Search This Blog

Friday, July 15, 2022

MASSACRE (MAUAJI YA HALAIKI) - 1

 





    IMEANDIKWA NA : NYEMO CHILONGANI



    *********************************************************************************



    Simulizi : Massacre (Mauaji Ya Halaiki)

    Sehemu Ya Kwanza (1)

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kila aliyekuwa akizisoma taarifa ambazo zilikuwa zimeandikwa katika magazeti mbalimbali yaliyokuwa yakitoka katika siku hiyo alibaki akishangaa tu. Watu wakashtuka kupita kawaida, habari ile ilionekana kuwasisimua kupita kawaida. Imani juu ya wachungaji ikaanza kuondoka katika mioyo ya watu, hasa waumini wa dini ya Kikristo.

    Kanisa likaonekana kupotea njia, kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea hasa katika makanisa mbalimbali kilionekana kuwa kama maigizo juu ya jukwaa au ndani ya luninga. Shetani akaonekana kuliteka kanisa na kulifanya alivyotaka kulifanya. Dhambi ambayo ilionekana kufanyika kwa kiongozi mmoja wa kanisa moja ikaonekana kama imetokea katika makanisa yote nchini Tanzania. Watu wengine wakataka kujitoa kutoka katika imani ya Kikristo kwa kudai kwamba shetani alikuwa amemzidi nguvu kila mtu.



    Wokovu wote ambao ulikuwa ukiendelea katika makanisa yote ukaanza kuyumba. Watu wengine wakaahidi kutokuhudhuria tena makanisani mwao kutokana na imani juu ya viongozi wao kuanza kupotea. Idadi kubwa ya watu wakaanza kupoteza uaminifu wao juu ya wachungaji wa makanisa yao.



    ‘MCHUNGAJI ATAKA KUMBAKA BINTI OFISINI’. Hicho kilikuwa ni kichwa cha habari ambacho kilikuwa kikisomekana katika magazeti mbalimbali jijini Dar es Salaam. Bado watu walikuwa wakiendelea kushangaa, hawakuamini kama mchungaji Matimya wa kanisa la Praise And Worship lililokuwa Mwenge angeweza kufanya kitu kama kile ambacho kilikuwa kimeonekana kuandikwa katika magazeti mengi.



    Habari ile ilionekana kuwa habari iliyokuwa na furaha kwa watu wote ambao walikuwa hawawapendi Watumishi wa Mungu. Watu wakaanza kupeana taarifa majumbani mwao huku kila aliyepewa taarifa ile akaanza kuelekea barabani kulinunua gazeti moja ambalo lilikuwa na habari ile.



    Katika mwaka mzima, habari ile ndio ambayo ilifanikiwa kuuza nakala nyingi kuliko habari yoyote iliyowahi kuandikwa katika mwaka huo. Mpaka inafika saa saba mchana, hakukuwa na gazeti lolote lililokuwa na habari ile ambalo lilikuwa katika meza ya wauza magazeti.



    Kila mtu ambaye alikuwa akiyaona magazeti yale, aliyanunua. Siku ya mwisho ikaonekana kukaribia kutokana na shetani kuonekana kulivamia kanisa hasa kwa viongozi mbalimbali wa makanisa. Aibu kubwa ikaanza kulikumba kanisa la Praise And Worship lililokuwa Mwenge.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Haiwezekani hata kidogo. Mbona huyu Mchungaji ni Mtumishi mzuri wa Mungu! Tena kwa sasa anataka kuwa Askofu Mkuu. Hawezi kufanya hivi” Sauti ya msichana mmoja ilisikika ikiwaambia wenzake huku mkononi akiwa ameshika Biblia katika kipindi ambacho walikuwa wakitoka kanisani siku hiyo ya Jumapili.



    “Kwa nini isiwezekane kwa mtu kama huyu kufanya hivi? Tumemkaribisha shetani sisi wenyewe. Acha awatumie watumishi wa Mungu anavyotaka” Mwanamke mmoja alisikika akisema huku akishika vizuri Biblia yake.



    Habari hiyo ndio ambayo ilikuwa imeshika hatamu katika kipindi hicho. Kila mtu ambaye alikuwa akiiona habari ile na kuisoma, alishtushwa kupita kiasi. Picha kubwa ya rangi ya mchungaji Matimya ilikuwa ikionekana vizuri katika kila gazeti ambalo lilikuwa na habari ile.



    Mchungaji Matimya alikuwa amekaa katika kiti cha nyuma kabisa ndani ya kanisa lake. Uso wake alikuwa ameuinamisha chini huku machozi yakimtoka. Mbele yake aliiona aibu kubwa ikiwa imemkuta, hakuelewa ni kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya ili Watanzania waelewe kwamba hakuwa amekifanya kile kitu ambacho kilikuwa kikitangazwa sana na vyombo vya habari.



    Hakukuwa na mtu ambaye alionekana kumuamini Mchungaji Matimya, kila mtu kanisani humo alimuona kuwa kama Mwakilishi wa shetani ambaye aliletwa kanisani humo kwa ajili ya kulitia aibu kanisa. Ingawa ibada ilikuwa ikiendelea kanisani humo, macho ya washirika wengi walikuwa yalikuwa yakimwangalia Mchungaji Matimya.



    Machozi yale ambayo yalikuwa yakimtoka, yalionekana kuwa kama ya kinafiki machoni mwa washirika wa kanisa lile. Mchungaji Matimya hakuwa peke yake, familia yake ilikuwa pembeni yake. Mkewe, Bi Meriana alikuwa upande wake wa kushoto huku watoto wake wawili, Benedict na Angelina wakiwa katika upande wa kulia.



    Kilio cha chini chini kilikuwa kikisikika kutoka kwa Bi Meriana. Kila alipokuwa akikumbuka aibu ile ambayo ilikuwa imemkuta mumewe, alizidi kuumia. Hawakuonekana kufuatilia kitu chochote kilichokuwa kinaendelea kanisani mule. Vichwa vyao vilikuwa vikifikiria mbali.



    Ibada iliendelea kama kawaida. Mara baada ya muda wa matangazo kuingia, Askofu wa dhehebu hilo la Praise And Worship, Askofu Lugakingira akasimama na moja kwa moja kuelekea katika madhabau ya kanisa hilo na kuchukua kipaza sauti. Kabla hajaongea kitu chochote kile, alitulia kwa muda huku akiliangalia kanisa.



    Kila mtu alikuwa kimya tayari kwa kusikiliza kile ambacho Askofu alitaka kukizungumza mahali hapo. Askofu alianzia mbali sana lakini huku lengo lake kubwa likiwa ni kufika katika kitu ambacho kilimfanya kuja katika kanisa lile katika siku hiyo ya Jumapili. Mara baada ya kutumia dakika kumi kuongea mambo tofauti tofauti, hapo hapo akamtaka Mchungaji Matimya kwenda mbele ya kanisa lile.



    Huku akionekana kuwa katika lindi la mawazo, Mchungaji Matimya akainuka kutoka katika kiti alichokuwa amekaa kule nyuma ya kanisa na moja kwa moja kuanza kuelekea mbele ya kanisa. Minong’ono ikaanza kusikika kutoka kwa washirika ndani ya kanisa lile, Mchungaji Matimya hakuonekana kujali, aliendelea kupiga hatua hadi mbele ya kanisa lile.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nadhani hakuna mtu asiyejua kitu ambacho kimenifanya kuja ndani ya kanisa hili kwa siku ya leo. Lilikuwa ni suala ambalo lilihitaji kumuita Mchungaji Matimya. Niliongea nae kwa kirefu sana na kukiri kila kitu pasipo kuficha kitu chochote kile” Askofu Lugakingira aliliambia kanisa na kuendelea.



    “Ningependa kumpa nafasi ya kulieleza kanisa kama hiki kitu ambacho kimetawala kila sehemu ni kweli au kuna uongo wowote” Askofu Lugakingira alisema na kisha kumpa kipaza sauti mchungaji Matimya.



    Mchungaji Matimya hakuongea kitu chochote kile, alibaki kimya huku macho yake yakiangalia chini. Kila alipotaka kuongea kitu, aliuona mdomo wake kuwa mzito kufunguka, hakujua aseme kitu gani mbele ya kanisa na mbele ya familia yake. Kumbukumbu ya maisha yake ya nyuma ikaanza kujirudia kichwani mwake, katika hatua nyingine, alijuta kwa nini aliitwa kuwa Mchungaji.



    “Nalihitaji kanisa msamaha. Ni kweli nilitaka kumbaka Judith ndani ya of….” Mchungaji Matimya alisema lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake, akaanza kulia. Sauti ya kilio chake kilisikika kanisa zima kutokana na kipaza sauti alichokuwa amekishika. Wanawake wakashindwa kuvumilia, nao wakaanza kulia.



    Mtoto wake, Benedict hakuweza kuvumilia kubaki kanisani hapo akasimama na moja kwa moja kuanza kuelekea nje ya kanisa lile. Moyo wake uliumia kupita kiasi, maneno ambayo aliongea baba yake mbele ya kanisa yalionekana kumuumiza kupita kawaida.



    Mara baada ya kufika nje ya kanisa, moja kwa moja akalifuata gari lao na kuingia ndani na kisha kuliwasha. Kila mtu ambaye alikuwa nje ya kanisa alikuwa akimwangalia Benedict ambaye akaliwasha gari lile na kuondoka katika eneo lile la kanisa.



    Mchungaji Matimya akashindwa kuendelea, akakikabidhi kipaza sauti kwa Askofu Lugakingira ambaye alikuwa akimbembeleza kwa kumpiga piga mgongoni. Mchungaji Matimya akazidi kulia zaidi na zaidi, akapiga magoti chini huku uso wake akiwa ameuinamisha chini kwa aibu huku machozi yaliyokuwa yakimtoka kuloanisha sakafu ya pale madhabahuni.



    “Kila kitu kina sheria zake. Na hili kama dhehebu la Praise And Worship, mchungaji Matimya hatokuwa mchungaji wa kanisa hili tena. Tunamfungia kufanya huduma yoyote kwa muda wa mwaka mmoja na nusu” Askofu Lugakingira aliliambia kanisa.



    Idadi kubwa ya washirika ikaonekana kufurahia. Thamani ya mchungaji Matimya ikaonekana kushuka. Pepo la uzinzi likaonekana kumvaa mchungaji Matimya ambaye bado alikuwa pale mbele ya kanisa akiendelea kulia kwa uchungu. Kila kitu ambacho kiliendelea katika maisha yake kilionekana kuwa kama ndoto ambapo baada ya muda fulani angeamka kutoka katika usingizi mzito.





    Uchaguzi wa Askofu mkuu ndio ambao ulikuwa ukikaribia, siku tano tu ndizo ambazo zilikuwa zimebaki kabla ya uchaguzi huo. Wachungaji wawili, mchungaji Matimya wa kanisa la Praise And Worship la Mwenge lililoko jijini Dar es Salaam pamoja na mchungaji Mwakipesile wa kanisa la Praise And Worship lililokuwa Morogoro ndio ambao walikuwa wakiwania nafasi ya kuwa Askofu mkuu nchini Tanzania.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kila mtu alionekana kuwa na nafasi nzuri ya kuchukua nafasi hiyo lakini mchungaji Matimya ndiye ambaye alionekana kuwa na nafasi kubwa zaidi. Kila kanisa la dhehebu la Praise And Worship lililokuwa nchini Tanzania, jina la mchungaji Matimya ndilo ambalo lilikuwa likitajwa mara kwa mara.



    Wachungaji wengi walikuwa wakitamani Mchungaji Matimya achukue nafasi hiyo kutokana na huduma nzuri ambayo alikuwa akiitoa katika kanisa lake na makanisa mengine mbalimbali nchini. Hakuwa na roho ya majivuno kama aliyokuwa nayo mchungaji Mwakipesile.



    Kila mtu alivutiwa nae, kila mtu akatamani mchungaji Matimya achukue nafasi ile na kuwa Askofu mkuu. Asilimia zaidi ya themanini ya wachungaji wote wa dhehebu hilo walitamani mchungaji Matimya achukue nafasi hiyo ambayo ilitarajiwa kuachwa na Askofu Lugakingira siku chache zijazo.



    “Ni lazima nifanye kitu” Mchungaji Mwakipesile alijisemea huku akionekana kukasirika.



    Mbele yake hakuona dalili zozote za ushindi katika nafasi ya Uaskofu. Baadhi ya wachungaji ambao walikuwa katika upande wake, katika kipindi hicho walikuwa wamemsaliti. Kila kitu katika kipindi hicho kilionekana kwenda tofauti na matarajio yake ya nyuma.



    “Nitamtumia hata mshirika wake mwenyewe” Mchungaji Mwakipesile aliendelea kujisemea.



    Hakutaka kuendelea kubaki Morogoro, kitu alichokifanya siku iliyofuata ni kuchukua ndege na moja kwa moja kuanza kuelekea jijini Dar es Salaam. Hakutaka mtu yeyote afahamu juu ya safari yake hiyo ya ghafla, hakumpa taarifa hizo mtu yeyote zaidi ya msichana mmoja tu, Judith Simon ambaye alikuwa akiishi ndani ya jiji la Dar es Salaam.



    Jina la Judith Simon wala halikuwa geni masikioni mwa washirika wa kanisa la Praise And Worship lililokuwa Mwenge. Binti huyu alikuwa na sifa zote ambazo msichana wa kisasa na mrembo alitakiwa kuwa nazo. Alikuwa na wembamba kama waliokuwa nao wasichana ambao walikuwa wakigombania nafasi ya kuwa mrembo wa Tanzania.



    Uso wake ulikuwa mwembamba, alikuwa akitembea kwa mwendo wa mapozi kana kwamba alikuwa hakanyag ardhi. Kila aliyekuwa akiuangalia mwendo wa Judith alikiri kwamba binti huyo alikuwa akitembea mwendo uliokuwa na mvuto kanisani hapo.



    Mashavu yake yaipendezeshwa na vishimo viliwili vilivyokuwa mashavuni mwake ambavyo vilikuwa vikionekana vizuri katika kila wakati alipokuwa akicheka au kutabasamu. Kila wakati Judith alionekana kuvutia.



    Uzuri wake ulikuwa ukionekana wakati wote. Haijalishi alikuwa amekarika, amenuna au ametabasamu, muda wote huo uzuri wake wa asili ndio ulikuwa ukionekana machoni mwa watu wengi.



    Judith alionekana kuwa mcha Mungu. Karama ya Uimbaji ambayo alikuwa nayo ndio ambayo ilimfanya kuzidi kukubalika katika kanisa hilo lililokuwa likiongozwa na mchungaji Matimya. Judith akaamua kujiunga na kwaya mojawapo iliyokuwa kanisani hapo. Kila mtu alionekana kubarikiwa katika vipindi vyote ambavyo Judith alikuwa akimsifu Mungu. Judith alikubalika na kila mtu kanisani hapo.



    Vijana hawakutaka kubaki nyuma kanisani hapo, harakati za kumtaka Judith zilikuwa zikiendelea kimya kimya kanisani hapo. Judith hakutaka kujirahisisha kwa wavulana kitu ambacho kiliwapelekea vijana wengi kusimamishwa huduma kanisani humo.



    “Watu wakijua?” Judith alimuuliza mchungaji Mwakipesile huku akionekana kuwa na hofu. Mchungaji Mwakipesile hakuongea kitu chochote, alibaki akimwangalia Judith na kisha kutoa tabasamu.



    “Utawaambia au?” Mchungaji Mwakipesile alimuuliza.



    Swali lile likaonekana kuwa gumu kwa Judith, alibaki kimya huku akimwangalia mchungaji Mwakipesile ambaye alionekana kumaanisha kile alichokuwa akikiongea kwa wakati huo. Alipoona Judith amekaa kimya, akachukua glasi iliyokuwa na juisi ya maembe na kisha kupiga fundo moja.



    “Kama hautowaambia nina uhakika hawatojua” Mchungaji Mwakipesile alimwambia Judith ambaye kwa kiasi fulani woga wake ukaonekana kupungua.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Na vipi kuhusu malipo?” Judith aliuliza.



    “Milioni tano baada ya kukamilisha kazi hii” Mchungaji Mwakipesile alijibu.



    “Sawa” Judith aiitikia na moja kwa moja kuondoka huku akijiandaa na kazi ambayo alitakiwa kuifanya



    Alipomaliza kuongea na viongozi mbalimbali wa kanisa lake, mchungaji Matimya akaanza kuelekea katika ofisi yake iliyokuwa pembeni ya kanisa hilo. Alipoingia ofisini mwake, akaanza kuifuata kiti chake na kukalia, akaichukua Biblia ambayo ilikuwa mezani na kuanza kusoma baadhi ya maandiko.



    Alitulia kimya huku akiendelea kupitia baadhi ya maandiko. Mara kwa mara uso wake ulikuwa ukionyesha tabasamu kila alipokuwa akisoma andiko ambalo lilionekana kumvutia. Alitumia muda wa dakika thelathini kuyasoma baadhi ya maandiko ambayo alikuwa ameyadhamiria kuyasoma katika kipindi hicho. Alipomaliza kuyasoma maandiko hayo, akaifunika Biblia yake na kuanza kusali.



    Huku akiwa katikati ya sala, mara mlango ukasikika ukianza kugongwa kitu ambacho kilimpelekea kukatisha sala yake na kumkaribisha mgongaji. Mlango ukafunguiwa na msichana Judith kuingia. Mchungaji Matimya akaonekana kushtuka kwani halikuwa jambo la kwaida kwa mgeni kuingia ndani ya ofisi yake katika kipindi hicho ambacho alijiandaa kufunga ofisi yake.



    Judith akaanza kupiga hatua kukifuata kiti cha wageni na kisha kutulia huku kikiwa mbele ya meza ile pale ofisini. Judith hakuongea kitu chochote kile, alibaki akimwangalia mchungaji kwa kutumia macho ambayo yalionyesha mshtuo mkubwa kwa mchungaji Matimya. Mchungaji Matimya akasimama na kuanza kumsogelea Judith ambaye alibaki kimya akijifikiria namna ya kufanya kile ambacho alitakiwa kukifanya kwa wakati ule.



    “Kuna nini tena judith?” Mchungaji Matimya alimuuliza Judith.



    “Nina kiu mchungaji” Judith alijibu.



    “Kiu ya Neno la Mungu au?”



    “Hapana. Nina kiu ya penzi lako” Judith alijibu huku akionekana kutokujiamini.



    Mchungaji Matimya akapigwa na mshtuko, jibu ambalo lilitoka mdomoni mwa Judith lilionekana kumshtua kupita kawaida. Hakujua kama masikio yake yalikuwa yamesikia vibaya au yalikuwa yamesikia kitu halisi ambacho kilikuwa kimetoka mdomoni mwa Judith.



    Akaanza kumwangalia Judith mara mbili mbili kana kwamba hakuwa amekielewa kile ambacho alikuwa amekisikia kutoka mdomoni mwa Judith. Uso wa Judith haukuonekana kutania hata kidogo, alionekana kumaanisha kile ambacho alikuwa akikiongea kwa wakati ule.



    Huku akionekana kutokujua ni kitu gani ambacho alitakiwa kufanya kwa wakati ule, akashtuka mara baada ya kumuona Judith akianza kuvua nguo zake katika kasi ambayo ilionekana kumshangaza.



    Mikono ya Judith ikapata nguvu ya ziada, akamvuta mchungaji Matimya na kisha kuanza kulivua shati lake ambapo likafunguka huku baadhi ya vifungo viking’oka. Mchungaji Matimya alijaribu kuleta purukushani za kutaka kujiondoa mikononi mwa Judith lakini hakufanikiwa.



    “Niachie…niach…..” Mchungaji Matimya alimwambia Judith lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake, akasukumwa na Judith ambaye alianza kupiga kelele za kuomba msaada huku akiifungua blauzi yake na kuyaacha matiti yake nje. Judith hakuona kuridhika, akaanza kuipandisha sketi yake juu ya kuyaacha mapaja yake wazi.



    “Ananibakaaaaaa…..ananibakaaaaa…..” Judith alipiga kelele huku akimsogelea mchungaji ambaye alionekana kuwa kama mtu aliyechanganyikiwa. Kwa kasi kubwa Judith akamvuta mchungaji na kisha kumuweka katikati ya mapaja yake na kisha kuibana miguu yake huku kelele za kubakwa zikiendelea kusikika.



    Ghafla mlango wa ofisi ile ukafunguliwa na wazee wa kanisa kuingia. Picha ambayo ilionekana ndani ya ofisi ile ilionekana kumshtua kila mtu. Judith alikuwa amelala juu ya meza huku mchungaji Matimya akiwa katikati ya mapaja yake yaliyokuwa wazi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Yesu wangu!” Mzee kiongozi wa kanisa hilo, Bwana Onesmo alijikuta akisema huku akiiweka mikono yake kichwani. Mara baada ya Judith kuona kwamba wazee wa kanisa walikuwa wamefika ndani ya ofisi ile na kuliona tukio lile, hapo hapo akajitoa na kuelekea pembeni huku akijitahidi kuyafunika matiti yake.



    “Mchungaji! Umefanya nini?” Mzee Sule aliuliza kwa mshtuko.



    Mchungaji Matimya hakutoa jibu lolote lile, alibaki kimya huku akimwangalia Judith usoni. Judith alikuwa akilia huku mashavu yake yakiwa yameloanishwa na machozi ambayo yalikuwa yakimtoka. Mchungaji Matimya hakuelewa ni kitu gani ambacho alitakiwa kuongea ili aeleweke kwa wazee wa kanisa kwamba hakuwa amefanya kile kitu ambacho Judith alikuwa akikisema kwa wakati ule.



    Muonekano wa Judith ambao alikuwa nao ndio ambao ulikuwa ukiwahakikishia wazee wa kanisa kwamba mchungaji Matimya alikuwa amefanya kile ambacho Judith alikuwa akikisema kwa wakati huo.



    Sketi yake ilikuwa imechanika na kuyafanya mapaja yake kuwa nje. Blauzi yake ambayo alikuwa ameivaa ilikuwa imeng’olewa vifungo na kuyafanya matiti yake kuwa nje. Kila mtu alimwamini Judith juu ya kile ambacho alikuwa akikisema kwa wakati ule.



    Muda wote huo mchungaji Matimya alibaki kimya huku akiwa hafahamu ni kitu gani ambacho alitakiwa kufanya. Alionekana kuchanganyikiwa.



    Katika kipindi chote mchungaji Matimya hakuonekana kuwa na furaha, kila wakati alikuwa mtu wa majonzi tu. Skendo ya kutaka kubaka ambayo ilikuwa imemkuta ndio ambayo ilichangia kuwa katika hali hiyo ya majonzi. Katika vipindi vyote ambavyo alipitia katika maisha yake, kipindi hicho ndicho kilionekana kuwa kuwa kipindi kigumu kuliko vipindi vyote maishani mwake.



    Mara kwa mara alikuwa akijifungua chumbani akisali, alijiona kuwa kama mtu mwenye dhambi mbele za Mungu. Shetani alionekana kupewa nafasi ya kumjaribu. Kila wakati alikuwa akisali huku machozi yakimtiririka, alilia kupita kiasi, hakuona msaada wowote mbele yake, alijiona kuwa kama mtu aliyetengwa pasipo msaada wowote ule.



    Marafiki zake wote aliokuwa nao walionekana kuwa kama kumtenga. Familia yake ndio ambayo ilionekana kuwa kila kitu katika maisha yake, hiyo ndio ilikuwa furaha yake, upendo wake na faraja yake kuu. Mchungaji Matimya hakupewa nafasi yoyote ya kujitetea, kila mtu alimuona kuwa mtu maalum ambaye aliitwa kanisani kwa ajili ya kuliharibu kanisa.



    Kanisani akawa akikaa katika viti vya nyuma pamoja na familia yake. Washirika wa kanisa hilo hawakuwaonyeshea upendo tena, kila mtu alionekana kuichukia familia hiyo. Tukio ambalo lilikuwa limetokea katika maisha yake lilionekana kutaka kuiyumbisha imani yake siku za usoni.



    Kila ibada ilipokuwa ikiisha, hakutaka kubaki kanisani hapo zaidi ya kuingia ndani ya gari na kuondoka pamoja na familia yake.



    Kila siku moyo wake ulikuwa na majonzi, furaha kwake ikapotea, majonzi yakautawala moyo wake. Mara kwa mara alikuwa akifikiria sababu zilizompelekea Judith kufanya kitendo kama kle ndani ya ofisi yake. Hakufikiria hata mara moja kama mchungaji Mwakipesile alikuwa nyuma ya tukio zima.



    Ndani ya gari kila mtu alikuwa kimya huku wote wakionekana kuwa na mawazo vichwani mwao. Vitendo ambavyo vilikuwa vikifanywa na washirika wa kanisa lile ndivyo ambavyo vilikuwa vikiwaumiza. Ukaribu ambao ulikuwepo kati yao na washirika wa kanisa lile ukaonekana kupotea. Familia nzima ilionekana kutenda dhambi isiyoweza kusameheka mbele za Mungu.



    “Siamini kama kanisa linaweza kufanya kitu kama hiki, yaani upendo wao wote umepotea, upendo ambao walikuwa nao kabla umepotea kabisa” Mzee Matimya alisema huku akionekana kuwa na majonzi.



    “Nafikiri Mungu anataka kuipima imani y….” Bi Meriana alisema lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake, Benedict akaingilia.



    “Silifikirii hilo mama. Hapa kuna kitu, ni lazima kutakuwa na mtu aliyefanya mpango huu” Benedict alisema huku mikono yake ikiwa imeshikiria usukani.



    “Hakuna mpango wowote Bened…..”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Usiseme hivyo baba. Sisi kama binadamu tuna udhaifu. Unaweza kukuta hata wachungaji wengine wamehusika katika hili” Benedict alisema huku akionekana kukasirika.



    “Usiseme maneno hayo juu ya watumishi wa Mungu, Benedict”



    Benedict hakutaka kuendelea kuongea kitu chochote kile kwani kila alipokuwa akiongea na ndivyo ambavyo hasira zilivyozidi kumpanda. Hakutaka kuwa na mapenzi yoyote na washirika wa kanisa la Praise And Worship. Alimchukia kila mtu kanisani. Akili yake haikukubaliana na kanisa kama kweli baba yake aliweza kufanya kitu kama kile. Alijua fika kwamba Judith alikuwa amefanya kitu kile kwa sababu ya kitu fulani.



    “Kuna mtu nyuma ya Judith” Benedict alisema mara baada ya ukimya kutawala kwa muda mrefu garini mule.



    Kila mtu akabaki akimwangalia Benedict ambaye alikuwa akitingisha kichwa chake juu na chini kuashiria kwamba alikuwa na uhakika juu ya kile ambacho alikuwa akikiongea katika kipindi kile.



    “Kuna mtu? Mtu gani?” Bi Meriana aliuliza huku akionekana kushangaa.



    “Simfahamu ni mtu gani lakini nafikiri mtu huyo atakuwa miongoni mwa wachun…”



    “Benedict…..” Mzee Matimya aliita kwa sauti iliyojaa hasira ambayo ilimfanya Benedict kunyamaza.



    ITAENDELEA...

    NO:06



    Katika kipindi chote mchungaji Matimya hakuonekana kuwa na furaha, kila wakati alikuwa mtu wa majonzi tu. Skendo ya kutaka kubaka ambayo ilikuwa imemkuta ndio ambayo ilichangia kuwa katika hali hiyo ya majonzi. Katika vipindi vyote ambavyo alipitia katika maisha yake, kipindi hicho ndicho kilionekana kuwa kuwa kipindi kigumu kuliko vipindi vyote maishani mwake.



    Mara kwa mara alikuwa akijifungua chumbani akisali, alijiona kuwa kama mtu mwenye dhambi mbele za Mungu. Shetani alionekana kupewa nafasi ya kumjaribu. Kila wakati alikuwa akisali huku machozi yakimtiririka, alilia kupita kiasi, hakuona msaada wowote mbele yake, alijiona kuwa kama mtu aliyetengwa pasipo msaada wowote ule.



    Marafiki zake wote aliokuwa nao walionekana kuwa kama kumtenga. Familia yake ndio ambayo ilionekana kuwa kila kitu katika maisha yake, hiyo ndio ilikuwa furaha yake, upendo wake na faraja yake kuu. Mchungaji Matimya hakupewa nafasi yoyote ya kujitetea, kila mtu alimuona kuwa mtu maalum ambaye aliitwa kanisani kwa ajili ya kuliharibu kanisa.



    Kanisani akawa akikaa katika viti vya nyuma pamoja na familia yake. Washirika wa kanisa hilo hawakuwaonyeshea upendo tena, kila mtu alionekana kuichukia familia hiyo. Tukio ambalo lilikuwa limetokea katika maisha yake lilionekana kutaka kuiyumbisha imani yake siku za usoni.



    Kila ibada ilipokuwa ikiisha, hakutaka kubaki kanisani hapo zaidi ya kuingia ndani ya gari na kuondoka pamoja na familia yake.



    Kila siku moyo wake ulikuwa na majonzi, furaha kwake ikapotea, majonzi yakautawala moyo wake. Mara kwa mara alikuwa akifikiria sababu zilizompelekea Judith kufanya kitendo kama kle ndani ya ofisi yake. Hakufikiria hata mara moja kama mchungaji Mwakipesile alikuwa nyuma ya tukio zima.



    Ndani ya gari kila mtu alikuwa kimya huku wote wakionekana kuwa na mawazo vichwani mwao. Vitendo ambavyo vilikuwa vikifanywa na washirika wa kanisa lile ndivyo ambavyo vilikuwa vikiwaumiza. Ukaribu ambao ulikuwepo kati yao na washirika wa kanisa lile ukaonekana kupotea. Familia nzima ilionekana kutenda dhambi isiyoweza kusameheka mbele za Mungu.



    “Siamini kama kanisa linaweza kufanya kitu kama hiki, yaani upendo wao wote umepotea, upendo ambao walikuwa nao kabla umepotea kabisa” Mzee Matimya alisema huku akionekana kuwa na majonzi.



    “Nafikiri Mungu anataka kuipima imani y….” Bi Meriana alisema lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake, Benedict akaingilia.



    “Silifikirii hilo mama. Hapa kuna kitu, ni lazima kutakuwa na mtu aliyefanya mpango huu” Benedict alisema huku mikono yake ikiwa imeshikiria usukani.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hakuna mpango wowote Bened…..”



    “Usiseme hivyo baba. Sisi kama binadamu tuna udhaifu. Unaweza kukuta hata wachungaji wengine wamehusika katika hili” Benedict alisema huku akionekana kukasirika.



    “Usiseme maneno hayo juu ya watumishi wa Mungu, Benedict”



    Benedict hakutaka kuendelea kuongea kitu chochote kile kwani kila alipokuwa akiongea na ndivyo ambavyo hasira zilivyozidi kumpanda. Hakutaka kuwa na mapenzi yoyote na washirika wa kanisa la Praise And Worship. Alimchukia kila mtu kanisani. Akili yake haikukubaliana na kanisa kama kweli baba yake aliweza kufanya kitu kama kile. Alijua fika kwamba Judith alikuwa amefanya kitu kile kwa sababu ya kitu fulani.



    “Kuna mtu nyuma ya Judith” Benedict alisema mara baada ya ukimya kutawala kwa muda mrefu garini mule.



    Kila mtu akabaki akimwangalia Benedict ambaye alikuwa akitingisha kichwa chake juu na chini kuashiria kwamba alikuwa na uhakika juu ya kile ambacho alikuwa akikiongea katika kipindi kile.



    “Kuna mtu? Mtu gani?” Bi Meriana aliuliza huku akionekana kushangaa.



    “Simfahamu ni mtu gani lakini nafikiri mtu huyo atakuwa miongoni mwa wachun…”



    “Benedict…..” Mzee Matimya aliita kwa sauti iliyojaa hasira ambayo ilimfanya Benedict kunyamaza.



    Mzee Matimya alibaki katika chumba chake cha kusalia. Macho yake yalikuwa yakiiangalia Biblia yake iliyokuwa juu ya meza. Aliiangalia kwa kipindi kirefu bila kufanya kitu chochote kile. Alitamani kuanza sala yake kama siku nyingine ambavyo alivyokuwa akifanya lakini kila alipojaribu kupiga magoti chini, aliiona miguu yake ikiishiwa nguvu.



    Aliendelea kutulia juu ya kiti ndani ya chumba kile. Alijikuta akipata nguvu mpya, akaipeleka mikono juu ya meza ile, akaichukua Biblia ile na kuifungua. Akaanza kusoma baadhi ya maandiko ambayo aliyaona yakimfariji. Ghafla macho yake yakaanza kujaa machozi ambayo baada ya muda fulani yakaanza kutiririka mashavuni mwake.



    Nguvu za kuendelea kusoma Biblia zikatoweka. Akaifunika Biblia na kuyaelekeza macho yake darini. Alijiona kuwa peke yake, tumaini lote likatoweka, hasira zikaanza kumpanda kila kila alipokuwa akimfikiria Judith.



    Aliendelea kubaki katika hali ile kwa dakika kadhaa, mara akashtuka baada ya simu yake kuanza kuita. Akaupeleka mkono wake mfukoni na kuitoa simu ile na kuanza kukiangalia kioo cha simu ile. Namba ambazo zilionekana katika kioo cha simu ile zilikuwa ngeni machoni mwake. Hakutaka kujali sana, alichoifanya ni kuipeleka simu ile sikioni na kuanza kuongea.



    “Bwana Yesu Asifiwe mchungaji” Sauti ya upande wa pili ilisikika.



    Mzee Matimya hakuitikia chochote kile. Kichwa chake kikaanza kujaza maswali juu ya mpigaji wa simu ile. Taarifa zilijulikana Tanzania nzima kama katika kipindi hicho hakuwa mchungaji tena mara baada ya kuvuliwa uongozi huo. Ni nani alikuwa akiongea upande wa pili? Je alikuwa ni rafiki yake ambaye walipotezana kipindi kirefu kilichopita au alikwa mtu mwingine?



    “Mchungaji……” Sauti ya upande wa pili iliita mara baada ya kuona ukimya umetawala kwa kipindi kirefu.



    “Amen….Amen…Nani anaongea?” Mchungaji aliitikia na kuuliza swali huku akionekana dhahiri kutokumjua mpigaji wa simu ile.



    “Ni mimi Patrick. Patrick Chonya. Umenisahau mchungaji?”Sauti ya upande wa pili ilisikika



    Mzee Matimya akaonekana kupatwa na mshtuko, ghafla tabasamu likaanza kuonekana usoni mwake. Kila kitu ambacho kilitokea katika maisha yak kilionekana kusahaulika kwa muda. Alimfahamu sana Patrick, kijana ambaye alikuwa mshirika wake kabla ya kuhamia jijini Mwanza. Alisafiri miaka miwili iliyopita kuelekea nchini Marekani kwa ajili ya kusomea udaktari wa mifupa.



    “Mungu wangu! Umerudi lini kutoka Marekani?” Mzee Matimya aliuliza huku akionekana tabasamu likiendelea kuwepo usoni mwake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Leo hii ndio nimekanyaga ardhi ya Tanzania. Njoo hapa uwanja wa ndege mchungaji. Nataka kukuachia mizigo yako kutoka kwa mchungaji Macbeth Lewis. Nataka kuchukua ndege kuelekea Mwanza” Sauti ya upande wa pili ilisikika.



    Tabasamu likaongezeka zaidi na zaidi usoni mwa mzee Matimya. Hakuamini kama mchungaji Macbeth kutoka nchini Marekani ndani ya jiji la Atlanta angeweza kumkumbuka kwa kumletea zawadi kwani kilipita kipindi kirefu sana tangu mchungaji Macbeth aje nchini Tanzania na kuhubiri ndani ya kanisa lake.



    Kwa haraka haraka akakata simu na kuanza kujiandaa. Moyo wake ulirejewa na furaha, kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea katika maisha yake alikiona kuwa kama mpango wa Mungu katika kudhihirisha kwamba bado alikuwa pamoja nae. Mara baada ya kumaliza kujiandaa, akatoka na kuanza kuelekea uwanja wa ndege huku tayari ikiwa imetimia saa kumi na mbili jioni.



    Muda ulizidi kwenda mbele lakini wala mchungaji Matimya hakurudi nyumbani. Kila mtu alionekana kuwa na wasiwasi kwani hali ile haikuonekana kuwa ya kawaida kutokea. Mara kwa mara Bi Meriana alijaribu kumpigia simu mchungaji Matimya lakini simu haikupatikana.



    Bi Meriana hakukata tamaa, bado aliendelea kumpigia simu mume wake lakini majibu yalikuwa yale yale, simu haikupatikana. Amani ikatoweka moyoni mwake, mashaka yakaanza kumjaa, mara kwa mara Bi Meriana alikuwa akiikodolea macho saa yake, masaa yalikuwa yakiendelea kusonga mbele lakini wala mzee Matimya hakurudi nyumbani.



    Bi Meriana akashindwa kuvumilia, akasimama na kuanza kuelekea sebuleni, alipofika, akatulia kochini huku macho yake yakiangalia darini hali iliyoonyesha kwamba alikuwa na mawazo katika kipindi hicho. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo alizidi kuwa na wasiwasi zaidi.



    “Mungu wangu! Saa sita!” Bi Meriana aliasema hali iliyofanya Benedict ambaye alikuwa sebuleni pale kushtuka.



    “Mbona umeshtuka hivyo?” Benedict alimuuliza.



    “Baba yako”



    “Amefanya nini?”



    “Hajarudi”



    “Toka aliyoondoka saa kumi na mbili?”



    “Ndio”



    Benedict akaacha kufanya kazi ambayo alikuwa akiifanya na kisha kuanza kumsogelea mama yake. Alipomfikia, akajiweka karibu nae na kuchomoa simu yake na kisha kuanza kumpigia baba yake, mzee Matimya. Simu ilikuwa vile vile, mawasiliano hayakupatikana kabisa hali ambayo ikaanza kuibua wasiwasi moyoni mwa Benedict.



    Simu mbalimbali zikaanza kupigwa kwenda kwa ndugu, jamaa na marafiki ili kujua kama mzee Matimya alikuwa huko lakini hawakufanikiwa kumpata. Wasiwasi ukaongezeka maradufu mioyoni mwao, kitu cha hatari kilionekana kumtokea mzee Matimya kwani halikuwa jambo la kawaida kitu kama hicho kutokea.



    “Kwa hiyo tufanye nini?” Benedict alimuuliza mama yake.



    “Labda tupige simu pol….” Bi Meriana alisema lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake, simu yake ya mkononi ikaanza kuita. Kwa haraka haraka akayapeleka macho yake katika kioo cha simu ile. Mara ya kwanza alifikiri kwamba mpigaji wa simu ile alikuwa mumewe, lakini mara baada ya kuangalia kioo cha simu yake, namba ilikuwa ngeni.



    “Hallooo…! Wewe ni mke wa mchungaji?” Sauti ya upande wa pili ilisikika ikiuliza swali kwa sauti ya juu hata kabla ya salamu. Bi Meriana hakujibu chochote kile, alibaki kimya kwa muda kama mtu ambaye alikuwa akijifikiria namna ya kulijibu swali lile.



    “Haloo..! Upo hewani?”



    “Ndio”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Basi njoo hapa kituo cha polisi haraka iwezekanavyo”



    “Kituo gani?” Bi Meriana aliuliza huku akionekana kuwa na wasiwasi.



    “Mbezi kwa Yusufu” Sauti ya upande wa pili ilijibu na simu kukatwa.



    Bi Meriana akabaki kimya huku simu ikiendelea kuwa masikioni mwake japokuwa simu ile ilikuwa imekatwa. Mwili wake ukaanza kumtetemeka huku miguu yake akiiona ikifa ganzi. Hakuendelea kubaki katika hali hiyo zaidi, machozi yakaanza kumtoka.



    “Mama. Nini tena?” Benedict aliuliza mara baada ya kumuona mama yake akiwa kimya muda mrefu.



    “Kituo cha polisi Mbezi kwa Yusufu”



    “Kimefanya nini?” Benedict aliuliza huku akionekana kushangaa.



    “Twende” Bi Meriana alisema.



    Hakukuwa na sababu yoote kubaki mahali hapo, kwa haraka haraka wakachomoka kutoka ndani na moja kwa moja kuelekea nje ambako wakaingia ndani ya gari na kuanza safari ya kuelekea katika kituo cha polisi cha Mbezi kwa Yusufu. Machozi yakaanza kumtoka Bi Meriana huku sauti ya kilio cha chini chini kikianza kusikikika.



    Simu ile ambayo aliipokea muda mchache uliopita ilionekana kumchanganya, tayari alikwishajua kwamba kulikuwa na kitu ambacho kilikuwa kimetokea. Maswali mfululizo yakaanza kumiminika kichwani mwake. Katika kipindi cha nyuma mzee Matimya aliaga kwamba alikuwa akielekea uwanja wa ndege ambako alikuwa akihitajika, kwa nini simu ilipigwa kutoka Mbezi? Tena mbaya zaidi katika kituo cha polisi.



    Kutokana na kutokuwa na foleni ya magari, walitumia dakika thelathini mpaka kufika Mbezi kwa Yusufu. Moja kwa moja wasimamisha gari lao nje ya kituo kile cha polisi na kisha kuelekea katika kituo hicho.



    “Karibuni” Polisi mmoja ambaye alikuwa zamu aliwakaribisha mara baada ya kuwaona.



    “Kuna nini afande?” Mume wangu yuko wapi?” Bi Meriana aliuliza maswali mawili mfululizo hata kabla ya salamu. Sauti ya kilio cha chini ikaanza kusikika kutoka kwa Bi Meriana. Kitendo cha swali lake kutokujibiwa ndicho ambacho kilionekana kumtia wasiwasi.



    “Nini kinaendelea?” Benedict alivunja ukimya kwa kuuliza swali.



    “Ni taarifa za masikitiko sana. Kitu ambacho kimetokea kimeonekana kumshangaza kila mtu” Polisi alisema mara baada ya kuchukua maelezo ya Benedict na Bi Meriana na kisha kuendelea.



    “Mlisema aliondoka toka saa kumi na mbili kuelekea uwanja wa ndege?” Polisi aliuliza.



    “Ndio”



    “Alirudi baada ya kuondoka?”



    “Hapana”



    Polisi hakutaka kuendelea kuuliza maswali, akainuka kutoka pale kaunta na kuanza kuelekea katika chumba kimojawapo kati ya vyumba ambavyo vilikuwa ndani ya kituo kile ambapo baada ya sekunde kadhaa, polisi mwingine ambaye alikuwa mahali pale nae kuingia ndani ya kile chumba.



    “Nini kinaendelea afande?” Benedict aliuliza mara baada ya polisi wale kurudi kaunta.



    “Jambo hili bado linafanyiwa uchunguzi”



    “Uchunguzi? Uchunguzi gani?”



    “Uchunguzi juu ya kifo chake” Polisi alijibu huku akionekana kuwa na wasiwasi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Jibu lile likaonekana kumchanganya kila mmoja, Bi Meriana akaanza kulia kwa uchungu. Neno ‘kifo’ ambalo lilitamkwa na polisi yule ndilo ambalo lilionekana kumuumiza. Wala hakuchukua hata dakika moja kuwa katika hali ile, macho yake yakaanza kuona giza ambapo baada ya sekunde chache akaanguka na kupoteza fahamu.



    ITAENDELEA





0 comments:

Post a Comment

Blog