Search This Blog

Friday, July 15, 2022

ULIKUWA WAPI - 1

 





    IMEANDIKWA NA : GRACE G.R



    *********************************************************************************



    Simulizi : Ulikuwa Wapi

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    Ulikuwa wapi wakati mama yangu anafariki? Ulikuwa wapi nikiomboleza kwa ajili ya baba yangu? ulikuwa wapi nafukuzwa shule kwa ajili ya ada? Ulikuwa wapi nilipoanza kuzurura mtaani? Ulikuwa wapi nauza bikira yangu kwa ajili ya maisha ya mdogo wangu? Ulikuwa wapi miaka yote 22 ya maisha yangu bila wazazi na bila msaada? Nawezaje kuona thamani yako?

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Namuuliza maswali hayo baba yangu mdogo, ambaye nakumbuka vizuri siku baba yangu anafariki alimuachia mimi na mdogo wangu, akampa maelekezo ya kututunza na kutusomesha. Siku ya huzuni zaidi kwenye maisha yangu, lakini sikujua ukubwa wa huzuni hiyo, mpaka nilipoanza maisha bila baba, bila mama. Kabla ya kifo cha baba, baba yangu mdogo, Musa, alionesha kutujali na kutupenda. Alikuja nyumbani mara kwa mara, akituletea chokoleti, pipi na zawadi nyingi za kitoto. Wakati huo alifanya kazi benki ya NBC, hivyo uwezo wake haukuwa mdogo. Kulingana na akili ya umri wangu wakati huo, niliona baba mdogo ana hela nyingi sana kwani niliwahi kuambiwa hela zote hupelekwa benki. Nilijua wafanyakazi wa benki wote ni wamiliki wa pesa nyingi zinazopelekwa huko.



    Mara nyingi baba alituambia anapeleka hela benki, au anaenda kuchukua hela benki, hivyo nikaiaminisha akili yangu kuwa baba mdogo atakuwa na pesa nyingi sana kuliko baba. Niliwahi kumuuliza mara kadhaa, “Eti bamdogo wewe si una hela nyingi sana? Benki si watu huwa wanaweka hela, nawewe ndio unafanya kazi huko?” Niliamini anamzidi baba pesa, na mara kadhaa nilimwambia hivyo, kwamba baba yetu ana pesa lakini wewe unamzidi pesa.



    Baba yangu, marehemu mzee Stephano Wanjiku, alizaliwa kama mtoto wa pekee kwa mama yake, aliyezaa na mkenya miaka ya nyuma, kisha hawakuoana na huyo mwanaume, mama yake ambaye ni bibi yangu akarudi Tanzania, akaolewa na mmasai mmoja, mzee Olengai. Walizaa naye watoto wa tatu, lakini mpaka napata akili mmoja alikuwa ameshafariki, na babu pia mzee Olengai. Bibi yetu tuliishi naye nyumbani kipindi fulani, mpaka baada ya kifo cha baba yangu, ndipo tukahamia kwa baba mdogo.



    Baba alifariki kwa ajali ya gari yake, lakini hakufa papo hapo, alikaa hospitali KCMC Moshi kwa muda wa wiki moja, akaruhusiwa kurudi nyumbani lakini wiki iliyofuata alipata mshtuko wa moyo na kufariki. Siku aliyofariki tulikuwa mimi na baba mdogo tumekaa naye sebuleni, mama akiwa jikoni na mdogo wangu amelala chumbani. Baba, kama mtu aliyejua kinachoenda kutokea, alianza kumwambia baba yangu mdogo maneno yaliyoashiria kuondoka kwake, mbele yangu,



    “Musa mdogo wangu, wewe ndiye mwanaume ninayekuamini kiasi cha kuweza kukukabidhi familia yangu. Mke wangu bado mdogo ki umri, hivyo ataolewa najua, maana pia ni mrembo sana, lakini siku zote jua hawa ni watoto wako, kabla na hata baada ya mke wangu kuolewa. Simaanishi umnyang’anye, lakini hakikisha unawatunza na wanasoma. Kustawi au kuharibika kwa maisha yao kuko mikononi mwako. Sijafanikiwa kuandika urithi, lakini naamini huna tamaa ya mali hivyo hautamnyang’anya mke wangu mali zake. Mimi naondoka, najua nitakufa tu, lakini naomba unitunzie familia yangu.” Baba aliongea hayo kisha akawa kama amebanwa na kitu kifuani, kabla hata hajatolewa nje kupelekwa hospitali, alifariki.



    Sikuwa mkubwa wakati huo, japo mpaka leo nakumbuka maneno ya mwisho ya baba yangu. umri wangu ulipata miaka nane tu, na mdogo wangu miaka mitatu. Baba alikuwa mfanya biashara mkubwa sana miaka hiyo, wa magari kutoka Japan, hivyo alikuwa kati ya matajiri waliotikisa Arusha miaka hiyo. Wakati wa msiba, mama alipoteza fahamu mara kadhaa. Nakumbuka kuna wakati ilibidi apelekwe hospitali. Katika utu uzima wangu ndio nimeelewa kiasi gani mama hakuwa amejiandaa kwa kifo cha baba, au labda baba hakumuandaa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya mazishi, akili ya mama ilikuwa kama imechanganyikiwa, kiasi cha kupelekwa hospitali. Mimi na mdogo wangu Zita tulichukuliwa, pamoja na bibi tuliyeishi naye pale nyumbani, tukapelekwa kwa baba mdogo, ambaye hakuwa ameoa wakati huo,na aliishi na mdogo wake pia, wa kiume, bamdogo Naise. Mama alipotoka hospitali, hakurudishwa tena nyumbani, lakini naye aliletwa kuishi nasi kwa baba mdogo Musa.



    Ghafla maisha yalianza kubadilika, mama alichukuliwa kama mtoto na sio mke wa baba tena. Bamdogo alimgombeza mama mbele yetu, hakuruhusiwa kufanya chochote bila ruhusa yake huku akimsema kwamba ni mgonjwa wa akili. Nakumbuka mara kadhaa nilikaa na mama chumbani, nikimbembeleza na kumfuta machozi. Mama alianza kudhoofu na mara kwa mara alipelekwa hospitali kwa matibabu ya msukumo wa damu yaani presha. Kuna wakati alizidiwa sana, nikapata wasiwasi kuwa atakufa na yeye. Nakumbuka siku moja, nimetoka shule, nilimkuta mama akiwa na Zita, peke yao nyumbani, huku mama anaumwa sana. Kulingana na maelezo ya mama, alianza kuumwa tangu asubuhi, bamdogo akiwepo pamoja na bibi, lakini bibi alitakiwa kupelekwa kliniki yake hivyo waliondoka baba zangu wadogo wote wawili na bibi, ili bamdogo Naise akakae na bibi kliniki wakati kaka yake akienda kazini. Sikuelewa kwanini hawakwenda pamoja na mama.



    Mara ya mwisho mama anaumwa, anapelekwa hospitali na kurudi, kabla ya siku hiyo, bamdogo Musa alisema ugonjwa wa mama ni wa kawaida tu, wameshauzoea kwa sasa, hivyo atapona hata bila dawa tena. Alisema kuanzia siku hiyo hatakuwa akitumia mafuta na muda wake tena kumpeleka hospitali, na ndicho alichofanya siku hiyo. Niliogopa sana kuona hali aliyokuwa nayo mama. Kwa bahati mbaya sana, eneo tuliloishi, Sakina, ni maeneo ya uzunguni kidogo, hivyo hakukuwa na majirani wa karibu wa kuwagongea. Nyumba ziliunganishwa kwa mageti. Nikiwa nimechanganyikiwa sana, bibi alikuja, na huyo mwanae Naise. Nikawakimbilia getini kuwaambia mama anaumwa. Bibi alipata hofu na kumtaka bamdogo Naise ampeleke hospitali, lakini hakukubali badala yake akaondoka akidai ameshamaliza siku nzima na mambo ya hospitali hivyo ana ratiba zake za muhimu zaidi. Bibi aliumwa miguu, hakuwa na uwezo wa kutembea hata mita mia moja.



    Sitasahau maumivu niliyopata, mama yangu akikata roho miguuni pangu. Niliona sasa dunia imefika mwisho. Binti wa miaka nane, nilikuwa napewa jukumu la kuwa baba na mama kwa mdogo wangu Zita. Nililia sana, mno yaani, bibi akanikumbatia, akalia namimi, akamfumba mama macho. Sikutaka mama atoke miguuni kwangu, nikiendelea kumuamsha kwa nguvu, huku tukisaidiana na mdogo wangu ambaye akili yake ndogo sana haikuelewa yanayoendelea ulimwenguni. Alianza kulia huku akiuliza kama mama naye watampeleka kule alikoenda baba. Aliomba sana wasimfukie mama kwani baba walimfukia na hakurudi tena.



    Tukimzika mama yangu, niliona kila kitu ni kichungu. Sikuona thamani tena ya kuishi, nikataka kujitupia kaburini nizikwe na mama, lakini nilimuhurumia mdogo wangu, na hata hivyo nisingeachiliwa kufanya hivyo. Nililia, kama mtu asiye na msaada wala tumaini lolote. Zita naye alilia sana, akiangalia wanamzika mama. Nilipomuangalia, sikuona mtoto, niliona jukumu kubwa mno ambalo sikujua namna gani naweza kulibeba. Maisha yalinigeuka kwa haraka sana, kupoteza baba na mama ndani ya miezi sita.



    Baada ya msiba, tulianza maisha mapya kabisa. Kuna msichana wa kazi aliyeishi pale nyumbani lakini alipewa maagizo ya kuanza kunifundisha kazi. Kila nilipotoka shule, nilitakiwa kufanya kazi za ndani mpaka wakati wa kulala. Nakumbuka miezi miwili iliyofuata tulifunga shule, nikabaki nyumbani. Hapo ndipo nilifanya kazi zilizo ndani na nje ya uwezo wangu. Nilidamshwa alfajiri kila siku, nikatakiwa kusafisha nyumba, kusafisha uwanja, kuandaa chai, kufua, na kazi zote huku dada wa kazi amenisimamia tu bila kunisaidia chochote. Nilichoshangaa, hata dada alishirikiana na baba zangu wadogo kunitumikisha kana kwamba si wajibu wake. Bibi alijaribu kunitetea lakini hata yeye hakuwa na kauli mbele ya watoto wake hao.



    Nakumbuka baada ya kufungua shule nilitakiwa kulipiwa ada kwa ajili ya muhula uliofuata. Nilisoma shule moja ya Kimataifa inaitwa Arusha Modern. Nilipopewa barua ya kulipa ada, niliipeleka kwa baba mdogo, lakini sitasahau siku nimempa ile barua. Aliichana mbele yangu, akanitukana sana huku akidai hawezi kutumia pesa yake kunilipia ada wakati anajua ntaishia kubeba mimba tu. Alisema kazi inayonifaa ni kufanya kazi za ndani na sio kusoma. Baba mdogo alisema kwamba ameshatumia gharama kubwa sana kwa ajili yetu hivyo inabidi nifanye kazi, msichana wa kazi aondoke.



    “Nina haja gani ya kuendelea kutumia pesa zangu kukusomesha, na pia kumlipa msichana wa kazi wakati wewe uko hapa na mdogo wako mnakula na kulala bure? Wewe mwenyewe unajua baba yako hakuwa na pesa kama zangu, na kwa taarifa yako miaka yote mimi ndiye nilimpatia pesa za kuwatunza. Sasa huu ndio mwisho wa kusoma kwako, utakaa hapa nyumbani na kufanya kazi za humu ndani, huyu binti wa kazi ataondoka.” Alisema maneno hayo baba mdogo, akimaanisha kunikatiza shule. Pia nadhani alichukulia ile kauli niliyokuwa nikimwambia kuwa yeye ana hela kuliko baba, akaamua kunidanganya hivyo. Niliendelea kwenda shule, lakini niliporudi niliongezewa kazi na wakati mwingine kupigwa bila sababu huku akinihakikishia kuwa sitaweza kuendelea kwani nitafukuzwa ada. Kweli ndani ya mwezi mmoja tu nilirudishwa na kuambiwa nisiende tena mpaka nitakapolipiwa.



    Nilitegemea dada aondoke siku chache baadaye na asirudi tena. Ni kweli aliondoka, lakini tofauti na matarajio yangu, alirudi baada ya kama mwezi au miezi miwili na kuanza tena kuishi pale. Niligundua baadaye kuwa alirudi akiwa mjamzito. Huyu dada sasa hakuwa dada Selina niliyemzoea kabla. Mara hii alinichukia na kunitesa kwa waziwazi, bila sababu. Nilipochelewa kuamka, aliniamsha hata kwa kunimwagia maji. Alitegemea nifanye kila kitu mwenyewe, mpaka kazi zake binafsi kama kufua nguo za ndani.



    Kuna siku niliamka naumwa, nikafanya kazi kwa ugumu sana, lakini dada Selina hakujali hilo kabisa. Siku hiyo nilitapika sana, mpaka bibi ilibidi aseme kwa ukali sana, ndipo jioni baba mdogo aliporudi nikapelekwa hospitali. Wiki hiyo nzima nilikua mgonjwa, lakini ni kwa utetezi wa bibi tu, tena akigombana sana na dada Selina, ndipo nikaruhusiwa kupumzika kwa siku kama tano. Haikupita muda, dada alihamia chumbani kwa bamdogo Musa. Akili ikaanza kuelewa kwamba huyu si dada tena bali ni mama mdogo na ndio sababu hakuendelea kuwa mfanyakazi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mateso yangu yalizidi sana, lakini nilipata faraja kwa bibi, aliyenitia moyo kuvumilia akiniahidi kuna siku hali itakuwa sawa tena. Pia mdogo wangu Zita, alinifanya nijitie nguvu na kuvumilia lolote ambalo ningefanyiwa. Bibi hakuwa na msaada kabisa kwa mateso yangu zaidi ya kunitia moyo, ukiacha hiyo mara moja nilipoumwa, kwani kila alipojaribu kunitetea nayeye aliishia kufokewa, “Nyamaza mama.” Ilifika mahala nilizoea kuwa mule ndani mimi, bibi na Zita sote ni kama watoto tusioweza kujitetea kwa lolote.



    Siku nyingine niliyoumia sana ni siku ambayo na bibi yangu pia alifariki, lakini kilichoniumiza sana ni kukosa msaada dakika kadhaa kabla ya kufariki. Baba mdogo na mke wake, dada Selina, walitoka jioni, na bamdogo Naise hakuwa ameshinda nyumbani siku nzima. Bibi akaanza kuumwa miguu huku akilia sana, mpaka anazimia, nikijaribu kumsaidia bila kujua cha kufanya. Kufika wakati wakubwa wanarudi, hali yake ilikuwa mbaya sana, kiasi kwamba nadhani hata hospitali hakufika. Alifariki bibi yangu, nikaanza kusemwa sana na bamdogo Naise kuwa nina laana, kwanini baba, mama na bibi, wote wafe mbele yangu. Hapo ndipo maisha yaligeuka na kuwa machungu zaidi ya shubiri. Niliishi miaka mitano ya lawama, kazi zilizonizidi umri, chuki na mateso ya kila namna bila faraja yoyote. Siku zilivyoendelea, mdogo wangu akili yake ilianza kukomaa, hivyo tukawa tukisaidiana kazi za ndani na kuzungumza hivyo kidogo nikaanza kupata faraja.



    Siku moja usiku, nikiwa na miaka 14, baba mdogo Musa na dada Selina wakiwa wametoka, alikuja bamdogo Naise akiwa amelewa, ingawa si sana. Alianza kunisema kuwa nina laana na hivyo anatakiwa anitoe laana. Alianza kunivua nguo na kunitaka kimapenzi, wakati huo tumekaa chumbani mimi na Zita. Nililia sana, nikimuomba anihurumie, lakini aliniambia nichague aidha amuue mdogo wangu mbele yangu au afanye mapenzi na mimi kwani ni lazima nitoe bikira yangu kwake ili kutoa laana. Aliahidi nisipokubali, angemfanyia hicho kitendo mdogo wangu, na kwa umri wake mdogo, angefanya hivyo mpaka mtoto angekufa. Aliponiambia nichague, ilibidi nikubali ili amuache mdogo wangu. Nililia mno, nikipiga kelele na kuomboleza, akanishika kinywa, akanifunga na nguo. Alimfunga Zita pia ili asipige kelele kisha alianza kunibaka mbele ya Zita. Niliumia, sana, nikalia machozi lakini hakujali hilo. Alipomaliza aliondoka na sikujua alienda wapi kwani hakurudi tena mpaka nimeondoka pale.





    Ilikuwa ni kawaida bamdogo Musa na mkewe wakirudi hupitiliza moja kwa moja chumbani, sisi tukiwa tumelala tayari, kwani walikuwa na funguo yao. Nilibaki nalia mpaka wanafika, Zita wakati huo amelia mpaka akapitiwa usingizi. Walifika na kuingia chumbani kwao kulala. Nilitamani ningewambia kuhusu tukio alilofanya bamdogo Naise, lakini sikupata huo ujasiri, nilijua hata ningesema ningeishia kugombezwa tu na wala nisingesaidiwa. Ni kweli, ndivyo ilivyokuwa kwani kesho yake kwa ajili ya kulia sana, nilichelewa kuamka, akaja dada Selina chumbani na kuniamsha kwa maji kama kawaida. Nilipoamka, aliona macho yangu yamevimba sana, na ya mdogo wangu pia, akaanza kutuhoji, nikajieleza huku nalia.



    Dada Selina alikaa kimya kama dakika nzima huku akionesha kama hali ya kustuka na huruma kiasi, lakini aliinuka na kwenda chumbani kwao, akamwambia mumewe nadhani, kwani muda mfupi baadaye alikuja bamdogo Musa wakaanza kututukana kuwa tumejilengesha kwa bamdogo Naise halafu tunasingizia kubakwa. Hapo ndipo niliona nyumba ile hainifai tena, nikakusudia kutoroka. Niliwaza ni nini hasa kinanikalisha, kwani hata chakula wakati mwingine tunakosa. Niliamua nitatoroka, nimchukue Zita pia, tukatafute kazi kokote ya kutupatia chakula. Nadhani walihisi kuwa ningetoroka na pengine kumshitaki bamdogo Naise polisi kwani wiki hiyo nzima ni kama dada Selina alibaki akituchunga. Hakuondoka kwenda popote tofauti na kawaida yake. Sikutumwa kwenda dukani kama nilivyozoea awali, lakini pia bamdogo Naise hakurudi tena. Bamdogo Musa akawa akinilaumu kwamba nimemfanya mdogo wake atoroke kwa kumsingizia ametubaka.



    Wiki iliyofuata ni kama walianza kuzoea, na kunituma dukani tena. Baadaye wakasahau kabisa na kuondoka tena wakati wa jioni. Nakumbuka ilikuwa siku ya Jumamosi, zimepita wiki tatu kamili tangu nibakwe, walitoka mida ya saa moja usiku, nadhani walienda kwenye sherehe ya harusi. Wakati huo nilishamuandaa Zita siku nyingi kuwa kuna siku tutaondoka hapo nyumbani na kumuonya asiseme. Walipoondoka tu, niliweka nguo zetu kwenye mfuko wa kiroba tulichoweka nguo, na kila kitu, tukala chakula chetu kwa haraka, tukaondoka mida ya saa mbili usiku. Kabla ya kuondoka nilijaribu kuangalia kama naweza kupata pesa kidogo chumbani kwa bamdogo, nikaingia na kupekua maeneo kadhaa nikabahatisha kuona kibunda cha pesa, laki mbili zimefungwa pamoja. Sikuchukua nusu wala sikuwaza kuwa nitaitwa mwizi, nilibeba na kuondoka nazo bila kuhesabu, nikaja kuhesabu kesho yake tukiwa safarini. Sikujua wapi tunaelekea usiku huo, lakini nilikusudia kutoka pale nyumbani na kutorudi kamwe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku hiyo tulilala mtaani, mbali kabisa na eneo la nyumbani, sehemu moja Arusha inaitwa Mbauda. Ili kuwa salama, niliona baada ya kuondoka tupande daladala na kuelekea popote, hivyo tukaenda Mbauda, tukatafuta sehemu moja nje ya duka, tukalala. Kama unavyojua Arusha, baridi ni kali mno. Lakini kati ya nguo chache nilizobeba, nilibeba za kujikinga na baridi zaidi, hasa kwa ajili ya mdogo wangu. Zita alilia mara kadhaa, lakini nilimfariji kuwa tunaachana kabisa na mateso ya kwa bamdogo. Tulilala hapo lakini usiku wazo lilinijia la kuondoka Arusha kabisa hivyo alfajiri sana nikamuamsha Zita, tukaanza kufanya mpango wa tiketi ya kwenda Dar es Salaam. Nilifanya hivi kwani nilishawahi kusikia kuwa Dar es Salaam kuna kazi nyingi, pia nilitaka nihakikishe kuwa hata nikitafutwa sitapatikana. Tulisafiri na kufika Dar, siku hiyo hiyo jioni.



    Nimeishi maisha machungu, ya mateso mno Dar es Salaam. nimetafuta kazi mara kadhaa, bila mafanikio. Kuna wakati nilipata kazi za ndani, lakini walinikataa kukaa na mdogo wangu. Baada ya miezi minne ya kulala mtaani, nilifanikiwa kupata kazi ya kuuza baa. Kazi hiyo ilianza vizuri kwani ilitupatia chakula na sehemu ya kulala, ingawa chumba kimoja tulilala wasichana wanne wafanyakazi, pamoja na Zita. Sikujali ni wapi tunalala, ila kulala ndani ya chumba kwangu ilikuwa ni ahueni kubwa. Miezi minne mizima ya kulala mtaani, kuomba omba na kuokota vyakula ilinifanya nitamani kazi yoyote. Kama hujawahi kuishi mtaani unaweza ukawa na ujasiri wa kutukana kila unayemuona akiomba omba. Yale maisha ni magumu asikwambie mtu. Watu wanakuona kama mbwa koko, asiyestahili hata kuongeleshwa na watu, wala hata kuangaliwa akivuka barabara ili asigongwe na gari.



    Mara kadhaa tulinusurika kubakwa, tena na wengine watu wenye akili zao kabisa. Kuna wakati ilitubidi kuhama eneo la kulala kwa kulinda usalama wetu, kwani ilitokea uvamizi wa usiku na hivyo kutafuta eneo salama zaidi. Zita alikuwa akilia lakini baadae alizoea kuwa haya ndio maisha. Niliumia sana siku aliyoomba turudi kwa bamdogo, Arusha. Kwangu kuishi mtaani na mateso yale ilikuwa ni sawa kabisa na kuisi kwa baba mdogo Musa, lakini tofauti yake ni kwamba huku mtaani nilikuwa na matumaini kwamba kuna siku ningepata kazi na maisha yakawa mazuri. Kwa bamdogo niliishi bila tumaini la kwamba siku moja nitakuwa huru, au maisha yatabadilika.

    Nilipopata kazi, nilianza kuona nafuu ya maisha, lakini tofauti na matarajio yangu, wanaume wengi walianza kunitaka kimapenzi.



    Kusema kweli kazi ni kazi lakini kazi ya baa ina changamoto kubwa mno. Nilikataa wanaume mara kadhaa, nikaitwa na meneja na kuonywa kuwa siwatendei haki wateja wake, huku akiahidi nikiendelea na tabia hiyo, nitafukuzwa. Nakumbuka mara ya kwanza nilikubali kuondoka na mwanaume mmoja, ananizidi zaidi ya miaka 25 nafikiri. Tulipofika nyumba ya wageni, nilianza kulia sana huku nikimuomba anisamehe. Akilini nilikumbuka maumivu niliyopata siku bamdogo Naise ananibaka, sikutamani yajirudie. Nililia sana, kiasi cha kumfanya anionee huruma na kuamua kuniacha. Aliondoka hapo bila kunirudisha kazini, ikabidi niondoke usiku huo, nikiulizia ulizia mpaka nikafika kazini ambapo ndipo tulilala pia.



    Meneja aliposikia aliniita na kunisema sana, akasema lile jambo likijirudia tena atanifukuza kazi. Tatizo la kazi ya baa, hauna muda kabisa wa kufanya kitu kingine chochote wala kutafuta kazi nyingine. Kuna wakati nilijaribu kuongea na wateja niliowaona wastaarabu, kuhusu kufanya kazi nyumbani kwao. Wengine walinitukana, wakidai kuajiri muuza baa ni kuleta Malaya nyumbani kwako. Wengine walinishitaki kwa meneja, nikagombezwa au kutandikwa vibao, wengine walinikubalia lakini wakaanza kuonesha kunitaka kimapenzi. Nilijitahidi kuongea zaidi na wateja wa kike, lakini unajua baa wateja wengi ni wa kiume ndio huja pekeyao, na kuongea na mtu akiwa na mume wake pembeni mara nyingi ilinifanya niambulie matusi tu.



    Siku moja kuna mwanaume, aliyeonekana mstarabu sana, niliongea naye, akanikubalia na kesho yake alikuja saa moja jioni na kunipeleka kwake. Niliamua nitaondoka kwanza mimi halafu nikihakikisha mazingira yanafaa ndipo nimchukue Zita wangu. Niliongea na Zita, akanielewa, nikaenda na yule mwanaume. Niliamini alishaongea na mke wake kuhusu kuniajiri, lakini cha ajabu nilipofika tu, mke wake baada ya kutambulisha aliingia jikoni na kutoka na maji ya moto, akanimwagia miguuni. “Hiki ndicho ninachowafanya mabinti wadogo wanaofakamia ndoa za watu,” alisema, huku akimwaga maji hayo. Nilitoka mbio sana nje, nikilia, nikaacha wakigombana na mume wake, nikaanza kukimbia. Sikuweza kukimbia kwa mwendo mrefu kwani maumivu makali yalianza na kunifanya nishindwe kutembea. Kwa bahati sana yule baba alikuja na kunikuta njiani nikiugulia maumivu, akanipeleka hospitali kwa gari yake, akaacha amenilipia bili yote na kunipa kiasi cha pesa huku akiniomba msamaha. Nililala hospitali, nikimuwaza mdogo wangu sana, kwani sikumzoesha kujitegemea.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku mbili baadaye, nilipata nafuu na kutoka hospitalini hapo, ingawa walishauri nikae zaidi lakini pesa niliyolipiwa ilikuwa imeisha na sikuwa tayari kuongeza. Niliondoka na kurudi kule baa, lakini Zita wangu sikumkuta. Wafanyakazi wenzangu walisema alienda kunitafuta alipoona sirudi. Kama sikuchanganyikiwa siku hiyo, sitachanganyikiwa tena. Nililia mno, nikawaza kujiua lakini nikajiuliza endapo Zita atarudi kunitafuta aambiwe nimekufa, atafanyaje. Niliwalaumu wafanyakazi wenzangu kwanini wamemruhusu aondoke, wakajitetea tu, lakini sikuona aliyeongea la maana. Niliondoka hapo kama kichaa, kuanza kuzunguka mtaani, nikimtafuta mdogo wangu, bila mafanikio. Niliacha maagizo kule baa kwamba ikitokea akarudi wasimruhusu aondoke mpaka nirudi. Nikawa kila ikifika jioni, narudi pale kuulizia, ingawa sikuruhusiwa tena kulala pale, isipokuwa kwa uficho.



    Wiki mbili zilipita bila kumpata mdogo wangu, nikakonda sana kwa kushindwa kula na kuwa na mawazo. Huyu mtoto kwangu alikuwa ni zaidi ya mdogo, bali kama rafiki wa karibu zaidi, ndugu pekee na kama mtoto wangu wa kumzaa. Nilijihisi nawajibika mno kwa maisha yake. Nilijilaumu kumuacha hata kwa siku moja, lakini nilijipa moyo kuwa kama kuna Mungu duniani, basi sitampoteza mdogo wangu. Nilianza kusali, sala fupi kabisa, “Mungu kama upo, na kama unasikiliza wanadamu, naomba umlinde Zita huko aliko, na unisaidie kumpata.” Nilifanya hivyo kila siku zaidi ya mara tano. Nililia kila nilipomfikiria Zita, huku nikiwa na tumaini dogo sana kwamba kwa kuwa hajafa basi huenda nikampata.



    Kuna wakati nilipata mawazo kwamba pengine atagongwa na gari au kupata chochote, lakini nilipingana sana na mawazo hayo mara zote. Uzoefu wangu wa misiba umenifundisha kuwa kufiwa hakuna mazoea. Siku aliyokufa baba, niliumia kana kwamba sina mtu mwingine yeyote duniani. Lakini siku aliyokufa mama, niliumia utadhani sijawahi kufiwa, ni mara ya kwanza. Siku aliyokufa bibi pia niliumia kama mtu aliyepoteza tumaini la maisha kabisa. Kufiwa na ndugu pekee aliyebaki kwenye maisha yangu, Zita, kungepoteza ladha na maana ya kuishi kabisa, na nadhani ningechukua uamuzi wa kujiua siku iyo hiyo.



    Baada ya wiki mbili, nakumbuka siku moja nilienda pale baa nilipofanya kazi awali, wakasema hajarudi, nikawa nimekata tamaa kabisa kama atakuja. Nikaanza kuondoka, sijui la kufanya tena, nalia machozi yasiyokauka. Nikiwa njiani, likasimama gari moja, aina ya harrier nyeusi nzuri sana. Alipofungua kioo ambacho kilikuwa tinted, mwanaume mmoja wa miaka kama 35 au zaidi kidogo, aliniuliza habari, nikamjibu na kumuamkia. Akaniuliza nalia nini, sikumjibu bali nikazidi kulia. Yule kaka alishuka kwenye gari, akaanza kunibembeleza, akaniomba sana niende naye kwake, atanisaidia. Kusema kweli nilikuwa na hofu kubwa mno, kuondoka na mtu nisiyemjua, lakini kwa jinsi nilivyokuwa nimejikinai, nilikubali. Nilijisemea moyoni, “Siku zote nayatunza maisha yangu kwa kutokubali kila kitu, lakini hamna faida, kwani sasa hata ndugu yangu pekee nimeshampoteza.”



    Nilipanda kwenye gari yake, iliyokuwa na video ndani, imewekwa video ya wimbo fulani ambao ulinikumbusha sana maisha ya nyuma. Wimbo huo uliimbwa na kundi moja la nchi ya Marekani nadhani, wa kingereza, uliitwa LOVE OF MY PAPA, OF MY MAMA, ikimaanisha upendo wa baba yangu, wa mama yangu. Huo wimbo ulirekodiwa kama muvi ya binti mdogo aliyeishi na wazazi wake vizuri sana, lakini wakafariki kwa ajali ya gari siku moja, kisha akaanza kuhangaika mtaani. Alionekana akiomba chakula mtaani, akinyeshewa mvua na kupigwa baridi. Nilishangaa mno kukuta wimbo wa maisha yangu. Nilikuwa nimenyamaza wakati naingia kwenye gari, lakini nikiangalia huo wimbo na video yake, nilianza kulia sana kama mtu aliyepigwa kiasi cha yule kaka kushindwa kuendesha gari. Alipaki pembeni haraka na kuanza kuniuliza nalia nini, nikamwambia kuna vitu nimekumbuka hivyo asinijali.



    Tuliendelea na na safari ya mwendo mrefu kidogo, tukakutana na foleni baadhi ya maeneo, baadaye tukafika kwake. Yeye alijitambulisha kwa jina la Bahati, namimi nikamwambia jina langu, Zawadi. Mlinzi alifungua geti, nyumba kubwa na nzuri sana, maeneo ya Salasala jijini Dar es Salaam, tukaingia ndani. Mida hiyo ilikuwa kama saa mbili usiku. Alikuja dada wa kazi, akatusalimia. Kaka Bahati baada tu ya kumjibu akamuulizia, “Yuko wapi mtoto?” “Yuko ndani, ametoka kuoga” Yule dada alijibu. Nilisubiri aulize habari za mke wake, nilisubiri pia nione jinsi mke wake ambavyo angehamaki baada ya kuniona, kwani bado nilikumbuka kwa ufasaha kabisa tukio alilofanya yule mama aliyeniunguza miguu. Nikazidi kuwaza jinsi alivyonisababisha kumpoteza mdogo wangu, nikaanza tena kulia, huku nikijipanga kwa lolote litakalotokea siku hiyo. Yule kaka, Bahati, alinituliza kidogo, akanialika mezani nikale. Muda wote huo sikuwa nimemueleza chochote kuhusu mimi zaidi ya jina langu na wala hakuonesha kuwa na haraka. Tulikaa mezani, akamwambia dada aende kumuhimiza mtoto aje kula.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa mara ya kwanza baada ya miaka, mbele yangu kulikuwa na chakula ambacho sijawahi kula tangu baba yangu afariki, yaani kuku. Siku zote tukiwa kwa baba mdogo, siku ambazo walipika kuku au nyama, walikula wao tu huku kila kinachobaki kikipelekwa chumbani na kufungiwa kwenye friji yao. Wakati bibi yupo, angalau tulikula nyama mara chache, kwani bibi alipikiwa ndizi zenye nyama au utumbo kila siku, na walipompakulia, alilazimisha na sisi tupakuliwe chakula chake. Baada ya bibi kufariki, sikuwahi tena kula nyama. Nakumbuka kuna siku nilikuwa napika, nikatamani sana nyama walau moja nionje, lakini dada Selina alikuja na kunikuta nikiwa na nyama mdomoni, akanipiga kiasi cha kutothubutu tena siku nyingine. Siku tulizopika nyama au kuku, haikutokea hata siku moja tukaachwa nazo mimi na Zita, kana kwamba ni dawa, haifai kwa watoto. Chakula chetu kikubwa kilikuwa ugali, na maharage au mchicha, na mara chache sana wali. Nilizoea kuwa hayo ndiyo maisha na kwangu haikunisumbua hata kidogo. Kama hiyo ndiyo ingekuwa changamoto pekee, basi nisingewahi kuondoka kwa bamdogo Musa.



    Ghafla, nikiwa napakua, alitokea binti mdogo, akasimama mezani tulipokuwa tumekaa kula. Nikasikia kaka Bahati akimhimiza akae ale, kwani alichukua kama dakika nzima amesimama, anashangaa. Nikamuangalia yule binti mdogo kwa makini sana kama mtu ambaye ninaota au nimeona mzimu. Sikuamini, akili haikukubali, nikasema hii ni ndoto nzuri tu naota lakini si kweli. Tukabaki tumeshangaana na mtoto yule sote tukiwa kama tumeona mizuka. Nikajua kuwa Mungu hutuma malaika zake kulinda wapendwa wetu na kujibu maombi yetu. Zita wangu hakuwa yule niliyeachana naye baa siku ile. Hakuwa mchafu, aliyevaa nguo moja kwa zaidi ya wiki. Hakuwa na nywele ndefu zisizochanwa. Hakuwa na harufu ya uchafu kama mimi, bali alisukwa nywele nzuri za uzi zenye shanga, amevaa nguo nzuri ya kulalia na ananukia mafuta mazuri sana. Nilisukuma sahani, nikainuka na kumkumbatia huku nikilia na kumuangalia mara mbilimbili kuhakikisha kwamba ni yeye. Tulikumbatana kama dakika tano nzima, kila mmoja wetu akionesha hisia zake kwa machozi, kaka Bahati akiwa ametuangalia tu.



    Baadaye tulikaa mezani, siwezi kusema furaha niliyokuwa nayo ni kubwa kiasi gani. Nilianza kumuhadithia kaka Bahati maisha yetu, kwa kirefu kabisa, lakini baada ya kunielezea alimpata wapi Zita. Kumbe siku ile alipoondoka pale baa kwenda kunitafuta, nayeye alitembea huku akilia sana kama mtu aliyefiwa, baada ya kutafuta masaa kadhaa bila kuniona. Nilitamani kumlaumu Zita kwa kuchukua uamuzi wa kwenda kunitafuta, lakini kwa mtoto wa miaka nane, nadhani akili yake bado haikuweza kufikiri bora zaidi ya hapo. Bahati alimkuta nje ya hoteli aliyokuwa akila chakula, mvua ikimyeshea, mida ya saa nane na nusu mchana.



    Nilianza kujiuliza maswali kadhaa, ambayo japokuwa kaka Bahati alijaribu kuyajibu, lakini bado sikuelewa kwanini ni mtu mwema kiasi hiki. Sikuwahi kukutana na mtu mwema, asiye na hila ndani yake, anayetendea wema hata watu asiowajua. Kwake, machozi ya mtoto au binti mdogo yalimuumiza sana. Nilikuja kuelewa ni kwanini baada ya kuishi naye miezi kadhaa, na kujua historia yake. Nikagundua si mimi pekeyangu niliyeumizwa na dunia.



    Kaka Bahati hakuwa na mke, wala mtoto. Kabla yangu na Zita, aliwahi kuchukua binti mwingine kulea, akawa akimsomesha shule ya bweni, hivyo hatukumkuta kwake. Alimtafutia shule Zita pia, changamoto ikawa kwangu kwani umri wangu ulikuwa mkubwa kidogo na niliishia darasa la tatu tu. Alinitafutia shule nzuri pia, akanitafutia na walimu wa tuisheni wanisaidie kunifundisha. Tulianza maisha mapya mimi na mdogo wangu, kwa kaka Bahati, ambaye alitupenda na kutujali kama watoto wake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Niliifahamu historia ya kaka Bahati baada ya kuishi naye miezi kadhaa, kwani hakuwa anazungumzia kila kitu mara moja. Yeye alizaliwa kama mtoto wa mwisho kati ya watoto watano kwa baba na mama yake. Waliishi maisha mazuri mno, ya kifahari, baada ya baba yake kuanza kufanya biashara za madini zikakubali. Baba yake hakusoma, wala mama yake, lakini alianza kama kutafuta vibarua kwenye migodi, akawa akipata pesa ndogo sana ya kujikimu.



    “Nikiwa mdogo sana, maisha yalikuwa ya shida mno, kiasi cha watoto kukosa chakula. Lakini baba alikuwa mpiganaji asiyechoka. Alikuja kufanikiwa kupata kama mchongo katika madini, ukampatia pesa nyingi mno, akafungua duka lake la kuuza vito vya thamani. Kwahiyo ni kati ya maduka ya sonara ya mwanzo kabisa, kabla biashara haijaenea sana. Biashara ile ilibadili maisha yetu ghafla sana, tukaanza kuishi kifahari, kwenda mpaka nchi za nje miaka hiyo na kusafiri safari za ndani kila mara. Baba yangu hakuwa mchoyo, alisaidia watu wengi sana. Kuna watoto wa ndugu zangu wengi baba aliwasomesha.



    Sitasahau siku ambayo tulipata ajali kama familia, miaka ya themanini. Wewe haukuwa umezaliwa wakati huo, lakini ni ajali iliyotangazwa kwenye vyombo vya habari nchini kuwa familia ya tajiri mkubwa yapata ajali maeneo ya mikumi na kuua karibu wanafamilia wote. Mimi, na kaka yangu wa kwanza ndio tulinusurika, lakini kaka aliumia vibaya na mpaka sasa ni mlemavu wa miguu yote. Baba, mama na ndugu zangu wengine wote walifariki, ambao hao ndugu zangu wote walikuwa wa kike.



    Katika familia, unajua kuna ndugu unakuwa karibu nao kuliko wengine. Sasa mimi, dada zangu nilikuwa karibu nao sana kuliko huyo kaka yangu. Kaka alikuwa mkali kidogo kwangu, tofauti na dada zangu ambao walinidekeza na kunitetea mara zote. Kusema kweli, katika akili yangu ya utoto, kipindi cha msiba, nilitamani kama walau dada mmoja angebaki, wabadilishane na kaka yangu. Sikuwa mdogo kiasi cha kutoelewa kinachoendelea wakati wa msiba, nilijua kabisa nimepoteza wazazi, na familia yote, nikajua maisha yatabadilika, lakini sikutegemea yangebadilika kiasi kile. Huwezi amini, hata matibabu ya kaka ilifika mahala yakawa shida utadhani sio mtoto wa tajiri mkubwa. Ama kweli, aliyekufa hana thamani tena,” Aliongea kaka Bahati, nikaona kama machozi yakimlenga. Kwa siku hiyo akaishia hapo, hakuendelea tena kuzungumzia mambo ya familia yake.



    Maisha niliyoishi na baba mdogo pamoja na maisha ya mtaani yalinifanya niwe muoga na mtu nisiyezoea watu kwa upesi. Lakini tulipoishi na kaka Bahati, taratibu nilianza kubadilika. Alituchukua kutupeleka chakula cha jioni, au kuogelea, alitutambulisha kwa marafiki zake ambao wengine walimcheka na kumwambia kwamba anakoelekea ataanzisha kituo cha kulelea yatima. Lakini nikabaki na maswali mawili kichwani ambayo bado sikuwa na ujasiri kumuuliza, hasa swali kuhusu kuoa. Nilijiuliza, kwanini kaka Bahati hana mke, na pili kwanini hatujawahi kuwaona ndugu zake. Ila pia nikakumbuka kwenye historia yake alisema ilifika mahala hadi matibabu ya kaka yake yalikuwa shida, kana kwamba hakuwa mtoto wa tajiri. Akilini nikahisi pengine ndugu walichukua mali zote na kuwaacha bila kuwajali.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ni kweli kabisa, siku nyingine Bahati alipoanza kunieleza kuhusu historia ya maisha yake, niligundua ndugu wengi wana roho mbaya kama baba zangu wadogo.



    “Tukiwa kwenye msiba, kaka hakuweza kuja kuzika kwani hali yake ilikuwa mbaya sana hospitali. Walijitokeza ndugu ambao hata mimi sijawahi kuwaona au wengine wa mbali kabisa kijijini, na kuanza kuzungumzia habari ya mali. Kila kitu kwangu niliona ni kigeni mno, hivyo sikuwa na cha kusema wala cha kufanya. Cha ajabu watu walionekana kugombania mali mpaka kubishana ila ilipokuja kwenye suala la sisi nani atatulea, walianza kupigiana danadana. Mwisho iliamriwa kuwa tutaishi kwa baba yetu mkubwa aliyeishi Manyara, kabla haujawa mkoa, tena kijijini. Nakumbuka kuna mtoto wake ambaye baba alikuwa akimsomesha shule moja ya bweni, Arusha, na kijana huyo aliendelea kusoma mpaka akamaliza kidato cha nne, akafeli na kushindwa kuendelea. Lakini kwangu mimi ilikuwa mwisho wa masomo yangu.



    Niliandikishwa shule huko kijijini ila hata nguo za shule, au viatu sikununuliwa zaidi ya nilivyokuwa navyo. Kaka yangu alipopata nafuu naye aliletwa kule Manyara, lakini alitakiwa kuendelea na matibabu kwa muda. Mara kwa mara vikao vya ndugu vilikaliwa, na kilichozungumziwa ni mali tu na sio malezi, elimu wala afya ya kaka yangu. Kuna siku kaka mwenyewe alijaribu kuuliza kwenye kikao kuhusu afya yake, wakamjibu kwa aibu kwamba kuna pesa zinafuatiliwa, zikipatikana ataenda kutibiwa. Waliishia kumpeleka vituo vya afya vidogo tu pale Manyara kwa muda wa miezi kadhaa kisha wakamtelekeza. Nimemuhudumia kaka mpaka amekuwa mtu mzima wa kuweza kujitegemea. Nashukuru badae kabisa aliweza kuishi kwa kujitegemea, ingawa akiwa na ulemavu wa miguu. Kwa sasa ameoa, ana mtoto mmoja, na huyo ndiye ninamsomesha shule ya wasichana ya Marian.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kila nilipomsikiliza kaka Bahati akiongea, hasira zilinishika, nikazidi kuwachukia ndugu wanaoachiwa watoto na marehemu. Nilikumbuka jinsi baba mdogo alivyoonekana kutupenda baba akiwa hai, na namna alivyotubadilikia baada ya msiba. Nafsini mwangu nilitamani nilipe kisasi, si kwa ajili yangu tu, bali kwa ajili ya yatima wote wanaoteswa na ndugu wa wazazi wao. Kaka Bahati amekuwa akinielezea kuhusu maisha yake kwa vipengele, mara nyingi baada ya kula usiku. Zita hulala mapema kidogo, ila mimi napenda kukaa sebuleni baada ya chakula. Licha ya kuzungumzia maisha na historia za nyuma, najifunza mambo mengi sana kwa kuongea na kaka Bahati.



    Kwake nimejifunza kupambana na maisha, kuwa mvumilivu, kuthamini watu, kutia bidii katika ,mambo yote na zaidi kusamehe. Nilivyoendelea kuishi naye niligundua kuwa natakiwa kusamehe wote waliowahi kuniumiza katika maisha yangu. Liliokuwa gumu zaidi ni kumsamehe bamdogo Naise, kwani kitendo alichofanya sio tu kiliniumiza, bali pia kiliacha alama mbaya kwenye maisha yangu. Nilimuhadithia kaka Bahati vitu vingi, lakini sikumwambia kuhusu kubakwa kwangu, kwani niliona aibu, mpaka siku moja yeye aliponiambia alifanyiwa jambo baya zaidi ya mimi kubakwa.



    “Tukiendelea kuishi kijijini, baba mkubwa alianza kuwa na maisha bora zaidi, nikajua ni mali za wazazi wangu. Kwa mtu wa kijijini, tena miaka hiyo, kununua gari, haikuwa jambo dogo kabisa. Alinunua gari, alianza kulimisha mashamba yake kwa kukodisha vijana wengi ambao baada ya kulima walikuja kula nyumbani. Aliajiri watu wa kupika na ni kama kila siku ilikuwa sherehe. Watoto wa bamkubwa wote walisoma bila shida, na kupatiwa mahitaji yote, isipokuwa mimi na kaka ambao hatukuonekana kama watoto wanaohitaji kuhudumiwa. Mahitaji yetu yote yalipuunzwa, kuanzia elimu mpaka mavazi. Muda ulivyoendelea ndipo tulizidi kuonekana kama watu waliovamia familia za watu, na hivyo tuliishi kama watumwa kabisa.



    Niliachishwa shule na kuanza kuchunga mifugo ya bamkubwa huku nikiendelea kumuhudumia kaka yangu, aliyekuwa hawezi hata kunyanyuka bila msaada wa mtu. Kaka yangu ameishi kwa shida mno, kiasi kwamba kuna wakati alitamani ajiue, akidai kuwa ananitesa na yeye akiteseka. Kwangu uwepo wake ulikuwa ni faraja kubwa mno, na hata siku moja sikuwahi kuona ni mateso kumuhudumia.



    Siku moja, nilienda kuchunga alfajiri sana kama nilivyozoeshwa. Kuna wakati nilikuwa na vijana wenzangu wakichunga mifugo yao, lakini mara nyingi walianza kuchunga jua limeshachomoza. Mwamzoni niliogopa sana, kwani mazingira ya kule yalinitisha, lakini baadaye nilizoea. Siku hiyo, nikitembea maeneo ambayo hayakuwa mbali sana na nyumbani, nasubiria kuwe na mwanga kidogo ndipo niende mbali, alitokea mwanaume mmoja, tena niliyemfahamu kama rafiki wa baba mkubwa, akaanza kuniuliza maswali kadhaa. Mwanaume huyu alionekana amelala kwenye pombe, kwani kule kijijini hiyo tabia haikuwa ya ajabu. Aliniuliza maswali kadha wa kadha, yasiyo na mbele wala nyuma, kisha akanishika mkono na kuanza kunivutia porini. Nilipiga kelele nyingi sana, nikiamini nitasikiwa. Kaka yangu anasema alisikia hizo kelele, akahisi ni mimi, lakini hakuwa na cha kufanya zaidi ya kupata hofu tu na kusubiri taarifa. Yeye alihisi pengine nimeliwa na mnyama mkali. Yule mwanaume alinichukua na kuanza kuniingia kinyume na maumbile huku akidai ananifundisha maisha. Nililia mno, nikapiga kelele, akiniziba mdomo na kuendelea na kile kitendo, halafu akaniacha hapo na kuondoka.”



    Kaka Bahati hakuwa na mke, wala mtoto. Kabla yangu na Zita, aliwahi kuchukua binti mwingine kulea, akawa akimsomesha shule ya bweni, hivyo hatukumkuta kwake. Alimtafutia shule Zita pia, changamoto ikawa kwangu kwani umri wangu ulikuwa mkubwa kidogo na niliishia darasa la tatu tu. Alinitafutia shule nzuri pia, akanitafutia na walimu wa tuisheni wanisaidie kunifundisha. Tulianza maisha mapya mimi na mdogo wangu, kwa kaka Bahati, ambaye alitupenda na kutujali kama watoto wake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Niliifahamu historia ya kaka Bahati baada ya kuishi naye miezi kadhaa, kwani hakuwa anazungumzia kila kitu mara moja. Yeye alizaliwa kama mtoto wa mwisho kati ya watoto watano kwa baba na mama yake. Waliishi maisha mazuri mno, ya kifahari, baada ya baba yake kuanza kufanya biashara za madini zikakubali. Baba yake hakusoma, wala mama yake, lakini alianza kama kutafuta vibarua kwenye migodi, akawa akipata pesa ndogo sana ya kujikimu.



    “Nikiwa mdogo sana, maisha yalikuwa ya shida mno, kiasi cha watoto kukosa chakula. Lakini baba alikuwa mpiganaji asiyechoka. Alikuja kufanikiwa kupata kama mchongo katika madini, ukampatia pesa nyingi mno, akafungua duka lake la kuuza vito vya thamani. Kwahiyo ni kati ya maduka ya sonara ya mwanzo kabisa, kabla biashara haijaenea sana. Biashara ile ilibadili maisha yetu ghafla sana, tukaanza kuishi kifahari, kwenda mpaka nchi za nje miaka hiyo na kusafiri safari za ndani kila mara. Baba yangu hakuwa mchoyo, alisaidia watu wengi sana. Kuna watoto wa ndugu zangu wengi baba aliwasomesha.



    Sitasahau siku ambayo tulipata ajali kama familia, miaka ya themanini. Wewe haukuwa umezaliwa wakati huo, lakini ni ajali iliyotangazwa kwenye vyombo vya habari nchini kuwa familia ya tajiri mkubwa yapata ajali maeneo ya mikumi na kuua karibu wanafamilia wote. Mimi, na kaka yangu wa kwanza ndio tulinusurika, lakini kaka aliumia vibaya na mpaka sasa ni mlemavu wa miguu yote. Baba, mama na ndugu zangu wengine wote walifariki, ambao hao ndugu zangu wote walikuwa wa kike.



    Katika familia, unajua kuna ndugu unakuwa karibu nao kuliko wengine. Sasa mimi, dada zangu nilikuwa karibu nao sana kuliko huyo kaka yangu. Kaka alikuwa mkali kidogo kwangu, tofauti na dada zangu ambao walinidekeza na kunitetea mara zote. Kusema kweli, katika akili yangu ya utoto, kipindi cha msiba, nilitamani kama walau dada mmoja angebaki, wabadilishane na kaka yangu. Sikuwa mdogo kiasi cha kutoelewa kinachoendelea wakati wa msiba, nilijua kabisa nimepoteza wazazi, na familia yote, nikajua maisha yatabadilika, lakini sikutegemea yangebadilika kiasi kile. Huwezi amini, hata matibabu ya kaka ilifika mahala yakawa shida utadhani sio mtoto wa tajiri mkubwa. Ama kweli, aliyekufa hana thamani tena,” Aliongea kaka Bahati, nikaona kama machozi yakimlenga. Kwa siku hiyo akaishia hapo, hakuendelea tena kuzungumzia mambo ya familia yake.



    Maisha niliyoishi na baba mdogo pamoja na maisha ya mtaani yalinifanya niwe muoga na mtu nisiyezoea watu kwa upesi. Lakini tulipoishi na kaka Bahati, taratibu nilianza kubadilika. Alituchukua kutupeleka chakula cha jioni, au kuogelea, alitutambulisha kwa marafiki zake ambao wengine walimcheka na kumwambia kwamba anakoelekea ataanzisha kituo cha kulelea yatima. Lakini nikabaki na maswali mawili kichwani ambayo bado sikuwa na ujasiri kumuuliza, hasa swali kuhusu kuoa. Nilijiuliza, kwanini kaka Bahati hana mke, na pili kwanini hatujawahi kuwaona ndugu zake. Ila pia nikakumbuka kwenye historia yake alisema ilifika mahala hadi matibabu ya kaka yake yalikuwa shida, kana kwamba hakuwa mtoto wa tajiri. Akilini nikahisi pengine ndugu walichukua mali zote na kuwaacha bila kuwajali.



    Ni kweli kabisa, siku nyingine Bahati alipoanza kunieleza kuhusu historia ya maisha yake, niligundua ndugu wengi wana roho mbaya kama baba zangu wadogo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Tukiwa kwenye msiba, kaka hakuweza kuja kuzika kwani hali yake ilikuwa mbaya sana hospitali. Walijitokeza ndugu ambao hata mimi sijawahi kuwaona au wengine wa mbali kabisa kijijini, na kuanza kuzungumzia habari ya mali. Kila kitu kwangu niliona ni kigeni mno, hivyo sikuwa na cha kusema wala cha kufanya. Cha ajabu watu walionekana kugombania mali mpaka kubishana ila ilipokuja kwenye suala la sisi nani atatulea, walianza kupigiana danadana. Mwisho iliamriwa kuwa tutaishi kwa baba yetu mkubwa aliyeishi Manyara, kabla haujawa mkoa, tena kijijini. Nakumbuka kuna mtoto wake ambaye baba alikuwa akimsomesha shule moja ya bweni, Arusha, na kijana huyo aliendelea kusoma mpaka akamaliza kidato cha nne, akafeli na kushindwa kuendelea. Lakini kwangu mimi ilikuwa mwisho wa masomo yangu.



    Niliandikishwa shule huko kijijini ila hata nguo za shule, au viatu sikununuliwa zaidi ya nilivyokuwa navyo. Kaka yangu alipopata nafuu naye aliletwa kule Manyara, lakini alitakiwa kuendelea na matibabu kwa muda. Mara kwa mara vikao vya ndugu vilikaliwa, na kilichozungumziwa ni mali tu na sio malezi, elimu wala afya ya kaka yangu. Kuna siku kaka mwenyewe alijaribu kuuliza kwenye kikao kuhusu afya yake, wakamjibu kwa aibu kwamba kuna pesa zinafuatiliwa, zikipatikana ataenda kutibiwa. Waliishia kumpeleka vituo vya afya vidogo tu pale Manyara kwa muda wa miezi kadhaa kisha wakamtelekeza. Nimemuhudumia kaka mpaka amekuwa mtu mzima wa kuweza kujitegemea. Nashukuru badae kabisa aliweza kuishi kwa kujitegemea, ingawa akiwa na ulemavu wa miguu. Kwa sasa ameoa, ana mtoto mmoja, na huyo ndiye ninamsomesha shule ya wasichana ya Marian.”



    Kila nilipomsikiliza kaka Bahati akiongea, hasira zilinishika, nikazidi kuwachukia ndugu wanaoachiwa watoto na marehemu. Nilikumbuka jinsi baba mdogo alivyoonekana kutupenda baba akiwa hai, na namna alivyotubadilikia baada ya msiba. Nafsini mwangu nilitamani nilipe kisasi, si kwa ajili yangu tu, bali kwa ajili ya yatima wote wanaoteswa na ndugu wa wazazi wao. Kaka Bahati amekuwa akinielezea kuhusu maisha yake kwa vipengele, mara nyingi baada ya kula usiku. Zita hulala mapema kidogo, ila mimi napenda kukaa sebuleni baada ya chakula. Licha ya kuzungumzia maisha na historia za nyuma, najifunza mambo mengi sana kwa kuongea na kaka Bahati.



    Kwake nimejifunza kupambana na maisha, kuwa mvumilivu, kuthamini watu, kutia bidii katika ,mambo yote na zaidi kusamehe. Nilivyoendelea kuishi naye niligundua kuwa natakiwa kusamehe wote waliowahi kuniumiza katika maisha yangu. Liliokuwa gumu zaidi ni kumsamehe bamdogo Naise, kwani kitendo alichofanya sio tu kiliniumiza, bali pia kiliacha alama mbaya kwenye maisha yangu. Nilimuhadithia kaka Bahati vitu vingi, lakini sikumwambia kuhusu kubakwa kwangu, kwani niliona aibu, mpaka siku moja yeye aliponiambia alifanyiwa jambo baya zaidi ya mimi kubakwa.



    “Tukiendelea kuishi kijijini, baba mkubwa alianza kuwa na maisha bora zaidi, nikajua ni mali za wazazi wangu. Kwa mtu wa kijijini, tena miaka hiyo, kununua gari, haikuwa jambo dogo kabisa. Alinunua gari, alianza kulimisha mashamba yake kwa kukodisha vijana wengi ambao baada ya kulima walikuja kula nyumbani. Aliajiri watu wa kupika na ni kama kila siku ilikuwa sherehe. Watoto wa bamkubwa wote walisoma bila shida, na kupatiwa mahitaji yote, isipokuwa mimi na kaka ambao hatukuonekana kama watoto wanaohitaji kuhudumiwa. Mahitaji yetu yote yalipuunzwa, kuanzia elimu mpaka mavazi. Muda ulivyoendelea ndipo tulizidi kuonekana kama watu waliovamia familia za watu, na hivyo tuliishi kama watumwa kabisa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Niliachishwa shule na kuanza kuchunga mifugo ya bamkubwa huku nikiendelea kumuhudumia kaka yangu, aliyekuwa hawezi hata kunyanyuka bila msaada wa mtu. Kaka yangu ameishi kwa shida mno, kiasi kwamba kuna wakati alitamani ajiue, akidai kuwa ananitesa na yeye akiteseka. Kwangu uwepo wake ulikuwa ni faraja kubwa mno, na hata siku moja sikuwahi kuona ni mateso kumuhudumia.



    Siku moja, nilienda kuchunga alfajiri sana kama nilivyozoeshwa. Kuna wakati nilikuwa na vijana wenzangu wakichunga mifugo yao, lakini mara nyingi walianza kuchunga jua limeshachomoza. Mwamzoni niliogopa sana, kwani mazingira ya kule yalinitisha, lakini baadaye nilizoea. Siku hiyo, nikitembea maeneo ambayo hayakuwa mbali sana na nyumbani, nasubiria kuwe na mwanga kidogo ndipo niende mbali, alitokea mwanaume mmoja, tena niliyemfahamu kama rafiki wa baba mkubwa, akaanza kuniuliza maswali kadhaa. Mwanaume huyu alionekana amelala kwenye pombe, kwani kule kijijini hiyo tabia haikuwa ya ajabu. Aliniuliza maswali kadha wa kadha, yasiyo na mbele wala nyuma, kisha akanishika mkono na kuanza kunivutia porini. Nilipiga kelele nyingi sana, nikiamini nitasikiwa. Kaka yangu anasema alisikia hizo kelele, akahisi ni mimi, lakini hakuwa na cha kufanya zaidi ya kupata hofu tu na kusubiri taarifa. Yeye alihisi pengine nimeliwa na mnyama mkali. Yule mwanaume alinichukua na kuanza kuniingia kinyume na maumbile huku akidai ananifundisha maisha. Nililia mno, nikapiga kelele, akiniziba mdomo na kuendelea na kile kitendo, halafu akaniacha hapo na kuondoka.”



    Kaka Bahati amepitia visa vingi sana katika maisha, kiasi cha kwamba karibu kila mara tukiongea, alisema kisa kipya. Umri wake haukuwa mkubwa sana wakati nakutana naye, lakini historia ya maisha yake ni kama ya mtu wa miaka hamsini. Lakini tofauti na ambavyo maisha yamemtenda, yeye ni mtu mpole na mwenye upendo mwingi sana. Hana chuki na mtu, anahurumia watu wa kila aina, na hana kinyongo kwa waliomkosea. Alinifundisha kuwa, unaposhindwa kusamehe aliyekukosea, kinachofanyika si kumuadhibu mkosaji, bali kujiadhibu mwenyewe.



    Siku moja tukiwa matembezi ya mwisho wa wiki, mimi, yeye na Zita, kuna maneno alisema nasi, yakanifanya nianze kujilazimisha kusamehe wote walioniumiza. “Nimeishi maisha ya chuki kwa muda mrefu, nikitamani na kusubiri kulipa kisasi kwa wote walioniumiza. Unajua ukiwa umebeba kisasi moyoni, hauishi maisha yako. Yaani kila kazi, shughuli au chochote nilichokuwa nikifanya, kilikuwa kwa ajili ya wale walionikosea. Nilifanya kazi kwa bidii, nikitaraji kupata pesa ili niwakomeshe. Nilitamani kutengeneza jina kubwa, nilitamani hata ningeweza kusomea sheria, kuingia kwenye siasa au kuwa mtu yeyote mkubwa na mwenye mamlaka duniani, lakini si kwa ajili yangu mwenyewe, wala kwa faida yangu, bali ili niwe katika nafasi ya kuwahukumu na kuwalaani walionitesa."Alizungumza kaka Bahati, halafu akaendelea.



    "Mara nyingi ukiwa mtu mwenye kisasi ndani yako, unaweza ukawa mtu unayewafanyia watu ubaya sana, lakini unajihesabia haki daima. Kuna wakati, nilipoanza kuingia kwenye mahusiano, niligundua kuwa nagombana sana na wanawake. Kwanza sikuwa najali kuwa mwaminifu, pia niliwafanya kama watu wasio na thamani huku akili ikiniambia watu wote duniani, ukiacha wazazi na ndugu wa damu, hawana upendo wa dhati. Kwangu wanawake niliona kama watu wa kupita tu kiasi kwamba mtu angenifanyia kosa dogo sana, lingesababisha nimuache. Nimewatesa mabinti wengi bila huruma.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Lakini pia kisasi kilinifanya nisiwe mtu wa marafiki wala wa kusaidia watu. Baba alikuwa na marafiki wengi sana akiwa hai, na alisaidia watu wengi. Kuna rafiki zake baba waliokuwa karibu na sisi kiasi kwamba ungetegemea wangejitolea hata kutulea baada ya wazazi kufariki, lakini niliishia kuwaona msibani. Kuna mmoja, baada ya kuhangaika sana na maisha na kutoroka kijijini, niliwahi kumtafuta na kwenda ofisini kwake, lakini alijifanya hanijui kabisa, na hata baada ya kujitambulisha, alijifanya ana mambo mengi sana na hivyo nimtafute siku nyingine. Nilimtafuta zaidi ya mara tano lakini mara zote alidai hana muda hivyo nije siku nyingine, mpaka nikakata tamaa.



    Lakini nakumbuka nikiwa na miaka 20, maisha yamenipiga sana wakati huo, nimetoroka na kumuacha kaka yangu, ingawa alishaweza kujitegemea kwa kiasi kikubwa, nikiwa nimehangaika Dar es Salaam kwa miaka miwili bila msaada wala tumaini lolote, kuna siku nilikutana na mtu akabadili mtazamo wa maisha yangu kwa kiasi, hasa katika suala la kusaidia watu. Kipindi hicho niliamua nitaanza kutafuta mitaji kwa watu nisiowajua, mtu yeyote tu. Nikaona njia rahisi ni kuanza kwenda kanisani. Nilihudhuria kanisa moja kubwa, nikawa kila nikitoka kanisani, nawafuata wanaume au wanawake wanaoonekana na uwezo kifedha kuwaomba msaada. Wakati huo wote, kulala na kula kwangu ilikuwa mtaani. Nilikula kila kitu, bila kujali ni kisafi au kichafu, maadamu ni chakula tu. Sikuangalia mazingira gani nakula au nalala. Maisha kwangu hayakuwa na thamani yoyote zaidi ya kula na kulala. Siku za Jumapili, nilijitahidi kuwa na nguo ambayo naweza kuingia nayo kwenye mikusanyiko ya watu, wasinifukuze, ingawa wengi hawakupenda kukaa karibu na mimi kanisani.



    Kila baada ya ibada nilihakikisha nimeongea na watu wawili au watatu, lakini hakuna aliyekuwa na msaada. Wengi wao walinipa jibu moja tu, “Sina hela”. Nilifanya hivyo kwa zaidi ya miezi sita mfululizo, bila kupata msaada wowote kabisa ingawa kanisa lilikuwa kubwa. Nilikariri watu wote wenyeji wa kanisa lile, kwani ilifika mahala nikawa siangalii sana muonekano wa nje, najaribu bahati tu. Siku moja nakumbuka alikuja mgeni kanisani hapo, mwanaume mmoja na familia yake. Wale watu walijitambulisha kuwa wametokea mkoa fulani hapa Tanzania na wamekuja kikazi kwa muda hivyo watakuwa wakisali hapo. Niliogopa kumfuata yule mtu siku ya kwanza baada ya kutoka ibadani, kwani angehisi ni tabia ya watu wa kanisa hilo.



    Nilimuacha kama wiki mbili zikapita, nikamfuata wiki ya tatu. Nilimsalimia na tofauti na watu wengi walioonesha kutojali kabisa, yeye alinijibu kama anajibu mtu mwenye thamani kwake. Aliniuliza habari yangu, akaniuliza kama bado nasoma au la. Wakati huo, familia yake ilikuwa ikimsubiri kwenye gari tayari. Nilipomwambia sisomi, aliuliza kwanini au kama nilishamaliza shule. Nilimjibu kwa kujieleza kidogo kuwa sikubahatika kuendelea na shule kutokana na wazazi wangu kufariki nikiwa mdogo.



    Yule mwanaume alionekana kuguswa sana na maelezo mafupi niliyompa, kiasi cha yeye mwenyewe kuniomba nimtafute ofisini kwake. Nilifanya hivyo haraka sana na kuonana naye, siku tuliyopanga. Alinikaribisha kwenye ofisi kubwa kama ofisi ya mkurugenzi wa kampuni kubwa sana au kiongozi mkubwa wa serikali. Siku hiyo nilijihisi, kwa mara ya kwanza, kwamba na mimi ni binadamu ninayeweza kuzungumza na watu na kusikilizwa. Mwanaume yule, bwana Magessa, alinisikiliza kwa muda wa karibu saa nzima nikimueleza historia ya maisha yangu huku akinidodosa kwa maswali kadhaa kama mtu anayeonesha umakini kusikiliza ninachomwambia. Baadaye aliniuliza kama nna mpango wowote wa maisha. Tangu nimeamua kuwafata watu, nilikuwa na mpango wa biashara fulani ndogo kichwani mwangu, ili mtu akiuliza anisaidieje, nisimuombe hela ya kula bali mtaji wa biashara. Nilimuelezea biashara yangu, lakini yeye alinishauri kwamba kwa biashara ndogo na inayoanza, na kwa mtu asiye na uzoefu kama mimi, ingenipa shida sana kusimama au ingesimama na baadae ikafa. Alinieleza kuwa bishara inahitaji uzoefu, mtu wa kunishika mkono na jitihada sana, ukiachilia mbali mtaji ambao sitaula.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya maongezi yetu ya muda na ushauri, bwana Magessa ambaye kwa sasa namuita baba, alinishauri nitafute chuo cha masomo ya uzoefu maalumu kama kompyuta, hoteli, uhazili au kitu chochote, kisha nikimaliza kusoma atanisaidia kutafuta kazi. Kwa wakati huo, ilihitaji kujua kusoma na kuandika tu, na labda kujifunza kiingereza kabla ya kuanza. Aliniahidi kunipatia pesa za matumizi kwa muda wote wa masomo yangu, mpaka nitakapoweza kupata kazi. Lakini aliongeza kusema kuwa atanisaidia, kwa kadiri nitakavyohitaji msaada, ila nikimaliza masomo, nikapata kazi na kuweza kupata kipato kinachonikidhi, basi nitamrudishia pesa yake taratibu.



    Siku zote nilienda kanisani, na wakati mwingine nilisikia mchungaji akihubiri kuwa Mungu anatupenda, lakini hilo jambo halikuwahi kuingia akilini mwangu, mpaka siku baba mzee Magessa aliponipa hii habari. Nilikuwa nikijiuliza sana, huyu Mungu wanayedai anatupenda, ni kweli yupo? Na kama yupo, anatupenda sote au ana ubaguzi kwa baadhi ya watu? Kama habagui, maisha yote niliyowahi kupitia na ninayopitia, hayaoni? Au labda hana uwezo wa kunisaidia? Kwangu mafundisho kuhusu upendo wa Mungu, uwezo wake, nguvu au chochote kuhusu Mungu niliona ni uongo na unafiki tu kwani haikuniingia akilini kwanini huyo Mungu wanayemzungumzia ashindwe kunisaidia mimi katika shida zote nilizokuwa nikipitia.



    Nililia sana, nilipopewa zile ahadi, huku nikidhani niko ndotoni. Katika maisha yangu yote, hakukuwa na mtu mwema nimewahi kukutana naye kama mzee Magessa. Kama angejitambulisha kama Mungu, hakika ningeamini bila shaka, lakini huku nikiendelea kumshukuru, alianza kuniambia, nimshukuru tu Mungu kwa kuwa ananipenda. Akili yangu hapo ilianza kukubali kuwa itakuwa kweli Mungu ananipenda.



    Nilitafuta chuo kimoja, nikasikiliza masharti yao, yaliyonitaka kujiunga na kozi ya kiingereza kwa miezi mitatu kabla ya kuanza masomo. Nilisoma kingereza, halafu nikaanza masomo ya kompyuta na utengenezaji wa kompyuta. Nilisoma kwa mwaka na nusu, yaani miezi 18, huku nikipata msaada wa kila kitu toka kwa mzee Magessa. Alihakikisha sipungukiwi chakula, nauli wala ada ya masomo. Alinipangishia na chumba pia hivyo ikawa mwisho wangu wa kulala mtaani. Nilichokifanya ni kuwa naandika kila pesa aliyonigharimia, ili nitakapofanikiwa, nianze kurejesha. Hakuwahi kukumbushia suala la kulipa, hakuwahi kuonesha kuwa ni mzigo kwake kunihudumia, na wala sikuhitaji kumuomba pesa ya matumizi. Alinipa kiwango kadhaa kwa ajili ya matumizi kila mwezi, akipiga hesabu ya usafiri, na chakula. Alilipa kodi ya chumba changu ya mwaka mzima na ilipoisha alinipa nyingine bila kumuomba. Alilipa ada yote mihula yote, akanisisitiza kumueleza endapo kutatakiwa kulipia gharama nyingine yoyote.



    Nilisoma kwa jitihada nyingi mno, huku nikijiona mtu mwenye deni kubwa juu ya mzee Magessa. Kurudi shule ilikuwa ni changamoto kiasi, lakini nilihakikisha nafanya vizuri sana. Nilimaliza masomo yangu na kama alivyoniahidi, alinisaidia kutafuta kazi mahala fulani kama mtaalamu wa ufundi wa kompyuta (computer technician). Unajua miaka hiyo hakukuwa na wataalamu wengi, hivyo hiyo kazi ilinipatia kipato na kunipa heshima kwa watu. Nilianza kupokea mshahara, wangu binafsi, pesa ambayo sikuwahi kukaa na kuota kwamba namimi nitafanya kazi na kulipwa mshahara. Miaka mingi ya utumwa na mateso ilinifanya nijione katika maisha sistahili hata kumfanyia mtu kazi akanilipa mshahara. Niliwahi kuwa nafanya vibarua na kupewa pesa kidogo za kujikimu, lakini wakati mwingine nilifukuzwa kwenye vibarua bila hata sababu za kueleweka, au wenzangu walianza kunifanyia vituko na kuniambia sitakiwi kwenye kazi zao, na mambo mengi ya namna hiyo. Kiufupi nimeishi maisha ya kukataliwa, na ndugu, marafiki hata watu wasionijua, tangu wazazi wangu wafariki, na mzee Magessa ndio alikuwa mtu wa kwanza kunikubali na kunionesha thamani yangu."-CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog