Search This Blog

Friday, July 15, 2022

KICHAA - 2

 







    Simulizi : Kichaa

    Sehemu Ya Pili (2)



    Siku ziliendelea kwenda na hata kupita zaidi. Huku Mavugo akiwa ndani ya gereza. Alipazoea sasa na alipata marafiki kadhaa ingawa akili zake zilikuwa zikija na kupotea kwa muda. Ukimuona Mavugo huwezi kushindwa mfananisha na kichaa. Kuna masaa aliongea kama mtu mwenye akili lakini pia kuna masaa aliongea kama mtu asiye na akili. Hiyo ilipelekea asiaminiwe kwa kila alilolisema na aliitwa kichaa muda wote.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Naam.. Nikweli kabisa kuwa, Mavugo alikuwa akirejewa na akili zake kwa dakika chache kisha akili hizo kutoweka kwa muda mrefu na kumfanya aonekane kichaa. Aliongea maneno ambayo wenzie yaliwa hakikishia kuwa mfungwa mwenzao ni kichaa. Ingawa yeye alijiona yupo sahihi. Kuna siri kubwa sana iliyojificha, ina muhusu yeye. Lakini hakuna alichokijua kutokana na kulukwa na akili. Kila alipoijiwa na akili, alikumbuka mambo ya ajabu ambayo yalimliza muda wote. Lakini punde tu. Akili zinapomtoka huurudia ukichaa wake. Taarifa za ugonjwa wa ukichaa ziliwapata wakuu wa gereza na wao kuzifikisha mahali husika. Walipomchunguza waligundua ni kweli kabisa Mavugo anaugonjwa wa akili na sio utani kama walivyodhani wao.



    Ati, walihukumu kichaa. Mtu ambae alifaa awe mirembe hosiptal, au bugando hosipil. Wao wakamuweka gerezani. Waligundua kuwa kwenye kitabu cha hukumu hakuna msitali hata mmoja unaomfunga kichaa. Hivyo waliamua kumpeleka tu. Kwenye hosipitali ya vichaa.



     Walimchukuwa na kumpeleka hospitali ya vichaa nae akaanza kuishi huko pamoja na vichaa.



    Ndugu msomaji ule msemo usemao kwamba, 'ukistaajabu ya mussa utayaona ya fir'auni' haukuwa na maana ya kuchekesha wala kudanganya bali ulikuwa na ukweli ndani yake.



    Binadamu muache aitwe binadamu pindi awapo na akili timamu. Hebu kwanza kabla hujaendelea kusoma mshukuru Mungu kwa kukufanya kuwa na akili timamu mpaka muda huu... Kule alipopelekwa Mavugo, alikutana na watu wa aina mbalimbali. Kuna wale muda wote wanacheka tu tena bila hata kufurahishwa. Kuna wale ambao muda wote wanazunguka utadhani wamepewa kazi ya kuweka usalama wa bosi fulani. Ati kuna wale ambao wao wanavua samaki hadi kwenye mabakuli.



    "Habari yako" Ni sauti ya Mavugo iliyokuwa ikimjulia hali kichaa mmoja ambae toka asubuhi yeye alishinda anakimbia tu mpaka muda ule jasho lilikuwa limemtoka lakini hakuahirisha. Alivyosikia sauti ya Mavugo akasimama kisha akamjibu,"Njema tu." Hapo sasa Mavugo akahisi huenda amepata rafiki maana alijua kuwa huko wote ni vichaa tu.



    "Vipi rafiki yangu. Mbona tangu jua lichomoze wewe unakimbia tu. Tena upohapahapa mpaka muda huu. Hauchoki?" Akairejea kazi yake ya uandishi wa habari kwa muda.



    "Nichoke!? Ohøoo.. Shauri yako, mwenzio kila siku nakimbia mpaka sasa nimeshafika dar-es-salaam. Lazma nitoroke Tanzania. Nataka kwenda somalia huko vitani, kwahiyo usinibughudhi kabisaaa! Wewe endelea kukaa hapo. Sie wenzio wanajeshi. Allaaa!!" Hapo Mavugo akashindwa kuelewa.



    Ati, yupo Dar-es-salaam. Ati, anatoroka aende somalia akapigane vita.. Mmmh! Mbona naona yupo palepale toka asubuhi. Hivi hata hiyo safari ya Somalia ataifika kwa hali hii kweli. Hebu achanimuulize tena. Aliwaza Mavugo kisha akamsemesha tena.



    "Rafiki, naonaga watu wakipanda magari na kwenda Dar, kisha wanachukuwa ndege na kwenda somalia. Tena huwa wanatumia muda mrefu sana kufika. Je, wewe hiyo safari yako ina muda gani hadi leo. Yaani kutokea hapa mpaka huko Dar ambapo umefika kwa sasa kama usemavyo."



    "hahahahaha! Rafiki una maswali ya utani wewe... Ok, nina miaka Saba toka nianze kusafiri. Nimepita mikoa mingi sana na nimeishi sana mahali mbalimbali lakini kila siku huwa naanzia safari yangu kituo hiki hiki na kuhusu hao wa mandege mie nikifika vitani nitayapanda tu. Usijali hebu kwanza niache kuna gari nashindana nalo hapa lisije kunipita bure." Alijibu kichaa yule na Mavugo akaanza kujiona yeye ukichaa wake unauafadhari.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akamuacha na kumfuata kichaa mwingine ambae yeye alikuwa bize huku mkononi akiwa ameshikiria iliyofungwa kamba ya ndoano, huku kichaa yule akiwa ameweka fimbo hiyo ndani ya bakuri dogo lenye maji. Mavugo alipomfikia kichaa yule akampa salamu. Lakini kichaa yule alimuonesha ishara ya kumtaka akae kimya ili samaki wasije wakatoroka.



    Bakuri? Samaki? Mmmh! Híi kali.. Alijisemea Mavugo kisha akaondoka maeneo yale na kuona bora tu akakaepeke yake. Aliiona sehemu moja yeye utulivu akaifuata kwa ajili ya kukaa. Alipofika nako huko akakutana na kichaa mmoja ambae yeye alikuwa amenuna. Mavugo aliamua kumsemesha iliajue nini kilichomsibu chakushangaza kichaa yule akaondoa hali yake ya kununa na kuanza kucheka. Alicheka kwa muda mrefu sana bila kupumzika. Hapo tena Mavugo akapaona hapamfai. Akaondoka na kwenda sehemu nyingine huko akatulia hadi usiku ulipofika.



    * * * *



    Mume wa Aneth alirejea kutoka dar-es-salaam na wakaendelea na Maisha yao. Aneth alimu hadithia mumewe juu ya yeye kumfukuza Aisha mwaka mmoja uliyopita. Ndipo mumewe alipomtafutia mfanyakazi mwingine na Maisha yakaendelea. Kama kawaida ya geti mani alimtaka mfanyakazi yule mpya wa ndani. Japokuwa mfanyakazi alikataa mwanzoni lakini mwishoni alijikuta amemkubalia. Wakaanzisha mapenzi. Kwakuwa mabosi wao walishinda kazini. Wao waliutumia mwanya huo kudumisha penzi lao. Mfanyakazi huyo binti aitwaye Pendo aliamua kumpenda geti mani na hata getimani aitwaye kibakuli naye pia aliamua kumpenda pendo. Getimani hakujijua kuwa tayari alikuwa ameathirika kutokana na damu yake ya grupu o.



    .... ... ... ....



    Mlevi na Aisha walizoeana, lakini hawakuwahi kufanya mapenzi wala kuwa wapenzi. Aisha alimuheshimu yule mlevi kwa jina la David, halikadhalika devid alimuheshimu Aisha kama Dada yake na alimchukulia mtoto wa aisha(Rehema) kama mpwa wake ingawa wote waliishi ndani ya nyumba moja.



    Aisee.. Wanasema mapenzi ni hisia zitokazo moyoni. Hisia hizo huwa hazitokei hivi hivi bali huanza taratibu na mwisho wake kudhihirika. Ile devi kumjali Aisha, kumkirimu yeye pamoja na mwanae pasina kudai malipo ilimpelekea Aisha kutumbukia kwenye dibwi la mapenzi. Alijikuta anampenda sana Devi(Kaka wa hiyari) lakini aliogopa kumwambia kama anampenda. Hiyo ilichangiwa na Devi kupenda ulevi. Yaani asubuhi anaenda kazini halafu jioni anarudi akiwa amelewa. Bahati nzuri kupombeka kwake hakukumuathiri sana kiasi cha kuwa mbogo ndani ya nyumba. Bali kulimuathiri kimaendeleo ya maisha pamoja na kuidhoofisha afya pekee.





    Aisha alijisikia aibu sana kuishi kwa aliyemsaidia bila fadhira zozote. Kila alipofikiria alitamani amlipe japo fadhira lakini hakuwa na chakumpatia kama fadhira. Kila akifikiria aliishia kumuhurumia kaka yake yule wa hiyari.



    Mmmh! Namimi hata sina aibu.. Analala chini. Ananiacha mimi na mwanangu kitandani ilhali hata hatufahamiani. Mimi sijiongezi, mpaka sasa umepita mwaka toka anisaidie. Ananiachia pesa za matumizi, nakula mimi na mwanangu. Yeye akirudi jioni anarudi kalewa na kujibwaga chini kisha analala. Hakuna.. Hakuna.. Inabidi nimlipeangalau hata fadhira, sina pesa, sina mali, bali nina mwili na mtoto pekee. Alaaa! Nimpe mtoto? Hapana mtoto si.. Damu yake. Inabidi nimpe mwili wangu kama fadhira. Lakinii... Lakini mimi ni muathirika. Nikisema nimpe mwili... Mmmh! Achani muache. Masikini, lakini Moyo wangu umeshampenda tayari. Najua tu ananivumilia kwa kujua kwamba ipo siku nitajiongeza. Lakini mimi namuhurumia. Sihtaji ni muambukize. Eeeh. Mungu nipe moyo wa uvumilivu. Nilinde na haya yanayoenda kunikabili. Hakika hadhaririki uliye mfanya rafiki. Ni maneno aliyowaza Aisha au Mama Rehema.



    Alitoka kwenye mawazo na kuchukuwa pesa ya matumizi. Moja kwa moja hadi sokoni yeye na mtoto wake mgongoni. Alinunua mahitaji kishaakaenda nyumbani kwa ajili ya mapishi. Alipika kisha akala. Alipomaliza kula kama kawaida alienda kwa jirani yao. Mama. Suzan. Kwasiku hiyo alienda kwa ajili ya kuomba ushauri.



    Alimuelezea yote yaliyomsibu katika maisha yake. Kisha shoga yake huyo akamshauri kuwa amwambie tu david kwamba yeye ni muathirika na hata hapo alipoanatumia madawa. Kasoro mwanae ambae yeye si muathirika na hata maziwa anayotumia ni yale ya kwenye chuchu za plastik.



    Aisha aliupokea ushauri ule na usiku ulipofika aliamua kuwa mkweli kwa david. David hakuonesha kukereka bali alimuhurumia Aisha na kumuhurumia mtoto wake Rehema. Kisha akamlalamikia kwa kutokumuambia toka mwanzo lakini Aisha alimpa sababu za kuridhisha mwisho wa siku wakaendlea kuishi kwa heshma hivyohivyo kama kaka na dada japokuwa Aisha alikuwa tayari ameshampenda sana devid.



    Siku zilienda siku zikapita. Ni siku moja iliyokuwa imetulia, siku hiyo Devid alirudi nyumbani mapema sana na hakuwa amelewa lakini alikuwa ameshikiria kilevi. Siku hiyo devid alikula chakula na kujipumzisha. Aisha alijua wazi kuwa Devi atakuwa anaumwa sana. Hata alipomfuata nakumuulizia juu ya kuwahi kuja nyumbani kwa siku hiyo. Yeye alijibu kuwa ni mawazo tu.



    "Hivi kaka! Wewe kwanini sijawahi hata kukusikia ukimuongelea wifi yangu hata siku moja?" Ni swali lenye mtindo wa kichokozi kutoka kwa Aisha.



    Devi alicheka sana kisha akainuka na kushikiria chupa ya bia na kuibusu, "Aisha mke wangu mimi ni pombe ambae wewe unamuita wifi." Ni majibu yaliyosisimua nywele za Aisha. Hapo akajawa na shauku ya kutaka kujua kwanini Devi amemjibu hivyo. Alitega sikio lakini devi muda huo alikuwa kimya. Ukimya ulipozidi ndipo Aisha akaamua aulize swali la kuchombeza iliajuzwe zaidi.



    "Kaka, mbona upo kimya. Hebu niambie kwanini unasema kwamba wewe mke wako ni pombe?." aliuliza kisha akakaa mkao wa kula iliapate majibu. Lakini chakushangaza Devid alifungua kifuniko chabia kisha akapiga funda kama tatu hivi halafu aka hema kwa kwa nguvu na kusema.."Dada yangu. Mwanamke, ukiwanae atakupa mawazo lakini kamwe mke wangu pombe huwa hanipi mawazo. Mwanamke atakusaliti lakini kamwe mke wangu pombe hajawahi kunisaliti. Pombe hunipa starehe ya nafsi na moyo lakini mwanamke ataiumiza nafsi na kuuchakaza moyo wangu kwa maumivu muda wote. Naipenda sana pombe." Aliposema maneno yale hapohapo akafatia kwa kulibusu chupa la bia.



    "Hapo kaka nakupinga. Hivi we.. Unaona ni bora ukauwe figo bandama sijui mapafu na hata utumbo kupitia kilevi kisa unaogopa kuumizwa. Aaah! Hapo umepotea." Aliongea Aisha huku akimtoa mtoto mgongoni na kuchukuwa chuchu iliyokuwa na maziwa kisha kuanza kumnywesha.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Aisha.." Aliita Devid kisha aisha akaitika kiupole huku akiendlea kumbembeleza rehema ambae kwa muda huo alikuwa hataki chochote zaidi ya maziwa tu.



    . "Najua itakuchukuwa muda sana kunielewa lakini yaliyonikuta katika maisha yangu. Ndio yaliyonipelekea kuipenda sana pombe," Alitulia kidogo Devid kishaakainamisha kichwa chake chini alitumia sekunde kadhaa kisha akainuka. Uso mzima tayari ukawa umelowa kwa machozi. Hapo Aisha akagundua kuwa huenda maneno yake yamemkumbusha mbali sana, hakutaka kuongea akamuacha Devid akiendelea na machozi yake.



    "Aisha.. Ndani ya hii dunia kuna mambo mengi sana ambayo yamejificha na hayaonekani mbele ya wengi. Huwatokea wachache tu na kutengeneza historia ngumu za maisha yao. Yote hayo ni mapito tu.



    Mimi leo ninaishi kwenye haka kajumba kabovu na kachafu lakini jana sikuwa hivi. Kila nikiikumbuka jana yangu hapo ndipo naona ni bora nilewe tu. Labda kuna kitu hujui Aisha.. Mimi zamani sikuwa nakunywa pombe, sikuwa najenga nyumba kama kibarua bali nilikuwa kijana mtanashati tena mstaarabu lakini. Dah! Hebu ngoja nikusimulie ili unielewe vizuri...." Palepale Devid akaanza kusimulia.



    ** ** **



    "Mwanangu... Mimi ma'yako umri umenitupa mkono na hitaji nicheze na wajukuu wangu. Lakini wewe kila nikwambiapo swala la kuoa unabadilika na kuwa mkali. Kwanini lakini mwanangu?" Ni sauti ya Ma'Devi ambae sasa alionesha kuchoshwa na tabia ya mwanae. Ni mwanae wapekee hakuwa na mtoto mwingine zaidi yake hivyo alikuwa anahitaji angalau mjukuu kwakuwa umri wa Mama huyo tayari ulikuwa umekwenda. Devid ambae kwa muda huo alikuwa mwalimu kwenye moja kati ya shule huko Chato mkoani Kagera. Yeye hakupenda kabisa kusikia habari za wanawake na wala hakuhitaji mwanamke kwa kipindi kile kutokana na kiapo alichojiapisha cha kutokupenda tena. Ni matatizo ya kimapenzi yaliyomfanya asihitaji tena mwanamke. Kila akikumbuka kipindi bado yupo mwanafunzi katika shule ya sekondari Buselesele aliishia kupinga kauli ya mama yake iliyomtaka aoe.



    "Mama. Mie sijapanga kuoa kwa muda huu. Labda miaka kadhaa ijayo. Pia nadhani unajua suala lakuoa sio la kukurupukia mama yangu. Inabidi nitulie ilinitazame yupi atakae nifaa."



    "Wewe mtoto ni mjinga sana. Nimeshakwambia nahitaji mjukuu. Hivi unadhani hiyo miaka yako kadhaa inaweza kukabiliana na uzee niliyonao? Tambua wewe ni mwanangu wapekee. Kama mama nahitaji nipate wajukuu ambao watanifanya nipate furaha na kusuuzika nafsi. Hebu niletee wajukuu hapa. Sitakikukuelewa kabisa," Alitulia kidogo mama yule kisha akavuta pumzi nakuendelea.



    "Hebu fikiria. Kama wanawake nimeshakuletea wengi sana. Si kwasababu mimi ni Mama nisiye na adabu. Laa.. Bali nikukutaka wewe mwanangu uoe. Mpaka imefikia kipindi mimi nimechoka sasa. Sitaki kusikia upuuzi wako nachohitaji kusikia ni sauti ya mjukuu wangu. We mwanamume gani usiyependa mtoto wewe.. Sasa nakupa wiki moja, nenda kajitafutie mke wa kuoa kwasababu kipindi na kubembeleza hadi kukuletea wanawake ulikuwa ukiwakataa. Na ikipita hiyo wiki moja bila wewe kutambulisha mwanamke hapa.. Mtafute Mama yako mwingine unaemsikia nasio mimi." Aliongea Mama Devid kisha akawa anaondoka sebureni na kuelekea jikoni.



    "Lakini mamaa..."



    "Eee.ee. Sihitaji mjadala na mtoto niliyomnya mwenyewe. Nimemaliza." Aliongea Mama devid kisha akaingia jikoni na kwenda kuendelea na Mapishi.



    Devid alibakia pale sebureni huku ameshikiria remote. Nguvu zilimuisha kufuatia maneno makali kutoka kwa Mama yake. Palepale akajibwaga kwenye sofa. Mara wazo likamuijia akaona ni bora atazame video. Kila chanel aliyobonyeza aliona kama haina maana hapo akaamua kuitupa remote pembezoni mwa sofa na yeye akainuka moja kwa moja mpaka chumbani mwake. Alipofika alijitupia kitandani bila heshima ya kitanda kile kisha akaanza kuutafuta usingizi. Alimaliza nusu saa nzima bila kupata hata lepe la usingizi bali mawazo yaliyomjaa. Hapo tena akaona kitanda hakina maana akajiinua na kwenda hadi kwenye maktaba yake ya vitabu kishaakaanza kupekuwa vitabu vya kusoma. Alianza na riwaya ya Joram kiango 'NAJISIKIA KUUA TENA' amesomasoma akaona nayoinazidi kumchanganya kutokana na maudhui yaliyomo ndani yake. Hapo akakirejesha kitabu kile na kukiendea kitabu cha NYONGO MKALIA INI. Hicho hata kukielewa hakukielewa kabisa. Hakuwa na hamu ya kusoma. Taratibu miguu ikamchukua na kumpeleka hadi nje ya nyumba yao. Alipotoka nje, aliwaza wapi aelekee.. Aliona ni bora aende sehemu yenye miti mingi huenda akapata ufumbuzi watatizo lake. Taratibu akaita tax na kuelekea eneo moja alilopenda kwenda kwa ajili ya kutatua matatizo yake ya kiakili. Alipofika alisogea kwenye moja kati ya miti iliyokuwa maeneo yale na moja kwa moja akaanza kupitiwa na upepo mzuri wa maeneo yale. Ghafla mawazo yakamtwaa na kumkumbusha mambo yaliyomtokea kipindi cha nyuma alipokuwa mwanafunzi huko shule ya sekondari buselesele iliyoko Chato...



    Mawazo yalimpeleka hadi siku aliyoenda kuripoti shuleni hapo. Akakumbuka jinsi alivyopokelewa na kupelekwa moja kwa moja hadi kwenye darasa alilopangiwa.



    "How are you students?" Ni sauti ya mwalimu wa darasa la kidato cha kwanza ambae kwa muda huo aliingia yeye pamoja na devid ambaye ni mgeni kabisa. Mwalimu huyo aliongea maneno ya kiingereza yaliyokuwa na maana ya kuwajulia hali wanafunzi wale wa kidato cha kwanza.



    "We are fine.. How about you?" walimjibu kuwa hawajambo kisha wakamuulizia juu ya hali yake.



    "Am fine too" aliwajibu kuwa naye yupo sawa.



    "Ok, students. Am here inorder to introduce ur new friend. As you see here. This is ur friend his name is Devid Damson. Ok" Aliongea Mwalimu wa darasa kwa lugha ya kigeni ikiwa inamaanisha utambulisho wa mwanafunzi huyo mpya.



    Baada ya utambulisho huo mfupi David alipewa siti ya ukutani na kukaa. Kwakuwa alikuwa mgeni, hakuwa na wakuongea nae wala hakutaka kujishughulisha na wanafunzi wenzie darasani humo. Alichukuwa kalamu yake na kuanza kuandika majina ya wachezaji mbalimbali wa mpira. Alikaa na upweke mpaka ulipofika muda wa mapumziko. Hakupenda kwenda kantine hivyo alibaki darasani.



    " Sista nd'o huyu aliyekushika mkono oya.. Wewe ndo Unajifanya unajua sana sindio... Hebu sogea hapa. Unapenda sana kushobokea madada za watu ngoja tukuoneshe boya wewe." Ni sauti ya kibabe iliyokuwa ikitoka nje ya darasa alilokuwemo David kwa muda huo. David aliisikia sauti hiyo lakini alíipuuzia na kuendelea na mambo yake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Nd'o huyo. Eti kimenikuta niko na maria kikaanza kunishika mkono. Nilipokiuliza eti kikanambia kinanipenda" Ni sauti nyororo yenye dhihaka ambayo ilipendeza masikioni mwa yeyote. Ingawa muongeaji aliitoa kwa dhihaka lakini ndio kwanza sauti yake iliendelea kuwa nzuri. Anaitwa Irene ni msichana mrefu kidogo modo, mwenye sauti ndogo halafu iliyo nyororo haina mikwaruzo hata pale alipolia iliongezeka na kuwa nyororo zaidi. Macho yake ya aibu ambayo hayakuwa na uwezo wa kuhimili kuangaliwa kwa sana pasina kuzileta kope zake ndefu kuyafumba, ndiyo yalikuwa kivutio kizuri zaidi na kuwapelekea vijana wengi kumdai moyo wao. Naam, ingawa ni modo lakini nyonga zake zilitanuka vizuri na kuwakilisha umbile la kibantu lililosimama, alikuwa na weusi uliyokolea vilivyo na kumfanya aonekane mrembo zaidi kulingana na umbile lake.



    "Ayaaah!... Jamani sirudii.. Yaishe tu. Tafadhali Irene naomba uniombee msamaha kwa makaka zako wataniua bure mtoto wa watu." Ni kipigo alichopewa Martin mpaka akaanza kuomba msamaha.



    Kaka wa Irene waliendelea kumshushia kisago Martin. Ukelele ulipozidi ilibidi David ambae alikuwa darasani, ainuke na kuchungulia dirishani. Alimuona Martin akiendelea kupata kisago kutoka kwa vijana Wanne ambao kwakuwa kadiria aligundua watakuwa wa kisoma vidato vya mbele. Lakini alipogeuza jicho lake pembeni kidogo nipo macho yake yakagongana na macho ya Irene ambae nae kwa muda huo aliangalia dirishani na hiyo ni baada ya kusikia dirisha limefunguliwa.



    Wanasema macho huongea tena kwa lugha yake, lugha ambayo wewe huwezi kuisikia ila moyo pekee ndio husikia lugha hiyo. Moyo wa Irene ulimruka baada ya kumuona kijana mtanashati, maji yakunde mwenye kifua chakukamata shati huku mwili wake wa mazoezi ukionekana. Sura nzuri iliyomvutia Irene, labda naweza sema na nywele za David ziliweza kuchangia maana alikuwa na nywele utadhani alidhuru uarabuni., naam.. Mapigo ya moyo yalimuenda kasi sana. Kumbe siyeye tu. Hata David naye alipatwa na kitu moyoni mwake, palepale alirejea na kukaa kwenye kiti kwa sababu David hakupenda ugomvi. Aliwachukia sana wale kaka zake na Irene ambao waliendelea kumpiga martin.



    Ni kama Irene aligundua jambo lile palepale aliwakataza kaka zake wasimpige jamaa yule. Kisha akatoka pale huku anakimbia moja kwa moja hadi kwenye darasa analosomea. Alipofika alikikimbilia kiti chake na kujilaza moja kwa moja huku mawazo yakile alichokiona yakiwa yamemjaa.



    Siamini... Bado sina uhakika kama kuna binadamu mzuri kiasi kile. Mmmh! Kweli kila shetani ana mbuyu wake. Alijisemea maneno yale huku fikra zake zikimrejesha pale alipokutanisha macho yake na macho ya David kisha hapohapo Moyo ukamdunda.



    Mmmh! Nimepatwa nanini leo. Mbona moyo wangu umekuwa hivi? Na mbona macho yangu yanatamani kuendelea kumuona yule kijana? Mungu wangu. Hadi mikono yangu inatamani kumpapasa kijana yule. Mh! Mh! Mh! Sijui uonjwa gani umenipata. Alijisemea tena Irene huku akiweka taswira ya David pamoja na jinsi anavyojisikia.



    Labda kwakuwa Irene hajawahi kupenda ndio maana hakugundua kuwa kwa muda huo alisumbuliwa na mapenzi. Au labda kwakuwa hajawahi kuwa na mpenzi ndio maana hakujua nini kilichompata...





    Ulifika muda wa darasani wanafunzi wote walirejea kwenye madarasa yao. Irene alisoma Kidato cha kwanza pia lakini mkondo ulikuwa tofauti na ule wa David. Aliingia mwalimu wa kiingereza darasani mwa kina Irene. Siku hiyo Irene hakuonesha uhusika mzuri darasani kama ilivyo kawaida yake. Alikuwa mtulivu na muda mwingi alijiinamia tu. Masomo hayakupanda kabisa mpaka wanafunzi wenzake ambao wamemzoea kama kina maria wakahisi huenda Irene akawa na matatizo.



    "Irene leo wewe ukoje? Unaumwa! Mbona umepooza hivyo." Ni swali kutoka kwa rafiki yake Maria.



    "Mmmh! Maria.. Nahisi kuna kitu kimeingia mwilini mwangu. Yaani.. Hata sijielewi. Kiufupi siko sawa Mary."



    "Mhhh! Pole sana. Basi twende nikusindikize ukaombe ruhusa iliuende nyumbani kupumzika."



    "bora.. Maana sijisikii kufanya chochote. Hebu nisindikize tukaombe ruhusa." walichukuwana kisha wakaenda moja kwa moja hadi ofisini na kuomba ruhusa. Mwalimu wa darasa alitoa ruhusa kisha akampatia kibari Maria iliaweze kumsindikiza mwenzie kwa baiskeli maana kutokea shuleni hadi mjini kuna kaumbali kidogo.



    Walifika nyumbani kwa kina Irene kisha Maria akarudi shule kwa ajili ya kuwahi vipindi vya mchana. Huku nyuma Irene alijibwaga kitandani kwake baada ya kuwasalimia wakubwa zake waliyokuwa nje.



    "Vipi mbona umerudi mida hii. Au umeburuzwa mboko huko shuleni eti."



    "Hapana dada. Sikofresh tu. Nimeona bora nije kupumzika nyumbani tu.



    "Mhhh! Haya mdogo wangu pole. Lakini... Nini hasa kinachokusumbua?"



    "Kichwa dada."



    "Kichwaa!? Kimesababishwa nani hicho kichwa"



    "mmmh! Mi ata selewi. Nimeshangaa tu kinaanza kugonga." Akatoka dada yake chumbani mwao na kuelekea sebureni kufuata dawa. Ile anarudi akashangaa kumuona mdogo wake anafurahi na kujitwika matabasamu hadi anaushika moyo wake huku akiongea maneno ya chinichini ya kumsifia yule kijana aliyemuona kule shuleni.



    "Irene.. Umependa! Wewe utakuwa umeangukia kwenye mapenzi mgonjwa wa kichwa hayupo hivyo mdogo wangu. Achakunidanganya. Sema tu ukweli umependa?" Kauli ile kutoka kwa dada yake ndiyo ilimgutua kwenye furaha yake na kumfanya agundue kumbe tayari dada yake alikwisha ingia ndani mule."



    "Ndio..! Hap..hap.. Hapana...!! Si... Sij.. Sijui.. Hapana dada sijapenda" Oooh. Irene alishindwa hata kujitetea na kubaki akijiumauma na kuzalisha vigugumizi visivyokuwa na faida. Kwa hali ile dada yake alikuwa tayari ameshagundua kuwa Irene anasumbuliwa na ugonjwa wa mapenzi. Alimpa ushauri na kumsii mambo kadha wakadha, kisha akamjaza sumu zakuwachukia wanamume na kumfunza jinsi ya kuwaona kama picha.



    Ni kama alikuwa anachukua maji na kuyamimina ndani ya kinu kisha anachukuwa mchi na kuyatwanga. Tayari Irene ameshapenda. Hakuna alichosikia wala kuweka akilini. Si kwanguvu zake bali kwa nguvu za mapenzi.



    Siku baada ya siku Irene alianzisha na kukomaza mazoea na David. Kwakuwa mapenzi hayana siri. Walijikuta wakizaa penzi tamu lenye mazoea. Kaka zake na Irene walipiga hadi wakachoka lakini David aliwaambia hawezi kumuacha Irene hata wakimuua.



    Walishawahi kumtoa mpaka alama za kudumu lakini hakukata tamaa. Walimuacha. Miaka ikasonga hadi walipofika kidato channe, alikuja mwalimu mgeni. Mvaa mavazi ya kisasa. Mwanzoni alipoanza kumtongoza Irene. Basi irene alimwambia mpenzi wake David. Lakini mwishoni Irene alishindwa kuviepuka vishawishi vya teacher na kujikuta anamsaliti David. Sasa penzi likawa kizaazaa. Irene akaanza kuzoea maneno ya David na kwakuwa mazoea nimabaya basi akajikuta hapati athari na kuanza kutamani ladha. Alianza kujitongozesha kwa wanamume huku usiku akienda kusoma kwa teacher. Tabia ile iliendelea mpaka siku moja David akaja kumkutaniza Irene geto kwa mshikaji wake. Na hata alipomuuliza. Irene akawa mbogo na kumkana David ambae kwa muda huo alikuwa ameshapenda. Hapo sasa ndipo davi alipoyapata Maumivu. Aliporomoka kimasomo, mwili ulimkonda huku akiendlea kumuomba Irene msamaha utadhani yeye ndiyo mkosaji. Mara ya mwisho davi alipewa ushauri na Rafiki kisha akajazwa sumu na kujikuta anawachukia wanawake. Akaweka wanawake pembeni na kukaza. Alianza kupanda kimasomo na hata mtihani wa kidato channe ulipofika alifanya mtihani vizuri. Matokeo yalitoka na kuruhusiwa kuendelea. Huku Irene matokeo yake yakawa mazuri lakini alishindwa kuendelea kutokana na kujazwa mimba. Aliondoka zake na asionekane tena. Na kwanzia hapo David hakutaka maswala ya kuwa na msichana tena.



    ...... ........

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kumbukumbu zile zilimtoka na akaanza kuyafikiria kauli ya Mama yake. Kauli ya Amri iliyomuamrisha aoe. Alichoka na kukunja ngumi kisha akakipiga kichwa chake mara kadhaa.



    "Kweli.. Kama maisha yapo mazuri. Kuishi na mke ninaweza. Kulea mtoto ninaweza. Kazi ninayo tena ya ualimu. Sasa kwanini nisioe. Eti.. Kisa Irene. Aaaaah! Nisiwe mjinga kiasi hiki! Aliyenitenda ni mmoja kwanini niichukie dunia nzima? Huenda alinitenda kwakuwa sikuwa na kazi. Je, leo nitatendwa? Hapana.. Haijalishi niliapa nini.. Inabidi nimletee Mama mjukuu......."





    "wajukuu watakao mfanya mama yangu asiujutie uzee bali afurahie kwa kutaniana nao. Ndio.. Nimeamua kuoa. Lakini!... Nitamuoa nani?" alijisemea Dev kishaakaendelea kutafakari zaidi juu ya mwanamke wa kuoa.



    Mpaka jua linazama devi alikuwa bado hajapata jibu sahihi la kuhusu mwanamke atakae muoa. Aliamua kurudi nyumbani kwakuwa giza lilianza kuingia. Alivyofika ndani alimkuta mama yake amenuna. Naye akajifanya hajui kinachoendelea, akachukua chakula na kula hiyo ni baada ya kuoga. Alipomaliza yote hayo alienda kupumzika. Akiwa kitandani amelala mara ghafla simu yake ikaita. Akaichukuwa alipoiangalia kwenye kioo ilisomeka namba ambayo haikuwa na jina kisha akaipokea.



    "Hello" sauti ya upande wa pili iliongea hvyo.



    "Ndio. Samahani sijui nani mwenzangu?" Hiyo ni sauti ya Devid na hiyo ni baada ya kusikia sauti iliyomvutia zaidi kutoka upande wa pili.



    "Naitwa Rose. Ni dada wa katalina anaesomea shule unayofundishia wewe."



    "oooh.. Katalina. Nimempata. Enhee! Ulikuwa unashida gani dada yangu?"



    "Mmmmh! Nilikuwa nashida ya kuonana nawe iliunipe maendeleo ya Katalina kwa hapo shuleni. Siunajua tena hawa watoto wanahitaji uangalizi sana."



    "Ok. Mr.Rose, kwakuwa leo ni jumapili. Hebu jitahidi kesho ufike shuleni ilinikupatie maelekezo vizuri."



    "Sawa teacher.. Nitashukuru sana."



    "ok.. Nakutakia usiku mwema."



    "Nawe pia"



    Rose akakata simu kishaakaiweka kitandani. Huku nae Devid akaitoa simu sikioni na kubaki anaitathmini namba ile. Aliiangalia kwa muda kidogo mpaka akajikuta ameikariri kisha akalala.



    Asubuhi ilipofika alijiandaa na alipomaliza alikunywa chai na kumuaga mama yake na kwenda moja kwa moja shuleni. Alipofika akasaini kishaakaanza majukumu yake. Vipindi vilipoanza yeye alienda madarasani nakufundisha. Hata ulipofika muda wa mapumziko alitoka hadi ofisini na kuchukua kiti huku pembeni mwa meza yake kukiwa na chakula. Alikichukuwa na kukiweka mezani kisha akakianzishia mashambulizi. Akiwa kwenye shughuli hiyo pevu ya ulaji alisikia simu yake inaita na hata alipoangalia namba aliigundua hapohapo akaiweka sikioni baada ya kuipokea.



    "Teacher. Mie nimefika."



    "ok.. Nimo ofisini tayari. Wewe ulizia tu ofisi ya taaluma kisha uingie."



    "Sawa teacher"



    Rose akakata simu kisha akaulizia ofisi ya taaluma kwenye kundi la wanafunzi kadhaa waliyokuwa wakipata vitamin d.



    Alipata maelekezo na moja kwa moja akaingia ofisini. Alimkuta teacher Devid ingawa teacher devid alikuwa hamjui Rose lakini hakushindwa kumuhisi pindi tu alipoingia ndani ya ofisi.



    Macho ya walimu wote wa kiume yaliyokuwa bize na madaftari. Yalitupa miale mwilini mwa Irene ambae alikuwa amevaa mavazi ya kisasa yaliyomkaa vilivyo. Umbo lake lilijichonga utadhani namba nane, hakuonesha kununa bali tabasamu lililopambwa na lipstick iliyomfanya aonekane mrembo zaidi. Walimu walijikuta wakishindwa kuandika wala kuandaa hints za kufundishia vipindi vya mchana kwa muda huo wakabaki kuushanga uzuri na urembo wa rose aliyepambika kwanzia sauti hadi mavazi.



    "Mr. Devid?" aliita Irene na kumgutua mwalimu devi ambae ni kama alikuwa mbali kimawazo pindi alipomuona tu dada yule.



    Mawazo ya kichwa chake yalimuijia kuwa. Ati, ameshamtongoza Irene na wakakubaliana kuoana kisha akaenda kumtambulisha nyumbani na ndoa ikapita. Baada ya ndoa walikaa mwezi mmoja na Rose tayari akawa na mimba yake miezi tisa ilifika nao wakapata mtoto wa kiume ikawa nifuraha. Akiwa katika mawazo hayo ndipo aliposhtushwa na sauti nzuri ya Rose.



    " Yes. Ndio mi...mimi." alijibu teacher Devid bila kuamini kama ni kweli amuonae mbele yake ndio yule msichana wa kwenye simu. Alikoswa pozi lakini akajitutumua kiume iliasioneshe paniki ambayo tayari alikwisha ipata. "bila shaka. Wewe ndio Rose. Dada wa Katalina?" kwa tabasamu Rose akajibu huku mkono wake mmoja akiushikisha kwenye meza ya mwalimu huyo ilikutengenza pozi. "Ndio mwenyewe wala haujakosea."



    "Ok, karibu sana. Jisikie amani. Mmmmh! Nipe dakika mbili nichukuwe viti nipeleke pale kwenye mti ilituweze kuongelea huko." Aliongea Devid. Rose hakuwa nakipingamizi alikubali.



    Devid alichukuwa viti viwili na kuwaomba radhi walimu wenzake kishaakaenda kuvitua karibu na mti ule uliokuwa na kivuli pamoja na upepo mwanana.



    "Mrs. Rose.. Nilikuwa nikijaribu kupitia baadhi ya mitihani ya nyuma inayomuhusu katalina, pamoja na kukagua madaftari yake na vitu kadha wa kadha. Takwimu inaonesha kuwa maendeleo ya Katalina yanaridhisha naam. Sio mabaya. Lakini mtoto huyu anasumbuliwa sana na utundu wa hapa na pale. Mara utasikia kachana daftari la mwenzie mara kajichafua na wino, mara ameumia.. Ilimradi tu utundu utundu basi. Ila kitaaluma anajitahidi sana. Chamuhimu mie ninawashauri mumpeleke awe anasoma masomo ya ziada kwa ajili ya kuifanya akili yake iwe imara na bora zaidi, aidha.. Kumkanya apunguze utundu wake." Aliongea mwalimu Devi huku akipatapata shida ya kulikwepa tabasamu zuri la Rose iliasiharibu kazi. Lakini mara kadhaa alishindwa kuliepuka.



    "Sawa Mwalimu mafanikio ya katalina yapo mikononi mwenu kama walimu wake. Kama walezi tunashukuru sana kuona mnavyotusaidia jukumu hili zito la kusimamia taaluma mpaka nidhamu. Kuhusu masomo ya ziada usijali swala hilo. Pia usijali kuhusu utundu utundu wake. Tutajitahidi kumkanya tu na nina imani kwa kushirikiana nanyi. Katalina atakuwa mwanafunzi mpole na mwema asiyependa makuu. Otherwise thank you." Aliongea Rose na mwisho wa kaulizake akapiga lugha ya magharibi ikimaanisha shukurani tu.



    "Usijali Rose huo nd'o wajibu wa kazi yetu. Kuhakikisha mwanafunzi anakuwa sawa." Aliongea Devid huku akiyasumbua macho yake mara ayatupie kwenye sura ya Rose, mara kwenye kifua, mara kwenye umbo la ujumla ilimradi tu apate taabu. Kila Rose kwa kutumia mapozi ya kichokozi nae hakuwa nyuma katika kuhakikisha anamteka Devid kimawazo.



    Ni fulu utamu wa aibu machoni mwa Devi. Alijitahidi kuyazuia macho yake yasiangalie mapaja mazuri ya Mrs. Rose ambayo yalikuwa yamejiweka kihasara. Lakini alishindwa kukabiliana na sumaku ya mapaja yale. Mara ghafla mwili wote wa Devi ukamsisimka. Mawazo yakamchukuwa na kumpeleka mbali sana.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Baby... Hakika wewe ndio kila kitu kwangu. Wewe ndio Asali wa moyo wangu. Hivyo nakuomba ufanye moyo wangu upate tiba kupitia wewe. Usije hata siku moja kuutupa kwani utaufanya utapetape bure na mwisho kupotea kabisa. Tafadhali endelea kuvaa vazi hilo la uaminifu na usije kulitupa." Ni sauti ya Rose siku ambayo alikuwa yupo kwenye kifua cha Devid. Na hiyo ni baada ya kutalii utalii wa ndani kwenye maeneo kadhaa ya mwili wa devi.



    "Furaha yangu ipo ndani yako. Sina chakusema zaidi ya kuyatunza uliyoniambia. Najua unanipenda tena sana tu. Nami sitotumia upendo wako kama gereza la mateso balinitaendelea kuutumia upendo wako kama nchi ya furaha kila siku iitwayo leo." Aliongea maneno yale Devid huku akitalii kwenye mashavu ya Rose.



    Mawazo yaliendelea kumsumbua na kumpeleka mbali zaidi. Muda wote huo Rose alikuwa akimuita Devid bila mafanikio. Alichokiona usoni devid ni tabasamu pekee. Alivyochoka kumuita hapo akajitoa kwenye pozi lake na kuchukuliwa na mkono wake kisha akautuwa begani mwa devid kishaakaanza kumuita huku akisaidizana na mkono. Ndipo Devid aliposhtuka na kushangaa kuiona sura iliyokuwa ikimliwaza muda kidogo ipo mbele yake. Bila hiyana wala uoga aliamua kuongea palepale.



    "Mrs. Rose. Kwakweli toka nikuone. Ni kama kuna kitu kimeukumba moyo wangu na kituhicho ni upendo. Hakika umeyatwaa mawazo yangu na kila uongeapo, uniangaliapo hata ugeuzapo pozi mbele yangu mwenzio na kosa raha. Nakuomba uwe wangu haijalishi kwa sharti lolote lile hata kama litahusika kuuweka rehani uhai wangu mimi nitafanya hivyo bila kipingamizi. Uzuri wako utatoshakabisa kutambua kwanini nakupenda hivyo sitegemei swali la namna hiyo. Tafadhali naomba unipokee." Kumbe Devid ni kama alimuwahi Rose maana naye alihitaji kuyanena yaleyale lakini aliona aibu tu. Na ndio maana alitumia sana vishawishi ilikujaribu kama angalau angeweza kumteka kimapenzi. Bila ajizi alisema kuwa, lengo lake kubwa mpaka kuja hapo shuleni sikwa ajili ya katalina bali ni kwa ajili yake. Na akaiongelea mara ya kwanza kuonana na Devi. Ilikuwa ni siku ambayo Katalina alikuwa anaumwa hivyo Rose akaenda kumuombea ruhusa hata alipoulizia mwalimu wa darasa ndipo alipoambiwa yupo bize. Ni kweli alikuwa bize lakini ubize wake haukumfanya Rose asimuone japo yeye hakumuona. Kwakuwa alikuwa na haraka aliamua kuomba namba za mwalimu yule kwa waalimu wenzie waliyokuwa nje ndipo walipompa. Lakini anasema kuwa alipomuona tu. Palepale alimpenda na ndio maana amefanya njama mpaka akapata kuonana naye. Devid alitumbua mimacho kama mjuzi aliyebanwa na mlango kwa kushangaa mambo yale. Palepale alianzisha penzi jingine kati yake na Rose. Mara kadhaa alitoa tahadhari huku akiichukuwa historia yake ya nyuma ya mapenzi ya usaliti kati yake yeye na Irene kama rejea ya tahadhari. Penzi lao lilichanua na ndani ya siku tano. Devid alienda kumtambulisha mpenzi wake nyumbani kwao. Mama yake alifurahi sana na kumsii mwanae aoe kama kweli huyo ndiye chaguo lake.



    Naam.. Mwezi uliyofuata watu walikula pilau na nyama huku wakisherehekea ndoa ya Mr. And mrs. Devid. Walikula kiapo cha kutokuachana mpaka Mungu atakapozichukuwa roho zao. Watu waliyohudhuria ndoa ile walikenua meno yao mara kwa mara kutokana na shamlashamla za hapa na pale. Vijana wa kisasa wanasema ati fulu shangwe tu. Na ndivyo ilivyokuwa siku hiyo.



    Naam.. Rose na Devid wakawa mke na mume. Wakaanza kuishi maisha yao rasmi. Maisha yalikuwa mazuri ndani ya mwezi mmoja ila yalianza kuingia doa baada ya mwezi huo kupita.



    "Chanzo cha mabadiliko hayo yasiyopendeza ni mkewangu kipenzi. Hakika alitenda mambo mazito ambayo sitoyasahau katika maisha yangu. Mambo ambayo yalinifanya mie niwaone wanawake hawana maana na kuamua kuioa pombe." Aliongea Devid huku uchungu ukiwa umemjaa kwa muda huo. Aisha alikuwa na shauku ya kutaka kujua nini Devd alichotendewa haswa.





     "Rose, nyie wanawake ni kama maua. Hunyauka tu hata kama mlianza kwa kupamba vipi. Nakumbuka kipindi hicho mke wangu alianza..."

    * * *



    Mke wa devid ambae ni Rose. Alianza kufura kwa hasira kila siku bila sababu za msingi. Akawa ni kama anamchukia mumewake. "Wewe mwanamume. Njoo uoshe vyombo. Mimi nataka kupumzika."



    "Lakini mke wangu... Hapa siumenipa kazi ya kudeki? Mbona hivyo baby?"



    "We mwanamume mbona mvivu sana. Hivi unategemea chai utapika muda gani kama tu kudeki unachelewa. Haya, hayo mavyombovyombo utaosha sangapi. Bwege wewe.."



    "Mmmh! Basi mpenzi. Usikasilike nitafanya yote kwa haraka zaidi. Basi eti."



    "aah! Hebu niache huko. Nani unamshika na mamikono yako hayo mabaya."



    "Lakini mke wangu. Kwani mie kukushika kuna tatizo gani?"



    Naam.. Hayo ndiyo maisha ya Devid baada ya mwezi mmoja wa ndoa. Hapo sasa akawa anachelewa kazini kutokana na kuchoka, akirudi nyumbani kutoka kazini. Mara afue, mara apige deki, mara aoshe vyombo, amtengee mkewe maji ya kuoga. Huku mke wake akibadili mapozi kwenye televisheni. Sio tu sebureni na nje. Bali hata chumbani mchezo wa ubabe uliendelea.



    "Hebu niache...! Unanishika nini..? Kwahiyo kama mkeo?"



    "Lakini mke wangu Rose. Hilo jambo sini haki yangu kama mumeo mbona unanifanyia hivyo jamani... Hebu tazama. Ni miezi mitatu sasa imepita bila wewe kunipa haki yangu. Huoni huo ni uonevu." Aliongea Devid huku akijisogeza na kujaribu tena kulifakamia umbile la mke wake.



    "Haki haipo kwako. Bwege mkubwa wewe. Muone kwanza. Wewe humu ndani nimfanya kazi. Hujaoa wewe allaaah. Shika adabu yako juha wewe." Aliongea Rose tena bila hiyana. Hakuishia hapo akasema tena. "hebu kwanza shuka chini utandike hapo maana unanitia kinyaa. Sitaki hata kukugusa. Shuka chini!! Mbweha wewe.." Nae Devid hakuwa na jinsi zaidi ya kushuka chini kisha akalala. Na huo ndio ukawa mwanzo wa Devid kulala chini.



    Siku hadi siku zilipita hatimae mtafaruku huo ulifika hadi miezi nane. Devid aliendelea kufanya kazi za nyumbani huku mkewake akiendelea kutumbulia macho televisheni. Usiku Devi alishindwa kuvumilia. Kama utaniakauanza mchezo wa kujichua uume wake. Kwa lugha ya magharibi wanaita 'masterburtion' ila kwetu sisi hutumia lugha ngumu kidogo. Kumradhi sitoitaja lugha hiyo. Lakini ndohivyo. Kujichua uume wake ukawa ndio mchezo wake kila usiku aliingia bafuni na mafuta kishaanavuta hisia na kuanza kufanya mapenzi na mkono wake huku akiiangalia picha ya mke wake. Mara kadhaa mkewe alishamkuta Devid akihangaishwa na penzi hilo. Lakini hakuna msaada aliyompatia zaidi ya kumcheka tu.



    Masikini Devid aliuzoea sana mchezo ule na akaupenda sana. Hapo sasa akawa kila muda anapoenda kuoga lazma ajichue. Akimuona tu mke wake hisia zinampanda kuyafakamia mafuta. Mke wake aliendelea kumuona mume wake akitaabika.



    Mama ndio kila kitu kwa mtoto. Mtoto hakui kwa mama hata siku moja. Kwakuwa mtu pekee wa karibu kwa devid alikuwa ni Mama yake hivyoaliamua kufunga safari na kwenda kumwambia mama yake. Mama alimpa ushauri wa kuvumilia kishaakamsihi kwamba amtegemee Mungu maana yeye ndie muweza wa kila jambo. Liwe kubwa liwe dogo hata lawastani.



    "Sawa mama nimekuelewa" Aliongea Devid. Lakini katu hakuuongelea ule mchezo wake wa kujichua mbele ya mama yake.



    "Hivi wewe Rose.... Mbona mumeo anakupenda, anakujali, anakuheshimu. Hakuna unachotaka ukakosa. Sasa iweje wewe humpatii haki yake na huu na ni miezi kadhaa sasa tangu uanze kumsumbua." Rose alikuwa ameinama muda wote. Kisha akajiinua huku amelowa uso wake na machozi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mama.. Mimi nampenda mme wangu. Lakini yeye hanipendi. Mara zote amekuwa akinipiga, akinitesa kwakuninyanyapaa. Hata sasa halali na mimi. Yeye sikuhizi analala chini tu. Nikimuuliza kwanini. Ananijibu majibu ya chooni. Lakini sikweli kwamba mimi namtesa mume wangu Devid. Nampenda sana na ndio maana nimeamua kuolewa nae. Mamaa namp... " Ni kama alishindwa kuendelea kuongea kutokana na kilio kile kilichozaa kwikwi hadi Mama devid akamuhurumia mwinga wake huyo ambae alionesha kabisa dhahiri kuwa Mumewe ndio anaemtesa. Kwakuwa kilikuwa ni kikao. Basi devid nae alikuwepo. Lakini muda wote alikaa kimya kwani hakuwa na sauti mbele ya mke wake.



    Ukimya wake ulitafsiriwa kuwa.. Ameumbuka, au amedharau maongezi yale. Na mwisho wa kikao yeye akawa na makosa.



    Alionywa kutokumpiga mke wake. Kikao kile kilichobeba wazazi wa pande mbili kiliisha kwa mawaidha. Kisha waliondoka wazazi na kuwaacha wana ndoa wale.



    "We mwanamume juha wewe.. Hivi kwa akili yako ulidhani kuwa utanishinda mimi eti! Sasa nakwambia hivi hiyo sijui haki yako hupati. Na mwendo wa kufua tu. Hapa bwege wewe... Allaaa." Aliongea mke wa Devid na hiyo ni baada ya kuyafuta machozi ya kinafki.



    Devid.. Mawazo yakamjaa. Alijiona kama mtuhumiwa. Hakuwa na msaada kwenye kesi ile ngumu ya kuhujumu maisha yake. Akaanza kukonda kutokana na mawazo. Hata shuleni alijaza barua za ruhusa ndani ya ofisi ya headmaster.





    . Devid hakuiacha ile kazi yake ya utumwa. Kila siku aliosha vyombo, alifua nguo za kwake pamoja na za mke wake, halafu kama kawaida usiku hakulala kitandani bali alitandika chini iliasimuudhi mke wake.



    " Eee Mola wangu. Ulisema hutomdhalilisha uliyomfanya rafiki. Na wala hautompa pumziko uliyemlaani. Pia niwewe huyohuyo ambae ulisema kuwa tuombe nawe utatupa. Basi mie nakuomba mbadilishe mke wangu mpendwa na umuongoze. Mpe utambuzi wakujua kwamba atendacho si sahihi na wala hakifai. Mfanye atambue kuwa mimi ni mmewe. Kumfulia nguo, kumpikia, na hata kupiga deki hizo si kazi zangu. Mke wangu kawa mkali zaidi ya mbwa wa polisi. Siwezi kumkanya kwasababu naogopa asijekuniacha ilhali bado na muhitaji. Nakutegemea wewe mwenyezi-Mungu. Naomba umfungulie njia mke wangu na umfanye aelewe kuwa atendacho si sahihi kwangu. Aamin." Ni kawaida ya Devid kumuombea mke wake kabla ya kulala. Muda huo Devi amuombeapo mke wake kumbe nae mke wake huomba kwa Mungu huyo huyo..



    "Najua Mungu unanisikia. Sina kimbilio zaidi yako, nakuomba kwa neema zako niondolee huu mzigo. Nimeshafanya kila njia ilikumfanya mwanamume huyu aniondoke, mambo mengine ni magumu. Kila siku namfulisha nguo, nampigisha deki kwakudhani kuwa huenda atanisikia lakini nd'o kwanza anafanya yote nimwambiayo. Ee mola wangu. Nafsi yangu inaniuma mimi.. Japo nafanya mambo utadhani napenda lakini... Sikweli kwamba mie napenda kulala kitandani peke yangu kisha kumlaza mwenye kitanda chini. Laa. Nafanya hivyo ilikumchokoza iliakasirike na kunifukuza lakini ndio kwanza. Hata mawazo anaonekana hana. Kiukweli mimi simpendi mume wangu. Ila niliamua kuolewa nae baada tu ya kupewa pesa na Mama mkwe. Ni maradhi yapesa: upendo wangu ulikuwa kwenye pesa za Mama yake. Lakini yeye hakuwa moyoni hata kidogo. Nami nahitaji furaha yangu. Nimempata ninaempenda hivyo najitahidi kufanya visa ilianiache lakini ndio kwanza hata hanieldwi. Tafadhali nakuomba niondoe kwenye mateso haya mie nilihadaika na pesa tu. Lakini sikuwa na mapenzi kwake. Nakuomba mfanye atambue kuwa simtaki. Aaamin." Ni maombi ya Rose kabla hajalala.



    Wote kwa pamoja hulala baada yakuwa wameomba hivyo.



    Mke wa Devid akaanza tabia ya kwenda disko na kurejea usiku wa manane lakini devid alimfungulia hivyo hivyo bila kuonesha chuki ingawa nafsi haikupenda mambo yale. Lakini aliogopa kumkanya mke wake kwa kuhofu kuharibu ndoa.



    Mke wa devid alipoona kuwa devid hana hata dalili ya kumuacha. Hapo sasa akaamua akodi mwanamume mwenye miraba minne kisha akamleta nyumbani na kumuingiza chumbani anapolala yeye na mumewe. Akaona kumuingiza haitoshi akaamua kumruhusu mwanamume yule auingilie mwili wake. Wakafanya ufuska wao juu ya kitanda alichonunua devid kwa mshahara wake aupatao kutokana na kazi yake ya ualimu. Kama hiyo haitoshi wakasinzia palepale huku wamewekeana mikono. Devid alipotoka kazini alishangaa kukuta mlango upo wazi halafu mke wake hayupo kwenye televisheni. Kwakuwa alikuwa amechoka aliona asijali sana na moja kwa moja alichukuliwa na miguu yake hadi chumbani.



    Devid.. Alishindwa kuyaamini macho yake baada ya kuona jitu lenye miraba minne limemkumbatia mke wake. Tena kwenye kitanda alichonunua kwa pesa yake mwenyewe. Alikuwa ameshikiria kisanduku chake kidogo lakini mikono yake ilikosa nguvu nakujikuta amekiachia hadi chini. Hapo akili yake ikamtuma awavagae wawili wale na awape adhabu ilinganayo na maumivu aliyonayo.



    "Nyie wapuuzi. Mmekosa gesti. Mpaka mmeamua kufanya ujinga huu ndani ya nyumba yangu tena kwenye kitanda changu. Halafu wewe mgoni wangu.. Hukujua kuwa huyu ni mke wangu?"



    Hapo devidi akachukuwa pombe yake akanywa tena kisha akamfunulia Aisha shati na kumuonesha upande wa kushoto wa kifua chake. "Aisha... Hili kovu unaloliona. Si kwamba nilienda vitani kupigania nchi yangu. Hapana.. Ndio maana nilikwambia kuwa. Bora mke wangu pombe yeye hunipa raha na katu hanisaliti." Kisha akaendelea na historia ile...



    * * * *



    Lile janaume laana kabisa lile.. "Ndio ni mke wako. Lakini mimi huyu ni mpenzi wangu. Na kuhusu suala la kulala... Aliamua tu kunileta hapa nyumbani kwake kwakuwa alilalamika kuwa wewe huwezi kukitendea haki kitanda chako. Mie nipo hapa kwa ajili ya kukirudisha kwenye hadhi..." Akadakia mke wangu Rose. Huku akimtomasa mgöni wangu tena mbele yangu pasina kuhisi aibu.



    "Majuha.. Huona kila watende walo nisahihi. Na hujifanya watii wa kila jambo. Kama kukwambia nimeshakwambia hadi mdomo ukachoka. Kama kukufanya uondoke nimeshajaribu sana. Lakini umeonesha ujuha wako. Sasa kama kusikia hukusikia inamaana hata vitendo hauvioni?" Aliongea huku akinibetulia midomo yake na kunifanya nikasirike zaidi. Hapo nikawa simjanja tena wa kuzizuia hasira zangu. Mkono ukaniponyoka na kuzalishakofi lililomfuata vilivyo mke wangu. Lilimpata kiukweli ukweli hadi akaenda chini na hiyo ndio mara yangu ya kwanza kumpiga mke wangu toka nianze kuishi nae.



    Mke wangu alianza kulia utadhani nimemuonea sana..





    .. Akiwa kwenye kilio kile mimi nilijiona mkosaji sana kwa muda huo. Mara nikashtuka baada ya kujikuta nipo chini huku damu zikinitoka puani na masikioni. Nilipojiuliza kilicho sababisha mimi kuwa vile. Ndipo nilipomuona mgoni wangu ambae kwa muda ule alikuwa ameikunja sura. Nilijaribu kusimama huku nikijipepesua lakini nilisukumwa na teke lililotua vilivyotumboni mwangu na kuniweka ukutani. Nilicheua damu nyingi na kuanzia hapo nikama nililala usingizi kwani sikusikia wala kuota. Zaidi ni yale maneno ya mwisho mwisho ambayo niliyasikia kwa taabu pindi mke wangu alivyokuwa akimwambia mgoni wangu kuwa.. Imetosha wasinipige zaidi.



    Nilikuja kushtuka nipo hosipitali huku pamba zikiwa masikioni pamoja na jiraha la kisu upande wa kushoto mwa kifua changu. Nilijiuliza marambilimbili sababu ya mimi kulazwa pale ndipo nilipokumbuka kile kipigo nilichopokea baada ya kumuwasha kofi mke wangu. Nilipandwa na hasira baada ya kupapasa macho na kuona mke wangu yupo pale tena karibu kabisa na kitanda nilicholazwa huku akionesha huzuni kana kwamba siyeye aliyesababisha mie nilazwe pale. Nilijitahidi kunyanyuka kitandani pale ilinimuoneshe hasira zangu, lakini sikuweza kutokana na maumivu niliyokuwa nayo. Hapo ndipo nilipougundua udhaifu wangu mwingine kuwa sina nguvu hata za kunyanyuka pale.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Wewe muuaji unalia nini? Hebu futa machozi ya kinafki na sitaki nikuone mbele ya macho yangu. Toka hapa.. Toka.." nilijikuta nikionge. Lakini chakushangaza daktari, nesi, mama, na rafiki zangu pamoja na mke wangu huyo ambae amesababisha nikawa kwenye hali ile. Walinishangaa na daktari akasema kuwa huenda akili yangu haipo sawa zaidi akamwambia nesi ati alete sindano ya usingizi. "Hapana dokta.. Mie nipo sawa kabisa. Tafadhali nitoleeni huyu mwanamke. Sitaki kumuona." Niropoka kwa uchungu huku akili yangu ikiendelea kukumbuka jinsi mke wangu alivyokuwa akimpa raha mwanamume mwingine tena mbele ya macho yangu. Zaidi ni pale nilipokumbuka kuwa yeye ndie alikuwa akimuamrisha mjinga yule anipige mimi. Nilipandwa na hasira nikaanza kujifukutua kwenye kitanda kile huku nikiyotoa madripu lakini sikufanikiwa kujitoa hata kitandani pale ila niliishia kujitonesha vidonda tu.



    Nesi alileta dawa ya usingizi kishawakanichoma hapo nikapatwa na usingizi mzito ulio nichukuwa kama masaa ishirini na nne hivi. Niliposhituka nilikuwa peke yangu nilipotupa jicho upande wa pili ndipo nikamuona mke wangu. Nae aliponiona akainuka na kurudishia mlango wa wodi ile kishaakaniambia kuwa, yeye hakunipenda mimi bali alikuwa na shida na pesa tu. Akanipa hadithi kuwa, siku moja Baba yake alikuwa mgonjwa sana na yeye hakuwa na pesa ya kumtibia kwani hospitali walisema kuwa hawawezi waka mtibu baba yake bila kuleta pesa hiyo. Akiwa anatoka hospitali huku kichwa chake kimechanganyikiwa. Ndipo alipokutana na mama yangu na alipomuelezea tatizo. Mama akamwambia kuwa atumie usichana wake kunishawishi mimi kimapenzi mpaka nikubali kuolewa naye ili aweze kumsaidia pesa ile iliyokuwa ikihitajika hospitali iliaokoe maisha ya baba yake. Kwakuwa alikuwa na shida ndipo alipoamua kukubali iliaweze kusaidiwa na mama. Ni kweli mama alimsaidia na matibabu kwa baba yake yakaanza. Hapo mimi nikiwa sina hili wala lile nilijikuta na angukia kwenye mapenzi ya Rose na kwakuwa mama yangu alihitaji mke ndipo nilipoamua kumpatia furaha yake kwa kumuoa rose pasina kujua kuwa kuna siri nzito kati ya mama yangu pamoja na Rose. Mapenzi yalinoga ndani ya mwezi mmoja. Kumbe baba yake na rose ugonjwa wake ulizidi na kupoteza maisha. Hapo ndipo rose alipoanza kunitesa mimi kwakuwa sikuwa chaguo la moyo wake. Alifanya kila njia lakini zilishindikana ndipo alipoamua kuniadhibu kwa mtindo ule.



    Alimaliza maneno yake na kuondoka hapohapo huku akiniambia kuwa nyumba yangu na vitu vyangu tayari ameuza kwahiyo nikipona nisitegemee chochote.



    Kiukweli Aisha niliumia sana. Sikuwa na lakufanya zaidi ya kuchanganyikiwa tu. Nilimchukia mama yangu na kuona kuwa yeye ndio chanzo cha yote yale. Pia nilimchukia mke wangu kwakiapo cha kinafki mbele ya kanisa. Halafu nikaanza kufikiria kuwa nyumba yangu imeuzwa kwahiyo sina kwangu tena. Nilipiga moyo konde nikavumilia hospitali mule bila ruhusa nilitoroka. Nilienda kwa rafiki yangu mmoja lakini siku taka kwenda kwa mama yangu kwakuwa nilimchukia sana. Huko nilikaa hadi nilipopata nafuu na huko ndipo nilipoianza pombe kwani rafiki yangu yule alinishauri kuwa muondoaji wa mawazo ni pombe, na nilipoanza kunywa pombe nikaamua kuipa maisha yangu. Pombe akawa baba yangu, pia mama yangu na mke wangu pia. Kwakuwa kazi yangu iliota nyasi kutokana na kuja wakaguzi ambao walikagua shuleni nami nikaonekana simuhudhuriaji wa vipindi na nimeisababishia shule kushuka kitaaluma kutokana na mimi kuwa mwalimu wa taaluma. Ndipo nilipopoteza kazi yangu na sikuwa na laziada zaidi ya kutoka huko chato na kuamua kuja huku mwanza kwa ajili ya kumtafuta rafiki yangu mmoja ambae nilisomanae shule ya msingi...



    Kwa mara ya kwanza nikatua ndani ya jiji hili la mwanza. Namshukuru Mungu nilipokelewa salama na rafiki yangu huyo. Tulicheka na hata tulipofika kwake mkewe alitupokea vizuri tukala na kunywa yaani fulu raha. Kwakuwa yeye ni maarufu kwa ufanyabiashara, aliona ni vyema tushilikiane. Hapo nikapata kazi kwa rafiki yangu huyo.



    Niliendelea kunywa pombe huku nikiamini kuwa hiyo ndiyo starehe yangu pekee. Siku zilienda hatimae nilimaliza mwaka mzima kwa rafiki yangu yule. Kwakuwa nami kwa kipindi hicho nilikuwa nimejipanga. Niliamua kujenga nyumba na baada ya miezi sita nikahamia nyumbani kwangu maisha mapya nikayaanza. Huku mikono ya shukurani nikiendelea kuinyanyua kwa rafiki yangu yule aliyenifadhili.



    Siku moja nikiwa nimetoka kupata moja moto moja baridi kama ilivyokawaida yangu. Nikiwa kwenye gari yangu mara ghafla nikamuona mtu mbele ya barabara. Nilivyomtizama kiumakini nikama nilimfahamu. Lakini alikuwa tofauti na nilivyomzoea. Nilipomkaribia nilimuita kwa jina lake.



    "Rose..!" Akageuka na kunitazama. Akanigundua masikini. Nilimuonea huruma jinsi alivyokuwa amechoka na kuchakaa, mwili wake uliyounda umbo lake la mwanzo, haukuwepo tena. Ule uzuri wake wa awali ulikuwa umepotea na kuzalisha sura kavu yenye tabasamu la kuogofya. Roho ya huruma ilinijaa nikamuuliza wapi anakwenda nae akanijibu kuwa anakwenda kutafuta pakulala. Nilishangaa sana. Nikambeba kwenye gari langu kwakuwa nilimuhurumia sana.



    Nilimchukua hadi kwangu na kumuuliza kipi kisa na mkasa mpaka akawa kwenye hali ile wakati mie nakumbuka aliniacha huku ameuza nyumba yangu. Swali langu ni kama liliyazalisha machozi yaliyokuwa yamejificha machoni mwa Rose.. Nilimuhurumia zaidi kwakuwa nilimpenda. Hapo akaniomba msamaha na kunihadithia kuwa, baada ya yeye kuondoka na kuniacha hospitali huku akiwa ameuza nyumba yangu na mali zangu. Aliamua kuondoka chato yeye pamoja na yule mwanamume ambae alihisi kuwa ni chaguo lake. Waliondoka na kuja huku Mwanza walipofika walifikia hotelini na kukaa huko huku wakifurahia maisha. Kwakuwa alimuamini yule mwanamume wake hakuona kama kuna haja ya kumnyima pesa. Akachukuwa pesa zote na kumkabidhi huku wakiwa na mawazo ya kununua nyumba pamoja na kufanya mambo mengine mengi. Hapo ndipo mwanamume yule alipoamua kumudhulumu pesa zote na kumuacha ndani ya hotel kwa siku tatu bila kuonekana. Bili ya hotel ilipoisha alifatwa na wahudumu kishaakaambiwa alipie bili nyingine aliomba muda nakuendelea kukaa kwa deni hotelini mule huku akimsubiria mumewake ambae kwa muda huo hakuwa anapatikana kwenye simu. Ndipo rose alipokuja kushituka na kugundua kuwa ameibiwa. Masikini Rose akanyanganywa nguo, simu, pamoja na mali nyingine alizokuwa nazo ilikulipia fidia ya hoteli hiyo. Na hapo ndipo alipoanza kuishi kwa kutangatanga. Bila kula na alikoswakoswa kubakwa mara kadhaa na wahuni wapatikanao hata siku niliyokutana nae ilikuwa kama bahati maana alikuwa anahofu kutokana na kusakwa na wahuni wale aliowakimbia. Na hadithi yake ikaishia hapo.



    Huwezi amini nilimuhurumia sana Rose, na nikajisemea kuwa atakuwa amejifunza, nikaona sina haja yakumtimua au kulipa kisasi chochote kile kwasababu tayari dunia imemfunza. Kwakuwa nilimpenda. Nikaamua kumsamehe na kurudi kuishi nae tena. Tumekaa miezi kama sita hivi. Mara siku moja nikiwa kazini nilishangaa napigiwa simu ati nyumba yangu imeuzwa, nilipofatilia nikaambiwa mke wangu Rose ndie ameiuza. Sikuamini, hapo ramani za maisha zikavurugika nikaanza kukopa kila siku hatimae madeni yaka nizidi. Nikajikuta naanza kuuza mali zangu hadi nguo. Nikakosa muelekeo wa maisha. Siku moja nikiwa natangatanga mtaani nilishangaa sana kukutana na Rose huku akiwa na yuleyule mwanamume wake. Hapo bila haya wala aibu usoni. Akaniambia kuwa huo ulikuwa ni mpango waliyoupanga kunifanya nipate taabu. Kisha Rose akaongeza kwakunambia kuwa mjini ni shule.



    Niliumia sana, hapo sikuwa na jinsi. Nilijiona mjinga wa wajinga. Nilitamani kujiua lakini kila nilipofikiria nafsi iliniuma. Nikatamani kurudi kwetu lakini nisiwe na nauli. Hapo mtoto wa kiume nikafuta machozi na kuanza kuchakalika kwenye vibarua. Nilianza kwa kuokota taka taka, baada ya mwezi nikaingia kwenye ufundi seremala. Huko ndipo nilipopatia hutu tuvyombo na kununua kitanda cha urithi wa mtu aliyefiwa na babu yake. Nilitokwa na hamu na wanawake nikaiweka hamu hiyo kwenye pombe. Nikaona bora pombe aniibe pesa kuliko mwanamke. Nikaona bora pombe anipatie maumivu ya mapafu na kuchoma utumbo kuliko mwanamke. Kwanzia hapo nikawa nikitoka kazini napita kwenye pombe kisha nakuja nyumbani kulala. Na hiyo ndio historia ya mimi na pombe. Sitaki kuoa wala hakuna wakunishawishi kuoa katika hii dunia nimeshafunga pingu za maisha na pombe tu." Mlevi yule ajulikanae kwa jina la Devid. Alimaliza historia yake kishaakaendelea kunywa pombe yake. Hapo Aisha mapuya. Macho yaka mtoka na kwa muda huo alisahau kumnywesha maziwa mtoto wake Neema.



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Aisee.. Pole sana kaka yangu. Kwa jinsi ulivyoumia sidhani kama utakuwa unawapenda wanawake. Lakini kaka, si wote wapo hivyo. Tunatofautiana, kuna wale ambao wameiweka mioyo yao kwenye tamaa za mali lakini pia wapo ambao wanahitaji mapenzi na hawaongei wala kuwaza chochote kuhusu mali. Tafadhali kaka punguza hasira najua ni vigumu sana wewe kukubali kuishi na mwanamke tena, lakini hebu jiulize. Je, hiyo pombe itakupa mtoto ambae atakuwa mrithi wako? Je, hiyo pombe itakupa utajili au kukufanya uwe chini kila siku? Haya maisha tu kaka yangu na hizi ndizo changamoto za maisha. Kuitwa mwanamume siyo kujua kuranda mbao, au kujua kunywa kuliko wenzio huko baa. Wala kuitwa mwanamume siyo kulalamika hovyo. Bali ni kukabiliana na changamoto zote nasiyo kuzikimbia kaka yangu. Bado unanafasi nyingine katika maisha yako ya kuishi na mtu, hivyo nakuomba tafuta anaekufaa wewe oa. Kumbuka nawe una moyo sasa iweje ujifanye mgumu kama jiwe wakati moyo wako unanyama na unaruhusu maumivu? Pole sana kwa yaliyokusibu. Lakini yote tunayaita maisha." Aisha alitoa hotuba na mawaidha kwa pamoja. Kiukweli, mawazo ya Aisha yalibadilika roho ya huruma ilimuijia na kumthamini Mlevi Devid. Nadhani hakuwaza kama devid angekuwa ni mwenye kupitia mapito hayo. Yeye alikuwa akijua huenda Devid ni mtoto aliyezaliwa kwenye familiya ya hohehahe. Wasiyo na mbele wala nyuma. Alibakiwa na maswali ambayo aliweza kujijibu.



    Maneno ya Aisha yalipita vilivyo kwenye masikio ya Devid lakini hayakuweza kuathiri chochote badala yake Devid alitoa majibu kuwa.. Mke wake yeye ni pombe. Mtoto wake ni pombe. Na kila kitu cha thamani kwake ni pombe.



    Ni kweli kabisa Aisha asingeweza kuupingua msimamo mkali kutoka kwa devid. Hapo ndipo alipoamini kuwa kuna watu kwenye hii dunia wanamisimamo. Alifananisha tatizo lake kisha akafananisha na la Devid akajicheka na kujisemea kuwa,



    "Nilikuwa nadhani mimi ndio mwenye matatizo makubwa. Kumbe wapo waliyoumia zaidi yangu." Devid, aliongeza jambo jipya kwa kusema,"Mama Neema. Mie niko radhi kumlea mwanao Neema kwa gharama yeyote ile. Na ninakuomba endelea kuishi namimi kama kaka na dada. Tumlee Neema wote kwa pamoja na siri hii iwe kati yetu. Tusiruhusu mtu ajue kuwa mimi na wewe ni mtu na dada yake. Fanya hivyo nakuomba." Neema alipata faraja na akaamini kweli kuna watu wema. Yaani hajazaa nae, wala si mpenzi wake lakini ameomba amlee mwanae tena waishi kama kaka na dada. Nasi.. Mtu na mume au mke wake. Alijikuta akiangua kilio cha furaha kwani hakuwahi kuamini kama kwenye hii dunia kuna mwanamume mwenye wema kama yule.



    Miaka ilisonga hatimae Devid akafungua kijiwe chake mwenyewe cha ufundi seremala na kazi yake ikawa na heri. Mtoto neema alikuwa hadi akafikisha miaka nane. Shule alipelekwa ile ya serikali, huko nae hakuwa msumbufu ni kama alijua yupo shule kwa sababu gani. Alikuwa na kipaji cha kucheza mpira. Kipaji hicho kilianza kujionesha kwanzia nyumbani alipokuwa akicheza mipira ya kupondana hadi hapo alipokwenda shule ambapo aliwatesa wenzake na zaidi alikuwa mbaya pale alipoanza kuutumikia mpira wa pete. Wanafunzi na hata waalimu wake waliuona uwezo wa mtoto huyo mdogo aliye pigana vikumbo na madada zake kwenye mechi mbalimbali. Hakika uwezo wake ulikuwa wa kutatanisha sana. Kila mtu shuleni alimjua mtoto yule, walimu walimpenda na kutamani kuongea nae muda wote atokapo darasani. Kulingana na uwezo wa ajabu aliyokuwa nao mtoto yule. Kamati ya shule ilibidi iwaite wazazi wake na kuwaambia wazazi wa Neema kuwa kuna wazamini wamejitokeza na wamehitaji wa msomeshe Neema. Wazazi walipolipata jambo lile Mama wa neema aitwae Aisha yeye alimshauri Kaka yake wa hiyari ambae ni mlezi mwenzie ajulikanae kwa jina la Devid, kuwa ni bora wakubali kusaidiwa. Lakini Devid alikataa katakata. Nakusema kuwa.. Aliahidi kumlea Neema kwa jasho lake hivyo hakuhitaji usaidizi wowote.



    "Baba, leo tumecheza mpira na timu ngumu!" aliongea Neema baada ya kumlaki Devid aliyekuwa amelewa kama ilivyo kawaida yake atokapo kazini. Ulevi wa devid haukumuathiri yeyote kwenye familia hiyo na ndio maana hata Neema alikuwa na uhuru wa kumkumbata Baba yake pasina kujali kuwa amelewa au la.



    "Mwaa.. Mwaanangu. Wewe ni mwamba. Popote unatimba. Bila kuremba. Hebu njoo kwanza ndani mwanangu." Alimsifia kisha akaingia ndani alipofika alikaa kwenye kochi na Neema alikaa pembeni. Kisha Baba Neema akasema. "Kumbuka wewe ni mwamba. Popote unatimba. Tena bila kuremb. Kwahiyo sidhani kama uliremba kwenye hiyo mechi. Vipi, walihimili mikikimikiki ya Mwamba? Au walishindwa?" Aliuliza Baba Neema.



    "Mmmh!! Baba.. Nadhani unanijua huwa sitanii kabisa kwenye anga zangu. Walijifanya wagumu lakini.. Mpaka sasa hawaamini kama ni mimi na udogo wangu." alijibu kwa majigambo Neema. Kama alivyozoea kumjibu baba yake huyo kipenzi.



    "Nakujua mwanangu.. Hebu kwanza niitie huyo Mama yako." Akatoka Neema kisha akarejea. "Umemuacha wapi?" aliuliza kisha akajijibu baada ya kumuona Mama Neema.





    . "Mpenzi.. Kumbe umefika. Nilikuwa sijakusikia, si unajua namie ni kiwa bize na upishi. Enhee nambie kwema huko? Maana mwanao alivyonifuata!." Aliongea Mama Neema baada ya kufika sebuleni alipo Devid.



    "Wewe mama Neema wewe... Ina bidi leo nikufumue haswa haswa."Alisema Devid.



    "Jamaani.. Kwa kosa gani tena mume wangu?" Aliuliza Mama Neema kwa sauti ya upole.



    "Neema!" Aliita baba Neema. Neema akaitika kisha baba Neema akaendelea. "Mwanangu. Nimpige mama yako? Au nisimpige.." Devid aliuliza kwa sauti ya upole huku akitingisha kichwa chake kilevi levi.



    "Msamehe tu Baba yangu. Si unajua tena Mama mwenyewe hana hata pakupiga, ukimpiga utajitafutia kesi bure!" Aliongea Neema kisha Mama Neema akamsukuma Neema kichwa chake kwa kutumia kidole cha shahada kumaanisha kuwa hajapendezwa na kauli ya mwanae.



    "e..eeeh. Una msonkola mwanangu. Wakati anakutetea." Alipanda juu Baba Neema.



    "Kwani. Mume wangu nimekosa nini?"



    "Eti.. Kwani mume wangu nimekosa nini?" aliigiza Maneno kwa Kubana pua kisha akasema. "Inamaana unataka kunambia kuwa hujui kama Mwanangu.. Hujampatia grucose ya kutosha. Hivi nimenunua grucose yote hiyo halafu mwanangu anachoka uwanjani. Kweli? Kama siyo hila za kumfanya superstar wangu ashindwe kufikia ndoto zake. We unadhani ninini ha..." kabla hata hajamalizia mkewe akadakia. "Jamaani.. Nilisahau kumpatia grucose lakini mbona hakunambia mimi. Eti wewe Neema mbona hukunambia mimi ukamwambia baba yako."



    "e. Eeeh.. Usimtuhumu mwanangu kiasi hicho. Kwakuwa umekili kosa wewe nenda kapike halafu utuache tuendelèe na yetu. Au siyo Mwamba?"



    "ndiyo.. Dady."



    "Mama. Akikuchanganya unakuja kunambia. Wewe ni Mwamba popote unatimba. Oohoo."



    Mama Neema alitoka na kwenda jikoni huku Neema na Baba yake wao wakiendelea kutaniana.



    Chakula kilitengwa na wote kwa pamoja wakala. Huku wakitaniana na kudumisha amani yao. Kama ilivyo ada. Neema hulala na Mama yake, pia Baba Neema hulala kivyake. Ndivyo walivyofanya. Ilipofika asubuhi, Neema aliamshwa na Mama yake kisha akaoga na kuvaa nguo za shule, baada ya hapo alikunywa chai nzito kisha akaenda shule.



    Maisha yaliendelea vilevile hadi hapo Neema alipofika darasa la sita ndipo rafiki yake wa kiume ajulikanae kwa jina la Mussa alipomletea barua ya kimapenzi. Siku hiyo Neema alichukia sana ingawa barua ile iliambatanishwa naombi la kutokumjuza yeyote lakini Neema alilipeleka swala lile hadi ofisini.



    "Unalia nini Neema." Ni sauti ya Madam Ana, aliyekuwa amesimama mlangoni mwa ofisi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Si.. Huyu Mussa. Eti ameniletea barua yenye tabia mbaya.." Alijibu Neema kisha akaulizwa ilichosema. Akajibu,"Mi sijui hata. Yeye ameandika eti ananipenda.. Mi nimeamua kuja kumsemea." alishtaki Neema huku akiendelea kulia.



    "Basii.. Futa machozi. Hebu nenda kamuite hapa." Akatoka anakimbia. Kisha akaenda kumuita.



    Mussa huwa anamuonea aibu sana Neema japo alimpenda lakini alishndwa kumwambia kwa kuogopa huenda angesemwa kwa mwalimu kwasababu Neema huwa anasuluhisha kesi zake stafu.



    "Ni..ni..ni..nini tena. Ne..ne.. Neema?" aliuliza Musa kwa sauti ya uoga.



    "Kwani hujui Musa? Hujui?.."



    "Ni..ni..ni..nini. Tena mbona hivyo. Au tatizo ile barua." Aliuliza kwa upole Musa huku akimtuliza Neema ambae sasa alianza kupaza sauti hadi darasa zima wakasikia, wote kwa pamoja wakawageukia kina Neema na kuwashangaa.



    "Inamaana. Hujui kuwa wewe uliniandikia barua ya tabia mbaya eti unanipenda. Sasa nimeenda kukusema kwa mwalimu.. Twende, ukafundishwe adabu." Hapo Musa akakosa nguvu na kuanza kulia kabla hata hajavuka mlango wa darasa. Wakati huo Neema alikuwa ameshaanza kuongoza njia ya kwenda kwa mwalimu. Darasa zima lilimuhurumia Musa kutokana na kesi ile ya mapenzi. Lakini halikuwa na lakufanya. Kwa upole Musa akaanza kujivuta hadi ofisini.



    "Wewe.. Musa, hizi tabia mbaya mbaya za kuwatumia wenzio barua umeanza lini. Na ninani kakufunza?" Aliuliza madam Ana.



    Musa kimya.



    "Inamaana hunisikii au kiburi" Hapo Musa akazungusha kichwa chake mashariki na magharibi kwa kumaanisha kukataa.



    "Unavyozungusha kichwaa inamaana unamaanisha huwezi kuongea au?"



    "Hapana mwalimu. Naomba msamaha." Ni jibu alilotoa Musa huku akiwa amepiga magoti. Kwapembeni yake alikuwepo Neema ambae alionekana kulia kwa kosa la kupendwa.



    Maadamu alimuuliza Neema, kuhusu adhabu ya kumpa Musa. "madamu.. Mimi sijui, ila nilikuja kumsema tu kwasababu sipendi tabia mbaya." Alijibu Neema. Hapohapo Neema aliagizwa viboko kisha waalimu kadhaa wakamzunguka Musa huku wanafunzi wanne wenye nguvu na maumbo makubwa wakimshika mikono na miguu kwa wakati huo tayari Musa alikwisha vuliwa unifomu zake za kushule na kubakizwa pensi iliyochanika chanika ovyo. Masikini Musa alichapwa viboko tena kwa zamu. Akichoka mwalimu huyu anaingia yule. Akichoka yule anaingia huyu. Mpaka anakuja kuachwa, tayari alikuwa amevimba kwanzia makalio, mapaja, mgongo, hadi mikono. Alilia bila machozi ilikujikaza mbele ya Neema. Lakini alikuwa tayari ameshapata aibu kutokana na kuvuliwa.



    Musa alipomaliza kupokea adhabu yake alivaa uniform zake za shule na akaamua kuongeza kosa jingine la kutoroka shuleni. Aliona ni bora kutoroka kuliko aibu ile aliyoipata.



    "Mamaaa! Ayaa... Pole pol.. Ayaa mama.."



    "Hebu tulia nikukande vizuri."



    "Mama, sasa mie sitaki maana wewe unanikanda utadhani unahasira namimi. Aya, bora uniache na maumivu yangu."



    "sawa mwanangu achanikukande taratibu. Lakini siunajua tena dawa huwa chungu. Ila nawewe mwanangu punguza utundu. Ona leo umechapwa hivi. Kesho siutakuja hauna hata huu mwili."



    Huo ulikuwa ni muda wa usiku pindi Mama Musa alipokuwa akiangaika kushughulikia majiraha ya Musa aliyoyapata shuleni. Musa alipoulizwa na mama yake juu ya kosa alilochapiwa. Alidanganya nakusema kuwa niuchelewaji tu wanamba.



    Hatimae Musa alimaliza kukandwa na hakuwa na la ziada zaidi ya kwenda kufakamia kitanda chake.



    "Mmmh! Ila namimi kwenye siku zote leo ndio nimeaibishwa. Yaani darasani wanafunzi sijui watanitazama vipi tu. Haya nikikutana na walimu sijui uso wangu nitauhifadhi wapi iliwasiuone. Mamamamama.. Bora hao, sasa vipi kwa Neema. Aliniona kipindi nachapwa ndani ya kaboka. Dah! Sijui hajawambia darasani wakaanza kunitania. Yaani.. Leo namimi nimepatikana, kama nyumbani kungekuwa na uwezo. Mimi ninge hama tu shule." Aliendelea kujisemea Musa peke yake huku akiwaza nini afanye ilikuepukana na ile adha.



    "Au nimuache Neema. Lakini... Nikimuacha neema sind'o tajiongezea mawazo sana. Mimi neema simuachi hata nifanywe nini. Bora waniue tu." kwa muda huo Musa akiendelea kukizungusha kichwa chake ndani ya mji wa mawazo. Huku nako Neema nae alipata muda wa kupumzika vivyohivyo kama Musa nae alikuwa mawazoni., "Eti, Neema nakupenda sana.. Yaani tena anabahati leo angechapwa fimbo nyingi. Kumbe mimi kumuheshimu kama dada yake, yeye akaona alete mambo yakijinga jinga. Ngoja na nikimuona lazma nimchambe. Anabahati jana alijiwahi kutoroka tu. Ngoja nilale kesho nisijekuchelewa bure. Nataka nikamuoneshe chamtemakuni." Alijiwazia Neema kisha akayafumba macho yake. Haikumchukuwa muda sana usingizi ukawa umeshampitia.



    Kama ilivyo ada Mama yake alimuamsha nakwenda shule, huku nae Musa aliamka na kwenda shule. Sikuhiyo Musa hakuwa na amani kabisa hata darasani alikuwa amejiinamia muda wote. Neema na kundi lake wakamfuata kwa ajili ya kwenda kumshushua.



    "Enhee.. Wewe... Eti nakupenda. Yaani nilikuwa nakuheshimu lakini heshima yote imeshuka. Nakuona kama kinyago. Lione ukomtoto unakimbilia mambo makubwa. Unalooo! Hata kama nikitaka kupendwa mtu kama wewe mimi nikupeleke wapi sasa. Tena nikwambie, kwanzia leo.. Sitaki mazoea, nenda hukohuko na tabia zako zisizo na kichwa wala miguu. Allaaa. Hebu twendeni nadhani taarifa ameipata." Neema alimshushua huku marafiki zake kama kina jeska wakimsonkola kichwani Musa ambae muda wote aliinamia chini si kwasababu ya usingizi mzito. Bali kwasababu ya kuuhifadhi uso wake. Aliona ni bora viungo vingine viaibike lakini sio uso. Hakuwa na pamba masikioni japo alihitaji kuwa nazo iliasisikie alichokuwa akiambiwa. Walipoondoka kina Neema haukupita muda sana kengele ya mapumziko ikagongwa. Wanafunzi wote walitoka nje, isipokuwa Musa ambae aliendelea kujilaza kwenye dawati huku uso wake ukiwa umelowa machozi.



    "Unamtafuta Musa? Daa.. Mwanangu Mkali wako leo kaaibishwa na kale kaneema."



    "Weewee. Usinambie.. Nini tena?"



    "Sijui alikatumia barua ya mapenzi jana. Sasa kakafura kichizi, siunajua kale huwa kesi zake zinatatuliwa kwa waalimu? Kaka mpeleka. Mchizi akadundwa ile mbaya. Aliona aibu na kwenda home, sasa kumbe kale kadem kalipanga na marafiki zake kuja kumchamba mkali Musa. Leo sasa.. Muda wa free, wakamvagaa mwana. Da, wakamchamba ileile. Halafu mwana ameinama tu, siunajua tena hakuwa na chakufanya. Ila pigo kama zile hazifai.. Sasa hivi sisi tumeshakuwa wakubwa maswala ya kusemana hayana inshu"



    "Dah! Masikini.. Kwahiyo mkali Musa yuko wapi?"



    "Sasa hivi. Yumo class amelala tu."



    "Poa beka. Acha mie nikamcheki. Halafu huyo dem anaejiona anakunya keki mie nitadili nae."



    "Poa Side. Achamie nikaombe ombe misuba huku. Siunajua madogo wa darasa la nne wengi wanapujapuja sana. Kwahiyo mie watanigeia tu."

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hayo yalikuwa ni maongezi kati ya Saidi ambae ni rafiki mkubwa wa Musa, pamoja na Bakari ambae nae ni rafiki wa Musa. Waliagana kisha Saidi akaenda hadi darasani kwa kina Musa na kumkuta rafiki yake kajiinamia. Alimuita lakini hakuitika, akamsogelea kisha akamuinua kichwa. Ndipo aliposhuhudia machozi ambayo sasa yalikauka kutokana na kulia sana kwa rafiki yake huyo. Alimuhurumia na kumuuliza kilichotokea, Musa alimuelezea kila kitu Side.. "Pole, ila we jikaze kiume.. Huyo demu anajifanya mzuri. Ngoja nitamuonyesha tu. Hawezi kukuzingua hivi mwanangu."



    "Musa, achananae tu. Hajui analolitenda. Hajui kuwa mimi siwezi kula kama amenikasirikia, siwezi kulala kama amenizingua. Ipo siku atajua. Mie bado nampenda ukimzingua. Mwisho aache kunipa hata salamu halafu nikawa naumia zaidi."



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog