata Chris na kumweleza kila kitu kilivyokuwa, akafurahi sana.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Usiku ulikuwa mrefu sana, alitamani asubuhi ifike haraka ili Laura afike nyumbani kwao. Alitaka kuona namna ambavyo bibi yake angemchukulia.

    ***

    Chris alikuwa wa kwanza kuamka asubuhi hiyo. Alidamka saa moja kasoro, muda ambao kwa kipindi hicho ambacho hakikuwa cha kilimo, ilikuwa mapema sana.

    Kwa kawaida wakati wa kilimo wanakijiji hadaamka mapema na kwenda mashambani. Si katika kipindi hicho cha kiangazi. Alifanya shughuli ndogondogo za nyumbani hadi saa mbili ndipo baba yake mdogo alipoamka.



    Chris alifurahi sana alipomuona baba yake mdogo akitoka nje. Baada ya salamu, wakaanza kupanga namna ya kufanya.



    “Hapa hakuna cha kujadili sana, twende tu juu kule juu tukachukue pikipiki tuondoke,” akasema Chris.

    “Sawa... lakini tupate kifungua kinywa kwanza.”

    “Hapana, tutakunywa supu Ibaga.”

    “Sawa.”



    Hawakuwa na muda wa kupoteza, walikwenda barabarani walipochukua pikipiki moja ambayo walipanda kwa mtindo wa mshikaki, safari ya kwenda Ibaga ikaanza.



    Kwa pikipiki ulikuwa ni mwendo wa dakika kumi tu, walikuwa wameshafika Ibaga. Chris ndiye aliyemlipa dereva, kisha wakatembea na kuelekea kwenye mgahawa mmoja maarufu eneo hilo.

    “Sasa dingi, we’ nisubiri hapa, ngoja nikamchukue.”

    “hivi ni wapi kwani?”



    “Tumefikia Sayuni Lodge.”

    “Sawa.”

    Shamakala na Chris walikuwa na umri unaokaribiana sana, Shamakala alikuwa mtoto wa mwisho katika uzao wa baba yake na Chris. Sababu hiyo iliwafanya wazoeane kwa kiasi kikubwa.



    Hata mazungumzo yao yalikuwa ya ujana zaidi kutokana na umri wao kukaribiana. Hata hivyo, hilo halikuvunja heshima waliyokuwa nayo. Bado Chris aliendelea kumheshimu Shamakala kama baba yake.

    Chris alifika Sayuni na kwenda kugonga katika chumba alichomuacha Laura jana yake. Aligonga mara moja tu, Laura alifungua. Chris alishangaa sana.



    Alikutana na Laura mpya kabisa. Laura alikuwa amevaa mavazi ambayo kwa kumwangalia tu unajua kuwa, alikuwa msichana aliyeishi kijijini. Alifafana nao kwa kila kitu.

    “Daah! Kweli umefunika mpenzi wangu. Hapo umepatia kabisa.”



    “Nashukuru mpenzi, nini kinaendelea?”

    “Kama uko tayari, tuondoke. Hakuna kitu cha kusubiri zaidi.”



    Ndivyo ilivyokuwa, walitoka na kwenda mgahawani alipokuwa Shamakala. Utambulisho mfupi ukafanyika kisha wote wakaagiza supu ya mbuzi. Walitumia dakika kumi tu kumaliza kula, kisha wote kwa pamoja wakainuka na kwenda kukodisha pikipiki iliyowafikisha kijijini Mkalama.



    Safari hii walifikishwa hadi nyumbani kwao kabisa. Walishuka kwenye pikipiki kisha wakapiga hatua za taratibu huku nyuso zao zikiwa zimepambwa na tabasamu pana. Bahati nzuri bibi alikuwa nje ameketi kibarazani.



    Bibi alipowaona, alionekana kuukunja uso wake. Hata Chris alipojaribu kutabasamu, bado bibi aliendelea kukunja uso wake.



    HAKUaliyejua kilichokuwa moyoni mwa bibi, hakuwa ameukunja uso wake kwa hasira. Uso ulikunjamana kwa mshangao wa kumuona mjukuu wake sasa alifikia uamuzi sahihi wa kuachana na ukapera.



    Chris na baba yake mdogo walipiga hatua za taratibu kumfuata bibi. Shamakala alikaa pembeni, bibi akawasogelea, wakakutana katikati. Alichokifanya bibi ilikuwa ni kuinama kidogo.



    Haraka Shamakala akamwonyesha Laura ishara kuwa apige magoti chini. Akafanya hivyo. Bibi akamshika mkono Chris. Akatema mate kidogo mkononi mwake kisha akampaka Chris usoni.



    Akamsogelea Laura, akamshika mikono yote miwili na kumwonyesha ishara asimame. Akafanya hivyo; akamvutia kwake na kumkumbatia, kisha akamtemea mate kidogo kwenye paji lake la uso.

    Laura akatabasamu!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwao ilikuwa heshima kubwa sana, kutemewa mate na bibi, ilimaanisha baraka na kukubalika katika familia. Bibi akamshika mkono na kumwongoza hadi sebuleni, kwenye nyumba ile ya zamani ya tembe.

    “Karibu sana mjukuu wangu,” bibi akamkaribisha Laura.



    “Ahsante bibi.”

    Tayari kifungua kinywa kilikuwa kimeshaandaliwa na mke wa Shamakala. Chai ilitengwa na vitafunwa vya maboga na mahindi ya kuchemsha. Wakaketi kwenye jamvi na kuanza kula. Wanaume walikula nje, wanawake ndani.



    Ilikuwa siku mpya kwa Chris. Siku ya utambulisho wa ‘Laura wa Kijijini!’. Ukweli wa mambo ulijulikana na Laura, Chris na Shamakala pekee.



    ***

    Moto ulikuwa unawaka huku moshi ukitoka. Ulikuwa usiku wa mbalamwezi. Watu wawili walikuwa wameuzunguka moto uliowashwa kwa kutumia kinyesi cha ngo’mbe. Ndani ya moto huo kulikuwa na karanga zikichomwa.



    Kazi yao ilikuwa ni kuchomoa na kuendelea kula taratibu. Hapakuwa na mazungumzo. Muda kidogo bibi alifika.



    “Hivi huyu msichana ni wa hapa Mkalama kweli?” bibi akamwuliza Chris.

    “Hapana bibi. Ni kutoka Mpambala kama tulivyokuambia,” Chris akajibu.

    “Lakini mbona hafahamu kinyumbani?”



    “Bibi hajakulia hapa, wazazi wake walihamia Mwanza muda mrefu sana, tangu akiwa mdogo, amesomea huko na sasa hivi anamalizia masomo yake Singida Mjini ndiyo maana hajui vizuri kinyumbani. Ni kama mimi tu.”



    “Hapo sawa.”

    “Vipi lakini bibi, umegundua tatizo lolote kutoka kwake?”

    “Tatizo? Hapana... ni msichana mzuri sana, mchapakazi na anayejua kujituma. Hana tatizo kabisa. Naweza kusema kwamba, mjukumuu wangu pale umepata mke sahihi.”



    “Ahsante sana bibi.”

    “Sasa lini mipango yako?”

    “Bado kidogo, nasubiri amalizie masomo yake tu. Amebakiza miezi sita. Hatutakuwa na muda wa kusubiri zaidi. Akimaliza kinachofuata ni ndoa.”



    “Sawa. Nyie endeleeni kuota moto lakini chakula kipo tayari, sasa hivi kinakuja.”

    “Sawa bibi.”



    ***

    Siku tatu zilitosha kabisa kwa Laura kuthibitishwa kuwa mke mtarajiwa wa Chris. Bibi alishatoa baraka zote. Ilikuwa furaha kubwa sana kwao. Waliagana wakiwa wenye furaha sana.



    “Karibu kwenye ukoo wetu mjukuu wangu, hakuna atakayepinga uamuzi huu. Hata kama nikifika leo, kabla ya ndoa yenu, watu wote wanaonihusu watambue kuwa nimeridhia ndoa yenu,” akasema bibi.

    “Ahsante sana bibi, nimefurahi sana kusikia hivyo,” Chris akasema.



    Chris na Laura wakaondoka. Walikwenda hadi kituoni ambapo walichukua pikipiki iliyowapeleka moja kwa moja hadi mji mdogo wa Ibaga. Walifikia kwenye gesti ileile, Sayuni.



    Walipoingia tu chumbani, wote walikumbatiana kwa furaha ya ushindi. Laura machozi yalimtoka kama maji yanavyotiririka kwenye mfereji uliopo bondeni.



    “Tulia mpenzi, najua ni kiasi gani una furaha moyoni mwako. Ni furaha yetu sote na ni haki yetu kufurahi,” akasema Chris.



    “Sikutegemea kama mambo yangeisha kwa wepesi kiasi hiki.”

    “Najua lakini usijali. Sasa tumebakiza eneo moja tu. Nyumbani kwenu. Lazima hili jambo lijulikane mpenzi wangu kama kweli tuna lengo la kuoana. Kuna kitu lazima kifanyike mpenzi.”



    “Ni kweli baba, nakuamini kwa mawazo yako, tunaanzia wapi?”

    “Nashauri tukitoka hapa, wewe usikae kabisa mjini, nenda moja kwa moja Mwanza, kazungumze na wazazi wako kuhusu hili suala ili nao pia wawe wanajua.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Maadamu tunapendana na bibi amesharidhia, naamini ni jambo jepesi sana kumhadaa mzee Shila!”

    “Kweli dear?”“Kabisa!”“Sawa.”



    Ikawa asubuhi nyingine yenye kupendeza zaidi. Furaha yao haikubaki mioyoni mwao pekee, ilitoa msukumo mkali na kuchemsha damu za miili yao. Wote wakawaka!

    Walijua namna ya kukitumia chumba kile vizuri kabisa!





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog