Search This Blog

Friday, July 15, 2022

SITASAHAU - 5

 







    Simulizi : Sitasahau

    Sehemu Ya Tano (5)

    .CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Aliponikaribia niliyaona macho ya Tayana yakimaanisha kitu..macho ya upendo huku mdomo wake ukihitaji kusema kitu ni kama ameshikwa na kigugumizi....Tukasogeleana!...Tukatazamana!....Tukajikuta tunakumbatiana. Kumbatio lenye kufungua ukurasa mpya wa urafiki...nikapigwa na bumbuwazi...nikapoteza kumbukumbu nzuri na kuwaza ni lini hasa mara ya mwisho mimi kukumbatia ama kukumbatiwa na sio tu kukumbatiwa na binti, binti mrembo? Nilihisi mwili wangu umepigwa na shoti ya umeme...shoti iliyokuwa inasambaa mwilini kwa wakati huo....akili haikutaka..zaidi ilikuwa uzoefu wenye kuvutia sana. " Nakupenda Richard, nakupenda sana Richard natamani uwe mume wangu Richard hata sasa" Alinitamkia Tayana bila woga. Nikashtuka!.... Nikavutwa! nikavutika! kizuri hapa ni kwamba tayari mimi nilishapenda tangu siku ya kwanza nilipomuona. Nikamjibu nampenda pia .....Tukaachiana.....

    Tayana akaniita.."Richard? Nataka kukukabidhi moyo wangu, tangu sasa nakukabidhi moyo wangu siwezi kuendelea kuumiza moyo wangu...sitaki kuhisi nakupenda...nataka kukwambia nakupenda Richard. Hichi nilichokuwa nacho kitakuwa kwa ajili yako peke yako, naapa sitampa mwingine sitakuumiza na naomba husiniumize Richard..tazama ujasiri niliouonesha Richard kwako?....Ni wanawake wachache wenye ujasiri kama wangu wa kumtamkia mwanaume hisia zake..tafadhali kubali ombi langu Richard...Husinikatili Richard, mimi ni kiumbe dhaifu mbele yako Richard."

    Nilimtazama Tayana kwa mshangao...nilivutiwa na ujasiri wake....bila kuchelewa nilimjibu...'Too late Tayana'...Nikamuona Tayana akishangaa! uso ukapoteza tabasamu lililokuwepo...nikagundua!.."sivyo ufikiriavyo Tayana" Nilimueleza.....akabakia ameshikwa na mshangao wenye taharuki! ... Nilikupenda tangu siku ya kwanza nilipokutia machoni Tayana. Nilipokuona siku ile kwa mara ya kwanza mwili wangu ulinisisimka na nikajua huyu ndiye mwanamke niliyekuwa namsubiria. Mwanamke wa ndoto yangu. Hata hivyo siku ile nilifikiri kama jambo hilo lisingewezekana milele...tofauti yangu na yako ilikuwa kubwa. Nikasahau mapenzi yana mambo mengi...mapenzi ni kama sanaa ambayo unaweza kuyatengeneza ukiamua karibu ndani yangu Tayana.....Sitakuumiza..nitakulinda Tayana. I don't know what happened........Hakika Tayana alivutiwa na mapishi yangu niliyomuandalia siku hiyo...

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ==============================================================

    Miezi sita baadaye mkono wangu wa kiume ulikuwa umemshika Tayana pembeni yangu ndani ya kanisa ya St Joseph tukielekea kwenye antare kwa ajili ya kiapo cha ndoa....ndani ya kanisa hilo lililojaa pomoni....furaha ilinitawala kila nilipowaona wazazi wangu wakifurahia......nawatazama marafiki wakinishangilia...najikuta nikiamini mimi ndiye mwanaume mwenye furaha kuliko wote Duniani. Tayari ninaye mkononi mwangu mwanamke mrembo anayeenda kutimiza ndoto zangu. Ndoto ya kuwa na mke mzuri....mke mrembo mwenye kujivunia kwa marafiki. Baada ya kula kiapo nikamgeukia Tayana ambaye sasa ni mke wangu rasmi nikamwambia; " Uwepo wa mmoja haukamiliki mpaka uwepo wa mwenza..asante moyo..asante moyo kwa kupenda" Mwanamke aliyenipatia Mungu.

    Mwisho wa Richard....Twende kwa Tayana naye tumsikilize kwa ufupi...ana lipi ambalo anahitaji jamii ijifunze kupitia yeye



    Simulizi hii ni ya ukweli mtupu ila majina halisi yamefichwa kwa sababu maalumu....ni baada ya kumsikia Richard ilibidi nifunge safari hadi kigamboni mahali ambapo Richard anaishi sasa. Nimeikuta familia yenye furaha sana..nikikaribishwa kwa uchangamfu wa hali ya juu. Nipo kwenye ukumbi mdogo uliotengwa mahususi kwa ajili ya wageni kama mimi..mbele yangu kwenye sofa amekaa Mr Richard na kwenye sofa la upande mwingine amejimwaga Tayana huku pete ya dhahabu inayoonekana ya thamani kubwa iking'aa kidoleni mwake sasa mke wa Richard.....uwanja ni wa Tayana sasa......Tayana kwa ufupi sana anaeleza;





    Nilizaliwa kwenye familia ya wazazi wasomi, wenye kujua nini maana ya familia. Mama yangu alikuwa daktari katika moja ya hospitali za rufaa nchini. Huku Baba yangu alikuwa mtumishi wa wizara ya fedha. Mama yangu na Baba yangu siku zote walikuwa wakinuia pamoja. Walipendana na kutulea kwenye misingi ya ucha Mungu na upendo wa hali ya juu. Tulijikuta sisi tukiwa watoto wenye heshima na adabu sana kiasi ambacho kikapelekea kusifiwa na jamii iliyotuzunguka mimi na kaka yangu. Sote wawili tulipenda imani yetu, tulipendana sana sisi kwa sisi kwa vile tulikuwa tumelelewa kimaadili kila mmoja alipata elimu nzuri. Kaka yangu alihitimu shahada ya mawasiliano ya umma katika chuo kikuu cha Nairobi kisha akaanza kusimamia biashara za familia. Mimi nina shahada ya Human resource kutoka chuo kikuu Mzumbe.

    Miezi michache kabla ya kutunukiwa shahada yangu.....pigo kubwa katika familia yetu ikatufikia. Baba na mama yangu walifariki kwa ajali ya gari maeneo ya Tegeta wakati wakitoka kutembelea shamba ya familia yetu lililopo Bagamoyo nje kidogo ya mkoa wa Dar Es Salaam. Baba yangu alikufa pale pale huku mama akifia mikononi mwangu Hospitali ya Muhimbili baada ya kufikishwa hapo wakijaribu kuokoa maisha yake.



    Kifo cha wazazi wangu Ilikuwa pigo kwangu na pigo la familia yetu. Baada ya kumaliza msiba wa wazazi wetu ilimlazimu kaka yangu achukue majukumu ya kusimamia mali za wazazi wetu ikiwemo kampuni ya usafirishaji. Na baada ya kumaliza chuo nikajiunga kufanya kazi kwenye kampuni yetu kama afisa wa Rasilimali watu yaani HR.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku moja nilikuwa nimetoka kuchukua nyaraka kwa mwanasheria wa kampuni yetu.....sikumbuki siku yenyewe ila bado kumbukumbu ile ingali ipo kichwani mwangu.....niligongana na Richard kwa bahati mbaya naweza kusema hivyo sasa. Kwa kipindi kile nilichukulia kuwa alifanya kusudi....inawezekana Mungu alipanga tukio lile liwe chanzo cha familia hii. Maneno yangu hayakuwa mazuri kwa Richard.....naumia nikikumbuka maneno yale..najutia kosa lile mpaka kesho.....nisamehe sana mume wangu nakiri nilifanya makosa makubwa mbele yako Richard.

    Nilimuona Tayana akitiririkwa na machozi huku akiyapangusa kwa utulivu husio na shaka...ndipo alipotufanya sote tupigwe na mshangao.....aliendelea kueleza Tayana...



    Nilikutana kwa mara ya pili na Richard ni wakati alipokuja kufanya usaili kwenye kampuni yetu. Katika kampuni ambayo mkurugenzi ni kaka yangu tumbo moja....Nilikuwa na maamuzi makubwa katika bodi ya kampuni. Nilimfanyia usaili Richard alionekana mvulana mwenye akili na mwerevu sana....alistahili kuajiriwa kwenye kampuni yetu na leo nakiri mbele yako...ulishinda usaili ule Richard lakini kwa wakati ule nilikuchukia sikutaka uwe sehemu ya wafanyakazi wa kampuni yetu kutokana na uadui uliojitokeza kati yetu. Ni mimi ndiye niliyeliondoa jina lako baada ya kupendekezwa na kwa alama nyingi na mwezangu.

    Nikamuona Richard akitikisa kichwa kama ishara ya kuumia moyoni mwake.....inaumiza hakika

    ....Tayana akaendelea kuhitimisha...CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Naomba unisamehe sana Richard...sikuwa natambua nikifanyacho kwa wakati huo. Leo naamini kila kitu kilichokuwa kinatokea kati yangu mimi na wewe kilipangwa kwa sababu maalumu...husichukie kwa kile nilichokutendea mume wangu. Nafikiri kama ungeajiriwa kwenye kampuni yetu ingekuwa vigumu mimi na wewe kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi. Ulipoteza kazi na ukapata kazi pia ukanipata mimi Richard. Yote haya hayakuja kwa bahati mbaya....Mungu alituonesha kupitia matukio yale na kuyatenda sasa. Nakupenda kuliko nilivyofikiria..nisamehe sana Richard.....

    Nimefahamu historia yako ya mahusiano yako yaliopita Richard lakini kwa upande wangu niliwahi kukueleza kwa ufupi sana mahusiano yangu yaliyopita na hata hukuwahi kuhitaji nikueleze kwa kirefu nachukua nafasi hii kukueleza ili moyo wako uwe na amani siku zote mume wangu.

    Nilikuwa na mvulana niliyempenda sana. Hakuna namna bora ya kuelezea machungu yangu aliyonisababishia kisha nikaeleweka. Nilimpenda sana Patrick, nilimpenda Patrick ilifikia wakati nikaamini atakuwa mwangaza bora katika maisha yangu. Niliamini yeye atakuwa nuru iangaziayo amani na furaha ndani ya moyo wangu. Katika kipindi cha furaha na huzuni. Mwisho aliniacha na kwenda kuoa mwanamke mwingine huku angali bado na mahusiano nami, ukatili husio na mfano. Jambo hilo likanifanya nichanganyikiwe kwa kiasi kikubwa.



    Kwa ajili yake nimelia sana na ilikuwa ngumu kuamini kilichotokea na sikujua maisha yangekuwaje bila yeye..sikuona sababu ya kuendelea kuishi katika Dunia hisiyo na huruma ndani yake huku Patrick akifurahia maisha na mwanamke mwingine..Patrick alioa mwanamke mwingine angali bado yupo na uhusiano nami huwezi kuamini, Patrick aliniambia tuachane siku moja kabla hajafunga ndoa...ukatili husio semeheka...nikafikia maamuzi ya kunywa sumu....sumu ilikuwa suluhisho sahihi kwa wakati ule ili kuondokana na kadhia hii. Bahati nzuri dakika chache baada ya kunywa sumu rafiki yangu aliwasili nyumbani kwangu bila kunitaarifu ujio wake. Mpaka leo sifahamu kwanini alikuja kwangu kwa wakati ule.....ndipo nilipowahishwa hospitali....nilinyonywa sumu yote iliyokuwa inasambaa mwilini mwangu.

    Kaka yangu alipigania maisha yangu kwa nguvu zote naweza kushukuru kwa hilo. Baada ya kupata nafuu nilipandishwa kizimbani kwa kosa la kujaribu kutaka kujiua.... Mwishowe nilihukumiwa kifungo cha nje cha miezi sita ni baada ya mwanasheria wetu kufanya kazi kubwa kuishawishi mahakama. Kisha nikapelekwa kwenye vituo vya ushauri Nasaa kwa washauri waliobobea katika masuala saikolojia na mahusiano ya kimapenzi ni hapo ndipo nilipojihisi kuwa kitendo nilichokuwa nataka kukifanya ni cha kipuuzi. Baada ya yote hayo nilipewa mapumziko ya wiki mbili katika kisiwa cha Zanzibar. Kaka yangu alinipeleka Melia hoteli ni huko ndiko historia yangu ilipobadilika. Ndipo mahala huzuni yangu ilipoishia na ndipo ambapo furaha yangu ikaanzia.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakati Tayana anamalizia kueleza simulizi yake, mume wake Richard hakuwepo sebuleni hapo......sikumbuki ni muda gani aliondoka? maana nilizama kwenye simulizi ya Tayana ila nafikiri wakati Tayana anamuelezea Patrick ndipo alipoondoka Richard...Ni wakati ambapo Tayana ananyanyuka na kumfuata Richard alipo....punde wote kwa pamoja wanarejea sebuleni...nabaki nawatumbulia macho yenye udadisi mwingi... Tayana mbele yangu anampigia magoti mumewe....

    Richard mume wangu....ukweli nakupenda sana. Bila wewe mimi si kitu...Maneno na matendo yako yamenipa ujasiri wa kuamini sikuwa nimekosea kukupendekeza katika maisha yangu. Najua utakuwa malaika na waridi wa moyo wangu. Kila ninapokufikiria moyo wangu unakuwa ukifarijika kwa furaha na kuburudika kwa shauku ya kukuona kila wakati. Nakuona kama jicho au roho yangu. ingawa sina uwezo mkubwa mume wangu nitahakikisha kila ulichodhamiria ndani ya ndoto zako zikifanikiwa. Maisha yako yatakuwa yangu na naamini utayafanya maisha yangu kuwa yako.

    Kwa ajili ya mapenzi yangu kwako kila muda nitatamani kuwa na wewe nahitaji kukufanya ucheke, ujidai na uone thamani na fahari ya kuwa na mwanamke kama mimi..mwanamke anayekupenda na kukuthamini Richard. Machozi yalianza kumtiririka Tayana..ndipo ambapo Richard aliposogea na kumkumbatia mkewe...kisha akamwambia...



    " Wewe ni Mama wa watoto wangu wawili.....nimekusamehe kila ulichonifanyia. Nakupenda sana mke wangu nataka uwe wangu milele yote yamepita mke wangu...ni wakati wa kutuliza hamu zetu kaa kwangu daima, nikupende sana wewe niwe wako daima. Nyakati haziwezi rudi nyuma tugange yajayo mke wangu".

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Yote niliyashuhudia yakitendeka mbele yangu. Simulizi yao ni kama tamthiliya fulani yenye kusisimua nikaadhimia kuicheza katika filamu simulizi hii ili jamii yote ipate elimu hii kupitia Richard na Tayana..wakati nikiendelea kuwatazama wapenzi hao wakiendelea kukumbatiana mbele yangu....."Mr and Mrs Richard" hatimaye niliwaita.....wote kwa pamoja waliachiana na kunigeukia huku wakinitazama kwa pamoja....nikatabasamu.....kisha nikawaambia...

    "Kila aliye na mahusiano na mtu anayempenda huwa katu hawezi kutamani kumpoteza. Kuwa na mtu unayempenda kwa dhati ni zaidi ya raha ya kawaida unaweza kujikuta muda wote uko na furaha, japo mipango ya maisha yako haijawa ya kuvutia. Faraja na amani utakayoipata kwa kuwa na yule unayempenda kwa dhati huweza kutibu majeraha yaliyopita, hatimaye kuyaona maisha kuwa ni kitu bora cha kufurahisha" nikawaona wapenzi hao wakitazamana huku wametabasamu......falsafa wasiojua nilichomaanisha.....



    Mlio wa mlango unaosukumwa ukatufanya sote tuyaelekeze macho yetu mlangoni kushuhudia kiumbe kinachoingia........watoto wawili mapacha wenye jinsia tofauti wenye umri kati ya miaka 2-3 walikuwa wanaingia eneo hilo huku yule wa kiume akimkimbilia mama yake na yule wa kike akienda kutua kifuani mwa baba yake. Tukio lenye kusisimua.....Bila shaka hawa ni watoto wao kutokana na mfanano wao..sikutaka hata kutambulishwa kwa jinsi walivyo fanana na wazazi wao....Atimaye wakanitambulisha watoto hao yule wa kike aliitwa Nadia nafikiri Richard alitaka kumuenzi Nadia binti wa ajabu aliyemlipia nauli kwenye bus huku yule wakiume akiitwa Johnson kwa heshima ya marehemu mzee Johnson Ndeluma"

    Ilinilazimu kuwaaga na kuondoka....wakati namalizia ngazi ya mwisho ili nitoke nje nikakumbuka kuna jambo sijalisema ambalo nilitaka niwaambie nikarejea haraka ndani nikawaita kwa mara nyingine "Mr and Mrs Richard"......Naomba niwaambie siku zote watu hujifunza kwa mifano. Mifano huwakilisha kwa ustadi wa hali ya juu hisia na hali halisi ya jambo fulani kwa tafsiri maridhawa. Kukutana kwenu ilikuwa katika namna ya tafsiri. Na kilichotokea kitakuwa mfano kwa vijana wengi nchini. Asante kwa ushirikiano wenu. Nakuahidi Mr Richard nitafanya kila jitihada, kuwatafuta popote sitachoka kutembea mchana hata usiku ikiwa nitawapata Patrick na Nice nitawakutanisha tena ili muifanye familia zao na yenu marafiki.....tafadhali kubalini ombi hili..... "Bila shaka" Wote walitamka kama vile walikuwa na mawazo yanayofanana.... Nikacheka! Nikacheka! kwa kupata bahati ya kuifahamu simulizi hii.

    Ni mwaka wa tatu sasa....naendelea kuwatafuta Nice na Patrick ili nitimize agano langu.....sijapata hata fununu za watu hawa walipo....najua simulizi hii itasomwa na watu hao bila shaka mtakapoisoma msisite kuwasiliana nami nahitaji kufahamu ukweli wenu....ukweli husiosahaulika.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mwisho.



    AHSANTENI SANA KWA KUWA NASI TANGU MWANZO MPAKA MWISHO WA KISA HIKI CHA KWELI. TUNATUMAI KUWA MTAKUWA MMEJIFUNZA JAMBO KWENYE KISA HIKI. TOA MAONI YAKO



0 comments:

Post a Comment

Blog